1000+ Vichekesho vipya: Vichekesho vya AckySHINE
Cha kufanya msichana akikukimbia halafu atake kukurudia
β¦β¦β¦ Kama msichana atakutupa kwa sababu huna pesa, na baadaye unapopata pesa akarudi tena kuomba msamahaβ¦ Ndugu yanguβ¦.. Msameheβ¦. Mpe ahadi ya ndoa, mwambie utamuoaβ¦. iambie familia yake unataka kufanya ukarabati wa nyumba yaoβ¦β¦ Ondoa paa lote la nyumba yao halafu TOWEKAβ¦..
πβ¦β¦β¦ πβ¦β¦.. π
Angalia alichojibu huyu mwanafunzi, Ungekua wewe ni mwalimu wake ungemfanyaje?
Mwanafunz alikuwa kila siku anachelewa shule, na kila siku alikuwa anachapwa, basi siku moja mwalimu akaona ngoja amuulize.
Mwalimu: Mbona unachelewa kila siku?
Mwanafunzi: Nakaa mbali mwalimu
Mwalimu: (huku ana hasira akauliza)Mbali mbinguni?
Mwanafunzi: Mbinguni kwa mbeleπππππ
Hapo sasa!! Ni shida!!
Umeshawahi saidiwa homework na mzazi halafu unapata zero?
Hapo ndio unajua shida siyo wewe
πππππππππππππππ
Angalia huyu mwanafunzi anachomjibu huyu mwalimu wake
1. Ticha:”Punda ni mnyama anaefugwa nyumbani,lakini akiwa mwituni anaitwa pundamiliaβ¦.Je sungura anayeishi mwituni anaitwaje?”
ZUZU:”Sunguramilia.”
2.Ticha:”Rais wa kwanza wa kenya aliitwa KENYATTAβ¦Je rais wa kwanza wa
Tanzania aliitwaje?”
ZUZU:”TANZANIATTA.”
3. Ticha:”Kuku yuko katika jamii ya NDEGEβ¦Je samaki yuko katika jamii ya nini?”
ZUZU:”MELI.”
4. Ticha:”Coach wa Arsenal anaitwa ARSENE,wa Man-city anaitwa MANCINIβ¦.Je wa
Liverpool anaitwaje?
ZUZU:”LIVER.”
5 Ticha:”Ukiwa na mbuzi 10,wezi waje waibe 5,utabaki na nini?”
ZUZU:”Hasira nyingi sana!”
Nilichokifanya leo
Leo nmemlipa konda nauli, akasahau kunishusha kituoni. Na mimi nkakaa KIMYAAA kumkomoaβ¦..
*nataka ujinga kwan mimiπππ*
Sahv narudi zangu kwa mguuπ©
Jambo usilolijua kuhusu mwili wako
JE WAJUA!β¦..
Msuli mrefu kuliko yote kwenye mwili wa binadamu unaunganisha kope za macho na sehemu ya kutolea haja kubwa ndo mana kila ukijaribu kubana jicho moja sehemu ya haja kubwa hufunguka bila kutarajia?
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
Nakuona unavojaribu kubana jicho β¦..
UTAKUJA KUNYA BUREEEE, hutaniwiii?!
ππππππππππππ
Bangi si mchezo, Angalia kilichowakuta hawa
Bangi si mchezo!
Jamaa kaikoleza si ikamtuma avue nguo!
Akavua nguo zote akaenda kwenye kioo, kujitazama akaona kama kavaa suti!
then akaenda kama alivyo zaliwa kwa masela wenzake akawauliza vp suti imenikaa? Mvuta bangi mwenzie akamwambia “imekutoa kinyama ila tai umeifunga chini sana”.
Angalia ndoto nyingine zilivyo na Majanga
Ndoto zingine bwana usiombe zikupate
Mimi usiku wa kuamkia Leo nikiwa nimelala nimeota naendesha gari Yangu aina ya BMW mpya Mara gafla ikakwama kwenye tope .hivyo ikabidi nishuke ili kuisukuma loh! Yani kudadeki ile kuamka nikakuta nimesukuma kitanda hadi sebleni Daaa ilinisikitisha sana jiangalie sana sese hivi ndio narudisha kitanda chumbani .angalizo angalia ndoto unazo ota unaweza kuota upo baharini ukaamka unajikukuta unaogelea kwenye Jaba la Maji shauri yako.
Sipendi ujinga. Cheki nilichokifanya
Nimeingia chumban nikakuta panya wamekula dawa yangu ya minyoo,
Na mimi nimechukua yakwao nikanywa.
Sipendagi ujinga mm!!
πππ
Angalia huyu jamaa alivyoachika na msichana wake kwa kujidai kuongea kingereza na mwishowe kuchanganya maneno
MSICHANA: Mbona jana nimekupigia simu hujapokea?
JAMAA: please beby forget me.
MSichAnA: eeeh unaniambia hivo mimi?
JAMAA: nakuomba sana forget me.
MSICHANA: aya bwana poa maisha mema.
Msichana anakata simu jamaa ndo ananiuliza.”sasa
sijui amekasirikia lipi?” Mi nikamwambia we zuzu
umemwambia AKUSAHAU, dah, kumbe
ningemwambiaje? hahaha, ungemwambia
ForgivE me! au Ungesema Tu NaombA nSameHe.
Swali la kizushi kwa wadada wanaovaa mawigi
Hivi wadada mnaovaa mawigi.
ππ½Β Utajisikiaje siku Boyfriend wako anaingia chumbani halafu anatundika NDEVU kwenye hengaπ€£
Utani wa wahindi, cheka kidogo
Mhindi afaulu mtihani wa Kiswahili
(1) Mfa maji ?β¦β¦β¦β¦β¦β¦.. Tampa life jacket.
(2) Mwenda pole?β¦β¦β¦β¦ Tachelewa fika.
(3) Usipoziba ufa ?β¦β¦β¦.. Mizi taona mpaka dani.
(4) Usilolijua ?β¦β¦β¦β¦β¦β¦ Uliza google.
(5) Mbio za utelezini ?β¦β¦. Chafua guo yako.
(6) Ukipenda boga ?β¦β¦β¦ Ngoja mezi ya ramzani tapata.
(7) Ukiona vinaelea ?β¦β¦.. iko nyepesi hiyo.
(8) Maji yakimwagika ?β¦β¦ Mambie dada tapiga deki.
(9) Chelewa chelewa ?β¦β¦β¦ Takosa guo ya sikukuuβ¦
(10) Kila ndege ?β¦β¦β¦β¦.. β¦Hutua Airport
(11) Bandu bandu ?β¦.. β¦β¦.Rafiki yake Jecha
(12) Mtaka cha Mvunguni ?β¦ Ondoa tanda
(13) Simba mwenda kimya?β¦.Kama sio gonjwa basi haina njaa.
(14) Aisifuye mvua ?β¦β¦β¦. Najua iko Mkulima hiyo
(15) Barabara ndefu ?β¦β¦.. Ongeza mwendo au tachelewa fika.
(16) Mlanawe hafi nawe ila?β¦. Takimbia
(17) Asie sikia la mkuu ? β¦β¦.. Tapeleka jela
(18) Hasira za mkizi ? β¦β¦β¦β¦..Tatafuna veve
(19) Mchamba wima ?β¦β¦.. Karibu ya Hurumzi
(20) Akumurikae mchana ?β¦.Kipofu hiyo
(21) Mficha maradhi ?β¦β¦.. Taenda Loliondo
(22) Mkataa wingi ? β¦β¦β¦.Taenda Chadema
(23) Bendera ?β¦β¦β¦β¦β¦. Kama sio ya CCM, ya CUF
(24) Baniani mbaya ?β¦β¦. Peleka Bombay Lakini sio HB kweli, naonea tu
(25) Akili nyingi ?β¦β¦β¦. Tapasi mtihani yote
(26) Penye kuku wengi ? β¦β¦.. Chija bili tatu ivi, hapana mtu najua.
Huyu bibi kweli kiboko, cheki alichofanya akiwa na babu
Bibi na Babu walisafiri wakielekea kwa mtoto wao ambae hawajamuona zamani.
Walipofika njiani wakawa wamechoka Sanaa. Wakaamua kutafuta hotel ili walale.
Wakakubaliana walale kwa masaa 4. Wakalala, Walipoamka, mfanyakazi wa Hotel akawatoza Tsh. 500,000/=
Wale wazee wakashangaa hata kama ni hotel ya kisasa lakini sio laki tano kwa masaa 4.
Babu akagoma kulipa akasema aitiwe meneja.
Meneja akaja kuwasikiliza
Babu: ” Kwanini bili ni kubwa hata kama ni hotel ya kisasa?”
Manager;“kuna maswiming puli, ya kisasa “
Babu; “Lakini hatukuyatumia”
Manager; “Ah ah ah. Lakini mungeweza kama mngetaka”
Babu: “Hata hivo bado haithamini kuwa laki 5”
meneja: “Pia Kuna waimbaji kutoka sauzi, Uganda , Congo”
Babu: “Lakini sisi hatukuwasikiliza”
Meneja: “Ndiooo. Lakini mngeweza kama mngetaka”
Babu; aka give up na kumwambia mkewe andika cheki uwape,,
Bibi akaandika akampa meneja.
Meneja anaangalia anaona sh. 50,000
Akashangaa na kusema. “VP mbona hamsini'”
Bibi akajibu “450,000 ya kulala na mimi”
Meneja akajibu; “Lakini sijalala”
Bibi :“ungeweza kama ungetaka”
Sababu ya mwanaume kunya kitandani alipokuwa kalala na mke wake
Jamaa flani alikuwa amelala na mkewe. Mara akamuona mtu amesimama kitandani.
Jamaa akafoka, “Toka hapa, we ni nani mpaka unakuja kitandani mwangu?”
Yule mtu akajibu, “Mi ni malaika na hapa sio kitandani mwako uko mbinguni!”
Jamaa, “Huh! Inamaana nimekufa,mbona mi bado kijanaβ¦ naomba nirudishwe!”
Malaika, “Inawezekana lakini siwezi kukurudisha kama mtu labda urudi kama mbwa ama kuku.”
Jamaa akakumbuka mbwa wanavyopata taabu ya kulinda, akaonelea arudi kama kuku.
Malaika akamgeuza kuku, akamwambia ajifunze kutaga kabla hajapelekwa duniani.
Akachuchumaa na kuanza kujikamua; yai la kwanza likatoka. akajikamua tena, yai la pili likatoka. Akajikamua tena mara ya tatu.
Wakati yai la tatu linatokaβ¦ akashtukia amepigwa konde ikifuatwa na sauti ya hasira ya mkewe, “Pumbav*! Balaa gani hiiβ¦. unakuny* kitandani!!”
Cheki kilichotokea stesheni ya treni, mambo mengine ukipaniki inakula kwako kama huyu jamaa
Jamaa Wawili Walifika Stesheni, wakakuta Treni ndo kwanza inaondoka. Wakaanza Kuikimbiza. Mmoja akafanikiwa kupanda akaondokaβ¦
Yule aliyebaki akaanza kucheka sanaa mpaka machozi yakamtoka. Watu wakamuullza, unacheka nini sasa wakati umeachwa? Akawajibu: “kinachonichekesha, yule aliyepanda alikuwa ananisindikiza.
Wanawake hii nayo ni romantic ?π
Alaf wale Madem wanaowavua maboy wao KOFIA alaf wanakimbia nayo thinking its FUNNY and ROMANTIC.. Hiv nyie mkivuliwa MAWIGI wakakimbia nayo mtajiskiaje?πΈπΈ
Cheki hawa washikaji wanachokifanya baada ya kuvuta bangi, Bangi si mchezo
Kuna washikaji walikuwa wakivuta bangiβ¦ kiberiti kikawaishiaβ¦ wakamtuma mwenzao akatafute kingineβ¦ bangi lilikuwa limemkoleaβ¦ akazungukazunguka hatimaye akarudi palepale kijiweniβ¦
MSHIKAJI:Β oyaaa wanangu eeehβ¦ niazimeni kiberiti mwanangu mwenyewe β¦..
WENZAKE:Β baharia ee subiria kimtindo kuna mwana tumemtuma akatafute kiberiti.
Jamaa alikuwa na tabia ya kutembea na binamu yake cheki kilichomkuta
Jamaa alikuwa na tabia ya kutembea na binamu yakeβ¦.
Alikuwa anasubiri mjomba na mkewe walale tu halafu ananyata mdogo mdogo mpaka chumbani kwa binamu yake.
Siku moja umeme ulikuwa umekatika ikabidi aamue kuvua nguo kabisachumbani kwakeβ¦.
Akanyata taratibua akafungua mlango akazama chumbani kwa mjomba ake bila kujua, ghafla umeme ukarudiβ¦
MJOMBA; we mshenzi umefata nini chumbani kwangu tena uko uchi
JAMAA; nimekuja kukuaga kesho naondoka
MJOMBA; ndo uje uchi?
JAMAA; ndio kwasababu nimeshapaki kila kitu kwenye begi
ππππππππππππ
Jamaa anayependa kuwafanyia watu uhuni leo kapatikana na huyu mdada
Mdada alienda super-market kununua
kuku, bahati mbaya kwenye frij
kulikuwa na kuku mmoja tu, muuzaji
akamtoa akamuweka kwenye
mzani, akaonekana ana kilo moja na robo.
Mdada akamuuliza
muuzaji,βHuna mkubwa zaidi?β Muuzaji
akamchukua yule kuku na
kujifanya kamrudisha kwenye friji, halafu
akamtoa tena kwenye friji na
kumrudisha kwenye mzani, safari hii
akagandamiza mzani kwa gumba,
kuku akaonekana ana kilo mbili. Mdada
akasema βDuh afadhali huyu
mkubwa kidogo,Β naomba unifungie
nawachukua wote wawiliβ
Mamaaaaa muuzaji sijui atatoa wap kuku wa piliπ
π π π π π Hapo ndipo utagundua kwa nini MUWA co TUNDA πΆπ½πΆπ½













































































I’m so happy you’re here! π₯³
Recent Comments