Mafundisho ya Msingi ya Kanisa Katoliki: Makala za Katoliki

MAANA YA SALA KWA MKRISTO

Sala ni kuinua mioyo yetu kwa Mungu na kuongea nae. Watu wote wanapaswa kusali, wema na wabaya. Inatupasa kusali kila siku bila kukata tama kwa ibada, kwa matumaini na kwa saburi. Kama mfano Yesu Alitufundisha sala ya Baba yetu.
Yatupasa kuwaombea wengine, watu wote wenye shida wakosefu na hata maadui zetu, vilevile tumtolee Mungu shukrani kila wakati na hasa kwa kuadhimisha Ekaristi Takatifu.
Masifu ni sala au wimbo unaomsifu na kumtambua Mungu kuwa Mungu.
Sababu za kusali
1. Kumuabudu Mungu
2. Kumshukuru Mungu
3. Kuomba Neema na Baraka kwa ajili yetu na wenzetu
4. Kuomba msamaha
Namna za sala
1. Sala ya sauti : Sala asaliyo mtu au kikundi kwa kutumia maneno
2. Sala ya fikra : Sala asaliyo mtu akiwa peke yake au na wengine kimya kimya akimuwaza Mungu.
3. Sala ya Taamuli: Kumtazama tuu Mungu kwa upendo Mkubwa Moyoni.
Nyakati zote zinafaa kwa sala hasa
1. Asubuhi na jioni
2. Kabla na baada ya kula
3. Kila dominika
4. Sikukuu za amri
5. Kabla na baada ya kazi
6. Katika kishawishi
Vyanzo vya sala za Kikristo
1. Neno la Mungu
2. Liturujia ya Kanisa
3. Fadhila za Kimungu
4. Matukio ya kila siku
Aidha Roho Mtakatifu ndiye mlezi wa ndani wa sala ya Kikristo akitufundisha kusali na kusali ndani mwetu.
Sala Muhimu kwa Mkristo
Sala kubwa ya kanisa ni Misa Takatifu na sala Bora kwa Bikira Maria ni Rozari Takatifu.
Sala nyingine Muhimu kwa Mkristu ni:
1. Baraka ya Sakramenti kuu
2. Andamo la Ekaristi
3. Litania Takatifu
4. Njia ya Msalaba
5. Rozari takatifu
6. Novena
Mtu anaweza kusali popote lakini kanisani ndio mahali rasmi pa sala, Aidha familia ni shule ya kwanza ya sala ambapo mtu hujifunza na kujizoesha kusali anapokua katika familia.
Changamoto na majaribu wakati wa kusali
1. Mtawanyiko wa mawazo
2. Ukavu wa Moyo
3. Uvivu na uregevu
Faida ya Sala
1. Zinaleta neema nyingi
2. Zinatuimarisha ili tushinde vishawishi na dhambi
3. Zinatuunganisha na Mungu
4. Zinatudumisha katika kutenda mema
Neno Amina katika sala linamaana ‘Na iwe hivyo’. Na neno Aeluya maana yake ni Msifuni Mungu.

Kujiweka chini ya Huruma ya Mungu: Kuponywa na Kupatanishwa

Kujiweka chini ya Huruma ya Mungu: Kuponywa na Kupatanishwa

Kila mmoja wetu amewahi kufanya makosa katika maisha yetu. Tunapohisi hatujui la kufanya, wakati mwingine tunakimbilia katika maamuzi ambayo yanatuletea hasara badala ya faida. Tunaweza kuathiriwa na mazingira au watu wanaotuzunguka ambao wanatufanya tufikirie vibaya. Lakini kuna njia ya kutoka kwa haya yote: kujiweka chini ya huruma ya Mungu. Hapa ni mambo ya kuzingatia unapotafuta kuponywa na kupatanishwa.

  1. Kusali

Sala ni muhimu sana kwa yeyote anayetaka kujipatanisha na Mungu. Kwa kupitia sala, tunaweza kujieleza kwa Mungu na kutafuta mwongozo wake. Kwa kusali, tunafungua mlango wa kujitolea na kujiweka chini ya huruma yake.

"Basi, njooni kwa kujitwika nira yangu, mjifunze kwangu; kwa maana mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu." (Mathayo 11:29)

  1. Kukubali makosa yako

Inaweza kuwa vigumu kukubali makosa yako. Lakini kukataa kuyakubali kutazuia mchakato wako wa kupatanishwa. Kukubali makosa yako ni hatua ya kwanza ya kujipatanisha na Mungu na kuwa tayari kuponywa.

"Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote." (1 Yohana 1:9)

  1. Kuacha mazoea mabaya

Kupata msamaha na kupatanishwa na Mungu haimaanishi kuendelea kuanguka katika dhambi za zamani. Tunapaswa kujitahidi kuacha mazoea mabaya na kujaribu kufanya mema.

"Lakini sasa mkiisha kuwa huru na kufanywa watumwa wa Mungu, mnastahili kupata tunda lako, ambalo ni utakatifu, na mwisho wake ni uzima wa milele." (Warumi 6:22)

  1. Kufunga

Kufunga ni njia nyingine ya kujikita katika kujipatanisha na Mungu. Fungo inaweza kuwa ya chakula, vinywaji, au kitu kingine chochote unachohisi kinakuzuia kufikia lengo lako. Kufunga kunakuweka karibu na Mungu na kusaidia kuondoa ulevi wa dhambi.

"Hapo ndipo watakapo fungua masikio yao kusikia habari njema ya ufalme wa Mungu; na kila mtu anayejitahidi kuingia, anaweza kufanya hivyo kwa nguvu ya kufunga." (Luka 16:16)

  1. Kuungama

Kuungama ni njia nyingine ya kujipatanisha na Mungu. Unapotambua makosa yako na kutaka kusamehewa, unaweza kufanya hivyo kupitia sakramenti ya Upatanisho. Kupitia kuungama, unapata msamaha wa Mungu na kujisikia mzima.

"Wakati huo Yesu akajibu, akasema, Nimehimili kwa muda mrefu sana na nanyi, na hujui. Ila Baba yangu anajua; nami naacha nafsi yangu mikononi mwa Baba yangu, hata siku moja hawa hawana haja ya kunitetea." (Luka 22:42-43)

  1. Kutafuta ushauri

Inaweza kuwa vigumu kujipatanisha na Mungu peke yako. Kutafuta ushauri kutoka kwa mtu anayemwamini Mungu ni njia nyingine ya kujipatanisha. Wanaweza kukupa mwongozo wa kiroho na kukuongoza katika mchakato wa kupata msamaha.

"Kwa maana watu wangu wamefanya makosa mawili: Wameniacha mimi, chemchemi ya maji yaliyo hai, na kuchimbia maashera, matangi yaliyovunjika yasiyoweza kubeba maji." (Yeremia 2:13)

  1. Kusamehe wengine

Kusamehe wengine ni njia ya kujipatanisha na Mungu. Unapofanya hivyo, unafungua mlango wa msamaha na upendo. Kusamehe ni kitendo cha kiroho na kinaleta amani ya ndani.

"Lakini mimi nawaambia ninyi, Wapendeni adui zenu, na kuwafanyia mema wale wanaowachukia ninyi, na kuwaombea wale wanaowaudhi na kuwatesa ninyi." (Mathayo 5:44)

  1. Kusoma Neno la Mungu

Kusoma Neno la Mungu ni njia nyingine ya kupata mwongozo na kujipatanisha na Mungu. Kupitia Biblia, tunajifunza jinsi Mungu anavyotaka sisi kuishi. Tunajifunza jinsi ya kumpenda na kumwabudu.

"Maana Neno la Mungu li hai, na lenye nguvu kuliko upanga uwao wote kuwili, na lachoma hata kuzigawa nafsi na roho, na viungo na mafuta yaliyoko ndani yake; tena li jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo." (Waebrania 4:12)

  1. Kujitolea kwa wengine

Kujitolea kwa wengine ni njia nyingine ya kujipatanisha na Mungu. Tunapojitolea kwa wengine, tunafanya kazi ya Mungu Duniani. Tunapata furaha na amani ya ndani kwa kujua kuwa tunawasaidia wengine.

"Ni afadhali kutoa kuliko kupokea." (Matendo 20:35)

  1. Kupokea sakramenti nyingine

Sakramenti nyingine, kama vile Ekaristi Takatifu na Ubatizo, ni njia nyingine ya kujipatanisha na Mungu. Kupitia sakramenti hizi, tunafikia karibu na Mungu na tunapata neema zake. Tunashiriki katika maisha yake ya kimungu na tunajifunza jinsi ya kufanya mapenzi yake.

"Kwa maana kama tulivyo wengi katika mwili mmoja, na viungo vyote havifanyi kazi ile ile." (Warumi 12:4)

Kujipatanisha na Mungu ni hatua ya kwanza ya kuponywa na kuishi maisha ya kiroho. Kwa kujitolea chini ya huruma ya Mungu, tunaweza kupata amani ya ndani na kufurahia maisha ya kiroho. Je, umefikia hatua ya kujipatanisha na Mungu? Je, unafanya nini kufikia hili? Tuambie katika sehemu ya maoni.

Mafundisho (Dogma) ya Kanisa Katoliki kuhusu Bikira Maria

Kuna mafundisho makuu manne kumhusu Bikira Maria ambayo ni lazima kila Mkatoliki ayasadiki kutokana na ufunuo wa Mungu: 1. B. Maria mkingiwa dhambi ya asili 2. B. Maria Mama wa Mungu 3. B. Maria Bikira daima 4. B. Maria kupalizwa mbinguni mwili na roho

Mkingiwa Dhambi ya Asili

Malaika alimsalimia Maria “umejaa neema” (Lk 1:28) maana ndiye tunda bora la ukombozi ulioletwa na Yesu. Ni imani ya Wakatoliki kwamba kwa stahili za Mwanae alikingiwa asirithi kwa wazazi dhambi ya asili na madonda yanayotokana nayo, wala asitende dhambi maisha yake yote. Kwa maneno mengine, Bikira Maria tangu atungwe mimba Mungu alimkinga na kila doa la dhambi kwa kutazamia stahili za Yesu Kristo aliye Mkombozi wa binadamu wote. Ndiye aliyekombolewa kwa namna bora kushinda viungo vyote vya Kanisa. Maisha yake yote hakutenda dhambi hata moja. Mapokeo ya mashariki yanamuita “A Panagia” = “Mtakatifu tu”. Dogma hiyo ilitangazwa na papa Pius IX mwaka 1854, halafu mwaka 1858 Bikira Maria alijitambulisha kama Mkingiwa kwa Bernadeta Soubirous huko Lurdi (Ufaransa). Tena mwaka 1917 huko Fatima (Ureno) aliwafunulia Lusia, Fransisko na Yasinta Marto moyo wake safi usio na doa.

Mama wa Mungu

Injili ya Yohane inaanza kwa kishindo, “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu” (Yoh 1:1). Huyo Mungu Mwana alitwaa ubinadamu katika Bikira Maria akazaliwa mtoto, jina lake Yesu, maana yake Mungu Mwokozi. Huyo ni binadamu kama sisi katika yote isipokuwa dhambi. Ubinadamu wa Yesu unategemea Nafsi yake ya Kimungu: akisema, ‘Mimi’, ni kwa Nafsi yake hiyo. Ndiyo maana aliwaambia Wayahudi, “Kweli nawaambia, kabla Abrahamu hajazaliwa, nalikuwepo” (Yoh 8:50). “Kama vile Baba alivyo asili ya uhai, ndivyo alivyomjalia Mwanae kuwa asili ya uhai” (Yoh 5:26).
Mtume Paulo akaeleza, “Wakati maalumu ulipotimia Mungu alimtuma Mwanae aliyezaliwa na mwanamke” (Gal 4:4). Bikira Maria ni Mama wa Mungu kwanzia wakati huo: tangu Bikira Maria alipojaliwa kumchukua mimba, kumzaa, kumnyonyesha na kumlea mtu ambaye kwa asili ni Mungu. Cheo hicho kimemuinua juu kuliko hata malaika. “Malaika alimwambia, ‘Hicho kitakachozaliwa kitaitwa Kitakatifu, Mwana wa Mungu’” (Lk 1:35).
Dogma ilitangazwa mwaka 431 kwenye Mtaguso wa Efeso uliomuita “Mzazi wa Mungu”, ukisema Maria anastahili kuitwa hivyo kwa sababu Mwana wa milele wa Mungu, ambaye ni Mungu sawa na Baba, alifanyika mtu toka kwake. Akiwa mja mzito alishangiliwa: “Umebarikiwa wewe katika wanawake, naye mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Limenitokeaje neno hili, hata mama wa Bwana wangu anijilie mimi?” (Lk 1:42-43). Ungamo hilo la Elizabeti likakamilishwa na Mtume Thoma aliyemuambia Yesu mfufuka: “Bwana wangu na Mungu wangu!” (Yoh 20:28).

Bikira na Mama

Wakristo na Waislamu wote wanakiri kuwa Yesu alitungwa bila ya mchango wa mwanamume. La ajabu zaidi katika imani hiyo ni kwamba hata uzazi wenyewe haukuondoa ubikira wake, bali uliutakasa: ni Bikira daima. Ingawa akili inasita, ni lazima kukiri na malaika, “Hakuna lisilowezekana kwa Mungu” (Lk 1:38). Yosefu, ingawa kisheria alikuwa mume wake, hakutenda naye tendo la ndoa.
Ni imani ya Wakatoliki na Waorthodoksi kuwa Mama wa Yesu anastahili kuitwa “Bikira daima” kwa sababu alimchukua mimba akiwa bikira, akamzaa bila ya kupotewa na ubikira, akabaki bikira hadi mwisho wa maisha yake. Hamu yake ya kuwa bikira hata kisha kuchumbiwa inajitokeza katika jibu alilompa malaika aliyemtabiria mimba: “Litakuwaje neno hili, maana sijui mume?” (Lk 1:35). Ni kielelezo cha Wakristo ambao Mtume Paulo aliwaandikia: “Nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi” (2Kor 11:2), “mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine” (1Kor 7:35).
Wanaosemwa katika Injili “ndugu zake Yesu” si watoto wa Bikira Maria, bali ndugu wa ukoo waliokuwa jirani sana na familia hiyo takatifu. Kama Bikira Maria angekuwa na watoto wengine, Yesu angekuwa amefanya kosa la kuwanyang’anya Mama yao na kumfanya awe Mama wa mtume Yohane alipomkabidhi msalabani, “‘Mwana, tazama Mama yako’. Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake” (Yoh 19:27).
Katika Agano Jipya yupo Yakobo anayeitwa na mtume Paulo “ndugu yake Bwana” (Gal 1:19): Yakobo huyo alikuwa maarufu katika Kanisa la Yerusalemu (Mdo 12:7; 15:13-21; 21:18-20; Gal 2:9). Yakobo huyo si mtume Yakobo kaka yake Yohane (Lk 6:12-16), bali ni Yakobo ndugu yake Yose na mama yao kwenye Injili anaitwa “Maria mwingine”, si Maria Mama wa Yesu. “Walikuwepo pia wanawake waliotazama kwa mbali. Miongoni mwao akiwa Maria Magdalena, Salome na Maria mama wa akina Yakobo mdogo na Yose” (Mk 15:40). Maria lilikuwa jina la kawaida kwa Wayahudi: akina Maria wakiwa wengi hivyo, tujue kuwatofautisha kwenye Injili, ambazo zinamtaja Bikira Maria kama “Mama wa Yesu”.

Kupalizwa Mbinguni mwili na roho

Baada ya maisha haya ya duniani Bikira Maria alipalizwa mbinguni mwili na roho, ishara ya mwanamke mshindi. “Ishara kubwa ikaonekana mbinguni, ambapo mwanamke aliyevikwa jua, pia na mwezi chini ya miguu yake, na taji la nyota kumi na mbili juu ya kichwa chake” (Ufu 12:1). Maneno ya shangilio lake yametimia: Mungu “amewaangusha wakuu katika viti vyao vya enzi; na wanyonge amewakweza” (Lk 1:52).
Imani hiyo ya mapokeo ya kale, yanavyoshuhudiwa na Mababu wa Kanisa, ilitangazwa rasmi na Papa Pius XII kwa niaba ya maaskofu wote mwaka 1950.

Je, Bikira Maria ni Bikira Daima au alizaa watoto wengine?

Jibu fupi ni kwamba Bikira Maria hakuzaa watoto wengine na hakuwa na watoto wengine zaidi ya Yesu
Hapo zamani hakuna mkristu au dehebu lolote lililokuwa linapinga kuwa Bikira Maria sio Bikira Daima hata Waprotestanti/walokole waliamini Bikira Maria ni Bikira Hata Baada ya Kumzaa Yesu. Kwenye Miaka ya 1400-1600 Watu wote wakwanza waliopinga Kanisa Katoliki walikubali kuwa Bikira Maria ni Bikira daima wakiwemo Martin Lutha aliyeanzisha kanisa la Lutheran, John Calvin aliyeanzisha Ulokole/Protestanti, Mchungaji Ulrich Zwingli, Heinrich Bullinger, and Thomas Cranmer. Kwa miaka zaidi ya 350 Waprotestant/walokole waliendelea kuamini kuwa Bikira Maria ni Bikira Daima.
Lakini baadae wakristo wengi walianza kupinga kuwa Bikira Maria ni Bikira Daima.

Tunaweza kuthibitisha kuwa Bikira Maria hakuzaa watoto wengine kwa kunukuu Biblia Kama ifuatavyo;

1. Bikira Maria Alikuwa Bikira Kabla ya kumzaa Yesu

Biblia inatuambia wazi kwamba Bikira Maria alikuwa Bikira Kabla ya kumzaa Yesu Kama tunavyosoma katika Luka 1:26-35
26 Mnamo mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu aende kwenye mji uitwao Nazareti huko Galilaya, 27 kwa msichana mmoja aitwaye Maria, mchumba wa mtu mmoja jina lake Yosefu, wa ukoo wa Daudi. 28 Malaika akamwendea, akamwambia, “Salamu Maria! Umejaliwa neema nyingi! Bwana yu pamoja nawe.” 29 Maria aliposikia maneno hayo alifadhaika sana, akawaza: maneno haya yanamaanisha nini? 30 Malaika akamwambia, “Usiogope Maria, kwa maana Mungu amekujalia neema. 31 Utachukua mimba, utamzaa mtoto wa kiume na utampa jina Yesu. 32 Yeye atakuwa mkuu na ataitwa Mwana wa Mungu Mkuu. Bwana Mungu atampa kiti cha mfalme Daudi, babu yake. 33 Kwa hivyo atautawala ukoo wa Yakobo milele, na ufalme wake hautakuwa na mwisho.” 34 Maria akamjibu, “Yatawezekanaje hayo, hali mimi ni bikira?” 35 Malaika akamjibu, “Roho Mtakatifu atakushukia, na uwezo wake Mungu Mkuu utakujia kama kivuli; kwa sababu hiyo, mtoto atakayezaliwa ataitwa Mtakatifu, Mwana wa Mungu. (Luka 1:26-35)

2. Biblia Haiwataji ndugu wa Yesu wakati Yosefu na Maria walipokimbilia Misri kumficha Yesu na wakati waliporudi

19 Baada ya kifo cha Herode, malaika wa Bwana alimtokea Yosefu katika ndoto kule Misri, 20 akamwambia, “Amka! Mchukue mtoto pamoja na mama yake, urudi tena katika nchi ya Israeli, maana wale waliotaka kumwua mtoto huyo wamekwisha kufa.” 21 Basi, Yosefu aliamka, akamchukua mtoto pamoja na mama yake, akarejea katika nchi ya Israeli. 22 Lakini Yosefu aliposikia kwamba Arkelao mwanawe Herode alikuwa mfalme wa Yudea mahali pa baba yake, aliogopa kwenda huko. Naye baada ya kuonywa katika ndoto, alikwenda katika mkoa wa Galilaya, 23 akahamia katika mji uitwao Nazareti. Ndivyo yalivyotimia maneno yaliyonenwa kwa njia ya manabii: “Ataitwa Mnazare.” Matayo 2:19-23
Kama wangekuwepo wadogo zake Yesu Biblia ingetuambia kwamba walikuwa wapi wakati huo na walikuwa na Yesu au la.

3. Biblia haituambii kuwa Yesu alikua na wadogo zake alipokuwa na miaka 12

Wakati wa Maria, Yoseph na Yesu walipoenda Yerusalemu Yesu akiwa na miaka 12 Biblia haituambii kuwa Yesu alikuwa na wadogo zake na walikuwa wapi. Kumbuka walikuwa na Desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka kwa ajili ya Pasaka familia nzima kama familia. Je hao watoto wengine walikuwa wapi. Kwa nini walikuwa na Yesu Mwenyewe? Maana yake ni kwamba Yesu hakuwa na Wadogo zake.
41 Wazazi wa Yesu walikuwa na desturi ya kwenda Yerusalemu kila mwaka wakati wa sikukuu ya Pasaka. 42 Mtoto alipokuwa na umri wa miaka kumi na miwili, wote walikwenda kwenye sikukuu hiyo kama ilivyokuwa desturi. 43 Baada ya sikukuu, walianza safari ya kurudi makwao, lakini Yesu alibaki Yerusalemu bila wazazi wake kuwa na habari. 44 Walidhani alikuwa pamoja na kundi la wasafiri, wakaenda mwendo wa kutwa, halafu wakaanza kumtafuta miongoni mwa jamaa na marafiki. 45 Kwa kuwa hawakumwona, walirudi Yerusalemu wakimtafuta. 46 Siku ya tatu walimkuta Hekaluni kati ya walimu, akiwasikiliza na kuwauliza maswali. 47 Wote waliosikia maneno yake walistaajabia akili yake na majibu yake ya hekima. 48 Wazazi wake walipomwona walishangaa. Maria, mama yake, akamwuliza, “Mwanangu, kwa nini umetutenda hivyo? Baba yako na mimi tumekuwa tukikutafuta kwa huzuni.” 49 Yeye akawajibu, “Kwa nini mlinitafuta? Hamkujua kwamba inanipasa kuwa katika nyumba ya Baba yangu?” 50 Lakini wazazi wake hawakuelewa maana ya maneno aliyowaambia. 51 Basi, akarudi pamoja nao hadi Nazareti, akawa anawatii. Mama yake akaweka mambo hayo yote moyoni mwake. 52 Naye Yesu akaendelea kukua katika hekima na kimo; akazidi kupendwa na Mungu na watu. (Luka 2:41-52).
Kwa hiyo Biblia haionyeshi kuwa Yesu alikuwa na kaka na dada wakati akiwa na miaka 12. Kama wangekuwepo wangetajwa hapa kuwa walikuwa pamoja na Wazazi wao kama Yesu au walikuwa na Yesu wakati anapotea. Biblia haituambii chochote kwa hiyo wakati huo hapakuwa na wadogo zake Yesu.

4. Kukosekana kwa neneo “Binamu” kwenye lugha ya Yesu

Wakristu wa kwanza pamoja na Yesu aliongea Kiaramaiki au Kiebrania. Katika lugha zote hizo hakuna neno “Binamu” kwa hiyo mabinamu walijulikana kama dada na kaka wa mtu. Kwenye Agano jipya Neno kaka na Dada lilitumika pia kuwakilisha binamu.
Biblia inapotuambia kuwa Kaka na dada zake Yesu haimaanishi kaka wa kuzaliwa bali ndugu au Binamu
55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?” (Mathayo 13:55-56)
Kwa hiyo wanaotajwa hapa ni ndugu wa Yesu kwa maana maneno kama; ndugu, kaka au dada lilitumika badala ya Binamu yaani mtoto wa shangazi au mjomba. Hapa juu Yosefu ametajwa kama kaka yake Yesu lakini tunajua kuwa Yosefu ni Baba yake Yesu. Baba na mwana hawawezi kuwa na jina sawa.

5. Biblia haitumii neno Ndugu, kaka au dada ikimaanisha ndugu wa kuzaliwa mama mmoja na baba mmoja

Sio mara zote Biblia imetumia neno Ndugu kumaanisha ndugu (Dada na Kaka) wa kuzaliwa yaani kaka na dada kwa mfano
Kwa kuangalia lugha ya Kiswahili na Kiingereza 1 Wakorintho 15:6 tunaona tafsiri tofauti.
KISWAHILI 6 Kisha aliwatokea ndugu zaidi ya mia tano kwa mara moja; wengi wao wanaishi bado, lakini baadhi yao wamekwisha kufa.
ENGLISH 6 After that, he appeared to more than five hundred of the brothers and sisters at the same time, most of whom are still living, though some have fallen asleep.
Kwa hiyo hapa neno kaka dada na ndugu linaonekana wazi halikumaanisha ndugu au kaka wa damu.

6. Undugu wa Yakobo, Simoni, Yosefu na Yuda kwa Yesu Sio wa mtu na kaka zake

Wasemao kuwa Bikira maria alikuwa na wana zaidi ya Yesu wananukuu kifungu hiki;
55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?” (Mathayo 13:55-56)
Kumbuka kulikuwa na Yakobo wawili wakati wa Yesu, Vifungu vifuatavyo yunaweza kuona kuwa kulikuwa na yakobo wawili ambao walikuwa ndugu za Yesu lakini sio kaka wa kuzaliwa kwa mama.
35 Yakobo na Yohane, wana wa Zebedayo, walimwendea Yesu wakamwambia, “Mwalimu, tunataka utufanyie kitu tutakachokuomba.” (Marko 10:35)
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. 56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo. (Matayo 27:55-56)
Tunaweza kuona Undugu huu na Yesu kwa kusoma;
19 Lakini sikuwaona mitume wengine isipokuwa Yakobo, ndugu yake Bwana. (Wagalatia 1:19)
Lakini Yuda anasema;
1 Mimi Yuda, mtumishi wa Yesu Kristo, ndugu yake Yakobo, nawaandikia ninyi mlioitwa na Mungu na ambao mnaishi katika upendo wa Mungu Baba, na katika ulinzi wa Yesu Kristo. (Yuda 1:1)
Kwa hiyo Yakobo na Yohane walikuwa watoto wa Mama mwingine ambao baba yao ni Zebedayo. Na Yakobo na Yosefu walikuwa watoto wa Maria Mwingine. Kwa hiyo ni Yakobo wa wili wa Mama wengine Tofauti na Maria. Yuda alikuwa ni ndugu yake Yakobo. Yakobo vilevile alikuwa ndugu yake Yesu.
Kuthibitisha kuwa Hawa kina Mama ndio waliokuwa Mama zao kina Yakobo wote hao wawili na wengine tunaweza kusoma;
25 Karibu na msalaba wake Yesu walikuwa wamesimama mama yake, na dada ya mama yake, Maria mke wa Kleopa, na Maria Magdalene. (Yohana 19:25)
Kwa hiyo kwenye (Yohana 19:25) tunaona Kuwa ni kwenye Msalaba wa Yesu alikuwepo Mama yake Yesu (Bikira Maria), Dada yake Bikira Maria, Mke wa Cleopa na Maria Magdalena. Na kwenye (Matayo 27:55-56) wamwtajwa ni Mama za kina nani kama inavyoonekana kwenye kifungu kifuatachi;.
55 Mahali hapo walikuwapo wanawake wengi wakitazama kwa mbali. Hao ndio wale waliomfuata Yesu kutoka Galilaya wakimtumikia. 56 Miongoni mwao walikuwa Maria Magdalene, Maria mama yao Yakobo na Yosefu, pamoja na mama yao wana wa Zebedayo. (Matayo 27:55-56).
Kwa hiyo hii ina maanisha kulikua na wanawake watatu wenye majina sawa ya Maria waliokuwa chini ya Msalaba. Yakobo na Yuda walikuwa watoto wa Maria Mke wa Cleofasi, na sio Mama wa Yesu, na hivyo sio kaka za Yesu.

7. Yesu alimwacha Mama yake kwa Yohane kwa kuwa hakuwa na Kaka na dada wakumwachia mamaye

26 Yesu alipomwona mama yake, na karibu naye amesimama yule mwanafunzi aliyempenda, akamwambia mama yake: “Mama! Tazama, huyo ndiye mwanao.” 27 Halafu akamwambia yule mwanafunzi: “Tazama, huyo ndiye mama yako.” Na tangu saa ile huyo mwanafunzi alimchukua akae nyumbani kwake.
Ndiyo maana Bikira Maria tangu siku ile alihamia kwa Yohani kwa kuwa hakuwa na watoto wengine.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu viongozi wa kidini na maaskofu?

Katika imani ya Kanisa Katoliki, viongozi wa kidini na maaskofu ni watu muhimu sana katika kufikisha ujumbe wa Mungu kwa wengine. Wao ni wawakilishi wa Kristo duniani na wanapaswa kufuata mfano wake wa kuwatumikia wengine kwa upendo na unyenyekevu.

Kanisa Katoliki linatambua kwamba maaskofu ni watendaji wa ngazi ya juu kabisa na wanayo mamlaka ya kufundisha, kuongoza, na kuwatawala waumini wa Kanisa. Kwa hivyo, wanapaswa kuwa na uadilifu wa hali ya juu na kuwa na uwezo wa kuonyesha mfano wa maisha ya Kikristo kwa waumini wao.

Kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, maaskofu ni wachungaji ambao wanahusika na huduma ya kufundisha, kuongoza, na kuwatawala waumini wa Kanisa. Wanapaswa kufanya hivyo kwa kuzingatia kanuni za Injili na kufuata mfano wa Kristo mwenyewe.

Maaskofu wanapaswa kuwa wakarimu, wanyenyekevu, na kuwatendea watu kwa upendo na huruma. Kwa kufanya hivyo, wanaweza kuwaongoza waumini wao kwa njia ya dhati na kuwasaidia kufikia ukamilifu wa maisha yao ya Kikristo.

Biblia inatupa mifano mingi ya jinsi viongozi wa kidini wanavyopaswa kuwa. Kwa mfano, Mtume Paulo alisisitiza umuhimu wa uadilifu katika uongozi wa kidini katika 1 Timotheo 3:2-3: "Basi askofu imempasa awe mtu asiye na lawama, mume wa mke mmoja, na mwenye kiasi, mwenye kujidhibiti, mwenye adabu, mwenye kupokea wageni, mwenye uwezo wa kufundisha; si mlevi, si mtu wa kujipenda mwenyewe, si mwenye hasira kali, si mtu wa kujitokeza sana, si mpiga-mkono".

Kanisa Katoliki linatambua kwamba hakuna kiongozi wa kidini au askofu anayeweza kuwa mkamilifu. Kwa hiyo, wanapaswa kuwa watu ambao daima wanatafuta kukua katika imani yao na kufanya kazi kwa bidii kumtumikia Mungu na waumini wao.

Kwa kweli, viongozi wa kidini na maaskofu ni watu muhimu sana katika Kanisa Katoliki. Kwa kufuata mfano wa Kristo na kuwa na uadilifu wa hali ya juu, wanaweza kuwa viongozi bora na kuwahudumia waumini wao kwa upendo na unyenyekevu.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya watoto wachanga?

Katika Kanisa Katoliki, watoto wachanga ni baraka kubwa kutoka kwa Mungu. Imani yetu inaamini kuwa kila mtoto anapewa uhai na Mwenyezi Mungu, na hivyo wanastahili heshima na upendo. Watoto wachanga ni zawadi kubwa kwa familia zao, na wanapaswa kuheshimiwa na kulindwa kwa kila hali.

Kanisa limeelezea kwa undani jinsi maisha ya mtoto wachanga yanapaswa kulindwa. Kwa mfano, kwa mujibu wa Catechism of the Catholic Church, "Maisha yote ni takatifu, tangu kuanzia mimba, mpaka kifo cha asili kinapotokea" (2258). Hii ina maana kwamba mtoto anayekua kwenye tumbo la uzazi anastahili heshima na kulindwa kama mtu mzima.

Kwa hiyo, Kanisa linapinga vitendo vyote vinavyoleta madhara kwa mtoto wachanga. Hii ni pamoja na utoaji mimba, ambao unaharibu uhai wa mtoto kabla hata hajazaliwa. Kanisa pia linapinga utoaji mimba kwa sababu yoyote ile, hata kama ni kwa ajili ya afya ya mama. Kanisa linatetea haki ya mtoto wa kuishi, na kuheshimu maisha yake kutoka mwanzo hadi mwisho.

Kanisa pia linawahimiza wazazi kuwa waangalifu katika jinsi wanavyokabiliana na watoto wachanga. Wazazi wanapaswa kuwa na upendo, uvumilivu, na subira katika kuwalea watoto wao. Kama ilivyoelezwa katika Catechism, "Wazazi wanapaswa kuwa mfano bora kwa watoto wao, na kuwafundisha jinsi ya kuishi kwa kumtegemea Mungu na kuwapenda wengine" (2225). Kwa hiyo, wazazi wanapaswa kuwa waangalifu katika kuchagua maneno yao na vitendo vyao wanapokuwa karibu na watoto wao.

Kanisa pia linawahimiza wazazi kuwabatiza watoto wao mara wanapozaliwa. Kupitia ubatizo, mtoto anapokea Roho Mtakatifu na anakuwa sehemu ya familia ya Kanisa. Ubatizo pia unafuta dhambi ya asili ya mtoto na kumweka katika njia ya kumfuata Kristo. Kwa hiyo, ubatizo ni muhimu sana katika maisha ya mtoto wachanga.

Kwa ufupi, maisha ya watoto wachanga ni muhimu sana katika imani ya Kanisa Katoliki. Watoto wachanga wanapaswa kulindwa kwa kila hali, na kutambuliwa kama zawadi kutoka kwa Mungu. Wazazi wanapaswa kuwa waangalifu katika jinsi wanavyowalea watoto wao, na kuhakikisha kuwa wanawafundisha jinsi ya kuishi kwa kumtegemea Mungu. Kupitia ubatizo, mtoto anakuwa sehemu ya familia ya Kanisa, na anapokea Roho Mtakatifu. Kwa hiyo, watoto wachanga ni baraka kubwa katika Kanisa, na wanapaswa kutunzwa kwa kila hali.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Yesu Kristo?

Habari za leo kwa wapenzi wa Yesu Kristo? Leo nitapenda kuzungumzia kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Yesu Kristo. Kama tunavyojua, Kanisa Katoliki ni moja ya madhehebu makubwa ya Ukristo na inaongozwa na Papa wa Roma. Ni dini inayoamini katika Mungu Mmoja, Mwana na Roho Mtakatifu.

Kanisa Katoliki linamwamini Yesu Kristo kama Mwana wa Mungu aliyezaliwa kwa Bikira Maria, aliyeteswa, akafa na kufufuka siku ya tatu. Kwa mujibu wa Kanisa Katoliki, Yesu Kristo ni Mkombozi wa ulimwengu na njia pekee ya kuokoka. Imani hii inathibitishwa na vifungu vingi vya Biblia, kama vile Yohana 3:16, "Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele."

Kanisa Katoliki pia linamwamini Yesu Kristo kama Mkuu wa Kanisa na kiongozi wa imani yetu. Kwa mujibu wa Injili ya Mathayo, Yesu alisema, "Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu" (Mathayo 16:18). Kanisa Katoliki linachukulia maneno haya kama msingi wa utume wa Papa na mamlaka yake kama kichwa cha Kanisa.

Kanisa Katoliki pia linamwamini Yesu Kristo kama Mtoaji wa Sakramenti. Sakramenti ni matendo ya neema ambayo Mungu anatupa kama njia ya kutuunganisha naye. Sakramenti saba ni ubatizo, kipaimara, ekaristi, kitubio, mpako wa wagonjwa, ndoa na upadri. Kwa mujibu wa Kanisa Katoliki, Yesu Kristo alianzisha Sakramenti hizi na ndiye anayetenda kazi kupitia Sakramenti hizi.

Kwa muhtasari, imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Yesu Kristo ni kuwa Yeye ni Mwana wa Mungu, Mkombozi wa ulimwengu, Mkuu wa Kanisa, Mtoaji wa Sakramenti na njia pekee ya Kuokoka. Hii ni msingi wa imani yetu kama Wakatoliki na tunaweza kushuhudia imani hii kwa kutenda mema na kuwa mashahidi wa upendo wa Kristo. Kama alivyosema Mtakatifu Paulo, "Hakuna mtu anayeweza kusema, ‘Yesu ni Bwana,’ isipokuwa kwa Roho Mtakatifu" (1 Wakorintho 12:3). Basi tuombe Roho Mtakatifu atupe nguvu ya kuendelea kushuhudia imani yetu kwa Yesu Kristo kwa njia zote tunazoweza. Amina.

Asili na matumizi ya Neno “AMINA” kama kiitikio muhimu katika Liturujia

Kiitikio hicho tunakifahamu sisi sote; tunaitikia mara nyingi lakini je, tunaelewa umuhimu wake? Binafsi nikichunguza wakati wa maadhimisho mbalimbali ya Liturujia hasa Adhimisho la Ekaristi, ni baadhi tu ya waamini wanaoitikiaAmina sehemu mbalimbali wakati wa Misa. Waamini wengine huitikia  kwa sauti  ya kuungama dhambi na wengine hawaitikii kabisa.

Asili yake 

Kwa asili Amina ni neno la kiebrania na maana yake ni: ni kweli kabisa.  Neno hilo lililotumika kukubali au kuthibitisha ukweli wa maneno au jambo lililokuwa limesemwa. Kwa hiyo mtu aliyesema Amina alitakiwa kusikia nini kilichosemwa na ndipo akubalie:    Amina.
Neno hilo limetumika katika Agano la Kale hasa katika Zaburi. Katika Agano Jipya Bwana Yesu alilitumia mara nyingi alipotaka kusisitiza siyo tu ukweli wa lile alilolisema bali pia uzito wake. Kwa namna hiyo Bwana Yesu alidhihirisha pia mamlaka yake katika lile alilosema.
Katika kitabu cha Ufunuo Yesu mwenyewe anaitwa Amina, kwani yeye ni mwaminifu kabisa katika maneno yake na kwamba yale anayosema kwa uhakika yatatimia. Tunasoma hivi: “Haya ndiyo anenayo yeye aliye Amina. Shahidi aliye mwaminifu na wa kweli…” (Ufu 3:14). Yesu mwenyewe anajiita  “njia, na  ukweli na  uzima”(Yn 14:6).

Katika Liturujia

Katika Liturujia yetu Amina ni kiitikio muhimu sana. Tunapoanza Sala zetu na kuhitimisha tunafanya Ishara ya Msalaba na kuitikiaAmina.Tunaposema Amina tunasisitiza umuhimu wa kuanza Sala au Liturujia tunayoadhimisha kwa jina la Utatu Mtakatifu. Kwa Sala hiyo msingi tunautukuza Utatu Mtakatifu na kuomba utuongoze katika Liturujia yetu tunayoadhimisha au Sala yetu tunayoitoa. Kwa kupiga Ishara ya Msalaba tunajiweka mikononi mwa Utatu Mtakatifu tunapoanza Sala zetu au kuadhimisha Liturujia, na tunapomaliza tunapiga tena Ishara ya Msalaba na kusemaAmina. Katika Adhimisho la Liturujia kwa kawaida kuhani huhitimisha kwa Baraka ndipo waamini hujiandika Ishara ya Msalaba.
Hata hivi katika Adhimisho moja la Liturujia kuna Sala mbalimbali ambazo kuhani au atazitamka kwa sauti peke yake kama mwongoza Adhimisho ili waamini wasikie na hatimaye waitikie Amina lakini kuna Sala ambazo kuhani hutakiwa kusali pamoja na waamini na wote watazihitimisha kwa pamoja kwa kiitikio hichohicho Amina. Tufuatane kuangalia Aminakatika Adhimisho la Ekaristi, yaani Misa.

Mwanzo wa Misa  

Mwanzoni kuhani huanza: Kwa Jina la Baba, na la Mwana, na la Roho Mtakatifu. Kama tulivyosema hapo juu hii ni Sala ya msingi ambayo inatuweka mikononi mwa Utatu Mtakatifu tunapoanza kuadhimisha Liturujia yetu. Kuhani akishasema vile Wakristo wote wanatakiwa kuitikia Amina. Wale wasioitikia wanafanya kosa kubwa la kutokukiri imani kwamba tunajiweka mikononi mwa Utatu Mtakatifu. Wanatakiwa kujiuliza wamefika kanisani kufanya nini?
Kuhani huwasalimu waamini na kisha hutualika kukiri dhambi zetu. Hapo kuna namna mbalimbali za kukiri dhambi, lakini zote huishia na Sala anayotamka kuhani: Mungu mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi zetu, atufikishe kwenye uzima wa milele. Waamini wote hutakiwa kuitikia  Amina. Kwa nini wengine basi hawaitikii?
Hata hivi tukumbuke tendo hilo ni la kukiri dhambi na kuomba msamaha wa jumla katika kujiweka tayari kuadhimisha mafumbo matakatifu kama mwaliko wa kuhani unavyosema. Hiyo siyo nafasi ya Sakramenti ya Kitubio na Upatanisho. Mkristo mwenye dhambi kubwa lazima aende kuungama kwa kuhani yaani padri au Askofu.
Baada ya tendo la kukiri dhambi na kuomba msamaha hufuata Utenzi wa Utukufu ambao huimbwa au kusemwa siyo na kwaya peke yaobali na waamini wote pamoja na kuhani. Utenzi huishia na Amina. Waamini wote pamoja na kuhani hukiri kwamba walivyoimba au kusali ni ukweli kabisa.
Sehemu ya Mwanzo wa Misa huhitimishwa na Sala iitwayo Kolekta, kutokana na neno la kilatini lenye maana ya kukusanya. Kuhani akishasema: Tuombe, inampasa kunyamaa kitambo ili kila Mkristo na kuhani mwenyewe wasali kimya ndipo kuhani ahitimishe maombi yao kwa sala iliyomo katika kitabu cha Misa. Sala anayosali kuhani ni kama inakusanya na kuhitimisha maombi ya Wakristo wote wanaoshiriki Misa hiyo. Mwishoni mwa Kolekta hiyo wote hutakiwa kuitikia Amina. Asiyeitikia huwaza nini moyoni mwake?

Liturujia ya Neno

Wakati wa Liturujia ya Neno, kabla ya Injili, kuhani hujiandaa kwa Sala fupi  ili kutangaza Injili. Iwapo Misa huongozwa na Askofu, shemasi au padri iwapo shemasi hayuko huomba Baraka kwa Askofu. Anapopata Baraka hupiga ishara ya Msalaba na kutikia Amina.
Baada ya mahubiri, siku za Dominika na Sherehe hufuata Kanuni ya Imani ambayo, kama utenzi wa Utukufu kwa Mungu juu, huimbwa au husemwa na Wakristo wote, na mwishoni wote humaliza kwa Amina.
Tunapomaliza sehemu ya Liturujia ya Neno kuhani huwaalika waamini kusali: Salini ndugu, ili sadaka yangu na yenu ikubalike kwa Mungu Baba mwenyezi. Wakristo wakishasali hawasemiAmina kwa sababu kuhani huendelea mara na Sala iitwayo Sala juu ya Vipaji (oratio super oblata) ambayo ni ya kuombea dhabihu. Baada ya Sala hiyo ndipo Wakristo wote huitikia Amina.Tujibidishe kufanya vile.

Sala Kuu ya Ekaristi

Sala ya kuombea vipaji huhitimisha sehemu ya kuandaa vipaji. Hufuata Sala Kuu ya Ekaristi inayoanza na dayalojia: Bwana awe nanyi,… Inueni mioyo .. Mwishoni mwa Sala Kuu ya Ekaristi hufuata kiitikio cha Amina, ambayo huitwa Amina Kuu. Waamini wote hutakiwa kuitikia kwa nguvu Amina hiyo Kuu. Katika Sherehe  waamini wote siyo kwaya peke yao, waimbe Amina mara tatu. Wanamuziki wazingatie hilo wakitunga muziki.
Baada ya Amina kuu hufuata sehemu ya kujiandaa kwa Komunyo Takatifu, inayoanza na Sala ya Bwana: Baba yetu uliye mbinguni. Baada ya sala hiyo hatuitikii Amina kwa sababu kuhani huendelea`mara :Ee Bwana, tunakuomba utuopoe …hatimaye wote huitikia: Kwa kuwa ufalme ni wako, na nguvu…
Hufuata mara Sala ya kuomba Amani ambayo kuhani husali na mwishoni wote huitikia Amina. Wakati wa kupokea Ekaristi kila Mkristo hutakiwa kuitikia Amina kabla ya kupokea Mwili wa Bwana. Ni tendo la kukiri imani kwamba unasadiki huo ni Mwili wa Kristo. Wote huitikiaAmina mwishoni mwa Sala baada ya Komunyo.

Hatima

Mwishoni mwa Misa wakati kuhani anapowabariki waamini ndipo wote wakiinamisha vichwa vyao, hupiga Ishara ya Msalaba na kuitikia Amina ya mwisho.Wito kwa Wakristo wote: Tuitikie AMINA wakati wa Liturujia, bila kusita.Kwa kufanya vile tunashiriki na kusali  na kuhani tena tunakiri imani yetu kwamba alivyotamka kuhani ninakubali, ni kweli kabisa na Sala hiyo huwa Sala yetu pia.

Huruma ya Mungu: Chemchemi ya Upendo Usiokwisha

Huruma ya Mungu ni chemchemi ya upendo usiokwisha. Tunaishi katika dunia ambayo imejaa shida na mateso, lakini tunapaswa kukumbuka kwamba Mungu daima yuko nasi. Uaminifu wetu kwake unatupa nguvu ya kuvumilia na kushinda majaribu. Katika makala hii, tutaangazia zaidi juu ya huruma ya Mungu na jinsi inavyotusaidia katika safari yetu ya kiroho.

  1. Huruma ya Mungu ni upendo wake usiokwisha. Yeye daima anatupenda, hata katika nyakati ngumu zaidi. Kwa mujibu wa Zaburi 103:8, "Bwana ni mwenye huruma na neema, si mwepesi wa hasira, naye ni mwingi wa rehema." Kwa hiyo, tunaweza kutegemea upendo wake daima.

  2. Huruma ya Mungu inatupatia msamaha wa dhambi zetu. Kwa mujibu wa Kitabu cha Isaya 43:25, "Mimi, naam, mimi ndimi yeye anayefuta makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitakumbuka dhambi zako." Kupitia msamaha wa dhambi, tunaweza kuwa huru kutoka kwa mzigo wa hatia na kuanza upya.

  3. Huruma ya Mungu inatupatia faraja. Katika Warumi 8:28, tunasoma, "Nasi twajua ya kuwa katika mambo yote Mungu hufanya kazi pamoja na wale wampendao ili mema yote yawasaidie, yaani, wale walioitwa kwa kusudi lake." Kwa hiyo, tunapaswa kuwa na imani kwamba Mungu anatenda kazi katika hali zetu zote na kwa hivyo tunapaswa kupata faraja.

  4. Huruma ya Mungu inatupatia nguvu ya kutenda mema. Kwa mujibu wa Wafilipi 4:13, "Naweza kufanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu." Bila huruma ya Mungu, tungekuwa hafifu na hatuna nguvu ya kutenda mema. Lakini kwa sababu ya upendo wake, tunaweza kupata nguvu zote tunazohitaji.

  5. Huruma ya Mungu inatupatia tumaini. Kama ilivyoelezwa katika 1 Petro 1:3, "Ahimidiwe Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, ambaye kwa rehema yake yenye wingi ametuletea uzima wa milele kupitia kwa ufufuo wa Yesu Kristo kutoka kwa wafu." Huruma ya Mungu inatuonesha kwamba ana mpango mzuri kwa ajili yetu, na kwamba tunaweza kuwa na tumaini kwa ajili ya siku zijazo.

  6. Huruma ya Mungu inatupatia uwezo wa kusamehe wengine. Tunapaswa kuwa na huruma kwa wengine kama vile Mungu anavyokuwa na huruma kwetu. Kama tunavyojifunza katika Mathayo 18:21-22, "Kisha Petro akamwendea, akamwuliza, Bwana, ndugu yangu atanikosea mara ngapi niweze kumsamehe? Kwa kuwa mara saba?" Yesu akamjibu, "Sikuambii hata mara saba, bali hata mara sabini mara saba."

  7. Huruma ya Mungu inatupatia amani ya ndani. Katika Yohana 14:27 Yesu alisema, "Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; nawaambia si kama ulimwengu unavyowapa mimi nawapa." Huruma ya Mungu inatupa amani ya ndani ya kuwa tunaweza kuwa na uhakika wa upendo wake na wokovu wetu.

  8. Huruma ya Mungu inatupa msukumo wa kuwahudumia wengine. Kama ilivyoelezwa katika 1 Yohana 3:17-18, "Lakini yeye mwenye mali ya dunia, akimwona ndugu yake akiteswa na kuufumba moyo wake kwake, je! Upendo wa Mungu wakaaje ndani yake? Watoto wadogo, tusipende kwa neno, wala kwa ulimi, bali kwa kazi na kweli." Tunaweza kumwonyesha Mungu tunampenda kwa kuwahudumia wengine.

  9. Huruma ya Mungu inatupa msamaha wa kila siku. Kama ilivyoelezwa katika Zaburi 103:12, "Kama mbali sana alivyo kuondosha makosa yetu na kututupa mbali na maovu yetu." Huruma ya Mungu inatupa msamaha kila siku, tunapoomba msamaha wa dhambi zetu.

  10. Huruma ya Mungu inakuja kwa njia ya sakramenti. Kama ilivyoelezwa katika Katekisimu ya Kanisa Katoliki, "Sakramenti ya kitubio haiwezi kukosekana kwa kila mmoja anayetaka kuishi kadiri ya mapenzi ya Mungu.. Katika sakramenti ya kitubio, tunapokea msamaha wa Mungu kwa dhambi zetu na tunapata nguvu ya kutenda mema.

Kwa hiyo, huruma ya Mungu ni muhimu sana katika safari yetu ya kiroho. Tunahitaji kuiweka imani yetu katika upendo wake usiokwisha na kuwa na tumaini la uzima wa milele. Tunapaswa kusamehe wengine na kuwahudumia kama Mungu anavyofanya kwetu. Na wakati tunapotenda dhambi, tunapaswa kutubu na kutafuta msamaha kupitia kwa sakramenti ya kitubio. Je, nini maoni yako juu ya huruma ya Mungu? Unafanya nini ili kuwa na huruma kwa wengine katika maisha yako ya kila siku?

Huruma ya Mungu: Kuponya Majeraha ya Roho

Huruma ya Mungu: Kuponya Majeraha ya Roho

Sote tunajua kuwa maisha yetu yanaweza kuwa magumu na mara nyingi tunajikuta tukiwa na majeraha ya kihisia na kiroho. Hata hivyo, kuna tumaini kwamba tunaweza kupona majeraha haya na kuwa na amani ya ndani ambayo tunatamani. Katika ulimwengu wa Kikristo, tunapata tumaini hili kwa Huruma ya Mungu.

  1. Huruma ya Mungu ni upendo wake kwa wote. Ni kitendo cha upendo ambacho Mungu anaonyesha kwa wanadamu, hata wakati hatustahili. "Lakini Mungu akiwa mwingi wa rehema, kwa sababu ya pendo lake kuu alilotupenda" (Waefeso 2:4). Ni huruma hii ambayo inatuwezesha kuponya majeraha yetu ya kiroho.

  2. Kuponya majeraha ya kiroho husaidia kuondoa mzigo wa dhambi zetu. Tunaishi katika ulimwengu wa dhambi, ambapo tunaweza kujikuta tukifanya mambo ambayo sio sahihi. Wakati tunatubu na kusamehewa, tunaweza kujikuta tukipata amani ya ndani na kupona majeraha yetu ya kiroho. "Mwenye haki atapata nafuu katika majeraha yake" (Mithali 12:18).

  3. Huruma ya Mungu inatuwezesha kusamehe wengine. Tunajikuta mara nyingine tukiwa na chuki na uchungu kwa wengine. Hata hivyo, tunapotambua upendo wa Mungu kwetu, tunaweza kusamehe wengine na kuwa na amani ya ndani. "Lakini iwapo hamjasamehe watu makosa yao, baba yenu wa mbinguni naye hatawasamehe makosa yenu" (Mathayo 6:15).

  4. Kuponya majeraha ya roho husaidia kujenga uhusiano mzuri na Mungu na wengine. Tunapopata amani ya ndani, tunakuwa na uwezo wa kuishi kwa upendo na kusaidia wengine. "Mtu yeyote akipenda, yeye huzaa matunda ya Roho" (Wagalatia 5:22-23).

  5. Huruma ya Mungu inatupa tumaini. Wakati majeraha yetu ya kiroho yanapopona, tunapata tumaini kwamba mambo yatakuwa bora. Tunajua kuwa Mungu yupo pamoja nasi na anatupenda. "Kwa maana naijua ile mawazo niwapayo ninyi, asema Bwana, mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku za mwisho" (Yeremia 29:11).

  6. Kupata huruma ya Mungu hutuletea furaha. Tunajua kuwa tunaponywa majeraha yetu ya kiroho, tunakuwa na furaha ya ndani na amani. "Mambo haya nimewaambia ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu iwe kamili" (Yohana 15:11).

  7. Huruma ya Mungu inatupa nguvu ya kusonga mbele. Wakati tunapoponywa majeraha yetu ya kiroho, tunakuwa na nguvu ya kusonga mbele na kukabiliana na changamoto za maisha. "Nakaza mwendo ili niifikie ile karama ya Mungu juu kabisa katika Kristo Yesu" (Wafilipi 3:14).

  8. Kuponya majeraha ya kiroho hutuletea amani ya ndani. Tunahitaji amani ya ndani ili kukabiliana na msongo wa maisha yetu. Tunapata amani hii kwa kuwa na uhusiano mzuri na Mungu na wengine. "Nami nitawapa ninyi amani, amani yangu nawapa; wala si kama ulimwengu uwapavyo mimi nawapa ninyi" (Yohana 14:27).

  9. Huruma ya Mungu inatupa upendo wa Mungu. Tunapopata huruma ya Mungu, tunatambua upendo wake kwetu na tunaanza kumpenda kwa moyo wote. "Kwa kuwa alimpenda sana huyo mtumishi wake, akamtuma kwenu yeye akiwa mwana wake, ambaye kwa yeye ameweka ulimwengu wote" (Yohana 3:16).

  10. Kupata huruma ya Mungu hutusaidia kuwa watakatifu. Tukipata huruma ya Mungu, tunaweza kuwa na moyo safi na kuwa watakatifu. "Sasa tujitakase sisi wenyewe na kujitakasa kila unajisi wa mwili na roho, tukimkamilisha utakatifu katika kumcha Mungu" (2 Wakorintho 7:1).

Kwa kumalizia, Huruma ya Mungu ni zawadi kubwa kutoka kwa Mungu wetu. Tunaweza kupata amani ya ndani na kuponya majeraha yetu ya kiroho kwa kumwamini na kumwomba Mungu. Kama Wakatoliki, tunaomba kwa ajili ya Huruma ya Mungu kila siku katika Rozari ya Huruma ya Mungu na kwa kumwomba kupitia nguvu ya Ukaribu wa Mungu na Sakramenti ya Upatanisho. Kwa njia hii, tunaweza kuishi maisha yenye amani na furaha, kwa sababu ya Huruma ya Mungu.

Je, unahisi vipi kuhusu Huruma ya Mungu? Unafikiriaje unaweza kuponya majeraha yako ya kiroho kupitia Huruma ya Mungu? Tupe maoni yako.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu ngono na maadili ya kijinsia?

Kanisa Katoliki ni moja ya madhehebu makubwa duniani, na imani yake juu ya ngono na maadili ya kijinsia ni muhimu sana. Kanisa hili linazingatia mafundisho ya Biblia na Catechism ya Kanisa Katoliki katika kuelezea maadili ya kijinsia na ngono.

Kwa mujibu wa Kanisa Katoliki, ngono ni kitendo kinachofanywa kati ya mwanamume na mwanamke, ambao wamefunga ndoa. Ni kitendo kitakatifu kinachopaswa kufanywa kwa upendo na kwa lengo la kuwaleta watoto duniani. Ni dhambi kufanya ngono kabla ya ndoa au kufanya ngono bila lengo la kuzaa watoto.

Kanisa Katoliki linasisitiza kuwa wanaume na wanawake wote ni sawa mbele ya Mungu na wanapaswa kutendewa kwa heshima na upendo. Uhusiano wa kimapenzi kati ya wanaume ama kati ya wanawake una kinyume na mafundisho ya Kanisa. Hata hivyo, Kanisa Katoliki linapenda na kuheshimu watu wote bila kujali kama wana tabia za kimapenzi ama la.

Kanisa Katoliki linasisitiza kuwa ngono inapaswa kutendeka kwa heshima na utu wa binadamu. Ni muhimu kufuata maadili ya kijinsia kwa kuepuka dhambi ya uzinzi, ngono haramu, na ukahaba. Kila mtu anapaswa kuishi maisha yenye maadili ya kijinsia, na kuhakikisha wanapata elimu ya kutosha juu ya maadili haya.

Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunasoma "Maadili ya kijinsia ni sehemu ya maadili ya kichungaji yanayohusiana na afya ya mtu na pia kuhusiana na maadili ya ndoa inayohusisha upendo wa kudumu kati ya mume na mke." (CCC 2351)

Kanisa Katoliki linasisitiza umuhimu wa kutumia njia za uzazi wa mpango ambazo hazimzuia Mungu kwa kuua mimba. Kanisa linapendekeza njia za uzazi wa mpango kama vile uzazi wa mpango wa asili, kufahamu kwa kina kuhusu mzunguko wa hedhi, na njia za uzazi wa mpango zinazorejesha udhibiti wa uzazi kwa mwanamke.

Kanisa Katoliki linakemea ngono kwa ajili ya kufurahisha nafsi ama kwa ajili ya ngono yenyewe, bila lengo la kuzaa watoto. Ngono inapaswa kuwa kwa lengo la kuunganisha mume na mke na kuwaleta watoto duniani kama zawadi kutoka kwa Mungu.

Hatimaye, Kanisa Katoliki linasisitiza umuhimu wa kuishi maisha ya utakatifu. Wanawake na wanaume wote wanapaswa kuishi maisha safi ya kijinsia, kufuata maadili ya kijinsia, kuheshimiana, na kuepuka kila aina ya dhambi. Kwa kufuata mafundisho ya Kanisa na kufuata Biblia na Catechism, tunaweza kuishi maisha yenye maadili ya kijinsia na mafanikio katika maisha.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema?

Leo tutajadili kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu msamaha na rehema. Kwa Wakatoliki, msamaha na rehema ni mada muhimu sana katika imani yetu. Tunakubali kwamba sisi sote ni wenye dhambi na tunahitaji kusamehewa dhambi zetu kwa ajili ya kufikia wokovu.

Tunamwamini Mungu kama mwenye rehema, ambaye anatupenda sana hata kama tumeanguka katika dhambi zetu. Kwa sababu ya upendo wake, Mungu ametoa njia ya msamaha na rehema kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu.

Kanisa Katoliki linahimiza Wakatoliki kutubu dhambi zao na kupata Sakramenti ya Upatanisho kama njia ya kupata msamaha wa dhambi. Sakramenti hii inaruhusu Wakatoliki kusema dhambi zao kwa padri na kufanya toba kwa ajili ya dhambi hizo. Padri kisha anawapa Wakatoliki msamaha wa dhambi zao kwa jina la Yesu Kristo.

Kanisa Katoliki linapenda kutumia Biblia kama mbinu ya kuwasilisha ujumbe wake. Katika wosia wa Yohana, tunasoma kwamba "ukiungama dhambi zako, yeye ni mwaminifu na wa haki hata akusamehe dhambi zako, na kukusafisha na uovu wote" (1 Yohana 1:9). Yesu mwenyewe pia alitoa uwezo wa kupata msamaha wa dhambi kwa wanafunzi wake katika Yohana 20:23.

Kanisa Katoliki pia linazingatia Catechism ya Kanisa Katoliki, ambayo inasema kwamba "Sakramenti ya Upatanisho inatupatia msamaha wa dhambi na kutufungulia njia ya kuwa na uhusiano mzuri na Mungu na Kanisa" (CCC 1422).

Kwa hiyo, msamaha na rehema ni muhimu sana katika imani ya Kanisa Katoliki. Tunamwamini Mungu kuwa mwenye rehema na tunajua kuwa kupata msamaha wa dhambi zetu ni njia ya kufikia wokovu. Kwa hiyo, tunahimiza Wakatoliki kuja kwa Sakramenti ya Upatanisho mara kwa mara ili kufurahia msamaha wa dhambi zao na kuwa na uhusiano mzuri na Mungu na Kanisa.

27. Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Daraja Takatifu?

Kwa wale ambao wamechagua njia ya Kikatoliki katika maisha yao, kanisa linaamini kuwa sakramenti ya Daraja Takatifu ni muhimu sana katika utendaji kazi wa maisha ya kanisa. Wakati wa kupokea sakramenti hii, wanaume wanapokea daraja ya Uaskofu, Upadri, na Ushemasi. Lakini ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti hii? Hapa chini ni maelezo fulani:

Kwa kuanza, Kanisa Katoliki linashikilia kuwa sakramenti ya Daraja Takatifu ni mojawapo ya sakramenti saba za Kanisa. Kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, sakramenti hii inampa mwanamume mamlaka ya kuwa kiongozi wa kiroho katika kanisa. Kwa hivyo, wanaume ambao wamepokea sakramenti hii wanakuwa na wajibu wa kuongoza kundi la waamini katika kufanya mambo ya kiroho.

Kuhusu ushirikishwaji wa Mungu katika sakramenti hii, Kanisa Katoliki linashikilia kwamba ni Mungu pekee ndiye anayeweza kuwapa wanaume mamlaka ya kuwa viongozi wa kiroho. Katika 1 Timotheo 4:14, kanisa linakumbuka maneno haya: "Usichukue tu kwa kiburi nafasi yako ya uongozi. Shughulika kwa bidii kila wakati, ukiendelea kujitahidi kufuata mafundisho ya Kanisa."

Kwa kuongezea, sakramenti ya Daraja Takatifu inahusiana sana na sakramenti nyingine za Kanisa. Kwa mfano, wanaume ambao wamepokea sakramenti hii wanaweza kutoa sakramenti ya Ekaristi Takatifu na kuwasamehe waamini dhambi katika sakramenti ya Kitubio. Kwa hiyo, sakramenti hii inahusiana sana na utendaji kazi wa kanisa kwa ujumla.

Mwishowe, Kanisa Katoliki linashikilia kuwa kuna wajibu mzito kwa wanaume ambao wamepokea sakramenti hii. Kwa mfano, wanapaswa kufuata maadili ya kikristo na kuheshimu mistari ya mamlaka. Katika Mathayo 23:11-12, Yesu anasema: "Mwenye kutawala kwenu, na awe mtumishi wenu. Kila mtu anayejitukuza mwenyewe atashushwa, na kila mtu anayejishusha atainuliwa."

Kwa hivyo, sakramenti ya Daraja Takatifu ni muhimu sana katika utendaji kazi wa kanisa. Wanaume ambao wamepokea sakramenti hii wanapaswa kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha kuwa kanisa linaweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuzingatia maadili ya kikristo. Kwa hivyo, sakramenti hii ni muhimu sana katika kufikia malengo ya kiroho ya kanisa.

Mambo yanayoweza kusababisha sala au maombi yako yasijibiwe

Mara nyingi tumekua tukiomba lakini hatupati, sababu zinaweza zikawa hizi ;

1. Mawazo na matarajio yetu

Mara nyingi tunajifunga kwenye maombi yetu pale tunapoomba na kisha kuanza kuwaza “hivi Mungu atanipa kikubwa au kidogo au atanisaidia sana au kidogo” Au tunaomba halafu tunakua na matarajio tofauti na kile tunachoomba. Aidha tunatarajia kupata kidogo au kikubwa.
Hali hii ni sawa na kumuwekea Mungu kizuizi kwenye maombi yako. Yaani kumuongoza Mungu afanye kwa kiasi kile unachofikiri.

2. Kulenga kutizamwa na watu.

Hii ni kuomba kwa majivuno yaani kuomba ili ukishapata watu waone kuwa umepata.
Jambo hili linamchukiza Mungu ndio maana unapoomba kupewa kitu au kusaidiwa kitu Mungu hafanyi /hakupi. Na Mara nyingine hata vile ulivyonavyo unanyan’ganywa kwa kuwa hauombi kwa utukufu wa Mungu bali kwa utukufu wako.
Hali hii ni sawa na kumuwekea Mungu ukuta kwenye maisha yako.

Namna njema ya kuomba ni hii

1. Kutokuomba mambo makuu sana ambayo huna haja nayo na hayana maana katika maisha yako.
2. Kutokuomba mambo madogo kwa mawazo labda nikiomba makubwa Mungu hataweza
3. Kutokuomba kwa ajili ya kutaka kuonekana na watu.

AHADI 15 ZA ROZARI TAKATIFU

Mama Bikira Maria alitoa ahadi 15 kwa yule au wale watakaosali Rozari takatifu kila siku. Ahadi hizi aliwapa Mtakatifu Dominic na mwenye heri Alan de la Roche.

1. Yeyote yule atakayesali kwa imani rozari hii takatifu atapokea neema kuu zenye nguvu
2. Naahidi ulinzi wa kipekee na neema za kipekee kwa yule atakayesali rozari hii
3. Rozari itakuwa silaha kubwa dhidi ya nguvu za kuzimu, itaharibu maovu, itapunguza dhambi na kushinda kutofautiana
4. Itafanya fadhila kukua, kazi nzuri kuongezeka, itapatia roho huruma tele toka kwa MUNGU, itaondoa hamu ya wanadamu kupenda mambo ya dunia na majivuno yake na kufanya wapende zaidi mambo ya mbinguni. Ooh, ni kwa namna gani roho hizo zitajifurahisha na kubarikiwa kwa namna hii.
5. Roho zitakazojikabidhi kwangu kwa njia ya kusali rozari, kamwe hazitapotea.
6. Yeyote atakayesali rozari kwa uaminifu huku akiyatafakari matendo makuu ya rozari, kamwe hatashindwa na ubaya. MUNGU hatamwadhibu katika hukumu yake, hatapotea katika kifo asichopangiwa na atabaki katika neema za MUNGU na kustahili kupata uzima wa milele.
7. Yeyote atakayekuwa mwaminifu katika kusali rozari, kamwe hatakufa bila ya kupokea Sakramenti takatifu za Kanisa.
8. Wote watakaokuwa waaminifu katika kusali rozari watadumu katika mwanga wa MUNGU katika maisha yao na saa yao ya kufa na kupata neema zake tele; katika saa yao ya kufa watashiriki fadhila za watakatifu waliopo peponi
9. Nitawatoa toharani wale wote waliokuwa waaminifu katika kusali rozari
10. Watoto wangu waaminifu katika kusali rozari watapata fadhila kuu ya utukufu Mbinguni.
11. Utapata yale yote unayoniomba kwa kusali rozari
12. Wote wale wanaoeneza rozari hii takatifu nitawasaidia katika mahitaji yao
13. Nimepata toka kwa mwanangu Mtukufu kuwa mawakili wote wa rozari takatifu watapata
waombezi toka baraza lote kuu la Mbinguni wakati wa maisha yao na wakati wa saa yao ya kufa.
14. Wote wanaosali rozari hii takatifu ni wanangu, na kaka na dada wa mwanangu wa pekee YESU KRISTO
15. Ibada kwa rozari takatifu ni ishara kuu ya kuelekea ukombozi

Swala la Mapadri kutooa limeandikwa wapi katika Biblia?

JE,SHERIA YA MAPADRE KUTOOA NA KUISHI USEJA IMEANDIKWA WAPI KATIKA BIBLIA AU IMETUNGWA TU NA PAPA?

Pengine umewahi kuulizwa swali hili wakati fulani.Na jibu lake ni kama ifuayavyo:
Mtu anapouliza kila kitu kimeandikwa wapi katika Biblia ni kudhihirisha kutokuijua au kuielewa vizuri Biblia Takatifu na historia yake.Mtu anapong’ang’ania “nionyeshe kitu fulani kimeandikwa wapi kwenye Biblia”ni kutaka kujiona ya kwamba yeye anaielewa sana Biblia na ameisoma yote kwa hiyo kila kitu kilichopo kwenye Biblia anakifahamu kumbe haijui Biblia bali anakariri Biblia!
Na hili suala la kushupalia swala la kuoa linadhihirisha jinsi gani tulivyo kizazi cha zinaa,ni kama tunadhani kuwa UZIMA upo katika kujamiiana!La hasha.
Paulo anasema “Kwasababu ya zinaa ni bora kuoa na kuolewa”(1Wakorintho 7:2.9) haya sio maneno ya kufurahia na kuchekelea tu maana “YANAWALENGA WALE WALIOSHINDIKANA KATIKA YALE YAPENDEZAYO”(1Wakorintho 7:1.8)sasa ni lazima tujiulize je tumeshindikana kiasi hicho?,hiyo sio sifa!
1Wakorintho 7:1.8
“Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika,ni heri mwanaume asimguse mwanamke,8.Lakini nawaambia wale wasiooa bado na wajane heri wakae kama mimi nilivyo”
Na Paulo Mtume anasema “Ni bora kuoa au kuolewa” lakini hakusema “Ni LAZIMA kuoa au kuolewa”
Suala la kutooa kwa mapadre kadiri ya historia lilianza tangu zamani kabisa mwanzoni mwa milenia ya pili katika mtagusi wa pili wa Laterani mwaka wa 1139 ili waweze kumtumikia Mungu kwa uhuru na bila mawaa wala pasipo vikwazo(1wakorintho 7:32-35)
1wakorintho 7:32-35
“32Lakini nataka msiwe na masumbufu.Yeye asiyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya Bwana ampendezeje Bwana;33.bali yeye aliyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendeza mkewe.34-Tena iko tofauti kati ya mke na mwanamwali.Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana ili apate kuwa mtakatifu mwili na Roho.Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendezesha mumewe.,35.Nasema hayo niwafaidie ninyi,si kwamba niwategee tanzi,bali kwaajili ya vile vipendezavyo,tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine”
Maandiko hayo hapo juu yanajieleza wala sidhani kama yanahitaji kufafanuliwa zaidi ya yanavyojifafanua yenyewe.
Watu wengine wanafikiri kwamba kutooa ni dhambi,kama ni hivyo basi hata Yesu mwenyewe alikosa maana hata yeye mwenyewe hakuoa.
Yesu mwenyewe anafundisha kuhusu ubikira(Mathayo 19:10-12)
Mathayo 19:10-12,
“Wanafunzi wake wakamwambia,kama mambo ya mme na mke yakiwa hivyo ni afadhali kutuooa kabisa.Lakini Yeye akawaambia ‘SI WOTE WAWEZAO KULIPOKEA NENO HILO,ILA TU WALE WALIOJALIWA,maana wako MATOWASHI waliozaliwa katika hali hiyo toka matumboni mwa mama zao;tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi,tena wako Matowashi WALIOJIFANYA WENYEWE KUWA MATOWASHI KWAAJILI YA UFALME WA MBINGUNI’,awezaye kulipokea neno hili na alipokee”
Yesu mwenyewe analifafanua jambo hili kwa mapana,katika orodha ya matowashi Yesu aliowataja,Mapadre ni Matowashi waliojifanya hivyo kwaajili ya huduma ya kanisa na ufalme wa Mungu.
Tena Yesu anatuambia waziwazi kwamba”sio wote wawezao kulipokea neno hilo”yaani sasa sio wote wawezao kuwa Matowashi(Mapadre)bali ni wale tu waliojaliwa na Mungu neema hiyo.wale wasioweza kuishi upadre huoa na kuwa na familia.Tena Yesu anamalizia kwa kusema “Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee”,kwa maana nyingine ni kusema “Fundisho au Utowashi huu sio wa lazima”anayeweza kuishi maisha hayo basi na ayapokee na yule asiyeweza basi aache!
Vilevile Mitume ili kumfuata Yesu kikamilifu waliyaacha yote waliokuwa nayo ikiwepo familia zao ili wamtumikie Bwana(Mathayo 19:27.29)
Mathayo 19:27.29:
“Ndipo Petro akajibu akamwambia ‘Tazama sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe,tutapata nini basi?29.Amini nawaambia,kila mtu aliyeacha nyumba au ndugu wa kiume au wakike,au baba au mama au watoto au mashamba KWAAJILI YA JINA LANGU,atapokea mara mia zaidi na kuurithi uzima wa milele”
katika injili hiyo,Yesu anadhihirisha kwamba aliyeacha hayo yaliotajwa si kwasababu hawezi kuyapata la hasha,bali ameyaacha hayo yote KWAAJILI YA JINA LA YESU atapokea mengi hapa duniani halafu tena ataurithi ufalme wa mbinguni.
Mapadre wameyaacha hayo yote,wameacha nyumba,familia zao na kila kitu SIO KWASABABU HAWANA UWEZO AU HAWAWEZI KUPATA MAMBO HAYO bali WAMEACHA KWASABABU YA KUMTUMIKIA MUNGU KWA KADIRI YA MAANDIKO MATAKATIFU na kwakutaka kwao kuyaishi kimamilifu MASHAURI YA INJILI ikiwepo USEJA.
Maneno ya Paulo na yale ya Yesu mwenyewe kuhusu kumtumikia Mungu bila kuoa sio ya bahati mbaya bali ndiyo njia bora na inayofaa sana na kukubalika mbele ya Mungu.
Kwahiyo unapowaona mapadre hawaoi ujue sababu yake ni hiyo kwamba “Wamejitoa kwaajili ya kulihudumia kanisa”
(Na pia huwa nawashangaa mno watu wanaowapiga vita Mapadre kwamba kwanini hawaoi,najiuliza je,hao Mapadre wamewakataza wao kwamba wasioe?.)..na kama jibu ni hapana,sasa Je,”Pilipili ya shamba usiyoila inakuwashia nini?”
TUMSIFU YESU KRISTO!

Je, Kanisa Katoliki linapinga utoaji mimba na kuhimiza kulinda na kuheshimu uhai wa watoto wachanga?

Karibu kwenye makala hii, ambapo tutajadili suala la utoaji mimba na jinsi Kanisa Katoliki linavyolipinga. Katika maandiko matakatifu, tunaambiwa kuwa kila uhai ni takatifu na kwamba hatuna haki ya kuutoa kwa namna yoyote ile. Hivyo, Kanisa Katoliki linahimiza kulinda na kuheshimu uhai wa watoto wachanga kwa kila njia.

Suala la utoaji mimba ni suala tata sana ambalo limegawanya jamii kwa muda mrefu sasa. Kwa upande wa Kanisa Katoliki, utoaji mimba ni dhambi kubwa, kwani kila mtoto aliyeumbwa na Mungu ana haki ya kuishi. Tunaambiwa katika Kitabu cha Zaburi 139:13-14 kuwa "wewe ndiwe uliyeniumba viungo vyangu, wewe umenifuma tumboni mwa mama yangu. Nitakusifu kwa kuwa nimeumbwa kwa jinsi ya ajabu ya kutisha; maana ya matendo yako ni ya ajabu, na nafsi yangu yajua sana."

Kwa hivyo, kila mtoto aliyeumbwa tumboni mwa mama yake ana thamani na haki ya kuishi, na hatuna haki ya kumnyima uhai wake. Hii ndiyo sababu Kanisa Katoliki linapinga utoaji mimba kwa nguvu zote.

Vile vile, Kanisa Katoliki linahimiza kulinda uhai wa watoto wachanga kwa kila njia. Kulingana na Katekisimu ya Kanisa Katoliki, kila mtoto aliyezaliwa ana haki ya kuwa na heshima na kulindwa, kwani kila mtoto ni zawadi kutoka kwa Mungu. Tunasoma katika Kitabu cha Isaya 44:24 kuwa "Bwana, Mkombozi wako, ndiye aliyekuumba tangu tumboni, asema hivi: Mimi ndiye Bwana, nifanyaye vitu vyote."

Kwa hiyo, kama Wakatoliki, tunapaswa kuheshimu na kulinda uhai wa watoto wachanga, kwani wanathaminiwa sana na Mungu. Tunapaswa kuwasaidia na kuwapa upendo wote wanahitaji ili kufikia ukuaji wao kamili.

Kwa kuhitimisha, Kanisa Katoliki linapinga utoaji mimba na kuhimiza kulinda na kuheshimu uhai wa watoto wachanga. Kwa kuzingatia maandiko matakatifu na kanuni za Kanisa, tunajifunza kwamba kila uhai ni takatifu na thamani yake ni kubwa. Kama Wakatoliki, tunapaswa kuwa mstari wa mbele katika kulinda uhai wa watoto wachanga na kuwasaidia katika safari yao ya maisha.

Ufalme wa simu wa sasa

➡ Asubuhi saa 12 : 00 mtu anaamka, kabla hata HAJAMUSHUKURU MUNGU, kabla hata hajatoka kitandani, kabla hata hajajifunua shuka,

👉ATARIPOTI KWA SIMU KWANZA KABLA YA KURIPOTI KWA YEYOTE, NDIO HAPO UNAONA MTU AKIAMKA KABLA HATA HAJASALI KWA MUNGU ANAAMKIA SIMU KWANZA KUIKAGUA,
– Nani alinitafuta?
-Nani alini-text?
-WhatsApp nani kanitumia msg?
– kwenye magroup kuna mpya gani?
– Fb kuna post gani kali?
– nani kaweka picha kali leo?
Nk.
Akimaliza KURIPOTI KWA Simu, faster faster, anapiga kaombi ka kidesturi, sekunde 20 basi.
Biblia ipo hapo kando tu ya kitanda, lkn anaona hana muda wa kuisoma.
✴BADALA YA KUANZA SIKU NA BWANA, MTU ANAANZA SIKU NA SIMU.
Pamoja na kazi za kuutwa, za mtu huyo, lkn atafanyq juu chini, apate muda wa KURIPOTI kwa SIMU.
Lakini mtu huyo huyo, hawez kbsa kupata muda wa kujitenga angalau kwa dk 3 tu, kw kutwa nzima ARIPOTI KWA MUNGU KWA NJIA YA MAOMBI.
Ana muda wa kusoma status kwenye social media kutwa nzima,
Lkn hana muda kbsa wa kupitia angalau sura moja tu, ya Biblia kwa siku.
Ana bundle la dk, sms, WhatsApp kila siku, lkn hana sadaka ya kumtolea Mungu.
Umeme ukikatika kutwa moja tu, akakosa kuwa na simu sababu ya chaji, anajisikia mpwekee, siku anaiona ndefuu, anajiona amepungukiwa saana!
Lakini huyo huyo, siku nzima inaisha, na ya pili, ya tatu , hajawahi kuwa na muda na Mungu wake hata kidogo, na anaona ni sawa tu.
Hata ktk siku ya ibada, yale masaa machache tu ya ibada, ambapo inatakiwa iwe ni mtu na Mungu wake tu, bila kuingiliwa na chochote, 👉mtu bado hawezi kukaa bila KURIPOTI kwa simu, ibada inaendelea huku mtu kawasha data, na anasoma na kujibu msg zake km kawaida.
👉 au kama ana kaustaraabu kidogo, atatoka nje, huko anaenda kukagua msg, kuangalia updates nk.
SIMU UNAYO KUTWA, KUCHWA, KIIILA SIKU, YANI HUKUWEZA KUVUMILIA KUIWEKA PEMBENI KWA MASAA TU?
➡ Swali nauliza, Mtu wa aina hiyo Mungu wake ni nani?
” Usiwe na miungu mingine ila mimi”.
KUTOKA 20 : 3
Kumuabudu Mungu peke yake, ni kumfanya Mungu awe wa KWANZA MOYONI NA MAWAZONI MWAKO.
Kumfanya awe kipaumbele kwenye kiila ulitendalo.
➡WENGI WAMEZIFANYA SIMU ZAO, ZICHUKUE NAFASI YA MUNGU KATIKA MIOYO, FIKRA NA MAISHA YAO KWA UJUMLA.
➡Wamekuwa tayari kupoteza karibu kiila kitu kwa ajili ya simu
– kupoteza marafiki > hawana muda na marafiki zao, wanajifungia ndani, wakichati.
– hawana muda na wazazi wao, hata kama wanaishi nyumba moja. > kijana akifika nyumbani, anapitiliza chumbani, ni yeye na simu, ataonekana muda wa kula tu, tena sometimes hata mezani anakuwa na simu, pale mezani wako wazazi wake kbsa, ndugu zake nk, lkn hajali uwepo wao, anaendelea na simu tu.
– Hawana muda na Mungu > Anahakikisha vyovyote itakavyokuwa, muda wa kuwa na simu unapatikana, HATA KAMA HILO LITAMAANISHA KUUPORA MUDA WA MUNGU (muda wa ibada).
Atakosa fedha za kusaidia wahitaji, fedha za zaka na sadaka, lkn fedha ya SIMU, (bundles) , lzm inakuwepo.
➡Mtu wa aina hiyo, anaiabudu simu bila kujua.
➡KITU CHOCHOTE KINACHOUVUTA MOYO KUTOKA KWA MUNGU, KUKIELEKEA CHENYEWE, KITU HICHO KINAJARIBU KUCHUKUA NAFASI YA MUNGU MOYONI.
NB: Sio lengo langu kupinga matumizi ya simu, lkn nilitaka tuwe na kiasi.

Mafundisho ya kumfundisha mtu mzima kabla ya ubatizo wa hatari

Ni lazima asadiki kwamba;
  1. Mungu yupo mmoja. Bwana wetu na Baba yetu, mwenye kuwatunza watu wema mbinguni na kuwaadhibu watu wabaya motoni milele (Mt. 15:41,46)
  2. Katika Mungu mmoja kuna nafsi tatu: Baba, Mwana na Roho Mtakatifu (Yoh. 14:16, 17).
  3. Nafsi ya pili alishuka duniani akajifanya mtu, akatuokoa utumwani mwa shetani, akatufundisha mambo gani tusadiki, mambo gani tutende, akatupa alama ya ukombozi wetu ndio ubatizo.
  4. Ubatizo wafuta kabisa uovu wa mtu na kutakasa roho zetu.
  5. Mwenye kubatizwa atubu na kurudisha alichoiba na kupatana na maadui n.k

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu upendo na huruma?

Karibu kwenye makala yangu kuhusu imani ya Kanisa Katoliki kuhusu upendo na huruma. Katika kanisa Katoliki, upendo ni jambo muhimu sana katika maisha yetu ya Kikristo. Kulingana na Biblia, Mungu ni upendo na ametualika sisi sote tuweze kuishi kwa upendo (1 Yohana 4:8).

Kanisa Katoliki linatueleza kuwa upendo ni kitu ambacho kinatoka kwa Mungu na kinapaswa kuongoza maisha yetu. Tunapaswa kuwapenda wenzetu kama tunavyojipenda wenyewe (Marko 12:31). Kwa hivyo, Kanisa Katoliki linatufundisha kufurahia upendo wa Mungu na kuwa na upendo kwa jirani yetu.

Katika kufuata njia ya upendo, Kanisa Katoliki pia linatufundisha kuhusu huruma. Huruma ni tendo la upendo ambalo linatupatia fursa ya kuonyesha upendo huo kwa wengine. Kama vile Mungu alivyotupatia huruma na msamaha kupitia Yesu Kristo, tunaweza pia kuwa na huruma kwa wengine.

Kwa kufuata kanuni za Kanisa Katoliki, tunapaswa kujitolea kwa wengine na kuwa tayari kuwasaidia wakati wanapohitaji msaada. Kwa kufanya hivyo, tunakuwa chombo cha upendo na huruma ya Mungu katika ulimwengu huu.

Kanisa Katoliki pia linatufundisha kuwa na huruma kwa wale wanaohitaji. Kama vile Yesu Kristo alivyowaonyesha huruma wenye shida, tunapaswa kuwa tayari kuwasaidia wale wanaohitaji msaada wetu. Kwa kufanya hivyo, tunakuwa vyombo vya upendo na huruma ya Mungu katika maisha yetu.

Kanisa Katoliki linatufundisha kuwa na huruma pia kwa wale ambao wametukosea. Kama vile Mungu alivyotupatia msamaha wetu kupitia Yesu Kristo, tunapaswa kuwa tayari kuwasamehe wale ambao wametukosea. Kwa kufanya hivyo, tunakuwa vyombo vya upendo na huruma ya Mungu katika ulimwengu huu.

Kwa kumalizia, Kanisa Katoliki linatueleza kuwa upendo na huruma ni muhimu sana kwa maisha yetu ya Kikristo. Kwa kufuata njia ya upendo na huruma, tunakuwa vyombo vya upendo na huruma ya Mungu katika ulimwengu huu. Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kuwa na upendo na huruma kwa wengine katika maisha yetu ya kila siku. Kama vile Catechism ya Kanisa Katoliki inatueleza, "Upendo ni roho ya maisha ya Kikristo".

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ndoa kama sakramenti ya agano la upendo na uaminifu?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ndoa kama sakramenti ya agano la upendo na uaminifu?

Ndio, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ndoa kama sakramenti ya agano la upendo na uaminifu. Kwa mujibu wa kanuni za Kanisa Katoliki, ndoa ni sakramenti ambayo inawezeshwa na Mungu kwa ajili ya wawili wanaokubali kwenda pamoja kwa maisha yao yote. Ndoa ina maana kubwa sana kwetu sote, kwani ni wakati ambapo tunaahidi kuwa na mtu mwingine maisha yetu yote.

Kama vile Kristo alivyohusisha sakramenti yake ya mwili na damu yake na Wakristo wake, vivyo hivyo ndoa inahusisha sakramenti ya upendo na uaminifu kati ya wawili wanaotaka kuwa pamoja maisha yao yote. Ndoa ina lengo la kuleta furaha, amani, na upendo kwa wawili hao, na kuunda familia ambayo inaishi kwa upendo na amani.

Ndoa ina thamani kubwa sana kwa Mungu, na ndio maana inahusishwa na agano la upendo na uaminifu. Katika agano hili, wawili wanakubali kuwa pamoja maisha yao yote, na kuahidi kuwa waaminifu kwa kila mmoja, kushirikiana katika matatizo na furaha, na kujenga familia ambayo inaishi kwa upendo na amani.

Katika Biblia, tunaona jinsi ndoa inavyopewa umuhimu mkubwa. Kwa mfano, katika Mwanzo 2:24, tunasoma "Kwa hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja." Hii inaonyesha jinsi Mungu alivyokusudia ndoa iwe kitu cha maana sana katika maisha yetu.

Kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, ndoa ina maana kubwa sana kwetu sote. Inasema kuwa ndoa ni "umoja wa maisha ya wanaume na wanawake, ambao unawekwa na Mungu mwenyewe, na ambao unapatikana kwa njia ya kujitolea kwa kila mmoja na kwa ajili ya ajili ya watoto." (Catechism ya Kanisa Katoliki, 1601).

Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha Ndoa kama sakramenti ya agano la upendo na uaminifu kwa sababu inajua jinsi muhimu ndoa ni katika maisha yetu. Ndoa inatuletea furaha, amani, na upendo, na inatufanya tuishi kwa amani na upendo na wale tunaowapenda. Tunapofuata kanuni za Kanisa Katoliki, tunaweza kuishi kwa amani na upendo na wale tunaowapenda, na kusaidia kujenga familia ambayo inaishi kwa upendo na amani.

Shopping Cart
28
    28
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About