Vyakula vya Kukuza nywele na kuzifanya ziwe na Afya

Kuwa na nywele zenye afya nzuri ni muhimu kwa wote bila kujali jinsi, hali hii husababisha wengi kutumia madawa ya aina mbalimbali ya kuhakikisha nywele zao zinastawi na kuwa na muonekano mzuri.
Kwa bahati mbaya, wengi waliotumia madawa yanayotengenezwa kwa kemikali hujikuta katika wakati mgumu siku za usoni wakikabiliwa na matatizo ya nywele kukatika na hata kupata madhara katika ngozi ya kichwa.

Njia bora na salama zaidi ya kustawisha nywele, kuzifanya ziwe na mvuto wa aina yake bila kujali wewe ni mtu wa asili ya bara Asia, Afrika au Marekani, ni kula vyakula vyenye virutubisho muhimu kwa afya ya nywele.

Vifuatavyo ni sehemu ya vyakula ambavyo hupatikana kirahisi barani Afrika na kwa bei nafuu, ambavyo vitakupa afya bora zaidi ya nywele zako.

1. Yai

Nywele za binadamu zina protini ambayo zimeumbiwa. Hivyo ni muhimu kuhakikisha kuwa zina protini ya kutosha, na hilo hufanyika kupitia vyakula. Protini ni nguzo kuu ya nywele za binadamu, na yai ni moja kati ya vyakula vyenye utajiri mkubwa wa protini. Hakikisha unakula yai angalau mara tatu kwa wiki.

2. Spinachi

Nywele zinahitaji madini ya chuma ili ziweze kuwa katika hali nzuri ya afya. Kukosekana kwa madini ya chuma husababisha nywele kunyonyoka. Mwili unapokosa madini ya chuma, hewa ya oxygen na virutubisho hushindwa kufika vizuri kwenye mizizi ya nywele hivyo hufanya nywele kuwa dhaifu na zisizo na muonekano mzuri.

Mboga za majani aina ya spinachi ni suluhisho, kwakuwa zina madini ya chuma kwa wingi ambayo seli za nywele huhitaji.

3. Jamii ya Machungwa, Limao

Mwili wa binadamu huhitaji vitamini C ambayo husaidia kuhuisha utendaji wa madini ya chuma. Hivyo, unapaswa kuongeza matunda ya jamii ya β€˜citrus’, kama vile machungwa, chenza, balungi na limao. Pia, unaweza kutumia na asali pamoja.

Vitamini C husaidia katika ukuaji wa nywele kusaidia usambaaji wa virutubisho na ukuaji wa haraka wa nywele.

4. Karoti

Ni muhimu sana kuhakikisha unakunywa juice ya karoti kila siku, kama unataka nywele zako zikue haraka zikiwa na mwonekano mzuri wenye afya. Vitamini A inayopatikana kwenye karoti ni muhimu sana kwa ukuaji wa seli za nywele. Kumbuka nywele zina tishu ambazo hukua haraka zaidi katika mwili.

Karoti ina mafuta asili yanayofahamika kama β€˜sebum’ na mizizi ambayo husaidia kukuza nywele kwa haraka.

5. Parachichi

Tunda aina ya parachichi lina kazi nyingi sana mwilini kama matunda mengine, lakini hili ni tunda la kipekee amnbalo lina utajiri wa vitamini E ambayo husaidia mzunguko wa damu na katika hilo husaidia mfumo wa ukuaji wa nywele kwa haraka.

Tunda hili husaidia kuhuisha na kurekebisha mafuta na kiwango cha PH (inayosafisha kemikalii mwilini) ambavyo kama vitazidi kwenye mwili vinaweza kusababisha kusimama kwa ukuaji wa nywele, yaani nywele hudumaa.

Kwa faida zaidi, vitamin E inayopatikana kwenye parachichi kwa wingi husaidia zaidi afya ya moyo wa binadamu na zaidi ngozi. Hakikisha unapata tunda hili kadiri iwezekanavyo.

Hivi ni baadhi tu ya vyakula na matunda kwa ukuaji mzuri wa nywele zako. Kama unatumia vizuri mlo wako, utakuwa adimu sana kutumia mafuta yenye kemikali ambayo yanaweza kukuletea madhara mabaya.

Jinsi ya kutengeneza Biskuti Za Tende

MAHITAJI

Unga – 4 Vikombe vya chai
Sukari ya laini (icing sugar) – 1 Kikombe cha chai
Baking powder – 2 Vijiko vya chai
Mayai – 2
Siagi au margarine – 1 Kikombe cha chai
Vanilla -1 Kijiko cha chai
Maziwa ya kuchanganyia – kiasi
Tende iliyotolewa koko – 1 Kikombe
ufuta (sasame) kiasi 1/4 kikombe

MAANDALIZI

Changanya unga, siagi, baking powder, na sukari katika mashine.
Kisha tia mayai, vanilla na halafu maziwa kidogo kidogo hadi mchanganyiko ushikamane.
Gawanya madonge mawili na usukume kama chapati, lakini sio nyembamba sana.
Tandaza tende robo ya duara na unyunyize ufuta duara zima: kisha kunja hadi mwisho na ukate kate, kisha upange katika trei ya kuvumbika.
Vumbika (bake) moto wa 350Β°F kwa muda wa dakika 20 au hadi vigeuke rangi na viwive.
Zikisha iiva ziache zipowe na zitakuwa tayari kuliwa.

Thamani ya Neno “Nimekusamehe”

Ni jambo jema kusamehe wale waliotukosea. Neno “Nimekusamehe” ni zuri kusikia masikioni kuliko neno “Ninakupenda”. Maana kusamehewa ni zaidi ya kupendwa kwani Msamaha ni matokeo ya Upendo.

Melkisedeck Leon Shine

Neno “Nimekusamehe”

Neno β€œNimekusamehe” ni moja ya maneno yenye nguvu kubwa sana katika lugha yoyote ile. Ni neno ambalo linabeba uzito wa moyo mzito uliojaa maumivu na hatimaye kuachilia mzigo huo. Ni jambo jema kusamehe wale waliotukosea, kwani msamaha unafungua milango ya amani na upatanisho.

“Kwa maana mkiwasamehe watu makosa yao, na Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi.” (Mathayo 6:14)
“Basi, vaeni kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, moyo wa rehema, utu wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu; mkichukuliana na kusameheana, mtu akiwa na neno juu ya mwenzake. Kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi.” (Wakolosai 3:12-13)
“Msameheane, na kwa maana hiyo msisahau jinsi Yesu Kristo alivyowasamehe ninyi, vivyo na ninyi msameheane.” (Waefeso 4:32)

Uzuri wa Kusamehewa

Neno β€œNimekusamehe” ni zuri kusikia masikioni kuliko neno β€œNinakupenda”. Maana yake ni kwamba, msamaha unaleta uzima wa moyo na uhuru wa ndani. Kila mtu anahitaji kusamehewa, na wakati mwingine msamaha una nguvu zaidi ya upendo wenyewe. Kwa maana kusamehewa ni zaidi ya kupendwa kwani msamaha ni matokeo ya upendo. Ni kupitia msamaha tunapata nafasi ya kuanza upya na kujenga mahusiano mapya yaliyojaa matumaini.

“Kwa maana nitatubia uovu wao, na dhambi yao sitaikumbuka tena.” (Yeremia 31:34)
“Naye asema, ‘Dhambi zao na uovu wao sitaukumbuka tena.'” (Waebrania 8:12) “Nanyi msifanye mambo ambayo mimi nimewaambia msifanye, bali ninyi pia msisahau kwamba, ikiwa ninyi mna uovu na msamaha, mimi pia ninasamehe na kuponya.”_ (Zaburi 103:3)

Msamaha: Daraja ya Upendo wa Kweli

Msamaha ni daraja inayoelekea kwenye upendo wa kweli. Bila msamaha, upendo hawezi kuwa kamili. Wakati tunapowapenda wengine, tunahitaji pia kujifunza kusamehe. Upendo usio na msamaha ni kama mti usio na mizizi, hauwezi kustawi na kuzaa matunda mazuri. Msamaha hufungua milango ya mawasiliano na kurejesha amani kati ya watu. Ni ishara ya kukubali udhaifu wa kibinadamu na kutambua kuwa sisi sote tunahitaji neema na rehema ya Mungu.

“Upendo hufunika wingi wa dhambi.” (1 Petro 4:8)
“Mwenye upendo huvumilia yote, huamini yote, hutumaini yote, hustahimili yote.” (1 Wakorintho 13:7)
“Kwa maana nimekasirika kiasi gani, kwamba nilipotaka huruma, ndipo nilipokasirika; lakini nikaachilia mbali upendo wangu, na hivyo nimesamehe.” (Mika 7:18)

Ukomavu Katika Imani na Msamaha

Kusamehe ni ishara ya ukomavu katika imani. Ni kuonyesha kwamba tumeelewa maana ya kweli ya upendo wa Kristo. Yesu alitufundisha umuhimu wa kusamehe kupitia maisha yake na kifo chake msalabani. Alisema, “Baba, uwasamehe, kwa kuwa hawajui walitendalo.” (Luka 23:34). Huu ni mfano wa hali ya juu kabisa ya msamaha na upendo. Tunapomwiga Kristo kwa kusamehe wengine, tunaonyesha kwamba tumezama katika upendo wake na tumeamua kufuata njia yake.

“Wakati Petro alipomwambia Yesu, ‘Bwana, nikisamehe ndugu yangu mara ngapi? Hata mara saba?’ Yesu akamjibu, ‘Sikuambii hata mara saba, bali hata saba mara sabini.'” (Mathayo 18:21-22) “Nanyi mtasameheani bure kama Bwana alivyosameheani ninyi, pia nanyi msameheani kwa bure.”_ (Wakolosai 3:13)
“Tafuteni amani na kila mtu, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao.” (Waebrania 12:14)

Kusamehe ni zawadi ya kipekee ambayo tunaweza kupeana sisi kwa sisi. Inahitaji unyenyekevu, uvumilivu, na upendo wa kweli. Tukumbuke kila siku kuwa na moyo wa kusamehe na kujenga mahusiano yenye msingi wa upendo na msamaha. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kuishi maisha yenye amani na furaha, tukifuata nyayo za Kristo ambaye alitufundisha maana ya kweli ya msamaha na upendo.

Jinsi ya kutengeneza Bisikuti Za Kaukau Na Kahawa (Cocoa Coffee Biscuits)

MAHITAJI

Maji baridi – kikombe 1

Biskuti za kawaida – paketi 2

Kaukau (cocoa) – vijiko 3 vya kulia

Kahawa ya unga – kijiko 1 cha kulia

Njugu mchanganyiko zilokatwakatwa – kikombe 1

Sukari – kiasi upendavyo

MAANDALIZI

Changanya maji na kaukau na kofi na sukari
Katakata biskuti kisha tia paketi moja na nusu uchanganye vizuri.
Kisha nusu ya biskuti zilobakia katakata vipande vikubwa na weka juu ya mchanganyiko, kisha changanya kidogo tu.
Weka katika foil paper na zungusha (roll)
Kisha fungua umwagie njugu au mkassaraat zilosagwa
Kisha roll katika foil paper na uweke katika freezer mpaka igande
Kisha kata kata slices na iko tayari

Jinsi ya Kutumia Bamia kuondoa chunusi Usoni

Wiki hii kwenye urembo tutaongelea mboga aina ya bamia jinsi inavyotibu chunusi na kuziondoa moja kwa moja. Mbali na chunusi, pia husababisha ngozi kuteleza na kuwa nyororo.

JINSI YA KUFANYA

Chukua bamia zikatekate vipande, ziweke kwenye brenda kisha chukua limao kipande na maji kidogo, weka kwenye brenda kisha saga. Baada ya kupata mchanganyiko wako upake usoni mpaka kwenye shingo, acha kwa muda likauke kisha bandua kama unavyoondoa maski nyingine usoni.

FANYA HIVI SIKU TATU KWA WIKI ITAKUSAIDIA KUONDOA CHUNUSI.

Jinsi ya kutengeneza Rock-cakes Za Njugu Na Matunda Makavu

Mahitaji

Unga – 4 Vikombe

Sukari -10 Ounce

Siagi – 10 Ounce

Mdalasini ya unga – 2 vijiko vya chai

Matunda makavu/njugu (kama lozi, Zabibu, maganda ya chungwa, Cherries na kadhalika – 4 ounce

Maziwa ya maji – 4 Vijiko vya supu

Maandalizi

Chukua siagi na sukari koroga na mixer mpaka iwe kama cream.
Tia vanilla mdalasini, tia yai moja mix tena endelea kuongeza yai lingine mpaka umalize yote, changanya mpaka iwe laini kama sufi (fluffy)
Tia unga na baking powder na dried fruits, changanya na mwiko.
Chota mchanganyiko na kijiko cha soup weka kwenye treya ya kupikia tandaza na uma ili upate matundu juu ya biskuti.
Pika (bake) kwenye oven lenye moto wa 375Β F. kwa muda wa dakika 15 hivi huku unazitazama tazama.

Jinsi ya kupika wali wa Tuna (samaki/jodari)

VIAMBAUPISHI VYA TUNA

Tuna (samaki/jodari) – 2 Vikopo

Vitunguu (kata kata) – 4

Nyanya zilizosagwa – 5

Nyanya kopo – 3 Vijiko vya supu

Viazi (vilivyokatwa vipande vidogo – cubes) – 4

Dengu (chick peas) – 1 kikombe

Kitunguu saumu(thomu/galic)&Tangawizi iliyosagwa 1 Kijiko cha supu

Hiliki – 1/4 kijiko cha chai

Mchanganyiko wa bizari – 1 kijiko cha supu

Chumvi – kiasi

Pilipili manga – 1 Kijiko cha chai

Vipande cha Maggi (Cube) – 2

VIAMBAUPISHI VYA WALI

Mchele – 3 Vikombe vikubwa (Mugs)

Mdalasini – 2 Vijiti

Karafuu – chembe 5

Zaafarani – kiasi
Jirsh (Komamanga kavu au zabibu kavu -raisins) – 1/2 Kikombe

JINSI YA KUANDAA

Kosha Mchele na roweka.
Kaanga vitunguu hadi viwe rangi ya hudhurungi (brown) chuja mafuta uweke kando.
Kaanga viazi, epua
Punguza mafuta, kaanga nyanya.
Tia thomu/tangawizi, bizari zote, vipande vya Maggi, nyanya kopo, chumvi.
Mwaga maji ya tuna iwe kavu, changanyisha kwenye sosi.
Tia zaafarani kidogo katika sosi na bakisha ya wali.
Chemsha mchele pamoja na mdalasini na karafuu.
Karibu na kuwiva, chuja maji utie katika chombo cha kupikia katika jiko (oven)
Nyunyizia zaafarani, mwagia vitunguu, viazi, na dengu juu ya wali.
Mwagia sosi ya tuna na pambia jirshi (au zabibu).
Funika wali na upike katika jiko moto wa 450ΒΊ kwa muda wa kupikika wali. Epua upakue.

Mapishi ya Pilau Ya Samaki Wa Tuna Na Mboga

Mahitaji

Mchele – 2 Mugs

Mboga mchanganyiko za barafu (Frozen veg) – Mug

Tuna (samaki/jodari) – 2 kopo

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi -2 vijiko vya supu

Garam masala – 1 kijiko cha supu

Nyanya – 2

Kitungu maji – 1

Mdalasini nzima – 2 vijiti

Karafuu – 6 chembe

Pilipili mbichi – 1

Chumvi – kiasi

Viazi – 3

Maji – 2 Β½ Mugs

Mafuta – 3 vijiko vya supu

Maandalizi

Osha mchele na uroweke kwa muda wa dakika 20
Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown).
Mimina viazi, thomu na tangawizi, bizari zote na kaanga.
Tia nyanya uliyokatakata ikaange mpaka iwive.
Tia tuna endelea kukaanga kidogo tu.
Tia maji, yatakapochemka tia mchele.
Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa Β½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari kuliwa.

Mapishi mazuri ya Wali Wa Kukaanga Kwa Kidari Cha Kuku

Vipimo vya Wali:

Mchele – 3 vikombe

*Maji ya kupikia – 5 vikombe

*Kidonge cha supu – 1

Samli – 2 vijiko vya supu

Chumvi kiasi

Hiliki – 3 chembe

Bay leaf – 1

Vipimo Vya Kuku

Kidari (chicken breast) – 1Kilo

Kitunguu – 1

Tangawizi mbichi – Β½ kipande

Kitunguu saumu(thomu/galic) – 7 chembe

Pilipili mbichi – 3

Ndimu – 2

Pilipilimanga – 1 kijiko cha chai

Mdalasini – Β½ kijiko cha chai

Jira/Cummin ya unga – 1 kijiko cha chai

Maji – ΒΌ kikombe

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Wali:

Osha na roweka mchele kisha weka sufuria katika moto tia samli ipashe moto.
Tia hiliki, bay leaf, kaanga, kisha tia mchele ukaange kidogo.
Tia maji, chumvi na kidonge cha supu, upike wali kama unavyopika pilau.
*Maji kisia kwa kutegemea mchele ulivyo.
*Unaweza kutumia supu yoyote badala ya kidonge.

Kuku:

Katakata kidari cha kuku vipande vya kiasi, weka katika sufuria, tia ndimu, bizari zote, chumvi.
Katakata kitunguu vipande vidogodogo, pilipili, na kitunguu thomu (chopped), tia katika kuku.
Chuna tangawizi mbichi tia katika kuku. Changanya vitu vyote vizuri.
Tia maji kiasi ΒΌ kikombe tu kiasi cha kumkaushia kuku. Weka katika moto mpike huku unageuzageuza. Anapokaribia kukauka epua akiwa tayari kuliwa na wali (na saladi upendayo)

Mapishi ya Pilau Ya Nafaka Na Nyama Ya Kusaga

VIAMBAUPISHI

Mchele – 3 vikombe

Nyama ya kusaga – 1 LB

Mchanganyiko wa Nafaka upendazo; maharagwe, njegere, mbaazi n.k 1 mug

Vitunguu maji kata vipande vipande – 3 vya kiasi

Kitunguu saumu(thomu/galic) na Tangawizi – 2 vijiko vya supu

Mafuta – Β½ Kikombe

Mchanganyiko wa bizari (Garam Masala) – 2 vijiko vya chai

Vipande vya supu (Maggi cubes) – 3

Maji (inategemea mchele) – 5

Chumvi – Kiasi

MAPISHI

Osha mchele na roweka.
Weka mafuta katika sufuria na kaanga vitunguu mpaka viwe brown.
Tia Thomu na tangawizi, kaanga kidogo.
Weka nyama ya kusaga, chumvi na garam masala, endelea kukaanga mpaka nyama iwive.
Mwaga maji yaliomo katika kopo la nafaka na utie nafaka pekee humo.
Tia maji na vipande vya supu (Maggi cubes) huku unavivuruga, koroga kidogo.
Tia mchele, koroga kidogo.
Funika na pika kwa moto mdogo mpaka karibu na kukauka ukikorogoka kidogo. (kama unavyopika pilau ya kawaida)
*Epua uipike katika moto wa oven 350-400 Deg kwa muda wa dakika 15.
*Kama sufuria uliyotumia sio ya kupikia katika oven, mimina katika chombo chochote kinachotumika kwa oven kama bakuli la pyrex au treya za foil.
Pakua katika sahani na iko tayari kuliwa.

Mapishi ya wali mtamu Wa Nazi Kwa Maharage Na Samaki Nguru Wa Kukaanga

Vipimo

Wali:

Mchele mpunga – 4 Vikombe

Tui la nazi – 6 vikombe

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Osha mchele weka kando.
Bandika tui jikoni likichemka tia mchele na chumvi.
Funika uchemke, tui likikauka wacha moto mdogomdogo hadi wali uive ukiwa tayari. Ikiwa unatumia mkaa unapalia juu yake.

Maharage Ya Nazi

Maharage – 3 vikombe

Tui la nazi zito – 1 kikombe

Tui la nazi jepesi – 1 kikombe

Kitunguu maji – 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) kilosagwa -1 kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Chemsha maharage mpaka yaive.
Katiakatia kitunguu maji na tia thomu, tia na tui jepesi kikombe kimoja.
Tia tui zito endelea kuweka katika moto mdogomdogo hadi yakaribie kukauka yakiwa tayari.

Samaki Nguru Wa Kukaanga

Samaki Wa Nguru – 4 vipande

Kitunguu saumu(thomu/galic) & tangawizi ilosagwa – 1 kijiko cha supu

Pilipili mbichi – 4

Ndimu – 2 kamua

Bizari ya samaki -1 kijiko cha chai

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Mwoshe samaki kisha mtie kitunguu thomu, tangawizi ilosagwa, chumvi, pilipilimbichi ilosagwa, ndimu na bizari ya samaki.
Mwache akolee viungo kwa muda kidogo.
Makaange katika mafuta hadi aive akiwa tayari.

Jinsi ya kupika vizuri Wali Wa Karoti Na Nyama

MAHITAJI YA WALI

Mchele – 3 Magi

Mafuta – 1/4 kikombe

Karoti unakata refu refu – 3

Vitunguu maji kata vikubwa vikubwa – 1 kikubwa

Pilipli manga – 1/2 kijicho chai

Hiliki – 1/2 kijiko chai

Karafuu ya unga – 1/4 kijiko cha chai

Mdalasini wa unga – 1/2 kijiko cha chai

Zaafarani (ukipenda) roweka katika maji – 1 kijiko cha chai

Zabibu kavu (ukipenda) – 1/4 kikombe

Chumvi kiasi

KUPIKA WALI

Kwenye sufuria tia mafuta na kaanga karoti kidogo.
Tia vitunguu kisha tia bizari zote.
Tia maji kiasi (kutegemea aina ya mchele) na chumvi
Tia mchele upike uwive.
Karibu na kuwvia tia zabibu ukipenda.
Funika endelea kuupika hadi uwive.

MAHITAJI KWA NYAMA

Nyama – 2 Ratili (LB)

Chumvi – Kiasi

Mafuta – 1/4 kikombe

Kitunguu (kata virefu virefu) – 1 Kikubwa

Pilipili mboga kubwa – 2 ukipenda moja nyekundu moja kijani unazikata vipande virefu virefu.

Figili mwitu (celery) kata vipande virefu virefu- Miche miwili.

KUPIKA NYAMA

Chemsha nyama hadi iwive
Ikaange kwa mafuta hadi iwe nyekundu
Weka vitunguu, pilipili mboga na figili mwitu
Kaanga kidogo tu kama dakika moja.
Tayari kuliwa na wali.

Mapishi ya Wali Wa Zaafarani Na Kuku Wa Kupaka

Vipimo

Wali:

Mchele – 3 Vikombe

Kitunguu kiichokatwa – 1

Pilipili boga nyekundu iliyokatwa vipande – 1

Mafuta – ΒΌ Kikombe

Zaafarani – 1 kijiko cha chai tia kwenye kikombe na maji robo roweka

Chumvi – 1 kiasi

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Katika sufuria, tia mafuta, kaanga kitunguu mpaka kiwe kidogo rangu ya udongo (brown)
Tia pili pili boga.
Tia mchele, kaanga kwa muda wa dakika 3, tia zaafarani na chumvi.
Tia supu uliyochemshia kuku iwe imoto.
Pika wali katika moto mdogo hadi uwive.

Kuku

Kuku Mzima -1

Mayai ya kuchemsha – 6

Namna Ya Kupika Kuku

Mchemshe kuku mzima na chumvi mpaka uhakikishe ameiva vizuri.
Mtowe na muweke pembeni. Supu yake tumia katika wali kama ilivyo hapo juuu.
Chemsha mayai, menya na kata vipande viwili kila yai moja weka kando

Vipimo Vya Sosi Ya Kuku Ya Nazi

Kitunguu – 1

Nyanya iliyokatwa vipande – 1

Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi – 1 kijiko cha supu

Garam Masala – Β½ kijiko cha supu

Bizari ya manjano – Β½ kijiko cha chai

Chumvi – kiasi

Pilipili masala ya unga – Β½ kijiko cha chai

Nyanya ya kopo – 1 kijiko cha supu

Nazi ya unga – 1 kikombe

Maji ya ukwaju – ΒΌ kikombe cha chai

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

Tia Mafuta vijiko 2 vya supu katika sufuria
Kaanga kitunguu maji mpaka kiwe rangi ya udongo (brown).
Tia thomu na tangawizi.
Tia nyanya nzima iliyokatwa katwa.
Tia garam masala, manjano, pilipili ya unga, nyanya ya kopo, kaanga vizuri.
Changanya kwenye sufuria na ukwaju. Iache ichemke vizuri.
Changanya nazi ya unga na maji vikombe viwili.
Mtie kuku mpike vizuri na hilo tui.
Mtie kwenye oveni kidogo.

Kupakuwa katika Sinia

Pakuwa wali kwanza katika sinia
Muweke kuku juu ya wali.
Pambia mayai

Utengenezaji wa Makalio ni Hatari na Hutakiwi kufanya

Mwanamke wa miaka mitatu amefariki baada ya kuripotiwa kuelekea Uturuki kwa aina ya upasuaji kwa jina Brazilian Butt Lift [uongezaji wa makalio}.

Ni kwa nini upasuaji huu ni maarufu mbali na kwamba ni hatari kufanyiwa upasuaji huo ughaibuni.

Leah Cambridge kutoka Leeds alipatikana na mishtuko mitatu ya moyo baada ya kudungwa sindano ya ganzi katika kliniki moja katika mji wa Izmir, mwenzake Scott Franks aliambia gazeti la the sun.

Anaeleweka kufanyiwa BBL ama upasuaji wa kuongeza makalio ambapo mafuta kutoka katika tumbo hutiwa katika makalio.

‘Mrembo huyo alikubali kufanya upasuaji ughaibuni ambapo ni bei nafuu ikilinganishwa na Uingereza baada ya kukerwa na mafuta mengi katika sehemu yake ya tumbo baada ya kupata watoto’, alisema bwana Frank.

Majirani wake wamemtaja kuwa mtu anayevutia, wakiongezea kuwa wanaamini alielekea kufanyiwa upasuaji huo mwezi uliopita bila kumshauri mpenziwe.

Na bi Cambridge sio mwanamke wa kwanza Muingereza ambaye hamu yake ya kuwa na makalio ya kuvutia yalimwangamiza akiwa ughaibuni.

Joy Williams alifanyiwa upasuaji wa kuongeza makalio yake mjini Bangkon nchini Thailand mnamo mwezi Octoba 2014.

Vidonda vyake vilipata maambukizi na mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 24 kutoka mjini London , alifariki akidungwa sindano ya ganzi.

Miaka mitatu kabla , Claudia Aderotimi mwenye umri wa miaka 20 , kutoka Hackney , mashariki mwa London alifariki kutokana na matibabu ya kujiongeza makalio yake katika hoteli moja nchini Marekani.

Upasuaji wa kuongeza makalio hauonekani kuwa hatari zaidi ya aina nyengine zozote za upasuaji, kulingana na daktari wa upasuaji wa urembo Bryan Mayou.

‘Hatari yake ni upasuaji huo kufanywa na madaktari ambao hawajahitimu, nje ya kliniki bila kuwa na maelezo ya jinsi ya kujichunga baada ya matibabu hayo kufanywa’, anasema bwana Mayou, mwanachama wa muungano wa madaktari wa upasuaji nchini Uingereza.

Iwapo mafuta yataingizwa katika tishu ya sehemu ya makalio kuna hatari ya kuingiza mafuta hayo katika mishipa mikubwa ya damu.

Mafuta hayo yanaweza kupita katika mishipa ya damu , kuingia katika mapafu kabla ya kusababisha kifo.

Bwana Frank aliambia gazeti la The sun : Leah alikuwa amedungwa sindano ya ganzi akakumbwa na matatizo baada ya mafuta kuingia katika mishipa yake ya damu hatua iliofanya viwango vyake vya oxygen katika damu kushuka .

Hali yake iliimarishwa lakini alikumbwa na mishtuko mitatu ya moyo na hawakuwa na la kufanya.

‘Madaktari wa upasuaji kutoka jamii za kimataifa wameunda jopo kuchunguza kuripoti kuhusu utaratibu huo”, anasema Mayou.

‘Viwango vya vifo vinavyotokana na utaratibu huo ni kisa kimoja kati ya 3000 huku vifo vyote vilivyochunguzwa vikihusisha mafuta yaliopatikana ndani ya mishipa ya misuli ya makalio’, anasema.

Ni mtindo wa kisasa, miaka kadhaa iliopita kila mtu alipendelea kuwa mwembamba na walikuwa wakisema kuwa wanataka kufanyiwa upasuji ili kufanya makalio yao kuwa madogo.

‘Na hiyo ndio mbinu ambayo inaweza kutumika iwapo mtindo mpya wa kuongeza makalio utakwisha na mwathiriwa anataka makalio yake kurudishwa yalivyokuwa’, anasema.

Kwa nini watu wanapendelea sana kuwa na makalio makubwa ? ni kutokana na utamaduni maarufu wa kushabikia maungo yanayovutia.

Watu maarufu kama vile Kim Kardashian , Kylie Jenner na Cardi B wana umaarufu mkubwa katika mitandao ya kijmaii ambapo huchapisha picha zao wakionyesha makalio yao yalio mviringo.

Jenner alichapisha katika blogi yake ambapo alisifu maumbile yake na uzani ulioongezeka.

”Sijaongezewa makalio. Unajua, nilikuwa na uzani wa 120 [lbs]. Nilikuwa mwembamba sana. Sasa nianelekea 136Ibs , lakini ni sawa napendelea uzani nilionao”.

Hatahivyo, Cardi B amefichua kwamba kabla ya kuingia katika fani ya muziki aliongezewa makalio huko mjini New York na kifaa alichowekewa ndani kilivuja kwa siku tano baadaye.

Katika mahojiano alisema kuwa alilipa takriban $800 (Β£564) kwa upasuaji huo baada ya kuwaona wachezaji densi wanzake walio uchi katika vilabu vya burudani walio na makalio makubwa wakipata fedha nyingi kumliko.

Chloe Simms, ambaye ni nyota wa kipindi cha runinga cha The Only Way Is Essex, amekuwa wazi kuhusu makalio yake aliyoongezewa baada ya kulalamika katika kipindi hicho kwamba alikuwa hana makalio.

Kumtafuta Mungu ni Jukumu lako Binafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na nafsi yake. Huwezi kumfuata Mungu kwa kufwata njia ya wengine. Njia yako ya kukuwezesha kumfikia Mungu ni tofauti na wengine, Kwa maana Mungu amemwita kila mtu kwa namna ya kipekee.

Melkisedeck Leon Shine

Kumtafuta Mungu: Jukumu la Mtu Binafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na nafsi yake. Kila mmoja wetu ana safari ya kiroho inayomwita kumtafuta Mungu kwa njia yake mwenyewe. Safari hii ni ya kipekee na haifanani na ya mwingine yeyote. Mungu anatuita kila mmoja wetu kwa namna ya kipekee, akitufundisha na kutuongoza kupitia maisha yetu binafsi. Kumtafuta Mungu si jambo la jumuia au kanisa, bali ni uamuzi wa kibinafsi unaohitaji moyo wa kujitolea na utayari wa kipekee.

“Nitajitokeza kwenu, nanyi mtaniona; nanyi mtakaponiomba, nitasikiliza.” (Yeremia 29:12-13)
“Wakati unapotaka kujua mambo ya Mungu, basi mpe nafasi, naye atakujulisha siri zake.” (Amosi 3:7)
“Ee Mungu, Mungu wangu, nakutafuta asubuhi; roho yangu inakuonea kiu, mwili wangu unakutamani, katika nchi kame na yenye kuia, isiyo na maji.” (Zaburi 63:1)

Njia ya Kipekee ya Kumtafuta Mungu

Huwezi kumfuata Mungu kwa kufuata njia ya wengine. Ingawa tunaweza kupata mwongozo na msaada kutoka kwa wale walio karibu nasi katika jumuia au kanisa, ni muhimu kutambua kuwa kila mtu ana njia yake ya kumfikia Mungu. Njia yako ya kukuwezesha kumfikia Mungu ni tofauti na wengine. Hii ni kwa sababu Mungu amemwita kila mtu kwa namna ya kipekee. Katika ulimwengu huu wa tofauti na utofauti, Mungu anazungumza nasi kwa njia ambazo zinaendana na maisha yetu binafsi na hali zetu za kipekee. Hili ni jambo la kibinafsi na si suala la jumuia au kanisa.

“Kwa maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu, asema Bwana.” (Isaya 55:8)
“Pendo la Mungu limemiminwa mioyoni mwetu na Roho Mtakatifu tuliyekirimiwa.” (Warumi 5:5)
“Mmoja na mmoja wenu, ajaribu sana kutafuta kibali mbele za Bwana, kwa moyo wote, maana hatuwezi kumpendeza Mungu bila imani.” (Waebrania 11:6)

Kutembea Katika Wito Wako

Mungu anatuita kila mmoja wetu kwa namna ya kipekee. Kila wito unaambatana na vipawa, changamoto, na fursa ambazo ni za kipekee kwa kila mmoja wetu. Kwa hivyo, ni muhimu kumsikiliza Mungu katika maisha yako na kutembea katika wito wako binafsi. Hii inamaanisha kujifunza kusikiliza sauti ya Mungu katika maombi, kusoma Neno lake, na kutafakari juu ya maisha yako. Kutembea katika wito wako ni hatua ya kibinafsi inayohitaji kujitolea na uwazi wa moyo.

“Bali nyote mtakuja kwa njia ya utulivu na kunyamaza; na mtafakari kwa utulivu wa moyo, ndipo mtakapoona nuru ya Bwana.” (Isaya 30:15)
“Jitoe kwa Bwana, na umetulie mbele zake; nawe atakupatia maombi ya moyo wako.” (Zaburi 37:4)
“Naye atatenda katika njia zako, atakuongoza kwa haki na njia zake zote.” (Mithali 3:6)

Umuhimu wa Maombi na Tafakari

Kumtafuta Mungu kunahitaji muda wa maombi na tafakari. Huu ni wakati wa kuwa kimya mbele za Mungu, kumwambia mahitaji yako, na kumsikiliza. Maombi ni mazungumzo na Mungu, na ni katika mazungumzo haya tunapopata mwongozo wa kiroho. Tafakari juu ya Neno la Mungu na jinsi linavyohusiana na maisha yako binafsi ni muhimu katika safari hii ya kiroho. Hili ni jukumu la kibinafsi, ambalo linaweza kufanyika vyema wakati unapotenga muda maalumu kuwa peke yako na Mungu.

“Basi, kesheni, mkiomba kila wakati, ili mweze kuokoka mambo haya yote yatakayotokea, na kusimama mbele ya Mwana wa Adamu.” (Luka 21:36)
“Kwa maana mkimtafuta kwa bidii mtampata, mkimtafuta kwa moyo wenu wote.” (Yeremia 29:13)
“Jilindeni, ninyi wenyewe, na usiache moyo wako upotee, bali mwombe Mungu kwa bidii, naye atakujulisha mapenzi yake.” (Yakobo 1:5)

Kusikiliza Sauti ya Mungu

Mungu anaweza kuzungumza nasi kwa njia nyingi tofauti. Anaweza kuzungumza kupitia Neno lake, kupitia watu wengine, au kupitia matukio katika maisha yetu. Ni muhimu kuwa na moyo wazi na kusikiliza kwa makini sauti ya Mungu. Unapokuwa na utayari wa kusikiliza na kufuata mwongozo wake, utaona njia zako zikifunguka na kupata mwanga mpya wa kiroho. Hii ni safari ya kibinafsi inayohitaji kujitoa na kuwa na moyo wa kusikiliza.

“Kwa maana Mungu hunena mara moja, Naam, hata mara mbili, lakini mwanadamu hajali.” (Ayubu 33:14)
“Ee Bwana, unayenifundisha na kuniongoza kwa njia ya haki, unayenipenda kwa upendo wa milele.” (Zaburi 32:8)
“Ee Mungu, unayejua kila kitu, unayejua kwamba nakupenda. Unayejua kwamba nakutafuta kwa moyo wote.” (Yohana 21:17)

Kumtafuta Mungu ni Jukumu la Kibinafsi

Kumtafuta Mungu ni jukumu la mtu binafsi na si suala la jumuia au kanisa. Mwisho wa siku, kila mmoja wetu atahitajika kusimama peke yake mbele za Mungu na kutoa hesabu ya maisha yake. Hatutaweza kutumia njia za wengine kama kigezo cha safari yetu ya kiroho. Ni muhimu kuchukua jukumu la kumtafuta Mungu kwa bidii na moyo wote, kwa kuwa hatimaye, ni uhusiano wetu binafsi na Mungu ndio utakaotupa uzima wa milele.

“Kwa maana kila mmoja wetu atatoa habari zake mwenyewe mbele za Mungu.” (Warumi 14:12)
“Usiwe na hofu, maana mimi nipo nawe; usishike, maana mimi ndimi Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia; naam, nitakushika kwa mkono wangu wa kuume wa haki.” (Isaya 41:10)
“Lakini wewe, unaposali, ingia katika chumba chako, funga mlango na umwombe Baba yako aliye sirini. Na Baba yako aonaye sirini atakupa.” (Mathayo 6:6)

Katika safari ya kumtafuta Mungu, kumbuka kwamba ni jukumu lako binafsi na nafsi yako. Usijaribu kufuata njia ya mwingine, bali tembea katika njia yako binafsi ambayo Mungu ameiweka mbele yako. Kwa kufanya hivyo, utaweza kumfikia Mungu kwa undani na kujenga uhusiano wa kipekee na wa kweli naye. Kumtafuta Mungu si jambo la jumuia au kanisa; ni mwito wa ndani unaohitaji kujitoa na kuwa tayari kusimama peke yako mbele za Mungu.

Jinsi ya kupika Wali Wa Kichina wa mboga mboga Na Mayai

Viambaupishi

  1. Mchele (Basmati) – 3 vikombe
  2. Mbogamboga za barafu (karot, njegere, spring beans na mahindi) – 1 kikombe
  3. Kuku Kidari – 1 LB (ratili)
  4. Mayai – 2 mayai
  5. Vitunguu (vikubwa) – 2 au 3 vidogo
  6. Pili pili manga – 1 kijiko cha chai
  7. Paprika – 1 kijiko cha chai
  8. Chumvi – Kiasi
  9. Mafuta – 1/3 kikombe cha chai
  10. Kitunguu saumu(thomu/galic) – 1 kijiko cha supu
  11. Tangawizi – 1 kijiko cha chai
  12. Kidonge cha supu – 1
  13. Soy sauce – 2 vijiko vya supu

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika Kuku

Kata kidari cha kuku vipande vidogo vidogo vya kiasi.

Tia mafuta kidogo katika wok (karai ya kichina)

Kisha mtie kuku, thomu, tangawizi, soy sauce, pilipilimanga, paprika chumvi.

Tia mboga za barafu, kidonge cha supu, kaanga kuku na mboga viwive yitu vyote na mchanganyiko ukauke.

Namna Ya Kutayarisha Na kupika Wali

Roweka mchele wa basmati kwa muda wa saa au zaidi.

Halafu chemsha mchele pamoja na chumvi

Wacha uchemke asilimia 70%

Chuja maji na weka kando

Katika sufuria, tia mafuta kidogo tu

Kisha tia mayai mawili ukaange haraka haraka (crumbled egg)

Changanya mchanganyiko wa kuku na mboga

Kisha tia wali changanye vizuri

Rudisha katika moto, funika upikike kidogo hadi uive

Kisha pakua katika sahani na tolea na mayai ya kuchemsha ukipenda.

Jinsi ya kupika Biriyani Ya Nyama Ng’ombe

Viambaupishi Vya Masala

Nyama vipande – 3 LB

Mtindi – Β½ kopo

Kitunguu (thomu/galic) – 1Β½ kijiko cha supu

Tangawizi – 1Β½ kijiko cha supu

Nyanya – 2

Pilipili mbichi – kiasi

Nyanya kopo – 4 vijiko vya supu

Vidonge supu – 2

Pilipili nyekundu paprika – kiasi

Bizari zote saga – 2 vijiko vya supu

Viazi – 4

Mafuta – 2 mug

Samli – Β½ kikombe

Vitungu – 6

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika masala

Kwenye sufuria tia nyama, saga nyanya na thomu, pilipili mbichi, tangawizi. Mimina kwenye nyama na mtindi, tia na nyanya kopo, bizari paprika, vidonge vya supu, chumvi kisha changanya vyote pamoja weka motoni.
Katika sufuria nyengine tia mafuta na samli kaanga vitungu mpaka viwe rangi ya hudhurungi toa weka pembeni.
Kanga viazi weka pembeni.
Chukua mafuta kidogo uliyokangia tia kwenye nyama acha katika moto wa kiasi mpaka nyama iwive na maji ya punguke.
Tia viazi na vitunguu vivunje vunje tia ndani ya nyama acha moto mdogo.

Vipimo Vya Wali

Mchele – 5 mug

Maji – kiasi

Chumvi – kiasi

Mafuta uliyokaanga vitungu – kiasi

Rangi ya biriani – ΒΌ kijiko cha chai

*Zafarani – Β½ kijiko cha chai

*roweka rangi na zafarani

Namna Ya Kutarisha Na Kupika Wali

Osha mchele roweka muda wa saa.
Chemsha maji kama magi 10 hivi na chumvi tia mchele.
Uache uchemke ukishaiva kiini nusu, mwaga maji chuja.
Mimina juu ya nyama tia rangi na mafuta kwa juu funika.
Aacha kidogo katika oveni kwa muda wa dakika 20 hivi kisha epua ikiwa tayari.

Makusudi ya Mungu kwa Kila Binadamu

Mungu anamakusudi na kila binadamu anayeishi duniani. Hakuna mtu aliyebora zaidi mbele ya Mungu au asiye wa thamani mbele ya Mungu kama anafwata mpenzi ya Mungu.

Melkisedeck Leon Shine

Makusudi ya Mungu kwa Kila Binadamu

Mungu ana makusudi na kila binadamu anayeishi duniani. Hakuna mtu aliyebora zaidi mbele ya Mungu au asiye wa thamani mbele ya Mungu kama anafuata mapenzi ya Mungu. Mungu ametuumba kwa upendo wake mkuu na kila mmoja wetu ana nafasi maalum katika mpango wake wa milele. Kila binadamu ana thamani isiyo kifani machoni pa Mungu, na kila mmoja amepewa wajibu na wito wa kipekee katika maisha yake.

“Maana najua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.” (Yeremia 29:11)
“Kwa maana sisi tu kazi yake, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende matendo mema, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili tuenende nayo.” (Waefeso 2:10)
“Basi, enendeni ulimwenguni kote, mkahubiri Injili kwa kila kiumbe.” (Marko 16:15)

Hakuna Aliye Bora Zaidi Mbele ya Mungu

Hakuna mtu aliyebora zaidi mbele ya Mungu au asiye wa thamani mbele ya Mungu kama anafuata mapenzi ya Mungu. Mungu hana upendeleo; anatupenda sote kwa usawa na kwa upendo usio na mipaka. Hii ina maana kwamba haijalishi cheo, utajiri, au hali yako ya kijamii, mbele za Mungu, sote tuna thamani sawa. Mungu anatupenda kwa jinsi tulivyo, na anatuona kuwa wa maana sana katika mpango wake wa wokovu.

“Kwa maana hakuna upendeleo kwa Mungu.” (Warumi 2:11)
“Mungu hatendi kwa mapendeleo; bali katika kila taifa mtu amchaye na kutenda haki hukubaliwa na yeye.” (Matendo 10:34-35)
“Kwa maana nyote mmekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani katika Kristo Yesu. Hakuna Myahudi wala Myunani, hakuna mtumwa wala huru, hakuna mwanamume wala mwanamke, kwa maana nyote mmekuwa mmoja katika Kristo Yesu.” (Wagalatia 3:26, 28)

Thamani ya Kila Mtu Mbele ya Mungu

Kila mmoja wetu ana thamani kubwa mbele ya Mungu. Katika maisha yetu ya kila siku, ni muhimu kutambua kwamba thamani yetu haipimwi kwa viwango vya kidunia, bali kwa jinsi tunavyoishi na kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu. Tunapofuata njia za Mungu, tunaonyesha thamani yetu halisi kama watoto wa Mungu. Mungu anatuita sote kumjua na kumpenda, na kwa kufanya hivyo, tunaonyesha thamani yetu mbele zake.

“Kwa kuwa mlilipwa kwa thamani. Kwa hiyo, mtukuzeni Mungu katika miili yenu.” (1 Wakorintho 6:20)
“Lakini ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita kutoka gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.” (1 Petro 2:9)
“Kwa maana Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa Mwanawe wa pekee, ili kila amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.” (Yohana 3:16)

Kujua Makusudi ya Mungu Katika Maisha Yetu

Ili kutimiza makusudi ya Mungu katika maisha yetu, ni muhimu kujua na kuelewa mapenzi yake. Hii inajumuisha kusoma Neno la Mungu, kuomba, na kutafakari juu ya maisha yetu ya kiroho. Mungu ana mpango maalum kwa kila mmoja wetu, na ni jukumu letu kumtafuta na kuuelewa mpango huo. Tunapojitahidi kujua na kufuata mapenzi ya Mungu, tunapata furaha ya kweli na amani ndani ya mioyo yetu.

“Jifunzene kuwa wenye subira, ili mpate kuyatimiza mapenzi ya Mungu na hivyo kupokea ahadi zake.” (Waebrania 10:36)
“Ee Mungu, nifundishe njia zako, nitafakari njia zako zote; unitegemeze, nami nitaheshimu amri zako.” (Zaburi 119:33-34)
“Katika moyo wangu nimeficha maneno yako, nisije nikakutenda dhambi.” (Zaburi 119:11)

Kufuata Mapenzi ya Mungu

Kufuata mapenzi ya Mungu ni muhimu sana katika safari yetu ya kiroho. Tunapofuata mapenzi ya Mungu, tunapata nguvu na mwongozo wa Roho Mtakatifu katika maisha yetu. Hii inatusaidia kukua kiroho na kutimiza wito wetu wa kipekee. Mungu anatupa neema na nguvu ya kuishi kulingana na mapenzi yake, na ni jukumu letu kujitolea na kujitahidi kumfuata katika kila jambo.

“Tazama, mimi nalikuja; katika chuo cha kitabu imeandikwa habari zangu; nifanye mapenzi yako, Ee Mungu wangu; ndiyo furaha yangu, na sheria yako imo moyoni mwangu.” (Zaburi 40:7-8)
“Basi, kama mlivyopokea Kristo Yesu Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye; wenye mizizi na kujengwa ndani yake, na kuthibitishwa katika imani, kama mlivyofundishwa, mkizidi kutoa shukrani.” (Wakolosai 2:6-7)
“Maana ndiyo mapenzi ya Mungu, kutakaswa kwenu, kwamba mjiepushe na uasherati.” (1 Wathesalonike 4:3)

Kwa hivyo, tujitahidi kila siku kujua na kufuata mapenzi ya Mungu, tukijua kwamba kila mmoja wetu ana thamani kubwa mbele za Mungu na ana nafasi maalum katika mpango wake wa milele. Kila hatua tunayochukua katika kumtafuta na kumfuata Mungu inatufanya kuwa karibu naye na kutimiza makusudi yake katika maisha yetu. Mungu anatupenda kwa upendo wa milele, na sote tunaweza kupata furaha na amani ya kweli tunapojitolea kumfuata na kuishi kulingana na mapenzi yake.

Mapishi ya Wali Wa Kichina Wa Kamba Na Kuku

MAHITAJI

Mchele wa pishori (basmati) – 4

Nyama ya kuku bila mafupa – 1 Lb

Kamba saizi kubwa – 1Lb

Mchanganyiko wa mboga – njegere, karoti,

mahindi, maharage ya kijani (spring beans) – 2 vikombe

Figili mwitu (Cellery) – 2 mche

Vitunguu vya majani (spring onions) – 4-5 miche

Kebeji – 2 vikombe

Pilipili ya unga nyekundu – 1 kijiko cha chai

Pilipili manga ya unga – 1 kijiko cha chai

Sosi ya soya – 3 vijiko vya supu

Mafuta – 1/4 kikombe

Chumvi – kiasi

MAPISHI

Osha na roweka mchele.
Tia kamba chumvi na pilipili nyekundu ya unga. Tia mafuta vijiko viwili katika kikaango (frying pan), kaanga kamba kidogo tu, weka kando.
Katakata kuku vipande vidogo vidogo, tia chumvi na pilipili manga. Kaanga kaTika kikaango (ongeza mafuta kidogo) Weka kando.
Katika karai, tia mafuta kidogo kama vijiko vitatu vya supu, tia kamba na kuku, tia mboga za mchanganyiko, sosi ya soya na chumvi, kaanga kidogo. (Kama mboga sio za barafu) itabidi uchemshe kidogo.
Katakata kebeji, figili mwitu (cellery) na vitunguu vya majani (spring onions) utie katika mchaganyiko. acha kwa muda wa chini ya dakika moja katika moto.
Chemsha mchele, tia mafuta kidogo au siagi, chumvi upikie uive nusu kiini, mwaga maji uchuje.
Changanya vyote na wali rudisha katika sufuria au bakuli la oveni, funika na upike kwa moto wa kiasi kwa muda wa dakika 15-20 takriban.
Epua na upakue katika sahani ukiwa tayari kuliwa.

Shopping Cart
🏠 Home πŸ“– Reading πŸ–ΌοΈ Gallery πŸ’¬ AI Chat πŸ“˜ About