Visa Vya Sikukuu Hii
Angalia huyu mtoto anachomjibu baba yake baada ya kutoka kwenye mtihani
BABA: mwanangu kwenye huu mtihani uliofanya natumaini utafanya vizuri.
DOGO: ndio baba nitapata mia kwa mia.
BABA: kwanini unasema hivyo?.
DOGO: kwasababu jana kanisani tulifundishwa “Yesu ni jibu” kwahiyo kote nimejaza Yesu.
BABA: kwel kazi ipo
JE UNGEKUWA WEWE HUYO NDO MWANAO UNGEMFANYAJE?
Wasichana wafupi wanafurahisha
Wasichana wafupi wananifurahisha sanaโฆ. Yaan siku ya Valentine, wakivaa magauni mekundu huwa wanakuwa kama Fire extinguishers au mitungi ya Oryx ๐๐๐๐๐
Sitasahau mwaka huu
Sitasahau mwaka ule ambapo nilipeleka barua ya maombi yangu ya kazi kwenye kampuni moja maarufu. Wakati nasubiri majibu siku moja nikaenda kwa mama ntilie kununua maandazi akanifungia vizuri, kufika nyumbani hamu yote ya maandazi iliniishia pale nilipogundua karatasi iliyofungiwa maandazi ni barua yangu ya kuombea kazi๐๐
Baada ya kunitumia SMS usiku ikawa hiviโฆ.
Jana usiku kuna Jirani yangu..kanitumia text “mambo vipi?”โฆhalafu tunakaa nae mtaa mmoja nikaona nikimjibu ni uharibifu wa hela nikaenda kumgongea mlango saa 7 usiku. Alipofungua nikamjibu “shwari”halafu nikarudi nyumbani kulala zangu..
Sipendagi kuchezea salio..
๐๐๐๐๐
Kilichotokea baada ya mzungu na mbongo kukaa siti moja, bongo wasanii wengi
Mzungu akamdharau sana Mbongo nakujiona anajua kila kitu duniani!,
Akamwambia Mbongo waulizane maswali na Mbongo akishindwa anatoa sh.500 na endapo yeye atashindwa atatoa 100,000/=.
Mzungu akauliza ni nchi ipi ilishindwa kwenye vita kuu ya kwanza ya Dunia?
Mbongo akatoa 500 kuashiria hajui.
Na yeye akamuuliza Mzungu ni kitu gani kikienda juu kina miguu minne na kikirudi chini kina miguu mitatu?
Mzungu akafikiria akakosa jibu akatoa 100,000/= kuashiria hajui ila akataka kujua, akauliza ni nini hicho?
Mbongo akatoa 500 kuashiria hata yeye hajui!.
SHARE na marafiki kama umemkubali Mbongo kwa ujanja. Lakini unafikiri Mbongo huyu kwa akili hizi atakuwa ametokea mkoa gani!?.
Jinsi nilivyogundua kuwa nina kipaji leo
LEO NIMEPITA MTAA FULANI NIKAKIMBIZWA NA MBWA, NDIO NIKAJUA NINA KIPAJI KINAPOTEA TUโฆโฆโฆ
SIO CHA KUKIMBIA, NI KUPIGA KELELE๐๐๐๐๐๐
Huyu mtoto kaongea point kweli, angalia anachomwambia baba yake
Mtoto alimwuuliza baba yake,
Mtoto: Baba unaweza kumwachia hilo gari lako house boy/girl akaliendesha?
Baba: siwezi kumwachia gari langu hili aliendeshe ni ghali sana.
Mtoto: je mnaweza kumwachia chumba chenu house boy/girl kikiwa wazi na mkaenda kazini?
Baba: haiwezekani kamwe kuna vitu vya gharama na pia heshima haitakuwepo.
Mtoto: unaweza ukampa house boy/girl ATM CARD yako na namba ya siri ukakuchulie pesa?
Baba: mtoto unatafuta balaa sasa, unataka siku akiiba hii card akachukue pesa zote tuwe maskini, sithubutu.
Mtoto: aahaaaaaa, kumbe hauwezi kumkabidhi chochote chenye thamani house boy/ girl, sasa kwa nini mnanikabidhi mimi kwa house boy/girl na nyie mnaenda kazini mpaka mnarudi kumbe mimi sina thamani kwenu eeeeh!
Sifa mbaya: Cheki kilichompata huyu mwanaume mpenda sifa
SIFA MBAYAโฆ
Jamaa alikuwa ndani ya daladala Mara simu ikaita alikuwa ni mkewe kwa sifa jamaa akaweka loud speaker ili watu wasikie wanavyopendana.
JAMAA;wife Mara hii umenimiss jaman
WIFE; kwa nini umekunywa uji wa mtoto?!!!
๐๐๐๐๐
Kwa nini watu hawapendi hesabu!! Sababu hii hapa!
Sababu ni hii
AL-SHABAB
AL-QAEDA
Kwenye MATHEMATICS pia kuna kundi linaitwa
“AL-GEBRA”
๐๐๐๐
๐ถ๐ป๐ถ๐ป๐ถ๐ป๐ถ๐ป๐ถ๐ป๐ถ๐ป
Kumbe ndo maana wengine hawapendi hesabu coz kuna element za ugaidi
Nilichomfanyia huyu aliyenizingua nilipomuazimisha pasi
๐๐๐๐๐๐
Jana nimeenda kuazima pasi chumba jirani, ili ninyooshe nguo zangu, Jamaa wakaniambia nichukue nguo nikanyooshe room kwao maana hawataki pasi yao itoke.
Sasa leo amekuja mmoja wao kuazima mopper akasafishe room, nimemwambia aje adekie humu humuโฆ
Jamaa ameondoka nadhani atakua ameenda kuchukua maji
๐ค๐ค๐ค
Askari na yeye kumbe muoga, cheki anachomjibu afande
Askari wametumwa nyumba iliyokuwa kuna ugomvi wakafika wakatakiwa kuripoti kwa njia ya simu juu ya walichokikuta
ASKARI: Mkuu tumekuta mama mwenye nyumba kampiga mumewe chuma cha kichwa na kumuumiza vibaya sanaa
AFANDE: Kha! kisa mkasa mpk akafanya hivyo
ASKARI: Mama mwenye nyumba alikua anapiga deki mumewe akaingia ndani viatu kabla sakafu haijakauka
AFANDE: Sasa mmesha mkamata huyo mwanamke
ASKARI: Bado mkuu
AFANDE: Kha! sasa mnangoja nini
ASKARI: Si tunangoja sakafu ikauke
MAMBO KUMI YA KUFURAHISHA NA HUWEZI KUYAFANYA
1. Huwezi kuosha Macho kwa Sabuni;
2. Huwezi kuhesabu Nywele zako;
3. Huwezi kupumua kwa Pua na huku umetoa Ulimi;
4. Unajaribu kufanya namba 3
6. Umeona inawezekana, sanasana unakuwa Kama Jibwa;
7. Unatabasamu kwa kuwa umejiona Mjinga!
8. Umeruka namba 5;
9. Unahakikisha Kama kweli 5 haipo.
10. Unacheka kwa kuwa nimekubamba!
Kilichompata huyu jammaa baada ya simu yake kuita msikitini
Jamaa alisahau kuzima simu akiwa msikitini anaswali GHAFLA simu ikaita akaingiza mkono ili aikate, kwa bahat mbaya akaminya cha kupokelea, alipohangaika kuzima akajikuta kaminya laudspika ikasikika sauti ‘ETI HONEY UMESEMA NIWEKE KITIMOTO KIASI GANI? ๐๐๐๐๐๐๐
Huu ndio uhondo na raha ya kupanda daladala wajameni
Wasiopanda dalaladala wanakosa uhondo wa kauli hizi
1. nitakupa
2. Atapewa mbele
3. Hujapewa mbele?
4. Utapewa nyuma
5. Nitakupa nikikaa vizuri
6. Ngoja isimame nikupe
7. subiri asimamishe nikupe
8. hivi nlivyo kaa ntakupaje?
9. Utapewa tulia
10. Nikupe mara ngapi?
Angalia huyu mwalimu alichomfamya huyu mwanafunzi
*Hadith ya Shemdoe na Mwalimu wa English:*
*Teacher:* `Who is a pharmacist?`
*Shemdoe:* ๐๐ฟ _(raised up his hand.)_
*Teacher:* `So itโs only Shemdoe that can tell who a pharmacist is in this class? Thus, no body else to answer the question except Shemdoe?`
_(There was no reply from the students)_
*Teacher:* `Ok. now Shemdoe, chukua hii fimbo, charaza vilaza hawa wote kila mmoja viboko 3.`
*Shemdoe* _(akiwa amevimba kichwa, akawatwanga viboko vitatu vitatu vya kushiba darasa nzima)_
*Teacher:* `Now, my dear Shemdoe tell this dumb students, who a pharmacist isโฆ?`
*Shemdoe:* `Yes, sir. a Pharmacist is a farmer who assists people.`
_*Shemdoe sasa hivi amelazwa MOI kwa wataalam wa mifupa*_๐๐๐
Simu ilivyozua utata
Mama alichukuwa simu akampa mwanawe. Mama..Mpigie babako mwambie chakula tayari. (Mtoto akachukuwa na kupiga) MtotoโฆMama simu ya baba imepokelewa na mwanamke. (Mama kwa hasira) Akirud atanitambua leo. (Baada ya muda kidogo baba akarud,kufika mlangon tu kapokewa na sufuria ya kichwa. Hajakaa vzur mwiko wa pua) Mama..Mwanangu ulipopiga simu ya babako mwanamke wake alisemaje?? Mtoto..Alisema mteja unaempigia hapatikan kwa sasaโฆ..
Haya mapenzi jamani! Umewah kumpenda kwa kihivi??
Sijui Kama ushawai fall in love ile haswaa..
yani unampenda mtoto hadi akikupigia ile sauti ilivo tamu unajiskia kutafuna na kuimeza hiyo simu
Akikuita tu “my love”unajiskia tu kuvua nguo mwenywe
..
hicho kiupendo ukiwa nae unajskia unaweza piga wanaume 8 kwa pamoja
Yani ile love mtashinda pamoja kutwa nzima afu usiku unakopa salio umpigie muongee
Yani yale mapenz kiasi ukiona love story za romeo na Juliet unaona hakuna wanachofanya coz mapenz yao hayafikii yenu..
ile true love akikuangalia machoni akuguse mashavu afu akwambie,”I love u”
Unajishikilia kwenye ukuta usizimie..
yani ukimfikiria unaweza kulala chini ya kitanda Ku dilute hiyo feeling coz ni too much..
Umewahi kufeel hivyo??
Kama ushawai experience hivyo?? Basi HIYO SIYO “LOVE” NI “BANGI” PLZ ACHA KUTUMIA!
#ishakua_biashara_kichaa
Je hili ni kweli kuhusu mpenzi maskini na Tajiri?
Siku hizi kudekezwa na kupetiwa petiwa tunawaachia matajiri
Hakuna mwanamke yupo tayar kulalia kifua cha maskini ambacho moyo unadunda
Deni,, Deni,Deni, Deni .
๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐คฃ๐ถ๐ฝโโ
Nilichokifanya baada ya kualikwa na mchumba wangu kwao
Mchumba wangu amenialika kwao nikawaone wazazi wake lakini akaniambia nisiende mikono mitupuโฆ
Nikaamua kuvaa glovesโฆ
Sipendagi aibu ndogo ndogo ukweni.๐๐๐
Recent Comments