SMS Nzuri: Meseji za Vituko Vya Kujienjoy Leo
Eti hili nalo ni kweli kwa dada yako?
Oya people hv kwa mfano Dada yako akisomea sheria ndo anaitwa sister in law? au
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
Kali ya mwaka iliyotokea Benki Baada ya wezi kuiba
Kuishi kijijini kunahitaji moyo sana
..unaenda kuoga, unakumbuka kuwa umesahau sabuniโฆunaenda kuchukua sabuni kurudi bafuni, unakuta ng’ombe amekunywa maji yote..unaamua kufuata mengne,unarudi unakuta mbuzi kala sabuniโฆ๐๐๐๐
Utoto raha..! Angalia hawa watoto wanachokifanya sasa
Leo nimepulizia Air Fresh yenye Harufu ya Pilau nyumbani kwangu sasa watoto wa Jirani wamehamia Mlangoni kwangu ndio wanacheza hapo. Kila nikitoka wananisalimia. Mama yao ndio kanimaliza kabisa nimetoka akaniambia
“Kumbe wewe ni Mpishi mzuri, Hongera”
Imebidi nisirudi nyumbani maana wale watoto wanaweza kuingia ndani kabisa na pilau hakuna.
#UTOTO RAHA ๐
๐๐๐๐๐๐ป๐๐ป๐๐ป
Hali za ndoa
Kuna kijana alikua anajua kuwa mke wake
anatoka nje ya ndoa basi akamwuliza mke,
mkewe akakataa, akamwambia baba yake
akaambiwa na babaake tulia mwanangu ndoa
zina mengi! akawa kila siku analalamika kwa
babaake, mwisho babaake akamwambia basi
ntakusaidia. Itabidi ujifanye unaumwa sana hoi
hujiwez halafu nitakuonyesha jawabu!
Basi kijana akajifanya anaumwa mzee akaitisha
kikao cha ndugu wote pande 2,
Mzee akaanza kueleza jaman kijana wetu
anaumwa amepata ugonjwa wa utata hospital
zote umeshindikana hivyo tumeenda kwa mganga
wa jadi amenipa dawa na ina masharti, inatakiwa
atakaye iandaa hii dawa awe mwanamke mwenye
ndoa ambaye hajawah kutoka nje ya ndoa tangu
alipoolewa ndo kijana wetu atapona!
Kama ametoka nje ya ndoa asiandae dawa hii
kwa sababu tukimpa kjana wetu watakufa wote!
Je kina mama nani ataandaa? Walitoka nje
wamama mmoja mmoja hadi mkewe na mamake
mzazi wakatoka, akafata mama ake kijana,
mashangazi na dada zake, mwisho wakabakia
wanaume peke yao! Mzee akamwambia
mwanangu umeona hali za ndoa zilivyo?
Acha kujisumbua tulia na mkeo nadhani
umejionea hali halisi.
Cha zaidi omba Mungu sana juu ya ndoa yako!
Kijana akazimia!
SOMA TENA KISHA MTUMIE NA MWENZIO.
Kweli mitandao imeharibu watu, angalia huyu anachokisema sasa
๐๐ kweli nimeamin mitandao inahribu watu
Leo kuna jamaa kamuona Dada akipita barabaran kapendeza jamaa kamwendea Dada akamwambia!
Dada nice photoย ๐๐๐๐
Cheki huyu mtoto anachomjibu mwalimu wake, kufundisha watoto ni kazi kweli kweli
Mwanafunzi wa darasa la 2 kaulizwa na mwalimu wake
Hivi:je ukipewa maandazi 5 ukiambiwa kula 3 tu yatabaki mangapi?
Akamjibu hivi:nikipewa na chai hakibaki kitu mwalimu.
Mke alichomfanyia mme wake kabla ya kwenda safari, Chezea mawaifu walokole wewe!
JAMAA alimuaga mke wake mlokole kuwa anaenda semina ya siku tatu, kumbe anakwenda kwa bi mdogo.
Mke akamwambia mumewe; “Tupige magoti tusali”,
Wakapiga magotiโฆ:
MKE: Eee baba msaidie mume wangu afike salama safari yake.
MUME: Emenโฆ
MKE: Mpe nguvu katika yote atakayoyafanya huko.
MUME: Emenโฆ
MKE: Akitaka kufanya uasherati ashindwe.
MUME: Kimyaโฆ
MKE: Akifanya uasherati apatwe na janga baya kwa uwezo wako bwana.
MUME: โฆโฆ.!!
MKE: Yaani akifanya uasherati afie hukohuko kwa mateso makali.
MUME: Maombi gani sasa hayo!!?. Haya basi siendi semina ufurahi wewe.
Chezea mawaifu walokole wewe!
Jinsi ya Kubana matumizi X-mass
Badala yakupika PILAU tutapika TAMBI kwenye Xmas maana tutakua tumeokoa sh.15,000/= Vitunguu swaumu 2000, Vitunguu maji 1000, hiliki 1000, Magome 1000, Michele wa 2000, Soda 3000, Nyama 5000 . Fedha hizi zitatumika kununua mfuko wa cement ili tuanze kujaza kibubu cha ujenzi wa nyumba badala ya kupanga. Karibuni saana maji ya kunywa tumechemsha ndoo nzima.
๐โจMarry Xmas & Happy new year.โจ๐
Cheka kidogo, angalia anachosema huyu mchaga
Mchaga baada ya kufa akaulizwa na malaika anayetoa roho: Mangi hapa ni njiapanda kulia ni Mbinguni na kushoto ni Jehanamu, Je unachagua kwenda wapi?
MANGI: Bwashee, mi nabaki hapa hapa njiapanda aisee.
MALAIKA: Kwa nini?
MANGI: Aisee, nikifungua duka hapa si nitapata wateja wa Mbinguni na Jehanam. Yani patakuwa senta ya hatari, supu na nyama choma muda wote. Hata we utafaidi, unavyoenda kuchukua roho unaniletea stock nakupa hela yako cash mkononi. Na kila ukipita hapa unapiga mchemsho wako wa ulimi na bia mbili chap kabla ya kuingia mbinguni.
Kwanza nashangaa Shirima alipitaje hapa bila kushika ploti, au alikufa amelewa sana?
Hii sasa kali kweli kweli! wazazi wanachofanya pale binti yao anapochelewa kuolewa
Wazazi wengine wanaandikaย MBWAโMKALIย kwenye geti lao kama binti wao ana miaka 18..
Binti akifika miaka 30 na hajaolewa wanapabadilisha na kuandikaย TUNAUZA BARAFU
๐๐๐๐๐๐๐
๐๐๐๐๐๐๐
Bongo usanii mwingi!!!
BONGO USANII UMEZIDI DAAH!!
โฆyani nakupeleka dinner unakula sana vipaja vya kuku na chips yai halafu nakupeleka bar unakunywa sana tu, tukitoka hapo nakupeleka club, Masaa yote hayo hakumbuki kuniambia upo periods hadi mdaa wakwenda kulala ndo beiby nipo kwenye siku zangu!! jamani jamaniโฆ Hapo ndo unaanza kupiga hesabu pesa iliyopotea buree๐๐๐๐
Ndooo maana mabinti wa kibongo ๐๐ป๐๐ป๐๐ป๐๐ป๐๐ป๐๐ป
Alichokifanya jamaa baada ya kuokota wallet yenye pesa za kumwaga
Jamaa aliokota wallet, alipofika nyumbani akapiga simu kwenye radio station
“Naitwa John nimepiga simu kutangaza kuwa nimeokota wallet ndani ina laki 7, ATM Card na kikaratasi chenye PIN ya ATM Card na kijimkufu cha dhahabu kinene hiviโฆ”
Mtangazaji akasema:- Akhasante sana John, kwa hiyo ungependa kumrudishia mwenyewe kama ana kusikiliza akutafute kwa No. Gani!?
John: Hapana, mi nilikuwa namshukuru tu maana amenitoa kwenye matatizo na ninapenda kumuombea Dedication wimbo wa Snura “MAJANGA” umfikie popote pale alipoโฆ!!!
Angalia nilichomfanyia huyu mwizi
Et jana usiku mwiz kavunja mlango kwangu
akaanza kutafuta kitu kila kona ikabid
na mie niamke namuuliza unatafuta nini ananijibu hela ndipo nilipoanza na mie kutafuta nae
maana hta hela ya kula Jana sikua
nayo alichoka zaid nilipomuliza una uhakika uliweka humu?
*sipendagi ujinga
Nilichomfanyia huyu aliyenizingua nilipomuazimisha pasi
๐๐๐๐๐๐
Jana nimeenda kuazima pasi chumba jirani, ili ninyooshe nguo zangu, Jamaa wakaniambia nichukue nguo nikanyooshe room kwao maana hawataki pasi yao itoke.
Sasa leo amekuja mmoja wao kuazima mopper akasafishe room, nimemwambia aje adekie humu humuโฆ
Jamaa ameondoka nadhani atakua ameenda kuchukua maji
๐ค๐ค๐ค
Angalia huyu house girl wa mzungu alichokifanya na anachokisema
House girl mmoja alipewa kazi na mzungu mara akavunja sahani.
Mzungu aliporejea,kazin akamuuliza ‘what happened to my plate?
House girl akajbu: ‘The dog wow wow friji paaa, mchuzi mwaaaa the vyombo pangalapangala the sahan ngelengenjeeโฆโฆthe pasuka paaaaaaaa
๐๐๐๐hadi saiz mzungu bado anasoma dictionary hajui lugha gani imetumika
Kama simu yako ina wifi
Kama simu yako ina Wi-fi ujue uko na mke wa mtuย ๐๐๐๐๐๐๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ๐๐ผ
Ziara za kushtukiza zinachekesha sana
Mimi Nimecheka sana
๐๐๐๐๐๐๐๐๐๐
ZIARA ZA KUSHTUKIZA๐๐
Mimi ni msomaji mzuri wa magazeti, na msikilizaji mzuri wa redio, huwa naangalia luninga mara chache sana kama nikibahatika kupita mahala kuna luninga. Sasa wiki hii nimesikia mengi kuhusu hizi ziara za kushtukiza za viongozi wetu, nikaona hili ni jambo zuri tena linafaa kuigwa na sisi wananchi wapenda maendeleo. Nikaona nijipange na mimi nifanye ziara kadhaa za kushtukiza katika sehemu mbalimbali zinazonihusu.
Nikaona nianze na ziara ya kushtukiza pale shuleni kwa huyu mwanangu, maana kila siku anakunywa chai na kuondoka na daftari zake na mie sijawahi kwenda shuleni kwao toka nilipomuandikisha shule mwezi Januari. Nilifika shuleni na kumuona mwalimu mkuu, ambae alianza kutetemeka nilipomuambia kuwa nimekuja pale kwa ziara ya kustukiza, sijui alidhani mi ni mmoja wa Mawaziri wapya, maana nilimuona jasho linamtiririka ghafla. Akanikaribisha ofisi yake iliyokuwa na vitabu kila kona, na kuita waalimu wote na kunitambulisha kuwa ni kiongozi nimekuja kwenye ziara ya kustukiza.
Nilipojitambulisha kuwa ni mzazi, waalimu wote nikawaona waanza kupumua kwa raha. Nikawaambia kuwa mimi nina mwanafunzi pale na nilikuja ziara ya kustukiza kujua maendeleo yake. Baada ya mwalimu mkuu kusaka jina la mwanangu nae akanambia, โMzee huyu mtoto hajaja shule mwezi wa tatu sasa, tulijaribu kukutafuta ikashindikana, hatujui yu wapiโ Jasho likaanza kunitoka mimi, yule mtoto kila asubuhi nampa nauli anaenda shule, na mara nyingi ananiomba michango kumbe hata shule haji. Niliondoka bila kuaga presha ikiwa juu.
Nikaona niende kwenye genge la mke wangu nae nikamfanyie ziara ya ghafla nimhadithie mambo ya mwanae, nilipofika pale nikakuta kuna mdada mwingine anauza genge. Nikamsalimu, na kumuuliza mwenye genge ntampataje, jibu lake lingeniua kama ningekuwa si mkakamavu, โMume wake kaja kumchukua na gari wameenda kununua shamba Bagamoyoโ. Nikaondoka nimechanganyikiwa, nikajuwa hapa dawa yangu moja tu, nayo ni Sabrina, mtoto wa Kinyaturu pale ambapo nikipata maudhi huwa naenda kubembelezwa.
Nikatwanga mguu kwa Sabrina nae nikamfanyie ziara ya ghafla ili anipoze moyo. Nilipogonga mlango wa chumba chake akatoka mbaba wa miraba minne, akanisalimia kwa upole, โSalama kaka unasemaje?โ Jibu likanitoka โSamahani mie nilimkopesha huyu dada wa chumba hiki vitenge, nilikuja kuuliza kama ameshapata hela yanguโ Ziara za kushtukiza zinataka moyo wa chuma jamani
Kingereza sio mchezo, angalia huyu anavyojichanganya
Jamaa fulani alikuwa ame2lia beach mzungu akapita akamuliza “Are u relax ? Jamaa akawa hamuelewi akamjibu No! Mzungu mwengine akapita akamuliza vilevile akajibu No!
Akaona hapa anasumbuliwa akasogea mbele kidogo ya maji akamuona mzungu mmoja alikuwa ame2lia. Akamuliza “are u relax? Mzungu akajibu yes jamaa akamkata makofi mawili na kumwambia kumbe we ndo relax inuka unatafutwa na wenzakoโฆ..Shenz mkubwa mie nasumbuliwa na wenzako kule we umejikausha!!
Haya nayo ni maajabu mengine kwa wazazi wa mabinti
BABA MWEUSI
MAMA MWEUSI
na ww walikuzaa mweusi lakini umefikisha miaka 20 umeanza kua mweupe
โฆ..HAPO NDO WAZAZI WANAJIULIZA hv mbegu ilkua ya kinyonga au๐๐๐๐
Recent Comments