SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Cheki huyu mzee alichomfanyia muuzaji wa pharmacy

Mzee kaingia pharmacy,
MZEE: Mambo mwanangu, kuna kitu naomba uonje nitakulipa
MFAMASIA: Kitu gani?….Mzee akatoa kichupa na kijiko akaweka …majimaji yaliyomo kwenye
kichupa kwenye kijiko na kumwambia mfamasia aonje, mfamasia akatia yale maji mdomoni na kuyazungusha zungusha mdomoni akionja;

MZEE: Nipe jibu, ina utamu wa sukari au chumvi au pilipili?
MFAMASIA: Kama chumvichumvi
MZEE: Hakuna sukari
MFAMASIA: Sukari hakuna kabisa
MZEE: Loh asante chukua hii alfu tano nashukuru sana, dokta alinambia nipime mkojo wangu kama nina kisukari, kumbe sina asante bwana mdogo

Angalia huyu Jamaa alivyomuweza huyu mrembo

Nipo kwenye daladala siti ya nyuma kabisa nimekaa na mrembo mzurii.sasa nikawa namtongoza kwa sauti ya chini sana watu wengine wasiskie,akawa hanijibu kitu,mala gafra akapayuka kwanguvu na kwa sauti ya juu iliyomshtua kila mtu.​
​”Nimesema stakii,stakii tena unikome”​😳😳

​Nami nikamjibu kwa sauti ya juu vile vile​
​”Kama umejamba nisikwambie bhanaa,kwani ww nani?”​☹

😂😂😂😂😂😂😂😂😂
​​MIMI SIO MTU WA MCHEZO MCHEZO​
Sipendag ujuinga mim

Jiwekee Utaratibu utakaokuwezesha kuamua vizuri juu ya fedha utakazopata

Jiwekee utaratibu utakaokupa uzoefu wa kuamua vizuri juu ya fedha unazopata. Watu tumekuwa tukitumia fedha tunazopata bila kufikiria jinsi ya kugawa ktk matumiz badala yake baada ya kutumia ndio una/ninaanza kujuta Kwa nin nime/umetumia tofauti na mahitaji uliyonayo. Kiasi cha fedha ulichonacho chaweza kukufanya uwe maskini au tajir kutokana na maamuz unayofanya juu ya hiyo fedha. Ukitaka ufanikiwe na ukue kifedha jaribu kugawa fedha uliyopata Kwa mafungu yafuatayo:

A. Sadaka: ndani ya sadaka kuna; a. malimbuko, mith 3:9, b. zaka na c. dhabihu malaki 3:8. Hii inakusaida wewe kumpa Mungu nafasi ya kwanza mth 6:33
2.pia unaonyesha ya kuwa unahitaji msaada na hekima zaid ktk kugawa fedha zilizobaki. Hagai 1:2-11
3. Shukrani Kwa Mungu alivyokuwezesha kumb torat 8:11-20 4. Unaonyesha unahitaj msaada wa Mungu ktk kupata mbinu za kuongeza fedha ktk maisha yako mith 3:9,10. Ktk bahasha hii waweza kuweka 10% au zaidi kutokana na Roho mtakatifu akavyokuongoza.

B. Akiba, Uwe na tabia ya kujiwekea akiba Kwa ajil ya baadae au ukiwa mzee, kumb torat 28:8 na mwanzo sura ya 41 hadi 47 tunamwona Yusuphu alivyoweka akiba 20% ya mavuno ktk miaka saba ya baraka ambayo ilisaidia ktk miaka saba iliyofuata ya ukame. Hii inajusaidia kuweka akiba Kwa ajil ya maisha ya baadae Kwa kiwango maalum na Kwa mda Fulani zab 144:13a. Jifunze Kwa Chungu anayeweka akiba ya chakula wakati wa jua ambacho humsaidia wakati wa ukame mith 6:6-8. Omba Roho mtakatifu akuongoze kuweka akiba ili utumie pind ambapo hutakuw na pato.
C. Kuwekeza ;hii inakusaidia ili kujijengea tabia ya kuwa na mtaji wa kukusaidia kuzalisha pesa zaid Kwa kuanzisha mradi mwingine Luk 19:12.
D. Matumizi yaliyo ya lazima. Mungu ana uwezo wa kutupa tunachohitaji ila Mungu anataka tuwe na mahitaji Tito 3:14. Haya in matumiz ya kila siku kama chakula etc.

Unaweza ukaongeza bahasha maalumu Kwa ajil ya kuweka au kutunza fedha za kulipia madeni /ujenzi/ada kama kuna wanaosoma/ kodi ya nyumba/ maandalizi ya harusi etc.
Kugawa fedha katika Mafungu ya bahasha inakusaidia kuwa na utaratibu maalum wa kutumia fedha na pia inakusaidia kufanya maamuzi mazuri ju ya kila fedha unayopata.

SWALI: Je, fedha unayopata unagawaje kabla ya kutumia? Je, Unakumbuka bahasha no. 4 tu, au 4 &3 au 4 &2 au 1 &4 au 1,2& 4 au 1,3 &4 au 1,2,3&4. In Roho wa Mungu atakayekuongoza kugawa fedha na sio vinginevyo.

Unaweza sema sina mtaji wa kutosha au sina biashara yoyote au nimejaribu kufanya biashara au kuwekeza cjafanikiwa etc, hivyo ni visingizio. Unapingiza visingizio au manung’uniko unapelekea kukataa tamaa na pia unamzuia Roho Mtakatifu kukusaidia kuvuka ktk hali hiyo.
Jifunze kutoka Kwa watumwa hawa waliopewa mtaji na bwana wao na jinsi walivyotumia kuzalisha. Kila mmoja alipewa kiasi kadri ya uwezo wa uwezo wa mtu vivyo hivyo walitofautiana kupata faida ingawaje mmoja wao aliamua kufukia na mwisho alinyang’anywa na kupewa yule mwenye zaidi, Luka 19:12-26 na mth 25:14-29.

Angalia huyu mgeni anachokifanya, wageni wengine ni hatari

Hata kama ni Mgeni this is too much.
Mwenyeji: Karibu mgeni karibu ukae,utapenda chai au soda?
Mgeni: Nipe nianze na soda wakati chai inachemka.
Mwenyeji: Utakunywa fanta au sprite?
Mgeni: Nipe fanta wakati sprite inapoa.
Mwenyeji: Utakunywa na keki au mkate?
Mgeni: Nipe keki mkate nitanywea chai ikishachemka.
Mwenyeji: Utapendelea ndiz au machungwa,
Mgeni: Nipe machungwa ndizi ntakula na wali
mchana.
Chezea mgeni ww.!!!

Ujumbe wa kuasa kudumu katika upendo na mapenzi

Hii ni mbegu bora inaitwa UPENDO ipande kwa ndg zako,na pale utakapokuta imeota imwagilie maji ya FURAHA,iwekee kivuli cha USHIRIKIANO, ipalilie kwa jembe la KUSAMEHE, iwekee mbolea ya AMANI, ipige dawa ya NENO LA MUNGU, itakayoua wadudu wote waharibifu kama ubinafsi, chuki, wivu, dharau, unafki, kiburi, choyo, tamaa na fitna kwenye mmea huu, MMEA HUU (UPENDO) UENDELEE KUWA MCHE BORA KULIKO YOTE KTK MAISHA YAKO SIKU ZOTE.

Angalia nilivyoingizwa mjini na ujanja wangu wote

Ndio nilikuwa nimeshuka kwenye basi la SAI BABA pale Ubungo, nina Begi kubwa Mgongoni na begi Dogo la Lap Top mkononi, sura inatazama Mbele Very Serious kama nipo kwenye Gwaride la Uhuru!..Mabega juu yanafanya Cheers na Mawingu!, natembea kwa madoido…..leo nimetoka Likizo Moshi,

“Brother Simu ya ukweli hii..kitu cha Tecno C9 bei poa” hii ilikuwa sauti ya Teja mmoja hivi!

Yaani huyu Teja Bwege kweli,anataka kumuuzia nani sabuni? mimi sio wa kuja!…kamwe Siwezi kuibiwa hapa Town,hakuna wizi au utapeli nisioujua!, Mimi nimezaliwa Mwananyamala kwa Manjunju, nikalelewa Tandale kwa Mtogole, Shule ya msingi nimesoma Turiani Magomeni, Hivi Mbwa gani aniibie?…kwa Style ipi?

Sipendi kabisa Upuuzi!, Wajinga ndio wataibiwa, sio Mimi!…sasa Kwa mwendo wa haraka nikatoka nje kabisa ya Stendi ya Ubungo straight mpaka Stendi ya dala dala za Kariakoo, hapo ndipo nikakutana na Vijana wawili wadogo wakiwa na mzani wa kupimia uzito,…hakika napenda sana vijana wanaojituma kama hawa na sio ile Mijizi ya kule ndani Stendi!!,….hapa sasa nikapata wazo!

“Dogo mnapima uzito kwa shilingi ngapi?”

“Mia mbili tu Kaka!”

”Ok”

Kwa mwendo wa kikakamavu nikapanda juu ya mzani,lengo hapa ni kujua uzito wangu, Mtori niliokula mwezi mzima kule kwa Mshekuu sio mchezo, hapa nahisi nacheza kwenye kg za John Cena,

“Mama wee! Dogo mzani mzima huu kweli? Mbona nina kilo 134?” (Nilihamaki)

“Aaah! Brother huoni umepanda na Mabegi juu ya mzani?”’

Hahaha! kweli nimechanganyikiwa!…Sasa nikatoa mabegi yote mawili na kurudi juu ya Mzani, hapa ndipo Uzito ukashuka kutoka kg 134 mpaka kg 56!…My God kweli Body la “One Pack ” haliongopi! thats means mabegi yaliniongezea kg 78! duh hii ni hatari!

“Yaani we Dogo kitambi chote hiki kg 56? huu Mzani Mzima kweli?”

Kimya…

“Dogo huu Mzani vipi?”

Kimya…

Dogo ana dharau huyu!…Sasa ndio nikabandua macho yangu toka kwenye kioo cha mzani ili nimtazame huyu dogo asiyejibu!….ndipo macho yangu yakakutana na Kigoda tupu kilichochongwa Mvomero!…Dogo hakuwepo!….na Mabegi pia hayapo!…lap top haipo!….NIMEPIGWA!

Ni dhahiri watoto wa Mjini walikuwa wameniacha juu ya Mzani, wamechukua Lap top ya Milioni na wameniachia Mzani chakavu wa elfu 40, what a stress!….sasa nilirudisha macho kwenye kioo cha uzito na sasa kilisoma KG 38!…yaani dakika hii hii nimepungua kilo zingine 18, Hakiyamama nahisi hata utumbo wangu wamebeba!…niitieni Ambulance!

🙆🏼🙆🏼🙆🏼🙆🏼🙆🏼🙆🏼🙆🏼🙆🏼🙆🏼🙆🏼🙆🏼

Soma huyu mtoto anachosema sasa, Ndoto za watoto bwana! Kazi ipo!

Mwalimu aliingia darasani na kuwauliza wanafunzi juu ya ndoto zao za baadae.
MWAL: John we unataka ukiwa mkubwa uwe nani?
JOHN: Nataka niwe daktari wa moyo niwasaidie watanzania wanaougua magonjwa ya moyo.
MWAL: vizuri. Na wewe Rose unataka kuwa nani?

ROSE: Nataka kuwa rubani, niweze kusaidia watu wanapenda kusafiri kw anga.
MWAL: Safi sana Rose. Utakua utakua mfano kwa wasichana wenzio kuwa na bidii kwenye masomo ya sayansi.
MWAL: Na wewe Nehemiah ??
Nehemiah : mimi nataka kuwa tajiri mkubwa sana. Niwe na nyumba Tanzania, S.Africa, Marekani na Dubai. Niwe na gari 7 za kutembelea. Kila siku nabadilisha. Leo nikipanda hii, siirudii hadi week iishe. Nataka niwe namiliki viwanda, Makampuni, ndege binafsi na mashamba makubwa. Nataka niwe na nguvu serikalini ya kuamua nani awe Rais na nani asiwe……”
Akameza mate kisha akaendelea….
“Nataka kuwa na walinzi 20 wenye silaha nzito wakinizunguka, na watumishi wakininyenyekea. Nataka kuwa bilionea ninayeogopwa. Lakini pia nataka kuwa na mke mzuuuri sana ambaye nitakuwa natembea nae kila mahali.”
MWAL: ndoto nzuri sn lakini unahitaji bidii sana kutimiza. Haya na wewe Jenny tueleze unataka kuwa nani??
JENNY: Nataka kuwa mke wa Nehemiah .!!

Kilichotokea kwa binti na mvulana wake walipotaitishwa na baba yake msichana

Msichana alikuwa amekaa na baba yake kibarazani, mara akamuona MVULANAfriend wake akija, yule mvulana alipokaribia tu, yule msichana akamwambaia:

MSICHANA: Umekuja kuchukua kile kitabu chako, kinachoitwa “DADDY IS AT HOME?” by Ngozi Okafor
MVULANA: Hapana!, Nimekuja kuazima kitabu cha Maombi kama kinaitwa “WHERE SHOULD I WAIT FOR YOU?” by Ngũgĩ wa Thiong’o
MSICHANA: Aaah! Icho sina ila ninacho kimoja kinaitwa “UNDER THE MANGO TREE” by Chimamanda Adichie
MVULANA: Ooh! Vizuri, Basi usisahau kuja nacho kesho kitabu cha Okot p’Bitek kile kinachoitwa “CALL ME IN 5 MINUTES BEFORE” Utakapokuja shule.
MSICHANA: Usijali, tena nina kitabu kipya kinaitwa “I WON’T LET YOU DOWN” by Chinua Achebe
Baba mtu akawatazamaaaa kisha akasema
BABA: Vitabu vyote hivyo, mbona vingi sana, atavisoma vyote kweli
MSICHANA: Ndio Daddy, huyu mvulana hupo smart sana na ana akili atavisoma vyote hivyo!
BABA: Sawa! Usisahau kumpatie na kile ambacho nimekiweka pale juu ya meza, kinaitwa “I AM NOT STUPID, I UNDERSTOOD EVERYTHING YOU’VE BEEN SAYING” by Shakespeare!
Na kuna kingine nimekiweka juu ya kabati la vyombo, kinaitwa “IF YOU GOT PREGNANT PREPARE TO GET MARRIED”

Chanzo na Matibabu ya Tatizo la Mtindio wa Ubongo (Kupooza ubongo)

Tatizo la Mtindio wa Ubongo au Kupooza ubongo kitaalamu ni Cerebral plasy (CP), ni hali ya kupooza ya moja kwa moja ya viungo vya mwili inayotokana na sehemu ya ubongo (seli) inayotawala viungo hivyo kufa katika kipindi cha mwanzo cha maisha (Utototni).

Mtindio wa Ubongo ni aina ya tatizo la mishipa ya fahamu inayoathiri misuli ya mwili inayotokana na selli za ubongo wa mtoto kufa au kutengenezeka vibaya katika kipindi cha mwisho wa ujauzito (3rd trimester), kipindi cha kuzaliwa au kipindi cha miaka miwili ya mwanzo wa mtoto.

Chanzo chake

Hii inatoka na sehemu ya ubongo kukosa oksijeni na virutubisho vya kutosha inayopelekea celli hizo kufa. Tunajua kuwa ubongo una kazi mbalimbali mfano kufikilia,kufanya maamuzi(decion making) pia inatawala sehemu mbalimbali ya viungo vya mwanadamu,mfano ubungo wa nyuma unahusika na kuona kama wakati mtoto akichelewa kulia cell za ubongo wa nyuma (occipital) zikafa mtoto huyu baadae atakuwa na matatizo ya kuona.

Sababu za Ubongo kupooza

Vitu vingi vinaweza kusababisha ubongo kupooza, navyo ni katika kipindi cha ujauzito (mtoto akiwa tumboni), wakati wa kujifungua(80%) na kuugua mtoto kipindi cha mwanzo kabla ya miaka miwili.

Kuchelewa kulia baada ya kuzaliwa

Zaidi ya 67% ya watoto wote wenye tatizo la ubongo kupooza(CP) Tanzania inatokana na kuchelewa kulia baada ya kuzaliwa(birth asphyxia) ambayo inatokana na mama mjamzito kukaa na uchungu kwa muda mrefu(prolonged labour).

Manjano na degedege

Ikifatiwa na manjano (severe neonatal jaundice) na degedege baada ya kuzaliwa inayopelekea celli za ubongo kufa.

Matatizo yoyote yanayoweza kuathiri ubongo

Kabla ya miaka 2, mtoto akipata homa ya uti wa mgongo(meningitis) mtoto kuanguka(head trauma), malaria kali, matatizo haya yanaweza kuathiri seli za ubongo za mtoto ambazo haujakomaa.

Matatizo wakati wa ujauzito

Katika kipindi cha awali ujauzito(1st trimester) mama akipata mashambulizi ya magonjwa na kipindi cha miezi ya mwisho ya ujauzito (3rd trimester) shinikizo la damu kuwa juu (Pregnancy Induced Hypertension) na kifafa cha mimba/eclampsia kinaweza sababisha usafirishaji wa damu yenye oksijeni na virutubisho kupitia kondo la nyuma kushindikana vizuri hii inaweza pelekea baadhi ya cell kwenye mwili wa mtoto aliye tumboni kufa.

Matatizo katika kipindi cha kujifungua

Kwa utafiti uliofanyika katika hospitali ya taifa ya Muhimbili mwaka 2013 kuhusiana na sababu za watoto waliopooza ubongo, inaonesha zaidi ya 80% ya watoto wenye tatizo hilo linatokana na matatizo katika kipindi cha kujifungua.

Matokeo/madhara.

Madhala ya ubongo kupooza huwa yanatofautiana kutoka mtu mmoja hadi mwingine kwasababu inategemeana na sehemu ipi ya ubongo iliyoathiriwa zaidi.

Kupooza ubongo(CP) kunaleta matokeo mabaya ya moja kwa moja(permanent) katika mwili wa mtoto, Kila mfumo katika mwili wa mtoto unaweza athiriwa mfano mfumo wa chakula, wa hewa, mkojo,fahamu, na wa misuli ,athari zenyewe ni kupata degedege, Kifafa, mtoto kuwa na kichwa kikubwa(macrocephaly), mtoto kuwa na kichwa kidogo sana(microcephaly), tatizo la kusikia, kuona, kuongea,kumeza pia kushindwa kutembea na kupata choo ngumu (constipation) , Pia utahila (mental retardation).

Matibabu ya Ugonjwa wa Mtindio wa ubongo

Tatizo la ubongo kupooza hakuna matibabu yake, kinachotibiwa ni matokeo ya tatizo hili yanayosaidia kubolesha maisha yao na kuwa na hali ya kujitegemea.
Katika matibabu kuna aina mbili nayo ni medical (dawa) na mazoezi(therapy).

Dawa zinazotumika mfano phenobarbitone na Carbamazepine kwa degedege na kifafa na kukakamaa (contracture,spasticity) hupewa BOTOX inayosaidia kupunguza tatizo.

Kuna therapy mbalimbali kwa watoto wenye CP, nazo ni Physiotherapy, Occupational therapy, Speech therapy n.k.

Kwa tatizo la kutoweza kutembea, watoto hawa wanaweza pata faida katika kitengo cha mazoezi(physiotherapy) mzazi anaweza kufundishwa ili kumsaidia , misuli ya mwili kupata nguvu,hupunguza kukakamaa na pia inasaidia kupata ujuzi wa kutembea n.k. Pia kuna Occupational therapy inamsaidia mtoto apate uwezo wa kula mwenyewe na kukaa.Speech therapy/kuongea, watoto wengi wenye CP huwa na tatizo la kuongea hii inatikana na misuli inayosaidia katika kuongea kuathiriwa, kuna vifaa vinavyotumika kumsaidia mtoto mwenye tatizo hili ili aweze kuongea vizuri.

Sio watoto wote wenye kupooza ubongo wana utahila (mental retardation), 36% ya watoto wenye ubongo kupooza wana utahila(mental retardation). Mtoto anaweza kuwa na tatizo la viungo ila ana uwezo mkubwa wa kufikilia.

Matokeo kwa jamii na familia.

Jamii:Kwa utafiti uliofanyika katika hospitali ya Muhimbili, inaonesha zaidi ya asilimia 30 ya wazazi wanahusisha tatizo hili na mambo ya kishirikina(superstition) Wazazi wengi wenye watoto hawa wanafanya maamuzi ya kuwaficha watoto wao vyumbani kutokana na mtazamo wa jamii husika .

Familia:Pia imegundulika kuwa ndoa nyingi huvunjika mara baada ya kuzaliwa watoto wenye CP, kati ya wanawake 100 wenye watoto hawa waliohojiwa katika hospitali ya Muhimbili 16 wanaishi peke yao baada ya kupata watoto hao, wengi wao wanadai kuwa waume zao wanawalahumu kuwa wenyewe ndio chanzo cha hao watoto.

Pia wanawake wengi hupata changamoto katika malezi ya watoto hawa, wengi wao huwatekeleza katika vyumba inayopelekea kuharibika kisaikolojia.Hii inatokana na hali ya uchumi wa familia, mama na wanafamilia wote kuondoka nyumbani kwenda kufanya ujasiliamari ili kujikimu na maisha.

Ushauri kwa familia

Familia :upendo unahitajika wa hali ya juu kwa watoto hawa, ili wasiharibike kisaikolojia. Kuna watoto wameweza kufanya vizuri katika masomo ambao wana tatizo hili, sio wote wanapata utahila, mtoto anaweza kushindwa kutembea lakini akawa na IQ kubwa, katika watoto waliokuwa wanahudhulia clinic ya watoto wa CP na kifafa Muhimbili, alikuwepo mmoja aliyekuwa anaongoza katika darasa analosoma na pia anamipango wa kusoma ili kuwasaidia watoto wenye tatizo hili, pia kuna madaktari bingwa wa mishipa ya fahamu kwa watoto walioko marekani(Paediatric neurologist) ambao wana matatizo hayo.

Wazazi wasikate tama kwa watoto hawa kwa sababu kwa therapi mbalimbali watoto wanaweza rudi katika hali kama watoto wengine, pia wakiendelea kutumia dawa na kuhuzulia clinic kama watu wenye sukari na presha.

Ushauri kwa viongozi serikali

Uongozi: Kupitia vyombo vya Habari na vipeperushi , jamii ya Tanzania katika miji na vijiji, elimu itolewe kuhusiana na sababu ya tatizo ili kuweza ziepuka. Pia kuna vituo vichache sana vya mazoezi (physiotherapy na occupational therapy) wazazi wanapata changamoto nyingi, katika jiji la Dar, wengi wao huenda katika hospitali ya taifa Muhimbili kwa ajili ya mazoezi, kutokana na hali ya uchumi, nauli inakuwa changamoto wanaamua kuacha kuhudhulia kliniki.

Fursa ya kufungua vituo vya mazoezi(physiotherapy) na shule katika kila wilaya kwa sekta binafsi na serikali itasaidia watoto wenye CP. Pia shule za watoto wenye CP katika nchi ya Tanzania hazipo, kuna shule chache za watoto wenye utahila, watoto wenye CP sio wote wenye utahila.

Shopping Cart
2
    2
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About