SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Mambo 8 ya kushangaza yanayofanywa na mwili wako kukulinda pasipo wewe kujua

Mwili wa binadamu unafanya mambo
mengi ya kibaiolojia ambayo mara
nyingi ni vigumu kuyaelewa. Mwili una mifumo mbalimbali ya ulinzi ambayo inatulinda na hatari zinazoweza kutudhuru. Mifumo hiyo
inatulinda masaa 24 ya siku, Siku zote 7 za wiki, katika mambo yote
yanayoweza kuhatarisha maisha yetu.
Yafuatayo ni mambo yanayofanywa
na mwili ambayo ni kati ya hiyo
mifumo ya ulinzi wa mwili wa
binadamu.

1. KUPIGA MIAYO (YAWNING)
Lengo kubwa la kupiga muayo ni
kuupoza ubongo baada ya joto kuzidi
kwenye ubongo au baada ya ubongo
kuchoka kufanya kazi.
Vile vile kama ukiwa umechoka au una
njaa husabababisha oxygen
kupungua kwenye damu na kwenye
mapafu, hii hupelekea tatizo la
kupumua, hivyo kupiga miayo
husaidia kuingiza oxygen ya ziada
mwilini ili irudishe mwili katika hali
yake ya kawaida.

2. KUPIGA CHAFYA (SNEEZING)
Mara nyingi tunapiga chafya pale pua
zetu zinapokua zimejaa bakteria wa
magonjwa ambao hawahitajiki
mwilini, Vumbi pamoja na takataka
mbali mbali zilizoingia kupitia pua.
Hivyo kupiga chafya ni kitenda cha
mwili kujisafisha kwa kuyatoa hayo
matakataka nje yaliyoingia mwilini.

3. KUJINYOOSHA (STRETCHING)
Kuninyoosha mwili ni kitendo kisicho
cha hiari ambacho lengo lake ni
kuuandaa mwili kwa ajili ya kazi
mbalimbali za kutumia nguvu
utakazokabiliana nazo kwa siku nzima.
Lakini pia kujinyoosha kunaipa misuli
ya mwili mazoezi na kuiweka sawa
vilevile kunarudisha mzunguko wa
damu katika hali yake ya kawaida na
kumtoa mtu katika uchovu.

4. KWIKWI (HICCUPING)
Najua umewahi kupata kwikwi, na
mara nyingi mara baada ya kumaliza
kula chakula. Je umeshawahi kujiuliza
ile sauti ya ajabu ya kwikwi
inasababishwa na nini au kwa
sabababu gani watu hushikwa na
kwikwi?
Hiyo yote husababishwa na
DIAPHRAGM (tamka DAYA – FRAM)
kiungo kinachopatikana ndani ya
mwili wa binadamu chini kabisa ya
kifua baada ya mapafu(lungs). Kazi
kubwa ya diaphragm ni kusaidia katika
upumuaji, (inhale) na (exhale). Pale
unapoingiza hewa ndani (inhale)
diaphragm hushuka chini ili kusaidia
kuivuta hewa ifike kwenye mapafu. Na
unapotoa hewa nje (exhale)
diaphragm hutulia kwa kubakia
sehem yake ili kuwezesha hewa chafu
kutoka nje kupitia pua na mdomo.
Sasa basi, kuna wakati diaphragm
kubugudhiwa na kuisababisha
kushuka chini kwa kasi sana jambo
linalosababisha wewe kuvuta hewa
(inhale) kwa kasi isiyo ya kawaida
kupitia koromeo la sauti, hewa ikifika
kwenye box la sauti (larynx), sehem
hiyo hujifunga kwa haraka sana ili
kuzuia hewa isipite huko na ndipo
KWIKWI hutokea.
Mambo mengine yanayoweza
kuibugudhi diaphragm na
kuisababisha kufanya kazi vibaya
mpaka kupelekea kwikwi ni kitendo
cha kula haraka haraka au
kuvimbewa.

5. KUJIKUNJA KWA NGOZI YA VIDOLE
VYA MIKONO BAADA YA KULOWA AU
KUKAA MUDA MREFU KWENYE MAJI.
Je umewahi shuhudia jinsi ngozi ya
vidole vyako inavyojikunja baada ya
kufua nguo muda mrefu au kushika
maji muda mrefu? Unajua ni kwa
sababu gani ngozi hujikunja kama ya
mtu aliyezeeka angali yu kijana mara
baada ya kukaa sana kwenye maji?
Watu wengi kabla walizani kwamba
kujikunja kwa ngozi hiyo hutokana na
maji kuingia kwenye ngozi na hivyo
ngozi hujikunja baada ya kulowa.
Lakini wanasayansi baada ya kufanya
utafiti kwa muda merefu juu ya nini
hasa hupelekea ngozi kujikunja?
Walisema HAPANA si kwa sababu ya
ngozi kulowana. Na walikuja na
majibu haya.
Mwili unapokutana na majimaji mara
moja hupeleka taarifa na kutafsiri
kwamba mazingira hayo yana UTELEZI
(Slippery) hivyo kutasababisha mikono
kushindwa kushika (Grip) au kukamata
vitu kwa urahisi kutokana na utelezi
huo. Hapo mwili huchukua hatua ya
haraka kuikunja ngozi ya mikono yako
ili kurahisisha ushikaji wa vitu
vinavyoteleza ndani ya maji pamoja na
kutembea kwenye utelezi.

6. VIPELE VIPELE VYA BARIDI KWENYE
NGOZI (GOOSEBUMPS)
Kazi kubwa ya vipele hivi ni kupunguza
kiasi cha joto la mwili linalopotea
kupitia matundu ya ngozi. Hivyo kwa
kufanya hivi humfanya binadamu
kutunza joto la mwili hata katika
mazingira ambayo hali yake ya hewa
si rafiki kwa mwili wa mwanadamu au
ni yenye baridi sana.

7. MACHOZI (TEARS)
Zaidi ya kuwa majimaji (MUCOUS
MEMBRANE ) yanayopatikana kwenye
Macho ambayo kazi zake ni kulilinda
jicho dhidi ya kitu chochote kigeni
kinachoingia jichoni (mfano
unapokata vitunguu au mdudu
anapoingia jichoni huwa unatoa
machozi mengi eeeh!! Pia dhidi ya
upepo na moshi) na pia hutumika
kama kilainishi cha jicho pale
linapokuwa linazunguka zunguka
(blink).
Vilevile machozi yana kazi ya
kupunguza HISIA ZA HUDHUNI
zinazozalishwa mwilini. Wanasayansi
wanaamini kuwa mtu anapokua
mwenye msongo wa mawazo (stress)
mwili hutengeneza kitu kipya ili
kwenda kubugudhi na kuharibu
maumivu yote ambayo mtu anajisikia.
Hivyo machozi yanayozalishwa hapa
huwa na kemikali na yanafahamika
kama NATURAL PAINKILLER. Machozi
haya ni tofauti na machozi ya kawaida,
lengo lake hasa la kuzalishwa ni kwa
ajili ya kuondoa kabisa maumivu
yaliyozalishwa mwilini
Hivyo mpaka hapa tumeona kua kuna
machozi ya aina tatu ambayo ni
i. Basal tears (vilainishi)
ii. Reflex tears (mlinzi)
iii. Emotion tears (mtuliza maumivu)

8. KUSHTUKA USINGIZINI
(MYOCLONIC JERKS or HYPNIC JERK).
Je! Ushawahi kutokewa na hali hii?
umelala halafu ghafla unashtuka
usingizini kwa mguvu nyingi kama
umepigwa na shoti ya umeme na akili
inakurudi ghafla huku mapigo ya
moyo yakikuenda mbio? Na hali hii
ikakutokea pasipo hata kuota ndoto
yoyote?
Basi usiogope au kuwasingizia watu
uchawi, hii ni hali ya sayansi ya
mwili.na ni njia moja wapo katika ile
mifumo ya mwili kujilinda.
Je hutokeaje?
Hii ni hali ya ajabu sana isiyofanywa
kwa hiari ambayo huwatokea watu
mara tu wamejinyoosha kitandani na
kupitiwa na usingizi, mwili
hutetemeshwa na kusukumwa kwa
nguvu na mtu hushtuka katika hali
kama vile kapigwa na shoti ya umeme.
Hali hii inaweza kupelekea mtu hata
kuanguka kitandani na humwamsha
mara moja kutoka usingizini.
Wanasayansi wanatuambia kua, pale
tu unapopata usingizi kiwango cha
upumuaji kinashuka ghafla, mapigo ya
moyo nayo taratibu yanapungua,
misuli inatulia kwa ku-relax, Kitu cha
AJABU hapa ubongo unatafsiri hali hii
kama ni DALILI ZA KIFO (brain’s
misinterpretation of muscle
relaxation), hivyo huchukua hatua za
haraka za kuushtua mwili kwa
kuutetemesha au kuuskuma kwa
nguvu, hali ambayo humfanya mtu
kuamka kutoka usingizini kwa KURUKA
kitu ambacho ni hali isiyo ya kawaida.
Hali hii ikimtokea mtu huambatana na
kuongezeka kwa mapigo ya moyo
(rapid heartbeat), kuhema haraka
haraka, na wakati mwingine mtu
hutokwa na jasho jingi.
Wakati mwingine mtu huamka ametoa
macho na kama ukimwangalia, nae
huishia hukuangalia tu huku akikosa
la kukujibu endapo utamuuliza vipi
kuna tatizo gani?
MWILI WAKO NI ZAIDI YA
UNAVYOUJUA. JAMBO LA MSINGI NI
KUONDOA HOFU KWANI MWILI WAKO
UNAJUA NINI UFANYE NA WAKATI
GANI ILI KUKULINDA USIKU NA
MCHANA KATIKA SIKU ZOTE ZA
MAISHA YAKO.

Utoto raha..! Angalia hawa watoto wanachokifanya sasa

Leo nimepulizia Air Fresh yenye Harufu ya Pilau nyumbani kwangu sasa watoto wa Jirani wamehamia Mlangoni kwangu ndio wanacheza hapo. Kila nikitoka wananisalimia. Mama yao ndio kanimaliza kabisa nimetoka akaniambia

“Kumbe wewe ni Mpishi mzuri, Hongera”

Imebidi nisirudi nyumbani maana wale watoto wanaweza kuingia ndani kabisa na pilau hakuna.

#UTOTO RAHA 😂

😂😂😂😂👆🏻👆🏻👆🏻

Hapo sasa patamu, cheki jamaa alivyowezwa na huyu dogo

Mfugaji mmoja alikwenda kwa mfugaji mwenzake (ambae pia ni bwana mifugo wa eneo lao) asubuhi moja. Alipobisha hodi mtoto wa kiume wa umri upatao miaka 12 akamfungulia mlango. Mazungumzo yafuatayo yakafuatia:

Mkulima: Baba yako yupo?

Mtoto: Hapana Mzee, amekwenda mjini.

Mkulima: Mama yako?

Mtoto: Nae kaenda mjini na baba.

Mkulima: Kaka yako Howard yupo?

Mtoto: Nae hayupo, wote yeye, baba na mama wamekwenda mjini. Kwani una shida gani? Kama kuna kitu unahitaji niambie maana nimeachiwa funguo na najua vifaa vinapowekwa.
Mzee akawaza kidogo halafu akasema: Kwa kweli nilitaka kuongea na baba, mama au kaka yako kwa kuwa kaka yako amempa mimba binti yangu.

Mtoto akafikiria kidogo halafu akasema: Kusema ukweli itabidi umsubirie baba, ila kwa kukusaidia ni kuwa baba hulipisha shilingi laki moja kwa kupandisha dume la ng’ombe na elfu hamsini kwa beberu. Ila sijui baba hutoza shilingi ngapi kwa Howard akifanikiwa kutia mimba.

Elimu ya biashara

Jifunze kujikagua, jifunze kujiuliza je hapa ndipo napotakiwa kuwa? Usifurahie tu kwamba upo hapo kwa muda mrefu yamkini unaona panakufaa and you are settled lakini ukweli ni kwamba sio pako na haukutengenezwa kuwa hapo. Hata kama tai ataonekana kwenye banda la kuku lakini ukweli ni kwamba tai kaumbiwa kuwa angani tofauti na kuku aishie bandani. Jiulize hapo ulipo ni pako??

Na ndio maana kwenye maisha, mafanikio ya leo ni matokeo ya tulichojifunza kutoka kwa waliopita, baada ya wao kukosea mahali nasi tukaboresha, na kwa hakika vizazi vijavyo navyo vitaendelea kurekebisha pale tunapokosea sisi na hii yote ndiyo huleta ladha ya maisha. Ukipitia Changamoto mwenyewe na ukapambana kujikwamua mwenyewe, utapata somo litakalokufunza zaidi kuliko kusimuliwa changamoto walizopiti wengine.

Maisha ni Maamuzi, aliyekula Sahani mbili za wali mchana ili usiku asile tena, anaweza kuwa sawa na aliyeamua kutokula Mchana ili usiku ale sahani mbili za wali, japo hawa hawawezi kuwa sawa sawia na aliyeamua kula sahani moja ya wali mchana na moja ya wali usiku, Ijapokua mwisho wa siku wote wamekula sahani Mbili za wali kwa siku. Jumapili Njema kwenu nyote.

JIKUNG’UTE….JIPANGE…..ANZA……

Hii ndio ndoto ya harusi ya kila msichana anayotamani

GIRL: Baby, hebu niambie harusi yetu itakuwaje?
BOY: Yaani hii haijawahi kushuhudiwa, ngoja nikupe kionjo kidogo tu
GIRL: Enhee…
BOY: Kwanza siku ya kupeleka mahari nitaswaga zizi zima la ng’ombe napeleka kwa babu yako
GIRL: Ooh baby u care..
BOY: Siyo hivyo tu, baba yako ntamnunulia Range Rover Sport na mama mkwe ntampa Range Rover Evoque
GIRL: Baby u are awesome…
BOY: Halagu mdogo wako wa kiume ntampa Prado Tx, na hapo nimesukutua tu mdomo sijaanza kula….
GIRL: Enhee…na sisi??

BOY: Sisi tutachukua mtaa mzima Oysterbay, kila wiki tutaishi nyumba tofauti
Halafu siku ya harusi yetu tutakodi zile meli zinabeba makontena ndiyo iwe ukumbi wetu, itatupeleka hadi Maldives
GIRL: Baby I love you
BOY: Tukitoka hapo tunaenda honeymoon Bahamas….halafu tunaenda Taiwan shopping ya fenicha, kisha Japan shopping ua electronics, halafu tunaenda Dubai nikununulie vito vya thamani
GIRL: Ooh my sweetheart…halafu tukitoka huko??
BOY: Tukitoka huko nachukua ndoo ya maji nakumwagia uzinduke usingizini na ndoto yako imeishia hapo

Angalia jinsi muda wako unavyopotea

Kila mtu ambaye ni hai amepewa muda Wa masaa 24 kila siku,168 kwa wiki,672 kwa mwezi,8064 kwa miezi 12 au kwa mwaka.

Katika hayo masaa 24 unayoyapata kila siku unayatumiaje katika suala zima la kukufikisha katika ndoto na malengo au mafanikio yako?

Kwa nini kuna matajiri na maskini na wote tunapewa masaa 24???
Tucheki mgawanyo Wa masaa 24 ulivyo….katika masaa 24 unayopewa kwa siku masaa 8 ni ya kazi,masaa 8 ni ya kulala na masaa 8 ni ya kufanya mambo yako mengine.

Tuseme katika Masaa 8 kwa ajili ya mambo yako mengine labda masaa manne yanapotea katika foleni au purukushani za maisha kama kula nk.
Je haya mengine manne yanaenda wapi?Tunayapotezea wapi?
Kwenye mpira?kwenye movie?kwenye TV?kwenye mitandao ya kijamii?kukaa na kuwajadili wengine na mashosti?

Hivi unajua kwa siku una wastani Wa kupoteza masaa manne kwenye masaa yako 24??
Kwa wiki unapoteza masaa 28 hali kadhalika masaa 112 kwa mwezi hupotea.
Kwa mwaka mmoja wenye masaa 8760 una wastani Wa kupoteza masaa 1344 ambayo ni sawa na siku 56 kwa mwaka kwa makadirio ya haraka haraka.

Kwa maana nyingine kwa kutumia hii “concept” kila miezi 12 ya mwaka mzima unapoteza miezi miwili kwa mambo ambayo sio “productive”.
Hii ni sawasawa na kupoteza mwaka mmoja ndani ya miaka 6…kwa maana nyingine kwa “the same concept” ya masaa 4 kwa siku kupotea ni kwamba unapoteza mwaka mmoja kwa mambo ambayo hayakusaidii chochote.

Hebu jiulize hapo ulipo una umri gani?umeshapoteza miaka mingapi kwa mambo ambayo sio productive??
Kama wewe ni mfanyakazi au muajiriwa ukifanya kazi kwa muda Wa miaka 40 au kwa muda Wa miaka 40 unapoteza miaka 6.6.

Je hebu jiulize muda wote huo unaoupoteza kwenye mambo ambayo sio “productive” ungekuwa ni muda ulioutumia vizuri kwa mambo ya uzalishaji mfano kuanza kidogo kidogo kujenga biashara yako sasaivi tungekuwa na mamilionea na mabilionea wangapi?
Ili uweze kujenga biashara ambayo ni “strong” inakuhitaji angalau uijenge kwa muda Wa miaka mitano kwa maana nyingine kwa kutumia masaa manne tu kwa siku ndani ya miaka 40 utakuta tayari wewe ni milionea na baada ya kustaafu ajira usingeanza kuangaishana na pensheni (kwanza ni shilingi ngapi) au kuanza kubembeleza kuomba uongezewe mkataba au kwenda kufanya tena part time employment…..kwa concept hiyo ni mamilionea wangapi tumewapoteza??

Ndio maana katika hii dunia yetu tunayoishi matajiri wote ni 3% na 97% ya watu waliobakia wanawafanyia kazi matajiri.
Matajiri waliweza kuiona hii concept kwa jicho la Tatu na wakaanza kuifanyia kazi and the rest is history.
Huwezi kumkuta tajiri anapoteza muda wake kwa mambo ya kizembe yasiyomuingizia chochote ndio maana matajiri wanazidi kuwa matajiri na maskini wanaendelea kuwa maskini.

Lakini bado muda na nafasi unayo sasa ukiamua na ukianza kuutumia muda wako ulio nao kwa ajili ya kuyatengeneza maisha yako.
Watu wengi hawako tayari kuumia na kujifunza biashara na kuielewa ndani ya miaka mitano itakayowapelekea kuwa matajiri na kuweza kuyafikia malengo na ndoto zao lakini wapo tayari kuajiriwa na kufa maskini ndani ya miaka 40.

Muda mzuri ndio sasa Wa kufanya maamuzi sahihi Wa kuyawekeza masaa manne kwenye biashara ili uje upate matokeo chanya.

Baada ya mwanamke kukataa kufungua mlango angalia kilichomkuta

MUME: Fungua mlango!

MKE: Leo sifungui! Nimechoshwa na ulevi wako.

MUME: kama hufungui najitupa kwenye hili shimo nife kabisa.

MKE. Kufa huna faida yoyote duniani!

MUME kachukua jiwe kubwa kalitupa kwenye shimo chubwiiiiiii!

MKE kajifunga kanga, kafungua mlango. Ghafla mume kaingia ndani na kumfungia mke nje.

MKE: Nifungulie la sivyo nitapiga kelele majirani waje.

MUME: Piga kelele na wakija uwambie unakotoka usiku huu na khanga moja.

Padri Akimbia wakati wa kuungamisha, chanzo ni hiki

Padri alikuwa amekaa katika confession booth kanisani
peke yake.
Mara kukaingia jamaa mmoja akapiga magoti upande wa
pili, akafanya ishara ya msalaba kisha akaanza kuungama
{confess}
“Padri nimekuja kuungama dhambi zangu, leo nimefanya
dhambi kubwa sana.”
Padri, “Endelea…”

“Bosi wangu aliniita nyumbani kwake, akaniambia
amegundua nimeiba shilingi millioni 100 kazini. Akasema
nisipozitoa atanipeleka polisi, sa kwa ukweli mi naogopa
kufungwa.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu,nikatoa bastola nikamuua….. Yesu atanisamehe?”

Padri: “Utasamehewa.”
“Basi wakati nataka kuondoka nikasikia mlango
unafunguliwa kutazama, Loh! Mke wa bosi, alipoona
kilichotokea akasema anapiga polisi simu.
Kutazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu, nikamuua na yeye pia… Yesu atanisamehe hilo?”
Padri: “Utasamehewa.”

Nikatoka nje, nikawasha gari niondoke, lakini mlinzi
akakataa kunifungulia, ati amesikia mlio wa
bastola. Nikaona ataniletea kizuizi huyu.
Nikatazama huku na huku nikagundua tuko wawili peke
yetu, nikamuua….. Yesu atanisamehe?”
Padri:”Utasamehewa.”

“Nikajifungulia geti mwenyewe nikaenda
nyumbani, wakati napanga kuja kuungama mtoto wa bosi
akabisha hodi, nikawaza mambo gani tena, akasema alirudi
nyumbani na kukuta yaliyotokea akanionesha diary ya
babake, inayoonesha nilikuwa na appointment naye
wakati nilipomuua. Nikamuuliza nani mwingine anayejua?
Akasema ameanzia kwangu kisha anaenda polisi.

Nikatazama huku na huku nikakuta tuko wawili peke
yetu, nikamuua….. Yesu atanisamehe na hilo?”

Kimyaa….
“Padri yesu atanisamehe?”
kimya….

Jamaa akatazama kwenye confession booth padri
hayupo, lakini kwenye kona moja akaona kabati la nguo
za mapadri linatikisika. Kufungua akaona padri kajificha ndani anatetemeka huku akitokwa na jasho.

Jamaa, “Sasa baba mbona umekimbia?”
Padri kwa taabu akajibu, “Nilitazama huku na huku
nikagundua tuko wawili peke yetu…….”

Kutibu chunusi kwa ute mweupe wa yai

Hii inaweza kuchukuliwa kama njia rahisi na isiyo na gharma katika kutibu chunusi. Kwa mjibu wa wanasayansi kutumia mchanganyiko wa ute mweupe wa yai na maji maji ya limau ni namna nzuri ya kutibu chunusi.

Changanya ute mweupe wa mayai matatu na kijiko kidogo kimoja cha maji maji ya limau na ukoroge vizuri. Pakaa mchanganyiko huu usoni na uache kwa dakika 15 hivi kisha jisafishe na maji moto.

Fanya zoezi hili mara 1 au 2 tu kwa wiki

Ujanja alioutumia msichana wa kazi ili apandishiwe mshahara na mama mwenye nyumba

Msichana wa kazi alitaka mama mwenye nyumba ampandishie mshahara….. Mama mwenye nyumba akamwambia msichana ampe sababu tatu za kutaka kupandishiwa mshahara.

Msichana: Napika vizuri kuliko wewe.

Mama: Nani kakuambia?
Msichana: Baba kaniambia.

Mama: ok. Sababu ya pili?
Msichana: Napasi nguo vizuri kuliko wewe

Mama: Nani kakuambia na hili?

Msichana: Baba pia kaniambia

Mama: ok, na sababu ya tatu?

Msichana: Najitahidi kitandani kuliko wewe.

(Hapa mama kaonekana kutaka kujua zaidi na akawa tayari kujiandaa kumrukia akate kichwa cha binti mara moja)

Mama: Mume wangu kakuambia na hili pia?

Msichana: Hapana ni Shamba boy kaniambia mimi najitahidi kitandani kuliko wewe.

Mama: Tafadhali punguza sauti baba yako asisikie. Nitakupandishia mshahara wako mara tatu…….

SMS nzuri ya mapenzi ya kutakia usiku mwema

Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka.
Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika.
Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka.
Kitale katikati yake ukila utaridhika.
Matamu na maji yake hukata kiu haraka.
Weupe watui lake lina ladha ukipika.
Kupaka mafuta yake mwili hulainika.
Na kwenye machicha yake kazi nying hufanyika.
Hata na upepo wake uvumapo utacheka.
Sikijui kitu chake kipi kisichotumika.usiku mwema

Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About