SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Unachotakiwa kujua kuhusu Shinikizo la chini la damu

Ugonjwa wa Shinikizo la chini la damu ambao hujulikana kama hypotension kwa Kiingereza ni hali ambayo shinikizo la damu ya mtu linakuwa chini sana.

Dalili za ugonjwa wa shinikizo la chini la damu

  1. kizunguzungu,
  2. uchovu,
  3. udhaifu,
  4. kupumua kwa shida,
  5. kupungua kwa nuru ya macho nk

Shinikizo la kawaida la damu vipimo vinatakiwa visome 120/80 mm Hg.

Ikiwa vipimo vitasoma una 90/60 mm Hg au chini ya hapa, una shinikizo la chini la damu. Shinikizo la damu linapokuwa chini zaidi linasababisha msukumo ulio chini wa damu kwenye ogani kama ubongo, figo, na kwenye moyo.

Mambo yanayosababisha shinikizo la chini la damu

  1. kupungua kwa maji mwilini,
  2. kulala sana,
  3. lishe duni,
  4. kushuka kwa wingi wa damu,
  5. matatizo ya moyo,
  6. ujauzito,
  7. Baadhi ya dawa za hospitalini
  8. homoni kutokuwa sawa nk.

Unaposhughulika na shinikizo la chini la damu inashauriwa kuongeza matumizi ya chumvi na maji. Hata hivyo wasiliana na daktari wako wa karibu kabla kuamua lolote mwenyewe binafsi.

Ugonjwa huu unaweza kupona japo Kupona kabisa kunategemea na aina hasa ya chanzo chake.

Njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke

Njia za kuamsha hamu ya kufanya mpenzi ya mwanamke au Hatua za kufuata kuamsha hisia za mwanamke ni kama ifuatavyo

Andaa mazingira

Andaa mazingira ya kuamsha hisia zake, fanya kitu kitakachowasogeza karibu na kuamsha hisia zake Kwenye akili yake kabla ya kugusa mwili. Mfano, weka mziki au muvi nzuri n.k. Kisha tengeneza mazingira ya kuwa karibu kimwili na kugusana.

 

Kaa kwa kubanana naye

Unapokuwa na mwanamke ambaye umemzimia, tafuta kisababu cha kukaa na yeye karibu. Toa simu muangalie pamoja videos kama vile za kuchekesha, ama unaweza kuchukua kitabu/gazeti umuonyeshe habari ambazo anapenda ilimradi tuu muwe karibu.

Usimwonyeshe/usiongee wazi kile unachotaka

Usijaribu kutumia lugha ya kutongoza ama utamfanya aanze kukushuku. Tayari anajua kuwa miguso ya mikono yako ya mara kwa mara inaashiria kitu fulani. Kile unachotakiwa kufanya ni kuivuruga akili yake kwa kuleta mada ambayo itamvutia huku ukiendelea gusa mwili wake

 

Anza kutumia lugha ya kumsuka

Wakati mtakuwa mnaendelea unaweza kutumia maneno ya kumsuka lakini yawe ya kichini chini. Mfano unaweza kumwambia “Unanukia utamu”, “nimependa kitambaa cha nguo yako”,”nishawahi kukuambia kuwa macho yako yanapendeza? Nimependa vile yanang’aa nikiwa karibu yako.” Maneno kama haya unaweza kumrushia mwanamke huyu bila hata yeye kusongea mbali na wewe. Mwanzo atakuwa anapenda kuyaskia.

Isome miondoko yake

Ukianza kumuona anazungumza polepole na kukusongelea karibu yako, ishara kuu ni kuwa yupo tayari. Kwa hiyo kufikia hapa unaweza kurudia hatua za kumsuka, kumgusa na kujaribu kufikia viungo vyake vingine vya mwili ilimradi nyote wawili mnafurahia.

 

Mbusu

Baada ya kuandaa mudi au mazingira na kuamsha hisia zake sasa tafuta namna ya kumbusu. Mbusu taratibu kwa namna ambayo haitamshtua na kumfanya aogope au akatae.

Mhikeshike

Wakati wa kumbusu mshike mwili wake ili kuamsha hisia zake. Anza na mikono kasha rudi kichwani Kwenye nywele zake na kisha maliza sehemu nyingine za kuamsha hisia zake

Usimlazimishe bali mbembeleze

Kama hataki usimlazimishe bali mbembeleze au muache mpaka wakati mwingine atakapokuwa tayari.

 

NB: Ni makosa makubwa na ni dhambi kufanya mapenzi kabla ya ndoa. Mbinu hizi zitumie kwa mwenzi wako wa ndoa

Yafahamu Mambo Mbalimbali kuhusiana na Wanawake kwa Ku-Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Kitabu hiki kina topiki Zifuatazo;
1. Mambo anayohitaji mwanamke kutoka kwa Mwanaume
2. Mambo yanayowavutia wanawake kutoka kwa wanaume
3. Mambo wanayoyapenda wanawake wakati wa kufanya mapenzi
4. Dalili za mwanamke kicheche
5. Maswali ya kujiuliza kama mwanamke anakupenda kwa dhati au anakudanganya
6. Tabia za mwanamke anayekupenda lakini hawezi kusema
7. Ishara za mwanamke aliyevutiwa na wewe
8. Dalili za mwanamke anayeelekea kukukubali
9. Mambo ambayo mwanamke hawezi kukwambia
10. Njia za kudumisha na kuamsha mapenzi na mwanamke

Kitabu hiki ni Soft copy [pdf] kwa hiyo unaweza kusoma moja kwa moja kirahisi kabisa hata kwenye simu yako. Utatumiwa Kopi ya kitabu hiki kwenye email yako na utaweza kukihifadhi na kusoma wakati wowote utakaotaka.

Faida za mnyonyo na mazao yake

Nyonyo Mbarika (Castor)
Mnyony(KiSwahili) Erand (KiHindi) Kastorka(KiRusi) ni mmea wa jamii ya Mbono Kaburi, kwa
jina la kitaalamu Japtropha

Baadhi ya faida za mnyonyo na mazao yake

Mbali na kuweza kutumia mnyonyo kama uzio hai,njia hii inaweza
kutumika kwa wale wasio na eneo kubwa la shamba ndipo sasa wakapata faida zake kama
ifuatavyo:🔽

Majani ya mnyonyo yanaweza kutumika kama tiba ya ugonjwa wa Kifua Kikuu (TB), kukanda
(massage) ili kuondoa maumivu na majani haya
yakifungwa kwenye mguu unaouma huleta nafuu hasa kwa maumiviu yanayokuja baada ya kuteguka, pia hutumika kutibu uvimbe kwa wanyama.

Mizizi ya mnyonyo huweza kutumiwa kama dawa
ya mafundo fundo, uvimbe, kuungua, macho ya
manjano, kuumwa koo na magonjwa ya
kuambukiza ya kisonono na kaswende. Ukijaza
maji baridi kwenye kikonyo cha mnyonyo na
kumpa mtu mwenye kwikwi kila baada ya dakika
mbili au tatu hivi, mara nyingi huondoa
usumbufu unaoletwa na kwikwi. Mbegu/Punje/Tunda/Njugu za mnyonyo zikimezwa na maji bilauri moja kila siku kwa muda wa siku tano huweza kutibu maumivu yaliyosababishwa na kuungua. Vile vile, mbegu hizi huweza kusagwa na kisha kuenguliwa mafuta
kwa ajili ya kulainisha mashine na mitambo viwandani. mbegu za mnyonyo kabla ya kukomaa
Mafuta
yatokanayo na
mbegu za nyonyo mfano
Ricinoleic Acid,
Oleic Acid,
Linoleic Acid
nk hutumika
kutibu ugonjwa
wa wa jongo
(rheumatism)unaowakumba watu wengi wanaoishi maeneo ya miinuko na
baridi, pia hutibu ugonjwa wa mifupa ujulikanao kwa jina la kitaalamu kama arthritis na gauti. Mafuta ya mnyonyo pia yanaweza kutumika
kama njia ya kupanga uzazi kwani yana kiasi
fulani cha sumu ya protini ijulikanayo kitaalamu kama ricin ambayo ikitumiwa kwa kiasi kidogo huharibu utungo,huweza pia kutumiwa kama
mafuta ya kupaka ama losheni katika sehemu za
siri ili kuua mbegu za uzazi za kiume wakati wa tendo la kujamiiana. uzazi wa mpango.

Tahadhari:

Mnyonyo ni mti wenye sumu
inayoweza kuua binadamu au
wanyama endapo itatumika kuzidi
kipimo. Mazao yoyote yatokanayo na mnyonyo huhatarisha au/na
kuharibu mimba na hata kuweza
kusababisha kifo cha mjamzito,
hivyo, matumizi yake lazima yawe
ya uangalifu mkubwa. Mafuta ya Ricinoleic acid
yanayopatikana kutokana na mnyonyo vile vile yanaweza kutumika kurekebisha hedhi
(mzunguko wa damu ya mwezi kwa wanawake) ikiwa mzunguko
umechelewa ama kusimama katika
umri usiotarajiwa. Huweza pia
kupunguza maumivu makali
yanayotokea wakati wa hedhi.

Mafuta ya mnyonyo yanayojulikana
kitaalamu kama Undecylenic Acid
huweza kutumika kutibu magonjwa
mbalimbali ya ngozi na vidonda
vinavyosababishwa na bakteria ama ukungu(fungus). mbegu za mnyonyo baada ya kukomaa

Akina mama wanaonyonyesha pia wanaweza kutumia mafuta
baridi ya mnyonyo (kiasi kidogo ili kuepuka madhara ya mafuta hayo kwa mtotokumbuka
hapo awali nimeandika kuwa mafuta haya
yakitumiwa kwa kiwango kikubwa ni sumu ) kuongeza wingi na mtiririko rahisi wa maziwa.

Nywele nzuri, safi, nadhifu na zisizokatika pia
ngozi imara inapatikana kutokana na matumizi ya mafuta ya mnyonyo.Mafuta ya mnyonyo pia ni
dawa nzuri ya kufungua tumbo la uyabisi(kuvimbiwa).

Mnyonyo unaweza pia kuwafaa watu wanaoishi na VVU (Virusi Vya UKIMWI) kwani mafuta yake ni sumu ya kuua vimelea vya
magonjwa kama vile bakteria na ukungu(fungus).

Njia:

Kupakaza: Chukua kipande cha nguo ama
kitambaa, kisha kiloweke kwenye mafuta ya
mnyonyo ndipo ufunge katika kiwiko ama
eneo lenye maumivu ama kidonda.Vinginevyo
chukua kiasi cha mafuta na kupaka eneo linalohusika mfano, penye kidonda, kuugua
ama pakaza kichwani au juu ya tumbo wakati
wa maumivu ya hedhi nk. Unaweza kuacha kwa muda wa saa moja kabla ya kunawa ili uipe ngozi muda wa kunyonya kiasi cha
mafuta. Unaweza kujifunga kitambaa hicho
tumboni ama mgongoni kama kibwebwe na kuendelea na shughuli za kawaida.

Kunywa: Chemsha mbegu chache za mnyonyo
pamoja na maji na maziwa kisha unywe kiasi kidogo kadiri ya nusu hadi bilauri moja ya ujazo wa mili lita mia mbili na arobaini.

Kusafisha utumbo: Kunywa mafuta ya mnyonyo vijiko viwili vikubwa vya chakula asubuhi, kisha pumzika kwa saa mbili ndipo unywe maji glasi mbili na endelea kunywa maji glasi moja kila baada ya saa moja.

Sababu ya tatizo la Tumbo kujaa gesi na jinsi ya kujitibu

Tatizo la tumbo kujaa gesi husababishwa na kumeza chakula pamoja na gesi inayotolewa katika vyakula mbalimbali tunavokula ambayo hujaa tumboni na kwenye utumbo mdogo. Hali hii husababisha tumbo kujaa au kuvimba na mtu hutoa gesi hiyo kwa njia ya ushuzi na kubeua.

Nini husababisha.

Tatizo ili mara nyingi husababishwa na huambatana na mambo yafuatayo:
1. Kula vyakula vyenye mafuta mengi ambayo huchelewesha tumbo kufunguka kwa ajili ya usagaji wa chakula.

2. Kunywa vinywaji vyenye Carbonates, cola na kula vyakula vyenye gesi kama maharage, bigiji, vitunguu, kabichi n.k

3. Msongo wa mawazo na hasira.

4. Kula haraka haraka na kula unaongea.

5. Uvutaji wa Sigara

6. Magonjwa na maambukizi katika mfumo wa chakula asa kwenye tumbo na utumbo ambayo huzuia kusagwa na kufyonzwa kwa chakula.

Jinsi ya kujitibu.

· Kunywa chai ya tangawizi au karafuu itasaidia kupunguza gesi.

· Unaweza kunywa glasi moja ya juisi ya Limao baada ya kula.

· Tafuna mbegu za maboga zinasaidia kulainisha mfumo wa chakula

· Lalia ubavu wa kushoto na pumua kwa kasi ili kupunguza gesi tumboni.

· Kunja miguu na ikalie uku ukinyoosha mikono na kuinamia mbele itasaidia.

· kuongeza kasi ya mfumo wa chakula kufanya kazi na kuondoa gesi.

· Fanya mazoezi mepesi ya kutembea na kuruka ruka.

· Kula na tafuna chakula taratibu na epuka vyakula vyenye gesi na mafuta mengi,.

· Nenda hospitali kama tatizo ili linaambatana na kuharisha, kutapika, maumivu makali ya tumbo, kinyesi chenye rangi tofauti au damu na maumivu ya kifua.

Mambo muhimu kujua Kuhusu Uvimbe kwenye kizazi cha mwanamke

Naamini umeshawahi kusikia kuhusu changamoto ya uvimbe kwenye kizazi kwa Wanawake yaani Fibroids. Uchunguzi unaonesha kuwa kati ya asilimia 30 mpaka 70 ya wanawake wapo kwenye hatari ya kupata tatizohili au wengine Tayari wameshalipata. Mpaka hivi sasa hakuna Sababu ya moja kwa moja ambayo inaelezwa kama chanzo cha tatizo hili.

JE NI NANI YUPO HATARINI ZAIDI KULIPATA UVIMBE KWENYE KIZAZI?

Ni Wanawake ambao wanakaribia kukoma hedhi (Menopause) hasa wa kati ya miaka ya 38-45.
Pia Wanawake wanene au wenye Matumbo makubwa (Obesity)
Pia wanawake wasiokuwa na watoto wapo kwenye hatari zaidi ukifananisha na wale wenye Watoto.

DALILI ZA UVIMBE KWENYE KIZAZI NI ZIPI

Tatizo hili linaweza kuwa na Dalili au Kutokuwa na Dalili kabisa. Lakini kwa mara nyingi Dalili zake ni hizi…

👉🏿Kutoka kwa Hedhi nzito pia kwa muda zaidi ya kawaida.
👉🏿Damu kutoka kipindi ambacho sio cha siku zake.
👉🏿Maumivu ya Sehemu za Kiuno.
👉🏿Maumivu ya Chini ya Mgongo.
👉🏿Kwenda haja ndogo mara nyingikwa hali isiyo ya kawaida.
👉🏿Maumivu wakati wa tendo la ndoa.

Sio lazima uwe na Dalili zote na mara nyingi hazitokei zote hasa ni moja au mbili.

Hivyo Kujikinga au kuepukana na Tatizo hili ni vyema kwa Mwanamke ukapungua Uzito hasa Kitambi au Tumbo kubwa.

Kisa cha mzaramo na mchaga

MZARAMO V/S MCHAGA.
Mzaramo alitangaza anatibu magonjwa yooooooote
kwa tsh. 100,000/=
Na kama akishindwa kukutibu anakurudishia laki
yako nakukuongeza laki nyingine.
MCHAGA akaona hii fursa yakujipatia hela aiwezi mpita akaenda kutibiwa.
MZARAMO: “unaumwa nini?”
MCHAGA: “Sisikii ladha ya aina yoyote mdomoni kabisaaaa..”
MZARAMO: “sawa, toa laki kabisa..”
Mchaga akatoa.
MZARAMO akamuagiza msaidizi wake; “Naomba kikopo no.27 mpe anywe huyu..”
MCHAGA akanywa akatema faster; “Puh puu puu, Aisee huu si mkojo huu..?”
MZARAMO: “Umepona karibu tena..”
Mchaga aka-mind sana Kesho yake akarudi tena hakuamini ameliwa pesa yake.
MCHAGA: aisee nina tatizo la kumbukumbu nasahau
sanaaaaa..”
MZARAMO akamwambia “hakuna tabu, toa laki tukupe tiba..’
MCHAGA akatoa pesa akijua leo lazima afanikiwe..’
MZARAMO: “nesi naomba kikopo no.27..”
MCHAGA: “ASA CHALII ANGU HICHO SI CHA JANA CHA MKOJO HICHO AISEE..?”
MZARAMO: “UMEPONA KUMBUKUMBU UNAYO.

😄😄😄😄😁😁😁😁😁😁

Una thamani gani?

Kazi au shughuli unayoifanya ina thamani gani kwa wengine?unawasaidia au unawaumiza??
Biashara unayoifanya ina thamani gani kwa wengine?ni lazima uwaumize ndipo ufaidike au uwasaidie ili nawe upate faida?

Elimu yako uliyo nayo ina faida au thamani gani kwako na kwa wengine?unawadharau na kujiona wewe ndiye msomi pekee au unawasaidia?

Una thamani gani kwa ndugu,jamaa,marafiki na majirani zako?unasaidiana nao katika kila kitu au unajiona wewe ndiye matawi ya juu unyenyekewe?

Una faida au thamani gani kwa wasiojiweza??umewahi kuwasaidia chochote?kuwatembelea watu wenye Shida mbalimbali kama wagonjwa,wafungwa nk

Kila unachokifanya kina thamani yoyote kwa wanaokuzunguka??
Kumbuka mafanikio ni kugusa maisha ya watu wengi kwa kuwasaidia wao kwanza wafanikiwe ndipo Baraka za mafanikio zitamwagika kwako.
Mafanikio sio wengine waumie ndipo uyaone mafanikio.

Jifunze kuwasaidia wengine waweze kutimiza malengo na ndoto zao ndipo nawe Mungu atakubariki kufikia ndoto zako.

Kumbuka kuna watu wengi wapo nyuma yako wanakusubiri wewe ubadilike ndipo nao waweze kuungana na wewe muweze kufanya kitu cha maana na chenye thamani kwa wengine.

Aina kuu ya mizinga bora ya nyuki kwa ajili ya kupata asali nyingi

Mizinga ya Kifuniko juu (Top bar)

Hii ni aina ya mizinga inayotumika sana na wengi. Gharama yake ni ndogo kiasi kulinganisha na mingine. Ni aina nzuri sana kwa mtu anaeanza ufugaji wa nyuki kwa kuwa ni wa gharama nafuu. Mfugaji wa nyuki anaweza kutengeneza mzinga Yya aina hii mwenyewe kama ana utaalamu wa useremala.

 

Mzinga wa Top bar

Faida ya Mizinga ya Kifuniko juu (Top bar)
• Ni rahisi kukagua asali iliyo tayari.
• Ni rahisi kuvuna asali kuliko kuvuna toka kwenye mzinga wa kienyeji.
• Ni rahisi kuwatunza nyuki wakati wa kiangazi na inapokuwa hakuna maua. Kwa mfano unaweza kuwapatia nyuki chakula ili kuongeza uzalishaji wa asali.
• Ni rahisi kurina asali ukilinganisha na mizinga ya magogo inayotundikwa juu ya mti, kwa kuwa haihitaji vifaa maalumu.
• Aina hii ya mizinga huwekwa kwa kuninginia jambo ambalo siyo rahisi kushambuliwa na wadudu/wanyama wanaokula asali kwa kuwa Inajaa haraka sana wakati ambao ni msimu wa asali kutengenezwa kwa wingi.

Hasara ya Mizinga ya Kifuniko juu (Top bar)
• Kichane kwenye mzinga wa boksi hakina kishikizo hivyo huvunjika kwa urahisi sana kama hakitashikwa kwa uangalifu.
• Masega huvunwa pamoja na asali, kwa hiyo nyuki wanalazimika kutengeneza tena masega mengine ambapo husababisha kupungua kwa uzalishaji wa asali.

Mzinga wa Langstroth

Mzinga wa Langstroth unaweza kukupatia asali zaidi kulinganishwa na mizinga mingine Hii ni aina nzuri na rahisa sana ya mzinga. Mizinga hii hufahamika kama mzinga wa fremu, kwa kuwa ina fremu ambazo vichane vya masega hujishikiza. Chumba kikubwa ambacho malkia hutagia mayai. Malkia anazuiliwa kuhama kwenda chumba kingine kwa kutumia waya. Kwenye chemba maalumu ya kutagia juu yake pana chemba ya kuhifadhia asali.

 
 

Mzinga wa Langstroth

Vichane vya masega vinatengezwa kwenye fremu na si kwenye nguzo kama ilivyo kwenye Top bar. Ili kuvuna asali, mfugaji akiwa na masega yaliyojaa asali, hutumia vifaa maalum kwa ajili ya urinaji na kuhifadhi asali bila kupata tabu.

Mzinga wa Langstroth ni gharama kiasi kulinganisha na mizinga mingine.Unaweza kuipata kutoka katika taasisi zinazojiusisha na uuzaji wa mizinga, taasisi na karakana binafsi, au wakala wa Serikali.

Angalia jinsi muda wako unavyopotea

Kila mtu ambaye ni hai amepewa muda Wa masaa 24 kila siku,168 kwa wiki,672 kwa mwezi,8064 kwa miezi 12 au kwa mwaka.

Katika hayo masaa 24 unayoyapata kila siku unayatumiaje katika suala zima la kukufikisha katika ndoto na malengo au mafanikio yako?

Kwa nini kuna matajiri na maskini na wote tunapewa masaa 24???
Tucheki mgawanyo Wa masaa 24 ulivyo….katika masaa 24 unayopewa kwa siku masaa 8 ni ya kazi,masaa 8 ni ya kulala na masaa 8 ni ya kufanya mambo yako mengine.

Tuseme katika Masaa 8 kwa ajili ya mambo yako mengine labda masaa manne yanapotea katika foleni au purukushani za maisha kama kula nk.
Je haya mengine manne yanaenda wapi?Tunayapotezea wapi?
Kwenye mpira?kwenye movie?kwenye TV?kwenye mitandao ya kijamii?kukaa na kuwajadili wengine na mashosti?

Hivi unajua kwa siku una wastani Wa kupoteza masaa manne kwenye masaa yako 24??
Kwa wiki unapoteza masaa 28 hali kadhalika masaa 112 kwa mwezi hupotea.
Kwa mwaka mmoja wenye masaa 8760 una wastani Wa kupoteza masaa 1344 ambayo ni sawa na siku 56 kwa mwaka kwa makadirio ya haraka haraka.

Kwa maana nyingine kwa kutumia hii “concept” kila miezi 12 ya mwaka mzima unapoteza miezi miwili kwa mambo ambayo sio “productive”.
Hii ni sawasawa na kupoteza mwaka mmoja ndani ya miaka 6…kwa maana nyingine kwa “the same concept” ya masaa 4 kwa siku kupotea ni kwamba unapoteza mwaka mmoja kwa mambo ambayo hayakusaidii chochote.

Hebu jiulize hapo ulipo una umri gani?umeshapoteza miaka mingapi kwa mambo ambayo sio productive??
Kama wewe ni mfanyakazi au muajiriwa ukifanya kazi kwa muda Wa miaka 40 au kwa muda Wa miaka 40 unapoteza miaka 6.6.

Je hebu jiulize muda wote huo unaoupoteza kwenye mambo ambayo sio “productive” ungekuwa ni muda ulioutumia vizuri kwa mambo ya uzalishaji mfano kuanza kidogo kidogo kujenga biashara yako sasaivi tungekuwa na mamilionea na mabilionea wangapi?
Ili uweze kujenga biashara ambayo ni “strong” inakuhitaji angalau uijenge kwa muda Wa miaka mitano kwa maana nyingine kwa kutumia masaa manne tu kwa siku ndani ya miaka 40 utakuta tayari wewe ni milionea na baada ya kustaafu ajira usingeanza kuangaishana na pensheni (kwanza ni shilingi ngapi) au kuanza kubembeleza kuomba uongezewe mkataba au kwenda kufanya tena part time employment…..kwa concept hiyo ni mamilionea wangapi tumewapoteza??

Ndio maana katika hii dunia yetu tunayoishi matajiri wote ni 3% na 97% ya watu waliobakia wanawafanyia kazi matajiri.
Matajiri waliweza kuiona hii concept kwa jicho la Tatu na wakaanza kuifanyia kazi and the rest is history.
Huwezi kumkuta tajiri anapoteza muda wake kwa mambo ya kizembe yasiyomuingizia chochote ndio maana matajiri wanazidi kuwa matajiri na maskini wanaendelea kuwa maskini.

Lakini bado muda na nafasi unayo sasa ukiamua na ukianza kuutumia muda wako ulio nao kwa ajili ya kuyatengeneza maisha yako.
Watu wengi hawako tayari kuumia na kujifunza biashara na kuielewa ndani ya miaka mitano itakayowapelekea kuwa matajiri na kuweza kuyafikia malengo na ndoto zao lakini wapo tayari kuajiriwa na kufa maskini ndani ya miaka 40.

Muda mzuri ndio sasa Wa kufanya maamuzi sahihi Wa kuyawekeza masaa manne kwenye biashara ili uje upate matokeo chanya.

Wabongo ni noma! Angalia huyu mbongo anachokifanya

Basi juzi kati hapa sehemu ndogo ya ukuta wa Ikulu ya Magogoni ilianguka!..
Wakapelekwa contractors watatu ili achaguliwe mmoja atakayejenga vzr na kwa bei nafuu!..
Wakwanza alikuwa MUHINDI, wa pili MCHINA na MBONGO!…

MUHINDI: “ntajenga kwa milioni 90!.., 40 za vifaa, 40 za mafundi na milioni 10 faida yangu”

MCHINA: “mi ntajenga kwa milioni 70!.., 30 za vifaa, 30 za mafundi na milioni 10 faida yangu”

MBONGO kuona vile akamvuta chemba msimamizi wa Magogoni!..
MBONGO: “mi ntajenga kwa milioni 270”

MSIMAMIZI WA MAGOGONI: “we una wazimu nn!.. yaani unathubutu kusema hivyo na unaona wenzako wametaja kiwango kidogo?!.”

MBONGO: “milioni 100 zako, 100 zangu alafu hiyo milioni 70 tunaajiri yule mchina”

Shopping Cart
2
    2
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About