SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

UKWELI KUHUSU MSHAHARA

1. Epuka kugeuza mshahara wako kuwa mali ya ukoo. Kamwe mshahara wako siyo mali ya ukoo. Siku utakapoacha kuufanya mshahara wako mali ya ukoo ndipo siku mshahara huo utakuwa mkubwa! Hapo ndipo mshahara utatosha.

2. Siku utakapokuwa na vyanzo vya mapato zaidi ya mshahara wako ndipo mshahara wako utakapotosha mahitaji yako ya kila mwezi.

3. Usiombe mwajiri wako akulipe overtime allowance, mwombe akupe muda wa kufanya kazi zako za ziada(perform your own overtime duties)

4. Epuka kuwasambazia pesa za mshahara wako watu wa ukoo wako ili uwaokoe na hali ngumu ya ukosefu wa fedha waliyonayo. Badala yake Wasaidie kuona fursa za kuwapatia Pesa!

5. Usiombe mwajiri wako akuongezee mshahara bali omba Mungu akuwezeshe Kupata kipato endelevu nje ya mshahara wako.

6. Mtu anayeishi kwa kutegemea mshahara wake tu ni sawa na mtu aliyejenga nyumba yake juu ya mchanga na mafuriko yalipokuja anguko la nyumba hiyo lilikuwa na mshindo mkubwa sana.

7. Mto Kagera au Maragalasi haijawahi kukauka maji yake. Kwa nini? Ni kwa sababu inapokea maji yake kutoka kwenye vyanzo vingi vya maji au vijito vingi! Mtu mwenye vyanzo vingi vya mapato zaidi ya mshahara atafanishwa na mto Kagera au Maragalasi isiyokauka maji yake.

8. Usisubiri kustaafu kazi ndipo ulipwe mamilioni ya pesa za kiinua mgongo bali tafuta kumiliki vyanzo sahihi vya pesa, na ndipo malipo ya kiinua mgongo utalipwa kila wiki mamilioni ya pesa.

9. Watu wenye busara hutafuta vyanzo vya pesa vinavyoweza kuwalipa mshahara au pensheni ya Tshs 150 milioni kwa mwezi badala ya kusubiri kulipwa kiinua mgongo cha Shs 150milioni baada ya kufanya kazi kwa miaka 30 au zaidi.

10. Waajiriwa wenye hekima na busara hutumia mishahara yao kutengeneza au kutandaza mabomba ya fedha au mtandao wa fedha endelevu ili hata kama hawatakuwepo tena duniani watoto wao na watoto wa watoto wao waendelee kupata mshahara kila mwezi!

Ujumbe kwa leo

Kuna baadhi ya LEVEL huwezi kufika…Kuna MAFANIKIO huwezi kuyafikia…Kuna HELA huwezi kuzipata…Kama umezungukwa na watu BASIC…
Kuanzia asubuhi mpaka jioni wanaongelea WATU TU..Fulani kamegwa na yule..halafu yule naniliu saivi anatembea na yule ex wa nanii…Asubuhi mpaka jioni DISCUSSING PEOPLE…Hawa ndio watu BASIC…Hata siku 1 hawatakupa Ushauri kuhusu HOW TO REACH SOMEWHERE…NEVER

Na ukionekana unaanza kufanya vitu EPIC watakugeuka kwamba UNARINGA.. UNAJISIKIA.. UMEWATENGA…UNAJIDAI UNA HELA…and lots of bullshit…
Pengine ulipaswa kuwa mbaaalii kibiashara lakini HUWEZI coz umezungukwa n Mbaazi tupu…BASIC PEOPLE…Ukiwaambia umesikia Kiwanja kinauzwa Kigamboni wanakwambia Kigamboni watu wanatapeliwa kuna mradi wa Joji Bushi…Ukiwambia unataka kujiunga Forever Living wanakwambia UNALIWA HELA…Ukiwaambia kuna SACCOSS wanatoa mikopo unataka uchukue ujenge wanakwambia INTEREST ZAKE UTASHINDWA na kujenga sio mchezo shosti..Unaamini unaacha!…Nataka kufanya Kitu flani WANAKUKATISHA TAMAA
Unahitaji kuzungukwa na watu wenye POSITIVE ENERGY ambao ukiwambia unataka kwenda Mbinguni kwa kupitia Mkuranga wanakuchangia Nauli…Niliposema naacha kazi watu ohh utakula nini..utaishije…Mji Mgumu huu..Wenzio wanatafuta kazi we unaacha utalosti…WHO SAID??Nadunda kama kawa..NEGATIVE PEOPLE WILL BRING U DOWN….Ukitaka Kupaa kaa karibu na ndege…We unataka kupaa unakuwa rafiki wa Nyangumi…UNAZAMISHWA SASA HIVI!!
Tangu nianze kukaa na watu Positive I have changed a lot…Nikiwaza jambo wanauliza HOW DO WE ACHIEVE THIS na sio FULANI ALIWAHIFANYA HII AKAFELI..
Ikikusaidia Chukua..
KILL ALL NEGATIVE PEOPLE AROUND YOU kama unataka kufikia Malengo Makubwa, I will be ur Lawyer at the Court na mwambie Hakimu nilikutuma mimi!
TIME TO DELETE ALL BASIC PEOPLE who wait of option😜😜😉😉

Jinsi ya kujisaidia unapopatwa shambulio la moyo ukiwa pekeyako

Tafadhali chukua walau dk 2 kusoma hii:

1. Chukulia ni muda wa saa 1:25 jion unarudi nyumbani peke yako, baada ya kazi ngumu zusizo za kawaida ofisini.

2. Umechoka sana, una hasira na umechanganikiwa.

3. Ghafla unajisikia maumivu makali kifuani yanaelekea mkononi na hata kwenye Taya. Upo umbali wa kama km5 tu kufika Hospitali iliyo karibu na kwako.

4. Bahati mbaya hujui kama utaweza kufika kwa vunavyojisikia.

5. Ulishafundishwa kumfanyia mtu CPR, lkn aliyekufundisha hakuwaambia unaweza kujifanyia mwenyewe.

6. JINSI YA KIJUSAIDIA UNAPOPATWA NA SHAMBULIO LA MOYO UKIWA PEKE YAKO.
Kwa kuwa watu wengi hupatwa na Shambulio la Moyo wakiwa peke yao bila msaada wowote, mtu ambaye mapigo yake ya Moyo hayako sawa na anaanza kuhisi kuzimia, au zimebaki sekunde 10 tu kabla hajapoteza fahamu.

7. Hata hivyo, waathirika hawa wanaweza kujisaidia kwa kujikoholesha mfululizo. Avute pumzi ndefu kila anapojikoholesha, na kikohozi lazima kiwe cha ndani mfululizo mpaka makohozi yatoke ndani ya kifua.

Kikohozi hicho kiendelee mpaka utakapopata msaada au mpaka mapigo ya Moyo yarudi kawaida tena.

8. Pumzi ndefu hupeleka Oksijeni mapafuni na kikohozi kiubana Moyo na kufanya mzunguko wa Damu uendelee. Nguvu ya kikohozi ya kuubana Moyo pia inasaidia kurudisha ktk mapigo ya kawaida. Kwa njia hii, waathirika wa shambulio la Moyo wanaweza kufika Hospitali.

Utajuaje kama unachoangalia ni filamu ya kibongo!!!!

Angalia hivi

-Mlinzi wa Getini lazima awe chizi
-Mtu yupo kijijini, maisha magumu ana Wave
kichwani.
-Kama bosi atakuwa na kampuni basi ni lazima
itakuwa ya Clearing and Forwading au ya uuzaji
Magari.
-Lazima waende Kununua nguo.
-Jambazi lazima avae koti lefu jeusi na Miwani.
-Mtu akichapwa kofi huangukia kwenye kochi
ama kitandani.
-Actress huwa hawapiki hata chai.
-Kwa mdada akiishi maisha ya kitajiri lazima
avae nguo inayoishia mapajani.
-Actress even after 5 yeas utakuta staili ya
nywele na rangi za kucha ni zile zile.
-Anaweka Sumu alafu anaonja kama imekolea.
-Movie zote wapenzi huitana Baby..
-Main actor wote ni wafanya biashara na lazima
wataongelea mizigo kutoka bandarini.
-Wakinywa Soda basi lazima wabakishe.

Jinsi ya kutibu chunusi kwa Chumvi na mafuta ya zeituni

Mchanganyiko wa chumvi na mafuta ya zeituni (olive oil) ni dawa nyingine inayotibu chunusi. Mafuta ya zeituni yandhibiti bakteria na huondoa sumu vitu ambavyo vinafanya kuwa dawa nzuri kutibu chunusi na matokeo ya chunusi.

Changanya nusu kijiko kidogo cha chai cha mafuta ya zeituni na kiasi kidogo cha chumvi katika chombo kisafi. Safisha vizuri uso wako. Kisha jipake mchanganyiko huu kwenye uso wako na uache kwa dakika 10 hivi.

Mwisho jisafishe vizuri na maji ya uvuguvugu.

Kichekesho cha mwalimu na wanafunzi

Mtoto: Mwalimu mimi nataka nisome darasa la nne kwani hili la3 halinifai.

Mwalimu: Kwa nini unasema hivyo?

Mtoto: Nina akili…

Basi mwalimu akamueleza mkuu wa shule na mkuu kaitisha interview kwa dogo. Maswali ni haya….

Mwalimu: Kwenye ndege kuna matofali 20 tukitoa moja tukalidondosha chini yatabaki mangapi?

Dogo: Yatabaki 19.

Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka tembo kwenye friji.

Dogo: Unafungua friji unamuweka tembo kisha unafunga.

Mwalimu: Nipe hatua za kumuweka nyani kwenye friji.

Dogo: Unafungua friji unamtoa tembo ulemuweka..unamueka nyani kisha unafunga friji.

Mwalimu: Kuna sherehe ya siku ya kuzaliwa kwa simba, wanyama wote wameenda kasoro mmoja. Ni nani na kwa nini?

Dogo: Ni nyani kwa sababu tumemuweka kwenye friji.

Mwalimu: Bibi kizee amevuka mto unaokuwaga na mamba na viboko wakali, aliwezaje?

Dogo: Aliweza kwani mamba na viboko nao walienda kwenye sherehe ya kuzaliwa kwa simba.

Mwalimu: Ingawa bibi kizee alivuka mto, baadae alikufa. Unadhani ni kwanini alikufa?

Dogo: Alidondokewa na lile tofali tulotoa kwenye ndege na kutupa chini.

Mwalimu mkuu: Huyu dogo akasome chuo kikuu….
😆😆😆😆😆😆😆😆

Mambo 8 ya kushangaza yanayofanywa na mwili wako kukulinda pasipo wewe kujua

Mwili wa binadamu unafanya mambo
mengi ya kibaiolojia ambayo mara
nyingi ni vigumu kuyaelewa. Mwili una mifumo mbalimbali ya ulinzi ambayo inatulinda na hatari zinazoweza kutudhuru. Mifumo hiyo
inatulinda masaa 24 ya siku, Siku zote 7 za wiki, katika mambo yote
yanayoweza kuhatarisha maisha yetu.
Yafuatayo ni mambo yanayofanywa
na mwili ambayo ni kati ya hiyo
mifumo ya ulinzi wa mwili wa
binadamu.

1. KUPIGA MIAYO (YAWNING)
Lengo kubwa la kupiga muayo ni
kuupoza ubongo baada ya joto kuzidi
kwenye ubongo au baada ya ubongo
kuchoka kufanya kazi.
Vile vile kama ukiwa umechoka au una
njaa husabababisha oxygen
kupungua kwenye damu na kwenye
mapafu, hii hupelekea tatizo la
kupumua, hivyo kupiga miayo
husaidia kuingiza oxygen ya ziada
mwilini ili irudishe mwili katika hali
yake ya kawaida.

2. KUPIGA CHAFYA (SNEEZING)
Mara nyingi tunapiga chafya pale pua
zetu zinapokua zimejaa bakteria wa
magonjwa ambao hawahitajiki
mwilini, Vumbi pamoja na takataka
mbali mbali zilizoingia kupitia pua.
Hivyo kupiga chafya ni kitenda cha
mwili kujisafisha kwa kuyatoa hayo
matakataka nje yaliyoingia mwilini.

3. KUJINYOOSHA (STRETCHING)
Kuninyoosha mwili ni kitendo kisicho
cha hiari ambacho lengo lake ni
kuuandaa mwili kwa ajili ya kazi
mbalimbali za kutumia nguvu
utakazokabiliana nazo kwa siku nzima.
Lakini pia kujinyoosha kunaipa misuli
ya mwili mazoezi na kuiweka sawa
vilevile kunarudisha mzunguko wa
damu katika hali yake ya kawaida na
kumtoa mtu katika uchovu.

4. KWIKWI (HICCUPING)
Najua umewahi kupata kwikwi, na
mara nyingi mara baada ya kumaliza
kula chakula. Je umeshawahi kujiuliza
ile sauti ya ajabu ya kwikwi
inasababishwa na nini au kwa
sabababu gani watu hushikwa na
kwikwi?
Hiyo yote husababishwa na
DIAPHRAGM (tamka DAYA – FRAM)
kiungo kinachopatikana ndani ya
mwili wa binadamu chini kabisa ya
kifua baada ya mapafu(lungs). Kazi
kubwa ya diaphragm ni kusaidia katika
upumuaji, (inhale) na (exhale). Pale
unapoingiza hewa ndani (inhale)
diaphragm hushuka chini ili kusaidia
kuivuta hewa ifike kwenye mapafu. Na
unapotoa hewa nje (exhale)
diaphragm hutulia kwa kubakia
sehem yake ili kuwezesha hewa chafu
kutoka nje kupitia pua na mdomo.
Sasa basi, kuna wakati diaphragm
kubugudhiwa na kuisababisha
kushuka chini kwa kasi sana jambo
linalosababisha wewe kuvuta hewa
(inhale) kwa kasi isiyo ya kawaida
kupitia koromeo la sauti, hewa ikifika
kwenye box la sauti (larynx), sehem
hiyo hujifunga kwa haraka sana ili
kuzuia hewa isipite huko na ndipo
KWIKWI hutokea.
Mambo mengine yanayoweza
kuibugudhi diaphragm na
kuisababisha kufanya kazi vibaya
mpaka kupelekea kwikwi ni kitendo
cha kula haraka haraka au
kuvimbewa.

5. KUJIKUNJA KWA NGOZI YA VIDOLE
VYA MIKONO BAADA YA KULOWA AU
KUKAA MUDA MREFU KWENYE MAJI.
Je umewahi shuhudia jinsi ngozi ya
vidole vyako inavyojikunja baada ya
kufua nguo muda mrefu au kushika
maji muda mrefu? Unajua ni kwa
sababu gani ngozi hujikunja kama ya
mtu aliyezeeka angali yu kijana mara
baada ya kukaa sana kwenye maji?
Watu wengi kabla walizani kwamba
kujikunja kwa ngozi hiyo hutokana na
maji kuingia kwenye ngozi na hivyo
ngozi hujikunja baada ya kulowa.
Lakini wanasayansi baada ya kufanya
utafiti kwa muda merefu juu ya nini
hasa hupelekea ngozi kujikunja?
Walisema HAPANA si kwa sababu ya
ngozi kulowana. Na walikuja na
majibu haya.
Mwili unapokutana na majimaji mara
moja hupeleka taarifa na kutafsiri
kwamba mazingira hayo yana UTELEZI
(Slippery) hivyo kutasababisha mikono
kushindwa kushika (Grip) au kukamata
vitu kwa urahisi kutokana na utelezi
huo. Hapo mwili huchukua hatua ya
haraka kuikunja ngozi ya mikono yako
ili kurahisisha ushikaji wa vitu
vinavyoteleza ndani ya maji pamoja na
kutembea kwenye utelezi.

6. VIPELE VIPELE VYA BARIDI KWENYE
NGOZI (GOOSEBUMPS)
Kazi kubwa ya vipele hivi ni kupunguza
kiasi cha joto la mwili linalopotea
kupitia matundu ya ngozi. Hivyo kwa
kufanya hivi humfanya binadamu
kutunza joto la mwili hata katika
mazingira ambayo hali yake ya hewa
si rafiki kwa mwili wa mwanadamu au
ni yenye baridi sana.

7. MACHOZI (TEARS)
Zaidi ya kuwa majimaji (MUCOUS
MEMBRANE ) yanayopatikana kwenye
Macho ambayo kazi zake ni kulilinda
jicho dhidi ya kitu chochote kigeni
kinachoingia jichoni (mfano
unapokata vitunguu au mdudu
anapoingia jichoni huwa unatoa
machozi mengi eeeh!! Pia dhidi ya
upepo na moshi) na pia hutumika
kama kilainishi cha jicho pale
linapokuwa linazunguka zunguka
(blink).
Vilevile machozi yana kazi ya
kupunguza HISIA ZA HUDHUNI
zinazozalishwa mwilini. Wanasayansi
wanaamini kuwa mtu anapokua
mwenye msongo wa mawazo (stress)
mwili hutengeneza kitu kipya ili
kwenda kubugudhi na kuharibu
maumivu yote ambayo mtu anajisikia.
Hivyo machozi yanayozalishwa hapa
huwa na kemikali na yanafahamika
kama NATURAL PAINKILLER. Machozi
haya ni tofauti na machozi ya kawaida,
lengo lake hasa la kuzalishwa ni kwa
ajili ya kuondoa kabisa maumivu
yaliyozalishwa mwilini
Hivyo mpaka hapa tumeona kua kuna
machozi ya aina tatu ambayo ni
i. Basal tears (vilainishi)
ii. Reflex tears (mlinzi)
iii. Emotion tears (mtuliza maumivu)

8. KUSHTUKA USINGIZINI
(MYOCLONIC JERKS or HYPNIC JERK).
Je! Ushawahi kutokewa na hali hii?
umelala halafu ghafla unashtuka
usingizini kwa mguvu nyingi kama
umepigwa na shoti ya umeme na akili
inakurudi ghafla huku mapigo ya
moyo yakikuenda mbio? Na hali hii
ikakutokea pasipo hata kuota ndoto
yoyote?
Basi usiogope au kuwasingizia watu
uchawi, hii ni hali ya sayansi ya
mwili.na ni njia moja wapo katika ile
mifumo ya mwili kujilinda.
Je hutokeaje?
Hii ni hali ya ajabu sana isiyofanywa
kwa hiari ambayo huwatokea watu
mara tu wamejinyoosha kitandani na
kupitiwa na usingizi, mwili
hutetemeshwa na kusukumwa kwa
nguvu na mtu hushtuka katika hali
kama vile kapigwa na shoti ya umeme.
Hali hii inaweza kupelekea mtu hata
kuanguka kitandani na humwamsha
mara moja kutoka usingizini.
Wanasayansi wanatuambia kua, pale
tu unapopata usingizi kiwango cha
upumuaji kinashuka ghafla, mapigo ya
moyo nayo taratibu yanapungua,
misuli inatulia kwa ku-relax, Kitu cha
AJABU hapa ubongo unatafsiri hali hii
kama ni DALILI ZA KIFO (brain’s
misinterpretation of muscle
relaxation), hivyo huchukua hatua za
haraka za kuushtua mwili kwa
kuutetemesha au kuuskuma kwa
nguvu, hali ambayo humfanya mtu
kuamka kutoka usingizini kwa KURUKA
kitu ambacho ni hali isiyo ya kawaida.
Hali hii ikimtokea mtu huambatana na
kuongezeka kwa mapigo ya moyo
(rapid heartbeat), kuhema haraka
haraka, na wakati mwingine mtu
hutokwa na jasho jingi.
Wakati mwingine mtu huamka ametoa
macho na kama ukimwangalia, nae
huishia hukuangalia tu huku akikosa
la kukujibu endapo utamuuliza vipi
kuna tatizo gani?
MWILI WAKO NI ZAIDI YA
UNAVYOUJUA. JAMBO LA MSINGI NI
KUONDOA HOFU KWANI MWILI WAKO
UNAJUA NINI UFANYE NA WAKATI
GANI ILI KUKULINDA USIKU NA
MCHANA KATIKA SIKU ZOTE ZA
MAISHA YAKO.

Siri ya mafanikio katika maisha Ni Kutoangalia Watu

Baada ya kusoma makala kuhusu hofu zinazotugharimu katika safari ya mafanikio, Leo nimekuandalia Makala hii ya Siri ya mafanikio.

Katika safari ya mafanikio, watu wanaweza kuwa kikwazo kikubwa kinachosababisha ugumu wa kuendelea mbele. Wanaweza kuleta upinzani, kukosa imani, au hata kuzua vikwazo visivyo na msingi. Hata hivyo, ni muhimu kuelewa kuwa changamoto hizi zilizoletwa na watu ni sehemu ya mchakato wa kufikia mafanikio. Ingawa inaweza kuwa ngumu kukabiliana na watu wenye upinzani au wasioamini katika safari yetu ya kufikia malengo yetu, tunapaswa kuzingatia kuwa hakuna mafanikio ya kweli ambayo hayakuja na changamoto. Naam, inaweza kuwa rahisi kufanya kazi peke yetu na kuepuka kukabiliana na watu wasioamini au wenye upinzani, lakini hiyo haitatupeleka mbali sana.

Tunahitaji kushughulikia changamoto hizi na kuona jinsi tunaweza kuzishinda. Kukutana na watu ambao hawana imani na malengo yetu inaweza kuwa kama mtihani mkubwa kwetu. Wanaweza kutushawishi kuacha au kuanza kutilia shaka uwezo wetu. Lakini ni muhimu kukumbuka kuwa imani yetu ndio itakayotuendesha mbele. Tunapaswa kujikumbusha kuwa mafanikio hayangeweza kupatikana ikiwa tungekuwa na imani ndogo ndani yetu wenyewe. Mbali na hilo, tunapaswa pia kutambua kuwa vikwazo visivyo na msingi vinaweza kuwepo katika safari yetu ya mafanikio. Watu wanaweza kuzua vikwazo hivi kwa sababu ya wivu, woga, au tu kutokuelewa malengo yetu. Ni muhimu kutambua kuwa hatuwezi kudhibiti tabia au mitazamo ya watu wengine, lakini tunaweza kujifunza kuweka mipaka na kuendelea kufuata malengo yetu licha ya vikwazo hivyo. Katika safari yetu ya mafanikio, tunapaswa kuwa na uvumilivu na subira.

Tunapaswa kutambua kuwa kila changamoto tunayokutana nayo inatupa fursa ya kukua na kujifunza. Tunapaswa kutumia changamoto hizi kama nguvu ya kuendelea mbele badala ya kutuacha tukata tamaa. Kwa kumalizia, ingawa watu wanaweza kuwa kikwazo katika safari yetu ya mafanikio, tunapaswa kuona changamoto hizi kama sehemu ya mchakato wa kufikia malengo yetu. Tunapaswa kuwa na imani thabiti ndani yetu wenyewe, kuweka mipaka na kuendelea kusonga mbele licha ya vikwazo vinavyoweza kuzuka. Kwa kufanya hivyo, tutapata mafanikio kamili na kuwa bora zaidi katika safari yetu ya kuelekea mafanikio.

Wakati mwingine, tunaweza kukutana na watu ambao hawana imani na uwezo wetu au wanajaribu kutuweka chini kwa sababu ya wivu au tamaa. Ni muhimu kujifunza kuweka mipaka na kuendelea kusonga mbele, kujiamini katika uwezo wetu na kuendelea kufanya kazi kwa bidii kuelekea malengo yetu.

Watu wanaweza pia kuwa vikwazo kwa kuwa na maoni tofauti au kutokuwa na uelewa kamili wa malengo yetu. Katika hali hizi, ni muhimu kuwa na uvumilivu na kuwasiliana kwa wazi ili kuelezea malengo yetu na kutafuta njia za kuwashawishi au kuwashirikisha katika safari yetu ya mafanikio.

Hakikisha pia kuwa unazungukwa na watu wenye mawazo chanya ambao wanakuunga mkono na kukusaidia kufikia malengo yako. Kuwa na timu ambayo inakusaidia na kukutia moyo ni muhimu sana katika safari ya mafanikio.

Kwa hiyo, tunapokabiliana na vikwazo kutoka kwa watu katika safari yetu ya mafanikio, ni muhimu kujifunza kutokana na hilo, kuweka mipaka, kuwasiliana kwa wazi, na kuwa na timu yenye msaada karibu nasi. Hatimaye, tunapaswa kuendelea kuamini katika uwezo wetu wenyewe na kufanya kazi kwa bidii ili kufikia malengo yetu.

Waziri mkuu wa zamani wa uingereza Sir Wiston Churchill aliwahi kusema;

“huwezi kufika mwisho wa safari yako kama utakuwa unasimama kila mahali kumtupia jiwe kila mbwa anaye kubwekea”

Sir Wiston Churchill

Kauli hii ina maana kwamba kama una picha kichwani ya kule unakokwenda au umekusudia kufikia na kutimiza lengo fulani katika maisha hupaswi kusikiliza, kupambana au kushindana nakila mtu.

Unapokuwa njiani kutimiza lengo lako lazima utakutana na watu wa aina hizi;

  1. Watakaokurudisha nyuma kwa kukuharibia mipango na juhudi zako
  2. Watakaokuvunja moyo na kukukatisha tamaa
  3. Watakaokusema vibaya hata kwa mazuri yako na kukuzushia uongo
  4. Watakaokuchukia kwa sababu ya bidii yako

Unaweza kushawishika kutaka kumjibu kila mtu anayekusema vibaya, kukuchukia au kukukatisha tamaa (hapo ndo unakuwa sawa na yule anayesimama kumtupia jiwe kila mbwa anayebweka).

Unaweza ashawishika kutaka kuona kila mtu anakukubali na kukuunga mkono, kitu ambacho hakiwezekani.
Kuna Msemo usemao “siri kubwa ya kufeli katika maisha ni kujaribu kumpendeza kila mtu”.

Hapa duniani huwezi kumpendeza kila mtu hata ufanye jambo zuri kiasi gani “hata ukichezea maji utaambiwa unatimua vumbi”. Mara nyingi tunajitahidi kufanya mambo mema na kuwa na nia njema, lakini bado kuna watu ambao hawatafurahia jitihada zetu na watatupinga tu. Hii inaweza kuwa changamoto kubwa kwetu kihisia na kijamii, kwani tunatamani kukubalika na kupendwa na kila mtu.

Lakini kumbuka, haifai kuchukulia kila upinzani kibinafsi au kuathiri thamani yako. Watu wana mitazamo tofauti na uzoefu wao binafsi, na huenda hawana ufahamu kamili wa hali yako au malengo yako. Badala yake, ni muhimu kuwa na imani katika nia zako na kuendelea kufanya mambo mema bila kujali jinsi watu wengine watakavyokuona au kukupinga.

Njia bora ya kushughulikia upinzani ni kujielewa na kuweka mipaka. Jifunze kuamini kwamba wewe ni wa thamani na una uwezo mkubwa wa kuathiri mazingira yako. Wacha maadili yako yaongoze vitendo vyako na usiruhusu maneno au maoni ya wengine kukufanya ujisikie vibaya au kupoteza lengo lako.

Kumbuka pia kuwa hakuna mtu aliyeweza kufanya kila mtu awe radhi. Hata watu mashuhuri na viongozi wa kiroho hawakuepuka upinzani. Kina Mandela, Mahatma Gandhi, au Martin Luther King Jr., walikabiliana na upinzani mkubwa, lakini waliendelea kusimama imara kwa imani zao na kufanikisha mabadiliko makubwa.

Ili kufanya mabadiliko katika jamii au ulimwengu, ni muhimu kuwa tayari kukabiliana na upinzani. Upinzani unaweza kukusaidia kukua kibinafsi na kitaaluma, kurekebisha njia zako, na kukuza uvumilivu wako. Ni nafasi ya kujifunza na kujenga hoja zako kwa msingi thabiti.

Hivyo, jinsi unavyokabili upinzani ina athari kubwa kwa maendeleo yako na mtazamo wako kwa maisha. Usikate tamaa na usiruhusu upinzani ukuzuie kufuata ndoto zako na kufanya mambo makubwa. Jiamini, thamini uwezo wako, na endelea kusonga mbele bila kujali kile ambacho wengine wanaweza kusema au kufikiria. Hakuna kitu kikubwa kilichofanyika bila ya upinzani, kwa hiyo endelea na safari yako na uhakikishe kuwa unaamini kwamba una nguvu ya kufanya tofauti.

Wewe fwatilia Mipango yako huku ukitazame hatima yako. Soma hapa mbinu hizi za kukunufaisha maishani.

Lakini haimaanishi uwachukie watu na kuwatendea mabaya ili ufanikiwe mwenyewe. Chuki na Mapambano hayanufaishi bali yanakufanya kuwa dhaifu.

Vivyo hivyo, Sio watu wote ni kikwazo. Kuna watu wa aina nyingine ambao wanaweza kukusaidia kufanikiwa. Unapaswa kuwa makini na kutumia Busara yako kuweza kuwatambua watu unaokuwa nao katika safari ya Mafanikio.

Angalia huyu baba alichowafanya mtoto wake wa kike na boyfriend wake

BABA OYEEEEEE💪💪
Soma hii…

Msichana alikuwa amekaa na baba yake kibarazani, mara akamuona MVULANA friend wake akija, yule mvulana alipokaribia tu, yule msichana akamwambia hivi:-

MSICHANA: Umekuja kuchukua kile kitabu chako, kinachoitwa “DADDY IS AT HOME?” by Ngozi Okafor

MVULANA: Hapana!, Nimekuja kuazima kitabu cha maombi kama kinaitwa “WHERE SHOULD I WAIT FOR YOU?” by Ngũgĩ wa Thiong’o

MSICHANA: Aaah! Hicho sina ila ninacho kimoja kinaitwa “UNDER THE MANGO TREE” by Chimamanda Adichie

MVULANA: Ooh! Vizuri, Basi usisahau kuja nacho kesho kitabu cha Okot p’Bitek kile kinachoitwa “CALL ME IN 5 MINUTES BEFORE” Utakapokuja shule.

MSICHANA: Usijali, tena nina kitabu kipya kinaitwa “I WON’T LET YOU DOWN” by Chinua Achebe

Baba mtu akawatazama kisha akasema

BABA: Vitabu vyote hivyo, mbona vingi sana, atavisoma vyote kweli

MSICHANA: Ndio Daddy, huyu mvulana yupo smart sana na ana akili atavisoma vyote hivyo!

BABA: Sawa! Usisahau kumpatia na kile ambacho nimekiweka pale juu ya meza, kinaitwa “I AM NOT STUPID, I UNDERSTOOD EVERYTHING YOU’VE BEEN SAYING” by Shakespeare!

Na kuna kingine nimekiweka juu ya kabati la vyombo, kinaitwa “IF YOU GET PREGNANT PREPARE TO GET MARRIED” by Wole Soyinka.

Wabongo ni noma! Angalia huyu mbongo anachokifanya

Basi juzi kati hapa sehemu ndogo ya ukuta wa Ikulu ya Magogoni ilianguka!..
Wakapelekwa contractors watatu ili achaguliwe mmoja atakayejenga vzr na kwa bei nafuu!..
Wakwanza alikuwa MUHINDI, wa pili MCHINA na MBONGO!…

MUHINDI: “ntajenga kwa milioni 90!.., 40 za vifaa, 40 za mafundi na milioni 10 faida yangu”

MCHINA: “mi ntajenga kwa milioni 70!.., 30 za vifaa, 30 za mafundi na milioni 10 faida yangu”

MBONGO kuona vile akamvuta chemba msimamizi wa Magogoni!..
MBONGO: “mi ntajenga kwa milioni 270”

MSIMAMIZI WA MAGOGONI: “we una wazimu nn!.. yaani unathubutu kusema hivyo na unaona wenzako wametaja kiwango kidogo?!.”

MBONGO: “milioni 100 zako, 100 zangu alafu hiyo milioni 70 tunaajiri yule mchina”

Umasikini isiwe sababu wala utajiri isiwe sababu ya kuwa mchafu au kutokuwa na usafi

Katika maisha, umasikini siyo sababu ya mtu kuwa mchafu au kutokuwa na usafi. Hali ya umasikini inaweza kuathiri uwezo wa mtu kumudu bidhaa za usafi au kuishi katika mazingira safi, lakini hii haimaanishi kuwa mtu mwenye utajiri automatically ni mtu mwenye usafi.

Kinyume chake, utajiri haujazi hakika mtu kuwa na kila kitu ambacho hahitaji. Utajiri ni kuwa na uwezo wa kununua au kumiliki vitu vingi, lakini ukweli ni kwamba tunahitaji tu vitu vichache sana katika maisha yetu. Tunapojikuta tukiwa na wingi wa vitu visivyotumiwa, tunaweza kujikuta tukichafua mazingira yetu na kutopenda kila kitu tunachomiliki.

Sasa angalia nyumbani kwako! Je, kuna vitu ambavyo haujahitaji kwa muda mrefu au vinachafua tu nafasi yako? Kufanya maamuzi ya busara na kujiondoa na vitu visivyohitajika, vitakuwezesha kuishi katika mazingira safi na yenye upangaji mzuri. Usafi sio lazima uendane na utajiri, bali ni suala la utaratibu na umakini katika kusimamia mazingira yetu.

Umasikini sio sababu ya kuwa mchafu wala utajiri Sio kuwa na kila kitu hata kama hukihitaji. Hebu angalia hapo nyumbani kwako!

Vitu msivyovihitaji Leo wala kesho mmeweka vya nini? Umenunua makochi mapya Yale ya zamani mmegawana vyumbani mnaishia kurundika minguo hapo na kufuga mipanya.

Godoro umenunua jipya la zamani umeviringisha juu ya kabati. Kabatini kwako kuna nguo ulivaa ukiwa secondary mpaka Leo unazo eti ukumbusho au utazivaa ukipungua.

Jikoni ndo shida iliposhika hatamu! Mivyombo ya plastiki imepaukiana imeyayuka na moto ipo tu eti vyombo vya watoto. Mahotpot yamekata roho imebaki kuwa sufuria we unalo tuu. Mxiuuu

Ndoo hata hazitumiki zipozipo tu, hata maua hazifai kupandia we unazogo tu huchomi, hutupi wala huzihitaji.. Sa zanini hapo?? 😡😡

Vyombo vya udongo vina mapengo na magego kama vinang’atwaga au vinapiganaga vyenyewe. 😂😂. Isitoshe kila kimoja na dizaini yake havifanani coz seti imeshavunjikavunjika hivo ndo vimebaki. Unaboa… 😏😏😏

Dressing table imejaa mikopo na mibox haina Kazi, perfume ya mwaka 2000 unayo hapo kisa ukumbusho wa zawadi. Ushamba huooo… 😫😫

Stoo yako mwenyewe ila unaiogopa kuingia coz imejaa vitu visivyohitajika imekuwa ghetto la panya na nyoka kama sio nge badala Ukiweka mnavyohitaji. Ipo siku mtakuta mamba humo.. 🐲🐲🐲

Nje ya nyumba kuna gari la urithi la babu lipogo tu hapo linafuga ndege na vibaka… Aaalaaaa 😡😡😡

Kutupa vitu visivyohitajika hamtupi eti Dhambi na kugawa hamgawi coz mmeviharibu hadi mwisho mtampa nani? Kutwa mnapishana mahospitalini mnaumwa mafua na vifua kila siku.

Kwann msiumwe na mnakaa dampo ? Hivi mnajua km huu ni ugonjwa? Unaitwa hoarder disorder. Tena mnawaambukiza watoto wenu kwani wanajua kwao hata kikopo cha icecream hakitupwagi kinaoshwa kinawekwa hapo.

Halafu bado unaendelea kumuomba Mungu akupe, akupe uweke wapi na kwako pameshajaa?

Kwa kweli, mtazamo wa kuridhika na hali ilivyo sio tu hatari kwa maendeleo binafsi, lakini pia kwa jamii kwa ujumla. Mazingira tunayoishi yanahitaji uangalizi na uhusiano wa moja kwa moja na afya zetu, usalama, na hata uchumi wetu. Kama ilivyosemwa awali, kila mmoja wetu – bila kujali hadhi yetu kifedha – ana wajibu wa kuchukua hatua za makusudi katika kudumisha usafi wa mazingira yetu.

Tunapaswa kuzingatia kuwa usafi na umakini wa mazingira yanatuhusu sote na yana faida zinazoonekana na zisizoonekana. Uchafuzi wa mazingira, kwa mfano, unaweza kuathiri ubora wa hewa tunayopumua na maji tunayotumia, na hivyo kusababisha matatizo ya kiafya. Kwa upande mwingine, mazingira safi na yenye kuendelezwa vizuri yana uwezo wa kuongeza thamani za mali, kuboresha uzuri wa jamii, na kuvutia uwekezaji na utalii ambao unaweza kukuza uchumi wa eneo husika.

Kila mtu anapaswa kuchukua hatua, iwe ni katika kutupa takataka mahali pake, kushiriki katika shughuli za kusafisha mazingira, kupanda miti, au kufunza wengine umuhimu wa uhifadhi wa mazingira. Serikali na asasi zisizo za kiserikali zinaweza kusaidia kwa kutoa elimu, rasilimali na sera zinazosaidia usafi na utunzaji wa mazingira.

Ni muhimu kutambua kwamba uamuzi wa kutunza mazingira unapaswa kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku na sio tu wakati wa maadhimisho au mikakati ya muda mfupi. Uendelezaji wa mazingira safi na salama ni jukumu letu la kudumu, linalohitaji kujitolea na ushirikiano kutoka kwa watu wote katika jamii.

Mambo madogo hayapaswi kupuuzwa – matumizi ya mifuko inayoweza kutumika tena badala ya plastiki zinazotupa sana, kutumia njia mbadala za nishati zinazoweza kujazwa upya ili kupunguza uchafu, na hata kusimamia taka za kielektroniki – yote haya ni sehemu muhimu ya kujenga mazingira endelevu. Hivyo basi, hebu tuchukue hatua, kila mmoja wetu, kwa mustakabali mzuri zaidi. Tunalo jukumu hilo, kwa ajili ya kizazi chetu na vizazi vijavyo.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About