Meseji za Vichekesho na Vituko
Huyu Baba ni noma, Cheki anachomjibu huyu mtoto wake
Mtoto: baba eti Botwasna ipo wap?
Baba: angalia itakuwa humo humo kabatini maana mama yako nae kwa kuficha kuficha vitu hajambo…
Duh! Angalia alichokula huyu mwizi! Wizi mwingine bwana!
Baada ya mwizi kuvunja mlango huko Tarime, akaingia kwenye stoo akaona vinyama kwenye bakuli vikiwa vimekauka. Akaonja 1 akaona kitamu na kina chumvi! Akavila vyote. Alipomaliza akaangalia juu ya mlango akaona pameandikwa; “chumba cha UKEKETAJI WANAWAKE”. Unafikiri atakuwa amekula nini?
Wanawake hii nayo ni romantic ?💞
Alaf wale Madem wanaowavua maboy wao KOFIA alaf wanakimbia nayo thinking its FUNNY and ROMANTIC.. Hiv nyie mkivuliwa MAWIGI wakakimbia nayo mtajiskiaje?🐸🐸
Chezea kufulia!
Huu Mwezi jinsi nilivyofulia yaani hata nikikuta mende wamesimama wawili najua wananisema
😂😂😂
Alichokijibu chizi baada ya kuanguka ghorofani
Chizi kaanguka toka kwenye gorofa fasta watu wakamfuata kumsaidia wakamuulza VP IMEKUAJE?
Chz akajbu: ”HATA CJUI NA MIE NDO NAFIKA SASA HIVI
Huyu jamaa kawaweza wapenda vya bure
Jamaa kaingia mgahawani kwa fujo
JAMAA : Nipe soda moja na kila mtu mpe yake maana ninapokunywa soda napenda kila mtu anywe
WATU : Ha! Ha! Ha! Haaaa!
JAMAA : Nipe mchemsho na kila mtu mpe wa kwake maana ninapokula mchemsho napenda kila mtu ale wake
WATU: Watu weweeee! Tena safari hii Na makofi juu..
JAMAA : Mhudumu, nipe bili na kila mtu mpe yake maana ninapolipa bili napenda kuona kila mtu analipa yake
😂😂😂😂😂😂😂
Ungekua wewe ndio mama wa huyu mtoto ungemfanyaje?
Kuna mtoto mmoja aliamka kutoka usingizini alipokuwa kalala na mama yake na kupiga kelele “mamaa” mama yake akaamka na kumwambia nin mwnangu mtoto akajibu “mama nimeota ndoto mbaya sana” ndoto gani hyo mwanangu mtoto akajibu “nimeota tumefungua shule”
😂😂😂😂😂
🌚🌚Kibaooooo nyau wewe
Mcheki Chizi na daktari
Tafakari na ujumbe huuuu!!!…
DAKTARI :- Unajisikiaje?
CHIZI:-Kila siku naota nyani wanacheza mpira wa miguu.
DAKTARI :- Nitakupa dawa leo hautaota tena.
CHIZI:-hiyo dawa nipe kesho sababu leo wanacheza fainali. na nilibet
😂😂😂😂
Angalia nilichokifanya Jana kumkomoa x-wangu
Mwenzenu nilikatiwa umeme jana basi leo si nikaamua kwenda kununua luku ya 10,000. Kufika njiani nikatamani fursana nikaingia kijisupermarket mara sindo nakutana na ex wangu! Mshenzi yule kaniona mimi sijui alikua na mpango wa kununua vocha ya jero eti kabadili kanunua vocha ya buku tano ilimradi nione maisha yake safi tangu tuachane. Mambo ya kijinga spendi kudadeky nimetoa buku kumi nikanunua mipampers nami nijifanye nimeowa nina mtoto halafu huyoo nikashika njia yangu.
Sasa washkaji zangu tafadhalini mwenye mtoto au shida ya pampers naomba anunue kwangu maana leo nalala tena kiza 🙆♂
Tofauti ya mke na mchepuko!!!
MKE NA MCHEPUKO.
Mke ni kama Tv na Mchepuko ni kama Simu.
Nyumbani unaangalia Tv lakini ukitoka unatoka na simu.
Mara chache unafurahia Tv lakini Muda mrefu unacheza na simu yako.
Tv ni bure kwa maisha yako yote, lakini Simu kama hujalipia hupati huduma.
Tv ni kubwa nzito na wakati wote ni ya zamani. Lakini simu ni nzuri, nyembamba, na ni rahisi kubeba.
Gharama za huduma za tv ni ndogo sana, Lakini gharama za huduma za Simu ni kubwa na pia ni lazima kuzitimiza.
Tv ina remote lakini Simu haina.
Kitu muhimu zaidi simu ina njia mbili za kuwasiliana unaongea na unasikiliza lakini Tv unalazimika kusikiliza hata kama hutaki au unataka.
Unaweza kununua Tv mara moja na ukatumia kwa kipindi kirefu lakini Simu mara zote unabadilisha inategemea na fasheni.
Ya mwisho na ya kuzingatia
Tv haina Virusi lakini Simu inayo.
KUWA MAKINI.
Dingi kauzu kuliko wote duniani ndiyo huyu hapa
Mtoto: Baba nitumie pesa ya matumizi huku shuleni hali ni mbaya sana la sivyo najinyonga.
Baba: Huku nyumbani hali ni mbaya kuliko huko shuleni kwahiyo kama unajinyonga utapunguza Bajeti, kopa Kamba dukani kwa Mangi nitalipa nikija kuchukua Maiti yako, Mungu akulaze mahali pema peponi Mwanangu…..
Angalia haya maswali ya huyu mtoto yalivyomagumu, ndio maana wazee wetu walikua wanatudanganya
Mtoto: Mama, hivi kabla hujanizaa uliniona!?
Mama: Hapana mwanangu sijakuona.
Mtoto: Kwahiyo ulivyonizaa ulijuaje kwamba ni mimi…!??
Vichekesho vya kukuondoa mawazo leo
Soma vichekesho hivi;
Mwizi wa atm
Jamaa aliibiwa kadi yake ya benk akaulizwa kama ameripoti polisi akajibu “sijaripoti bado, mwizi mwenyewe hamfikii matumizi kama mke wangu.
Cheka kidogo
Njia rahisi kusahau matatizo yako (japo kwa muda mfupi) vaa viatu vinavyokubana.
Mlizi mbio mbio
Tulikuwa bar moja jana mlinzi kaingia spidi, akamwambia jamaa mmoja aliyekaa kaunta, Mlinzi: Mzee gari lako limeibiwa Mzee: Umemtambua aliyeiba? Mlinzi: Hapana lakini nimeandika namba za gari hizi hapa.
13, 13…
Jamaa alikuwa anapita nje ya wodi ya vichaa akasikia mtu anasema, 13, 13, 13, 13, 13, 13,….. akaamua kuchungulia kwenye kitundu alichokiona ajue kuna nini, ile kuchungulia tu akamwagiwa mchanga wa machoni, sauti ikabadili ikaanza 14,14,14,14,14……
WATAALAM
Jamaa alikuwa anaumwa sana, mkewe akamwita daktari, alipofika akamkuta jamaa kafumba macho;
Dokta: Huyu mbona amekwisha kufa?
Jamaa: Sijafa bwana
Mke: Hebu nyamaza bwana acha kubishana na wataalamu.
Ya leo mgonjwa
Dokta alipotembelea wodi ya mgonjwa wake aliyepata ajali. Mgonjwa akiwa amening’inizwa mikono juu akauliza “dokta ntaweza kweli kupiga kinanda nkitoka hospitali?”
Dokta: Bila shaka utaweza, wewe ni mpiga kinanda mzuri enh?
Mgonjwa: Hapana sijawahi kabisa bado.
4WD
Mwanaume alimnunulia pete ya almasi mkewe, rafiki akauliza “si ulisema anapenda gari yenye four wheel drive, mbona umenunua pete?” Mume akajibu “unadhani wapi ntapata rav4 feki?”
Ajali ilivyotokea
Trafiki polisi akihoji palipotokea ajali “ahaa! Sasa naanza elewa embu nielezee jinsi ajali ilivyotokea wewe ukiwa kama dereva mhusika.” Dereva akajibu “hata sikumbuki nlifumba macho”
Faini ya kukojoa
Polisi alimdaka jamaa anakojoa pembezoni mwa ukuta.
Polisi: Wewe unajua panakatazwa kukojoa hapa?
Jamaa: Sasa nimebanwa nifanyaje?
Polisi: Faini yake elfu tano.
Jamaa akatoa noti ya elfu 10.
Polisi: Sasa chenji tunaipataje?
Jamaa: Tafuta chenji unipe changu.
Polisi: Basi kojoa tena…
Mume anaenda kazini
Jamaa kaamka asubuhi sana Jumamosi, mvua inanyesha kang’ang’ania kuwa anaenda ofisini. Kawasha gari yake, kufika njiani hali ilikuwa mbaya kaamua kurudi. Kafika home kavua nguo kaingia tena kitandani, kamnong’oneza mkewe aliyekuwa usingizini; “Yaani hali ya hewa huko nje mbaya sana” Mke: Si ndio nimemshangaa huyu mpumbavu eti kaenda kazini…
Hasira za mtoto
Baba na mtoto:
Baba: Mwanangu ukiwa na hasira unafanya nini?
Mtoto: Naenda chooni.
Baba: Chooni? Kufanya nini?
Mtoto: Kusafisha.
Baba: Halafu ndio hasira zinaisha?
Mtoto: Ndio. Nasafisha choo kwa mswaki wako.
Mgonjwa na Dokta
Mgonjwa: Dokta nimekuja nahisi ninaumwa Malaria na kifua.
Dokta: Sasa ushajua unaumwa nini hapa umefuata nini kwangu?
Mgonjwa: Sasa si nimekuja kwa dokta.
Dokta: Wanaojua kuwa wanaumwa kama wewe wanapitiliza maabara.
Pilau la bachela
Bachela mmoja aliyekua akiishi kwa muda mrefu peke yake kwenye nyumba aliyopanga siku moja alitaka kupika pilau kwa mara ya kwanza. Sasa asijue nini kinachobadilisha rangi ya wali kuwa rangi ya brown, yeye akapika kama kawaida (wali) kisha wakati wa kula akavaa miwani yenye rangi ambayo ukiuangalia wali unauona kama pilau wakati anakula.
Mwizi na chizi
Mwizi kaiba TV na kuanza kukimbia nayo, kumbe ile nyumba mlikuwa na chizi, akaanza kumkimbiza yule mwizi. Kila mwizi akiongeza mbio chizi nae huyo, mwishowe mwizi akasalimu amri na kusimama, yule chizi akamsogelea na kumwambia.. Daah umesahau remote hii hapa mwizi kafleti.
Chemsha bongo
Baba akimuuliza chemsha bongo mwanae anayesoma shule ya chekechea “haya niambie kitu gani hakiwezi kuliwa wakati wa breakfast?” Mtoto akajibu “hiyo mbona rahisi baba, si lunch na dinner”
Huyu mme ni shida
MKE..mume wangu unaweza kuua simba kwasababu yangu???
MME: Hapana mke wangu, sema kingine
MKE:unaweza kunipa nione watsapp yako nione msgs?
MME: Haya sema huyo simba yukwap nikamuue
Darasa lolote lile halikosi watu kama hawa
Darasa lolote lile (hasa vyuoni) lazima liwe na wanafunzi wafuatao:
1. Mrembo wa darasa.
2. Playboy/playgirl. Hawezi kutembea na msichana/mvulana mmoja mara mbili.
3. Group ya marafiki watatu. Kila mara wako pamoja.
4. Mtu mwenye maswali ya kuudhi/kukera.
5. Msongolist kimeo. Huyu huwa anasoma sana bt hana bahati ya kufanya vizuri. Yani msuli tembo, bt matokeo sisimizi.
6. Mlafi. Huyu huwa hakatai offer.
7. Mtoro wa kudumu. Haji darasani hata km hana sababu.
8. Mchelewaji wa kudumu. Anakuja kipindi kiko katikati au kinakaribia kuisha.
9. Miss/Mr.Misifa. kila mara ataeleza the way nyumbani kwao walivyo matajiri.
10. Less talkative bt kiwembe. Jamaa mkimya bt unakuta ametembea na karibu wasichana 15 hapo class.
11. Handsome boy ambaye hana mpango na wanawake.
12.Chips addicted. Hawa wanaweza kula chips asubuhi mchana na jioni. Jumatatu hadi jumatatu.
13. Back benchers. Hawa huwa watundu sana na ni watu wa jokes. Huwa hawajibu swali, but wanasubiri wakati wa kushangilia waongeze bezi.
14. Wambea. Hawapitwi na kitu darasani na washazoea kufeli.
15. Mchungaji/Mtumishi wa Mungu,
16. Waimbaji/Wasanii,
17.Walevi
18.Mabishoo.
19. Team popo. Hawa wewe na hela wasiwe na hela wanakesha club,
20.Mwenye aibu kusimama mbele za watu. Wakati wa Presentation anakimbilia kusimama nyuma ya wenzie,
21. Viherehere. Hawa mara nyingi hutokea kupendwa sana na waalimu.
22. Wanaosoma ili kushindana kwny GPA.
23. Kupe. Huyu boom likitoka atawaganda wenzie hadi ziishe, halafu yeye anaanza kula zake alone.
24. Wise man/woman. Huyu huwa ni mtu anayeaminika na kila mtu darasani. Hutumika sn kushauri pale mambo yanapoenda mrama. Mara nyingi huwa ni mtu mzima.
25.mpenda supu” yeye hata ya nyani atakunywa tu.
26.Fix man. Huyu atakuomba jero, akafuatilie dili la milioni kumi town, kumbe hana hela ya chai.
27. Photocopy machine. Huyu ukimuonesha majibu kwny mtihani anaweza kucopy hadi jina lako.
💥Usposema wewe uko namba ngapi mwngine atakusema😜😜😅😅😅😅😅
Cha kufanya msichana akikukimbia halafu atake kukurudia
……… Kama msichana atakutupa kwa sababu huna pesa, na baadaye unapopata pesa akarudi tena kuomba msamaha… Ndugu yangu….. Msamehe…. Mpe ahadi ya ndoa, mwambie utamuoa…. iambie familia yake unataka kufanya ukarabati wa nyumba yao…… Ondoa paa lote la nyumba yao halafu TOWEKA…..
😂……… 😂…….. 😂
Duh! Hiki nacho chombo cha moto?
_Sheria inasema kila anaetembea na chombo cha moto barabarani sharti awe na leseni._
_Sasa hawa wauza kahawa mbona wanatembea na chombo cha moto lakini hawakamatwi 😡._
_Hizi sheria zinapendelea._
😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂😂
Huyu mke ni shida!
MUME: “Unajua mi unanishangaza sana, kila siku nakusikia mara useme TV yangu, gari yangu, chumbani kwangu, mara hoo watoto wangu. Sisi ni mke na mume, kila kitu ni chetu. Jirekebishe bwana”.👴😎😎😒
MKE: Yuko kimya anaendelea na shughuli zake za kupekua kabatini kama hasikii, na hakumjibu kitu mumewe.👵😷
MUME: Akamuuliza kwa hamaki,”Sasa hapo unatafuta nini?”.👴😡
MKE: “Sidiria yetu!!”👙💏
MUME: (kamfungia kabatini alafu kamwambia. “nipo chumbani , “)👴😷😷
💃💃💃💃💃💃
😂😂😂😂😂😂
Kama mpezi wako akikuita MAMITO Unatakiwa umjibu hivi
Akina dada mpenzi wako akikuita MAMITO usikubali
na yeye mwite MAFORONYA kama mbwai na iwe mbwai🤪🤪🤪🤪🤪🤪
Recent Comments