Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto halisi ya dhambi zangu, nakutolea moyo wangu dhaifu. Nifanye mnyenyekevu, mvumilivu na safi, nikikubali na kuyatii kabisa mapenzi yako. Ee Yesu mwema, unijalie niishi nawe na kwa ajili yako. Unilinde niwapo katikati ya hatari, unifariji katika mateso, unipe afya ya mwili na msaada katika mahitaji ya mwili, Baraka yako juu ya kila nilifanyalo, na neema ya kifo chema. Amina.
Ee Yesu uliyesema βKweli nawaambieni, ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, gongeni nanyi mtafunguliwaβ, tazama ninagonga, ninatafuta na kuomba β¦β¦.. (Taja ombi lako)
Baba Yetuβ¦.., Salamu Maria β¦β¦.., Atukuzwe Babaβ¦β¦..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Yesu uliyesema βKweli nawaambieni, chochote mtakachomwomba Baba kwa jina langu mtapewaβ, tazama kwa jina lako ninaomba β¦β¦. (Taja ombi lako)
Baba Yetuβ¦.., Salamu Maria β¦β¦.., Atukuzwe Babaβ¦β¦..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Yesu uliyesema βKweli nawaambieni, mbingu na dunia zitapita lakini maneno yangu hayatapita kamweβ, tazama, nikitiwa nguvu na maneno yako ya kweli ninaomba β¦β¦.. (Taja ombi lako)
Baba Yetuβ¦.., Salamu Maria β¦β¦.., Atukuzwe Babaβ¦β¦..
Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutumainia kwa moyo wote!
Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ambaye kwako ni kitu kimoja tu kisichowezekana, ambacho ni kutoacha kutowaonea huruma wenye huzuni, utuhurumie sisi wakosefu maskini na utujalie neema tukuombayo kwa njia ya Moyo Imakulata wa Maria, Mama yetu mpole.
Sali βSalamu Malkiaβ na kuongezea, βMtakatifu Yosefu Baba Mlishi wa Yesu, utuombeeβ.
P.S. β Sala hii ya Novena ilisaliwa kila siku na PADRE PIO kwa ajili ya kuwaombea wale wote waliomwomba msaada wa sala zake. Unaweza kuisali kwa namna tofauti tofauti. Mfano, kama Novena ya siku tisa, ambapo unasali sala hii mara moja au zaidi kila siku kwa siku tisa, au unaweza kuifanya kama Novena ya masaa, ambapo unasali sala hii kila baada ya saa moja kwa masaa tisa kwa siku hiyo hiyo, hasa kama kitu unachokiomba ni cha haraka au umesongwa moyoni. Vilevile unaweza kuifanya sala hii kama sehemu ya sala zako za kila siku katika mwezi Juni ambao ni mwezi uliotengwa na Kanisa kwa ajili ya kuuheshimu Moyo Mtakatifu wa Yesu, na hapo utaitumia kuwaombea watu waliokuomba msaada wa sala zako kama alivyofanya Mtakatifu Padre Pio. Pia unaweza kuitumia kama sala yako ya siku zote au ya mara kwa mara kwa ajili ya mahitaji mbalimbali.
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Baraka kwako na familia yako.
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Tembea kwa imani, si kwa kuona
ππ Neema za Mungu zisikose
ππ Nakusihi Mungu
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Rehema zake hudumu milele
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πβ¨ Mungu atakuinua
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Nguvu hutoka kwa Bwana
Katika imani, yote yanawezekana
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
ππ Mungu wetu asifiwe
Mungu akubariki!
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Neema ya Mungu inatosha kwako
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
Neema na amani iwe nawe.
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
Mwamini katika mpango wake.
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Tumaini ni nanga ya roho
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mungu ni mwema, wakati wote!
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Amina
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πβ€οΈ Mungu akubariki
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
ππ Mungu akujalie amani
Sifa kwa Bwana!
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
ππ Mungu alete amani
Mwamini Bwana; anajua njia
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Endelea kuwa na imani!
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
πππ
πππ Mungu akufunike na upendo
πππ« Mungu ni mwema
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
ππ Nakushukuru Mungu
Rehema hushinda hukumu
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πππ
Nakuombea π
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Dumu katika Bwana.
ππ Mbarikiwe sana