Roho ya Kristo unitakase
Mwili wa Kristo uniokoe
Damu ya Kristo unifurahishe
Maji ya ubavu wake Kristo yanioshe
Mateso ya Kristo nguvu yanizidishie
Ee Yesu mwema unisikilize
Katika madonda yako unifiche
Usikubali nitengwe nawe
Na adui mwovu unikinge
Saa ya kufa kwangu uniite
Uniamuru kwako nije
Na watakatifu wako nikutukuze
Milele na milele.
Amina.