SOMO 1: Yos. 5:9a, 10-12
Bwana akamwambia Yoshua, Siku hii ya leo nimeivingirisha hiyo aibu ya Misri iondoke juu yenu.
Basi wana wa Israeli wakapanga hema zao huko Gilgali; nao wakala sikukuu ya pasaka siku ya kumi ya nne ya mwezi, jioni, katika nchi tambarare za Yeriko. Nao wakala katika mazao ya nchi siku ya pili ya kuiandama hiyo sikukuu ya pasaka, mikate isiyotiwa chachu, na bisi, siku iyo hiyo.
Ndipo ile mana ikakoma siku ya pili yake, baada ya wao kuyala hayo mazao ya nchi; na hao wana wa Israeli hawakuwa na mana tena; lakini wakala katika viliwa vya nchi ya Kanaani mwaka huo.
WIMBO WA KATIKATI: Zab. 34:1-6 (K) 8
(K) Onjeni muone ya kuwa Bwana yu mwema.
Nitamhimidi Bwana kila wakati,
Sifa zake kinywani mwangu daima.
Katika Bwana nafsi yangu itajisifu,
Wanyenyekevu wasikie wakafurahi. (K)
Mtukuzeni Bwana pamoja nami,
Na tuliadhimishe jina lake pamoja.
Nalimtafuta Bwana akanijibu,
Akaniponya na hofu zangu zote. (K)
Wakamwelekea macho wakatiwa nuru,
Wala nyuso zao hazitaona haya.
Maskini huyu aliita, Bwana akasikia,
Akamwokoa na taabu zake zote. (K)
SOMO 2: 2 Kor. 5:17-21
Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita; tazama! Yamekuwa mapya. Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho; yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho. Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo mpatanishwe na Mungu. Yeye asiyejua dhambi alimfanya kuwa dhambi kwa ajili yetu, ili sisi tupate kuwa haki ya Mungu katika Yeye.
SHANGILIO: Lk. 15:18
Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako.
INJILI: Lk. 15:1-3, 11-32
Basi watoza ushuru wote na wenye dhambi walikuwa wakimkaribia wamsikilize. Mafarisayo na waandishi wakanung’unika, wakisema, Mtu huyu huwakaribisha wenye dhambi, tena hula nao. Akawaambia mfano huu, akisema.
Mtu mmoja alikuwa na wana wawili; yule mdogo akamwambia babaye, Baba, nipe sehemu ya mali inayoniangukia. Akawagawia vitu vyake. Hata baada ya siku si nyingi, yule mdogo akakusanya vyote, akasafiri kwenda nchi ya mbali; akatapanya mali zake huko kwa maisha ya uasherati.
Alipokuwa amekwisha tumia vyote, njaa kuu iliingia nchi ile, yeye naye akaanza kuhitaji. Akaenda akashikamana na mwenyeji mmoja wa nchi ile; naye alimpeleka shambani kwake kulisha nguruwe. Akawa akitamani kujishibisha kwa maganda waliyokula nguruwe, wala hapana mtu aliyempa kitu. Alipozingatia moyoni mwake, alisema, Ni watumishi wangapi wa baba yangu wanaokula chakula na kusaza, na mimi hapa ninakufa kwa njaa. Nitaondoka, nitakwenda kwa baba yangu na kumwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena; nifanye kama mmoja wa watumishi wako. Akaondoka, akaenda kwa babaye.
Alipokuwa angali mbali, baba yake alimwona, akamwonea huruma, akaenda mbio akamwangukia shingoni, akambusu sana. Yule mwana akamwambia, Baba, nimekosa juu ya mbingu na mbele yako; sistahili kuitwa mwana wako tena. Lakini baba aliwaambia watumwa wake, Lileteni upesi vazi lililo bora, mkamvike; mtieni na pete kidoleni, na viatu miguuni; mleteeni ndama yule aliyenona mkamchinje nje; nasi tule na kufurahi; kw akuwa huyu mwanangu alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana. Wakaanza kushangilia.
Basi, yule mwanawe mkubwa alikuwako shamba na alipokuwa akija na kuikaribia nyumba, alisikia sauti ya nyimbo na machezo. Akaita mtumishi mmoja, akamwuliza, Mambo haya, maana yake nini? Akamwambia, Ndugu yako amekuja, na baba yako amemchinja ndama aliyenona, kwa sababu amempata tena, yu mzima. Akakasirika, akakataa kuingia ndani.
Basi babaye alitoka nje, akamsihi. Akamjibu baba yake, akasema. Tazama, mimi nimekutumikia miaka mingapi hii, wala sijakosa amri yako wakati wowote, lakini hujanipa mimi mwana-mbuzi, nifanye furaha na rafiki zangu; lakini, alipokuja huyu mwana wako aliyekula vitu vyako pamoja na makahaba, umemchinjia yeye ndama aliyenona.
Akamwambia, Mwanangu, wewe u pamoja nami siku zote, na vyote nilivyo navyo ni vyako. Tena, kufanya furaha na shangwe ilipasa, kwa kuwa huyu ndugu yako alikuwa amekufa, naye amefufuka; alikuwa amepotea, naye ameonekana.
Neno la Bwana…sifa kwako Ee Kristo
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Sifa kwa Bwana!
Mwamini katika mpango wake.
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Imani inaweza kusogeza milima
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Mungu ni mwema, wakati wote!
Baraka kwako na familia yako.
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika imani, yote yanawezekana
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu akubariki!
Dumu katika Bwana.
Neema ya Mungu inatosha kwako
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Rehema zake hudumu milele
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Endelea kuwa na imani!
Mwamini Bwana; anajua njia
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Neema na amani iwe nawe.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Nakuombea 🙏
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Rehema hushinda hukumu
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Tumaini ni nanga ya roho