Mafundisho ya Katekisimu

Amri Kumi za Mungu: Mambo ya Msingi unayopaswa kufahamu

Amri kumi za Mungu ni zipi?

1. Ndimi Bwana, Mungu wako usiabudu miungu wengine.
2. Usiape bure kwa jina la Mungu wako.
3. Fanya siku ya Mungu

4. Waheshimu Baba na Mama, upate miaka mingi na heri duniani.
5. Usiue
6. Usizini
7. Usiibe
8. Usiseme uongo
9. Usitamani mwanamke asiye mke wako.
10. Usitamani mali ya watu.


Je, ni lazima kila mtu ashike Amri kumi za Mungu?

Ndiyo. Ni lazima kila mtu ashike Amri kumi za Mungu hata kama si Mkristo kwa sababu Mungu ni mkubwa wa watu wote. (Kut 20:1-17, Kumb 5:1-21)


Kwa nini Mungu alitupa Amri kumi?

Mungu alitupa amri kumi ili kutufudisha mambo yatupasayo kwa Mungu, kwa watu na kwetu sisi wenyewe


Katika amri ya kwanza ya Mungu tumeamriwa nini?

Tumeamriwa tusadiki kuwa Mungu ni mmoja, ndiye Baba yetu na Mkubwa wetu: tumpende, tumwabudu yeye peke yake. (Mt 10:33, Kumb 6:4-9)


Wakatoliki tunamwabudu Mungu kwa namna gani?

Tunamwabudu Mungu kwa sala , sadaka na matendo mema


Katika amri ya kwanza ya Mungu tumekatazwa nini?

Tumekatazwa kumdharau Mungu na kuweka imani yetu katika viumbe badala ya Mungu.


Je, kuna viumbe ambavyo tunaviheshimu kwa kumtukuza Mungu?

Ndiyo twamuheshimu Bikira Maria, Malaika na Watakatifu.


Kwa nini yatupasa kuwaheshimu Watakatifu?

Kwa sababu hao ni washindi, rafiki wa Mungu na waombezi wetu.


Je, tuna ruhusa ya kuwaabudu Watakatifu?

Hatuna ruhusa ya kuwaabudu Watakatifu tunawaheshimu tu.


Je sanamu zimekatazwa?

Sanamu hazijakatazwa, ila tunaziheshimu kwa sababu zinatukumbusha Mungu na Watakatifu. (Kut 25:18-22).

18 Nawe fanya makerubi mawili ya dhahabu; uyafanye ya kazi ya kufua, katika hiyo miisho ya kiti cha rehema, huku na huku. 19 Weka kerubi moja mwisho mmoja, na kerubi la pili mwisho wa pili; fanya hayo makerubi ya kitu kimoja na kiti cha rehema, mwisho huku na mwisho huku. 20 Na hayo makerubi yatainua mabawa yao juu, na kukifunika hicho kiti cha rehema kwa mabawa yao, na nyuso zao zitaelekeana hili na hili; nyuso za hayo makerubi zitaelekea kiti cha rehema. 21 Weka kiti cha rehema juu ya hilo sanduku, kisha utie huo ushuhuda nitakaokupa ndani ya sanduku. 22 Nami nitaonana nawe hapo, na kuzungumza nawe pale nilipo juu ya kiti cha rehema, katikati ya hayo makerubi mawili yaliyo juu ya sanduku la ushuhuda, katika mambo yote nitakayokuagiza kwa ajili ya wana wa Israeli. Kutoka 25 :18-22.

Vile vile Mungu alishawahi kuwaagiza Waisraeli Wachonge sanamu ya nyoka na yeyote atakayeumwa na nyoka akiiangalia atapona.


Mfano wa sanamu takatifu ni zipi?

Sanamu ya Bikira Maria, Mtoto Yesu, Mt. Yosefu, Moyo wa Yesu na za Watakatifu.


Ni nanai ana kosa kumuabudu Mungu?

Anayekosa kumuabudu Mungu ni yule;

1. Anayeacha kusali au anayesali hovyo
2. Anayemkufuru Mungu
3. Anayeamini na kushika mambo ya kipagani


Mambo gani yanavunja amri ya kwanza ya Mungu?

Mambo hayo ni;

1. Kuabudu sanamu
2. Kufanya matambiko
3. Kwenda kwa waganga
4. Kupiga bao au ramli
5. Kuvaa hirizi
6. Kushiriki mambo ya kichawi n.k.


Ni nini maana ya kuabudu sanamu?

Kuabudu sanamu ni kukipa kiumbe chochote heshima au upendo anaostahili Mungu peke yake.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu utunzaji wa mazingira?

Kanisa Katoliki limekuwa likitangaza utunzaji wa mazingira kama jukumu la kikristo kwa miaka mingi. Ni wajibu wa kila mmoja wetu kuhakikisha kwamba tunalinda na kuhifadhi mazingira kwa ajili ya vizazi vijavyo. Utunzaji wa mazingira ni kazi yetu sote na inatokana na imani yetu ya kikristo na maadili tunayoyafuata.

Katika kitabu cha mwanzo 2:15, Mungu anamwamuru Adamu awatunze na kuilinda bustani ya Edeni. Kwa hivyo, imani ya Kanisa Katoliki inaamini kwamba sisi ni wasimamizi wa mazingira na tunapaswa kulinda kila aina ya uhai uliopo. Kwa kufanya hivyo, tunawajibika kwa Mungu na kwa vizazi vijavyo.

Kanisa Katoliki linategemea falsafa ya kiekumene katika kutunza mazingira. Falsafa hii inasema kwamba binadamu na mazingira ni sehemu moja ya ulimwengu mmoja. Tunapata maisha yetu kutoka kwa mazingira na kwa hivyo, tunapaswa kuilinda mazingira kama sehemu ya jukumu letu la kibinadamu.

Vilevile, imeandikwa katika KKK 2402, "uharibifu wa mazingira ni kinyume cha maadili na inaweza kuathiri maisha ya watu." Kwa hivyo, Kanisa linasisitiza umuhimu wa kutunza mazingira kama sehemu ya maadili yetu.

Katika Mkutano wa Mazingira wa Vatican uliofanyika mnamo 2019, Baba Mtakatifu Francis aliwataka watu wote kuchukua hatua za kuhifadhi mazingira. Aliwataka wakristo kuhakikisha kwamba wanawajibika kwa kufuata mafundisho ya kanisa na kuishi maisha yenye kuheshimu mazingira.

Kwa hivyo, tunapaswa kulinda mazingira kwa kufuata kanuni za utunzaji wa mazingira kama vile kupunguza utumiaji wa plastiki na kukuza utumiaji wa nishati mbadala. Tunapaswa pia kuhakikisha kwamba tunatumia rasilimali za dunia kwa njia yenye uwajibikaji na kwa kuzingatia mahitaji ya vizazi vijavyo.

Kwa kuhitimisha, Kanisa Katoliki linatukumbusha kwamba utunzaji wa mazingira ni jukumu letu kama wakristo. Tunapaswa kuhakikisha kwamba tunatumia rasilimali za dunia kwa njia yenye uwajibikaji na kuheshimu kila aina ya uhai uliopo. Tunapaswa kuwa wasimamizi wa mazingira na kutoa mfano wa maisha yenye kuheshimu mazingira kwa vizazi vijavyo.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu maisha ya sala?

Kanisa Katoliki linathamini sana maombi kama sehemu muhimu ya maisha yetu ya kiroho. Imani yetu inatufundisha kuwa kupitia maombi tunawasiliana na Mungu na kuimarisha uhusiano wetu naye. Hii ni kwa sababu tumeumbwa kwa mfano wa Mungu na tunaishi kwa neema yake.

Maombi ni mawasiliano ya moyo na Mungu, ambayo yanatuwezesha kumwomba msamaha kwa dhambi zetu na kupata nguvu za kushinda majaribu. Kwa hivyo, sala ni sehemu muhimu ya maisha ya Kikatoliki na inahitajika kwa maendeleo yetu ya kiroho.

Tunapata mafundisho haya kutoka kwa Yesu mwenyewe, ambaye aliwaambia wanafunzi wake kuwa wasali daima na kutokata tamaa (Luka 18: 1). Katika Yohana 15: 7, Yesu anatuambia kuwa ikiwa tunakaa ndani yake na neno lake linakaa ndani yetu, tunaweza kuomba chochote tunachotaka, na Mungu atatupa.

Kanisa Katoliki pia linatupa mfano wa sala kwa kufundisha kwamba sala ya Bwana ni muhimu sana. Sala hii inatufundisha kumwomba Mungu kwa njia ya kinafiki na kutambua kwamba yeye ndiye muumba wetu. Tunamuomba Mungu kwa mahitaji yetu ya kila siku, pamoja na kupata nguvu za kushinda dhambi.

Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunaambiwa kuwa sala ya Kanisa ni muhimu sana. Sala hii inaundwa na sala za Wakristo wote na inaunganisha Kanisa kama mwili wa Kristo. Sala hii inatupa nguvu za kuishi maisha ya Kikristo kwa kupata nguvu zetu kutoka kwa Roho Mtakatifu.

Kwa hivyo, kama Wakatoliki, tunahimizwa kuomba kwa nguvu zetu zote na kwa moyo wote. Tunatafuta kumjua Mungu vizuri zaidi na kukuza uhusiano wetu naye kupitia sala. Kwa njia hii, tunaweza kuwa na maisha yenye furaha, amani, na raha ya ndani.

Kwa hiyo, tunakuhimiza, mpendwa msomaji, kuanza maisha ya sala na kujitolea kwa Bwana wetu. Kwa kufanya hivyo, utapata furaha ya kweli na utaishi maisha yenye maana. "Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; pigeni hodi, nanyi mtafunguliwa" (Mathayo 7: 7).

Mambo ya Msingi kufahamu kuhusu Ndoa ya Kikatoliki

Daraja na ndoa ni tofauti na sakramenti nyingine kwa sababu gani?
Daraja na ndoa ni tofauti na sakramenti nyingine kwa sababu hazilengi hasa faida ya mtu anayezipokea, bali huduma zake kwa ajili ya Kanisa na jamii. Daraja inatia uwezo wa Kristo kwa ustawi wa Kanisa, Bibi arusi wake. Ndoa inatia upendo wake mwaminifu kwa ustawi wa familia, kanisa dogo la nyumbani.
“Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha kanisa lake Mungu, alilolinunua kwa damu yake mwenyewe” (Mdo 20:28).
“Hakuna mtu anayeuchukia mwili wake popote; bali huulisha na kuutunza, kama Kristo naye anavyolitendea Kanisa. Kwa kuwa tu viungo vya mwili wake. Kwa sababu hiyo mtu atamwacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe na hao wawili watakuwa mwili mmoja. Siri hiyo ni kubwa; ila mimi nanena habari ya Kristo na Kanisa” (Ef 5:29-32).

Kadiri ya mpango wa Muumba, ndoa halisi ina sifa ngapi?
Kadiri ya mpango wa Muumba, ndoa halisi ina sifa tatu: umoja, uimara na utayari wa kuzaa.
“Hamkusoma ya kwamba yeye aliyewaumba mwanzo, aliwaumba mtu mume na mtu mke, akasema, ‘Kwa sababu hiyo, mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe, na hao wawili watakuwa mwili mmoja?’ Hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja. Basi aliowaunganisha Mungu, mwanadamu asiwatenganishe” (Math 19:4-6).
“Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, ‘Zaeni, mkaongezeke, mkaijaze nchi, na kuitiisha’” (Mwa 1:28).
Mitara, uzinifu, talaka, ushoga na kukataa uzazi ni kinyume cha mpango huo.

Yesu aliweka sakramenti ya ndoa kwa sababu gani?
Yesu aliweka sakramenti ya ndoa kwa sababu ya umuhimu wa familia kwa ustawi wa mume na mke, watoto, jamii na ufalme wa Mungu, na kwa sababu ya uzito wa majukumu yanayohusika.
“Siku ya tatu palikuwa na arusi huko Kana, mji wa Galilaya; naye mama yake Yesu alikuwepo. Yesu naye alikuwa amealikwa arusini pamoja na wanafunzi wake” (Yoh 2:1-2), akaleta divai bora ya ndoa sakramenti badala ya ndoa ya kimaumbile.
Hivyo ametuandalia neema tuweze kushinda “ugumu wa mioyo” (Math 19:8) unaohatarisha daima uzuri wa mpango wa Mungu kuhusu upendo mwaminifu katika ndoa. “Mungu aliona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana” (Mwa 1:31).

Ndoa ya Wakristo ni sakramenti ya nani?
Ndoa ya Wakristo ni sakramenti ya Yesu na Kanisa lake.
“Njoo huku, nami nitakuonyesha yule Bibi arusi, mke wa Mwanakondoo” (Ufu 21:9).
Wakiwa na ndoa halisi, mume na mke waliobatizwa ni ishara wazi ya hao wanaarusi wawili wasioonekana.
“Kama vile Kanisa limtiivyo Kristo, vivyo hivyo wake nao wawatii waume zao katika kila jambo. Enyi waume, wapendeni wake zenu, kama Kristo naye alivyolipenda Kanisa, akajitoa kwa ajili yake” (Ef 5:24-25).
Ndiyo sababu Mkatoliki hawezi kufunga ndoa bila ya kuhusisha Kanisa na kufuata taratibu zake.

Ni zipi Sakramenti za Huduma ya ushirika na utume?
Ni Sakramenti mbili ambazo ni Sakramenti ya Daraja na Sakramenti ya Ndoa

Sakramenti ya ndoa ni nini?
Sakramenti ya ndoa ndio yenye kuwaunganisha wakristo wawili mume namke waliopendana kwa hiari bila shuruti au vitisho au kizuizi kwa kuwapa neema ya kuishi pamoja kitakatifu wakiwalea watoto wao katika utakatifu

Je, ndoa halali yaweza kuvunjwa?
Sakramenti ya ndoa iliyofungwa kihalali hudumu milele kwani Yesu anafundisha kuwa “Alichokiunganisha Mungu mwanadamu asikitenganishe” (Mt 19:6)

Ndoa imewekwa na nani?
Ndoa imewekwa na Mungu mwenyewe na Yesu Kristo ameeinua na kuifanya Sakramenti. (Mwz 2:18; Mt 19:1-12)

Kabla ya kupokea Sakramenti ya Ndoa hutakiwa nini?
Kabla ya kupokea Sakramenti ya Ndoa hutakiwa;
1. Uhuru wa kila mmoja
2. Matangazo ya ndoa
3. Wachumba wawe na nia ya kweli ya kuoana
4. Mafundisho na semina ya ndoa
5. Wasiwe na kizuizi chochote cha ndoa
6. Wasikae suria na wapokee Sakramenti ya Kitubio

Mtu aweza kupokea Sakramenti ya ndoa zaidi ya mara moja?
Ndiyo, mwenzi akifa yule aliyebaki yupo huru kufunga ndoa tena (1Kor 7:39)

Vizuizi vya ndoa ni kitu gani?
Vizuizi vya ndoa ni vile vinavyofanya ndoa isiwe halali tangu mwanzo

Vizuizi vya ndoa ni vipi?
Vizuizi vya ndoa ni;
1. Upungufu wa umri
2. Uhanithi
3. Ndoa awali halali
4. Tofauti za dini au upagani
5. Daraja Takatifu
6. Nadhiri
7. Utekaji au kutumia nguvu
8. Taksiri au Jinai au Mauaji ya mwenzi wa ndoa
9. Uhusiano wa damu
10. Uhusiano wa ndoa
11. Ugoni au uhawara
12. Kuasili mtoto au Uhusiano wa kisheria

Ndoa mchanganyiko maana yake ni nini?
Ndoa mchanganyiko ni ndoa kati ya Mkristo Mkatoliki na Mkristo asiye Mkatoliki

Ndoa ya utofauti wa Imani maana yake ni nini?
Ndoa ya utofauti wa Imani ni ndoa kati ya Mkristo Mkatoliki na mtu ambaye hajabatizwa kwa mfano Mpagani, Mwislamu, Yehova, Mlokole tangu kuzaliwa n.k

Mkristo Mkatoliki awezaje kufunga ndoa mchanganyiko au utofauti wa dini kwa uhalali?
Aweza kufunga ndoa hiyo kwa uhalali baada ya kupata ruhusa maalumu ya Askofu kwa Barua.

Ili Askofu atoe ruhusa ya kufungisha ndoa ya mchanganyiko au dini tofauti kuna Masharti gani?
Ndiyo, Askofu atatoa ruhusa baada ya Mkristo Mkatoliki kuahidi kwamba;
1. Atabaki Imani Katoliki mpaka kufa na isiwe amedanganya
2. Watoto wote watabatizwa na kulelewa katika Kanisa Katoliki
3. Huyo anayefunga naye ndoa akubali bila masharti yoyote

Je, Mchumba Mkatoliki aweza kuiacha Imani yake kwa sababu ya Ndoa?
Hapana, Kwa kuwa Kanisa Katoliki limeasisiwa na Mungu kwa njia ya Yesu Kristo kama la lazima kwa kupata wokovu, wanaokataa kuingia au kuhudumu ndani yake hawawezi kuokolewa.

Kuna kosa gani kama mmoja wapo atakuwa amedanganya ili aruhusiwe kufunga ndoa mseto au mchanganyiko
Kama mmoja amedanganya basi ndoa hiyo ingawa imefungwa haitakuwa halali kabisa mpaka mwisho. Watadumu katika dhambi mpaka kufa au watubu.

Kanisa linatoa ushahuri gani kuhusu ndoa halali au ya mseto?
Kanisa linatambua hatari kubwa kwa Imani linashauri watoto wake wawe na busara kubwa wanapoamua kupendana kwa lengo la kufunga ndoa.

Je, ndoa halali inaweza kuvunjwa?
Hapana, Hakuna yeyote anayeweza kuvunja ndoa halali isipokuwa kifo. (Mt 19:4-6)

Anayevunja ndoa na kuoa au kuolewa anaweza kupokea Sakramenti?
Hapana, Anayevunja maagano ya ndoa na kuoa au kuolewa hawezi kupokea Sakramenti ya Ekaristi wala Kitubio hadi afanye toba na kurekebisha hali hiyo. (Mk 10:11-12)

Ni nani wahudumu wa Sakramenti ya ndoa?
Wahiudumu rasmi wa Sakramenti ya ndoa ni wachumba wenyewe, Padri kama shahidi rasmi wa kanisa. Tena ni lazima ifungwe mbele ya mashahidi wengine wawili.

Watu wa jinsia moja waweza kuoana?
Hapana, watu wa Jinsia moja hawawezi kuoana na wakifanya hinyo wanatenda dhambi kubwa inayomlilia Mungu. (Wal 18:22)

Mafundisho kuhusu Neema

Je, tunaweza kuhakikisha neema ya utakaso?
Hapana, hatuwezi kuhakikisha neema ya utakaso kwa kuwa ni tukio ambalo linapita maumbile na kufanyika rohoni, hivyo halifikiwi na hisi zetu. Pengine Mungu anatokeza dalili fulani za badiliko hilo kama vile furaha ya ndani au karama ya nje, lakini hizo hazihitajiki wala hazitoshi kuthibitishia mtu amepata neema hiyo.
“Wengi wataniambia siku ile: Bwana, Bwana, hatukufanya unabii kwa jina lako, na kwa jina lako kutoa pepo, na kwa jina lako kufanya miujiza mingi? Ndipo nitawaambia dhahiri: Sikuwajua ninyi kamwe; ondokeni kwangu, ninyi mtendao maovu” (Math 7:22-23).
“Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo na upatu uvumao. Tena nijapokuwa na unabii, na kujua siri zote na maarifa yote, nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu mimi. Tena nikitoa mali zangu zote kuwalisha maskini, tena nikijitoa mwili wangu niungue moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu” (1Kor 13:1-3).

Neema ni nini?
Neema ni kipaji cha roho kinachopita nguvu za viumbe vyote; ndicho kipaji tupewacho na Roho Mtakatifu ili tupate uzima wa milele. (Lk 1:30, Rum 5:2)

Kuna aina ngapi za neema?
Kuna aina mbili za neema
1. Neema ya utakaso
2. Neema ya msaada

Neema ya Utakaso ni nini?
Neema ya Utakaso ni uzima wa Kimungu unaomiminwa na Roho Mtakatifu mioyoni mwetu. (Yoh 1:16, Yoh 3:3-5)

Neema ya Utakaso yapatikanaje?
Neema ya Utakaso yapatikana kwa;
1. Kwanza kwa Sakramenti ya Ubatizo
2. Sakramenti ya Kitubio
3. Kwa majuto kamili (majuto ya mapendo)
4. Yaongezwa kwa kupokea Sakramenti nyingine
5. Kwa Sala
6. Kwa Ibada Takatifu
7. Kwa matendo mema

Neema ya Utakaso yapoteaje?
Neema ya Utakaso yapotea kwa kutenda dhambi kubwa (dhambi ya mauti)

Kuna Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso?
Faida ya kuwa na Neema ya Utakaso ni;-
1. Kupendwa na Mungu hapa duniani
2. Na kupokelewa kwake mbinguni baada ya kufa

Neema ya Msaada ni nini?
Neema ya Msaada ni msaada tupatao kwa Roho Mtakatifu kutuongezea nguvu Rohoni tutende mambo mema na tuepuke Mabaya

Neema ya Msaada yapatikanaje?
Neema ya Msaada yapatikana kwa kupokea Sakramenti, kusali, na kutenda mambo ya Ibada (Yoh 15:5, 1Tim 2:4)

Amri ya Sita ya Mungu: Kutunza usafi wa moyo na kuwa waaminifu

Katika Amri ya Sita na Tisa Mungu ametuamuru nini?

Mungu ametuamuru kutunza usafi wa moyo na kuwa waaminifu katika ndoa.


Usafi wa Moyo ndio nini?

Usafi wa Moyo ni fadhila ya kiutu, zawadi ya Mungu, neema na tunda la Roho Mtakatifu.


Kwa sababu gani yatupasa kuwa na usafi wa moyo?

Yatupasa kuwa na usafi wa moyo kwa sababu:

1. Mungu awapenda hasa wenye usafi wa moyo. (Mt 5:8)
2. Sisi Wakristo ni Hekalu la Roho Mtakatifu. (1Kor 3:16-17)


Tumekatazwa nini ili tulinde usafi wa moyo?

Tumekatazwa haya;

1. Kutazama mwili kwa Tamaa mbaya na kuvaa vibaya
2. Kusema na kuimba, ngoma zisizo na adabu.
3. Kusikiliza machafu, kucheza michezo mixhafu.
4. Kutenda machafu peke yetu au pamoja na wenzetu. (Efe 5:3)
5. Kusoma vitabu na magazeti machafu na kuangalia picha chafu.


Katika Amri ya Tisa ya Mungu tumekatazwa nini?

Tumekatazwa haya;

1. Kutomtamani mke au mume wa mwingine
2. Kutamani mambo ya zinaa


Dhambi za uchafu huleta hasara gani?

Huleta hasara hizi;

1. Kuharibu usafi wa Moyo na Hekalu la Mungu
2. Huleta Magonjwa duniani na hasara ya baadae. mf UKIMWI. (Efe 5:5)
3. Huvunja amani ya familia
4. Kujijengea mazoea ya uchafu


Tulinde usafi wa Moyo namna gani?

1. Kusali mara dhidi ya kishawishi.
2. Kupokea sakramenti hasa Kitubio na Ekaristi mara nyingi
3. Kuepuka uvivu, ulevi na madawa ya kulevya.
4. Kukimbia nafasi dha dhambi.
5. Kutunza haya au soni
6. Kuwa na mazoea ya kufunga na kujinyima.

Maswali na Majibu kuhusu Kifo

Motoni ni nini?

Motoni ni makao mabaya kwa Shetani walaaniwa wakaapo mbali na Mungu wakiteswa milele. (Mt 25:41, Mik 9:42-43, 1Yoh 14:15)


Uzima wa milele ni nini?

Uzima wa milele ni maisha ya kukaa mbinguni na Mungu yasiyokua na mwisho.


Mambo makuu manne ya mwisho ni yapi?

Mambo hayo ni;
1. Kifo
2. Hukumu
3. Jehanamu (Motoni)
4. Paradiso. (Toharani/Mbinguni)


Je, ni muhimu tujiandae kufa?

Ndiyo, ni muhimu tujiandae kufa wakati wowote na namna yoyote kwa kuishi kitakatifu sasa na kwa kujiombea neema tutakazohitaji saa ya kufa kwetu, tukijua tumewekewa “kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu” (Eb 9:27).
“Katika mambo yako yote uukumbuke mwisho wako, hivyo hutakosa kamwe hata hatima” (YbS 7:36).
“Hamjui yatakayokuwako kesho! Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka” (Yak 4:14).
“Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni” (Math 26:41).


Je, ina thamani machoni pa Bwana mauti ya mtu aliyemcha?

Ndiyo, “ina thamani machoni pa Bwana mauti ya wacha Mungu wake” (Zab 116:15).
Hasa utiifu wa Yesu msalabani umegeuza laana ya kifo iwe baraka kwa waamini wake.
“Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao” (Ufu 14:13).


Tutakapofariki dunia itatutokea nini?

Tutakapofariki dunia roho yetu isiyokufa, mbali na mwili unaooza, itapewa tuzo au adhabu tuliyostahili kwa maisha yetu. “Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake” (Lk 16:22-23). “Kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida… ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo, maana ni vizuri zaidi sana” (Fil 1:21,23). “Nasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana” (2Kor 5:8). Kwa kuwa kifo ni “mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa” (Mhu 12:7). Siku ya ufufuo roho na mwili vitaungana tena kwa ajili ya uzima au moto wa milele. “Pumzi iliwaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno” (Ez 37:10).

Je baada ya kufa ni hapo hapo roho inaenda motoni au mbinguni, Au ni mpaka Siku ya hukumu Yesu Atakaporudi?

Ni siku ile ile Roho ya mtu aliyekufa inaenda Mbinguni, toharani au Motoni. Yesu alimwahidi yule mtu waliyesulubiwa pamoja kuwa watakuwa peponi pamoja siku hiyo hiyo na sio siku ya hukumu.
“Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.” 43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.” (Luka 23:42-43)
Sauli aliweza kuongea na Samweli hata baada ya kufa na Samweli alimbashiria mambo yatakayotokea kwa Sauli maanake ni kwamba Japokuwa alikuwa amekufa bado anayomuungano na Mungu ndio maana aliweza kumwambia Sauli mambo yatakayompata,
“7Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi ili nimwendee nipate kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.” 8Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie na unipandishie huyo nitakayekutajia,” 9Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya mfalme Sauli. Amewakatilia mbali wapunga pepo, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?” 10Sauli akamwapia huyo mwananmke kwa Jina la BWANA, akasema, “Kwa hakika kama BWANA aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.” 11Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani? Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.” 12Yule mwanamke alipomwona Samweli alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamwuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.” 13Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini? Yule mwanamke akasema, “Naona Mungu anapanda kutoka ardhini.” 14Sauli akamwuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi uso wake hadi ardhini. 15Samweli akamwuliza Sauli, Kwa nini unanitaabisha, kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe lakufanya.” 16Samweli akamwuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadam BWANA amekuacha na kuwa adui yako? 17BWANA ametenda lile alilotangulia kusema kwa kupitia kwangu. BWANA ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani, Daudi. 18Kwa sababu wewe hukumtii BWANA, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, BWANA amekutendea mambo haya leo. 19Zaidi ya hayo, BWANA atawatia Israeli pamoja na wewe mkononi mwa Wafilisti na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. BWANA pia atalitia jeshi la Israeli mkononi mwa Wafilisti.
Mfano Wa Tajiri Na Maskini Lazaro Yesu alisimulia hivi
19 Akasema, “Palikuwa na tajiri mmoja aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, nguo za gharama kubwa, kila siku. 20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima, alikuwa akiletwa mlangoni kwa huyo tajiri kila siku. 21 Lazaro alikuwa akitamani kula makombo yaliyodondoka mezani kwa tajiri. Hata mbwa walikuwa wakiramba vidonda vyake. 22 “Hatimaye, yule maskini alikufa. Malaika wakamchukua akakae pamoja na Ibrahimu mbinguni. Yule tajiri naye pia akafa, akazikwa. 23 Alipokuwa kuzimuni ambapo alikuwa akiteseka, alita zama juu, akamwona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro karibu yake. 24 Akaita, ‘Baba Ibrahimu, nionee huruma umtume Lazaro achovye japo ncha ya kidole chake katika maji aupoze ulimi wangu maana ninateseka kwenye moto huu.’ 25 Lakini Ibrahimu akamjibu, ‘Mwa nangu, kumbuka kwamba ulipokuwa hai ulipata kila kitu kizuri uli chotaka, ambapo Lazaro alipokea mabaya. Lakini sasa anafarijika hapa na wewe unateseka. 26 Isitoshe, kati yetu na ninyi huko, kumewekwa bonde kubwa lisilopitika ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko au kutoka huko kuja huku wasiweze.’ 27 Akasema, ‘Basi, baba, tafadhali umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu, 28 awaonye ndugu zangu, wasije wao pia wakaletwa mahali hapa pa mateso watakapokufa.’ 29 Ibrahimu akamjibu, ‘Ndugu zako wanazo sheria za Musa na maandiko ya Manabii. Itawapasa watii hayo.’ Lakini yule tajiri akazidi kumsihi, 30 ‘Hapana baba Ibrahimu, ndugu zangu hawatashawishiwa na hayo. Lakini mtu kutoka kuzimu akitumwa kwao watatubu na kuziacha dhambi zao.’ 31 “Ibrahimu akamwambia, ‘Wasiposikiliza na kutii sheria za Musa na Maandiko ya manabii, hawatashawishika kutubu hata kama mtu akifufuka kutoka kuzimu.”’ (Luka 16:19-31)
Wakati Yesu anabadilika Sura walitokea Musa na Eliya.
“Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu. 2 Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang’aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru. 3 Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye. 4 Hapo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya.” (Mathayo 17:1-5)
Yesu alituambia kuwa Mungu sio wa wafu bali wa walio hai ndio maana akaitwa Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo kwa kuwa Wote wako hai kwake.
37Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila keteketea, alipomwita Bwana ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki na Mungu wa Yakobo.’ 38Yeye Mungu si Mungu wa wafu bali wa walio hai, kwa kuwa Kwake wote ni hai.” (Luka 20:37-38)
Yesu alimwahidi yule mtu waliyesulubiwa pamoja kuwa watakuwa peponi pamoja siku hiyo hiyo na sio siku ya hukumu.
“Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.” 43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.” (Luka 23:42-43)
Angalia pia wakati Stefano akipigwa Mawe aliikabidhi roho yake kwa Mungu baada ya kuona mbingu zimefunguka hii ni kama Yesu alivyokuwa pale msalabani aliikabidhi Roho yake kwa Baba yake.
55Lakini yeye Stefano akiwa amejazwa Roho Mtakatifu, alikaza macho mbinguni, akaona utukufu wa Mungu, naye Yesu akiwa amesimama mkono wa kuume wa Mungu. 56Akasema, “Tazameni! Naona mbingu zimefunguka na Mwana wa Adamu amesimama upande wa kuume wa Mungu.’’ 57Lakini wao wakapiga kelele kwa sauti kubwa, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja. 58Wakamtupa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka nguo zao miguuni mwa kijana mmoja aitwae Sauli. 59Walipokuwa wakimpiga mawe, Stefano aliomba, “Bwana Yesu, pokea roho yangu” 60Kisha akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa akasema, “Bwana usiwahesabie dhambi hii.’’ Baada ya kusema haya, akalala. (Mdo 7:55-60)
Kwenye Ufunuo tunasoma (Ufunuo 6:9-10) “Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi? Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao.”
Kwa hiyo mtu akifa anaenda mbinguni au motoni kulingana na alivyoishi.
“Nasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana” (2Kor 5:8). Kwa kuwa kifo ni “mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa” (Mhu 12:7).
Siku ya ufufuo roho na mwili vitaungana tena kwa ajili ya uzima au moto wa milele.
“Kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida… ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo, maana ni vizuri zaidi sana” (Fil 1:21,23).
Mtume Petro ameandika hivi…
“18 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri; 20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji.” (1Petro 3:18-20)


Je, sisi wanyonge tunaweza kushiriki uzima wa milele wa Mungu?

Ndiyo, sisi wanyonge tunaweza kushiriki uzima wa milele wa Mungu: hapa duniani katika mwanga hafifu wa imani, na kisha kufa katika uangavu wa utukufu usiofifia kamwe. Kwa kuwa lengo la Baba ni kwamba tuungane na Yesu Mwanae kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ili tuwe na utukufu wake.
“Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma” (Yoh 17:3).
“Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa” (2Pet 1:3-4).
Sisi tuliobatizwa tunaitwa “wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo!” (1Yoh. 3:1).
Kwa sababu tumesadiki kwamba “Mungu ni upendo” (1Yoh 4:8) na kwamba “hakuna lisilowezekana kwa Bwana” (Lk 1:37).
“Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, ‘Aba!’ yaani, ‘Baba!’ Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu” (Gal 4:6-7).


Aliyezungumzia moto wa milele ni nani?

Aliyezungumzia moto wa milele ni hasa Yesu: akitufunulia ukuu wa upendo wa Mungu, aliye heri yetu pekee, alituangalisha juu ya hatari ya kutengana naye milele kwa dhambi. Mwenyewe atatoa hukumu hiyo:
“Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake” (Math 25:41).
“Humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki” (Mk 9:48).
“Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku” (Ufu 14:11).


Toharani maana yake nini?

Toharani maana yake kuna hali ya muda ambayo huruma ya Mungu inawatakasa marehemu waliofariki dunia katika urafiki naye lakini bila ya usafi kamili unaotakiwa kwa kuingia mbinguni. Sisi tunaweza kuharakisha utakaso wao kwa kumtolea Mungu sala na sadaka, hasa ekaristi. Yuda Mmakabayo “alichanga fedha kwa kila mtu jumla drakma elfu mbili, akazipeleka Yerusalemu kutoa sadaka ya dhambi.
Kwa kufanya hivi alitenda vema na kwa haki, kwa kuwa aliukumbuka ufufuo wa wafu. Maana kama asingalitumaini ya kuwa wale waliokufa watafufuka, ingalikuwa kazi bure isiyo na maana kuwaombea wafu. Lakini kwa kuwa aliufikiri utukufu wa thawabu waliowekewa wale wafao katika utauwa, wazo lake lilikuwa takatifu na la kicho. Ndiyo sababu alifanya upatanisho kwa wafu ili wafunguliwe dhambi zao” (2Mak 12:43-46). Imani hiyohiyo iliongoza Wakristo wa kwanza kuwafanyia marehemu ibada ambayo haieleweki vizuri, lakini hailaumiwi na Mtume Paulo: “Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao?” (1Kor 15:29).


Je, mwili utakaofufuliwa ni huuhuu tulionao sasa?

Ndiyo, mwili utakaofufuliwa ni huuhuu tulionao sasa, lakini katika hali tofauti: > “hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika” (1Kor 15:42).
Siku ya ufufuo “ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi” (Lk 21:27).
“Saa yaja ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuko wa uzima, na waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu” (Yoh 5:28-29).
“Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele” (Math 25:46).


Siku ya ufufuo Kristo mfalme atatuhukumu vipi?

Siku ya ufufuo Kristo mfalme atatuhukumu kwa kudhihirisha misimamo ya watu wote ambao, kwa kupokea au kukataa upendo wa Mungu moyoni mwao, wametenda mema au la.
“Imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyopenda, kwamba ni mema au mabaya” (2Kor 5:10).
“Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu” (1Kor 4:5).
“Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake. Na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto. Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, ‘Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika; nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia… Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi’” (Math 25:31-36,40).
“Heri wenye rehema, maana hao watapata rehema” (Math 5:7).


Baada ya hukumu ya mwisho itakuwaje?

Baada ya hukumu ya mwisho, waadilifu watatukuzwa mwili na roho pamoja na Yesu, na ulimwengu pia utageuzwa.
“Kama ilivyo ahadi yake, tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake” (2Pet 3:13).
“Na Roho na Bibi arusi wasema, ‘Njoo!’ naye asikiaye na aseme, ‘Njoo!’… Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, ‘Naam, naja upesi’. Amina. Na uje, Bwana Yesu! Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina” (Ufu 22:17,20-21).

Mambo ya Msingi kujua kuhusu Sakramenti ya Kitubio

Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu gani?
Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu alijua udhaifu wa binadamu hauishi mara anapopokea uzima wa Mungu kwa sakramenti tatu za kuingizwa katika Ukristo. Hivyo alipanga kusaidia mpaka mwisho wa dunia waamini wake watakaopatwa na dhambi na ugonjwa, kama alivyowasaidia wengi aliokutana nao katika maisha yake.
“Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, ‘Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako’… ‘Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi’ – amwambia yule mwenye kupooza – ‘Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako’. Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake. Makutano walipomwona, walishikwa na hofu, wakamtukuza Mungu, aliyewapa watu amri ya namna hii” (Math 9:2,6-8).

Mungu aliwapa watu (mapadri) amri/uwezo ya kusamehe dhambi kwa njia ya nani? Ni halali kuungama kwa padre?
Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi kwa njia ya Mwanae. Yesu mfufuka aliwaonyesha Mitume alama ya mateso mwilini mwake, “akawavuvia, akawaambia, ‘Pokeeni Roho Mtakatifu. Wowote mtakaowaondolea dhambi, wameondolewa; na wowote mtakaowafungia dhambi, wamefungiwa” (Yoh 20:22-23).
Katika Kanisa tunafurahi kupewa msamaha wa dhambi kila tunapohitaji, mradi tutubu. Kwa njia ya mwandamizi wa Mitume, Yesu anatuambia,
“Umesamehewa dhambi zako… Imani yako imekuokoa, enenda zako kwa amani” (Lk 7:48,50).
Si dhana wala hisia tu, bali ni neno la hakika tunalolipokea kwa masikio yetu.

Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi zipi?
Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi zote, kwa sababu upendo mtiifu wa Mwanae aliyejitoa kuwa sadaka ya wokovu wetu unampendeza kuliko dhambi zote zinavyomchukiza. Ila hatuwezi kusamehewa dhambi ya kukataa neema ambayo Roho Mtakatifu anatusukuma tuamini na kutubu, kwa sababu pasipo imani na toba hapana msamaha.
“Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa” (Math 12:31).
“Nasi tukitenda kazi pamoja naye twawasihi msiipokee neema ya Mungu bure” (2Kor 6:1).

Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi kwa sababu gani?
Mungu aliwapa watu amri ya kusamehe dhambi kwa sababu amependa washiriki katika kazi zake. Ametuumba kwa njia ya wazazi na kutulea na kutusaidia kwa njia ya wengine pia. Hasa ametuokoa kwa njia ya Yesu, ambaye yupo nasi sikuzote katika Mwili wake, yaani Kanisa, na katika wale walioshirikishwa mamlaka ya Mitume.
“Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho; yaani, Mungu alikuwa ndani ya Kristo, akiupatanisha ulimwengu na nafsi yake, asiwahesabie makosa yao; naye ametia ndani yetu neno la upatanisho. Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo, kana kwamba Mungu anasihi kwa vinywa vyetu; twawaomba ninyi kwa ajili ya Kristo: mpatanishwe na Mungu” (2Kor 5:18-20).

Je, tumuendee padri ili kuondolewa dhambi?
Ndiyo, tumuendee padri ili kuondolewa dhambi tulizotenda baada ya ubatizo, kwa kuwa hatuwezi kupokea msamaha tukikataa masharti yake, na Mungu ametupangia watu ambao watuondolee kwa niaba yake.
“Watu wote na watoza ushuru waliposikia hayo, waliikiri haki ya Mungu, kwa kuwa wamebatizwa kwa ubatizo wa Yohane. Lakini, Mafarisayo na wanasheria walilipinga shauri la Mungu juu yao, kwa kuwa hawakubatizwa naye” (Lk 7:29-30).
Yesu mwenyewe alikubali kubatizwa na Yohane ili atimize mpango wa Baba.
“Yohane alitaka kumzuia, akisema, ‘Mimi nahitaji kubatizwa na wewe, nawe waja kwangu?’ Yesu akajibu akamwambia, ‘Kubali hivi sasa; kwa kuwa ndivyo itupasavyo kuitimiza haki yote” (Math 3:14-15).
Je, sisi tukatae kumkimbilia padri wa Mungu ili kupokea huruma yake tunayoihitaji kuliko hewa?

Tumuungamie padri dhambi zetu kwa lengo gani? Kwa nini Wakatoliki wanaungama kwa padri?
Tumuungamie padri dhambi zetu ili aweze kutushauri na kuamua kama tuko tayari kuondolewa. Tumweleze kwa unyofu makosa yote tuliyoyafanya na nia tuliyonayo ya kuyafidia na kutoyarudia.
“Tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. Tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo, wala neno lake halimo mwetu” (1Yoh 1:8-10).
Tukumbuke tulivyo viungo vya Mwili mmoja, hivi kwamba dhambi zetu zimewadhuru wenzetu. “Ungameni dhambi zenu ninyi kwa ninyi na kuombeana, mpate kuponywa” (Yak 5:16).
Kutokuwa tayari kufanya hivyo walau sirini kwa padri ni dalili ya kiburi na ya kutotubu.

Je, padri akiwa mkosefu, anaweza kutuondolea dhambi?
Ndiyo, padri akiwa mkosefu, anaweza kutuondolea dhambi kwa niaba ya Mungu aliyempa mamlaka hiyo. Hatusamehewi na utakatifu wa padri, bali na huruma ya Baba kwa njia yake.
Yeye anamtumia padri yeyote ili kuturahisishia kazi, tusihitaji kuchunguza kwanza ubora wa maisha yake, wala kwenda mbali tukampate mmoja asiye na dhambi. Tungefanyeje kuhakikisha ni mtakatifu, wakati hatuwezi kusoma moyo wake? Ingekuwa hivi, tusingepata kamwe hakika ya kusamehewa. Kumbe inatutosha kujua ni padri, kwamba Mungu amempa mamlaka ya kusamehe dhambi, kama Yesu alivyowapa Mitume siku tatu baada ya kumkimbia na hata kumkana. Kila padri anaweza kukiri,
“Ni neno la kuaminiwa, tena lastahili kukubalika kabisa: ya kwamba Kristo Yesu alikuja ulimwenguni awaokoe wenye dhambi, ambao wa kwanza wao ni mimi” (1Tim 1:15).
Amri ya kusamehe dhambi wamepewa watu, si malaika.
“Tuna hazina hii katika vyombo vya udongo, ili adhama kuu ya uwezo iwe ya Mungu, wala si kutoka kwetu” (2Kor 4:7).

Je, nje ya kitubio tunaweza kuondolewa dhambi tuliyotenda baada ya ubatizo?
Ndiyo, nje ya kitubio tunaweza kuondolewa dhambi tuliyotenda baada ya ubatizo, lakini ni vigumu zaidi, kwa sababu hatupati msaada wa sakramenti hiyo maalumu.
Pamoja na nia ya kumuungamia padri mapema tunahitaji neema ya kutubu kikamilifu, si kwa kuhofia adhabu, bali kwa kumpenda Mungu tuliyemchukiza.
“Amesamehewa dhambi zake ambazo ni nyingi, kwa kuwa amependa sana” (Lk 7:47).

Sakramenti ya Kitubio ni nini?
Sakramenti ya Kitubio ndiyo Sakramenti ya kuwaondolea watu dhambi walizotenda baada ya Ubatizo (Yoh 20:22-23)

Lini na kwa maneno gani Yesu aliweka Sakramenti ya Kitubio?
Yesu aliweka Sakramenti ya Kitubio jioni ya ufufuko wake alipowapulizia mitume na kuwaambia maneno haya “Pokeeni Roho Mtakatifu. Wowote mtakaowaondolea dhambi watakua wameondolewa, wowote mtakaowafungia dhambi watakua wamefungiwa” (Yoh 20:22-23)

Mwenye kuwaondolea watu dhambi ni nani?
Mwenyezi Mungu pekee yake aweza kuwaondolea watu dhambi. Ndiye aliyewapa Mitume, Maaskofu na Mapadri uwezo wa kuwaondolea watu dhambi (Yoh 20:21-23)

Nani yampasa kupokea Sakramenti ya Kitubio?
Kila mkristo aliyetenda dhambi yampasa kupokea Sakramenti ya Kitubio

Mkristo akitaka kupokea Sakramenti ya Kitubio yampasa nini?
Mkristo akitaka kupokea Sakramenti ya Kitubio yampasa haya
1. Kutafuta dhambi moyoni (Yoh 3:20-21)
2. Kujuta dhambi
3. Kukusudia kuacha dhambi
4. Kuungama kwa padre
5. Kutimiza malipizi
6. Kumshukuru Mungu aliyemwondolea dhambi

Wakati wa Sakramenti ya Kitubio Utamwomba Roho Mtakatifu kwa sala gani?
Utamuomba Roho Mtakatifu kwa sala hii:
Uje Roho Mtakatifu unisaidie nitambue dhambi zangu, nijute sana, niungame vema, nipate kutubu kweli. Amina

Kutafuta dhambi maana yake ni nini?
Kutafuta dhambi maana yake ni kujiuliza moyoni dhambi nilizotenda Tangu ungamo la mwisho (Ef 4:17-32)

Utafuteje dhambi wakati wa kujiandaa kuungama?
Tafuta dhambi kwa njia hizi
1. Kwa kukumbuka uliyokosa kwa mawazo, kwa maneno na kwa vitendo
2. Katika Amri za Mungu na za Kanisa
3. Katika vichwa vya dhambi
4. Katika kutimiza wajibu

Kutubu dhambi maana yake ni nini?
Kutubu dhambi maana yake ni kuona uchungu na chuki moyoni juu ya dhambi tulizotenda na kukusudia kutotenda dhambi tena (Yoh 8:11)

Kwa nini tujute dhambi zetu?
Tunajuta dhambi zetu kwa sababu tumeukosea Utatu Mtakatifu na tunastahili adhabu yake, na pia bila majuto hatuwezi kupata maondoleo ya dhambi.

Kuna majuto ya namna ngapi?
una majuto ya namna mbili,
1. Majuto kamili/Majuto ya mapendo
2. Majuto yasiyokamili/majuto pungufu/majuto ya hofu

Majuto kamili ni nini?
Majuto kamili ni kujuta kwa sababu tumemchukiza Mungu mwenyewe aliye mwema na mpendelevu kabisa

Majuto yasiyo kamili au majuto pungufu ni nini?
Majuto yasiyokamili ni kujuta kwa sababu tumepoteza furaha za Mbinguni na tunahofia adhabu ya Mungu

Asiyejuta aweza kuondolewa dhambi?
Asiyejuta hawezi kuondolewa dhambi kabisa, na anayeungama bila kujuta anatenda dhambi kubwa ya kufuru.

Kabla ya kuungama ni lazima kufanya nini?
Kabla ya kuungama ni lazima kukusudia kuacha dhambi na kuepuka nafasi kubwa ya dhambi bila kusahau kufuata hatua sita za kabla na baada ya kupokea kupokea Sakramenti ya Kutubio ambazo ni,
(1) kuwaza/kutafuta dhambi moyoni,
(2)kutubu/ kujuta,
(3)kukusudia kuacha dhambi,
(4)kuungama kwa padri,
(5)kutimiza kitubio,
(6)kumshukuru Mungu

Anayetaka kweli kuacha dhambi afanye nini?
Anayetaka kuacha dhambi afanye nguvu kuvishinda vishawishi, asali/aombe na apokee Sakramenti Mara nyingi hasa Sakramenti ya Kitubio na Ekaristi Takatifu.

Kuungama ni kufanya nini?
Kuungama ni kumwambia Padri wazi wazi dhambi zako ulizotenda, zipi na ngapi ili upate maondoleo.

Anayeficha kusudi dhambi ya mauti katika ungamo anaondolewa?
Haondolewi, Bali anatenda dhambi kubwa ya kukufuru Sakramenti ya Kitubio. (Mt 7:21-23, Yoh 20:23, Gal 6:7)

Anayekufuru Sakramenti ya Kitubio yampasa nini?
Yampasa kuziungama tena dhambi zake zote alizotenda tangu ondoleo la mwisho

Padri anaondolea dhambi mahali pa nani?
Padri anaondolea dhambi mahali pa Mungu

Padri anaondolea dhambi kwa maneno gani?
Padre anaondolea dhambi kwa maneno haya: Nami “Nakuondolea dhambi zako zote kwa Jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu”.

Kitubio tuwezacho kupewa na padre ni nini?
Kitubio tuwezacho kupewa na Padre ni kama sala, kufunga, kutoa sadaka kwa maskini, kusoma maandiko matakatifu, kuwatazama wagonjwa, n.k.

Kitubio tupewacho na padre chatosha?
Ni shida kutosha. Mara nyingi chataka malipizi ya hapa duniani kama kufunga, magonjwa, masumbuko, sala n.k mateso yasipotosha hapa duniani yatakamilishwa toharani

Kutimiza malipizi maana yake ni ni nini?
Kutimiza malipizi maana yake ni kutekeleza kiaminifu sala au matendo aliyotuagiza padre muungamishi ili kulipa adhabu za muda. (Rom 8:17)

Kwa Sakramenti ya Kitubio tunapata neema zipi?
Kwa Sakramenti ya Kitubio tunapata neema hizi;
1. Maondoleo ya dhambi zote kubwa na adhabu ya milele
2. Maondoleo ya dhambi ndogo na adhabu nyingine za muda (Isa 6:5-7, Yoh 8:11)
3. Twarudishiwa na kuongezewa neema ya utakaso
4. Twasaidiwa kuepa dhambi na twapata nguvu ya kutenda mema
5. Twarudishiwa tena mastahili tuliyopoteza kwa dhambi zetu

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu matakwa ya Mungu na mapenzi ya binadamu?

Kanisa Katoliki linatambua kuwa Mungu aliumba ulimwengu na binadamu kwa mapenzi yake, lakini pia Mungu alitupa uhuru wa kuchagua. Ni wajibu wa binadamu kutimiza matakwa ya Mungu na kuishi maisha yanayoambatana na mapenzi yake.

Katika Waraka wa Yohane Paulo II, Fides et Ratio, Kanisa Katoliki linatilia mkazo kwamba binadamu ana jukumu la kutafuta ukweli na kuelewa mapenzi ya Mungu. Kupitia kwa imani na akili, binadamu anaweza kufikia maarifa ya ukweli huu.

Katika Maandiko Matakatifu, tunaona jinsi ambavyo Mungu anatutaka kufuata mapenzi yake. Mtume Paulo aliandika katika Waraka wa Waebrania 10:36, "Kwa hiyo, ninyi mnahitaji subira ili mtimize mapenzi ya Mungu na mpokee ahadi yake." Hii inamaanisha kuwa kwa kumtii Mungu na kufuata mapenzi yake, tunaweza kufikia ahadi zake.

Kanisa Katoliki linamfundisha mtu anapaswa kumtii Mungu na kusubiri mapenzi yake. Hii inamaanisha kuwa tunapaswa kufuata amri za Mungu na kuishi maisha yenye haki na kwa upendo. Katika KKK 2822, inasemekana, "Tunatafuta mapenzi ya Mungu katika maisha yote, hasa katika maamuzi yetu muhimu."

Katika Maandiko Matakatifu, tunajifunza kwamba Mungu anataka tufanye kazi yetu kwa bidii na kwa upendo. Paulo aliandika katika Waraka wa Wakolosai 3:23-24, "Kila mfanyalo, fanyeni kwa moyo wenu wote, kama kwa Bwana, si kwa ajili ya wanadamu, kwa maana mnajua ya kuwa mtapokea ujira wa mrithi kutoka kwa Bwana."

Kanisa Katoliki linatilia mkazo kwamba inatupasa kufanya kazi kwa heshima na kwa uaminifu, kwa kuwa kwa kufanya hivyo tunamfurahisha Mungu. Kanuni ya Maadili ya Kikatoliki inatufundisha kuwa tunapaswa kutoa kazi yetu kwa Mungu na kuifanya kwa uangalifu na upendo, ili kuonyesha upendo wetu kwa Mungu.

Kwa hiyo, Kanisa Katoliki linatambua kwamba tunapaswa kutimiza matakwa ya Mungu na kuishi maisha yanayoambatana na mapenzi yake. Tunapaswa kumtii Mungu, kufanya kazi yetu kwa bidii na kwa upendo, na kutafuta ukweli na maarifa ya mapenzi yake. Kwa kufanya hivyo, tunapata baraka za Mungu na kupokea ujira wake wa milele.

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili?

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili? Jibu ni ndio! Kanisa Katoliki linatamani sana waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili. Ni wito wa Mungu kwetu sote kuishi maisha matakatifu na kushuhudia Injili kwa wengine. Katika makala hii, tutaangalia jinsi Kanisa Katoliki linawahimiza waamini wake kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili.

Kanisa Katoliki linakumbusha waamini wake kuwa wao ni watu wa Mungu na wanapaswa kuishi maisha yao kama sehemu ya mpango wa Mungu. Maisha matakatifu ni maisha yenye utakatifu, upendo, na wema. Tunapaswa kuwa na nia njema kwa wengine, kujitolea, na kuishi katika haki na ukweli. Tumeitwa kuwa watakatifu, na Kanisa linatuhimiza kushiriki katika utakatifu wa Mungu. Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Waebrania 12:14, "Badilisheni maisha yenu, mpate kuwa watu watakatifu kama vile Mungu, Baba yenu, alivyo mtakatifu."

Kanisa Katoliki linatuhimiza pia kuwa mashuhuda wa Injili. Injili ni ujumbe wa upendo wa Mungu kwa wanadamu, na sisi kama waamini tunaitwa kuishuhudia kwa wengine. Tunapaswa kuonyesha upendo kwa wengine, kusamehe, na kuwa na huruma. Kanisa linatuhimiza kuwa wajumbe wa amani na upendo, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Mathayo 5:9, "Heri wenye amani, kwa sababu wao watapewa jina la wana wa Mungu."

Kanisa Katoliki linatukumbusha kuwa Utakatifu ni wito wa wote. Katika Catechism of the Catholic Church, inasema, "Utakatifu ni wito wa wote: "Hii ndiyo mapenzi ya Mungu, utakatifu wenu" (1 Thesalonians 4:3). Utakatifu unamaanisha kuwa mtu anakaribia Mungu na kuwa sehemu ya jamii ya waamini watakatifu. Utakatifu unafanana na mwanga wa Mungu unaowaongoza watu wote, na tunapaswa kuuweka mwanga huu ukiwaka ndani yetu na kuwaonyesha wengine.

Kanisa Katoliki linatumia sakramenti kama njia ya kutusaidia kuishi maisha matakatifu. Tunapopokea sakramenti ya Ekaristi Takatifu, tunakutana na Kristo mwenyewe na kuwa na nguvu ya kukuza upendo na utakatifu katika maisha yetu. Tunapopokea sakramenti ya Upatanisho, tunaweza kuungana tena na Mungu na wengine na kuwa na nia njema ya kubadilisha maisha yetu. Kanisa linatuhimiza kutumia sakramenti kama njia ya kukuza maisha yetu ya utakatifu.

Kanisa Katoliki linatukumbusha kuwa kujitolea ni sehemu muhimu ya kuishi maisha matakatifu. Tunapaswa kujitolea kwa wengine, hasa wale wanaohitaji msaada. Kama ilivyoandikwa katika kitabu cha 1 Yohana 3:18, "Watoto wangu, mapenzi yangu si kuzungumza tu kuhusu upendo, bali kuhusu kutenda." Tunapaswa kuwa wajenzi wa jamii ya upendo, kujitolea kwa wengine, na kuhakikisha kuwa wote wanafurahia maisha.

Kwa hiyo, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuishi maisha matakatifu na kuwa mashuhuda wa Injili. Tunapaswa kujitahidi kuwa na utakatifu, upendo, na wema. Tunapaswa kuishi kama watu wa Mungu na kushuhudia Injili kwa wengine. Tunapaswa kutumia sakramenti kama njia ya kukuza maisha yetu ya utakatifu. Na tunapaswa kujitolea kwa wengine na kuhakikisha kuwa wote wanafurahia maisha. Hivyo, tuishie kwa neno la Mtakatifu Paulo katika kitabu cha Wafilipi 4:13, "Ninaweza kufanya kila kitu kwa nguvu yake yeye anayenipa nguvu."

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu kuombea wafu?

Ni jambo la kawaida kwa Kanisa Katoliki kuombea wafu. Kuombea wafu ni sehemu ya imani yetu kama Wakatoliki. Tunaamini kuwa sala zetu zinaweza kuwasaidia wafu kufikia maisha ya milele kwa haraka. Katika mafundisho yetu ya kikristo, wafu ni sehemu ya familia ya Mungu. Kwa hiyo, ni wajibu wetu kuwaombea, kuwakumbuka na kuwatakia neema za Mungu kwa ajili ya wokovu wao.

Kuombea wafu ni muhimu sana kwa sababu wafu wanahitaji sala zetu kama tunavyohitaji sisi. Hatuwezi kuwa na uhakika kama wafu hao walikufa wakiwa katika amani na wokovu. Kwa kuwaombea, tunajitahidi kuwapatia nguvu za kiroho na kuwasaidia kuingia katika ufalme wa Mbinguni.

Kama Wakatoliki, tunaamini kuwa sala zetu na sadaka zetu zinaweza kuwasaidia wafu kupunguza maumivu ya mateso ya dhambi zao. Tunafahamu kuwa hakuna dhambi inayoweza kuzuia upendo wa Mungu kwa wafu. Kwa hiyo, tunajitahidi kuomba neema za Mungu kwa ajili ya wafu wetu ili waweze kupata maisha ya milele.

Katika Maandiko Matakatifu, tunaweza kuona jinsi sala za kuombea wafu zinavyotajwa mara kwa mara. Kwa mfano, katika Kitabu cha 2 Macabees 12:46 tunasoma, "Kwa hiyo akatoa sadaka kwa ajili ya wafu, ili wapate huruma ya msamaha wa dhambi zao." Katika Waraka wa Yakobo 5:16, tunahimizwa kuwaomba wengine watusali kwa ajili yetu, na kufunua haja za wengine kwa sala zetu.

Kwa kuombea wafu, sisi kama Wakatoliki tunazingatia mafundisho ya Kanisa. Kwa mfano, Katekisimu ya Kanisa Katoliki inatueleza kuwa sala zetu kwa ajili ya wafu zinaweza kuwasaidia kupata utakaso wa mwisho na kuwawezesha kuingia katika ufalme wa Mbinguni (KKK 1032). KKK pia inatueleza kuwa kuwaombea wafu ni sehemu ya huduma yetu kwa wengine, na ni ishara ya upendo wetu kwa wafu (KKK 958).

Kwa hiyo, kama Wakatoliki, tunaomba neema za Mungu kwa ajili ya wafu wetu, na tunaamini kuwa sala zetu zinaweza kuwafikia na kuwasaidia katika safari yao ya kuelekea kwa Mungu. Kuombea wafu ni sehemu ya imani yetu kama Wakatoliki, na tunashukuru kwa fursa ya kuziomba sala za kuwaokoa.

Maswali na Majibu kuhusu dhamira

Dhamiri adilifu ni nini?
Dhamiri adilifu, iliyo ndani kabisa mwa mtu, ni uamuzi wa akili ambao kwa wakati wake unamuagiza mtu atende mema na kukwepa maovu


Katika hukumu zake dhamira ifuate nini?
Katika hukumu zake dhamira ifuate daima Injili, Amri za Mungu na za Kanisa na wajibu zetu.


Twajenga na kutunza dhamira zetu namna gani?
Twajenga na kutunza dhamira zetu kwa;-
1. Kufuata sauti ya Roho Mtakatifu
2. Kuzingatia mafundisho ya dini
3. Kuzingatia mila na desturi njema tulizopata katika malezi.
4 Kufuata mifano na tabia njema ya wenzetu na ya Watakatifu


Hadhi ya nafsi ya mtu inadai nini kuhusu dhamiri adilifu?
Hadhi ya nafsi ya mtu inadai unyofu wa dhamiri adilifu, yaani upande wa akili na sheria ya Mungu


Dhamiri adilifu inaundwa namna gani iwe nyofu na ya kweli?
Dhamiri nyofu inayosema kweli inaundwa kwa;
1. Malezi
2. Upokeaji wa neno la Mungu
3. Upokeaji wa Mafundisho ya Kanisa
4. Sala
5. Utafiti wa dhamiri


Dhamiri adilifu inatengenezwa na kusaidiwa na nini?
Dhamiri adilifu inatengenezwa na vipaji vya Roho Mtakatifu na kusaidiwa na mashauri ya watu wenye busara.


Dhamiri inatakiwa kufuata daima masharti gani?
Dhamira inatakiwa kufuata daima masharti yafuatayo
1. Hairuhusiwi kutenda maovu kusudi yapatikane mema
2. Yoyote muyatakayo mtendewe na watu, ninyi watendeeni vivyo hivyo. (Mt 7:12)
3. Upendo hufuata daima nia na heshima kwa jirani na kwa dhamira yake

Maswali na Majibu kuhusu Hukumu ya Mwisho

Ufufuko wa wafu maana yake nini?
Ufufuko wa wafu maana yake mwisho wa dunia watu wote watafufuka na miili yao na kwenda nayo katika furaha ya milele au moto wa milele. (Ayu 19:25-26, Mt 22:30-32, Yh 28-29)


Baada ya kifo cha mtu nini hutokea?
Baada ya kifo roho yake inafika mbele ya Mungu kwa hukumu ya mtu binafsi.


Matokeo ya hukumu hiyo ni nini?
Matokeo ya Hukumu hiyo ni roho kwenda Mbinguni, Toharani au Motoni. (Mt 25:34-46)


Mbinguni ni mahali pa namna gani?
Mbinguni ni makao mema ya heri na furaha (2Kor 5:1, Ufu, 2:17).
Waendao mbinguni ni wale wanaokufa katika hali ya neema ya utakaso na urafiki na Mungu na waliotakaswa kikamilifu


Motoni ni nini?
Motoni ni makao mabaya kwa Shetani walaaniwa wakaapo mbali na Mungu wakiteswa milele. (Mt 25:41, Mik 9:42-43, 1Yoh 14:15)


Uzima wa milele ni nini?
Uzima wa milele ni maisha ya kukaa mbinguni na Mungu yasiyokua na mwisho.


Toharani ni mahali gani?
Toharani ni mahali pa mateso zinakosafishwa roho ambazo hazikutimiza kitubio vizuri baada ya kuungama dhambi. (1Kor 3:15, 1Pet 1:7).


Je, hatuwezi kupunguza mateso ya roho za marehemu waliokwenda toharani?
Ndiyo: twaweza kupunguza hata kuyamaliza kwa kuwasalia na kuwapatia rehema na hasa kwa kuadhimisha Misa kwa ajili yao. (2Mik 12:38-46)


Mambo makuu manne ya mwisho ni yapi?
Mambo hayo ni;
1. Kifo
2. Hukumu
3. Jehanamu (Motoni)
4. Paradiso. (Toharani/Mbinguni)


Je, ufufuko wa Yesu ni muhimu kwetu pia?
Ndiyo, ufufuko wa Yesu ni muhimu kwetu pia, kwa sababu kwa njia yake tu tunatiwa uzima: sasa rohoni kwa kuondolewa dhambi, na siku ya mwisho mwilini pia kwa kufufuliwa.
Mwenyewe alisema, “Mimi ndimi huo ufufuo, na uzima. Yeye aniaminiye mimi ajapokufa, atakuwa anaishi; naye kila aishiye na kuniamini hatakufa kabisa hata milele” (Yoh 11:25- 26).
“Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala. Maana kwa kuwa mauti ililetwa na mtu, kadhalika na kiyama ya wafu ililetwa na mtu” (1Kor 15:20-21).
“Alitolewa kwa ajili ya makosa yetu, na kufufuka ili tupate kuhesabiwa haki” (Rom 4:25).


Je, ni muhimu tujiandae kufa?
Ndiyo, ni muhimu tujiandae kufa wakati wowote na namna yoyote kwa kuishi kitakatifu sasa na kwa kujiombea neema tutakazohitaji saa ya kufa kwetu, tukijua tumewekewa “kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu” (Eb 9:27).
“Katika mambo yako yote uukumbuke mwisho wako, hivyo hutakosa kamwe hata hatima” (YbS 7:36).
“Hamjui yatakayokuwako kesho! Uzima wenu ni nini? Maana ninyi ni mvuke uonekanao kwa kitambo, kisha hutoweka” (Yak 4:14).
“Kesheni, mwombe, msije mkaingia majaribuni” (Math 26:41).


Je, ina thamani machoni pa Bwana mauti ya mtu aliyemcha?
Ndiyo, “ina thamani machoni pa Bwana mauti ya wacha Mungu wake” (Zab 116:15).
Hasa utiifu wa Yesu msalabani umegeuza laana ya kifo iwe baraka kwa waamini wake.
“Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. Naam, asema Roho, wapate kupumzika baada ya taabu zao; kwa kuwa matendo yao yafuatana nao” (Ufu 14:13).


Tutakapofariki dunia itatutokea nini?
Tutakapofariki dunia roho yetu isiyokufa, mbali na mwili unaooza, itapewa tuzo au adhabu tuliyostahili kwa maisha yetu. “Ikawa yule maskini alikufa, akachukuliwa na malaika mpaka kifuani kwa Ibrahimu. Yule tajiri naye akafa, akazikwa. Basi, kule kuzimu aliyainua macho yake, alipokuwa katika mateso, akamwona Ibrahimu kwa mbali, na Lazaro kifuani mwake” (Lk 16:22-23). “Kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida… ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo, maana ni vizuri zaidi sana” (Fil 1:21,23). “Nasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana” (2Kor 5:8). Kwa kuwa kifo ni “mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa” (Mhu 12:7). Siku ya ufufuo roho na mwili vitaungana tena kwa ajili ya uzima au moto wa milele. “Pumzi iliwaingia, wakaishi, wakasimama kwa miguu yao, jeshi kubwa mno” (Ez 37:10).
Je baada ya kufa ni hapo hapo roho inaenda motoni au mbinguni, Au ni mpaka Siku ya hukumu Yesu Atakaporudi?
Ni siku ile ile Roho ya mtu aliyekufa inaenda Mbinguni, toharani au Motoni. Yesu alimwahidi yule mtu waliyesulubiwa pamoja kuwa watakuwa peponi pamoja siku hiyo hiyo na sio siku ya hukumu.
“Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.” 43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.” (Luka 23:42-43)
Sauli aliweza kuongea na Samweli hata baada ya kufa na Samweli alimbashiria mambo yatakayotokea kwa Sauli maanake ni kwamba Japokuwa alikuwa amekufa bado anayomuungano na Mungu ndio maana aliweza kumwambia Sauli mambo yatakayompata,
“7Basi Sauli akawaambia watumishi wake, “Nitafutieni mwanamke mwenye pepo wa utambuzi ili nimwendee nipate kuuliza kwake. Watumishi wake wakamwambia, “Yuko mwanamke mmoja huko Endori.” 8Hivyo Sauli akajigeuza kwa kuvaa mavazi mengine, naye usiku akiwa amefuatana na watu wawili wakaenda kwa huyo mwanamke. Akamwambia, “Nibashirie na unipandishie huyo nitakayekutajia,” 9Huyo mwanamke akamwambia, “Wewe unajua lile alilofanya mfalme Sauli. Amewakatilia mbali wapunga pepo, wapiga ramli wote na wachawi katika nchi. Mbona umenitegea maisha yangu ili wapate kuniua?” 10Sauli akamwapia huyo mwananmke kwa Jina la BWANA, akasema, “Kwa hakika kama BWANA aishivyo, hutaadhibiwa kwa ajili ya jambo hili.” 11Ndipo yule mwanamke akauliza, “Je unataka nikupandishie nani? Sauli akasema, “Nipandishie Samweli.” 12Yule mwanamke alipomwona Samweli alipiga yowe kwa sauti kuu, naye akamwuliza Sauli, “Mbona umenidanganya? Wewe ndiwe Sauli.” 13Mfalme akamwambia, “Usiogope. Unaona nini? Yule mwanamke akasema, “Naona Mungu anapanda kutoka ardhini.” 14Sauli akamwuliza, “Ni mfano wa nini?” Yule mwanamke akasema, “Ni mwanaume mzee amevaa joho anayepanda.” Ndipo Sauli akatambua kwamba ni Samweli. Sauli akasujudu kifudifudi uso wake hadi ardhini. 15Samweli akamwuliza Sauli, Kwa nini unanitaabisha, kunipandisha juu?” Sauli akasema, “Mimi ninasumbuka sana, kwa maana Wafilisti wanapigana vita dhidi yangu, naye Mungu ameniacha. Hanijibu tena wala kwa njia ya manabii wala kwa ndoto. Kwa hiyo nimekuita wewe ili unijulishe lakufanya.” 16Samweli akamwuliza, “Kwa nini uniulize mimi, maadam BWANA amekuacha na kuwa adui yako? 17BWANA ametenda lile alilotangulia kusema kwa kupitia kwangu. BWANA ameurarua ufalme kutoka mikononi mwako, naye amempa mmoja wa jirani zako, yaani, Daudi. 18Kwa sababu wewe hukumtii BWANA, wala hukumtimizia ghadhabu yake kali juu ya Waamaleki, BWANA amekutendea mambo haya leo. 19Zaidi ya hayo, BWANA atawatia Israeli pamoja na wewe mkononi mwa Wafilisti na kesho wewe na wanao mtakuwa pamoja nami. BWANA pia atalitia jeshi la Israeli mkononi mwa Wafilisti.
Mfano Wa Tajiri Na Maskini Lazaro Yesu alisimulia hivi
19 Akasema, “Palikuwa na tajiri mmoja aliyevaa nguo za rangi ya zambarau na kitani safi, nguo za gharama kubwa, kila siku. 20 Na maskini mmoja, jina lake Lazaro, mwenye vidonda mwili mzima, alikuwa akiletwa mlangoni kwa huyo tajiri kila siku. 21 Lazaro alikuwa akitamani kula makombo yaliyodondoka mezani kwa tajiri. Hata mbwa walikuwa wakiramba vidonda vyake. 22 “Hatimaye, yule maskini alikufa. Malaika wakamchukua akakae pamoja na Ibrahimu mbinguni. Yule tajiri naye pia akafa, akazikwa. 23 Alipokuwa kuzimuni ambapo alikuwa akiteseka, alita zama juu, akamwona Ibrahimu kwa mbali na Lazaro karibu yake. 24 Akaita, ‘Baba Ibrahimu, nionee huruma umtume Lazaro achovye japo ncha ya kidole chake katika maji aupoze ulimi wangu maana ninateseka kwenye moto huu.’ 25 Lakini Ibrahimu akamjibu, ‘Mwa nangu, kumbuka kwamba ulipokuwa hai ulipata kila kitu kizuri uli chotaka, ambapo Lazaro alipokea mabaya. Lakini sasa anafarijika hapa na wewe unateseka. 26 Isitoshe, kati yetu na ninyi huko, kumewekwa bonde kubwa lisilopitika ili wale wanaotaka kutoka huku kuja huko au kutoka huko kuja huku wasiweze.’ 27 Akasema, ‘Basi, baba, tafadhali umtume Lazaro aende nyumbani kwa baba yangu, 28 awaonye ndugu zangu, wasije wao pia wakaletwa mahali hapa pa mateso watakapokufa.’ 29 Ibrahimu akamjibu, ‘Ndugu zako wanazo sheria za Musa na maandiko ya Manabii. Itawapasa watii hayo.’ Lakini yule tajiri akazidi kumsihi, 30 ‘Hapana baba Ibrahimu, ndugu zangu hawatashawishiwa na hayo. Lakini mtu kutoka kuzimu akitumwa kwao watatubu na kuziacha dhambi zao.’ 31 “Ibrahimu akamwambia, ‘Wasiposikiliza na kutii sheria za Musa na Maandiko ya manabii, hawatashawishika kutubu hata kama mtu akifufuka kutoka kuzimu.”’ (Luka 16:19-31)
Wakati Yesu anabadilika Sura walitokea Musa na Eliya.
“Baada ya siku sita, Yesu aliwachukua Petro, Yakobo na Yohane nduguye, akaenda nao peke yao juu ya mlima mrefu. 2 Huko, wakiwa wanamtazama, akageuka sura, uso wake ukang’aa kama jua na mavazi yake yakawa meupe kama nuru. 3 Mose na Eliya wakawatokea, wakawa wanazungumza naye. 4 Hapo Petro akamwambia Yesu, “Bwana, ni vizuri sana kwamba tupo hapa! Ukipenda nitajenga vibanda vitatu: kimoja chako, kimoja cha Mose na kimoja cha Eliya.” (Mathayo 17:1-5)
Yesu alituambia kuwa Mungu sio wa wafu bali wa walio hai ndio maana akaitwa Mungu wa Ibrahimu, Isaka na Yakobo kwa kuwa Wote wako hai kwake.
37Hata Mose alidhihirisha kuwa wafu wanafufuka, kwa habari ya kile kichaka kilichokuwa kikiwaka moto bila keteketea, alipomwita Bwana ‘Mungu wa Abrahamu, Mungu wa Isaki na Mungu wa Yakobo.’ 38Yeye Mungu si Mungu wa wafu bali wa walio hai, kwa kuwa Kwake wote ni hai.” (Luka 20:37-38)
Yesu alimwahidi yule mtu waliyesulubiwa pamoja kuwa watakuwa peponi pamoja siku hiyo hiyo na sio siku ya hukumu.
“Kisha akasema, “Ee Yesu! Unikumbuke wakati utakapoingia katika ufalme wako.” 43 Yesu akamwambia, “Nakwambia kwa hakika, leo utakuwa pamoja nami peponi.” (Luka 23:42-43)
Angalia pia wakati Stefano akipigwa Mawe aliikabidhi roho yake kwa Mungu baada ya kuona mbingu zimefunguka hii ni kama Yesu alivyokuwa pale msalabani aliikabidhi Roho yake kwa Baba yake.
55Lakini yeye Stefano akiwa amejazwa Roho Mtakatifu, alikaza macho mbinguni, akaona utukufu wa Mungu, naye Yesu akiwa amesimama mkono wa kuume wa Mungu. 56Akasema, “Tazameni! Naona mbingu zimefunguka na Mwana wa Adamu amesimama upande wa kuume wa Mungu.’’ 57Lakini wao wakapiga kelele kwa sauti kubwa, wakaziba masikio yao, wakamrukia kwa nia moja. 58Wakamtupa nje ya mji, wakampiga kwa mawe. Nao mashahidi wakaweka nguo zao miguuni mwa kijana mmoja aitwae Sauli. 59Walipokuwa wakimpiga mawe, Stefano aliomba, “Bwana Yesu, pokea roho yangu” 60Kisha akapiga magoti, akalia kwa sauti kubwa akasema, “Bwana usiwahesabie dhambi hii.’’ Baada ya kusema haya, akalala. (Mdo 7:55-60)
Kwenye Ufunuo tunasoma (Ufunuo 6:9-10) “Na alipoifungua muhuri ya tano, nikaona chini ya madhabahu roho zao waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu, na kwa ajili ya ushuhuda waliokuwa nao. Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, Ee Mola, Mtakatifu, Mwenye kweli, hata lini kutokuhukumu, wala kuipatia haki damu yetu kwa hao wakaao juu ya nchi? Nao wakapewa kila mmoja nguo ndefu, nyeupe, wakaambiwa wastarehe bado muda mchache, hata itakapotimia hesabu ya wajoli wao na ndugu zao, watakaouawa vile vile kama wao.”
Kwa hiyo mtu akifa anaenda mbinguni au motoni kulingana na alivyoishi.
“Nasi tunaona ni afadhali kutokuwamo katika mwili na kukaa pamoja na Bwana” (2Kor 5:8). Kwa kuwa kifo ni “mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa” (Mhu 12:7).
Siku ya ufufuo roho na mwili vitaungana tena kwa ajili ya uzima au moto wa milele.
“Kwangu mimi kuishi ni Kristo, na kufa ni faida… ninatamani kwenda zangu nikae na Kristo, maana ni vizuri zaidi sana” (Fil 1:21,23).
Mtume Petro ameandika hivi…
“18 Kwa maana Kristo naye aliteswa mara moja kwa ajili ya dhambi, mwenye haki kwa ajili yao wasio haki, ili atulete kwa Mungu; mwili wake akauawa, bali roho yake akahuishwa,19 ambayo kwa hiyo aliwaendea roho waliokaa kifungoni, akawahubiri; 20 watu wasiotii hapo zamani, uvumilivu wa Mungu ulipokuwa ukingoja, siku za Nuhu, safina ilipokuwa ikitengenezwa; ambamo ndani yake wachache, yaani, watu wanane, waliokoka kwa maji.” (1Petro 3:18-20)


Je, sisi wanyonge tunaweza kushiriki uzima wa milele wa Mungu?
Ndiyo, sisi wanyonge tunaweza kushiriki uzima wa milele wa Mungu: hapa duniani katika mwanga hafifu wa imani, na kisha kufa katika uangavu wa utukufu usiofifia kamwe. Kwa kuwa lengo la Baba ni kwamba tuungane na Yesu Mwanae kwa uwezo wa Roho Mtakatifu ili tuwe na utukufu wake.
“Na uzima wa milele ndio huu, Wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma” (Yoh 17:3).
“Kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa, kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe. Tena kwa hayo ametukirimia ahadi kubwa mno, za thamani, ili kwamba kwa hizo mpate kuwa washirika wa tabia ya Uungu, mkiokolewa na uharibifu uliomo duniani kwa sababu ya tamaa” (2Pet 1:3-4).
Sisi tuliobatizwa tunaitwa “wana wa Mungu; na ndivyo tulivyo!” (1Yoh. 3:1).
Kwa sababu tumesadiki kwamba “Mungu ni upendo” (1Yoh 4:8) na kwamba “hakuna lisilowezekana kwa Bwana” (Lk 1:37).
“Na kwa kuwa ninyi mmekuwa wana, Mungu alimtuma Roho wa Mwanawe mioyoni mwetu, aliaye, ‘Aba!’ yaani, ‘Baba!’ Kama ni hivyo, wewe si mtumwa tena bali u mwana; na kama u mwana, basi, u mrithi kwa Mungu” (Gal 4:6-7).


Aliyezungumzia moto wa milele ni nani?
Aliyezungumzia moto wa milele ni hasa Yesu: akitufunulia ukuu wa upendo wa Mungu, aliye heri yetu pekee, alituangalisha juu ya hatari ya kutengana naye milele kwa dhambi. Mwenyewe atatoa hukumu hiyo:
“Ondokeni kwangu, mliolaaniwa, mwende katika moto wa milele, aliowekewa tayari Ibilisi na malaika zake” (Math 25:41).
“Humo funza wao hafi, wala moto hauzimiki” (Mk 9:48).
“Na moshi wa maumivu yao hupanda juu hata milele na milele, wala hawana raha mchana wala usiku” (Ufu 14:11).


Toharani maana yake nini?
Toharani maana yake kuna hali ya muda ambayo huruma ya Mungu inawatakasa marehemu waliofariki dunia katika urafiki naye lakini bila ya usafi kamili unaotakiwa kwa kuingia mbinguni. Sisi tunaweza kuharakisha utakaso wao kwa kumtolea Mungu sala na sadaka, hasa ekaristi. Yuda Mmakabayo “alichanga fedha kwa kila mtu jumla drakma elfu mbili, akazipeleka Yerusalemu kutoa sadaka ya dhambi.
Kwa kufanya hivi alitenda vema na kwa haki, kwa kuwa aliukumbuka ufufuo wa wafu. Maana kama asingalitumaini ya kuwa wale waliokufa watafufuka, ingalikuwa kazi bure isiyo na maana kuwaombea wafu. Lakini kwa kuwa aliufikiri utukufu wa thawabu waliowekewa wale wafao katika utauwa, wazo lake lilikuwa takatifu na la kicho. Ndiyo sababu alifanya upatanisho kwa wafu ili wafunguliwe dhambi zao” (2Mak 12:43-46). Imani hiyohiyo iliongoza Wakristo wa kwanza kuwafanyia marehemu ibada ambayo haieleweki vizuri, lakini hailaumiwi na Mtume Paulo: “Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao?” (1Kor 15:29).


Je, mwili utakaofufuliwa ni huuhuu tulionao sasa?
Ndiyo, mwili utakaofufuliwa ni huuhuu tulionao sasa, lakini katika hali tofauti: > “hupandwa katika uharibifu; hufufuliwa katika kutokuharibika” (1Kor 15:42).
Siku ya ufufuo “ndipo watakapomwona Mwana wa Adamu akija katika wingu pamoja na nguvu na utukufu mwingi” (Lk 21:27).
“Saa yaja ambayo watu wote waliomo makaburini wataisikia sauti yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuko wa uzima, na waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu” (Yoh 5:28-29).
“Na hao watakwenda zao kuingia katika adhabu ya milele; bali wenye haki watakwenda katika uzima wa milele” (Math 25:46).


Siku ya ufufuo Kristo mfalme atatuhukumu vipi?
Siku ya ufufuo Kristo mfalme atatuhukumu kwa kudhihirisha misimamo ya watu wote ambao, kwa kupokea au kukataa upendo wa Mungu moyoni mwao, wametenda mema au la.
“Imetupasa sisi sote kudhihirishwa mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo ili kila mtu apokee ijara ya mambo aliyotenda kwa mwili, kadiri alivyopenda, kwamba ni mema au mabaya” (2Kor 5:10).
“Basi ninyi msihukumu neno kabla ya wakati wake, hata ajapo Bwana; ambaye atayamulikisha yaliyositirika ya giza, na kuyadhihirisha mashauri ya mioyo; ndipo kila mtu atakapoipata sifa yake kwa Mungu” (1Kor 4:5).
“Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu wake, na malaika watakatifu wote pamoja naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu wake. Na mataifa yote watakusanyika mbele zake; naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; atawaweka kondoo mkono wake wa kuume, na mbuzi mkono wake wa kushoto. Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono wake wa kuume, ‘Njoni, mliobarikiwa na Baba yangu, urithini ufalme mliowekewa tayari tangu kuumbwa ulimwengu; kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika; nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia… Amin, nawaambia, kadiri mlivyomtendea mmojawapo wa hao ndugu zangu walio wadogo, mlinitendea mimi’” (Math 25:31-36,40).
“Heri wenye rehema, maana hao watapata rehema” (Math 5:7).


Baada ya hukumu ya mwisho itakuwaje?
Baada ya hukumu ya mwisho, waadilifu watatukuzwa mwili na roho pamoja na Yesu, na ulimwengu pia utageuzwa.
“Kama ilivyo ahadi yake, tunatazamia mbingu mpya na nchi mpya, ambayo haki yakaa ndani yake” (2Pet 3:13).
“Na Roho na Bibi arusi wasema, ‘Njoo!’ naye asikiaye na aseme, ‘Njoo!’… Yeye mwenye kuyashuhudia haya asema, ‘Naam, naja upesi’. Amina. Na uje, Bwana Yesu! Neema ya Bwana Yesu na iwe pamoja nanyi nyote. Amina” (Ufu 22:17,20-21).

Je, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo?

Je, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo? Ndio, Kanisa Katoliki linakiri na kufundisha amri kumi za Mungu kama mwongozo wa maisha ya Kikristo. Amri hizi ni kanuni za msingi za maisha ya Kikristo na zinapaswa kufuatwa na Wakristo wote. Kwa kufuata amri hizi, Wakristo wanaweza kuishi maisha yao kwa kufuata mapenzi ya Mungu.

Katika Agano la Kale, Mungu alitoa amri kumi za kufuata kwa watu wake. Amri hizi zilikuwa na lengo la kuwafundisha watu wake jinsi ya kuishi maisha yao kwa kumtii Mungu. Amri hizi zilikuwa ni mwongozo wa maisha ya Kikristo na zinabaki kuwa ndivyo hadi leo.

Katoliki inafundisha kuwa amri kumi za Mungu ni za msingi na zinapaswa kufuatwa na Wakristo wote. Kufuata amri hizi kunamaanisha kuwa tunamheshimu Mungu, tunawaheshimu wazazi wetu, tunawapenda jirani zetu kama sisi wenyewe, tunaheshimu maisha ya wengine, tunawaheshimu washirika wetu wa maisha, tunazungumza kwa ukweli, tunawaombea wengine, tunachukia uovu, tunathamini vitu vya wengine, na hatutamani vitu vya wengine.

Kufuata amri hizi kunaleta baraka za Mungu katika maisha yetu na inatuwezesha kuishi maisha yenye furaha na amani. Kupitia Biblia, tunajifunza kuwa kufuata amri hizi ni muhimu sana kwetu kuishi maisha ya Kikristo.

Kanisa Katoliki linafundisha kuwa amri kumi za Mungu ni sehemu muhimu ya Maandiko Matakatifu. Kwa mfano, katika Kitabu cha Kutoka 20: 1-17, Mungu anatoa amri kumi za kufuata. Katika Kitabu cha Kumbukumbu la Torati 5: 6-21, amri kumi za Mungu zinarejelewa tena. Pia, katika Agano Jipya, Yesu Kristo anasisitiza umuhimu wa kufuata amri hizi.

Kanisa Katoliki linasisitiza umuhimu wa kufuata amri hizi kwa sababu zinaonyesha upendo wetu kwa Mungu na kwa jirani zetu. Wakati tunafuata amri hizi, tunatii mapenzi ya Mungu na tunaheshimu wengine kama sisi wenyewe. Kufuata amri hizi ni muhimu sana katika kujenga jamii ya Wakristo ambayo ina upendo, furaha, na amani.

Kwa ufupi, kufuata amri kumi za Mungu ni muhimu sana katika maisha yetu ya Kikristo. Amri hizi ni mwongozo wa maisha yetu na zinapaswa kufuatwa kwa umakini. Kufuata amri hizi kunatuletea baraka za Mungu na inatuwezesha kuishi maisha yenye furaha na amani. Kama Wakatoliki, tunapaswa kuwa na hamu ya kufuata amri hizi na kuishi maisha ya kujitolea kwa Mungu na kwa wengine. Kama inavyoelezwa katika Catechism of the Catholic Church, amri kumi za Mungu ni "misingi ya maadili ya Kikristo, kwa sababu zinakumbusha wajibu wa upendo wa Mungu na jirani."

Je, Kanisa Katoliki linatetea na kufundisha maadili ya kijinsia na thamani ya ndoa kati ya mwanaume na mwanamke?

Katoliki ni dini inayoheshimu na kufundisha thamani ya maisha ya binadamu. Kanisa Katoliki linafundisha maadili ya kijinsia na thamani ya ndoa kati ya mwanaume na mwanamke. Katika maudhui haya, tunaweza kuelewa jinsi Kanisa Katoliki linavyolinda na kufundisha thamani ya kijinsia na ndoa.

Kanisa Katoliki linatetea maadili ya kijinsia kwa sababu binadamu aliumbwa kwa mfano wa Mungu na anastahili kuheshimiwa. Maadili ya kijinsia yanahusu uhusiano kati ya mwanaume na mwanamke. Kwa maana hiyo, Kanisa linafundisha kwamba ngono ni kitendo kitakatifu na kinapaswa kufanywa ndani ya ndoa tu.

Ndoa ni sakramenti na ina thamani kubwa katika Kanisa Katoliki. Inapasa ichukuliwe kama ndoa ya kiroho, kati ya mwanaume na mwanamke, na haihusishi mtu mwingine yoyote katika uhusiano huo. Kama ilivyoelezwa katika Kitabu cha Mwanzo, mwanaume na mwanamke waliunganishwa na Mungu wakati walipoumbwa. Ndoa inaunganisha mwanamume na mwanamke katika upendo wa Mungu.

Neno la Mungu linaelezea wazi na kwa undani jinsi Kanisa Katoliki linavyofundisha maadili ya kijinsia na thamani ya ndoa. Kwa mfano, katika Mathayo 19:5 inasema, "Kwa sababu hiyo, mwanamume ataacha baba yake na mama yake, ataambatana na mkewe; na hao wawili watakuwa mwili mmoja." Hii inaonyesha kwamba ndoa ni kati ya mwanaume na mwanamke na hawapaswi kutengana.

Kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, ndoa inapaswa kuwa na upendo wa dhati kati ya wawili na inapaswa kuheshimiwa. Kwa mfano, ndoa inapaswa kutimiza mahitaji ya kiroho, kihisia na kijamii ya wanandoa. Ndoa inapaswa kuwa ya kitakatifu na inapaswa kutimiza matakwa ya Mungu.

Kwa ufupi, Kanisa Katoliki linatetea na kufundisha maadili ya kijinsia na thamani ya ndoa kati ya mwanaume na mwanamke. Ndoa inapaswa kuwa ya kitakatifu na kutimiza mahitaji ya kiroho, kihisia, na kijamii ya wanandoa. Ndoa ni sakramenti katika Kanisa Katoliki na linapaswa kuheshimiwa na kufanywa ndani ya ndoa, kulingana na neno la Mungu.

Mafundisho kuhusu Toharani

Toharani ni mahali gani?

Toharani ni mahali pa mateso zinakosafishwa roho ambazo hazikutimiza kitubio vizuri baada ya kuungama dhambi. (1Kor 3:15, 1Pet 1:7).

 


 

Je, hatuwezi kupunguza mateso ya roho za marehemu waliokwenda toharani?

Ndiyo: twaweza kupunguza hata kuyamaliza kwa kuwasalia na kuwapatia rehema na hasa kwa kuadhimisha Misa kwa ajili yao. (2Mik 12:38-46)

 


 

Toharani maana yake nini?

Toharani maana yake kuna hali ya muda ambayo huruma ya Mungu inawatakasa marehemu waliofariki dunia katika urafiki naye lakini bila ya usafi kamili unaotakiwa kwa kuingia mbinguni. Sisi tunaweza kuharakisha utakaso wao kwa kumtolea Mungu sala na sadaka, hasa ekaristi. Yuda Mmakabayo “alichanga fedha kwa kila mtu jumla drakma elfu mbili, akazipeleka Yerusalemu kutoa sadaka ya dhambi.
Kwa kufanya hivi alitenda vema na kwa haki, kwa kuwa aliukumbuka ufufuo wa wafu. Maana kama asingalitumaini ya kuwa wale waliokufa watafufuka, ingalikuwa kazi bure isiyo na maana kuwaombea wafu. Lakini kwa kuwa aliufikiri utukufu wa thawabu waliowekewa wale wafao katika utauwa, wazo lake lilikuwa takatifu na la kicho. Ndiyo sababu alifanya upatanisho kwa wafu ili wafunguliwe dhambi zao” (2Mak 12:43-46). Imani hiyohiyo iliongoza Wakristo wa kwanza kuwafanyia marehemu ibada ambayo haieleweki vizuri, lakini hailaumiwi na Mtume Paulo: “Kama wafu hawafufuliwi kamwe, kwa nini kubatizwa kwa ajili yao?” (1Kor 15:29).

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu ngono na maadili ya kijinsia?

Kanisa Katoliki ni moja ya madhehebu makubwa duniani, na imani yake juu ya ngono na maadili ya kijinsia ni muhimu sana. Kanisa hili linazingatia mafundisho ya Biblia na Catechism ya Kanisa Katoliki katika kuelezea maadili ya kijinsia na ngono.

Kwa mujibu wa Kanisa Katoliki, ngono ni kitendo kinachofanywa kati ya mwanamume na mwanamke, ambao wamefunga ndoa. Ni kitendo kitakatifu kinachopaswa kufanywa kwa upendo na kwa lengo la kuwaleta watoto duniani. Ni dhambi kufanya ngono kabla ya ndoa au kufanya ngono bila lengo la kuzaa watoto.

Kanisa Katoliki linasisitiza kuwa wanaume na wanawake wote ni sawa mbele ya Mungu na wanapaswa kutendewa kwa heshima na upendo. Uhusiano wa kimapenzi kati ya wanaume ama kati ya wanawake una kinyume na mafundisho ya Kanisa. Hata hivyo, Kanisa Katoliki linapenda na kuheshimu watu wote bila kujali kama wana tabia za kimapenzi ama la.

Kanisa Katoliki linasisitiza kuwa ngono inapaswa kutendeka kwa heshima na utu wa binadamu. Ni muhimu kufuata maadili ya kijinsia kwa kuepuka dhambi ya uzinzi, ngono haramu, na ukahaba. Kila mtu anapaswa kuishi maisha yenye maadili ya kijinsia, na kuhakikisha wanapata elimu ya kutosha juu ya maadili haya.

Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunasoma "Maadili ya kijinsia ni sehemu ya maadili ya kichungaji yanayohusiana na afya ya mtu na pia kuhusiana na maadili ya ndoa inayohusisha upendo wa kudumu kati ya mume na mke." (CCC 2351)

Kanisa Katoliki linasisitiza umuhimu wa kutumia njia za uzazi wa mpango ambazo hazimzuia Mungu kwa kuua mimba. Kanisa linapendekeza njia za uzazi wa mpango kama vile uzazi wa mpango wa asili, kufahamu kwa kina kuhusu mzunguko wa hedhi, na njia za uzazi wa mpango zinazorejesha udhibiti wa uzazi kwa mwanamke.

Kanisa Katoliki linakemea ngono kwa ajili ya kufurahisha nafsi ama kwa ajili ya ngono yenyewe, bila lengo la kuzaa watoto. Ngono inapaswa kuwa kwa lengo la kuunganisha mume na mke na kuwaleta watoto duniani kama zawadi kutoka kwa Mungu.

Hatimaye, Kanisa Katoliki linasisitiza umuhimu wa kuishi maisha ya utakatifu. Wanawake na wanaume wote wanapaswa kuishi maisha safi ya kijinsia, kufuata maadili ya kijinsia, kuheshimiana, na kuepuka kila aina ya dhambi. Kwa kufuata mafundisho ya Kanisa na kufuata Biblia na Catechism, tunaweza kuishi maisha yenye maadili ya kijinsia na mafanikio katika maisha.

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kufuata na kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yao?

Katika imani ya Kanisa Katoliki, Mungu ni muumba na mwanzilishi wa maisha yote duniani. Kama waamini, tunapaswa kufuata na kutekeleza mapenzi yake katika maisha yetu ya kila siku. Kufanya hivyo kutatusaidia kufikia lengo letu la mwisho, ambalo ni kufurahia uzima wa milele pamoja na Mungu.

Tunapofuata mapenzi ya Mungu, tunafuata miongozo ya kiroho ya Yesu Kristo ambaye ni mwombezi wetu mbele ya Mungu. Kupitia Yesu Kristo, tunaposamehewa dhambi zetu, tunapata uwezo wa kufanya yaliyo mema kwa ajili ya Mungu na jirani zetu. Katika Yohane 14:15 Yesu anasema, "Mkinipenda, mtazishika amri zangu." Kwa hiyo, kufuata mapenzi ya Mungu ni uthibitisho wa upendo wetu kwake.

Kanisa Katoliki linatuhimiza sana kufuata na kutekeleza mapenzi ya Mungu katika maisha yetu ya kila siku. Kwa kuwa Mungu ndiye muumba wetu, yeye anajua kile kilicho bora kwetu. Kupitia Neno lake, tunaweza kujua mapenzi yake. Kama tunavyosoma katika 2 Timotheo 3:16-17, "Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwafundisha haki; ili mtu wa Mungu awe kamili, amekamilishwa kabisa, kwa kila tendo jema."

Kanisa Katoliki linatupa mafundisho ya kiroho kupitia Catechism of the Catholic Church ambayo inaandaa waamini kufuata mapenzi ya Mungu. Wakati tunapata mafundisho haya, tunakuwa na mwongozo thabiti ambao unatuwezesha kufuata mapenzi ya Mungu na kutekeleza yale anayotaka kutoka kwetu. Kwa mfano, kifungu cha 2829 cha Catechism kinatufundisha kuomba kwa mamlaka ya jina la Yesu Kristo. Hivi ndivyo Yesu mwenyewe alivyofundisha wanafunzi wake kuomba. Tunapofuata mafundisho ya Kanisa, tunakaribia zaidi kwa Mungu.

Kufuata mapenzi ya Mungu katika maisha yetu ni muhimu sana. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kupata amani na furaha ya kweli ambayo inatokana na utimilifu wa maisha yetu. Kama tunavyosoma katika Warumi 12:2, "Wala msifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya akili zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu."

Kwa hiyo, tunapaswa kuwa wafuasi wa kweli wa Yesu Kristo, ambao unajumuisha kufuata mapenzi ya Mungu katika maisha yetu ya kila siku. Kama Kanisa Katoliki, tunatuhimiza kufanya hivyo kupitia mafundisho ya Catechism na Biblia. Kwa kufanya hivyo, tutakuwa tumejifunza kufuata na kutekeleza mapenzi ya Mungu, na mwisho tutafurahia uzima wa milele pamoja na yeye.

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa umoja na mshikamano kati ya Wakristo?

Je, Kanisa Katoliki linahubiri na kufundisha umuhimu wa umoja na mshikamano kati ya Wakristo? Jibu ni ndio! Kanisa Katoliki linahimiza Wakristo kuishi kwa upendo na kuwa na umoja katika Kristo. Hakuna mtu anayeweza kuishi peke yake na kufikia wokovu wa milele. Umoja na mshikamano ni muhimu sana ili kuendelea katika imani ya Kikristo.

Katika Waraka wa kwanza wa Mtume Paulo kwa Wakorintho 12:12-14, tunasoma kuwa "Kwa kuwa mwili mmoja ni wenye sehemu nyingi, na zile sehemu zote za mwili mmoja, ingawa ni nyingi, zinafanya mwili mmoja, vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana kwa Roho mmoja sisi sote tulibatizwa kuwa mwili mmoja, iwe Wayahudi au Wayunani, watumwa au huru, nasi sote tulinyweshwa Roho mmoja." Maneno haya yanatusaidia kuelewa kuwa sisi sote ni sehemu ya mwili mmoja wa Kristo na kwa hiyo tunapaswa kuishi pamoja kwa umoja na mshikamano.

Kanisa Katoliki limeeleza umuhimu wa umoja na mshikamano katika Mafundisho yake. Kwa mfano, Catechism of the Catholic Church inasema, "Makanisa yote yanayoheshimu Biblia kwa kweli na kwa unyenyekevu wanakutana pamoja katika Roho Mtakatifu ili kutafakari na kuomba na kufanya kazi kwa pamoja, na hivyo kuwaelekea kwa umoja wa kweli, ambao ni kielelezo cha Kanisa la Kristo" (838).

Kwa kweli, umoja na mshikamano ni muhimu sana katika imani ya Kikristo. Hatuwezi kufikia wokovu wa milele kama sisi ni sehemu ya mwili mmoja wa Kristo lakini tunahangaika kwa kujipiga vita kila wakati. Badala yake, tunapaswa kufanya kazi pamoja kwa ajili ya utukufu wa Mungu na kwa ajili ya wokovu wa wote.

Kwa hiyo, ni muhimu kwetu kama Wakristo kuhakikisha kwamba tunakuwa pamoja katika Kristo. Tunapaswa kuomba pamoja, kusoma Neno la Mungu pamoja, kushirikiana katika huduma, na kufanya kazi kwa pamoja ili kutambua malengo ya Kristo. Hatimaye, tunapaswa kuwa na mshikamano katika Kristo ili kutimiza utume wetu wa kuhubiri Injili na kuwa nuru ya ulimwengu.

Kwa kumalizia, Kanisa Katoliki linahimiza umoja na mshikamano kati ya Wakristo. Tukiishi kwa upendo na umoja, tutaweza kufikia lengo letu la kutafuta wokovu wa milele na tutakuwa nuru ya ulimwengu huu. Hebu tufanye kazi kwa pamoja na kuhakikisha tunakuwa na mshikamano katika Kristo!

Je, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini kuitunza na kuilinda mazingira kama zawadi kutoka kwa Mungu?

Katoliki ni dini kubwa duniani ambayo inaamini kuwa Mungu ndiye muumba wa ulimwengu na kila kitu kilichomo ndani yake. Kupitia mafundisho yake, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini wake kuitunza na kuilinda mazingira kama zawadi kutoka kwa Mungu.

Mazingira ni muhimu sana kwa binadamu na viumbe vingine. Kupitia mazingira, tunapata chakula na maji safi, hewa safi, na maisha yanayowezekana. Hivyo, Kanisa Katoliki linatambua umuhimu wa kutunza na kuilinda mazingira. Kwa mujibu wa Waraka wa Papa Francis wa 2015, "Laudato Si", Kanisa linawahimiza waamini wake kudumisha mazingira kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Kupitia Biblia, tunajifunza kuwa Mungu aliumba ulimwengu na kila kitu kilichomo ndani yake. Katika Kitabu cha Mwanzo 1:26-28 tunasoma kuwa Mungu alimuumba mwanadamu kwa mfano wake na akampa nguvu na mamlaka juu ya viumbe vyote. Hivyo, tunapaswa kutenda kwa hekima na upendo ili kupita ujumbe wa Mungu kwa kila kiumbe.

Kanisa Katoliki linatambua kuwa mazingira yanahitaji kulindwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya vizazi vijavyo. Kupitia Waraka wa Kitume wa Papa Francis wa 2015, "Laudato Si", Kanisa linawahimiza waamini wake kuzingatia kanuni za kiekolojia na kudumisha mazingira. Kwa mfano, tunapaswa kupunguza matumizi yetu ya rasilimali za asili kama vile maji, kuepuka uchafuzi wa hewa na maji, na kutunza viumbe hai kwa ajili ya maisha ya baadaye.

Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunajifunza kuwa binadamu ana wajibu wa kutunza na kuilinda mazingira. Kwa mujibu wa Catechism, "binadamu anatakiwa kutanguliza matumizi ya rasilimali za asili kwa njia ya busara na upendo kwa ajili ya wote, kwa wale ambao watafuata baada yetu." (Catechism ya Kanisa Katoliki, 2402). Kwa hiyo, kila mmoja wetu ana jukumu la kudumisha mazingira kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Katika hitimisho, Kanisa Katoliki linawahimiza waamini wake kuitunza na kuilinda mazingira kama zawadi kutoka kwa Mungu. Hii inatokana na imani yake kuwa Mungu ndiye muumba wa ulimwengu na kila kitu kilichomo ndani yake. Kupitia Biblia, tunajifunza umuhimu wa kulinda na kudumisha mazingira kwa ajili ya vizazi vijavyo. Na kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, binadamu ana wajibu wa kutunza na kuilinda mazingira kwa ajili ya wote. Kwa hiyo, ni jukumu letu sote kuhakikisha kuwa tunaitunza mazingira kwa ajili ya vizazi vijavyo.

Shopping Cart
1
    1
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About