Vituko Vya Kukuchangamsha

Kilichotokea baada ya kichaa kumfumania mke wake na mwanamme mwingine

Jay akaruhusiwa kwenda nyumbani kutoka hospital ya Vichaa, akapakiwa ktk ambulance hadi karibu na nyumbani kwake, akaulizwa unapakumbuka? akajibu ndio nyumba yangu ileee, mara wakatoka watoto wawili wamevaa uniform akasema watoto wangu walee wanakwenda shule.. akatoka mwanamke akasema na mke wangu yulee, ghafla akatoka mwanaume Jay akasema na mimi yule naenda kazini. hivi Jay kweli kapona?

Angalia huyu ticha wa Hesabu alichofanyiwa

Looku Looku* 👀👀

*Ama Kweli Mkuki Kwa Nguruwe kwa Binadamu Mchungu Skia Hii….!!*

*Ishawahi kutokea Pale nilipokutana njiani na mwalimu aliyekufundisha MATHS secondary afu akaniambia nimuelekeze njia ya kwenda sehemu fulani.*

*_Nenda mbele kama 2KM hivi kisha kata kushoto,ila hakikisha ANGLE inakuwa ni 30.5 KUSINI MASHARIKI.Kisha tumia PYTHAGORAS na hakikisha una FOUR FIGURE ili kupata thamani ya ANGLE._*

*Mwalimu alisonya na kuondoka.*😏😏😏😒😒

*Stakagi ujinga kabisa mimi, wakati ananichapa alifikiri sifa*😂😂

😅🙌🏽🙌🏽 *Mniache Tuu Mimi Sio Kwa Bifu Ilo Aiseee*🏃🏾

Soma hii, kama wewe ndio mzazi wa huyu msichana ungefanyaje?

Wewe ni mzazi mwanao anasoma kidato cha tatu mkoani umemsafirisha leo kwenda shule baada ya masaa matano ukasikia gari alilo panda mwanao limepata ajali wamekufa watu wote upo ktk harakati za kuandaa msiba,

mwanao anakupigia simu baba/mama mimi mzima sijafa mpenzi wangu ABDUL aliniambia nishuke Chalinze ili niwe nae kwa siku mbili alafu niende shule je, wewe mzazi unge mfanyaje mwanao?

Angalia mchezo wa kutuma message mara zikubali mara zikatae.. Lilishakukuta hili???

GARLFREND»»hellow sweetheart

BOYFREND»»hellow darling(SENDING FAILED)

GARLFREND»»kwanin hutaki kujibu sms yangu,au huna mda»??

BOYFREND»>najitahid kukujibu lakin mtandao unasumbua,imefika??(SENDING FAILED)

GARLFREND»»kama hunipend bhas usinijbu,kama unanipenda kwel bhas nijibu

BOYFREND»»i love you (SENDING FAILED)
GALFREND»»do you lov me????

BOYFREND»»i lov you baby(SENDING FAILED)

GARLFREND»»usiongee na mimi tenaaaaa

BOYFREND»»i love you sweetieeee(SENDING FAILED)

GARLFREND»»unataka mim na wew tuachaneee????

BOYFREND»»nshachoka mie na huu upUmbavu,shenz (MESSAGE SENT)

👆👆👆👆👆😄😄😄😄😄😄😄😄👆👆👆👆😄😄😄😄👆👆😄😄👆👆

Cheki hawa wachungaji

CHEKA KIDOGO

Wachungaji watatu walikutana kwa siri na kuelezana matatizo yao ili waweze kuombeana.

MCHUNGAJI WA KWANZA: mimi tatizo langu ni wizi, kila nikimaliza ibada lazima niibe pesa za sadaka.

WA PILI: Mimi tatizo langu ni wanawake yani nimeshalala na wana kwaya wote pamoja na mke wa ASKOF.

WA TATU akaanza kulia badala ya kuongea.WENZAKE:

We vp unatatizo gani mbona unalia???

AKAJIBU: jamani mimi tatizo langu ni “umbea” haya yote tuliyoongea lazima nikaseme!

😂😂😂😂😂👆🏻😂😂

Misemo 17 ya kuchekesha

1) gari la kuvutwa halina overtake
2) kisigino hakikakai mbele
3) wimbo wa taifa haupgwi disko
4) feni haiwashwi beach
5) mshkaki hauchomwi kwa jiko la ges
6) mganga haagiz tembele
7) hata bibi alikuwa bint
8) mke wa mtu sumu,mume wamtu maziwa
9) kipara bila pesa ni kovu
10) mbwa hanenepi migiuu
11) picha ya rais haina bodyguard
12) mjini shule kijiji tuition
13) saa ya ukutani haivaliwi mkonon
14) heshima pesa shkamoo makelele
15) ulinz pesa bastora mzgo
16) kuku ni kuku jogoo mbwembwe
17) kusoma kuelewa kukesha mbwembwe

Unakumbuka hizi enzi za utoto?

Kitambo tukiwa watoto ulikuwa unaitwa uje ule kwa lugha tofauti kulingana na chakula kilichopikwa siku na muda husika

1. UGALI NA KUNDE
Mwitaji : 🗣Joniiiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Uje ukule

2. UGALI NA SAMAKI
Mwitaji: 🗣 we Joniiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Unaitwa na Mama

3. WALI NA NYAMA/KUKU
Mwitaji: 🗣 Joniiii
Mwitikiaji : Eeeh
Mwitaji : Shauri yako!
😂😂😂😂😂😂

Hawa wanaume wanaopenda wanawake hovyo barabarani wamepatikana, hawatarudia 😂😂😂

Marafiki wawili (Jose na Ben) walikuwa wanatembea mtaani akatokea mwanamke akarusha busu kwa mmojawapo kupitia dirishani katika jengo la ghorofa tatu.

Wakaanza kujadiliana kama ifuatavyo:

Ben: Muone yule mrembo amenirushia busu

Jose: tafadhali achana na huyo mwanamke, usimjali..

(baadae yule mwanamke akamuashiria aende)

Ben: yule mwanamke ameniita!

Jose: Rafiki yangu, usiende. Nakutafadhalisha.

Ben: Kwa nini unaniambia nisiende Wakati mrembo kama yule ananiita? Huo ni wivu

Jose: Ben, Ninakutafadhalisha tena, usiende, tafadhali usiende kule (akihisi kutotiliwa maanani)

(Rafiki yake alimpuuza na alienda kwa yule mwanamke, mwanamke alishuka kukutana naye na wakapanda juu. Ghafla wakiwa wanataka kuanza taratibu za kula uroda, wakasikia mlio WA gari getini).. 🔊🔊

Lady: _(akiangalia kupitia dirishani)_
Oooh! Yule ni mume wangu!!

Ben: Mama yangu !
Nipo matatani, kweli ? ..!!

Lady: Usiwe na khofu, jifanye kuwa Dobi na anza kupiga pasi hizo nguo

(akimuonyesha lundo la nguo)

(Ben alitumia masaa matano kukamilisha kunyoosha zile nguo kwa sababu yule mume hakutoka tena siku ile)

(Siku iliyofuatia Ben alikwenda kwa Rafiki yake)

Ben: Kaka, unaweza kuamini Jana nimepiga pasi nguo kwa masaa matano???

Jose: Lakini nilikwambia usiende. Nguo zote hizo ulizonyoosha, Nilizifua Mimi Juzi!!
😂😂😂😂😂😂😂😂😂

When an experienced person speaks … 👂you must listen..!

Ulevi noma! Angalia huyu mlevi alichomfanyia huyu jamaa usiku! Ungekua wewe ungefanyaje?

Jamaa alikuwa amelaa na mkewe saa tisa ya usiku akastuka baada ya kusikia mtu anabisha hodi kwenda kufungua mlango
Akamkuta jamaa kalewa sana mlangoni kwao
JAMAA: Nini tena mheshimiwa kuamshana saa hizi?
MLEVI: Naomba uje unisukume.
Jamaa akiamini kuwa pengine kuna gari la huyu mlevi limezima jirani akamwambia subiri nikavae viatu. Baada ya kuvaa viatu akatoka na wakaanza kusindikizana na mlevi. Mlevi akaongoza njia
mpaka kwenye mabembea ya jirani akakaa kwenye bembea moja na kumgeukia jamaa na kumwambia.. Okay nisukume basi.

Mambao ya saluni ni shida, cheki kilichotokea kwa huyu

DADA alienda Salon wakati anasukwa akaingia
MKAKA mtanashati,
DADA akaamua kujaribu bahati yake.
DADA:Mambo? KAKA:Poa.
DADA:Mimi na wewe tunaweza kuongea baade?
KAKA:Kuhusu nini?
DADA:Nimekupenda nataka nikutoe out.
KAKA:Sawa ila nitamwambia nini
MKE wangu?
DADA:Aah ilo sio tatizo mdanganye tu,mwambie unakwenda kumtembelea rafiki yako hospitalini.
KAKA:Mwambie mwenyewe huyo hapo anayekusuka.

 

Unajua nn kiliendelea?

Angalia kilichojiri katika semina ya wanandoa kuhusu upendo

Kulikuwa na semina ya wanawake kuhusu namna ya kuishi kwa upendo katika ndoa.
Mwalimu aliwauliza ni wangapi wanawapenda waume zao? Wote wakanyoosha mikono kama ishara ya kuwa wanawapenda waume zao.
Mwalimu akauliza tena, “Ni lini mara ya mwisho umemwambia mumeo “Nakupenda Mpenzi”?

Majibu yalikuwa kama ifuatavyo:
Wengine wakisema Asubuhi ya leo,
Wengine jana,
Wengine wiki iliyopita
Wengine mwezi uliopita
Na wengine wakasema hawakumbuki!
Mwalimu aliwapa kazi kila mwanasemina achukue simu yake na kumtumia mume wake meseji yenye neno “NAKUPENDA MPENZI”
Baada ya meseji kwenda aliwaamuru kubadilishana simu kila mtu na jirani yake.
Kila mwanasemina aliambiwa kusoma meseji za majibu kwenye simu aliyoshika

Simu ya 1 – “Samahani, nani mwenzangu”!
Simu ya 2 – “Samahani, wrong number”!
Simu ya 3 – “Si nimekuambia usinitumie messages kwenye namba hii”!
Simu ya 4 – “Mh! leo mvua itanyesha”!
Simu ya 5 – “Nikija tutaongea zaidi”!
Simu ya 6 – “……Imedhibitishwa umepokea Tsh300,000 kutoka kwa ……”!
Simu ya 7 – “Me too”!
Simu ya 6 – “Huu ujumbe ndio ulikuwa unamtumia huyo hawara yako ee, leo utanikoma”!

Angalia haya mazungumzo ya msichana na mvulana, mapenzi ya ajabu haya

Demu: Hny mambo jamani!
Man: Safi nipe habari wangu wa moyo
Demu:Wafanya kazi gani vile wangu?
Man: Ni fundi wa kufunga ATM
Demu: Wow dont tel me i love you myn mwa mwa mwaaaaah

Man: Mbona wafurahia?
Demu: Nami natamani kuja kufanya kazi za kibenki.
Man: Itakua poa sana nami natamani pia
Demu: Hee si umesema wafanya kazi ya kufunga ATM?
Man: Hukunielewa mie ninafunga mashine na za kunulia condom kwenye bar
Demu: nipishe huko

Shopping Cart
1
    1
    Your Cart
    Kitabu cha SMS Maalumu kwa Umpendaye
    Kitabu cha SMS Maalumu kwa Umpendaye
    1 X Sh2,500 = Sh2,500
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About