Ujasiriamali: Kujitambua na Kuwa na Mafanikio Katika Maisha

Una thamani gani?

Kazi au shughuli unayoifanya ina thamani gani kwa wengine?unawasaidia au unawaumiza??
Biashara unayoifanya ina thamani gani kwa wengine?ni lazima uwaumize ndipo ufaidike au uwasaidie ili nawe upate faida?

Elimu yako uliyo nayo ina faida au thamani gani kwako na kwa wengine?unawadharau na kujiona wewe ndiye msomi pekee au unawasaidia?

Una thamani gani kwa ndugu,jamaa,marafiki na majirani zako?unasaidiana nao katika kila kitu au unajiona wewe ndiye matawi ya juu unyenyekewe?

Una faida au thamani gani kwa wasiojiweza??umewahi kuwasaidia chochote?kuwatembelea watu wenye Shida mbalimbali kama wagonjwa,wafungwa nk

Kila unachokifanya kina thamani yoyote kwa wanaokuzunguka??
Kumbuka mafanikio ni kugusa maisha ya watu wengi kwa kuwasaidia wao kwanza wafanikiwe ndipo Baraka za mafanikio zitamwagika kwako.
Mafanikio sio wengine waumie ndipo uyaone mafanikio.

Jifunze kuwasaidia wengine waweze kutimiza malengo na ndoto zao ndipo nawe Mungu atakubariki kufikia ndoto zako.

Kumbuka kuna watu wengi wapo nyuma yako wanakusubiri wewe ubadilike ndipo nao waweze kuungana na wewe muweze kufanya kitu cha maana na chenye thamani kwa wengine.

JITAMBUE: Kipi hauna kati ya pesa na muda?

Soma kidogo hapa.. Kuna watu wa aina NNE tunapoongelea pesa na muda.

1. WANA MUDA MWINGI ILA HAWANA PESA

Watu ambao hawana pesa ila wana muda wa bwerere. Hawajui thamani ya muda. Hawa ndo wale ambao hawajui cha kufanya. Anaamka mpaka analala usiku hana specific timetable. Unaweza kumkuta anaenda dukani ukamwambia nisindikize saluni na akakubali. Yupo yupo tu. Unaweza kuta ameingia Facebook hajui hata kwa mini. Basi tu kwa sababu ana bando. Akiperuzi akaona mahali wanaongelea mpira yumo. Akiscroll post za chini akakuta kuna mtu kapost kuhusu UKAWA yumo. Akikuta kuna mtu kapost mtu ana uvimbe mkuuubwa watu wameambiwa wacomment AMEN na yeye huyo anacomment AMEN. Akikuta watu wanaongelea TRUMP na yeye anaingia kucomment. Kundi hili ni kundi lenye watu wengi mno. Watu wa aina hii kufanikiwa ni bahati nasibu. Labda kwa bahati tu akutane na post nzuri kama hii na post zingine nzuri huenda ikamsaidia. Otherwise hawa ndo hawaelewi maisha yanaenda wapi maana hawana kitu fulani specific wanachofanya. Wakisikia tu kuna kitu kiko kama dili hivi wanaenda. Wakikuta kumbe kinahitaji bidii na kujituma wanaondoka. Wanataka maisha mazuri yaje tu yenyewe.

2. WANA PESA ILA HAWANA MUDA

Hili ni kundi la watu wenye shughuli fulani ya kiuchumi. Labda ameajiriwa au amejiajiri. Wako busy kweli kweli. Na ukweli pesa inaonekana. Hawa huwezi kumwambia njoo tuonane akaja hapo hapo. Huyu lazima apange kwanza ratiba zake. Maana yupo busy. Au lazima aombe ruhusa kazini maana hana uhuru na muda wake. Muda wake kamuuzia mtu (mwajiri). Au labda atoroke ndo anaweza kupata muda wa kufanya mambo yake binafsi. Au asubiri weekend ambapo kila ratiba itategemea siku hizo mbili, kama ni ibada, usafi, kutembelea wagonjwa au ndugu kwenda mahali kuona labda kiwanja kinauzwa au kuona ujenzi au mradi wake unaendeleaje nk. Mara nyingi watu wa kundi hili hushindwa kufanya vitu vingi vinavyohusu maendeleo yako binafsi mfano kujisomea, kuhudhuria semina zinazofundisha mambo yanayoweza kuwa na manufaa kwake nk. Sababu ana ratiba iliyobana. Ukiwa na sherehe ukamwomba mchango hashindwi kukuchangia angalau chochote kile lakini muda wa kuja kujumuika na wewe ni vigumu akaupata.
Hili ni kundi ambalo kuna watu wanaitwa MIDDLE CLASS people. Watu wa maisha ya kati. Mambo yako si mabaya sana lakini si kwamba ni mazuri. Wasomi wengi na watafutaji wengi wapo hapa. Afu ndo wanahisi wanajua kila kitu. Na wengi wao huishia kupata changamoto za kifedha na kiafya ukubwani au uzeeni kama stress na maradhi mbali mbali nk. Sababu ya kutokuwa na muda hata wa kuangalia wa kuinvest na kujifunza biashara au ujasiriamali mapema wala kujishughulisha na afya zao, mazoezi, kupumzika vizuri nk kwa kuwa walikuwa busy siku zote. Maisha ya watu hawa middle class mwishoni huja kuwa magumu kwa kuwa hata kuwa na muda na majirani tu ilikuwa ishu. Kwa kuwa wengi wana magari (mengi ni mkopo. Wengine gari la kazini) na kwa kuwa wanaweza kulipa kodi ya nyumba au hata kupata kakiwanja na kuanza kujenga huko Malamba Mawili basi wanaridhika. Hawawezi kuota kumiliki nyumba Masaki au kununua kiwanja Upanga. Kama upo kundi hili lazima uanze kutafuta mbinu mbali mbali za kuyakabili maisha vizuri siku za usoni. Waangalie wastaafu ambao walikuwa busy zamani. Saivi utasikia mgongo, miguu, macho nk vinasumbua. Hawa middle class people ndo ukimkuta social media wengi wao wako critical kwa kila kitu. Maana haoni kama ana shida yoyote.

3. HAWANA MUDA WALA HAWANA PESA

Ulishasikia mtu anaambiwa “busy for nothing”? Ni kitu kama hicho. Yani mtu unakuta labda ni kibarua tu mahali anatumwa kazi asubuhi mpaka jioni. Labda ameajiriwa kazi ya ulinzi, au gereji, au kwenye mradi wa ujenzi anabeba zege au kupaka rangi. Hashindi njaa ni kweli lakini ukweli hana hela. Wala hatamani kuendelea kuwa hivyo. Kuamka alfajiri kulala saa tano usiku. Hela anayopata inatosha kula kwa mama ntilie tu na nauli. Basi. Hawezi kuota hata gari. Hata ya mkopo. Maana hata hakopesheki. Huyu hata muda wa Facebook ni nadra akiingia ni kupitisha macho afu anatoka. Au hata simu ya Facebook hana.

4. WANA MUDA NA WANA PESA

Hapa ndo utakuta wale ambao hana tena shida ya pesa. Pesa iko. Hana tena shida ya muda. Akihitaji kwenda mahali haombi ruhusa wala kuaga mtu labda kumuaga mwenza wake tu. Anaweza kusikia kuna shamba linauzwa mahali na hahitaji kutafuta hela tena ili akalinunue bali anaanza michakato ya kisheria pale pale kununua kama amelipenda. Kuna siku nilienda Morocco Square hapo Kinondoni jirani na Airtel kuna Apartments zinajengwa nikaonana na watu wa NHC waliokuwa wanakagua ujenzi unaendeleaje. Nikawauliza hizo apartments zinauzwaje wakasema kuna za milioni 600 na za milioni 800. Na unatakiwa kulipa cash 10% (yaani aidha milioni 60 au 80 cash) halafu inayobakia unaweza kuimalizia ndani ya miezi 12. Na kuna watanzania kadhaa wamenunua tena kwa hela halali. Hawa wako kundi hili hapa. Hela ipo. Muda upo. Kuna watu walienda kutembea Marekani kibiashara walipokuwa njiani kurudi wakapita mahalinchi nyingine wakakuta kuna mnada wa nyumba kwenye nchi hiyo. Hawakujiuliza mara mbili wakanunua. Kuna wazee fulani wana mtoto wao alikuwa akisoma Canada. Alipograduate wakamuuliza unataka kuishi wapi akasema huku huku Canada wakamnunulia nyumba Canada. Ukisikia hivyo unaanza kuwaza ni mafisadi. Mawazo yako ninkuwa bila ufisadi watu hawanunui nyumba Canada. Kwa taarifa yako Hawa siyo waajiriwa serikalini wala popote ni wafanya biashara.. Kundi la watu kwenye pesa. Na muda. Wanaweza kuamua kesho wakaenda kutembea visiwa vya Comoros. Watu wanaoishi kundi hili wana discipline kubwa ya maisha. Na watu wengi wanatamani kufika kundi hili. Lakini HAWANA discipline ya kujifunza tabia zinazoweza kukufikisha huko.

Swali muhimu tu la kujiuliza tu ni kuwa je, wewe upo kundi lipi.

Una muda mwingi lakini huna hela? = FUKARA

Una hela nyingi lakini huna muda? = MIDDLE CLASS

Huna muda wala huna hela.. Vijisenti unavyopata vinaishia nauli kula kodi ya nyumba nk? = MASKINI

Au una muda mwingi na hela siyo shida tena? = TAJIRI

Hofu inavyo tugharimu katika safari ya ujasiriamali na Jinsi ya kuiepuka

Wengi wetu tunapenda Mafanikio, tunapenda kufika mbali tunapeda kuwa kama Mengi siku moja.

Tunavyo kuwa tunaendelea kutamani kiwa kama wakina Azam au Mengi nyuma ya pazia tuna matatizo nayo ni hofu kuu,

1. Hofu ya kuchekwa
Wengine tuna hofu ya kuchekwa kwamba tunafanya biashara gani hizi? Tuna lima kilimo gani hiki au tunafuga nini? Kuna watu hofu ya kuchekwa tu inatosha kumtoa Barabarani mazima.
Mtua leo hii anashindwa Kuanzisha project anayo peda kwa sababu tu anaogopa kuchekwa

2. Hofu ya kushindwa kabla ya kuanza
Tuna hofu za kushindwa, naona nikifuga kuku nitashindwa, naona nikilima nitashindwa tu, hofu hii inatufanya tuone bora kusubilia kwanza
Fear of Unknown inatusumbua.
Watu tunashindwa kuanzisha miradi kisa tu mtu anaogopa kushindwa.

3.Hofu baada ya kuona walioa anza wakashindwa
Hii ni kubwa sana, mtu anakuambia fulani alifuga Broiler wakafa wote, fulani alifuga layers wakamshinda, Fulani alilima nyanya kavuna debe moja tu, fulani.
Watu wengi tunashindwa kuanza kwa sababu fulani alishindwa. Sikiliza fulani sio wewe, fulani ana akili yake na wewe una akili na nguvu zako.

4. Hofu ya Elimu zetu.
Kuna walio bahatika kusoma hadi Univesity na wana Degree na Wengine Masters. Sasa elimu zetu nazo zimekuwa.kikwazo, mtu anaona kwa elimi yake hapaswi kufanya aina fulani ya biashara, hapaswi kufuga au kulima anapaswa kufungua Yard ya kuuza Magari
Elimu zetu ni.kama tulienda kusomea uoga vile.

5. Hofu ya Ndugu,jamaa, Marafiki na kadhika.
Kuna mtu mpaka sasa hawezi fuga au anzisha mradi kwa sababu tu ndugu jamaa na marafiki hawatamuelewa. Mama hatanielewa kwamba nalima na nimesoma, Mama mkwe na Baba mkwe watanishangaa sana kwamba nafuga Bata,
Mchumba hatanielewa kabisa na anaweza nikimbia mazima kwa sababu nalima Nyanya na nina Degree,

6. Hofu ya kukosa baadhi ya vitu.
Mtu anaona kuliko akose kwenda kutazama mpira na washikaji bora huo mradi usianze tu, kuliko nishindwe kwenda viwanja bora nisianze ,siwezi enda kulala shambani nikashindwa kwenda kuona npira au kucheki move.

Kwa Kifupi tuna hofu nyingi sana zinazo tugharimu.

SASA BASI

Kama unaishi kwenye hofu za aina hizo kamwe sahai kufanikiwa labda tu ukomae na ajira,

Nilazima utambue kwamba uko wewe na honor uwezo wako, ipe heshima Uwezo wako.
Ukiona hofu hizo ni kikwazo kwako na huwezi ziacha kama una mtaji basi kanunue vipande ya hata UTT na usubilia gawio, au nunua hisa za kampuni na subiliaga gawio kulingana na faida.

Kwenye ulimwengu wa Ujasiriamali lazima kwanza Uonekane mwehu, lazima second person akuone kichaa, lazima watu wakushangae ,
Ujue hata kichaa yeye huwa hajui kama ni kichaa ila second person na third ndo tunaona na tunajua kwamba fulani ni kichaa, the same na wewe kwamba lazima ifikie mahali watu washindwe kukuelewa kati ya haya yaani wajiulize maswal mengi bila majibu.
– Fulani hivi kafukuzwa kazi?
– Fulani hivi kweli alimaliza chuo? Au alidisco?
– Fulani anaongea mwenyewe barabarani
-Fulani maisha ni kama yamemkamata, hapa kisa tu huonekani viwanja.
-Fulani haonekani viwanja kabisa.
– Fulani anacheza na ujasiriamali hiyo awaachie wakina Mangi

Watu wakianza story za aina hizi basi jua uko kwenye track nzuri.

UJASIRIAMALI SIO ISHU YA KITOTO, LAIZMA UWE KAMA UKO ULIMWENGU MWINGINE KABISA

Kwa ushauri huu jitambue upate mafanikio

Ukiona unalala masaa 9 wakati Donald Trump analala manne tu. Afu unaamka huna nauli na bado kesho unalala masaa manane tena.. Ujue unashabikia mafanikio.

Ukiona Bill Gates anasoma kitabu kimoja kwa wiki. Na wewe unasoma kimoja kwa miezi sita ujue nod maana kuna tofauti ya Bill Gates na wewe.

Ukiona unasema utakuwa successful siku moja afu huna DAILY GOALS. Yani hujui ukiamka ufanye nini na jioni utapimaje kama kweli umekifanya ujue hujaelewa vizuri maana ya kuwa successful.

Hard Work beats talent.

You must sleep less and work harder until you get what you want.

Ujumbe wa leo kwa mtu anayetaka kufanikiwa katika maisha kiuchumi

Kila mtu aliyefanikiwa ukifuatilia historia yake pengine unaweza kukata tamaa kabisa Na kusema mimi hii njia siiwez.

Lakin siri ya mafanikio ni uvumilivu Na kujituma ktk kazi uifanyao.

Ni kweli vijana wengi humaliza vyuo Na kusubiri ajira wanashindwa kusoma alama za nyakati, hawatambui kuwa sasa wasomi ni wengi sana ajira chache.

Mimi pia ni mwanafunzi wa Chuo kikuuu lakini ni mjasiri amali vilevile.

Vijana wenzangu tubadilike fursa zipo tuache kuchagua kazi eti kisa unashule kichwani!

Tumia vyeti vinapo hitajika pia viweke pemben unapohitaji kutumia nguvu.

Jaman mungu ni wawote hana upendeleo utatoka tu!!! Tusijitenge eti kwasababu tumeingia darasan uonekane wakipekeee ila tujichanganye Na watu tuliowaacha mtaani tutaongeza maarifa Na watatuonesha fursa tusizozijua.

Shule ni nzuri sana ila pia ni mbaya hasa ya Tanzania maana haitufundishi kujitegemea bali inatufanya tuwe tegemezi cku zote

Chamsingi vijana wenzangu tuamini maarifa tuliyonayo kuwa ndo muhimu kuliko vyeti tulivyo navyo

“Tafuta maarifa ustafute shule tafuta pesa ustafute vyeti”

Kuna watu wameajiriwa lakn hadi Leo wanaishi nyumba za kupanga

Mwisho wa yote niambie uliwahi kuona wapi tajiri aliyeajiriwa? Wote wanamaisha ya kawaida tu.

Angalist ya matajiri Tanzania Na duniani kote hamna aliye ajiriwa hata mmoja.

Yatie akilini hayo jali mafanikio katika maisha yako

MAFANIKIO YA MAISHA SIO ELIMU TU, UTHUBUTU, KUJIAMINI NA UJASIRI WA MAAMUZI

✍🏽Ukichunguza katika jamii, utabaini kuwa sehemu kubwa ya matajiri ni wale ambao wana elimu ndogo ama hawakusoma kabisa.

👉🏾Katika miji na maeneo yote; wenye majengo ya maana, wenye makampuni makubwa, wenye utitiri wa malori na mabasi, wenye maduka makubwa ni wale wa “darasa la saba” au wale ambao hawakuingia darasani kabisa

🙇🏽📚 Wasomi wengi wana maisha ya kawaida yaani yale ya kiwango cha kubadilisha mboga, wakijitahidi sana wanaishia kujenga nyumba za kuishi 🏡 na 🚗 🚙magari mawili ya kutembelea (tena kwa mikopo!)

👉🏾Wapo 🙇🏽📚wasomi wengi tu wanaoishi kimasikini, kwa lugha ya kistaarabu tunasema wana maisha ya kuungaunga. Kiukweli idadi ya wasomi walio matajiri ni ndogo sana

👉🏾Lakini Umasikini wa wasomi wengi umeanzia huko shuleni na vyuoni wanakopatia usomi wao. Madarasani kuna mambo mawili wanafundishwa wasomi ambayo ndio yanayowaroga

Hii inachangiwa na mambo mawili:-
👇🏽
I. Wameelimishwa na kuaminishwa kwamba yule anaepata maswali yote kwa usahihi ndio anaonekana amefaulu. Ukikosea unahesabika kuwa u mjinga na wenyewe wanaita umefeli

👉🏾Hata hivyo katika maisha ya kawaida hasa kwenye mchakato wa kutafuta hela, kujaribu na kukosea ni sehemu ya mafanikio

👉🏾Kadiri unavyojaribu na kukosea mara nyingi ndivyo unavyojifunza na ndivyo nafasi ya kutajirika kwako inakuwa kubwa!

🙇🏽📚Wasomi wengi kwa sababu ya “mentality” ya kuogopa kukosea huwa hawapendi kujaribu biashara kwa hofu ya kushindwa kuiendesha, na huamua kufa kimasikini wakitegemea mishahara pekee kwa sababu mishahara ndio pato lao la uhakika
👇🏾
II. Madarasani kunahimizwa ubinafsi badala ya umoja. Angalia namna mitihani inavyofanyika. Kila mwanafunzi anafanya mtihani peke yake, na ukikutwa unaangalizia ama mnasaidiana na mwenzio ndani ya chumba cha mtihani mtapata adhabu kali ikiwemo kufutiwa mtihani!

👉🏾Katika maisha ya kawaida hasa ya kusaka fedha, unahitajika ushirikiano mkubwa sana, baina yako na wadau, wateja, wafanyakazi wenzio, marafiki n.k. Kwa kifupi unatakiwa kuwa na Networking ya kutosha.

✋🏾Huwezi kufika mbali kiuchumi kama utakuwa na “mentality” ya ubinafsi unaosisitizwa madarasani!

🤔Simaanishi kusoma hakuna maana, isipokuwa ninakwambia: Kama ukipata nafasi ya kusoma, soma kwa bidii; lakini usibebe kila wanachokulisha madarasani; ukakileta huku mtaani

🛣Mtaani panahitaji akili ambayo ni tofauti na hiyo iliyopimwa kupitia kukariri ya vitabuni, mwishoni wanakuzawadia makaratasi yaitwayo vyeti

😎Ukitaka kufanikiwa ungana na waliofanikiwa wakuelekeze

😀🙏🏽 Hii habari haitaki hasira, vumilia tu na jiongeze

Jipe moyo kamwe usikate tamaa

Nilikuwa naangalia mpira wa miguu katika uwanja wa
shule.
Nilipokaa, Nilimuuliza kijana mmoja juu ya Matokeo ya mchezo.

Kwa tabasamu, alijibu “Wako mbele yetu 3-0”!
Nikasema, Kweli!
Mbona huonekani kukata tamaa..?

“Kukata tamaa?
“Yule mvulana aliuliza kwa mshangao….”!?

Kwanini nikate tamaa wakati bado refa hajapuliza kipenga cha mwisho?

Nina imani na timu yangu na meneja wa timu; Nina hakika tutashinda!

Na kweli, mchezo uliisha 5-4 timu ya kijana ikiwa mbele!

Alinipungia mkono taratibu, na tabasamu zuri akiondoka uwanjani; nilishangaa, mdomo wazi, ujasiri mkuu kiasi hiki; such beautiful faith;

Nilipofika nyumbani usiku ule, swali lake lilizidi kuja kwangu zaidi:
“Kwanini niogope wakati refa hajapuliza kipenga cha mwisho?”

Maisha ni kama mchezo.
Kwanini ukate tamaa wakati mwenyezi Mungu ndiye meneja wako?

Kwanini ukate tamaa wakati kungalipo uhai ndani yako?

Kwanini ukate tamaa wakati kipenga chako cha mwisho bado hakijapigwa?

Ukweli ni kwamba watu wengi hujipulizia wenyewe vipenga vyao vya mwisho.

Lakini maadamu ungalipo uhai, hakuna kisichowezekana muda haujakuacha.

Nusu kipindi si kipindi kizima na ratiba ya Mungu kwa mwanadamu si ratiba ya mwanadamu kwa Mungu.

Usijipulizie kipenga chako cha mwisho we mwenyewe.

JIPE MOYO USIKATE TAMAA!

KWA MUNGU YOTE YANAWEZEKANA.

KAMWE USIKATE TAMAA.

Ilinde ndoto yako

Ndoto ni nini?

Ndoto ni zile ndoto za kiuhalisia ambazo mtu anaweza kuwa nazo akiwa macho na anatumia mawazo yake kutengeneza au kuunda picha ya maisha anayotamani kuishi siku zijazo. Hizi si ndoto ambazo mtu anaota usiku akiwa usingizini, bali ni matakwa ya dhati ambayo yanamfanya mtu ajizatiti na kutia bidii katika mambo anayofanya ili kuyafikia malengo yake.

Kila mtu ana ndoto tofauti ambazo anatamani kuzifikia, na mara nyingi ndoto hizi huwa zinaongoza maisha yake na kumpa dira na mtazamo wa maisha yake ya baadaye. Ndoto hizi zinaweza kuwa kubwa au ndogo, na zinaathiri jinsi mtu anavyochagua kuishi maisha yake ya kila siku, jinsi anavyofanya maamuzi, na hata jinsi anavyoingiliana na watu wengine.

Kwa mfano, mtu mwenye ndoto ya kuwa Rais atajituma katika masuala ya uongozi, atajifunza mambo mbalimbali yanayohusiana na siasa na uongozi wa jamii au nchi. Ataweza pia kujihusisha na harakati mbalimbali za kijamii au kisiasa ili kujenga umaarufu na kuwa na uwezo wa kufikia ndoto yake.

Kwa upande mwingine, mtu anayetamani kuwa mwimbaji bora atajikita katika kuendeleza kipaji chake cha uimbaji, kuhudhuria mashindano ya muziki, na pengine atajitahidi kuwa karibu na watu wengine waliofanikiwa katika tasnia hiyo ili ajifunze mbinu za kufanikiwa.

Wale wenye ndoto za kumiliki vitu kama nyumba za kifahari, magari, au kuwa bilionea, mara nyingi wanajikuta wakihusika katika kufanya kazi kwa juhudi zaidi, kujifunza na kutafuta taarifa juu ya uwekezaji, na kutafuta njia bora za kukuza uchumi wao binafsi.

Ndoto za kutembelea nchi fulani zinaweza kumfanya mtu aweke akiba ya pesa, ajifunze kuhusu tamaduni mbalimbali, na hata kujifunza lugha tofauti ili kujiandaa kwa safari yake. Kwa kufanya hivi, mtu huyo anajiweka katika nafasi nzuri ya kufikia ndoto yake na kuifanya iwe halisi.

Kwa ujumla, ndoto za mchana ni muhimu sana katika kuhamasisha na kutoa motisha kwa mtu kufikia mafanikio makubwa maishani. Zinamfanya mtu kuwa na malengo, azimio la dhati, na muelekeo wa wapi anapenda maisha yake yawe siku za usoni. Ndoto hizi zinapoambatana na mipango mizuri na jitihada za makusudi, mara nyingi huwa na matokeo chanya na kutimia kwa matarajio ya mtu.

Zote hizo ni ndoto ambazo kila mmoja alikua nazo huenda ni kipindi anakua au hata sasa bado anayo.
Kwa bahati mbaya sana watu wengi wamekuwa na ndoto kubwa sana wakiwa wadogo na kuzipoteza walipoanza kuingia kwenye uhalisia wa maisha.

VITU VINAVYOWEZA KUIPOTEZA NDOTO YAKO.

Ugumu wa Maisha.

Maisha yanavyozidi kubadilika na kuwa magumu ndipo baadhi ya watu huanza kuasahu vile vitu ambavyo walikua wanatamani waje kuwa navyo. Maisha yanapokuwa magumu sana wengi huona haiwezekani tena wao kufikia ndoto zao hivyo kukata tamaa kabisa na kuamua kuwa na maisha ya kawaida.
Mtu anaweza kujitazama vile alivyo na kuona yeye hafananii kabisa kuja kuwa Rais wa nchi hii labda kutokana na familia aliyotokea au maisha yanayoendelea sasa hivi.
Nakuomba kama unapitia hali hiyo anza kuikataa kabisa ili usije kupotea.

Marafiki wabaya.

Marafiki na watu unaokuwa nao mara kwa mara wanaweza kuwa sababu kubwa sana kukupoteza kabisa na kukufanya wewe uache kupigania ndoto yako.
Ndoto yako ni ya thamani sana ndio maana inapata upinzani.
Ndio maana utaambiwa haiwezekani. Ndio maana watakucheka ukiwaambia wewe unataka kuwa Rais wa nchi hii au unataka kua Bilionea.
Mara zote watu wanakuhukumu kutokana na hali uliyonayo sasa hivi.
Unaweza kuachwa na Mpenzi wako umpendaye kwa sababu tu yeye anaangalia maisha uliyonayo sasa hivi na hata ukimueleza ndoto zako haamini kutokana na hali yako ya maisha uliyonayo sasa.

Ufanyeje?

Kaa nao mbali wale watu ambao hawana ndoto kama za kwako. Kaa mbali na watu ambao wanafikiri kama kuku. Yaani wao wamejiona kwamba ni maskini na haiwezekani kuwa tajiri labda kuiba tu. Inawezekana ni watu wako wa karibu sana labda kaka, dada, wazazi.
Ufanyeje?
Usikubali kuwasikiliza weka pamba sikioni. Mimi kuna mtu aliniambiaga hizo ni ndoto za mchana haziwezi kutokea kamwe lakini sijakata tamaa naendelea kufanyia kazi ndoto zangu.

UNALINDAJE NDOTO YAKO?

Iandike.

Kama unasema una ndoto lakini bado ipo kichwani bado hujaelewa maana yake. Katafute Notebook nzuri sana ya gharama Huwezi kuandika ndoto ya kuwa Bilionae kwenye note book ya elfu mbili aisee.
Tafuta notebook ya Gharama hata ya 20,000 ili uweze kuitunza vizuri. Andika kila kitu unachokitaka kwenye dunia hii. Hakikisha umeandika kila Kitu na usiache hata kimoja.
Hii ni njia ya kwanza ya kuilinda ndoto yako. Nikikutana na wewe sehemu Uniambie au unionyeshe kilipo kitabu chako cha ndoto. Andika ni Jinsi gani unaweza kupata vile vitu. Ni ujuzi wa namna gani unahitaji ili uweze kufikia ndoto zako. Ni watu wa namna gani unahitaji kuambatana nao ili ufanikiwe kwenye doto zako. Andika ni Baada ya Muda gani utakua umefikia Ndoto zako. Sasa hapa Ni somo jingine kabisa jinsi ya kuandika malengo. Malengo ya muda mfupi na Muda mrefu.

Soma ndoto zako kila siku Asubuhi na kabla ya Kulala.

Soma kila siku namaanisha kila siku asubuhi na jioni. Kwanini usome kila siku ? Unaichora au unaiingiza picha ya ndoto zako ndani ya ubongo wako hii itakufanya chochote utakachokutana nacho kama hakiendani na ndoto yako uweze kukiepuka na kama kinaendana basi uweze kukivuta. Unaposoma inajijenga kwenye akili yako na kutengeneza ukaribu wa wewe kuifikia zaidi.
Soma na tafakari.

Tenga Muda peke yako.

Hakikisha unatenga Muda wa peke yako angalau kila wiki ukiwa peke yako sehemu ambayo haina usumbufu wowote. Sehemu hiyo utakua unaipa akili yako nafasi ya kutafakari juu yako wewe. Jitazame ulivyo sasa halafu jitazame wewe ukiwa umefikia kwenye ile ndoto yako. Kama ni gari basi anza kujiona jinsi unavyoliendesha lile gari la ndoto yako. Kama ni Rais ebu jione ukiwa Ikulu basi Jione ukiongoza majeshi. Kama ni Bilionea anza kuona ukiwa Bilionea utakavyokua. Utakavyoweza kubadilisha maisha ya watu wengi sana Duniani. Ona jinsi dunia inavyofurahia Mungu Kukuumba wewe kwasababu maisha yao yamebadilika. Nashauri hili ufanye angalau lisaa limoja ukiwa peke yako bila simu wala kifaa chochote cha mawasiliano.

Soma Vitabu na Fanyia Kazi ndoto yako Kila siku.

Soma vitabu ambavyo vitakuza ufahamu wako ili wewe uweze kuifkia ndoto yako.
Kama unataka kuwa Rais wa Nchi lazima ujue kua unakwenda kuongoza watu hivyo vitabu gani usome ili ukuze ufahamu wako.
Unataka kuwa Bilionea hutaweza kuwa bilionea na ufahamu ulionao sasa hivi mali zote zinatakiwa ziongozwe na wewe hivyo jijengee tabia ya kujisomea vitu mbalimbali juu ya ile ndoto yako.
Ili ufikie Ubilionea unaanza na hatua moja anza leo kupiga hatua moja moja hadi ufikie kule unakotaka. Usikubali kabisa siku ipite ujafanya chochote juu ya Ndoto yako ni kupoteza fursa.

Kama tunavyojua fursa ya kwanza ni uhai tulionao leo hivyo usitumie vibaya leo siku zote unakuwaga na leo tu. Ukiweza kuipangilia leo vizuri itakufikisha kwenye ndoto yako.

Jipongeze

Kwenye kila hatua unayopiga jipongeze ili kujiongezea hamasa na wewe uweze kusonga mbele. Unaweza kujipa zawadi ndogo ndogo ambazo huwa unazipenda kila unapopiga hatua kuelekea kule unapotaka.

Iseme ndoto yako sehemu yeyote unapokuwa.

Kwanini uiseme kwa sababu una Imani na Imani ni kua na hakika juu ya mambo yasiyoonekana.
Hata Yusuf alianza kuwaambia ndugu zake kwamba anaona ndoto anaona akiwaongoza. Walimkemea lakini hakusita kuendelea kuwaambia.
Hii itakusaidia unapokamilisha iwe ushuhuuda kwamba huyu jamaa alituambiaga anakuja kuwa Rais, Bilionea, Mtu mkuu sana.

Kuwa na ndoto kubwa ni jambo la muhimu sana katika maisha. Mara nyingi, inasemekana kwamba ikiwa una ndoto ambazo hazikutoi usingizi, basi unaelekea katika mwelekeo sahihi. Mara nyingine, watu watakuita mchawi au Freemason wanapoona unafanikiwa. Lakini, kumbuka, maneno hayo hayana msingi kama yanasemwa wakati unapoanza tu kuota ndoto zako kubwa, kama vile kujenga ghorofa au kumiliki gari la kifahari kama BMW, wakati huna chochote.

Watu wanaokatisha tamaa mara nyingi ni wale wale ambao hawawezi kuona mbali kuliko hali yako ya sasa. Hawaelewi kwamba ndoto huenda zaidi ya hali ya sasa. Kama mtoa hamasa Norman Vincent Peale alivyosema, “Panda picha ya mafanikio ya kustaajabisha katika akili yako. Fikiria hili kwa nguvu. Kisha, fanya kazi kwa ujasiri kila siku kufanya picha hiyo kuwa uhalisia.”

Ni muhimu pia kutambua kwamba kuisema ndoto yako, kuiweka wazi mbele ya wengine na kujiamini, kunaweza kukujengea ujasiri. Hiyo ina maana ya kuendelea kutafakari kwa bidii jinsi ya kuifanya ndoto yako iwe kweli. Usemi unasema, “Ujumbe mzito huvunjika moyo pale unapotamkwa.” Hivyo, endelea kuongea kuhusu matarajio yako, mipango yako, na ndoto zako. Hii itakupa nguvu ya kuvumilia nyakati ngumu na kukusaidia kubaki thabiti katika njia yako.

Naamini una kila kitu kinachohitajika kuilinda ndoto yako. Itapasa uwe na nidhamu, uvumilivu, na azma thabiti. Kikubwa zaidi, uwe tayari kujifunza na kukua. Kila hatua unayopiga kuelekea katika ndoto yako, hata ikiwa ni ndogo, ni hatua muhimu.

Kumbuka kwamba hakuna jambo la maana ambalo hutokea usiku mmoja. Mafanikio ya kweli hujengwa kidogokidogo. Kwa hiyo, hata kama unakabiliwa na kejeli au shutuma, usiruhusu hiyo ikuvunje moyo. Kama alivyosema mwanasiasa na mwandishi wa Marekani Adlai Stevenson, “Ni jambo kubwa kuweza kukumbuka wakati umefanikiwa, kwamba kuna wakati pia uliwahi kushindwa, na kwa vipimo vilevile, ukatumia fursa hiyo kukua na kuboresha.”

Hivyo basi, lipokee wazo la mafanikio moyoni mwako, liweke hai katika mazungumzo yako na hatua zako, na kisha, lifanyie kazi kwa ajili ya kesho yenye matumaini. Jitahidi kwa kila njia kuona ndoto yako ikitimia. Jipe moyo na usisahau kusherehekea kila hatua unayopiga kwa mwelekeo chanya.

Hichi ndicho unatakiwa uwe nacho kulingana na umri wako

20 – 25 =Iwe kama ni kielimu hujafikia malengo yako,sitisha mara moja tafuta kazi/biashara ya kufanya,pigana kufa na kupona ili kama vipi urudi shule kwa pesa yako.

25 – 30 = Hakikisha uwe na angalau na SHUGHULI RASMI kama umeajiliwa au umejiajili.

30 – 35 = Uwe na angalau kama sio nyumba basi kiwanja,tena ujitahidi uwe umeoa/umeolewa kama sio kuishi nae,tena si mbaya ukawa umeshatengeneza familia,kwa maana ya kuwa na watoto kama mungu kakuwezesha.

35 – 40 = Ni umri wa kama kiwanja kiwe kimejengwa, na kama ni tayari basi nenda step nyingine ya kumiliki kama ni Gari au kuongeza nyumba na hakikisha vinaenda sambamba na ongezeko la familia.

40 – 45 = Ni umri wa masahihisho, kama hukuwahi kununua kiwanja au kujenga basi hapa pambana afe kipa afe beki,kama umegundua mkeo hazai fanya mchakato kwingine kama ni mwanaume na kama mwanamke umegundua mumeo ndio mwenye shida basi tafuta nje umletee mtoto. Kifupi ni umri wa masahihisho.Ila kwa wale ambao wameenda vizuri huko nyuma basi hapa kama ni wale watoto wapo kwenye level tofauti za elimu,kwahiyo ni muda wa kuwawekea malengo ya kimasomo watoto wao.

45 -50 = Kwa yule ambaye hakukosea huko nyuma,basi umri huu ni wa kuanza kuwatengenezea mazingira watoto wako,kama ni shuguli zako ni kuanza kuwahusisha,huku wewe ukijiweka pembeni taratibu na kuangalia fulsa za umri wako. Lakini kwa wale waliokosea hapa ni kupitia zile hatua za 35 -40.

50 – 60 = Ni kujiandaa na maisha mapya ya kustaafu au kujiweka mbali na shughuli za shulba.Na kama ulijitenga na msikiti/kanisa huu ndio muda wako.

60 – 70 = kula matunda yako huku ukiangalia misingi ya wanao inaendaje.

70 – 80 = kula matunda.

80 – n.k= unamsikilizia Mungu anasemaje

JITAMBUE : Maisha yako ya kesho hayalingani na maisha yako ya jana, Anza sasa

THERE IS NO FUTURE IN THE PAST.** Ukitaka kufanikiwa usiangalie nyuma yako kunanini na ulishindwa mara ngapi. Siku zote kukaa Chini nakuanza kujuta kwa makosa uliofanya uko nyuma nikupoteza muda, huo muda Utumie kwa kupanga ya kesho.

Bahati nzuri Mungu alitujalia kusahau, ivyo siku zote sahau ya nyuma na waza yale ya mbele yako.

Maisha bora ya mbele hayawezi kuja kama akili yako imebeba kushindwa kwa nyuma.

Binadamu yeyote anayeweza kupoteza muda wake wa leo kwa kulaumu mabaya ya jana, kesho atapoteza muda akilaumu mabaya ya leo.

Tambua ya kuwa, “hakuna awezaye kurudi nyuma na kuanza upya, bali waweza kuanza leo na kutengeneza maisha yako ya kesho”

Kadri unavyofikiria ya nyuma ndivyo unavyochelewa kufika mbele zaidi. Penda zaidi ndoto yako ya kesho kuliko historia yako ya jana,maana hatima yako siku zote iko mbele na sio nyuma.

Siku zote utashindwa kwa kuendekeza mambo yaliopitwa na wakati maana utakuwa unatumia ujuzi uliopitwa na wakati.

“Habari njema ya siku ni leo, na siku nzuri yako ni ya kesho “

Ukiona umesononeka kwa maisha kuwa magumu jua unaumia kwaajili ya maisha yako ya nyuma, maana unawaza jinsi ulivyo shindwa kulipa kodi ya nyumba,ulivyoshindwa kulipa umeme, maji, ada za watoto na ulivyoshindwa kuendesha biashara yako au ulivyoshindwa kuitetea ajira yako. Usipoteze Muda wako kwa kuwaza yaliopita badala yake waza kesho yako itakuwaje.

Waswahili wanasema yaliopita si ndwele, tugange yajayo. Huwezi kubadilisha jana, Bali waweza kubadilisha kesho yako kwa kufanya maamuzi leo.

Usipoteze Muda kwa kugeuza shingo yako kutazama ya nyuma, utajikuta unadumbukia katika shimo la maisha magumu.

“You can’t have a better tomorrow if you are thinking about yesterday all the time “

Maisha yako ya kesho hayalingani na maisha yako ya jana. Anza sasa.

Umeshawahi kufanya hili jaribio?

Figisu ya Leo. UMESHAWAHI KUFANYA HILI JARIBIO.?

kadri temperature inavyo ongezeka chura nae huwa ana increase temperature ya mwili wake..

pindi inapokaribia kufika boiling point yaani nyuzi 100 chura atashindwa kuongeza temperature ktk mwili wake na hapo ndipo atataka kutoka ktk maji hayo ya moto na yanayo endelea kuchemka..
kutokana na kutumia nguvu nyingi sana ktk kuongeza temperature ktk mwili wake,pindi anapotaka kuruka atashindwa na atakufa humo ndani ya chombo cha maji yanayochemka..
SWALI; NINI KIMEMUUA CHURA.!??
Najua utaniambia ni maji ya moto…
La hashaa.!
kilichomuua chura ni kushindwa kufanya maamuzi mapema ya kutoka katika chombo cha maji yanayochemka hali ya kuwa bado nguvu anazo..
FUNZO
Fanya maamuzi sahihi sasa kabla nguvu za kutaka kufanya changes hazijakuishia kama yaliyomkuta chura..
NOTE; Kuvumilia jambo usiloliweza ni sifa ya punda.
BADILIKA.

Ushauri wangu kwa leo: Zingatia hili, hamasika, badilika

Tupo kwenye dunia ambayo tulikuta watu na tutawaacha watu.
Vyote tulivyovikuta vilianzishwa na binadamu wengine wenye mawazo mema na wenye mawazo mabaya pia. Vitu vingi tunavyovifanya tunaendeleza tulivyovikuta ni mara chache kukuta kitu kipya ambacho hakitegemei mazingira na asili ya tulivyovikuta.

Hivyo basi kwa vyovyote vile unahitaji mtu wa kukuongoza au kuku Coach ili ufanikiwe katika pande zote za maisha.

Nitakwenda kuzungumzia sehemu kuu tatu za muhimu sana ambazo unatakiwa uwe na watu wa kukuongoza ili uweze kukua na kupanda viwango kila wakati.

Ni vitu vya kawaida sana lakini leo nitakwenda kuzungumzia uone ilivyo muhimu sana wewe kua na vitu hivi maana bila vitu hivi mafanikio yatakua magumu sana kufikia. Safari yako itakua ngumu zaidi kama utakosea sehemu hizi tatu.

Nitaomba tuelewane kwamba hapa huendi kuiga au kuwa hawa watu utakua wewe na utatimiza lile kusudi la Mungu ndani yako.

Kwanza kabisa uko hivyo ulivyo kwa sababu ya mazingira uliyokulia na watu ulioishi nao tangu ukiwa mtoto hadi hapo ulipo.

Kuna tabia nyingi sana unazo kutokana na mazingira uliyokulia.

(Hapa ndipo nakutana na kitu ambacho nakipenda sana kujifunza kwa wengine napenda kujifunza kwenye mazingira mapya na kwa watu wapya kwa kua wameishi maisha ambayo mimi siyajui na wanafahamu vitu vingi ambavyo mimi sifahamu. Watu wana utajiri mwingi sana ndani yao ukiweza kukaa na mtu ambaye humjui kabisa unaweza kujifunza mambo mengi ya ajabu kwake. )

Hawa ndio watu wa Muhimu sana kwenye safari yako usiwakose ili uweze kusonga mbele.

Sifa zao kabla hujawachagua ni za muhimu sana pia ili wasije wakakupoteza badala ya kukufikisha kule unakotaka kwenda.

(a)Awe na mafanikio (Amefika Mbali) kwenye hiyo sehemu.

(b)Awe na Tabia njema zinazokubalika na jamii yake na dini yake. (mfano hapa ukikutana na mtu ambaye anakuelekeza kuhusu biashara na ni mlevi na mzinzi hizi tabia lazima atakuambukiza kwasababu atakua mtu wako wa karibu sana)

(c)Awe amekuzidi sana kwenye kile unachotaka akulelee (akuongoze).

Hizo ni sifa za muhimu tu za kuangalia zipo nyingine nyingi sana utajifunza mwenyewe.

1. Mlezi wako wa Kiroho

Huyu ni mtu wa muhimu sana na nimemweka wa kwanza.

Bila roho hakuna mwili.

Bila roho mwili wako unakua umekufa.

Unahitaji ukue kiroho na upande viwango kila wakati ili uweze kuvutia mafanikio ya nje.

Ukishindwa hapa hata ukiwa bilionaire inaweza kuwa kazi bure.

Hutaweza kuzifurahia hizo pesa.

Tafuta mtu wa kukulelea kiroho.

Mtu wa kukufundisha kumcha Mungu.

Kama huna katafute mtu wa kukulea kiroho sifa nimezitaja hapo juu.

Mtu huyu anatakiwa akufahamu vizuri na wewe umfahamu vizuri.

Yaani muwe na mahusiano ya karibu sana.

Mtu huyu awe anafuatilia maendeleo yako ya kiroho kwa karibu sana.

Haijalishi uko Dini gani lazima umpate mlezi wa roho yako.

Dini ndio inahusika kulisha roho zetu.
Ndio maana hatufundishwi biashara kule.

2. Mlezi wa Mahusiano/Uchumba/Ndoa

Hapa ni kwa muhimu sana.

Ukiwa vizuri kiroho mahusiano yakawa na tatizo hutafika mbali.

Ukiwa vizuri kiroho ndoa ikasumbua nayo ni tatizo.

Tafuta mtu wa kukulea kwa upande huu pia mtu aliefika mbele zaidi yako.

Aliefanikiwa zaidi yako.

Kama unatafuta mchumba tafuta mtu aliye kwenye ndoa na amefanikiwa.

Ukimtafuta single mwenzako atakupoteza😀.

Mtu huyu awe karibu yenu kabisa kulea mahusiano/ uchumba au ndoa yenu.

Hakuna aliyezaliwa anajua kila kitu tunajifunza hapa duniani kwa waliotutangulia na waliopo pia.

3. Mlezi wa Maono yako/Ndoto zako/Malengo yako/Biashara Yako/Pesa. (Coacher).

Mtu huyu ni wa muhimu pia katika maisha yako.

Unataka kumiliki utajiri wa dollar billion moja lazima utafute mtu wa kukulelea na kukuwezesha ufikie huko.

Huwezi kwenda mwenyewe.

Unahitaji mtu wa kukuongoza kwenye kila unachotaka kukifanya.

Wengi wanakata tamaa kwa kua hawana watu hawa wa kuwalelea.

Mtu huyu anatakiwa awe anakufuatilia hatua kwa hatua kwenye kile unachokifanya.

Awe anapata taarifa za maendeleo yako kila wakati ikiwezekana hata kila week.

Ukipata mafanikio yeyote ajue pia ukipata changamoto ajue.

Mtu huyu anatakiwa awe amekupita kwenye kile unachokitaka na hapa huendi kuwa Follower,anakwenda kukutengeneza wewe uwe kiongozi.

Uweze kusimama mwenyewe na hatimae uongoze wengine.

Kwa Tanzania wapo watu wanaofanya kazi hizi kwa malipo pia.

Lakini hapa unaweza kuanza na mtu ambaye una mahusiano nae ya karibu awe anakulelea.

Siku hizi teknolojia imekua rahisi sana unaweza kuwa na mawasiliano na mtu yeyote unayemtaka popote alipo duniani.

Unaweza kujifunza pia vitu vingi sana kupitia mitandao hii kama hapa facebook.

Unaweza kusoma vitabu na vitu vingi sana vile unavyovitaka.

Naomba nimalizie kwa kusema kwamba.
Kwa hiki ulichokipata leo ukikifanyia kazi.

Utakua mshindi uliyezaliwa kuwa.

Utafikia Hatma yako kwa kufuata haya, namaanisha wewe uliyesoma hapa.

I will see you at the top!

Mambo ya kufanya mwezi Disemba

Ikiwa leo ni tarehe **1/12 huwezi amini kuwa hakuna tarehe 1 nyingine tutakayoiona ya mwaka huu hivyo sichelei kusema kuwa mwaka umeisha .Lakini mwaka unaishaje??? pengine hili ndilo swali gumu na la muhimu la kujiuliza .Je, Mwaka unaisha ukiwa umefanya nini cha kujipongeza??? .Je mwaka unakaribia kuisha maarifa yako yakiwa yameongozeka kwa kiasi gani???.Haya ni maswali muhimu sana unavyooanza kufikiria juu ya sherehe za mwisho wa mwaka.

Watu waliopiga hatua katika fikra – yaani, wale waliofanikiwa kutimiza malengo na mipango waliyojiwekea – wanajikuta katika kipindi cha kipekee ifikapo mwezi huu. Ni wakati ambao wanapaswa kuchukua muda na kutafakari kwa kina juu ya safari yao ya mwaka uliopita. Huu si tu wakati wa kuzingatia mafanikio na mafunzo, bali pia ni kipindi cha kulinganisha matarajio yaliyokuwa yamewekwa dhidi ya yale yaliyotimia.

Kurudi kwenye malengo yaliyowekwa hapo awali ni zoezi la muhimu linaloleta tafakuri juu ya uendelevu na ufanisi wa mikakati iliyotumika. Watu hawa wanaweza kujiuliza maswali kama, je, malengo yalikuwa yanatekelezeka? Je, walikutana na changamoto gani, na walizishinda vipi? Changamoto hizi zinaweza kuwa za ndani kama vile kutunza motisha, au za nje kama vile mabadiliko ya kiuchumi na kijamii yaliyokuwa yameshuhudiwa.

Inawezekana pia walikuwa na malengo ambayo hayakutimia. Katika hili, kuna fursa ya kujifunza na kuchukua hatua za marekebisho. Mwisho wa mwaka ni muda mwafaka wa kutathmini upya na kuweka mikakati mipya, kuondoa yaliyopitwa na wakati na kuja na mawazo mapya yatakayowasukuma mbele zaidi. Uchambuzi wa kina utawasaidia kuweka malengo yanayoweza kutekelezeka kwa mwaka unaofuata pamoja na kutengeneza mpango kazi madhubuti ambao utawaongoza katika hatua zao zijazo.

Kwa kuangalia nyuma na kufanya tathmini yenye unyoofu, waliopiga hatua katika fikra wanaweza kupata msingi imara wa kujenga juu yake. Wanaweza kujitathmini na kujipanga upya, kuchukua mwelekeo wenye nguvu na mpya ambao utawawezesha kutimiza malengo yao yaliyosasishwa na yaliyo wazi zaidi. Kila hatua, kila mafanikio, kila funzo, yote huchangia katika safari yao ya kipekee ya maendeleo binafsi na ya kitaaluma.

Leo nataka nikuekeze mambo muhimu ya kufanya mwezi huu pamoja na kuwa unawaza sikukuu na kusafiri kwenda kwenu .Mambo haya unaweza kuwa hujawahi kufanya lakini ni muhimu sana ukafanya mwaka huu ili mwakani tuone mabadiliko .Mambo hayo ni pamoja na ;

1.Fanya Tathimini (Evaluation)

Tathimini ni kipimo kinachoonesha kushindwa kwako na kufanikiwa kwako .Mwezi huu ni mwezi wa kukaa chini na kurejea kwenye malengo na mikakati uliyokuwa umejiwekea na kuona ni kwa jinsi gani umefanikiwa .Ainisha mambo uliyofanikiwa na ambayo hujafanikiwa .Kwa yale uliyofanikiwa jipongeze kwa kufanikiwa kwa yale ambayo hujafanikiwa jiulize kwanini hayajafanikiwa ili yakupe mbinu na hatua mpya mwaka ujao.

Andika kwa mtindo huu;

SEHEMU A:MAMBO NILIYOFANIKIWA HUU

-Mwaka huu nilifanikiwa kuwapata marafiki wazuri wanaounga mkono maono yangu
-Mwaka huu nilifanikiwa kuanzisha biashara ya genge
-Mwaka huu nilifanikiwa kusoma vitabu viwili

*Jitihidi sana kujipongeza kwa yale uliyofanikiwa na hii ni tabia ya watu waliofanikiwa .Usione umefanya madogo lahasha.*

SEHEMU B:MAMBO AMBAYO SIKUFANIKIWA mwaka huu

-Sikufanikiwa kuhudhuria semina hata moja ya ujasiriamali
-Sikufanikiwa kuboresha ofisi

Kwa yale ambayo hukufanikiwa jiulize kwanini hukufanikisha utagundua wewe ndiye sababu kubwa ya kutoyafanikisha .

2.Anza kuandaa malengo ya mwaka ujao (GOAL SETTING)

_Pasipo maono, watu huacha kujizuia_
~(Biblia)

Ndiyo bila malengo hutafika na utafanya kila kitu bila mpangilio .Huu ndio mwezi kwako ambao unapaswa kuandaa malengo ya mwaka ujao haijalishi hukuwahi kuweka malengo toka unazaliwa .Najua malengo yako yalikuwa yanakaa kichwani mwaka huu amua kuandika kwenye notebook Nzuri .Andika kwa ujasiri mkubwa sana .Malengo yako yafuate kanuni za malengo(yapimike,yawe na ukomo,yawe mahususi na yakufikika ).

Andika kwa mfano huu;

-Kufikia Mei  nitakuwa nimefuga kuku watatu hata kama nyumba yangu ni ndogo .

-Kufikia Agosti   nitakuwa nimehudhuria semina 2 za ujasiriamali

Ukiandika kwa mfumo huo itakusaidia kuyafikia malengo yako maana yamefuata kanuni za malengo.

3. Andaa Bajeti ya mwaka  (Budgeting)

Hii ni sehemu ambayo inaleta shida sana .Na hii ni kwa sababu hata wazazi wetu wametulea bila kutufundisha bajeti.Masomo ya darasani wengi hatufundishwi kuishi kwa bajeti .Lakini Tusilaumu sana kutofundishwa maana lawama ni tabia ya kimaskini tuamue mwakani 2017 kuishi na kutembea na bajeti

Mara nyingi tukiulizwa hela zetu zinaenda wapi huwa hatuna majibu sahihi .Hii ni kwasababu hatuna bajeti .Kwanini bajeti??? .Bajeti hutusaidia kupunguza matumizi yasiyo ya lazima na yaliyo nje ya bajeti .Bila bajeti sehemu ya kutembea kwa mguu utapanda bodaboda .Bila bajeti utanunua simu ya laki saba wakati unasema huna mtaji wa laki sita.Bajeti itaamua uchangie harusi na kitchen party ngapi kwa mwaka.

Ndiyo lazima tubadilike hata mimi nimeamua hivyo mwaka ujao.Kama una familia kaa na mke wako tengeneza bajeti ya mwaka.Kuna vitu vinaweza kujitokeza njiani na hivyo kumbuka kuweka dharura .

Bajeti iliyopangwa kwa mwaka ujao ni kama ramani inayoonesha njia ya malengo na maelekezo ya kifedha ambayo shirika au mtu binafsi anapaswa kufuata. Inatoa muhtasari wa kina kuhusu matarajio ya mapato na matumizi, na hivyo kumwezesha mtu au shirika kupanga kwa ufanisi zaidi juu ya rasilimali zake. Kuweza kwenda sambamba na bajeti hii, mtu au shirika linahitaji kuelewa vizuri vipaumbele vyake na kuweka mipango thabiti kwa kila sehemu ya matumizi au uwekezaji.

Katika kuhakikisha ufanisi, ni muhimu kwa shirika kuwekeza nguvu katika upangaji wa bajeti ulio sahihi, utafiti wa masoko ili kufahamu mwenendo wa kiuchumi unaoweza kuathiri mapato na matumizi, pamoja na uboreshaji wa mbinu za usimamizi wa fedha. Ufuatiliaji wa mara kwa mara wa bajeti na utathminini wa maendeleo halisi ikilinganishwa na yale yaliyopangwa ni muhimu sana. Nguvu katika kufuatilia na kurekebisha mtiririko wa bajeti inaweza kumaanisha tofauti kati ya kufikia malengo ya kifedha au kukabiliana na upungufu.

Kuwekeza nguvu inamaanisha pia kuwa na nidhamu na ufuatiliaji madhubuti wa matumizi ya kila siku, kujifunza kutokana na takwimu na ripoti za awali za fedha, na kujitayarisha kukabiliana na changamoto zinazoweza kujitokeza. Mwisho, uwekezaji katika mafunzo kwa wafanyakazi wanaoshughulikia fedha na matumizi inaweza kuongeza ufanisi na kuimarisha uzingatiaji wa bajeti iliyowekwa.

Jifunze kitu kupitia kisa hiki cha boss na mwajiri wake

BARUA YA BOSI ILIBADILI FIKRA ZANGU KUHUSU PESA KATIKA DAKIKA ZA MWISHO ZA MAISHA YANGU

Duna Lawrence (78) ni raia wa Togo ambaye alijitosa kwenda nchini Ujerumani kutafuta maisha mwanzoni mwa miaka ya 80. Baada ya kufika huko, alipata kazi, akawa muaminifu kwa Bosi wake ili aweze kupata mafanikio.

Baada ya miaka mingi kupita, Duna alirudi nchini mwake kwa mara ya kwanza na akaoa, kisha kurejea tena Ujerumani. Bwana Duna aliendelea kufanya kazi kwa bidii huku mafanikio yake kimaisha yakizidi
kushuka chini, akaomba kuongezewa mshahara ili kukidhi mahitaji yake, lakini hiyo haikumpa unafuu.

Jamaa huyu bado hakuona mafanikio yoyote, kazi zikaendelea kuwa nyingi, familia yake nayo ikawa kwenye wakati mgumu. Bwana Duna umri ulizidi kumtupa mkono, huku akijiona hana chochote cha kujivunia katika kazi anayofanya.

Duna akawa mzee, nguvu nazo zikamuisha, ufanisi kazini ukapungua na magonjwa ya kiutu uzima yakaanza kumwandama, akamweleza Bosi wake hali halisi ya kiafya, akaomba alipwe stahiki zake ili arudi nyumbani. Bosi wake alimwonea huruma Mzee Duna, ila hakuwa na namna nyingine ya kumsaidia zaidi ya kumpa stahiki zake zote. Mzee Duna alirejea nchini Togo.

Mzee Duna akiwa anapekua begi lake wakati wa usiku, alikutana na barua ikiwa na dola 2000 na kuandikwa maneno haya:

“… Duna umefanya kazi kwa muda mrefu lakini ulishindwa kuniuliza jinsi ya kuwa tajiri kama mimi, hilo hukuliona kuwa na maana kwako, ukang’ang’ania kuongezwa mshahara na kudai malimbikizo yako, halikuwa jambo baya, ni haki yako. Ulikuwa kama mfungwa kwangu kwa sababu ya kufanya kazi ukitegemea kupata pesa, uliitumikia pesa kwa muda mrefu na haikuweza kukuondolea umasikini. Ninachokushauri, licha ya umri kuwa mkubwa ila anza kujali mambo yako, Mind Your Own Business, Not Another One’s. Tumia pesa niliyokupatia kujali mambo yako, umejali mambo yangu kwa muda mrefu sana, jifunze kujali shughuli zako… “

Mzee Duna alisikitika sana, akatoa machozi kwa uchungu, hakujali suala la umri kumtupa mkono, akajitosa kutafuta fursa mbalimbali ndani ya nchi yake akiwa na mtizamo tofauti kuhusu pesa. Mzee Duna alifungua mgahawa, akaajiri vijana kadhaa kwa ajili ya kumsaidia kuwahudumia wateja. Biashara ikawa nzuri, akazidi kutanua biashara yake, akaongeza eneo ili kuwahudumia wateja wengi zaidi. Mzee Duna alipata maeneo kadhaa, akafungua migahawa mikubwa na kuipa jina la “MIND YOUR OWN BUSINESS RESTAURANT”.

Nini tunajifunza?

Ifikie wakati kila mtu aanze kujali mambo yake katika kuamua hatima ya maisha yake kiuchumi. Kuendelea kuomba nyongeza ya mshahara, malipo ya ziada, na malupulupu mbalimbali hayatakufanya ujitegemee kiuchumi, bali kuwa tegemezi. Una miaka zaidi ya kumi kazini lakini bado huna uchumi imara, jaribu kujiuliza unamtajirisha nani, nani ananufaika kupitia jasho lako. Lazima ukumbuke kuwa maisha yako yote hayataishia kwenye kazi tu, kuna kipindi hutaweza kufanya kazi kabisa. Je, utaishi kwa njia gani? Anza kufikiria kuhusu maisha yako, timiza ndoto yako na si ya mtu mwingine. Anza kutengeneza mazingira rafiki kwa ajili ya kujiajiri, usiache kazi kwa papara.

1.Tafadhali fuata hatua makini ili uanze kujali mambo yako.

2.Usifikiri kile wanachofikiri wengi ndicho sahihi.
Fikiri kile kinachokunufaisha wewe ndicho sahihi.

2.Jua maana ya mafanikio!Je, ni kumiliki pesa, vipi kuhusu afya?

Je, mafanikio ni afya, kula vizuri, kuvaa na kula vizuri?Vipi kuhusu mahusiano mazuri ya kijamii na Mungu wako?

Je, maisha ni mahusiano mazuri na Jamii na Mungu?Vipi kuhusu ubinafsi uchoyo na fitna moyoni mwako?

Penda wenzako kwa dhati!Mjue Mwenyezi Mungu wa kweli, Simama imara katika matendo na akili yako.Heshimu na waheshimu wenye mamlaka ama amali za kijamii.

Furahi, ona mbali,fanya kazi, zingatia afya, Mjue Mungu wa Kweli. pumzika vizuri!

Mungu akubariki!

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About