SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Usichokijua kuhusu sungura, panya na jamii yao

JE WAJUA?

Sungura, panya na Jamii zao huwa na mwendo wa kukimbia na kuruka muda wote na umri wao wa kuishi ni miaka 15. Kobe ni mnyama mwenda pole, asiye na papara wala pilika, muda mwingi hujificha na kupumzika ndani ya jumba lake akikwepa maadui. Umri wa kuishi kobe hufikia hadi miaka 300.
FUNZO: Mazoezi ni kiinimacho na uongo mtupu. Jipumzikie mwaya!!!
🏃🏾🏃🏿‍

Tabia za wachepukaji

WACHEPUKAJI WENGI WANATABIA HIZI

1.Hachezi mbali na simu yake kila wakati.
2.Inbox na sending items hufutwa kila
wakati.
3.Ukimuomba simu yake ghafla lazima
akwambie hebu
kwanza…….
4. Kamwe haiiti always vaibration.
5. Namba nyingi ha save.
6. Kuna simu hapokei hata
iweje….anapenda sms zaidi
7.Majina mengi kwenye simu yameseviwa
kwa majina ya
kufikirika.
8.Muda mwingi ni mtu wakujihami.
9.Anapenda password na anabadili mara
kwa mara.
10.Akiazima simu yako, akitumia tu
anafuta dial no
haraka.
11.Always yuko na simu…..hadi bafuni
ikibidi.
12. Anajazba ukimuuliza chochote kuhusu
simu….anajishtukia.
13. Akiwa anachati anakuangalia mara kwa
mara
kiwiziwizi
14. Hana jeuri ya kukuweka profile picture
na akikuweka
humalizi masaa anakudampu huko
Hapa kuna ukweli asilimia millioni moja
kabisa
Share na washikaji zako😜😜😜😜😜

Matumizi ya kahawa kutibu presha ya kushuka au shinikizo la chini la damu

Kahawa husaidia kuongeza presha au shinikizo la damu. Unashauriwa Kunywa kikombe kimoja cha kahawa kunaweza pia kusaidia kupandisha shinikizo lako la damu kwa muda.

Kama unapatwa na kushuka kwa shinikizo la damu mara kwa mara basi kunywa kikombe cha kahawa asubuhi au unywe wakati unakula cha mchana na cha jioni.

Usizidishe matumizi ya kahawa kwakuwa kahawa ina madhara mabaya kwa afya ya mwili kwa ujumla.

Wabongo ni noma! Angalia huyu mbongo anachokifanya

Basi juzi kati hapa sehemu ndogo ya ukuta wa Ikulu ya Magogoni ilianguka!..
Wakapelekwa contractors watatu ili achaguliwe mmoja atakayejenga vzr na kwa bei nafuu!..
Wakwanza alikuwa MUHINDI, wa pili MCHINA na MBONGO!…

MUHINDI: “ntajenga kwa milioni 90!.., 40 za vifaa, 40 za mafundi na milioni 10 faida yangu”

MCHINA: “mi ntajenga kwa milioni 70!.., 30 za vifaa, 30 za mafundi na milioni 10 faida yangu”

MBONGO kuona vile akamvuta chemba msimamizi wa Magogoni!..
MBONGO: “mi ntajenga kwa milioni 270”

MSIMAMIZI WA MAGOGONI: “we una wazimu nn!.. yaani unathubutu kusema hivyo na unaona wenzako wametaja kiwango kidogo?!.”

MBONGO: “milioni 100 zako, 100 zangu alafu hiyo milioni 70 tunaajiri yule mchina”

Umasikini isiwe sababu wala utajiri isiwe sababu ya kuwa mchafu au kutokuwa na usafi

Katika maisha, umasikini siyo sababu ya mtu kuwa mchafu au kutokuwa na usafi. Hali ya umasikini inaweza kuathiri uwezo wa mtu kumudu bidhaa za usafi au kuishi katika mazingira safi, lakini hii haimaanishi kuwa mtu mwenye utajiri automatically ni mtu mwenye usafi.

Kinyume chake, utajiri haujazi hakika mtu kuwa na kila kitu ambacho hahitaji. Utajiri ni kuwa na uwezo wa kununua au kumiliki vitu vingi, lakini ukweli ni kwamba tunahitaji tu vitu vichache sana katika maisha yetu. Tunapojikuta tukiwa na wingi wa vitu visivyotumiwa, tunaweza kujikuta tukichafua mazingira yetu na kutopenda kila kitu tunachomiliki.

Sasa angalia nyumbani kwako! Je, kuna vitu ambavyo haujahitaji kwa muda mrefu au vinachafua tu nafasi yako? Kufanya maamuzi ya busara na kujiondoa na vitu visivyohitajika, vitakuwezesha kuishi katika mazingira safi na yenye upangaji mzuri. Usafi sio lazima uendane na utajiri, bali ni suala la utaratibu na umakini katika kusimamia mazingira yetu.

Umasikini sio sababu ya kuwa mchafu wala utajiri Sio kuwa na kila kitu hata kama hukihitaji. Hebu angalia hapo nyumbani kwako!

Vitu msivyovihitaji Leo wala kesho mmeweka vya nini? Umenunua makochi mapya Yale ya zamani mmegawana vyumbani mnaishia kurundika minguo hapo na kufuga mipanya.

Godoro umenunua jipya la zamani umeviringisha juu ya kabati. Kabatini kwako kuna nguo ulivaa ukiwa secondary mpaka Leo unazo eti ukumbusho au utazivaa ukipungua.

Jikoni ndo shida iliposhika hatamu! Mivyombo ya plastiki imepaukiana imeyayuka na moto ipo tu eti vyombo vya watoto. Mahotpot yamekata roho imebaki kuwa sufuria we unalo tuu. Mxiuuu

Ndoo hata hazitumiki zipozipo tu, hata maua hazifai kupandia we unazogo tu huchomi, hutupi wala huzihitaji.. Sa zanini hapo?? 😡😡

Vyombo vya udongo vina mapengo na magego kama vinang’atwaga au vinapiganaga vyenyewe. 😂😂. Isitoshe kila kimoja na dizaini yake havifanani coz seti imeshavunjikavunjika hivo ndo vimebaki. Unaboa… 😏😏😏

Dressing table imejaa mikopo na mibox haina Kazi, perfume ya mwaka 2000 unayo hapo kisa ukumbusho wa zawadi. Ushamba huooo… 😫😫

Stoo yako mwenyewe ila unaiogopa kuingia coz imejaa vitu visivyohitajika imekuwa ghetto la panya na nyoka kama sio nge badala Ukiweka mnavyohitaji. Ipo siku mtakuta mamba humo.. 🐲🐲🐲

Nje ya nyumba kuna gari la urithi la babu lipogo tu hapo linafuga ndege na vibaka… Aaalaaaa 😡😡😡

Kutupa vitu visivyohitajika hamtupi eti Dhambi na kugawa hamgawi coz mmeviharibu hadi mwisho mtampa nani? Kutwa mnapishana mahospitalini mnaumwa mafua na vifua kila siku.

Kwann msiumwe na mnakaa dampo ? Hivi mnajua km huu ni ugonjwa? Unaitwa hoarder disorder. Tena mnawaambukiza watoto wenu kwani wanajua kwao hata kikopo cha icecream hakitupwagi kinaoshwa kinawekwa hapo.

Halafu bado unaendelea kumuomba Mungu akupe, akupe uweke wapi na kwako pameshajaa?

Kwa kweli, mtazamo wa kuridhika na hali ilivyo sio tu hatari kwa maendeleo binafsi, lakini pia kwa jamii kwa ujumla. Mazingira tunayoishi yanahitaji uangalizi na uhusiano wa moja kwa moja na afya zetu, usalama, na hata uchumi wetu. Kama ilivyosemwa awali, kila mmoja wetu – bila kujali hadhi yetu kifedha – ana wajibu wa kuchukua hatua za makusudi katika kudumisha usafi wa mazingira yetu.

Tunapaswa kuzingatia kuwa usafi na umakini wa mazingira yanatuhusu sote na yana faida zinazoonekana na zisizoonekana. Uchafuzi wa mazingira, kwa mfano, unaweza kuathiri ubora wa hewa tunayopumua na maji tunayotumia, na hivyo kusababisha matatizo ya kiafya. Kwa upande mwingine, mazingira safi na yenye kuendelezwa vizuri yana uwezo wa kuongeza thamani za mali, kuboresha uzuri wa jamii, na kuvutia uwekezaji na utalii ambao unaweza kukuza uchumi wa eneo husika.

Kila mtu anapaswa kuchukua hatua, iwe ni katika kutupa takataka mahali pake, kushiriki katika shughuli za kusafisha mazingira, kupanda miti, au kufunza wengine umuhimu wa uhifadhi wa mazingira. Serikali na asasi zisizo za kiserikali zinaweza kusaidia kwa kutoa elimu, rasilimali na sera zinazosaidia usafi na utunzaji wa mazingira.

Ni muhimu kutambua kwamba uamuzi wa kutunza mazingira unapaswa kuwa sehemu ya maisha yetu ya kila siku na sio tu wakati wa maadhimisho au mikakati ya muda mfupi. Uendelezaji wa mazingira safi na salama ni jukumu letu la kudumu, linalohitaji kujitolea na ushirikiano kutoka kwa watu wote katika jamii.

Mambo madogo hayapaswi kupuuzwa – matumizi ya mifuko inayoweza kutumika tena badala ya plastiki zinazotupa sana, kutumia njia mbadala za nishati zinazoweza kujazwa upya ili kupunguza uchafu, na hata kusimamia taka za kielektroniki – yote haya ni sehemu muhimu ya kujenga mazingira endelevu. Hivyo basi, hebu tuchukue hatua, kila mmoja wetu, kwa mustakabali mzuri zaidi. Tunalo jukumu hilo, kwa ajili ya kizazi chetu na vizazi vijavyo.

Maisha ya Wasichana Wa facebook na instagram

Wiki ya kwanza
Status:”Location flani amazing”
“Having fun”
“I love my life”
“sijali mnayosema nafanya nachotaka”

BAADA YA MIEZI MIWILI
STATUS:”Binadamu wengi ni wasaliti”
“trust nobody”
“Na hili nalo litapita”
BAADA YA MIEZI SITA
Status:”Yesu wewe ndio rafiki wa kweli”
“Bwana ndiye mchungaji wangu”
BAADA YA MIEZI TISA NA KIDOGO
STATUS: “Nakupenda mwanangu😅😅😀😆😆😆😂😂😂😂😄

Kama Mwanamme Download Kitabu cha SIRI ZA MWANAMKE

Salamu za kuaga mwaka na kukaribisha mwaka mpya

KWAHERI MWAKA JANA. UMENIFUNZA MENGI.

Mwaka umefika mwisho, zimebaki siku tatu tu
kuingia mwaka mwingine lakini yapo mengi
niliyojifunza mwaka huu na pengine ningepesha
kushare:

1. Kwamba si lazima sana kuwa na rundo la
marafiki kama hawaleti positive effects kwenye
maisha yako. Urafiki wa maongezi yasiyoleta
maendeleo ni uzamani chakavu.
2. Matumizi madogomdogo yasiyo ya lazima
huchelewesha maendeleo makubwa yenye kiu na
mimi. Nmekuwa na matumizi yasiyo ya lazima na
ndio matundu hayo madogo yamezamisha meli.
3. Mungu ndio kila kitu. Anza na maliza siku na
Mungu. Ukikosacho hakukupangia, usiumie,
muombe akuletee atakacho.
4. Harusi zinaumiza. Usipojiwekea kiwango
maalum na idadi ya harusi za kuchangia kwa
mwaka na kwa umuhimu utakuja kujenga nyumba
kwenye harusi za wenzako.
5. Lawama ni muhimu sana ili maisha yaende,
usiogope hasa pale unapokuwa unasimamia lililo
la kimaendeleo kwako. Kumridhisha kila binadam
ni ngumu. Kuna muda ni kwa maendeleo yako
inabidi uwe mbinafsi.
6. Mapenzi ni mazuri ila yasikuzidi ‘kimo’, vipo
vyamaana vya kulilia sio mapenzi. Kikulizacho
ndicho ulichokipa kipaumbele. Mtu aamuapo
kukuliza na wewe ukalia basi umemtukuza.
Mapenzi yasiyosumbua na yaliyojaa mijadala ya
kimaendeleo ndiyo mapenzi yenye afya.
7. Watu waliowengi hasa kwenye mitandao ya
kijamii wana matatzo na ukichaa, usibishane nao
hasa kwenye mambo yasiyokuletea wewe
maendeleo. Usione hasara kuwafanya wajione
washindi.
8. Wazazi ni Muhimu sana, sala zao ni muhimu
kwako. Usipende kuhonga mpita njia akuachaye
siku yeyote ukawasahau wazazi wako. Wapo
watu sikukuu hizi wametumia maelfu ya shilingi
kuhudumia wanawake zao au wanaume zao
wapitaji wakasahau wazazi wao hata kwa pesa
ya dawa.
9. Kuahirisha mambo ni ugonjwa wa kuridhika na
dhiki. Uahirishapo atakaye uwe chini anafurahi.
Muaibishe shetani kwa mipango thabiti.
10. Panga kwaajili ya MWAKA kabla haUjafika,
kupanga kunakupa nafasi ya kujihakiki.
Mpya mwaka wa kucheza na ‘altenatives’.

SEASON GREETINGS…..HAPPY NEW YEAR.

Shopping Cart
41
    41
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About