Kuna njia Tatu kuu za Kuiishi Huruma ya Mungu ambazo ni kama ifuatavyo; Matendo Hii ni kwa kutenda matendo ya Huruma kwa wengine Maneno Hii ni kwa kunena maneno ya Huruma kwa wengine Sala Kusali kwa kuwaombea wengine Huruma ya Mungu
Tag: Katoliki: Huruma ya Mungu

Wakati mtu anapoanguka dhambini ndio Yesu anakua karibu zaidi, lakini tatizo ni kwamba huo ni wakati ambao mtu hawezi kutambua uwepo wa Yesu. Neno moja tuu la Matumaini na Upendo wakati huo linaweza kumfungua mtu na kumbadilisha.
Mambo manne ya mwisho katika maisha
Mambo manne ambayo ni ya mwisho katika maisha ni; Kifo Hukumu Mbinguni Motoni Mambo haya yote yanaweza kutokea wakati wowote bila kujua wala kutarajia Kifo Kifo ni kitu ambacho kinaweza kumpata mtu yeyote wa umri wowote awe mtoto kijana au mzee na kwa wakati wowote.Maranyingi watu hawapendi kuongelea kuhusu kifo…
Mafundisho kuhusu Toharani
Toharani ni mahali gani?
Toharani ni mahali pa mateso zinakosafishwa roho ambazo hazikutimiza kitubio vizuri baada ya kuungama dhambi.
Mambo ya Muhimu kufahamu kuhusu Mungu
Mungu ndiye muumba wa kila kitu katika uwingu na nchi, Mkubwa wa ulimwengu mwenye kuwatuza watu wema na kuwaadhibu watu wabaya.
Mambo ya Muhimu kujua kuhusu dhambi
Dhambi ya asili ndio nini? Dhambi ya asili ambayo binadamu wote wanazaliwa nayo, ni hali ya kukosa utakatifu na hali ya asili ya urafiki na Mungu Adhabu gani walipewa Adamu na Eva? Adamu na Eva kwa ukubwa wa dhambi yao ya kiburi na ya uasi: 1. Walipoteza neema ya utakaso…
Ahadi kumi na mbili za Moyo Mtakatfu wa Yesu
Bwana Yesu mwenyewe kwa kutumia kinywa cha Mtakatifu Margareta Maria Alakoki aliahidi Baraka na neema zifuatazo kwa wale wote watakaouheshimu Moyo wake Mtakatifu. Na kwa maneno yake mwenyewe, Bwana Yesu aliahidi: 1. “Nitawajalia neema zote watakazozihitaji katika hali yao ya maisha 2. Nitawajalia amani katika familia zao 3. Nitawafariji katika…
Zaburi ya Toba, Zaburi ya 51
Hii ndiyo Sala ya Toba Zaburi 51 1 Ee Mungu, unirehemu,Sawasawa na fadhili zako.Kiasi cha wingi wa rehema zako,Uyafute makosa yangu. 2 Unioshe kabisa na uovu wangu,Unitakase dhambi zangu. 3 Maana nimejua mimi makosa yanguNa dhambi yangu i mbele yangu daima. 4 Nimekutenda dhambi Wewe peke yako,Na kufanya maovu mbele…
Mambo ya Msingi kujua kuhusu Sakramenti ya Kitubio
Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu gani? Yesu aliweka Kitubio na Mpako wa Wagonjwa kwa sababu alijua udhaifu wa binadamu hauishi mara anapopokea uzima wa Mungu kwa sakramenti tatu za kuingizwa katika Ukristo. Hivyo alipanga kusaidia mpaka mwisho wa dunia waamini wake watakaopatwa na dhambi na ugonjwa,…
Maswali na Majibu kuhusu Rehema
Rehema ni nini?
Rehema ni msamaha au ondoleo la adhabu ya dhambi tulizostahili sababu ya dhambi zilizokwisha ondolewa
Maswali na Majibu kuhusu Ufufuko wa wafu
Ufufuko wa wafu maana yake nini?
Ufufuko wa wafu maana yake mwisho wa dunia watu wote watafufuka na miili yao na kwenda nayo katika furaha ya milele au moto wa milele.