MWANZO
Zab. 47:2
SOMO 1
2 Fal 4:8-11,14-16
Ilikuwa siku moja, Elisha alikwenda Shunemu; na huko kulikuwa na mwanamke mmoja mwenye cheo; nave akamshurutisha aje ale chakula. Ikawa kila alipopita njia ile, huingia kula chakula.
Yule mwanamke akamwambia mumewe, Tazama, mimi naona ya kuwa mtu huyu apitaye kwetu mara kwa mara ni mtu mtakatifu w’a Mungu. Nakuomba, tumfanyie chumba kidogo ukutani; na ndani yake tumwekee kitanda, na meza, na kiti, na kinara cha taa na itakuwa, atujiapo, ataingia humo.
Ikawa siku moja akafikia huko, akaingia katika chumba kile akalala. Akasema, Basi, atendewe nini? Gehazi akajibu, Hakika hana mwana, na mumewe ni mzee. Akamwambia, Kamwite. Naye alipokwisha kuitwa, akasimama mlangoni. Akasema, Panapo wakati huu mwakani, utamkumbatia mwana.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
WIMBO WA KATIKATI
Zab. 89 : 1-2, 15-18 (K) 1(K)
Fadhili za Bwana nitaziimba milele. Fadhili za Bwana nitaziimba milele; Kwa kinywa changu nitavijulisha vizazi vyote uaminifu wako. Maana nimesema, Fadhili zitajengwa milele;Katika mbingu utauthibitisha uaminifu wako. (K)
Heri watu wale waijuao sauti ya shangwe, Ee Bwana, kuenenda katika nuru ya uso wako. Kwa jina lako hufurahi mchana kutwa,Na kwa haki yako hutukuzwa. (K)
Maana fahari ya nguvu zao ni Wewe, Na kwa radhi yako pern be yetu itatukuka.
Maana ngao yetu ina Bwana,Na mfalme wetu ni wake Mtakatifu wa Israeli. (K)
SOMO 2
Rum. 6:3-4,8-11
Hamfahamu ya kuwa sisi sote tuliobatizwa katika Kristo Yesu tulibatizwa katika mauti yake? Basi tulizikwa pamoja naye kwa njia ya ubatizo katika mauti yake, kusudi kama Kristo alivyofufuka katikawafu kwa njia ya utukufu wa Baba, vivyo hivyo na sisi tuenende katika upya wa uzima.
Lakini tukiwa tulikufa pamoja na Kristo, twaamini ya kuwa tutaishi pamoja naye; tukijua ya kuwa Kristo akiisha kufufuka katika wafu hafi tena, wala mauti haimtawali tena. Maana kwa kule kufa kwake, aliifia dhambi mara moja tu; lakini kwa kule kuishi kwake, amwishia Mungu. Vivyo hivyo ninyi nanyi jihesabuni kuwa wafu kwa dhambi, na walio hai kwa Mungu katika Kristo Yesu.
Neno la Bwana… Tumshukuru Mungu.
SHANGILIO
Mt. 11:25
Aleluya, aleluya,
Nakushukuru, Baba, kwa kuwa mambo haya uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto wachanga.
Aleluya.
INJILI
Mt. 10:37-42
Yesu aliwafundisha mitume wake hivi: Apendaye baba au mama kuliko mimi, hanistahili; wala apendaye mwana au binti kuliko mimi, hanistahili. Wala mtu asiyechukua msalaba wake akanifuata, hanistahili. Mwenye kuiona nafsi yake ataipoteza; naye mwenye kuipoteza nafsi yake kwa ajili yangu ataiona.
Awapokeaye ninyi, anipokea mimi; naye anipokeaye mimi, ampokea yeye aliyenituma. Ampokeave nabii kwa kuwa ni nabii, atapata thawabu ya nabii; naye ampokeaye mwenye haki kwa kuwa ni mwenye haki, atapata thawabu ya mwenye haki.
Na mtu awaye yote atakayemnywesha mmojawapo wa wadogo hawa ngaa kikombe cha maji ya baridi, kwa kuwa ni mwanafunzi, amin, nawaambia. haitampotea kamwe thawabu yake.
Neno la Bwana……..Sifa kwako Ee Kristo
Nguvu hutoka kwa Bwana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Rehema zake hudumu milele
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Katika imani, yote yanawezekana
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Nakuombea 🙏
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Dumu katika Bwana.
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Mwamini Bwana; anajua njia
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Rehema hushinda hukumu
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Imani inaweza kusogeza milima
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Sifa kwa Bwana!
Endelea kuwa na imani!
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Baraka kwako na familia yako.
Tumaini ni nanga ya roho
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Neema na amani iwe nawe.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Mungu akubariki!
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Mwamini katika mpango wake.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi