Makala za Tafakari za Melkisedeck Leon Shine

Tafakari Kuhusu Matumizi Ya Mali

Usiwe Bahili wa kutumia Mali ulizojaliwa na Mungu. Mungu amekupa Mali hizo ili ufurahie maisha uliyonayo ambayo siku moja yana mwisho.

Biblia inatufundisha hivi katika Kitabu cha Hekima ya Yoshua Bin Sira;

3Si sawa kwa mtu mchoyo kuwa tajiri.
Utajiri una maana gani kwa mtu bahili?
4Mtu anayekusanya mali kwa kujinyima mwenyewe,
anawakusanyia watu wengine.
Hao wataiponda mali yake katika anasa.
5Aliye bahili kwake mwenyewe atakuwa mkarimu kwa nani,
kama hafurahii utajiri wake mwenyewe?
6Hakuna mtu bahili kuliko anayejichukia mwenyewe;
ndivyo ubaya wake unavyomlipa yeye mwenyewe.
7Hata kama akitenda wema, hutenda kwa ajali,
na mwishowe hujulisha hali yake duni.
8Mtu mwenye kijicho ni mwovu;
huangalia pembeni na kuwadharau watu.
9Jicho la mchoyo haliridhiki na kile alicho nacho,
na uchoyo huidhoofisha roho.
10Mtu mchoyo ni bahili wa chakula,
haweki chakula mezani pake.
11Mwanangu, tumia vitu vyako kukufurahisha uwezavyo,
na mtolee Bwana tambiko zitakiwazo.
12Kumbuka kwamba kifo hakitakawia,
na kwamba hujatangaziwa kauli ya kuzimu.
13Mtendee rafiki yako mema kabla hujafa;
uwe mkarimu na kumpa kadiri ya uwezo wako.
14Usijinyime siku moja ya furaha,
usiache sehemu yako ya furaha halali ikuponyoke.
15Siku moja utawaachia wengine matunda ya jasho lako;
yote uliyochuma kwa kazi ngumu yatagawanywa kwa kura.
16Wape wengine na kupokea kwao ujifurahishe moyo,
maana mtu hatazamii starehe huko kuzimu.
17Viumbe vyote hai huchakaa kama vazi,
maana kauli ya tangu zama ni: “Lazima mtakufa!”
18Kama vile majani katika mti uliotanda matawi:
Hupukutika yakaanguka na mengine huota,
ndivyo ilivyo kwa binadamu wenye mwili na damu:
Mmoja hufa na mwingine huzaliwa.
19Kila kilichotengenezwa huchakaa na kutoweka,
naye mtengenezaji hutoweka na kazi yake. (Sira 14:3-19)

Unaweza ukajikuta unatafuta Mali katika Maisha yako yote kwa kujinyima na kujikatalia lakini mwisho wa siku Mali ulizotafuta hutozifaidi wewe. Tena hata wale watakaozifaidi wanaweza wakasahau kwamba wewe ndio uliyezitafuta. Na tena wanaweza wakazitumia vibaya.

Inawezekana unajibana masha yako yote kutafuta hela bila hata kula chakula kizuri na kunywa vizuri pamoja na kuishi maisha ya furaha, lakini maisha yako yatakapokuwa yameisha wale utakaowaachia mali hizo wakaziponda na kuzitumia vibaya.

Kwa ubahili na ugumu wa kutumia Mali unaweza ukashindwa kuonyesha upendo wako kwa watoto wako, ndugu na marafiki zako. Ukiwa bahili wa kutumia mali huna nafasi ya kufurahi na wanao, ndugu na marafiki. Wakati maisha yako yatakapokuwa yameisha hao uliowabania kutumia mali zako wataishia kukuona kuwa hukuwapenda japokuwa ulitafuta mali kwa ajili yao na umewaachia mali hizo. Utakaowaachia mali hawatakukumbuka kwa sababu hukuwahi kuishi nao kwa furaha kwa kuwa ulikuwa unabania matumizi ya mali zako.

Kwa sababu ya ubahili unashindwa kutimiza wajibu wako kwa Mungu wako wa kutoa zaka na sadaka pamoja na kusaidia masikini na wahitaji.

Matokeo ya ubahili wa matumizi ya mali ni kukosa yote na kupoteza yote.

ANGALIZO: Sikwambii kwamba utumie mali vibaya bila kujalli Maisha yako ya baadae na maisha ya wale wanaokutegemea. Nakwambia kwamba tumia mali zako kwa staha na kwa kujinufaisha mwenyewe na wale ulionao wakati ungali hai. Usijibane sana kwa kujinyima nafasi ya kufurahia maisha yako na ya wale unaoishi nao.

Ni vizuri kujiwekea akiba ya Maisha ya baadae lakini ni vizuri zaidi kuweka wazi kwamba ni nani atakayemiliki mali zako wakati utakapokuwa haupo. Ukishaamua ni nani atakayemiliki mali zako wakati ukiwa haupo, ni wajibu wako pia kumuandaa na kumlea kwa namna ambayo ungependa aendeleze yale uliyoyaanza ili juhudi zako zisiishie tuu pale unapokua haupo, bali ziendelee hata utakapokuwa haupo.

Maisha ya binadamu ni kama majani ya mti; yanachipua, yanakomaa, yananyauka na mwishowe yanaanguka. Wakati jani linakauka na kuanguka, yapo mengine yanayo anza kujichipua na kukomaa. Jani likianguka, linaachia nafasi yale yanayochomoza na kukomaa.

Tutumie Maisha yetu vizuri, kwa furaha, amani na upendo huku tukiwatengenezea wale watakaokuja baada yetu mahali pema pa kuishi.

Zaidi sana, Tumuombe Mungu atupe hekima na Busara ya kutumia Mali anazotujalia kwa manufaa yetu na manufaa ya wenzetu huku tukimtukuza Mungu.

Mungu Anakuita Na Kukupa Nafasi Ya Kutubu Na Kumrudia Yeye Ili Akusamehe na Kukubariki

Ingekuwa heri leo msikie sauti yake! Msifanye migumu mioyo yenu. Zab 95:7-8

Tunaalikwa kutubu na kumrudia Mungu kwa Mioyo yetu yote na kwa nia dhabiti. Mungu ni mwaminifu, atatusamehe dhambi zetu na kutufanya kuwa wapya.

Dawa ya dhambi ni kutubu na kusamehewa.

Kutubu sio kusema tuu “Ninatubu” au “Ninaomba msamaha”. Kutubu ni kuona uchungu kweli rohoni kwa dhambi tulizotenda, tukizikataa na kunuia kutokuzitenda tena.

12“Lakini hata sasa,”
nasema mimi Mwenyezi-Mungu,
“Nirudieni kwa moyo wote,
kwa kufunga, kulia na kuomboleza.
13Msirarue mavazi yenu kuonesha huzuni
bali nirudieni kwa moyo wa toba.”
Mrudieni Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu;
yeye amejaa neema na huruma;
hakasiriki upesi, ni mwingi wa fadhili;
daima yu tayari kuacha kuadhibu.
14Huenda Mwenyezi-Mungu, Mungu wenu, atabadili nia
na kuwapeni baraka ya mazao,
mkamtolea sadaka za nafaka na kinywaji.
15Pigeni tarumbeta huko Siyoni!
Toeni amri watu wafunge;
itisheni mkutano wa kidini.
16Wakusanyeni watu wote,
wawekeni watu wakfu.
Waleteni wazee,
wakusanyeni watoto,
hata watoto wanyonyao.
Bwana arusi na bibi arusi
na watoke vyumbani mwao.
17Kati ya madhabahu na lango la hekalu,
makuhani, wahudumu wa Mwenyezi-Mungu,
walie na kuomba wakisema:
“Wahurumie watu wako, ee Mwenyezi-Mungu.
Usiyaache mataifa mengine yatudharau
na kutudhihaki yakisema,
‘Yuko wapi basi Mungu wao?’” Yoeli 2:12-17

Uzuri wa Mungu ni kwamba anasamehe na kusahau, tunapotubu dhambi zetu Mungu anatufutia makosa yetu, anaponya majeraha au madhara yaliyoletwa na dhambi hiyo na kisha antubariki kwa Neema na Vipawa vya kusonga Mbele.

Maana nitawasamehe makosa yao, wala sitazikumbuka tena dhambi zao.” Yeremia 31:34

Mungu anatambua kwamba Binadamu ni dhaifu na anaweza kuanguka dhambini ndio maana anatupa nafasi ya Kutubu na Kumrudia yeye.

13Afichaye makosa yake hatafanikiwa;
lakini anayeungama na kuyaacha atapata rehema. Methali 28:13

Mungu anazifahamu juhudi zetu katika kutafuta kutenda mema ndio maana anakubali toba ya kweli na anatupa matumaini ya kusonga mbele.

“Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu”. Isaya 1:18

Biblia inatuambia kuwa anaheri yule atubuye na kusamehewa kosa lake kwa sababu hana hatia mbele ya Mungu.

1 Heri yake mtu aliyesamehewa kosa lake,
mtu ambaye dhambi yake imeondolewa kabisa.
2Heri mtu ambaye Mwenyezi-Mungu hamwekei hatia,
mtu ambaye hana hila moyoni mwake. Zaburi 32:1-2

Tunapaswa kukumbuka kuwa toba ya kweli ya kutupa msamamaha inaambatana na kuwasamehe wengine na kuondoa kinyongo kwa wengine waliotukosea. Yesu anatufundisha kuwa inatupasa tusamehe ili na sisi tusamehewe.

14“Maana mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe nyinyi pia. 15Lakini msipowasamehe watu makosa yao, naye Baba yenu hatawasamehe nyinyi makosa yenu. Mathayo 6:14-15

Tena, Mungu anatusamehe Makosa Yetu bila kujali tunakosea Mara nagpi na tunarudi kwake mara ngapi. Ndio maana Yesu alitufundisha kuwa tunapokosewa na wenzetu ni lazima tuwasamehe haijalishi wametukosea mara ngapi.

3Jihadharini! Kama ndugu yako akikukosea, muonye; akitubu, msamehe. 4Na kama akikukosea mara saba kwa siku, na kila mara akarudi kwako akisema, ‘Nimetubu,’ lazima umsamehe.” Luka 17:3-4

Unapotubu na kuomba msamaha ni sharti uwasamehe pia wale waliokukosea ili na wewe usamehewe. Kusameheana na wenzetu ndio tabia ya Kimungu ambayo yatupasa kujifunza na kuiishi ili na sisi tuwe watoto wema wa Mungu.

12Nyinyi ni watu wake Mungu; yeye aliwapenda na kuwateua. Kwa hiyo, basi, vaeni moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu. 13Vumilianeni na kusameheana iwapo mmoja wenu analo jambo lolote dhidi ya mwenzake. Mnapaswa kusameheana kama Bwana alivyowasamehe nyinyi. Wakolosai 3:12-13

Tumuombe Mungu atujalie Moyo wa toba na kujirudi kwake Kila tunapokosea. Na tumuombe pia atupe nguvu na uwezo wa kuwasamehe wale wanaotukosea.

KUMBUKA: Unapotubu dhambi zako na kusamehewa ndipo inapokuwa rahisi kwa sala zako kujibiwa. Mungu ni rafiki ya waliosafi Moyoni, na ndio anaowasikiliza na kuwaonyesha nguvu na uwezo wake.

Nakualika kwa Sala ya Toba, uweze kurudi kwa Mungu. Sali kutoka moyoni, kwa kujua kuwa unapendwa na Mungu, Kwa Imani na Matumaini Kwake.

Sala ya Toba

Mungu wangu, Baba wa mbinguni, nakuja mbele zako nikiwa na moyo uliovunjika na toba ya kweli. Nakiri kuwa mimi ni mwenye dhambi, na nimekosa mbele zako kwa njia nyingi. Nimefanya mambo ambayo hayakupendeza, na nimeshindwa kutenda yale uliyoniagiza. Kwa kuwa Neno lako linasema, “Kwa maana wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu” (Warumi 3:23).

Ee Bwana, naomba unisamehe dhambi zangu zote. Nimetenda dhambi kwa mawazo, kwa maneno, na kwa matendo. Ninatubu kwa dhati na kwa kweli kutoka moyoni mwangu. Naomba unioshe kwa damu ya Yesu Kristo, Mwanao mpendwa, ambaye alikufa msalabani kwa ajili ya dhambi zangu. Kama unavyosema katika Neno lako, “Lakini ikiwa tutatembea katika nuru kama Yeye alivyo katika nuru, tu ushirika sisi kwa sisi, na damu yake Yesu Kristo, Mwana wake, yatusafisha dhambi yote” (1 Yohana 1:7).

Ninakiri kuwa mimi ni mnyonge bila wewe, na siwezi kufanya lolote bila msaada wako. Naomba unijaze na Roho Mtakatifu, aniongoze na kunipa nguvu ya kushinda majaribu na dhambi. Ee Mungu, niongoze katika njia zako za haki, na unisaidie kuishi maisha yanayokupendeza. Kwa kuwa Neno lako linasema, “Basi kwa kuwa mmefufuliwa pamoja na Kristo, yatafuteni yaliyo juu, Kristo aliko, ameketi mkono wa kuume wa Mungu” (Wakolosai 3:1).

Ninakuja mbele zako nikiwa na unyenyekevu na moyo wa toba. Naomba unirehemu na unifanye kuwa kiumbe kipya ndani ya Kristo. Kama unavyosema katika Neno lako, “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita, tazama! yamekuwa mapya” (2 Wakorintho 5:17). Asante kwa upendo wako usio na kikomo, na kwa neema yako inayotosha kila siku. Naomba haya yote kwa jina la Yesu Kristo, aliye Mwokozi wangu.

Bwana, naomba unifundishe kuwa mtiifu na kuwa na moyo wa shukrani kwa kila jambo. Acha neno lako likae kwa wingi ndani yangu, na linibadilishe kutoka ndani hadi nje. Nisaidie kuacha njia zote za dhambi, na kuwa mwaminifu kwako katika kila hali. Kwa kuwa Neno lako linasema, “Neno lako nimeliweka moyoni mwangu, nisije nikakutenda dhambi” (Zaburi 119:11).

Ninakubali kuwa mimi ni mnyonge na ninahitaji msaada wako kila siku. Nakiri dhambi zangu na naomba unisamehe. Naomba unipatie moyo safi, na kunifufua kiroho. Kama unavyosema katika Neno lako, “Ee Mungu, uniumbie moyo safi, unirejeshee roho iliyotulia ndani yangu” (Zaburi 51:10). Naomba unifanye kuwa mwanga na chumvi duniani, ili niweze kuonyesha upendo wako kwa wengine. Kwa kuwa Neno lako linasema, “Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji hauwezi kusitirika ukiwa juu ya mlima” (Mathayo 5:14).

Asante, Bwana, kwa kusikia sala yangu. Naamini kuwa umesikia na kujibu ombi langu. Ninatangaza kuwa mimi ni wa Kristo, na ninakubaliana na mapenzi yako maishani mwangu. Kama unavyosema katika Neno lako, “Ninaweza kufanya mambo yote katika yeye anitiaye nguvu” (Wafilipi 4:13). Kwa jina la Yesu, Amina.

Tofauti Wakati Wa Kukomunika Wakati Wa Kupokea Mwili Na Damu ya Yesu Kristo

Wakati wa kukomunika Kila mtu anampokea Yesu kwa namna tofauti kulingana na yeye alivyojiandaa, utayari wake, IMANI, na anachokitaka kutoka kwa Yesu.

Mfano kama mtu anapokea tu kwa vile anapokea komunio na Yesu ataingia kwake tuu bila nguvu au kuonyesha neema zake, Kama mtu anapokea komunio kwa upendo na Yesu atakuja kwake kwa Upendo

Vile unavyompokea Yesu ndivyo na yeye anavyokuja na vile unavyokua tayari Yesu afanye kazi ndani yako ndivyo atakavyofanya kazi ndani Yako.

Wakati wa Kupokea Ekaristi Takatifu: Maandalizi, Imani, na Mapokeo

Katika mafundisho ya Kanisa Katoliki, kupokea Ekaristi Takatifu ni tendo la heshima kuu na lenye umuhimu mkubwa katika maisha ya kiroho ya Mkristo. Ekaristi Takatifu, inayojulikana pia kama Komunyo, ni sakramenti ambayo Mkristo anapokea Mwili na Damu ya Yesu Kristo. Wakati wa kupokea Komunyo, kila mtu anampokea Yesu kwa namna tofauti, kulingana na jinsi alivyojiandaa, utayari wake, imani, na matarajio yake kutoka kwa Yesu.

“Kwa maana mimi nalipokea kwa Bwana niliyowapa ninyi; ya kuwa Bwana Yesu usiku ule aliotolewa alitwaa mkate; naye akiisha kushukuru akaumega, akasema, Huu ndio mwili wangu ulio kwa ajili yenu; fanyeni hivi kwa ukumbusho wangu.” (1 Wakorintho 11:23-24)

Maandalizi Kabla ya Kupokea Ekaristi Takatifu

Maandalizi kabla ya kupokea Ekaristi ni muhimu sana. Maandalizi haya yanajumuisha toba ya kweli, sala, na tafakari juu ya neema ya kupokea Yesu Kristo mwenyewe. Kanisa linahimiza waumini kujitakasa kwa kukiri dhambi zao kupitia Sakramenti ya Kitubio (Kipaimara) kabla ya kupokea Komunyo, ili wawe na mioyo safi na roho zilizo tayari kumpokea Yesu.

“Kwa hiyo kila mtu ajichunguze mwenyewe, na hivyo aule mkate na kunywe kikombe.” (1 Wakorintho 11:28)
“Kama tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na mwenye haki, atasamehe dhambi zetu na kutusafisha na udhalimu wote.” (1 Yohana 1:9)
“Basi, tubuni mkageuke, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana.” (Matendo 3:19)

Imani na Utayari Katika Kupokea Ekaristi

Imani na utayari ni vipengele muhimu vya kupokea Ekaristi. Wakati wa kupokea Komunyo, namna mtu anavyomkaribisha Yesu inaathiri jinsi Yesu anavyoingia na kufanya kazi ndani ya maisha yake. Kama mtu anapokea tu kwa sababu ni desturi au anafuata tu utaratibu wa misa, Yesu ataingia kwake bila nguvu au kuonyesha neema zake kwa ukamilifu. Lakini kama mtu anapokea Komunyo kwa upendo, imani, na shauku kubwa, Yesu atakuja kwake kwa upendo mkuu na neema nyingi.

“Nanyi mtaomba lolote kwa jina langu, nalo nitafanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana.” (Yohana 14:13)
“Yesu akawaambia, Mimi ndimi mkate wa uzima; yeye ajaye kwangu hataona njaa kamwe; na yeye aniaminiye hataona kiu kamwe.” (Yohana 6:35)
“Kwa maana kwa neema mmeokolewa, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu.” (Waefeso 2:8)

Mapokeo na Matokeo ya Kupokea Ekaristi

Vile unavyompokea Yesu ndivyo na yeye anavyokuja na vile unavyokuwa tayari Yesu afanye kazi ndani yako ndivyo atakavyofanya kazi ndani yako. Kupokea Ekaristi kwa moyo uliowekwa wakfu na shauku ya kweli ya kumkaribisha Yesu hufungua milango ya neema na baraka tele. Yesu anafanya kazi ndani ya mioyo ya waumini walio na imani na utayari wa kuongozwa na Roho Mtakatifu.

“Nipo pamoja nanyi siku zote, hadi ukamilifu wa dahari.” (Mathayo 28:20)
“Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma.” (Yohana 17:3)
“Tazama, nasimama mlangoni na kubisha; mtu akisikia sauti yangu na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami.” (Ufunuo 3:20)

Hitimisho

Kupokea Ekaristi Takatifu ni tendo la kiroho lenye nguvu na neema nyingi. Maandalizi, imani, na utayari ni muhimu ili kumkaribisha Yesu kwa moyo wa kweli. Kwa kufanya hivyo, waumini wanajipa nafasi ya kuwa na ushirika wa karibu na Yesu Kristo, kupata neema zake, na kuona matunda ya upendo na imani katika maisha yao ya kila siku. Kwa hivyo, ni muhimu kujiandaa vizuri na kuwa na moyo wa imani na upendo wakati wa kupokea Ekaristi, ili kumruhusu Yesu afanye kazi kikamilifu ndani yetu.

Hii Ndiyo Namna Pekee ya Kuwa na Amani Katika Maisha Yako

Utangulizi

Namna pekee ya kuwa na Amani ni kuishi Mapenzi ya Mungu,

Kwa njia hii Moyo wako hautafadhaika, hautayumbishwa na hautajuta kwa kuwa utakua upo katika njia ya Mungu na njia ya Mungu haina Majuto kwa kuwa ni njema.

Njia zetu zinakua na Majuto kwa sababu hazifuati mapenzi njia na matakwa ya Mungu.

Namna Pekee ya Kuwa na Amani ni Kuishi Mapenzi ya Mungu

Katika dunia hii yenye changamoto na misukosuko mingi, kila mmoja wetu anatamani kuwa na amani ya kweli moyoni. Hata hivyo, amani hii haipatikani kwa wingi wa mali, umaarufu, au mafanikio ya kidunia. Namna pekee ya kuwa na amani ya kudumu ni kuishi kwa kufuata mapenzi ya Mungu. Tunapochagua kuishi kwa mujibu wa mapenzi yake, tunapata utulivu wa ndani, furaha ya kweli, na uhakika wa maisha.

Moyo Wako Hautafadhaika

Tunapoishi kwa kufuata mapenzi ya Mungu, moyo wetu unapata utulivu wa ajabu. Kila hatua tunayochukua inakuwa na uhakika kwa sababu tunajua tuko katika njia sahihi. Yesu alisema katika Yohana 14:27:

“Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; mimi nawapa, kama vile ulimwengu usivyotoa. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msione hofu.” (Yohana 14:27)

Amani anayotoa Yesu ni ya kudumu na ya kweli. Inatufariji na kutupa nguvu ya kuendelea mbele licha ya changamoto na magumu ya maisha.

Hautayumbishwa

Maisha yanapokuwa na misukosuko na mawimbi ya matatizo, wale wanaoishi kwa kufuata mapenzi ya Mungu hawatayumbishwa. Imani yetu inatufanya tuwe na msingi imara ambao hautikisiki na dhoruba za maisha. Mithali 3:5-6 inasema:

“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako.” (Mithali 3:5-6)

Tunapomtumaini Mungu na kumtegemea katika kila jambo, anatuongoza na kutupatia mwongozo wa maisha ambao hautushawishi na mawimbi ya dunia.

Hautajuta

Kuishi kwa mujibu wa mapenzi ya Mungu hakutaleta majuto. Njia ya Mungu ni njema, yenye baraka na inayotuelekeza kwenye uzima wa milele. Mungu ana mpango mzuri kwa kila mmoja wetu, na anataka tuishi kwa kufuata mapenzi yake ili tupate mema yote aliyoandaa kwa ajili yetu. Yeremia 29:11 inatukumbusha:

“Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema Bwana, ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.” (Yeremia 29:11)

Tunapomfuata Mungu na kuishi kwa mujibu wa mapenzi yake, tunapata uhakika wa kuwa katika mpango wake mzuri na hatutajuta.

Njia Zetu Zinakua na Majuto

Njia zetu binafsi zinaweza kuwa na majuto kwa sababu mara nyingi hazifuati mapenzi, njia na matakwa ya Mungu. Wakati tunapojaribu kufanya mambo kwa nguvu zetu wenyewe na bila kutafuta mwongozo wa Mungu, tunaweza kujikuta tunafanya makosa na kupata majuto. Isaya 55:8-9 inasema:

“Maana mawazo yangu si mawazo yenu, wala njia zenu si njia zangu; asema Bwana. Kwa maana kama vile mbingu zilivyo juu sana kuliko nchi, kadhalika njia zangu ziko juu sana kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.” (Isaya 55:8-9)

Njia za Mungu ni bora zaidi na zina mwongozo sahihi kwa ajili ya maisha yetu. Tunapomfuata Mungu na kuishi kwa mujibu wa mapenzi yake, tunajiepusha na majuto ya njia zetu binafsi.

Hitimisho

Amani ya kweli na ya kudumu inapatikana tu tunapoishi kwa kufuata mapenzi ya Mungu. Kwa njia hii, moyo wetu hautafadhaika, hautayumbishwa na hautajuta kwa kuwa tutakuwa katika njia ya Mungu, ambayo ni njema na yenye baraka. Njia zetu za kibinafsi mara nyingi zinatupeleka kwenye majuto kwa sababu hazifuati mapenzi, njia na matakwa ya Mungu. Hivyo basi, tumtafute Mungu kwa moyo wetu wote, tumtumaini na kufuata njia zake ili tuwe na amani ya kweli na furaha ya milele.

Mwenendo Unaongozwa na Roho Mtakatifu

Basi, nasema hivi: Mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia. Maana tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na Tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamuwezi kufanya yale mnayotaka nyinyi wenyewe.

(Wagalatia 5:16-22)

Mwenendo Unaongozwa na Roho Mtakatifu

Basi, nasema hivi: Mwenendo wenu na uongozwe na Roho, nanyi hamtafuata tena tamaa za kidunia. Maana tamaa za kidunia hupingana na matakwa ya Roho; na matakwa ya Roho hupingana na tamaa za kidunia. Mambo hayo mawili hayaafikiani; kwa sababu hiyo hamuwezi kufanya yale mnayotaka nyinyi wenyewe.

“Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtatimiza kamwe tamaa za mwili. Kwa maana mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.” (Wagalatia 5:16-17)

Maana ya Kuongozwa na Roho Mtakatifu

Kuongozwa na Roho Mtakatifu maana yake ni kuacha maisha yetu yaongozwe na maadili na kanuni za kiroho zinazotoka kwa Mungu. Roho Mtakatifu hutupa nguvu, hekima, na mwongozo wa kila siku katika safari yetu ya kiroho. Tunapoongozwa na Roho, tunakuwa na uwezo wa kupambana na tamaa za kidunia ambazo zinatufanya tuwe mbali na Mungu.

“Lakini Roho wa kweli atakapokuja, atawaongoza awatie kwenye kweli yote. Kwa maana hatasema kwa shauri lake mwenyewe, lakini yote atakayoyasikia atayasema, naye atawapasha habari za mambo yajayo.” (Yohana 16:13)
“Basi, kama mlivyopokea Kristo Yesu Bwana, enendeni vivyo hivyo katika yeye; wenye mizizi na kujengwa ndani yake, na kuthibitishwa katika imani, kama mlivyofundishwa, mkizidi kutoa shukrani.” (Wakolosai 2:6-7)
“Basi, enendeni kama watoto wa nuru, kwa kuwa tunda la nuru ni katika wema wote na haki na kweli.” (Waefeso 5:8-9)

Kupambana na Tamaa za Kidunia

Tamaa za kidunia ni yale mambo yanayotupotosha na kutufanya tuishi kinyume na mapenzi ya Mungu. Ni lazima tujifunze kuzishinda kwa kuimarisha uhusiano wetu na Mungu kupitia maombi, kusoma Neno la Mungu, na kushirikiana na wengine waaminio. Roho Mtakatifu hutusaidia kuona na kutambua uovu na udanganyifu wa tamaa za kidunia na kutupa nguvu ya kuzishinda.

“Basi, ndugu zangu, sisi tuna deni, si kwa mwili, kufuatana na mwili; kwa maana kama mkiishi kufuatana na mwili, mnakufa; bali kama mkiyaangamiza matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi.” (Warumi 8:12-13)
“Wala msiifanye miili yenu kuwa silaha za dhambi kwa kutenda uovu, bali jitoeni wenyewe kwa Mungu kama watu waliotolewa katika wafu na kupewa uhai, na miili yenu iwe silaha za haki kwa Mungu.” (Warumi 6:13)
“Kwa maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome; tukibomoa mawazo na kila kitu kilichoinuka, kijiinue juu ya elimu ya Mungu; tukiteka nyara kila fikra ipate kumtii Kristo.” (2 Wakorintho 10:4-5)

Kutembea Katika Nuru ya Roho

Kutembea katika nuru ya Roho Mtakatifu ni kuishi maisha yaliyojaa matunda ya Roho, kama vile upendo, furaha, amani, uvumilivu, wema, fadhili, uaminifu, upole, na kiasi. Tunapojitahidi kuishi kwa njia hii, tunakuwa mashahidi wa kweli wa Kristo na tunavutia wengine kwake. Ni muhimu kufahamu kwamba hatuwezi kutembea katika nuru ya Roho kwa nguvu zetu wenyewe, bali kwa neema na uwezo wa Roho Mtakatifu ndani yetu.

“Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.” (Wagalatia 5:22-23)
“Nanyi mkivumiliana na kusameheana, mtu akiwa na sababu ya kumlaumu mwenzake; kama Bwana alivyowasamehe ninyi, vivyo nanyi. (Wakolosai 3:13)
“Tazama ni jinsi gani upendo wa Baba alivyotupa, kwamba tuitwe watoto wa Mungu; na ndivyo tulivyo.” (1 Yohana 3:1)

Hitimisho

Kuongozwa na Roho Mtakatifu ni wito wa kila Mkristo. Ni mwaliko wa kuacha maisha yetu yaongozwe na Mungu, na kuishi kulingana na mapenzi yake. Tamaa za kidunia ni kikwazo kikubwa kwa uhusiano wetu na Mungu, lakini kwa nguvu na mwongozo wa Roho Mtakatifu, tunaweza kuzishinda na kuishi maisha yaliyojaa matunda ya Roho. Tuishi maisha ya kuongozwa na Roho, tukijua kwamba Mungu yupo nasi na anatupatia nguvu ya kushinda kila jaribu na changamoto.

Nguvu na Umuhimu wa Upendo

Utangulizi

Katika fadhila zote, upendo ndio unaonyesha uwepo wa fadhila nyingine

Upendo ni Amri kubwa kuliko zote

Upendo ni Utimilifu wa Sheria

Upendo ni Utakatifu

Upendo ni Ukamilifu

Upendo unazaa umoja

Upendo unadumisha Amani

Upendo ni Kila Kitu

Nguvu na Umuhimu wa Upendo katika Maisha ya Kikristo

Katika maandiko ya Kikristo, upendo una nafasi ya pekee na una nguvu kubwa sana katika kuonyesha uwepo wa fadhila nyingine zote. Upendo ni msingi wa kila tendo jema na ni kiini cha imani yetu. Hebu tuangalie kwa undani jinsi upendo unavyojidhihirisha katika nyanja mbalimbali za maisha yetu ya kiroho na kijamii.

Upendo ni Amri Kuu Kuliko Zote

Yesu Kristo alifundisha kwamba upendo ni amri kuu zaidi kuliko amri zote. Katika Mathayo 22:37-39, Yesu alisema:
“Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote. Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ya kwanza. Na ya pili inafanana na hiyo, Mpende jirani yako kama nafsi yako.” (Mathayo 22:37-39)

Amri hizi mbili zinabeba uzito wa sheria yote na manabii. Upendo kwa Mungu na upendo kwa jirani ni msingi wa maisha ya Kikristo na ni muhimu kwa kufanikisha maisha ya kiroho.

Upendo ni Utimilifu wa Sheria

Mtume Paulo anaeleza kwamba upendo ni utimilifu wa sheria. Katika Warumi 13:8-10, Paulo anasema:
“Msilimane deni lo lote, isipokuwa kupendana; kwa maana ampendaye mwenzake ameitimiza sheria. Kwa maana lile usizini, usiue, usiibe, usitamani, na likiwapo lingine lo lote, linajumlishwa katika neno hili, ya kwamba, Mpende jirani yako kama nafsi yako. Upendo haumfanyii jirani neno baya; basi upendo ndio utimilifu wa sheria.” (Warumi 13:8-10)

Upendo unatimiza sheria kwa sababu hautendi mabaya kwa wengine. Badala yake, upendo unaleta matendo mema na huruma kwa jirani.

Upendo ni Utakatifu

Upendo unahusiana moja kwa moja na utakatifu. Mungu ni upendo (1 Yohana 4:8) na anawaita wafuasi wake kuwa watakatifu kama yeye alivyo mtakatifu. Mtakatifu ni mtu anayefuata amri za Mungu na kuonyesha upendo kwa wengine. Upendo wa kweli unatufanya kuwa kama Mungu kwa matendo na tabia.

Upendo ni Ukamilifu

Yesu aliwafundisha wafuasi wake kuwa wakamilifu kama Baba yao wa mbinguni alivyo mkamilifu. Katika Mathayo 5:48, Yesu alisema:
“Basi, iweni wakamilifu, kama Baba yenu wa mbinguni alivyo mkamilifu.” (Mathayo 5:48)

Ukamilifu huu unafanikiwa kwa njia ya upendo. Tunapopenda bila masharti, tunajitahidi kufikia kiwango cha ukamilifu ambacho Mungu anatamani tuwe nacho.

Upendo Unazaa Umoja

Upendo unaleta umoja miongoni mwa watu. Mtume Paulo aliandika katika Wakolosai 3:14:
“Zaidi ya yote jivikeni upendo, ndio kifungo cha ukamilifu.” (Wakolosai 3:14)

Upendo ni kama gundi inayounganisha watu pamoja na kudumisha umoja katika jamii na kanisa. Kwa upendo, tunavumiliana, tunaelewana, na kushirikiana kwa lengo la kufanikisha kusudi la Mungu.

Upendo Unadumisha Amani

Amani inapatikana kupitia upendo. Mtume Paulo katika Warumi 12:18 alieleza umuhimu wa kuwa na amani na watu wote:
“Kama ikiwezekana, kwa upande wenu, mkae katika amani na watu wote.” (Warumi 12:18)

Upendo unatusaidia kuishi kwa amani na majirani zetu, kuleta maelewano na kuondoa migogoro. Tunapopenda, tunakuwa tayari kusamehe, kuvumilia, na kuleta amani katika mazingira yetu.

Upendo ni Kila Kitu

Upendo ni msingi wa kila kitu katika maisha ya Kikristo. Mtume Paulo alisisitiza umuhimu wa upendo katika 1 Wakorintho 13:1-3:
“Nijaposema kwa lugha za wanadamu na za malaika, kama sina upendo, nimekuwa shaba iliayo, au upatu uvumao. Tena nijapokuwa na kipawa cha unabii, na kujua siri zote, na maarifa yote; nijapokuwa na imani timilifu kiasi cha kuweza kuhamisha milima, kama sina upendo, si kitu. Tena nijapowapa maskini mali yangu yote, na nijapojitoa mwili wangu nichomwe moto, kama sina upendo, hainifaidii kitu.” (1 Wakorintho 13:1-3)

Bila upendo, matendo yetu yote ni bure. Upendo unatuwezesha kufanikisha maisha ya kiroho na kutimiza mapenzi ya Mungu kwa uaminifu.

Hitimisho

Upendo ni nguvu kuu inayojidhihirisha katika fadhila zote. Kwa upendo, tunatimiza sheria, tunakuwa watakatifu, tunakamilika, tunaleta umoja, na kudumisha amani. Upendo ni kila kitu katika maisha ya Kikristo na ni njia ya pekee ya kuonyesha uwepo wa Mungu ndani yetu. Kwa hivyo, na tujitahidi kuishi kwa upendo, tukiwa na uhakika kwamba tunafuata mapenzi ya Mungu na kutimiza wito wetu kama wafuasi wa Kristo.

Mungu ni mwenye upendo, Huruma na Rehema hasa kwa Wenye dhambi

Mungu ni mwenye upendo Huruma na Rehema hasa kwa Wenye dhambi.
Mungu yupo tayari kumsikiliza mtu yeyote mwenye dhambi kama ameutambua, amekiri na Kutubu makosa yake.

Mungu akishamsamehe mtu uovu wake anambariki.

Hakuna mtu ambaye hatasamehewa na Mungu kama Ametubu, amekiri na Kuomba msamaha wa makosa yake.

Mungu wakati wote yupo akisubiri wenye dhambi waende kwake kwa Toba ili awasemehe.

Lakini tatizo ni la watu wengi wanazani kua wakati wakiwa dhambini Mungu anakua amewakasirikia, Ukweli ni kwamba unapokua dhambini Mungu anakuonea Huruma na anatamani umrudie yeye.

Unaweza ukawa umetenda dhambi lakini hujamuasi Mungu, Kumuasi Mungu ni pale Unapoona kuwa Mungu hana nafasi katika maisha yako tena. Lakini ukiwa dhambini huku unamtumaini Yeye basi bado upo katika njia yake kwa kuwa yeye ni sawa na Baba kwako na kumkosea Baba yako sio kumuasi kama tuu utarudi Kuomba msamaha na Kuheshimu nafasi yake katika maisha yako.

Upendo wa Mungu Kwa Wenye Dhambi

Mungu ni mwenye upendo, huruma, na rehema hasa kwa wenye dhambi. Biblia inatufundisha kwamba Mungu hachoki kuwakaribisha wenye dhambi wanaotubu kwa dhati. Mungu yupo tayari kumsikiliza mtu yeyote mwenye dhambi ambaye ameutambua, amekiri, na kutubu makosa yake. Huruma na rehema zake haziishi kamwe, na anasubiri kwa shauku kubwa kuona wanae wakirudi kwake kwa toba.

“Basi, Bwana, Mungu wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, mwingi wa rehema na kweli.” (Kutoka 34:6)
“Acha waovu na watu wanaodharau sheria wamrudie Bwana, naye atawahurumia. Warudi kwa Mungu wetu, maana atawasamehe kabisa.” (Isaya 55:7)
“Wote wanaokuja kwangu sitawatupa nje kamwe.” (Yohana 6:37)

Msamaha na Baraka za Mungu

Mungu akishamsamehe mtu uovu wake, anambariki. Hakuna mtu ambaye hatasamehewa na Mungu kama ametubu, amekiri, na kuomba msamaha wa makosa yake. Hii inaonyesha upendo wa ajabu wa Mungu kwa wanadamu wake, upendo ambao haujali ukubwa wa dhambi, bali ukubwa wa toba ya mtu.

“Tubu basi, geuka ili dhambi zako zifutwe.” (Matendo 3:19)
“Na dhambi zao na uasi wao sitaukumbuka tena kamwe.” (Waebrania 10:17)
“Maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitakumbuka tena.” (Yeremia 31:34)

Mungu Anasubiri Wenye Dhambi Warudi Kwake

Mungu wakati wote yupo akisubiri wenye dhambi waende kwake kwa toba ili awasamehe. Huu ni ujumbe wa matumaini kwa kila mtu anayehisi ameanguka mbali na neema ya Mungu. Mungu ni kama baba anayesubiri mwanae mpendwa arudi nyumbani. Ana shauku ya kumsamehe na kumrejesha kwenye familia ya kiroho.

“Bwana si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa fadhili, husamehe uovu na makosa, lakini hatahesabu kuwa hana hatia mwenye hatia.” (Hesabu 14:18)
“Mkiungama dhambi zenu, yeye ni mwaminifu na mwenye haki, atasamehe dhambi zenu na kuwasafisha na udhalimu wote.” (1 Yohana 1:9)
“Furahini pamoja nami, kwa sababu mwana wangu alikuwa amekufa, naye amerudi tena kuwa hai; alikuwa amepotea, naye ameonekana.” (Luka 15:24)

Wakati wa Dhambi: Huruma ya Mungu

Tatizo ni kwamba watu wengi wanadhani kuwa wakati wakiwa dhambini Mungu anakua amewakasirikia. Ukweli ni kwamba unapokuwa dhambini, Mungu anakuonea huruma na anatamani umrudie yeye. Unaweza ukawa umetenda dhambi lakini hujamuasi Mungu, Kumuasi Mungu ni pale unapomkataa kabisa na kuona kuwa hana nafasi katika maisha yako tena.

“Nanyi mtarudi, na kuona tofauti kati ya wenye haki na waovu, kati ya yeye amtumikiaye Mungu na yeye asiyemtumikia.” (Malaki 3:18)
“Hata kama dhambi zenu ni nyekundu sana zitakuwa nyeupe kama theluji.” (Isaya 1:18)
“Bwana ni mwingi wa huruma na neema, si mwepesi wa hasira, ana wingi wa fadhili. Hata mshika hasira yake daima, wala hatawakemea milele.” (Zaburi 103:8-9)

Kurejea kwa Mungu kwa Toba

Ukiwa dhambini huku unamtumaini Mungu, basi bado upo katika njia yake kwa kuwa yeye ni sawa na baba kwako. Kumkosea Baba yako sio kumuasi kama tu utarudi kuomba msamaha na kuheshimu nafasi yake katika maisha yako. Toba ya kweli inarejesha uhusiano wetu na Mungu, na anatupokea kwa mikono miwili.

“Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, ndivyo Bwana anavyowahurumia wamchao.” (Zaburi 103:13)
“Nikaribieni mimi, nami nitawakaribia ninyi, asema Bwana.” (Yakobo 4:8)
“Heri wenye huruma, maana hao watapata rehema.” (Mathayo 5:7)

Kwa hivyo, tunapokuwa dhambini, tunapaswa kukumbuka kwamba Mungu anatuona kwa macho ya huruma na upendo. Yupo tayari kutusamehe na kutubariki, mradi tu tutambue dhambi zetu, tukiri, na kutubu kwa dhati. Tunapomrudia Mungu kwa toba, tunapokea huruma na neema zake zisizo na kipimo.

Siri ya Yesu: Mwangaza Wa Maisha

Siri ni hii, Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza. Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu. Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu. Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Kujikabidhi Kwa Yesu Kristu Yeye Aliye Mwangaza Wa Maisha

Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza

Giza na Mwanga havichangamani. Yesu hakai pamoja na uovu.
Giza haliwezi kuzidi Mwanga. Uovu hauwezi kumzidi Yesu.
Mwanga ukija giza linaondoka. Yesu akija uovu unakwisha.

Yesu Kristu ni mwangaza wa maisha yetu, akiwepo giza lote hutoweka.
Yesu akiwepo hakuna haja ya kufukuza giza bali giza litatoweka Lenyewe.

Unapomkaribisha Yesu katika maisha yako umekaribisha mwanga katika maisha yako na utashinda dhambi na uovu kwa kuwa Yesu aliye mwanga atavifutilia mbali.

Kikubwa ni kumkaribisha Yesu katika maisha yako na kumruhusu atawale Maisha yako na kila kitu katika maisha yako. Ukiweza kuachilia yote kwa Bwana Yesu na kumpa maisha yako basi utashinda uovu/dhambi. Vile unavyojiweka karibu na Yesu ndivyo unavyoshinda dhambi na uovu wote.

Kumkabidhi Yesu Maisha ni Kuamua kuishi kulingana na Mafundisho yake, kuachilia yote katika maongozi yake, kumshirikisha Yesu kwenye kila kitu katika maisha yako na Kuwa mkweli na muwazi mbele ya Yesu katika kila kitu.

Unapomkabidhi Yesu Maisha yako na vyote ulivyonavyo yeye huyatakatifuza na kuyafanya yawe kama yanavyotakiwa kuwa kitakatifu.

Changamoto kubwa kwa Wakristu ni kushindwa kujiweka Mikononi mwa Yesu kwa kuachilia yote na kukabidhi yote kwake. Wengi wanashindwa kufanya hivyo kwa sababu ya ubinafsi na uchu wa kusimama wenyewe. Wengine wanashindwa kwa sababu ya kukosa Imani. Hawana uhakika kwamba wanachokifanya wanakifanya kweli.

Lakini ukiweza kweli kumkabidhi Yesu Maisha yako, kila kitu kinakua sawa na utafanikiwa kwenye kila kitu. Utaanza kuona unashinda uovu na dhambi kulingana na vile unavyojikabidhi na kujiachilia kwa Yesu.

Anza leo kujikabidhi kwa yesu kwa kiasi kile unachoweza. Yesu anaelewa ubinadamu na madhaifu yetu. Atakusaidia. Hata kama kuna wakati unaweza kujikabidhi kwake na kisha unaanguka tena, yeye ni mwenye huruma na ni mwelewa haswa kuhusu hali yako, atakusaidia na kukuwezesha. Weka nia ya kujikabidhi kwake na kisha utaendelea kidogo kidogo mpaka utajikuta umejikabidhi mikononi kwake kabisa.

KUMBUKA: Yesu ni Mwanga na Uovu ni giza, mwanga ukiwepo giza halibaki linaondoka. Hata siku moja Giza haliwezi kuuzidi mwanga

Uwe na Imani basi, Mtumainie Yesu Kristu atakushindia uovu.

Yesu ndiyo dawa ya uovu na dhambi, kila unapoanguka dhambini mkimbilie yeye naye atakusamehe na kukuwezesha kushinda dhambi na uovu. Usichoke, kila siku jaribu na kujaribu mpaka utashinda.

Nami nakuombea kwa Jina Takatifu la Yesu, Akushindie Uovu na dhambi

Unafahamu kuwa Imani ni Cheti cha Kuweza Kupata Yote?

Utangulizi

Imani ni kuwa na uhakika hata kwa mambo yasiyoonekana na yasiyowezekana. Ni kujua au kutarajia kwa uhakika kwa mambo ambayo bado hayajawa bayana (wazi) kuwa yapo au yatafanyika.

Kwa Imani Kila Kitu Kinawezekana. Kwa Sala na kwa Matendo.

Yesu Kristu anatufundisha tuwe na Imani kupitia Mfano huu;

18Yesu alipokuwa anarudi mjini asubuhi na mapema, aliona njaa. 19Akauona mtini mmoja kando ya njia, akauendea; lakini aliukuta hauma chochote ila majani matupu. Basi akauambia, “Usizae tena matunda milele!” Papo hapo huo mtini ukanyauka.

20Wanafunzi walipouona walishangaa wakisema, “Kwa nini mtini huu umenyauka ghafla?” 21Yesu akawajibu, “Kweli nawaambieni, kama mkiwa na imani bila kuwa na mashaka, mnaweza si tu kufanya hivyo, bali hata mkiuambia mlima huu: Ng’oka ukajitose baharini, itafanyika hivyo. 22Na mkiwa na imani, chochote mtakachoomba katika sala, mtapata.”
Mathayo 21:18-22

Basi Ili tuweze kuwa na Imani tumuombe Mungu atujalie Imani. Tuombe tujaliwe fadhila ya Imani hasa Tunaposali. Vile vile tumwombe Mungu atujalie Imani katika yale yote tunayoyafanya.

Tuombe hasa Imani isiyokuwa na Mashaka. Mashaka na Kusita sita ndiyo adui mkubwa wa Imani.

Imani ni Cheti cha Kuweza Kupata Yote

Imani ni kuwa na uhakika hata kwa mambo yasiyoonekana na yasiyowezekana. Ni kujua au kutarajia kwa uhakika kwa mambo ambayo bado hayajawa bayana kuwa yapo au yatafanyika. Imani ni msingi wa maisha ya Kikristo, na ni muhimu kuelewa jinsi inavyofanya kazi na jinsi inavyoweza kubadilisha maisha yetu. Katika maisha ya kiroho, imani inaweza kulinganishwa na cheti kinachokupa uwezo wa kupokea baraka na neema zote kutoka kwa Mungu. Kama cheti kinavyokupa sifa na uwezo wa kupata kitu, vivyo hivyo, imani inatupa uwezo wa kupokea kutoka kwa Mungu.

Imani ni Cheti cha Kuweza Kupata Yote

Kama vile cheti kinavyothibitisha sifa zako za kupokea kitu fulani, imani yetu inathibitisha sifa zetu mbele za Mungu na kutupa uwezo wa kupokea baraka zake. Bila imani, ni vigumu kupokea kutoka kwa Mungu kwa sababu imani ndio msingi wa uhusiano wetu naye. Waebrania 11:1 inasema:

“Basi imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo, ni bayana ya mambo yasiyoonekana.” (Waebrania 11:1)

Imani inatufanya tuwe na matumaini na kuamini kwamba mambo ambayo tunatarajia yatatimia, hata kama hatuyaoni bado kwa macho yetu ya kawaida.

Imani Inafanya Kila Kitu Kinawezekana

Kwa imani, hakuna lisilowezekana. Imani inafanya miujiza iwe sehemu ya maisha yetu ya kila siku. Kwa sala na matendo, imani yetu inadhihirika na kuwa na nguvu za kutenda mambo makubwa. Yesu Kristo anatufundisha kuwa na imani kupitia mfano huu kutoka Mathayo 21:18-22:

“Yesu alipokuwa anarudi mjini asubuhi na mapema, aliona njaa. Akauona mtini mmoja kando ya njia, akauendea; lakini aliukuta hauna chochote ila majani matupu. Basi akauambia, ‘Usizae tena matunda milele!’ Papo hapo huo mtini ukanyauka. Wanafunzi walipouona walishangaa wakisema, ‘Kwa nini mtini huu umenyauka ghafla?’ Yesu akawajibu, ‘Kweli nawaambieni, kama mkiwa na imani bila kuwa na mashaka, mnaweza si tu kufanya hivyo, bali hata mkiuambia mlima huu: Ng’oka ukajitose baharini, itafanyika hivyo. Na mkiwa na imani, chochote mtakachoomba katika sala, mtapata.'” (Mathayo 21:18-22)

Yesu anatufundisha kuwa na imani thabiti bila mashaka. Anatushawishi kuelewa kwamba kwa imani, tunaweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu, hata kuhamisha milima.

Kuomba Imani kutoka kwa Mungu

Ili tuweze kuwa na imani, tunapaswa kumwomba Mungu atujalie imani. Imani ni zawadi kutoka kwa Mungu, na tunahitaji kumwomba atupe fadhila hii tunaposali. Kwa kumwomba Mungu, tunapata nguvu na uhakika wa kuamini bila kusita.

Yakobo 1:6-7 inasema:

“Lakini aombe kwa imani, pasipo shaka yoyote; maana mwenye shaka ni kama wimbi la bahari lililochukuliwa na upepo na kupeperushwa huku na huku. Mtu kama huyo asidhani ya kuwa atapokea kitu kwa Bwana.” (Yakobo 1:6-7)

Hii inatukumbusha umuhimu wa kuomba kwa imani isiyokuwa na mashaka. Mashaka na kusita-sita ni adui mkubwa wa imani, na ni lazima tuwe na imani kamili ili tuweze kupokea kutoka kwa Mungu.

Imani Katika Sala na Matendo

Imani yetu inapaswa kudhihirika si tu katika sala zetu bali pia katika matendo yetu ya kila siku. Tunapomwomba Mungu kwa imani, tunapaswa pia kuchukua hatua kwa imani, tukiamini kwamba Mungu atatenda. Yakobo 2:17 inasema:

“Vivyo hivyo na imani, isipokuwa ina matendo, imekufa nafsini mwake.” (Yakobo 2:17)

Imani bila matendo ni imani isiyo na uhai. Tunapomwomba Mungu kwa imani, tunapaswa pia kuwa tayari kuchukua hatua kwa kuamini kwamba Mungu atatenda kupitia juhudi zetu.

Kuomba Imani Thabiti

Tunapomwomba Mungu atujalie imani, ni muhimu tuombe imani thabiti isiyokuwa na mashaka. Yesu alitufundisha kwamba tunaweza kufanya mambo makubwa kama tu tuna imani bila mashaka. Kwa hiyo, tuombe kwa bidii ili tujaliwe na Mungu imani inayoweza kuhamisha milima, imani inayoweza kufanya mambo yasiyowezekana yawezekane.

Mifano Halisi ya Imani katika Biblia

Biblia imejaa mifano ya watu waliojawa na imani na jinsi walivyoweza kupata mambo makubwa kupitia imani yao. Hapa kuna mifano sita ya imani kutoka katika Biblia:

  1. Ibrahimu:
    Ibrahimu alionyesha imani kuu kwa Mungu alipoambiwa kumtoa mwanawe Isaka kama sadaka. Alikuwa tayari kumtii Mungu, akiamini kwamba Mungu anaweza kumfufua Isaka kutoka kwa wafu. Imani yake ilimfanya awe baba wa mataifa mengi. (Waebrania 11:17-19)
  2. Musa:
    Musa alionyesha imani alipowaongoza Waisraeli kutoka utumwani Misri, licha ya changamoto nyingi alizokutana nazo. Aliamini ahadi za Mungu na kuamini kwamba Mungu atawatua kwenye nchi ya ahadi. (Waebrania 11:24-29)
  3. Yoshua na Yeriko:
    Yoshua alionyesha imani alipowaongoza Waisraeli kuzunguka ukuta wa Yeriko kwa siku saba kama alivyoamriwa na Mungu. Siku ya saba, ukuta wa Yeriko ulianguka, na Waisraeli walishinda mji huo. (Yoshua 6:1-20)
  4. Danieli:
    Danieli alionyesha imani kubwa alipoendelea kumwomba Mungu licha ya amri ya mfalme ambayo ilipiga marufuku maombi. Aliwekwa kwenye tundu la simba, lakini Mungu alimlinda na simba hawakumdhuru. (Danieli 6:10-23)
  5. Mwanawake aliotokwa na Damu:
    Mwanamke aliyekuwa akitokwa na damu kwa miaka kumi na miwili alionyesha imani kubwa alipogusa vazi la Yesu akiamini kwamba ataponywa. Imani yake ilimponya mara moja. (Marko 5:25-34)
  6. Petro:
    Petro alionyesha imani alipomwomba Yesu amruhusu kutembea juu ya maji. Alipoanza kutembea juu ya maji kuelekea kwa Yesu, aliona nguvu za Mungu. Ingawa alianza kuzama alipokuwa na mashaka, imani yake ilimfanya aweze kutembea juu ya maji kwa muda. (Mathayo 14:28-31)

Hitimisho

Imani ni cheti cha kuweza kupata yote. Kwa imani, tunaweza kuona mambo makubwa yakitendeka katika maisha yetu. Imani inatufanya tuwe na uhakika wa mambo yasiyoonekana na yasiyowezekana. Tunapaswa kumwomba Mungu atupe imani thabiti, na imani hiyo inapaswa kudhihirika katika sala na matendo yetu ya kila siku. Kwa kumtumaini Mungu bila mashaka, tunaweza kufanya mambo makubwa na ya ajabu, tukijua kwamba kwa imani, kila kitu kinawezekana.

Kwa nini Mungu hatendi mpaka umwambie au umuombe? Kwa nini tusali?

Utangulizi

Mungu anapenda kutenda jambo baada ya mtu kumuomba/kusali ili mtu aelewe Ukuu wa Mungu na ili Mungu atukuzwe.

Kama kila kitu mtu anachotaka kingekua kinafanyika, Binadamu asingemkumbuka Mungu na Mungu asingetukuzwa

Kwa hiyo, tunasali kumuomba Mungu atende ili atukuzwe

Mungu anasubiri umuombe akutendee ili akuonyeshe Upendo nguvu na Uwezo wake

Mungu Anapenda Kutenda Jambo Baada ya Mtu Kumuomba: Ukuu na Utukufu wa Mungu Katika Sala

Mungu ni mwingi wa upendo, mwenye nguvu na uwezo usio na kipimo. Anapenda kutenda mambo makuu katika maisha yetu, lakini mara nyingi hufanya hivyo baada ya sisi kumuomba kwa sala. Kwa nini Mungu huchagua njia hii? Ni kwa sababu anataka tuweze kuelewa ukuu wake na ili jina lake litukuzwe duniani.

Mungu Anataka Tuelewe Ukuu Wake

Sala ni njia ya mawasiliano kati ya mwanadamu na Mungu. Wakati tunapomwomba Mungu atende jambo katika maisha yetu, tunajenga daraja la mawasiliano na uhusiano wa karibu naye. Mungu anapotenda baada ya sisi kumuomba, anatufundisha kutambua na kuelewa ukuu wake. Tunapomshuhudia akijibu sala zetu, tunaweza kuona jinsi anavyoweza kushinda changamoto zetu, kutupatia mahitaji yetu na kutulinda. Hii hutusaidia kuelewa kwa undani zaidi jinsi alivyo mkuu na mwenye uwezo wote. Kama ilivyoandikwa katika Yeremia 33:3:

“Niite, nami nitakuitikia, nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.” (Yeremia 33:3)

Mungu Anataka Atukuzwe

Mungu hutenda mambo makuu baada ya sala zetu ili jina lake litukuzwe. Kama kila kitu tunachotaka kingetokea bila ya kumuomba Mungu, tusingemkumbuka na kumsifu. Mwanadamu kwa asili ana tabia ya kusahau pale mambo yanapokuwa mazuri na rahisi. Lakini tunapokuwa na haja, tunaponyenyekea na kumuomba Mungu kwa sala, na Yeye kujibu, inatufanya tutambue kuwa tunamhitaji kila wakati. Hili linatufanya tumtukuze kwa sababu ya matendo yake makuu. Zaburi 50:15 inasema:

“Uite mimi siku ya taabu; nitakuokoa, nawe utanitukuza.” (Zaburi 50:15)

Kumbukumbu ya Mungu Katika Maisha ya Binadamu

Kama kila kitu mtu anachotaka kingekuja bila ya kumwomba Mungu, tungeweza kujisahau na kuishi maisha yasiyo na shukrani na utambuzi wa uwepo wa Mungu. Sala inatufanya tukumbuke kuwa Mungu ndiye chanzo cha baraka zetu zote. Tunapomuomba na Yeye kujibu, tunatambua kuwa hatuwezi kufanya chochote bila msaada wake. Hii inatufanya tumtukuze na kumshukuru kwa upendo wake na neema zake. Mithali 3:5-6 inatukumbusha:

“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe; katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako.” (Mithali 3:5-6)

Sala Inamwinua Mungu

Tunaposali, tunamwinua Mungu na kumwomba atende kwa ajili ya utukufu wake. Hii ina maana kwamba tunatambua kuwa sisi ni viumbe dhaifu wenye kumhitaji Muumba wetu katika kila jambo. Tunapomuomba Mungu atende mambo makuu katika maisha yetu, tunampa nafasi ya kuonyesha upendo, nguvu na uwezo wake kwetu. Matendo yake katika kujibu sala zetu yanatufanya tuimbe sifa zake na kushuhudia wema wake kwa wengine. Yakobo 4:8 inatuhimiza:

“Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.” (Yakobo 4:8)

Mungu Anasubiri Umuombe

Mungu anasubiri kwa upendo na subira ili tuje kwake kwa sala. Anatamani kutenda mambo makuu katika maisha yetu, lakini anataka tuonyeshe imani na unyenyekevu wetu kwa kumuomba. Anasubiri tumuombe ili aweze kutuonyesha upendo wake, nguvu zake na uwezo wake wa kutushinda. Sala zetu zinamwonyesha Mungu kwamba tunamtambua na kumtumaini kwa kila jambo. Yesu alisema katika Mathayo 7:7-8:

“Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa. Kwa maana kila aombaye hupokea; naye atafutaye huona; naye abishaye atafunguliwa.” (Mathayo 7:7-8)

Hitimisho

Mungu anapenda kutenda jambo baada ya mtu kumuomba kwa sababu anataka tuweze kuelewa ukuu wake na ili jina lake litukuzwe. Sala zetu ni ishara ya imani na utegemezi wetu kwake, na Yeye kwa upendo anasubiri atuonyeshe nguvu zake na uwezo wake kupitia majibu ya sala zetu. Tunaposali na kumuomba Mungu atende katika maisha yetu, tunamtukuza na kumwinua juu, tukijua kwamba hatuwezi chochote bila msaada wake. Hivyo basi, tusikose kumwomba Mungu kwa kila jambo, tukijua kwamba anatupenda na anasubiri kutenda makuu katika maisha yetu kwa ajili ya utukufu wake.

Tafakari na uchukue muda wa kusali kila siku, na utambue kwamba Mungu yuko tayari kutenda maajabu katika maisha yako. Mtukuze kwa kila jambo, na uone jinsi atakavyofungua milango na kutenda mambo makuu kwa ajili ya utukufu wake.

Mambo ya kutafakari unapokuwa katika shida kubwa, unapoelekea kukata tamaa

Tafakari Kuhusu Wakati wa Shida

Leo tunatafakari kuhusu wakati wa shida. Maisha ya mtu yanabadilika wakati wowote kwa namna yoyote. Yanaweza yakawa mazuri mpaka ukashangaa au yanaweza yasiwe mazuri kama unavyotarajia. Yote hayo ni sehemu ya maisha.

“Nimejifunza kuwa na kuridhika na hali yoyote niliyo nayo. Najua jinsi ya kuwa na hali duni, najua jinsi ya kuwa na hali ya wingi. Katika hali zote na mambo yote, nimefundishwa jinsi ya kushiba na jinsi ya kuwa na njaa, jinsi ya kuwa na wingi na jinsi ya kupungukiwa.” (Wafilipi 4:11-12)

Kumbuka Wakati wa Matatizo

Unapokua na matatizo makubwa katika maisha, kumbuka haya yafuatayo:

1. Mungu Yupo na Anakuona

Mungu yupo na anakuona. Mwambie matatizo yako, huo ndio wakati wake wa kuonyesha uwepo wake na nguvu zake. Wewe tu kusema na Mungu kwa utayari na uwazi, hivyo utakao kuwezesha kupata au kutatua tatizo lako.

“Naomba BWANA akujibu siku ya dhiki, jina la Mungu wa Yakobo likuinue.” (Zaburi 20:1)
“Mchungueni Bwana na nguvu zake, utafuteni uso wake siku zote.” (1 Mambo ya Nyakati 16:11)
“Bwana ni ngome yao katika wakati wa shida.” (Zaburi 37:39)

2. Matendo na Maamuzi Yako

Maneno, vitendo, na maamuzi yako ndiyo yanaweza yakawa njia ya kutatua matatizo yako. Usiogope kuchukua hatua zinazohitajika. Tafuta hekima na uongozi kutoka kwa Mungu katika kila hatua unayochukua.

“Yehova atakuelekeza siku zote, na kukusibisha katika nchi yenye ukame, na kukuimarisha mifupa yako. Utakuwa kama bustani iliyomwagiliwa, na kama chemchemi ya maji ambayo maji yake hayatapungua.” (Isaya 58:11)
“Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, wala usizitegemee akili zako mwenyewe. Katika njia zako zote mkiri yeye, naye atayanyosha mapito yako.” (Mithali 3:5-6)
“Nawafundisha njia iliyo njema na adili; msiiachilie sheria yangu.” (Mithali 4:11-13)

3. Matatizo Hayako Sio Mwisho wa Maisha

Tatizo lako sio mwisho wa maisha yako, sio mwisho wa yote mazuri ya jana, leo, na kesho. Bado unayo mambo mengi mazuri yanakungojea. Mungu anapanga mambo mazuri kwa ajili ya wale wanaompenda na kumtumainia.

“Maana ninajua mipango niliyo nayo kwa ajili yenu, asema Bwana, ni mipango ya amani na si ya mabaya, ili niwape tumaini katika siku zenu za usoni.” (Yeremia 29:11)
“Na tusiache kutenda mema, kwa maana tutavuna kwa wakati wake tusipozimia roho.” (Wagalatia 6:9)
“Bwana atakamilisha mambo yangu; Ee Bwana, fadhili zako ni za milele; usiache kazi ya mikono yako.” (Zaburi 138:8)

4. Uangalizi wa Tatizo

Kumbuka tatizo lako linaweza likawa sio kubwa ila wewe ndio unaliona kubwa. Wewe sio wa kwanza kuwa na tatizo kama hilo, wengine hayo ndo maisha yao. Angalia kwa mtazamo wa matumaini na uombe hekima ya Mungu ili uweze kuona njia ya kutoka kwenye tatizo lako.

“Mkipungukiwa na hekima, na aombe kwa Mungu, naye atampa kwa ukarimu wala hachukii.” (Yakobo 1:5)
“Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku.” (2 Wakorintho 4:16)
“Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” (Wafilipi 4:13)

Kwa hivyo, wakati wa shida, ni muhimu kujikumbusha kwamba Mungu yupo, anakusikiliza, na yupo tayari kukusaidia. Usiache matumaini, endelea kuamini na kutenda kwa hekima na imani, ukijua kwamba matatizo yako ni sehemu ya safari yako ya kiroho na Mungu anapanga mazuri mbele yako.

Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About