Mafundisho ya Msingi ya Kanisa Katoliki: Makala za Katoliki

Ibada ya Huruma ya Mungu: Njia ya Ukarabati na Uongofu

Ibada ya Huruma ya Mungu: Njia ya Ukarabati na Uongofu.

Ndugu yangu, Ibada ya Huruma ya Mungu ni njia ya kuishi kwa imani na upendo kwa Mungu wetu mwenye rehema. Ibada hii ilipokelewa kutoka kwa Yesu Kristo mwenyewe kupitia kwa mtakatifu Maria Faustina Kowalska, ambaye alipokea ujumbe huu kutoka kwa Mungu mwenyewe.

Ibada ya Huruma ya Mungu inatualika kuonesha huruma na upendo kwa wengine kama vile tunavyotaka upendo na huruma kutoka kwa Mungu. Kupitia ibada hii, tunaweza kupata ukarabati wa kiroho na uongofu kwa sababu Mungu anatualika kumsamehe na kusameheana na wengine.

Hapa kuna mambo ya kuzingatia kuhusu Ibada ya Huruma ya Mungu:

  1. Mungu ni mwenye huruma na upendo. Kupitia Ibada ya Huruma ya Mungu, tunaweza kujifunza juu ya huruma hii na upendo wake usiotarajia malipo yoyote. "Bwana ni mwenye huruma na neema, si mwepesi wa hasira, mkubwa wa rehema" (Zaburi 145:8).

  2. Ibada hii inatualika kusali kwa ajili ya wengine, hasa wale wanaohitaji huruma ya Mungu. Kupitia sala, tunaweza kuwaombea wengine ili waweze kupata ukarabati na uongofu pia.

  3. Tunaalikwa kusameheana kama vile tunavyotaka Mungu atusamehe. "Na mkiwasamehe watu makosa yao, Baba yenu wa mbinguni atawasamehe ninyi" (Mathayo 6:14).

  4. Ibada hii inatualika kujinyenyekeza na kumwomba Mungu msamaha wa dhambi zetu. "Kama tunakiri dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu na kutusafisha na uovu wote" (1 Yohana 1:9).

  5. Kupitia Ibada ya Huruma ya Mungu, tunaweza kupata msamaha wa dhambi zetu kabla ya kifo chetu. "Kwa maana kama unavyofanya, ndivyo atakavyokufanyia" (Mathayo 7:2).

  6. Tunaweza kupata msamaha kwa kina dhambi zetu kupitia sakramenti ya kitubio. "Bwana akiruhusu dhambi zetu ziondoke, basi ni kwa kusamehe" (Zaburi 103:3).

  7. Katika Ibada hii, tunafundishwa kumwamini Mungu kwa imani kamilifu na kutegemea huruma yake. "Nimeweka tumaini langu kwa Bwana, na hivyo nafsi yangu inamngojea" (Zaburi 130:5).

  8. Ibada ya Huruma ya Mungu inatualika kuchukua hatua ya kuishi kwa upendo na huruma kwa wengine. "Kwa maana kila mtu ajitukuze mwenyewe, lakini hatajifikiria juu ya mwenzake" (Warumi 12:10).

  9. Kwa kupitia Ibada ya Huruma ya Mungu, tunaweza kuwa mashuhuda wa upendo na huruma ya Mungu kwa wengine. "Ninyi ndio nuru ya ulimwengu… ili wote waone matendo yenu mema, na kumtukuza Baba yenu aliye mbinguni" (Mathayo 5:14-16).

  10. Ibada ya Huruma ya Mungu inatualika kumkaribia Mungu kwa moyo safi na wazi ili tupate kujipatanisha na Yeye. "Kumbuka Bwana, rehema yako na fadhili zako, maana zimekuwako tangu milele" (Zaburi 25:6).

Kwa kuhitimisha, Ibada ya Huruma ya Mungu ni njia ya kuishi kwa imani na upendo kwa Mungu wetu mwenye rehema. Kupitia ibada hii, tunaweza kupata ukarabati wa kiroho na uongofu. Kwa kufuata mafundisho haya ya huruma na upendo, tunaweza kuwa mashuhuda wa wema na upendo wa Mungu kwa wengine. Tumwombe Mungu atusaidie kukua katika ukaribu na upendo wake, na atusaidie kuwa na moyo wa huruma na upendo kwa wengine. Je, unafikiria nini kuhusu Ibada ya Huruma ya Mungu?

Mambo ya kufahamu katika kipindi cha kwaresima

Nini maana ya Kwaresima?

Kwa Kilatini na Kiitaliano neno Kwaresima lilimaanisha “40” yaani siku 40 za kufunga za wiki kati ya Jumatano ya Majivu hadi Jumamosi Kuu. Kwa Kijerumani Kwaresima maana yake “Kipindi cha kufunga.”

Kwaresima ilianzaje?

Kabla ya kuona Kwaresima jinsi ilivyoanza, ni vizuri kuongea kidogo kuhusu Sikukuu ya Pasaka ili tuweze kupata mwanga wa kuelewa mwanzo wa kipindi hiki muhimu cha Kwaresima.
Habari Njema yatuambia kwamba YESU KRISTO alifufuka “Siku ya kwanza ya juma.” “Hata sabato ilipokwisha, ikipambazuka siku ya kwanza ya juma, Mariamu Magdalene, na Mariamu yule wa pili, walikwenda kulitazama kaburi.” (Mt.28:1) Hii ni kwasababu Wakristo walianza kukutana pamoja kwa sikukuu ya ufufuko wa BWANA kila wiki sio Jumamosi kama Wayahudi, bali siku iliyo fuata. “Hata siku ya kwanza ya juma, tulipokuwa tumekutana ili kumega mkate, Paulo akawahutubu, akiazimu kusafiri siku ya pili yake, naye akafuliza -`maneno yake hata usiku wa manane.” (Mdo.20:7). “Siku ya Kwanza ya juma kila mtu kwenu na aweke akiba kwake, kwa kadiri ya kufanikiwa kwake: ili kwamba michango isifanyike hapo nitakapokuja.” (1Kor.16:2), siku ambayo Warumi waliita “Siku ya Jua”. Mara moja jina hilo lilibadilika na kuwa “Siku ya BWANA”
Kanisa la mwanzoni halikusherehekea sikukuu kama vile Noel, Sikukuu kwa heshima ya Mama Bikira Maria au sikukuu yeyote ile. Kulikuwepo na adhimisho la ufufuko wa BWANA kila wiki na hakuna zaidi.
Miaka mingi ikapita kanisa likiwa katika hali hii. Baadaye kulikuwepo na hitaji la kusherehekea tukio la kiini cha imani yetu kwa namna ya pekee. Wakristo waliona umuhimu wa kuwa na muda kwa sikukuu ya kwanza kati ya sikukuu zao yaani “Jumapili ya Pasaka”, ambayo ilifikiriwa kama “Mama wa Jumapili zote”, “Mama wa skikukuu zote”. Waliiona sikukuu hiyo kama “Malkia wa sikukuu zote, wa Jumapili zote, na kiujumla kama Malkia wa siku zote za mwaka. Tangu mwanzoni mwa karne ya pili, Jumuiya zote za Kikristo walikuwa wanasherehekea sikukuu hii ya Pasaka. Sherehe zilikuwa zinahitimishwa na kusanyiko la sala lililofanyika usiku na kumalizikia na Ekaristi. Ushiriki wa kwenye ibada hiyo, ulichukuliwa kama ni kitu muhimu sana kwa mkristo.

Kuanza kwa Kwaresma

Wote tunafahamu kwamba, ufanisi au mafanikio yoyote ya sikukuu au ya jambo lolote yanategemea sana maandalizi yake. Miaka miambili hivi baada ya KRISTO, Wakristo walitaka kuvuna matunda ya kiroho ya Paska kwa wingi. Ili kufanikisha hili, walianzisha utamaduni wa kuwa na siku tatu kabla ya Pasaka kwa sala, tafakari na kufunga kwa nia ya kuonyesha masikitiko yao juu ya kifo cha YESU KRISTO. Kutokana na ukubwa na umuhimu wa sikukuu hii, mbali ya kuona umuhimu wa maandalizi, walitafuta njia za kuongeza muda wa furaha na utajiri wa kiroho utokanao na Pasaka. Hivyo walianzisha “Wiki Saba,” yaani siku 50 za Pentekoste ambapo walisherehekea na kuzipitisha siku hizo kwa hali ya furaha. Askofu Mt. Ireneus alisema kuwa muda huo wa siku 50 ni kama Sikukuu ya Siku moja yenye umuhimu sawa na Jumapili. Katika kipindi cha siku za Pentekoste, sala zilikuwa zinasaliwa hali wamesimama, kufunga kulikatazwa na sakramenti ya ubatizo ilikuwa ikiadhimishwa. Ni kama vile sikukuu ya Pasaka ilidumu kwa kipindi chote cha siku 50. Miaka 150 ilipita na mwishoni mwa mwaka 350 B.K., Wakristo waliona kama siku tatu hazikutosha kwa maandalizi ya sikukuu kama hii. Hivyo waliongeza hadi kufikia siku 40. Hivi ndivyo Kwaresima ilivyoanza.

Kwa nini siku 40?

Tunaposema kuku wanne au kilo saba za mchele tuna maana kama ilivyo yaani kuku wanne na kilo saba za mchele. Si zaidi au pungufu.
Namba au tarakimu mbalimbali tunazokutana nazo katika Biblia zinaashiria lugha za picha na siyo kuchukulia katika thamani ya kuhesabu. Hivyio basi, tunapokutana na namba kama 40 huenda isimaanishe 40 kama tunavyo hesabu fedha. Kati ya maana nyingi zilizotolewa kwa namba 40, kuna moja yenye maana ya pekee, inamaana ya kipindi cha maandalizi cha kutosha kisichokuwa na muda maalum, kwa tukio kubwa. Kwa mfano , Gharika ilidumu kwa siku 40 usiku na mchana…na ilikuwa ni maandalizi ya ubinadamu mpya; Waisraeli walitumia muda wa miaka 40 jangwani…maandalizi ya kuingia nchi ya ahadi; watu wa Ninawi walifunga na kufanya kitubio siku 40…maandalizi ya kupokea msamaha wa MUNGU; Elia alitembea kwa siku 40 mchana na usiku…kama maandalizi ya kufika mlima wa MUNGU; Musa na YESU walifunga kwa siku 40 mchana na usiku… kama maandalizi kabla ya kuanza utume wao. “Kisha ROHO alimwongoza YESU mpaka jangwani ili ajaribiwe na ibilisi. Akafunga siku arobaini usiku na mchana, na mwishoe akaona njaa” (Mt.4: 1-4)
Natumaini hadi hapo tumeelewa nini maana ya namba 40. Je, ni siku ngapi ambazo zinahitajika kwa ajili ya maandalizi ya sikukuu kubwa kuliko zote za kikristo? Bila shaka ni 40. (Kuanzia Jumatano ya majivu hadi Jumamosi Kuu ukiondoa Jumapili zote) Siku 40 ni muda wa kutosha wa kufanikisha kitu fulani chema, kizuri na chenye thamani.

Lengo la Kwaresima ni nini?

Lengo kuu la Kwaresima ni kufanya upya maisha yetu ya kiroho na kutufanya kuwa watu ambao MUNGU anataka tuwe yaani ni kipindi chenye kutupatia utakatifu, tukikumbuka kuwa sote tumeitwa kuwa watakatifu kama BABA yetu wa mbinguni alivyo mtakatifu (Mt. 5:48). Ni kipindi cha kuuvua utu wetu wa kale na kuvaa utu mpya. Kwani tunasoma:- “Mvue kwa habari ya mwenendo wa kwanza utu wa zamani, unao haribika kwa kuzifuata tamaa zenye kudanganya; na mfanywe wapya katika roho na nia zenu; mkavae utu mpya, ulioumbwa na MUNGU katika haki na utakatifu wa kweli. Basi uvueni uongo, mkaseme kweli kila mtu na jirani yake…Mwibaji asiibe tena…Neno lolote lililo ovu lisitoke vinywani mwenu, bali lililo jema na kufaa…tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama MUNGU katika KRISTO alivyowasamehe ninyi.” (Efe.4:22-32.)
Kwaresima kwa hakika ni kipindi pia cha kuachana na matendo ya mwili. “Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya: uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo;” (Gal.5:19 – 20).
Kwa ufupi Kwaresima ni kipindi cha kuachana na maisha ya dhambi na kurudi kwa MUNGU kwa kuishi maisha yanayompendeza MUNGU kwa njia ya kufanya toba ya kweli isiyo ya mazoea, na malipizi yasiyo ya nje tu, bali hasa mapinduzi ya kiroho. Katika kipindi hiki tunalazima ya kubadili hali yetu ya ndani. Badala ya kujitafuta wenyewe na kufuata mapenzi yetu, inatupasa sisi kumwelekea MUNGU na kuyatimiza mapenzi yake katika mawazo, maneno na matendo yetu.

Nguzo tatu kuu za Kwaresima ni:

i. Sala.

“Wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani. Usali mbele ya BABA yako aliye sirini; na BABA yako aonaye sirini atakujazi.” (Mt. 6:6)
Kupata muda wa sala pamoja na MUNGU. Sio tu kunena maneno ya sala fulani, lakini pia kumsikiliza MUNGU akizungumza mioyoni mwetu. Kumuomba MUNGU nguvu ya kubadilika, yaani uongofu wa kweli. Ndiyo maana tunaambiwa. “Tubuni na kuiamini Injili”. Hayo ndiyo MUNGU aombayo kwetu wakati wa Kwaresima. MUNGU anatuita kutoka kwa dhambi, na tuupokee ujumbe wake kwetu – Injili, na kuwa waamninfu kuishi kadiri ya Injili. Ni wakati pia wa kuhudhuria misa mara kwa mara kwa ibada na uchaji, kuhudhuria ibada mbalimbali, kama vile Baraka ya Sakramenti Kuu, Kuabudu Ekaristi Takatifu, kusoma Neno la MUNGU na kuliishi baada ya kuyatafakari maneno hayo ya MUNGU ambayo ndiyo sauti yake MUNGU na kutumia muda wetu kwa mambo ya ki-MUNGU yaliyo matakatifu.

ii. Kufunga.

“Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso wako ili usionekane na watu ukifunga, ila na BABA yako aliye sirini; na BABA yako aonaye sirini atakutuza.” (Mt. 6:17-18). Kufunga sio tu kujinyima kutokunywa pombe, kutokula chakula, kutovuta sigara n.k. Kifupi ni kwamba kufunga kuondokana na ubinafsi wetu na kuwafikiria na kuwasaidia wenye shida. Uovu hauwezi kushindwa bila kujitoa nafsi na bila kutoa na kuwapa wahitaji vile tuvipendavyo. MUNGU hapendezwi na kufunga tu, bali upendo kwa wanaoteseka utusukume na kufunga tupendavyo kwa ajili ya kuwasaidia wahitaji. Hivyo kuna mahusiano makubwa sana kati ya kufunga na ukarimu. Kufunga lazima kuendane na ukarimu. Kufunga bila ukarimu huo ni mfungo tasa.

iii. Kutoa Sadaka.

“Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu kusudi mtazamwe nao. Bali wewe utoapo sadaka hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wa kuume; na BABA yako aonaye kwa siri atakujazi.” (Mt. 6:1) Hayo yanamaanisha kwamba usidai shukurani wala malipo kwa wema wowote uwatendeao jirani zako kwa sadaka yako. Malipo utakayopata uyatazamie tu kutoka kwa BABA yako wa mbinguni. Kutoa tunachojinyima kwa kumsaidia KRISTO anayeteseka kwa wenzetu. Kushirikiana na wengine tulivyo navyo kama vile fedha, nguo, chakula, ama kuwakaribisha wahitaji nyumbani.
Hivyo basi, Mazoezi tunayofanya katika kipindi cha Kwaresima kama kusali zaidi, kusikiliza au kusoma Neno la MUNGU, kutenda matendo ya huruma kwa wahitaji, kufunga chakula na kujihinisha kinywaji pamoja na kuzuia tamaa potovu za mwili wetu, yawe na kusudi la kuibadili hali yetu, kutufanya kuwa na upendo zaidi na huruma kwa wenzetu na kutufanya tuweze kuunganika zaidi na KRISTO MFUFUKA. Tumvue mtu wa zamani katika nafsi zetu na tumvae mtu mpya, yaani KRISTO Mfufuka.

Nini makusudi ya kufunga?

YESU alifunga ili awape wanadamu mfano au kielelezo halisi na sahihi cha kuiga, na apate kuokoa roho zetu. Watu wawe na namna bora ya kufanya malipizi, kuuadibisha na kuutumikisha mwili na tamaa kwa kuwa anatenda dhambi.

Nani anapaswa kufunga?

Inatubidi tujiangalie sana kwani miili yetu ni midhaifu na myepesi kwa kutenda dhambi na kuipeleka roho motoni. Tusiiendekeze miili yetu, bali tuitawale kwa kufuata maadili ya kimungu na kuinyima madai yake, ambayo ni kishawishi kinachotupeleka upotevuni. Tunapoamua kufuata njia hii, hakika, KRISTO atatuimarisha na kutuongoza kwenye uzima wa milele; na kutupa neema ya kupambanua mema na dhambi, huku tukielekea uzimani. Mdomo unao nena dhambi, na mwili unaotenda dhambi, sherti vyote vitende pia mema, siyo dhambi.
Mtu asiyetenda dhambi hana haja ya kufunga. Lakini hakuna mtu anyefikia utu uzima ambaye hatendi dhambi machoni pa MUNGU hata Wacha MUNGU wana dosari. Kwa hiyo, kila mtu afunge kufidia dhambi zake. Tusipofunga kuna hatari kubwa ya kuungua moto. Ni vizuri waamini wote wafunge ili kulipia fidia ya dhambi zinazotendwa. Tumwabudu KRISTO kwa unyofu na unyenyekevu, ili kwa huruma yake kuu atusamehe dhambi zetu na adhabu tunazostahili.

Maana ya siku ya Jumatano ya Majivu

Utangulizi

Wakati umetimia na ufalme wa Mungu umekaribia, tubuni na kuiamini Injili, (Mk 1:15), haya ndiyo maneno ya kwanza ya Yesu ambayo kadri ya Mwinjili Marko yanafungua kazi ya hadhara ya Yesu, kwa maana hiyo kazi ya Yesu inaanza kwa kuwaandaa watu katika toba ili hatimaye, wapate kuukaribia au kuingia katika ufalme wa Mungu.
Na wakati ndiyo sasa. Wakati ni sasa, Yesu anatuhubiria na Kwaresima imewadia, na ndiyo maana siku ya Jumatano ya majivu, kwa kuitikia mwito wa maneno ya Yesu kanisa linatualika kuingia katika kipindi cha Kwaresma, ambacho ni kipindi cha kujikusanya, kujitayarisha, kijitengeneza na kujikarabati hasa kwa toba, kufunga, kusali na kujitoa sadaka zaidi mambo yanayorutubishwa kwa tafakari ya kina ya Neno la Mungu.

Nini maana ya Jumatano ya majivu?

Jumatano ya majivu ni mwanzo wa kipindi cha kwaresima katika kanisa, Ni mwanzo wa siku arobaini za kutafakari kwa undani fumbo kuu la upendo wa Mungu linalofunuliwa kwa kujitoa kwake na kufa msalabani, kifo cha aibu cha Msalaba ili kuichukua aibu yetu au dhambi zetu.

Kwaresma ni nini?

Kwaresma ni kipindi cha siku 40 cha kujiandaa kuadhimisha Sherehe kuu ya PASAKA yaani kufufuka kwa Bwana wetu Yesu Kristo. Tunajiandaa kwa Kufunga Kusali, Kutubu, na Matendo mema.
Mama kanisa anatupatia kipindi hiki ili tuweze kutafakari njia na mienendo yetu na kubadilika kama haimpendezi Mungu
Tunapofunga tunatakiwa kuzuia vilema vyetu na kuviacha kabisa, tunaomba kujaliwa moyo wa toba, tunainua mioyo yetu na tunaomba Mungu atujalie nguvu na tuzo. Haitoshi tu kukiri makosa yetu bali tunahimizwa kuungama na kutubu hayo makosa na kuwa tayari kuanza upya. Kipindi cha Kwaresima huanza tangu Jumatano ya majivu. Mwanzoni mwa kazi yake ya kuhubiri Habari njema Yesu anaanza kwa kusema tubuni na kuiamini Injili – Mk 1,15. Maneno haya haya tunayasikia/tumeyasikia kila tunapopakwa majivu. Mwaliko huu wa Yesu unatuingiza katika kipindi cha toba – tubuni na kuiamini Injili. Huu ni mwaliko wa uzima. Ni mwaliko ili tuongoke, tuanze maisha mapya, maisha ya sala, kufunga na kutoa sadaka.

Kwa nini ikaitwa Jumatano ya majivu?

Jina linatokana na desturi ya kumpaka mtu majivu kichwani pamoja na kumtamkia maneno ya kumhimiza afanye toba inavyotakiwa na kipindi hicho cha liturujia kinachoandaa Pasaka.
Kwa kawaida siku ya Jumatano ya majivu unaanza mfungo unaofuata kielelezo cha Yesu kufunga chakula siku arubaini jangwani baada ya kubatizwa na Yohane Mbatizaji na kabla ya kuanza utume wake mwenyewe.

Nini maana ya majivu tunayopaka?

Majivu ni ishara ya majuto, nayo hufanywa visakramenti kwa kubarikiwa na kanisa. Tunapopakwa majivu katika paji la uso hutusaidia kutafakari na kutukumbusha kuwa wanadamu sisi tu mavumbi na mavumbini tutarudi. Hutukumbusha zaidi kuwa maisha ya hapa duniani tunapita na safari yetu itakamilika pale tutakapoungana na Bwana na mwokozi wetu katika ufalme wako.
Angalia; Isaya 61:3, Ester 4:1-3, Yeremia 6:26, Ezekieli 27:30, Mathayo 11:21 na Luka 10:13.

Kwa nini majivu yanapakwa kwenye paji la uso na si vinginevyo?

Ishara yoyote iwekwayo katika paji la uso huonesha umiliki (soma Ufunuo 7:3, Ufunuo 9:4, Ufunuo 14:1, Ezekieli 9:4-6, ). Tunapochorwa ishara ya msalaba katika paji la uso ni ishara kwamba sisi tupo chini yake yeye aliyekufa msalabani kwa ajili yetu.
Hali kadhalika hutukumbusha ishara ya msalaba tuliyochorwa na mafuta matakatifu siku ya ubatizo wetu, hutukumbusha ahadi tuliyoiweka siku hiyo ya ubatizo na kutuita tuishi maisha ya utakatifu

Padri hutamka maneno gani wakati anapaka majivu?

Tunapopakwa majivu Padre husema; Mwanadamu kumbuka u mavumbi na mavumbini utarudi AU Tubuni na kuiamini Injili.

Maneno anayosema padre yana maana gani?

Maneno haya kwa upande mmoja hutukumbusha tunapoelekea, tusisikitike kwamba siku moja tutarudi mavumbini bali tuwe na furaha kwani wakati miili yetu unarudi mavumbini roho zetu zitakwenda kuungana na Mungu Baba mbinguni.
Hivyo maandalizi tunayoalikwa kuyafanaya si maandalizi ya kuelekea mavumbini bali maandalizi ya kuelekeza roho zetu mbinguni. Ndio maana pia twaambiwa tubuni na kuiamini Injili.

Majivu tunayopakwa yanatoka wapi?

Majivu tunayopakwa hutoka katika matawi yaliyotumika katika jumapili ya matawi ya mwaka jana. Majivu haya hubarikiwa na kuwa visakramenti. Hivyo majivu yanapoashiria toba na majuto pia hutukumbusha wema wa Mungu na utayari wake wa kutusamehe.

Kwa nini unatumia matawi ya Jumapili ya Matawi?

Matawi haya yalimkaribisha Yesu Yerusalemu akiwa tayari kufa kwa ajili ya dhambi zetu, yalimpokea mfalme kwa furaha na shangwe kuu. Matawi haya yanapochomwa na sisi kupakwa majivu yetu yanatukumbusha kuwa ni kwa ajili ya dhambi zetu Mungu alimtoa mwanae wa pekee kufa msalabani kwa ajili ya dhambi zetu sisi wanaadamu. Hivyo hututafakarisha kuacha dhambi.

Kanisa limekataza nini siku ya Jumatano ya majivu?

Tumekatazwa kula chakula siku ya Jumatano ya Majivu na kula nyama siku ya Ijumaa Kuu katika Amri ya Pili ya Kanisa.

Nani analazima kufunga siku ya Jumatano ya majivu na Kwaresma?

Kila Mkristo aliyetimiza miaka 14 na zaidi anapaswa kufunga kula nyama (Ijumaa kuu) na mwenye miaka zaidi ya 21 kufunga chakula Jumatano ya Majivu

Tunaposema kujinyima wakati wa Kwaresma tunamaana gani?

Kujinyima ni kujikatalia kitu ukipendacho mfano nyama, pombe, sigara, muziki, safari, maongezi n.k.

Mwisho

Wakati wa Kwaresma Waamini wanapaswa kujitakasa zaidi kwa kusali, kufunga, toba na matendo mema
Kipindi cha Kwaresima ni fursa makini ya kumkimbilia Mwenyezi Mungu, kwani kwa njia ya dhambi wamejikuta wakiwa mbali na Uso wa huruma ya Mungu, kiasi hata cha kupoteza imani na matumaini kwa Mwenyezi Mungu. Hii ni changamoto ya kumpenda Mungu na jirani badala ya kukumbatia malimwengu yanayoendelea kuwatumbukiza katika utupu wa maisha ya kiroho. Kwaresima ni kipindi cha waamini kukimbilia na kuambata huruma ya Mungu inayoganga na kuponya dhambi. Ni wakati wa sala, upendo na kufunga.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu imani na matendo?

Kanisa Katoliki ni moja ya madhehebu makubwa zaidi ya Ukristo duniani. Na kama madhehebu mengine ya Kikristo, Kanisa Katoliki linasisitiza umuhimu wa imani na matendo. Kwa ufupi, imani ni msingi wa maisha ya Kikristo, lakini matendo ni matokeo ya imani hiyo. Katika makala hii, tutazungumzia ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu imani na matendo.

Kwanza kabisa, Kanisa Katoliki linasisitiza kuwa imani ni msingi wa maisha ya Kikristo. Imani ina maana ya kuamini kuwa Mungu yupo, na kwamba Yeye ni Muumbaji wa ulimwengu na wa binadamu. Imani pia inamaanisha kuamini kuwa Yesu Kristo ni Mwana wa Mungu, ambaye alikuja duniani kuwaokoa watu kutoka dhambi zao. Imani hii inajidhihirisha katika sakramenti za Kanisa, ambazo ni ishara za neema ya Mungu kwa binadamu.

Pamoja na imani, Kanisa Katoliki pia linasisitiza umuhimu wa matendo. Matendo ni matokeo ya imani hiyo, na ni njia ya kuiishi imani hiyo katika maisha ya kila siku. Kwa mfano, Kanisa Katoliki linasema kuwa sio tu ni muhimu kuamini kuwa Mungu yupo, bali pia ni muhimu kumtumikia Mungu kwa kufanya matendo ya haki. Hii inamaanisha kuwa Kikristo anapaswa kujitahidi kuishi maisha ya upendo na wema, kwa kuwasaidia wengine na kufanya kazi nzuri katika jamii.

Biblia inasisitiza umuhimu wa imani na matendo pia. Kwa mfano, katika kitabu cha Yamesi, Biblia inasema "Imani bila matendo ni mfu" (Yakobo 2:26). Hii ina maana kuwa imani pekee haitoshi, bali ni muhimu kuiishi katika matendo. Kwa upande mwingine, katika kitabu cha Wagalatia, Biblia inasema "Kwa maana katika Kristo Yesu, wala kutahiriwa hakufai kitu, wala kutokutahiriwa, bali imani iliyo kwa njia ya upendo hufanya kazi." (Wagalatia 5:6). Hapa, Biblia inasisitiza kuwa imani na upendo ni vitu muhimu sana katika maisha ya Kikristo.

Kanisa Katoliki linatufundisha zaidi juu ya imani na matendo katika Catechism of the Catholic Church. Kwa mujibu wa Catechism, imani ni "hakikisho la mambo tunayotumaini, ni yakini ya mambo tusiyoyaona" (CCC 1814). Matendo ya haki, kwa upande mwingine, yanaelezewa kama "matendo yote yanayohusiana na upendo kwa Mungu na kwa jirani" (CCC 1825). Kwa hiyo, Kanisa Katoliki linasisitiza kuwa imani na matendo ni mambo yanayohusiana sana, na kwamba ni vigumu kusema kuwa unayo imani bila kuonyesha matendo ya haki.

Kwa muhtasari, Kanisa Katoliki linasisitiza umuhimu wa imani na matendo katika maisha ya Kikristo. Imani ni msingi wa maisha ya Kikristo, lakini matendo ni matokeo ya imani hiyo. Biblia inasisitiza umuhimu wa imani na matendo pia, na Catechism ya Kanisa Katoliki inatufundisha zaidi juu ya mada hii. Kwa hiyo, ni muhimu kwa Kikristo kuiishi imani hiyo katika matendo ya haki, kwa kuwasaidia wengine na kufanya kazi nzuri katika jamii.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Roho Mtakatifu?

Katika Kanisa Katoliki, Roho Mtakatifu ni Mungu mmoja katika Utatu Mtakatifu (Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu). Ni kwa njia ya Roho Mtakatifu tu ndipo tunapata uwezo wa kuelewa na kukubali mambo ya Mungu. Katika Biblia, Roho Mtakatifu anaelezwa kama "Mlinzi", "Msaidizi", "Mwalimu", na "Mwongozi".

Kanisa Katoliki linamwamini Roho Mtakatifu kama mtakatifu na mmoja wa wanaume wa Mungu watatu. Roho Mtakatifu anahusika katika kazi ya Mungu ya wokovu wa mwanadamu. Katika Luka 11:13, Yesu anasema, "Baba yenu wa mbinguni atawapa Roho Mtakatifu wale wanaomwomba." Hii inaonyesha wazi kuwa Roho Mtakatifu ni zawadi ya Mungu kwa watu wake.

Katika Kanisa Katoliki, Roho Mtakatifu anachukua jukumu muhimu katika sakramenti nyingi za Kanisa. Kwa mfano, wakati wa Ubatizo, Roho Mtakatifu anamdhihirisha mwanadamu kama mwana wa Mungu. Wakati wa Kipaimara, Roho Mtakatifu anaimarisha neema ya ubatizo na kuwawezesha Wakristo kushiriki kikamilifu katika maisha ya Kanisa.

Katika Waraka kwa Wagalatia 5:22-23, Paulo anaelezea matunda ya Roho Mtakatifu: "Upendo, furaha, amani, uvumilivu, urafiki mwema, fadhili, uaminifu, upole na kiasi." Kanisa Katoliki linakubali kuwa Roho Mtakatifu ndiye anayewezesha watu kuzalisha matunda haya maishani mwao.

Kwa hivyo, imani ya Kanisa Katoliki kuhusu Roho Mtakatifu ni kwamba ni mmoja wa wanaume wa Mungu watatu, na anachukua jukumu muhimu katika maisha ya Wakristo na katika sakramenti za Kanisa. Roho Mtakatifu anatupa uwezo wa kuelewa na kukubali mambo ya Mungu, na anatupa matunda ya upendo, furaha, amani, na zaidi. Kwa hivyo, ni muhimu kwetu kumwomba Roho Mtakatifu katika maisha yetu ya kila siku, ili aweze kutuongoza na kutusaidia kuishi maisha ya Kikristo.

27. Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Daraja Takatifu?

Kwa wale ambao wamechagua njia ya Kikatoliki katika maisha yao, kanisa linaamini kuwa sakramenti ya Daraja Takatifu ni muhimu sana katika utendaji kazi wa maisha ya kanisa. Wakati wa kupokea sakramenti hii, wanaume wanapokea daraja ya Uaskofu, Upadri, na Ushemasi. Lakini ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti hii? Hapa chini ni maelezo fulani:

Kwa kuanza, Kanisa Katoliki linashikilia kuwa sakramenti ya Daraja Takatifu ni mojawapo ya sakramenti saba za Kanisa. Kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, sakramenti hii inampa mwanamume mamlaka ya kuwa kiongozi wa kiroho katika kanisa. Kwa hivyo, wanaume ambao wamepokea sakramenti hii wanakuwa na wajibu wa kuongoza kundi la waamini katika kufanya mambo ya kiroho.

Kuhusu ushirikishwaji wa Mungu katika sakramenti hii, Kanisa Katoliki linashikilia kwamba ni Mungu pekee ndiye anayeweza kuwapa wanaume mamlaka ya kuwa viongozi wa kiroho. Katika 1 Timotheo 4:14, kanisa linakumbuka maneno haya: "Usichukue tu kwa kiburi nafasi yako ya uongozi. Shughulika kwa bidii kila wakati, ukiendelea kujitahidi kufuata mafundisho ya Kanisa."

Kwa kuongezea, sakramenti ya Daraja Takatifu inahusiana sana na sakramenti nyingine za Kanisa. Kwa mfano, wanaume ambao wamepokea sakramenti hii wanaweza kutoa sakramenti ya Ekaristi Takatifu na kuwasamehe waamini dhambi katika sakramenti ya Kitubio. Kwa hiyo, sakramenti hii inahusiana sana na utendaji kazi wa kanisa kwa ujumla.

Mwishowe, Kanisa Katoliki linashikilia kuwa kuna wajibu mzito kwa wanaume ambao wamepokea sakramenti hii. Kwa mfano, wanapaswa kufuata maadili ya kikristo na kuheshimu mistari ya mamlaka. Katika Mathayo 23:11-12, Yesu anasema: "Mwenye kutawala kwenu, na awe mtumishi wenu. Kila mtu anayejitukuza mwenyewe atashushwa, na kila mtu anayejishusha atainuliwa."

Kwa hivyo, sakramenti ya Daraja Takatifu ni muhimu sana katika utendaji kazi wa kanisa. Wanaume ambao wamepokea sakramenti hii wanapaswa kufanya kazi kwa bidii kuhakikisha kuwa kanisa linaweza kufanya kazi kwa ufanisi zaidi na kuzingatia maadili ya kikristo. Kwa hivyo, sakramenti hii ni muhimu sana katika kufikia malengo ya kiroho ya kanisa.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu haki na haki za binadamu?

Kanisa Katoliki ni mojawapo ya madhehebu makubwa duniani na linazingatia sana haki na haki za binadamu. Katika imani yake, Kanisa linaamini kwamba haki na haki za binadamu zinatokana na Mungu na zinapaswa kulindwa kwa nguvu zote. Ni kwa sababu ya imani hii, Kanisa Katoliki linajitahidi kusimama kidete kulinda haki za binadamu na kuhakikisha kwamba kila mtu anaishi katika hali ya amani na usawa.

Biblia inatufundisha kwamba binadamu wote wameumbwa kwa sura na mfano wa Mungu (Mwanzo 1:26-27), na kwa hiyo, kila mtu ana haki ya kuishi kwa heshima, usawa, na amani. Haki hizi zinapaswa kulindwa na kuheshimiwa na wote, bila kujali jinsia, rangi, dini, au asili. Kanisa Katoliki linasisitiza kwamba kila mtu anapaswa kuheshimiwa na kutendewa kwa haki, na kwamba hakuna mtu anayepaswa kudhulumiwa au kudharauliwa.

Kanisa Katoliki linazingatia sana haki za binadamu na limeanzisha taratibu kadhaa za kulinda haki hizo. Kwa mfano, Kanisa linakataza kabisa vitendo vyote vya ubaguzi na unyanyasaji, na linasisitiza kwamba kila mtu anapaswa kutendewa kwa heshima. Kanisa pia linasisitiza kwamba kila mtu ana haki ya kuishi kwa amani na kwamba hakuna mtu anayepaswa kuteswa au kutishiwa kwa sababu ya imani yake.

Catechism of the Catholic Church inafundisha kwamba kila mtu ana haki ya kuwa huru, na kwamba uhuru huu unapaswa kulindwa na kuheshimiwa kwa nguvu zote. Uhuru huu unatokana na haki ya kila mtu ya kumiliki uhai wake na kujiamulia mambo yake mwenyewe. Kanisa Katoliki linasisitiza kwamba uhuru huu unapaswa kutumika kwa njia nzuri na inayoendana na sheria za Mungu.

Kanisa Katoliki linatambua kwamba haki na haki za binadamu zinatokana na Mungu na kwamba ni Kanisa lenye jukumu la kulinda haki hizo. Kwa hiyo, Kanisa linajitahidi kusimama kidete kulinda haki za binadamu na kuhakikisha kwamba kila mtu anaishi katika hali ya amani na usawa. Kama Wakatoliki, ni jukumu letu sote kulinda haki na haki za binadamu na kuhakikisha kwamba kila mtu anapata heshima na usawa unaostahili.

Biblia inavyothibitisha kuwa Bikira Maria Mama wa Yesu ni Mama wa Wakristu Wote

Ufunuo 12:17
17Kisha lile joka likapatwa na hasira kali kwa ajili ya huyo mwanamke, likaondoka ili kupigana vita na watoto waliosalia wa huyo mwanamke, yaani, wale wanaozitii amri za Mungu na kuushika ushuhuda wa Yesu Kristo.
Kwa hiyo Bikira Maria ni Mama wa Wakritu wote yaani, wale wanaozitii amri za Mungu na kuushika ushuhuda wa Yesu Kristo

Ukisoma kwa urefu inasomeka hivi

Ufunuo 12:1-18

1 Kukaonekana ishara kuu mbinguni: Palikuwa na mwanamke aliyevikwa jua na mwezi ukiwa chini ya miguu yake na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa kichwani mwake. 2Alikuwa na mimba naye akilia kwa uchungu kwa kuwa alikuwa anakaribia kuzaa. 3Kisha ishara nyingine ikaonekana mbinguni: Likaonekana joka kubwa jekundu lenye vichwa saba na pembe kumi na taji saba katika vichwa vyake. 4Mkia wake ukakokota theluthi ya nyota zote angani na kuziangusha katika nchi. Ndipo lile joka likasimama mbele ya yule mwanamke aliyekuwa karibu kuzaa ili lipate kumla huyo mtoto mara tu atakapozaliwa. 5Yule mwanamke akazaa mtoto mwanamume, atakayeyatawala mataifa yote kwa fimbo yake ya utawala ya chuma. Lakini huyo mtoto akanyakuliwa na kupelekwa kwa Mungu kwenye kiti Chake cha enzi. 6Yule mwanamke akakimbilia nyikani, ambako Mungu alikuwa amemtayarishia mahali ili apate kutunzwa huko kwa muda wa siku 1,260. 7 Basi palikuwa na vita mbinguni: Mikaeli na malaika zake wakapigana na hilo joka, nalo joka pamoja na malaika zake likapigana nao. 8Lakini joka na malaika zake wakashindwa na hapakuwa tena na nafasi kwa ajili yao mbinguni. 9Lile joka kuu likatupwa chini, yule nyoka wa zamani aitwaye Ibilisi au Shetani, aupotoshaye ulimwenguni wote. Akatupwa chini duniani, yeye pamoja na malaika zake. Ushindi 10Kisha nikasikia sauti kuu mbinguni ikisema, “Sasa Wokovu na uweza na Ufalme wa Mungu wetu umekuja na mamlaka ya Kristo wake. Kwa kuwa ametupwa chini mshtaki wa ndugu zetu, anayewashtaki mbele za Mungu usiku na mchana. 11Nao wakamshinda kwa damu ya Mwana-Kondoo na kwa neno la ushuhuda wao. Wala wao hawakuyapenda maisha yao hata kufa. 12Kwa hiyo, furahini ninyi mbingu na wote wakaao humo! Lakini ole wenu nchi na bahari, kwa maana huyo Shetani ameshuka kwenu, akiwa amejaa ghadhabu, kwa sababu anajua ya kuwa muda wake ni mfupi!’ 13Lile joka lilipoona kuwa limetupwa chini duniani, lilimfuatilia yule mwanamke aliyekuwa amezaa mtoto mwanamume. 14Lakini huyo mwanamke akapewa mabawa mawili ya tai mkubwa, kusudi aweze kuruka mpaka mahali palipotayarishwa kwa ajili yake huko nyikani, ambako atatunzwa kwa wakati na nyakati na nusu wakatia ambako yule joka hawezi kufika. 15Ndipo lile joka likamwaga maji kama mto kutoka kinywani mwake, ili kumfikia huyo mwanamke na kumkumba kama mafuriko. 16Lakini nchi ikamsaidia huyo mwanamke kwa kufungua kinywa na kuumeza huo mto ambao huyo joka alikuwa ameutoa kinywani mwake. 17Kisha lile joka likapatwa na hasira kali kwa ajili ya huyo mwanamke, likaondoka ili kupigana vita na watoto waliosalia wa huyo mwanamke, yaani, wale wanaozitii amri za Mungu na kuushika ushuhuda wa Yesu Kristo. Lile joka likasimama kwenye mchanga wa bahari. 18Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari.

Tunajifunza nini

Mwanamke ni Bikira Maria

Mwanamke aliyetukuzwa Uf 12:1

1 Kukaonekana ishara kuu mbinguni: Palikuwa na mwanamke aliyevikwa jua na mwezi ukiwa chini ya miguu yake na taji ya nyota kumi na mbili ilikuwa kichwani mwake.

Anamzaa mtoto

Analindwa nyoka asimdhuru

Nyoka anapambana na wanawe

IShara ya joka kama Shetani

Akisubiri kuzaliwa kwa mtoto ili amdhuru kisha alishindwa na kutupwa duniani na kutaka kupambana na yule mwanamke Akashindwa na kuishia kupambana na watoto wa Yule mwanamke yaani, wale wanaozitii amri za Mungu na kuushika ushuhuda wa Yesu Kristo Uf 12:17

Mtoto Aliyezaliwa mwenye mamlaka

Ambaye ndiye Yesu Kristu

Kwa hiyo, Bikira Maria Aliwezeshwa kumshinda Shetani na ni Mama wa Wakristu wote

Uzinzi na Uasherati ndio mtego wa kizazi hiki

Uzinzi na uasherati wakati huu umekuwa ndio sumaku kuu ya kuwanasa watu ili waende jehanamu.

Sumaki hii imewanasa hata ambao hawakutegemewa wala kutarajiwa.

Uzinzi uzinzi uzinzi umekuwa kama perfume ya kujipulizia kila Mara mtu akipenda.

Uasherati umekuwa kama heshima ya kibinadamu kwa vijana wengi.

Mbingu zimenyamaza kwa sababu iko jehanamu inawangoja wazinzi na waasherati.

Dhambi hii imekuwa sumaku kubwa ya shetani ya kukamata wanadamu ili waende jehanamu.

Wanadamu wa Leo ukimwambia kwamba aache uzinifu maana wazinzi na waasherati hawataenda uzima wa milele, mtu huyo anakuambia unamhukumu.

Ni Neno la MUNGU ndile limesema katika maandiko mengi tu kwamba wazinzi na waasherati sehemu yako itakuwa katika ziwa la moto.

Hata makanisani baadhi ya watu wamenasa kwenye sumaku hii.

Dada mmoja ambaye kila wiki anasimama na kushika mic kanisani kwao siku moja aliniambia kwamba hawezi kumaliza wiki bila kufanya ngono, na hajaolewa. Niliumia sana rohoni nikamwambia aache kutumika madhabahuni, yeye akasema itakuaje maana yeye ndiye tegemeo.

Mama mmoja alisema yeye ana mume mema sana na mume wake ni mwaminifu sana katika ndoa yao lakini yeye huyo mama ndio hutoka nje ya ndoa Mara kwa Mara, ni hatari inayohitaji neema ya MUNGU tu ili kutubu na kuacha.

Mama mmoja yeye ana watoto zaidi ya wawili na yuko katika ndoa lakini hana uhakika kama watoto wale ni wa mume wake wa ndoa, ni hatari sana.

Baba mmoja akiwa ndani ya ndoa amezaa watoto zaidi ya watatu nje ya ndoa tena wanawake zaidi ya wanne(4) tofauti tofauti.

Mwanaume moja ambaye husimama madhabahuni yeye kila Mara humdanganya mkewe kwamba anaenda safari kumbe ana mahawara karibia kila mkoa, ni hatari sana.

Watu wengi sasa wanaona uzinzi na uasherati ndio fashion nzuri ya wakati kuu.

Kila kijana ana girlfriend kwa lengo la ngono tu na sio vinginevyo.

Kila binti ana boyfriend kwa ajili ya uasherati.

Ukitaka watu wakuchukie basi kemea uzinzi na uasherati.

Watu wengi wamekuwa vipofu wa kiroho kwa sababu ya uzinzi na uasherati.

Lakini upo mwisho mmoja kwa watenda dhambi wote ambayo ni jehanamu.

Ndugu unahitaji kutubu Leo na kuacha dhambi.

Ndugu mmoja akasema yeye anaishi maisha matakatifu ila dhambi moja tu yaani uzinifu ndio imemshinda, hiyo ni hatari.

Leo hata ndoa takatifu zimeadimika maana wahusika huanza kwanza uzinzi na uasherati ndio baadae ndoa, ndugu mnahitaji kutubu.

Ndugu yangu unayenisikiliza kwa njia ya ujumbe huu nakuomba tubu na acha dhambi hiyo.

Amua kuiacha.

Mwisho wa uzinzi na uasherati ni kifo(Mauti) na baada ya kifo ni hukumu(Waebrania 10:27)

Nimekuonya wewe Leo ili ukishupasa shingo usije ukalaumu siku ile ukiwa katikati ya bahari ya moto huku kifo kimezuiliwa ili uteseke milele.

Mimi naamini utatengeneza ndugu baada ya kuusoma ujumbe huu.

Mimi naamini utaachana na mahawara na kuanza kuiheshimu ndoa yako.

Mimi naamini hutamsaliti tena mkeo/Mumeo.

Mimi naamini utaachana na huyo girlfriend/Boyfriend, wengine wanao zaidi ya mmoja, nakuomba ndugu achana nao.

Kijana au binti kaa tulia hadi wakati wako wa ndoa.

Uliyenisikia na utatubu na kuacha dhambi hiyo, MUNGU akubariki sana.“`

ALIYE NA AKILI AWEKE MOYONI MANENO HAYA. AMINA

Swala la Mapadri kutooa limeandikwa wapi katika Biblia?

JE,SHERIA YA MAPADRE KUTOOA NA KUISHI USEJA IMEANDIKWA WAPI KATIKA BIBLIA AU IMETUNGWA TU NA PAPA?

Pengine umewahi kuulizwa swali hili wakati fulani.Na jibu lake ni kama ifuayavyo:
Mtu anapouliza kila kitu kimeandikwa wapi katika Biblia ni kudhihirisha kutokuijua au kuielewa vizuri Biblia Takatifu na historia yake.Mtu anapong’ang’ania “nionyeshe kitu fulani kimeandikwa wapi kwenye Biblia”ni kutaka kujiona ya kwamba yeye anaielewa sana Biblia na ameisoma yote kwa hiyo kila kitu kilichopo kwenye Biblia anakifahamu kumbe haijui Biblia bali anakariri Biblia!
Na hili suala la kushupalia swala la kuoa linadhihirisha jinsi gani tulivyo kizazi cha zinaa,ni kama tunadhani kuwa UZIMA upo katika kujamiiana!La hasha.
Paulo anasema “Kwasababu ya zinaa ni bora kuoa na kuolewa”(1Wakorintho 7:2.9) haya sio maneno ya kufurahia na kuchekelea tu maana “YANAWALENGA WALE WALIOSHINDIKANA KATIKA YALE YAPENDEZAYO”(1Wakorintho 7:1.8)sasa ni lazima tujiulize je tumeshindikana kiasi hicho?,hiyo sio sifa!
1Wakorintho 7:1.8
“Basi kwa habari ya mambo yale mliyoandika,ni heri mwanaume asimguse mwanamke,8.Lakini nawaambia wale wasiooa bado na wajane heri wakae kama mimi nilivyo”
Na Paulo Mtume anasema “Ni bora kuoa au kuolewa” lakini hakusema “Ni LAZIMA kuoa au kuolewa”
Suala la kutooa kwa mapadre kadiri ya historia lilianza tangu zamani kabisa mwanzoni mwa milenia ya pili katika mtagusi wa pili wa Laterani mwaka wa 1139 ili waweze kumtumikia Mungu kwa uhuru na bila mawaa wala pasipo vikwazo(1wakorintho 7:32-35)
1wakorintho 7:32-35
“32Lakini nataka msiwe na masumbufu.Yeye asiyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya Bwana ampendezeje Bwana;33.bali yeye aliyeoa hujishughulisha zaidi na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendeza mkewe.34-Tena iko tofauti kati ya mke na mwanamwali.Yeye asiyeolewa hujishughulisha na mambo ya Bwana ili apate kuwa mtakatifu mwili na Roho.Lakini yeye aliyeolewa hujishughulisha na mambo ya dunia hii,jinsi atakavyompendezesha mumewe.,35.Nasema hayo niwafaidie ninyi,si kwamba niwategee tanzi,bali kwaajili ya vile vipendezavyo,tena mpate kumhudumia Bwana pasipo kuvutwa na mambo mengine”
Maandiko hayo hapo juu yanajieleza wala sidhani kama yanahitaji kufafanuliwa zaidi ya yanavyojifafanua yenyewe.
Watu wengine wanafikiri kwamba kutooa ni dhambi,kama ni hivyo basi hata Yesu mwenyewe alikosa maana hata yeye mwenyewe hakuoa.
Yesu mwenyewe anafundisha kuhusu ubikira(Mathayo 19:10-12)
Mathayo 19:10-12,
“Wanafunzi wake wakamwambia,kama mambo ya mme na mke yakiwa hivyo ni afadhali kutuooa kabisa.Lakini Yeye akawaambia ‘SI WOTE WAWEZAO KULIPOKEA NENO HILO,ILA TU WALE WALIOJALIWA,maana wako MATOWASHI waliozaliwa katika hali hiyo toka matumboni mwa mama zao;tena wako matowashi waliofanywa na watu kuwa matowashi,tena wako Matowashi WALIOJIFANYA WENYEWE KUWA MATOWASHI KWAAJILI YA UFALME WA MBINGUNI’,awezaye kulipokea neno hili na alipokee”
Yesu mwenyewe analifafanua jambo hili kwa mapana,katika orodha ya matowashi Yesu aliowataja,Mapadre ni Matowashi waliojifanya hivyo kwaajili ya huduma ya kanisa na ufalme wa Mungu.
Tena Yesu anatuambia waziwazi kwamba”sio wote wawezao kulipokea neno hilo”yaani sasa sio wote wawezao kuwa Matowashi(Mapadre)bali ni wale tu waliojaliwa na Mungu neema hiyo.wale wasioweza kuishi upadre huoa na kuwa na familia.Tena Yesu anamalizia kwa kusema “Awezaye kulipokea fundisho hili na alipokee”,kwa maana nyingine ni kusema “Fundisho au Utowashi huu sio wa lazima”anayeweza kuishi maisha hayo basi na ayapokee na yule asiyeweza basi aache!
Vilevile Mitume ili kumfuata Yesu kikamilifu waliyaacha yote waliokuwa nayo ikiwepo familia zao ili wamtumikie Bwana(Mathayo 19:27.29)
Mathayo 19:27.29:
“Ndipo Petro akajibu akamwambia ‘Tazama sisi tumeacha vyote tukakufuata wewe,tutapata nini basi?29.Amini nawaambia,kila mtu aliyeacha nyumba au ndugu wa kiume au wakike,au baba au mama au watoto au mashamba KWAAJILI YA JINA LANGU,atapokea mara mia zaidi na kuurithi uzima wa milele”
katika injili hiyo,Yesu anadhihirisha kwamba aliyeacha hayo yaliotajwa si kwasababu hawezi kuyapata la hasha,bali ameyaacha hayo yote KWAAJILI YA JINA LA YESU atapokea mengi hapa duniani halafu tena ataurithi ufalme wa mbinguni.
Mapadre wameyaacha hayo yote,wameacha nyumba,familia zao na kila kitu SIO KWASABABU HAWANA UWEZO AU HAWAWEZI KUPATA MAMBO HAYO bali WAMEACHA KWASABABU YA KUMTUMIKIA MUNGU KWA KADIRI YA MAANDIKO MATAKATIFU na kwakutaka kwao kuyaishi kimamilifu MASHAURI YA INJILI ikiwepo USEJA.
Maneno ya Paulo na yale ya Yesu mwenyewe kuhusu kumtumikia Mungu bila kuoa sio ya bahati mbaya bali ndiyo njia bora na inayofaa sana na kukubalika mbele ya Mungu.
Kwahiyo unapowaona mapadre hawaoi ujue sababu yake ni hiyo kwamba “Wamejitoa kwaajili ya kulihudumia kanisa”
(Na pia huwa nawashangaa mno watu wanaowapiga vita Mapadre kwamba kwanini hawaoi,najiuliza je,hao Mapadre wamewakataza wao kwamba wasioe?.)..na kama jibu ni hapana,sasa Je,”Pilipili ya shamba usiyoila inakuwashia nini?”
TUMSIFU YESU KRISTO!

Huruma ya Mungu: Karama ya Upatanisho na Ukarabati

Karibu kwenye makala hii inayoeleza kuhusu huruma ya Mungu na jinsi karama hii inavyohusiana na upatanisho na ukarabati. Kama Mkristo, unajua kwamba Mungu ni mwingi wa huruma na upendo. Kwa hivyo, jukumu letu kama wafuasi wake ni kuigiza huruma yake kwa wenzetu.

  1. Huruma ya Mungu ni zawadi kubwa kwetu sisi binadamu. Inatupa fursa ya kufanya upatanisho na Mungu wetu na hivyo kuwa karibu naye. Kama ilivyoelezwa katika Kitabu cha Isaya 55:7 "Mwenye dhambi na aache njia yake mbaya, Na mtenda maovu aache mawazo yake; Naye arudi kwa Bwana, Naye atamrehemu, Na kwa Mungu wetu, Maana atasamehe kwa wingi."

  2. Upatanisho ni mojawapo ya matunda ya huruma ya Mungu. Yeye hupatanisha na kutulinda kama ilivyoelezwa katika Warumi 5:10 "Kwa maana kama tulipokuwa adui tulipatanishwa na Mungu kwa mauti ya Mwana wake; zaidi sana sasa, tulipokuwa tayari tumepatanishwa, tutahifadhiwa na kifo chake cha uzima."

  3. Upatanisho ni jukumu letu kama Wakristo. Kupatanisha na wenzetu na Mungu ni sehemu muhimu ya huduma yetu ya kiroho. Kama ilivyoelezwa katika 1 Wakorintho 5:18 "Lakini haya yote yanatoka kwa Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, na kutupa huduma ya upatanisho."

  4. Kukubali upatanisho kutoka kwa Mungu kunahitaji kuungama na kutubu dhambi zetu. Kama ilivyoelezwa katika 1 Yohana 1:9 "Tukiziungama dhambi zetu, yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote."

  5. Ukubali wa upatanisho kutoka kwa Mungu unakuja na neema ya kujikomboa kutoka kwa dhambi. Kama ilivyoelezwa katika Warumi 6:14 "Kwa sababu dhambi haitatawala juu yenu, kwa maana hamko chini ya torati, bali chini ya neema."

  6. Huruma ya Mungu pia inahusiana na ukarabati wetu. Yeye hutuponya kutoka kwa majeraha ya dhambi zetu. Kama ilivyoelezwa katika Zaburi 147:3 "Anaponya waliopondeka moyo, Na kuwaunganisha katika maumivu yao."

  7. Ni muhimu kujua kwamba Huruma ya Mungu inapatikana kwa wote, sio kwa watu wachache. Kama ilivyoelezwa katika Warumi 10:12-13 "Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani; kwa maana yeye yule ni Bwana wa wote; naye ni mwingi wa rehema kwa kila mtu amwitaye; kwa kuwa, Kila mtu atakayeliitia jina la Bwana ataokoka."

  8. Kupitia huruma ya Mungu, tunaweza kushinda dhambi na kukua kiroho. Kama ilivyoelezwa katika Tito 2:11-12 "Kwa maana neema ya Mungu iwaokoayo wanadamu wote imefunuliwa, na kufundisha sisi, tukataa ubaya na tamaa za kidunia, tupate kuishi kwa kiasi, na haki, na utauwa, katika ulimwengu huu wa sasa."

  9. Huruma ya Mungu inatulea kuwa na unyenyekevu kwa wenzetu. Tunatakiwa kuwa na roho ya kusamehe na kusaidia wengine. Kama ilivyoelezwa katika Wagalatia 6:2 "Bear ye one another’s burdens, and so fulfil the law of Christ."

  10. Hatimaye, Huruma ya Mungu inatupatia fursa ya kumjua Mungu wetu vizuri zaidi na kuishi kwa kufuata mafundisho yake. Kama ilivyoelezwa katika Yohana 17:3 "Na uzima wa milele ndio huu, wapate kukujua wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma."

Katika Catechism ya Kanisa Katoliki, tunajifunza kwamba huruma ya Mungu inahusiana na neema, ukombozi, na upatanisho. Pia tunajifunza kwamba karama hii inatufundisha kuwa na huruma kwa wengine. Katika Kitabu cha Diary of Saint Maria Faustina Kowalska, tunasoma juu ya huruma ya Mungu na jinsi tunaweza kuinyenyekea kwa wengine.

Kuwa Mkristo ni kujifunza kujitoea kwa Mungu na kwa wenzetu. Kupitia huruma ya Mungu, tunaweza kupatanisha na kuwa karibu na Mungu wetu, kujikomboa kutoka kwa dhambi, na kujenga mioyo yetu kwa kumjua Mungu vizuri zaidi.

Je! Wewe ni mfuasi wa Kristo? Je! Unatambua huruma ya Mungu katika maisha yako? Je! Unajitahidi kumtumikia Mungu na kujitoea kwa wenzako? Jibu maswali haya na utusaidie kujifunza zaidi juu ya karama hii ya upatanisho na ukarabati kupitia huruma ya Mungu.

Kuishi katika Huruma ya Mungu: Njia ya Utakatifu na Ukarimu

Kuishi katika Huruma ya Mungu: Njia ya Utakatifu na Ukarimu

  1. Kuishi katika huruma ya Mungu ni muhimu sana katika kufikia utakatifu. Kwa kufanya hivyo, tunajifunza kutenda kwa ukarimu na upendo kwa wengine, kama vile Mungu alivyofanya kwetu. (1 Peter 4:8)

  2. Kuwa mkarimu ni sehemu ya utakatifu. Tunapaswa kujitolea kwa wengine na kufanya kazi zilizo bora kwa faida ya wengine. Hii inajumuisha kuwasaidia wasio na uwezo, kuwafariji walio na huzuni, na kuwapa riziki wale walio na njaa. (Yakobo 2:14-17)

  3. Kama Wakatoliki, tunapaswa kuzingatia mfano wa Yesu Kristo, ambaye alikuwa mkarimu kwa wote aliokutana nao. Aliponya wagonjwa, aliwafariji walio na huzuni, na aliwapa wengine riziki. (Mathayo 25:35-36)

  4. Kwa kuishi katika huruma ya Mungu, tunajifunza kutenda kama Kristo alivyotenda. Tunapaswa kuwa wema kwa wengine kama vile Mungu alivyokuwa kwetu. (Waefeso 4:32)

  5. Kifo cha Kristo msalabani ni mfano mkuu wa huruma ya Mungu. Alitujalia msamaha wetu hata kama hatustahili. Kwa hiyo, tunapaswa kuwajalia wengine msamaha na huruma, kama vile Mungu alivyotujalia. (Warumi 5:8)

  6. Tunajifunza kutenda haki na kumtukuza Mungu kwa kuishi katika huruma yake. Tunapaswa kufanya kazi kwa bidii kwa ajili ya wengine na kwa utukufu wa Mungu. (Wakolosai 3:23-24)

  7. Katika Kitabu cha Ufunuo, tunaona mfano wa watakatifu wanaoishi katika huruma ya Mungu. Wanaokoa maisha ya wengine na kuwasaidia kwa ukarimu. (Ufunuo 7:9-10)

  8. Kutubu na kupokea msamaha wa Mungu ni sehemu muhimu ya kuishi katika huruma yake. Tunapaswa kujitahidi kuepuka dhambi na kuomba msamaha kwa Mungu wakati tunakosea. (Zaburi 32:5)

  9. Kuna watakatifu wa Kanisa Katoliki ambao walikuwa wakarimu sana na waliishi katika huruma ya Mungu. Kwa mfano, Mtakatifu Francis wa Assisi alikuwa na upendo mkubwa kwa wanyama na watu wote, wakiwemo maskini na wagonjwa.

  10. Kwa kufuata njia ya utakatifu na ukarimu, tunaweza kuwa chombo cha Mungu kwa wengine. Tunaweza kuwa na athari nzuri katika maisha ya wengine na kuzidisha huruma ya Mungu duniani.

Je, wewe ni mkarimu kwa wengine? Je, unajitahidi kuishi katika huruma ya Mungu? Njia hii inaweza kuboresha maisha yako na kufungua fursa za kuwahudumia wengine.

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu familia na ndoa?

Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu familia na ndoa? Kanisa Katoliki linaamini kuwa familia na ndoa ni muhimu sana kwa ustawi wa jamii na kwa maendeleo ya wanadamu. Kulingana na Biblia, Mungu alimuumba Adamu na Eva na kuwapa amri ya kuzaa na kujifanyia utawala wa dunia yote.

Kanisa Katoliki linazingatia familia kama msingi wa jamii. Familia ni mahali ambapo watu hupata upendo, usalama na kujifunza kuhusu utu wao. Kwa hivyo, Kanisa linapigania ustawi wa familia na kuhakikisha kuwa inapata msaada wa kiroho, kifedha na kisheria.

Kanisa Katoliki limeelezea ndoa kama muungano wa kudumu kati ya mwanamme na mwanamke ambao hufungwa na Mungu. Kwa hivyo, ndoa ni sakramenti takatifu ambayo haiwezi kuvunjwa na kila mmoja anapaswa kuilinda kwa heshima na upendo. Kulingana na Kanisa Katoliki, ndoa sio tu kuhusu kupata watoto, lakini pia ni kuhusu kujenga uhusiano wa kudumu ambao unajumuisha upendo, uvumilivu, na kujitolea.

Kanisa Katoliki linadai kuwa ndoa inapaswa kufungwa kwa hiari na uhuru kamili wa mawazo. Kwa hivyo, kila mwanamume na mwanamke anapaswa kuelewa wajibu wake kabla ya kuingia kwenye ndoa. Kanisa linapinga talaka na anahimiza ndoa zifungwe kwa kudumu. Talaka inachukuliwa kama kitendo cha kuvunja mkataba wa sakramenti ya ndoa na hivyo ni kinyume na mapenzi ya Mungu.

Kanisa Katoliki pia linaamini kuwa familia ni muhimu sana kwa maendeleo ya binadamu. Familia inapaswa kuwa mahali ambapo watoto wanapata maadili ya kimaadili, kiroho, na kimaadili. Kwa hivyo, Kanisa linahimiza familia zifanye kazi kwa pamoja katika kuelimisha watoto na kuwaongoza katika safari ya maisha yao.

Kanisa Katoliki linatoa msaada wa kiroho kwa familia kwa njia ya mafundisho ya kikatoliki, maombi, na sakramenti. Kwa hivyo, Kanisa linahimiza familia zifanye kazi kwa pamoja katika kuelimisha watoto na kuwaongoza katika safari ya maisha yao.

Kwa hivyo, ni muhimu kwa familia na ndoa kufuata mafundisho ya Kanisa Katoliki. Kwa kufanya hivyo, familia na ndoa zitakuwa imara na kudumu zaidi. Katika Wakolosai 3:14-15, tunasoma "na juu ya yote hayo jipeeni upendo ambao ni kifungo kikamilifu cha kusanyiko; na amani ya Kristo iitawale mioyoni mwenu, kwa maana kwa jambo hilo mmeitwa katika nafsi moja, tena iweni wenye shukrani." Kwa hivyo, tunahitaji kujitolea kwa upendo na kujenga amani ndani ya familia na ndoa zetu ili kufikia utimilifu katika maisha yetu.

Tarehe ya Pasaka inavyopatikana

KWANINI TAREHE ZA PASAKA HUBADILIKA KILA MWAKA ??

JIBU:
KALENDA za mwanzo ziliutumia mwezi wa
angani kama kipimo cha muda. Ziliitwa “Lunar
calender” au Kalenda-Mwezi. Tarehe 1 ya
Mwezi ilikuwa ni siku ulipoandama yaani
Mwezi-Mdogo (Crescent Moon).
Mwezi unapofika siku ya 15 unakuwa umefikia
ukubwa wa juu na huitwa Mwezi-Mkubwa (Full
Moon). Hivyo kwa kalenda ile tarehe 15
ilikuwa ni siku ya Mwezi-Mkubwa.
Mwaka 45KK, Julius Caesar alitangaza kalenda
mpya ikaitwa “Julian Calender” iwe na siku
365.

Wakati huo ikijulikana kwamba jua
huzunguka kwa siku 365.25. Hivyo pengo la
kalenda na mzunguko likabaki robo siku.
Robo hiyo ifidiwe kila baada ya miaka minne
mwishoni mwa mwezi Februari ambayo sasa
ulifanywa kuwa wa pili baada ya January.
Inapofanyika hivyo, huo ukaitwa mwaka-mrefu
(Leap year).
Mwaka mrefu ukachaguliwa kuwa ni ule tu
unaogawanywa kwa nne mfano miaka ifuatayo
1700, 1800, 1900, 2100, 2200, 2300.
Baadaye iligundulika kuwa dunia huzunguka kwa
siku 365.24218967 ziitwazo “Tropical year”.
Hizi ni chache kuliko siku 365.25
zilizokadiriwa mwanzoni. Uchache huu
husababisha kuwe na pengo la dakika 11 na
sekunde 14.812512 kwa mwaka.
Pengo hili ni dogo, lakini hupanuka hadi kuwa
siku nzima kila baada ya miaka 128.0355.
Mwaka 1545 lilivuka siku 9.25.
Kuondoa tatizo hili, Papa Gregory XIII aliamuru
iundwe kalenda mpya na akachagua Oktoba
04, 1582 iwe siku ya mwisho kutumika “Julian
Calender”. Kesho yake, kalenda mpya ikaanza
kutumika. Ungetegemea hiyo kesho iwe ni
Oktoba 05, 1582. Lakini ili uzibe pengo lile
lililofikia siku kumi, ilibidi kalenda mpya
kuziruka siku hizo siku kumi. Hivyo hii mpya
iliyoitwa “Gregorean Calender” ikaanza kama
Oktoba 15 badala ya Oktoba 05.
Ndiyo sababu katika historia ya nchi nyingi
Ulaya, hakuna tarehe za Oktoba 05, 1582 hadi
Oktoba 14, 1582. Watu walilala Oktoba 04,
1582 kesho yake wakaamka ikiwa ni Oktoba
15, 1582.

Teresa Alonso huandikwa kwamba alifariki
Oktoba 1582, kwenye usiku wa tarehe NNE
kuamkia tarehe KUMI NA TANO! Alipotangazwa
kuwa Mtakatifu, Kanisa Katoliki likaifanya
Oktoba 15 kuwa siku ya kumkumbuka, yaani
siku ya Mtakatifu Teresa wa Avila.
Usipofahamu kwamba Mtakatifu Teresa alifariki
siku kalenda zinabadilishwa, utadhani
aliyeandika vile tarehe za kifo chake
amekosea!
Waandishi, William Shakespeare wa Uingereza
na Miguel de Cervantes wa Spain huandikwa
kwamba wote walifariki Aprili 23, 1616. Lakini
ukweli ni kwamba hawakufa siku moja bali
walipishana siku kumi kwani England
ilichelewa kwa karibu miaka 200 kuikubali
“Gregorean Calender”!
“Gregorean Calender” haikuundwa ili kuishia
kuliziba lile pengo. Bali pia, kuhakikisha
halitokei tena. Tumeshaona kuwa lile pengo ni
dakika 11 na sekunde 14.812512. Hivyo,
linapanuka na kuwa siku tatu ndani ya miaka
400.

Hivyo kuliziba inatakiwa kupunguza siku tatu
kila baada ya miaka 400. Je, zipunguzweje?
Kipande cha miaka 400 kina miaka mitatu ya
karne inayogawanyika kwa 4 lakini
haigawanyiki kwa 400.
Ikakubalika kwamba unaogawanyika kwa 4,
lakini haugawanyaiki kwa 400, usiendelee
kuwa mrefu. Humo siku moja ichomolewe na
uwe mfupi.
Ndipo miaka 1700, 1800, 1900 haikuwa tena
mirefu. Ndivyo pia miaka 2100, 2200, 2300
nayo haitakuwa mirefu. Kwa sababu ni miaka
ambayo “Gregorean Calender” inachomoa siku
moja ili kutosababisha pengo tena.
Kipande hiki cha miaka 400 kikaleta wastani
mpya wa siku 365.2425 kwa mwaka. Sasa lile
pengo lile la siku moja si rahisi kufikiwa.
Kwenye “Julian Calender” tumeona lilikuwa
miaka 128.0355 lakini sasa limekuwa miaka
3,222.
Sasa tuijadili tarehe ya siku ya Pasaka tukiwa
na ufahamu wa kalenda zile. Je, tarehe ya
Pasaka imetajwa ndani ya Biblia? Kuna kifungu
kinasema hivi:
“..Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya
mwezi, wakati wa jioni, ni Pasaka ya BWANA.
Na siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni
sikukuu ya BWANA, ndiyo siku ya mikate
isiyotiwa chachu. (Walawi 23:5)..”. Hivyo
Pasaka ni tarehe 15 ya mwezi wa Kwanza.
Lakini Biblia pia inautaja mwezi wa kwanza
kwa jina la Nisan (Esta 3:7, Nehemia 2:1).
Yesu alisulubiwa mwaka ambao Ijumaa
iliitangulia sikukuu ya Pasaka kwa siku moja
(Yohana 18: 28, Marko 15:42-43). Hivyo
tarehe ya Yesu kusulubiwa ni Ijumaa, Nisan
14. Siku moja kabla ya Nisan 15. Siku moja
kabla ya Mwezi-Mkubwa.
Baada ya Yesu, Wakristo wengi Pasaka
waliiadhimisha Jumapili, lakini utata ulijitokeza
kuhusu tarehe ya kuiweka hiyo Jumapili ya
Pasaka. Ilifika wakati jimbo moja la Wakristo
linaadhimisha siku tofauti na jingine na kwa
njia wanayoijua wao.

Utata huu uliondolewa kule Nicaea mwaka 325
ambapo Kanisa Katoliki lilipoamua kuwa,
tarehe ya Pasaka iwe moja tu duniani kote,
yaani iwe ni Jumapili inayokuja baada ya
Mwezi-Mkubwa (Full Moon) unaotokea baada
ya siku ya Ikweta, yaani baada ya Machi 21
(Equinox).
Baada ya uamuzi huu, wataalamu walipania
kuunda chati maalum zenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa zitazokasaidia kuitambua tarehe ya
Pasaka kwa mwaka wowote.
Mwezi huizunguka dunia kwa siku
29.5305891203704 (Synodic Month), wakati
dunia hulizunguka jua kwa siku 365.24218967
(Tropical year).
Mizunguko hii miwili ikianza safari siku moja,
itapishana kila mwaka, lakini itakutana tena
mwezi unapokamilisha mizunguko 235. Dunia
nayo inakuwa imekamilisha mizunguko 19,
yaani miaka 19.
Wataalamu wakaitumia hii miaka 19
kutengeneza chati yenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa unaotokea March 22 hadi April 18.
Tarehe zile zikaitwa tarehe za Mwezi-Mkubwa
Wa Pasaka au Ecclesiastical Full Moon (EFM).
Ndani ya ile miaka 19, kila mwaka ukapewa
tarakimu iitwayo Golden Number inayosimama
badala ya mwaka ikiwa na tarehe zile
ziliorekodiwa za Mwezi Mkubwa wa Pasaka.
Chati yenyewe ya Golden Number na tarehe
zake (siku/Mwezi) ni hii ifuatayo: {1=5/4,
2=25/3, 3=13/4, 4=2/4, 5=22/3, 6=10/4,
7=30/3, 8=18/4, 9=7/4, 10=27/3, 11=15/4,
12=4/4, 13=24/3, 14=12/4, 15=1/4, 16=21/3,
17=9/4, 18=29/3, 19=17/4}
Golden Number ya mwaka inapatikana kuanza
kuugawa mwaka kwa 19. Tulifundishwa
mashuleni kuwa namba inayosalia baada ya
kugawa huitwa “Baki” . Hii “Baki” ukiijumlisha
na 1 unapata Golden Number (GN).
Mfano unatafuta GN ya 27. Hatua ya kwanza ni
kutafuta “Baki” baada ya kugawa 27 kwa 19.
Hizi ni hesabu za “modulo” , yaani zinahitaji tu
namba inayobaki baada ya kugawa.
Ikiandikwa hivi: (27 mod 19) inatakiwa namba
inayobaki baada ya kuigawa 27 kwa 19. Jibu
ni 8. Hivyo tulipaswa tuandike hivi: (27 mod
19=8). “Baki” 8 tuliyoipata, ndiyo tunaihitaji ili
tuijumlishe na 1 ili tupate GN ambayo hapa ni
9 kwani (8+1=9).

Tungeweza pia kuandika hivi : 27 mod 19 +
1=9. Hivyo kanuni ya kupata GN kwa mwaka
wowote ni hii:
(MWAKA mod 19 + 1). Yaani, ugawe huo
mwaka kwa 19, kisha namba itakayobaki
ijumlishe na moja.
Ukishaipata GN, itafute kwenye ile chati
ambapo utaiona ikiwa na mwezi na tarehe.
Jumapili inayofuata baada ya tarehe hii ndiyo
tarehe ya Pasaka ya mwaka huo.
Tutumie chati ile na kanuni hii kujua tarehe ya
Pasaka ya mwaka 1474. GN ni (1474 mod 19 + 1=12). Hivyo GN ni 12.
Kwenye chati, 12 inaonyesha ni tarehe 4/4.
Hivyo, mwaka 1474 Mwezi-Mkubwa wa
Pasaka ulikuwa tarehe 4/4/1474. Hiyo ilikuwa
ni Jumatatu. Hivyo Pasaka ilikuwa ni Jumapili
iliyofuata yaani tarehe 10/4/1474.
Lakini, Kanisa Katoliki liliikubali kanuni hii
karne ya sita. Hii ndiyo sababu, tarehe za
Pasaka zinazojulikana ni zile tu zinazoanza
mwaka 533.

Ndivyo Pasaka ilivyotafutwa miaka ile. Sasa
tuone Pasaka ya kizazi chetu. Kizazi cha
“Gregorean Calender” iliyoanza mwaka 1582.
Tumelijadili lile pengo la siku lililofikia ambalo
mwaka 1582 lilishafika siku 10. Ukweli ni
kwamba kabla halijazibwa, Pasaka ilikuwa
inawadia lakini uhalisi ni kwamba inakuwa
tayari imepitwa siku 10. Kinyume kabisa na
maamuzi ya Kanisa kule Nicaea!
Ili kulizuia lisitokee tena, tumeona uchomoaji
wa siku moja toka kwenye miaka inayofunga
karne, isiyogawanyika kwa 400. Uchomoaji
huu umewekwa kwenye kanuni (formula)
iitwayo “Solar Equation”.
Kama mwendo wa kuzunguka jua
umezingatiwa na “Gregorean Calender”, vipi
kuhusu mwendo wa mwezi?
Tumeuona kwamba mizunguko ya mwezi na
dunia hukutana kila baada ya miaka 19.
Kadirio la dunia kuzunguka kwa siku 365.25
linafanya ikizunguka kwa miaka 19 zinakuwa
siku 6,939.75. Mwezi utakuwa nao
umezunguka mara 235, huku kila mzunguko
ukitumia siku 29.5305891203704.
Hivyo, kukutana kule ndani ya kila miaka 19,
huleta pengo dogo la saa 1, dakika 28,
sekunde 38.5.
Mapengo madogo haya tunayoyapuuza
mwanzoni, yameshatugharimu vya kutosha.
Pengo hili kwa mwaka ni dogo lakini kwa
miaka 2500 linakuwa hadi kufika siku nane.
Kwenye hesabu za kutafuta Pasaka
urekebishaji wa hili pengo hutokea kwenye
kanuni iitwayo “Lunar Equation”. Lakini kwa
sababu ya tofauti ya uelekeo wa mzunguko wa
mwezi na dunia, “Lunar Equation” hujumlisha
mara nane kila baada ya miaka 2500.
Hivyo, mahesabu yoyote ya kuitafuta tarehe ya
Pasaka hayakosi kanuni hizi mbili “Solar
Equation” na “Lunar Equation” .
Tumeona kwamba kalenda ilianza mwaka
1582. “Solar Equation” inaondoa siku moja
toka kwenye miaka 1700, 1800, 1900. Hivyo,
ni kujidanganya kusema kwamba miaka yote
inayogawanyika kwa nne ni mirefu, jambo
ambalo hata mimi nilifundishwa shuleni. Hapa
tumeona kwamba “Solar Equation” imeondoa
siku moja kwenye mwaka 1900 na hivyo
haukuwa mwaka mrefu ingawa unagawanyika
kwa nne.

“Lunar Equation” huongeza siku moja kwenye
miaka 1800, 2100, 2400. Mwaka 1800
unaguswa na vyote “Solar Equation” na “Lunar
Equation”. Hivyo hauathiriki.
Kanuni zote za kuitafuta Pasaka huzingatia
zaidi ya niliyoyaeleza, lakini cha muhimu zaidi
ni hizi mbili yaani “Solar Equation” na “Lunar
Equation” ambazo sijawahi kuzisikia kwa
kiswahili.
Ni vigumu kuepuka hesabu za “modulo” au
“mod” unapotafuta tarehe ya Pasaka. Lakini
ukiwauliza wanafunzi wa darasa la nne
kwamba machungwa 2011 yakipangwa kwenye
mafungu 19, ni mangapi yatakosa fungu?
Wapo watakaopata jibu sahihi kwamba ni
machungwa 16. Kimahesabu swali hilo
linaandikwa hivi: (2011 mod 19) na jibu lake
ni 16, yaani (2011 mod 19=16).
Ifuatayo ni moja ya kanuni zinazotumika
kuipata tarehe za Pasaka ya mwaka wowote
kuanzia 1700 hadi 2099:
(1) : a=MWAKA mod 19;
(2) : b=MWAKA \ 100;
(3) : c=MWAKA mod 100;
(4) : d=b \ 4;
(5) : e=b mod 4;
(6) : f=c \ 4;
(7) : g=c mod 4;
(8) : h=(b + 8)\25;
(9) : i=(b – h + 1)\3;
(10) : j=(19xa + b – d – i + 15) mod 30;
(11) : k=(32 + 2xe + 2xf – j – g) mod 7;
(12) : m=(a + 11xj + 22xk) \ 451;
(13) : n=j + k – 7xm + 114;
(14) : Tarehe=(n mod 31) + 1
(15) : Mwezi =n\31;

Penye neno MWAKA, andika mwaka unaotafuta
kujua tarehe yake ya Pasaka. Panapotokea
alama (\) ni kugawanya ambako hata kama
jibu litaleta desimali, basi hiyo desimali
unatakiwa kuachana nayo ili jibu libaki namba
nzima. Penye alama (x) hiyo ni ya kuzidisha.
Yafuatayo ni majibu niliyopata kwa hatua zote
baada ya kuuingiza mwaka 2017 ili kujua siku
ya Pasaka ya mwaka huu: (1): 3, (2): 20, (3):
17, (4): 5, (5): 0, (6): 4, (7): 1, (8): 1, (9): 6,
(10): 21, (11): 4, (12): 0, (13): 139, (14): 16,
(15): 4.
Tarehe imepatikana kwenye hatua ya 14
ambako jibu ni “16”. Mwezi umepatikana
kwenye hatua ya 15 ambako jibu ni “4”. Hivyo
Pasaka ya mwaka (2017) huu ni Tarehe 16,
mwezi wa 4.
Hivyo, kwa njia hii, unaweza kujua tarehe za
Pasaka kwa miaka ijayo kama unavyoijua
tarehe ya Krismas. Kama kuna tukio lilifanyika
siku ya Pasaka miaka iliyopita na hukumbuki
tarehe, basi tumia kanuni hii.
Zifuatazo ni siku zinazoitangulia Pasaka kwa
idadi ya siku zilizoandikwa kwenye mabano:
Jumatano Ya Majivu (46), Jumapili ya Matawi
(7), Ijumaa Kuu (2).
Zinazotanguliwa na Pasaka ni hizi zifuatazo:
Kupaa (42), Pentekoste (49), Utatu Mtakatifu
(56), Ekaristi (63).
Mwanzo tuliona kwamba Mwezi-Mkubwa wa
Pasaka au “Ecclesiastical full Moon” ni ule wa
March 22 hadi April 18. Ukitokea March 22
basi kuna uwezekano siku hiyohiyo ikawa
Pasaka na ikawa imevunja rekodi ya kuwahi
mapema.
Ukitokea April 18, kuna uwezekano wa Pasaka
kuwa siku saba zaidi ya hapa yaani April 25,
na hiyo ikawa ni tarehe ya juu mno ya Pasaka.
Hivyo, Pasaka yoyote haiwezi kuwa chini ya
Machi 22, wala haiwezi kuwazaidi ya April 25.
Pasaka tuliyoiona mwaka 2008 ndiyo ya
mwisho kwa kizazi chetu kuiona ikiwahi
mapema kiasi kile, kwani ilitokea Machi 23 na
itairudia tena tarehe hiyo mwaka 2160!

NB: iyo ni moja tu ya kanuni(formula) zitumikazo kupata tarehe na mwezi wa pasaka ya kila mwaka

Nawatakia kwaresma njema…..

Je, Kuangalia Picha za Ngono ni dhambi?

Neno la Msingi:
Zaburi 101:3
“Sitaweka mbele ya macho yangu Neno la uovu. Kazi yao waliopotoka naichukia, Haitaambatana nami.”
Watu wengi wameanguka katika mtego huu wa Ibilisi na kujikuta wakifanya mambo ya “AIBU” wanapokuwa sehemu zao za Siri iwe ni chumbani au bafuni.
Wanaume wamejikuta wakipiga punyeto (Mastubation) na Wanawake wakijisaga ( wanatumia mikono yao na viungo vyao vingine kama njia ya kujikidhi hali zao za tamaa mbaya waliloziamsha wao wenyewe). Haipaswi kamwe kuwa hivyo. Biblia inasema tusiyachochee wala kuyaamsha “mapenzi” mpaka yatakavyoona yenyewe (Wimbo ulio bora 2:7, 3:5). Naomba tufuatane pamoja kwenye somo hili muhimu sana ambalo litakuweka huru mbali na “utumwa wa fikra za kingono”

1. MAANA YA PICHA ZA NGONO

Neno PICHA ni kivuli cha mtu, watu, kitu n.k. PICHA si kitu halisi bali ni kivuli chake. Unaweza ukapewa PICHA ya mtu lakini usifahamu urefu wake au ni mfupi kiasi gani lakini sura yake ukawa umeiweka katika kumbukumbu yako. NGONO ni kitendo cha mtu, watu kufanya kitendo cha kujamiana (Tendo la Ndoa) na pia ni ile hali ya kuwa uchi wa mnyama. Kuangalia picha za ngono ni kitendo cha kuangalia watu wakifanya Matendo ya kujamiana iwe kwa njia ya asili, kinyume na maumbile au kufanya na wanayama. Kitendo hicho huleta kuchochea tamaa ya miili kiasi ambacho watu wengine hufanya mambo ya “AIBU” katika nyumba zao (Warumi 1:24-28). PICHA za NGONO zimeenea kila mahali kwa sasa, kwenye simu yako unaweza ukakutana na “uchafu” wa namna hiyo. Wahindi wao picha za ngono huziita “kachumbali” na unaweza ukamkuta Mhindi amekaa na familia yake anaangalia “kachumbali” wanadai inanogesha utamu wanapofika kitandani. Huko ni kujidanganya Mungu hakumletea Adamu PICHA ya NGONO bali alimletea mke ambaye watashirikiana naye kwenye Tendo Takatifu (Mwanzo 2:18, 21-25). Wakati mmoja Mfalme Daudi wakati watu wake wa vita wamekwenda vitani yeye akawa yuko ghorofani anaangalia “PICHA LIVE” ya NGONO mwanamke alikuwa akioga matokeo yake yakawa ni kufanya kitendo chenyewe na kuamua kumuua mume wa Bathsheba (2Samweli 11:2-27).
“Ikawa wakati wa jioni, Daudi akaondoka kitandani, akatembea juu ya dari ya jumba la mfalme; na alipokuwa juu ya dari aliona mwanamke anaoga; naye huyo mwanamke alikuwa mzuri sana, wa kupendeza macho. Naye Daudi akapeleka, akauliza habari za yule mwanamke. Mtu mmoja akasema, Je! Huyu siye Bath-sheba, binti Eliamu, mkewe Uria, Mhiti?”………..
Kile kitendo cha Daudi “kuona” lilikuwa kosa kubwa la kiufundi katika akili yake likamchanganya. Ndivyo ilivyo kwa PICHA ZA NGONO lazima ukiangalia upate “UKICHAA” wa muda ukajikuta umeng’ang’ania sabuni au ndizi ukiwa unapiga punyeto. Ni aibu sana sana mtu mwenye heshima zako kama wewe labda wewe ni meneja, mkurugenzi, mtu mwenye Elimu yako ya maana unakutwa unaangaika sabuni, godoro au toy la jinsia ya kiume.

2. JE! KUANGALIA PICHA ZA NGONO NI DHAMBI?

Kuangalia picha za ngono “NI DHAMBI” kwa herufi kubwa. Katika Sheria ya Musa ilikuwa mtu anahesabika kuwa ametenda dhambi pale ambapo atakutwa akifanya kitendo hicho au kukiwa na mashahidi wawili au watatu atatakiwa kuhukumiwa sawasawa na Sheria husika. Kwenye dhambi ya uzinzi mtu alitakiwa apigwe mawe hadi afe sivyo kwa Sheria ya Kristo yenyewe inazungumzia juu ya kitendo cha “kutamani” tu unahesabika kuwa umefanyika DHAMBI (Mathayo 6:27-29, Waebrania 10:28). Tamaa mbaya ni dhambi kama dhambi nyinginezo. Kwa kawaida tamaa huja na ile tamaa huchukua mimba na baadaye huzaa dhambi (Yakobo 1:13-16). Kitendo cha kuangalia picha za ngono hupofusha “FIKRA” nzuri za mtu alizonazo. Mawazo machafu uanza kutawala katika ubongo wako hadi “USHUSHE” huo mzigo ulioko kwenye viungo vyako vya uzazi. Ahaaa ni hatari aiseeee. Wewe unayengalia picha za ngono Kama ndiyo starehe yako unaiharibi nafsi yako “unakuwa zezeta wa akili” Biblia inasema “taa ya Mwili jicho na jicho lako likiwa safi mwili wako wote utakuwa na nuru. Lakini jicho lako likiwa bovu mwili wako wote utakuwa na giza..”(Mathayo 6:22-23). Kwa wale wanandoa ni “MWIKO” kutumia picha za ngono ili kunogesha kufanya Tendo la Ndoa. Wewe mume unaye hapo “chombo” unakiona “live” na kimethibitishwa na Mungu mwenyewe sasa hiyo mipicha ya nini? Kila kiungo Mungu alikiweka kwa ajili ya kusudi maalum kama ni mdomo kwa ajili ya kuongea na kupitisha chakula na si kunyonya sehemu za Siri za mwenzi wako. Mungu ameweka sehemu ya “haja kubwa” kwa ajili ya kutolea uchafu uliotengenezwa na tumbo na si kiungo kingine kiende kukoroga “zege” hilo huo ni uchafu(Ufunuo 22:10-15).
Warumi 1:26:27
“Hivyo Mungu aliwaacha wafuate tamaa zao za aibu, hata wanawake wakabadili matumizi ya asili kwa matumizi yasiyo ya asili; wanaume nao vivyo hivyo waliyaacha matumizi ya mke, ya asili, wakawakiana tamaa, wanaume wakiyatenda yasiyopasa, wakapata nafsini mwao malipo ya upotevu wao yaliyo haki yao.”

3. JINSI YA KUSHINDA DHAMBI YA KUANGALIA PICHA ZA NGONO

PICHA ZA NGONO zinavutia sana kuziangalia ila zina maangamizo makubwa sana katika maisha yako. Lazima ufikie mahali kukata shauri ndani ya Moyo wako kuambatana na Mungu. Kusudi kubwa la shetani kuachilia mambo yake ya NGONO kwenye mitandao ili apate wafuasi wengi zaidi. Hakuna kitu unachoweza kukifanya katika simu za Android wengine wasikitambue. Kila unalolipitia na kuliangalia kwa Siri siku ya siku litaletwa hukumuni na Mungu mwenyewe (Warumi 2:16, Mhubiri 12:14)

USHAURI WAKIVITENDO:

I) Yatie Nuru macho yako – Zaburi 13:3, 19:8 – Yaruhusu macho yako yaingiziwe nuru na Yesu. Chukua muda wa kutosha kuingiza PICHA zinazomhusu Mungu zaidi. Angalia wahubiri mbalimbali.
II) Tazama mambo ya Adili(mema) – Zaburi 17:2-3 – Kuna nguvu kubwa sana tunapokuwa tunaangalia mambo mema. Vipindi vizuri vya neno la Mungu. PICHA zinazojenga siyo zinazoharibu fikra zetu.
III) Kumuomba Mungu afumbue macho yako – Zaburi 119:18, 146:8- Maombi ni muhimu ili kufanya macho yako kuona kusudi la Mungu na Kutambua uwepo wa shetani katika PICHA ZA NGONO.
IV) Weka maneno ya Mungu Mbele za macho yako – Mithali 4:20-21
Wakati wote soma neno la Mungu kupitia kifaa chochote cha ki-electronic ili uweze kumjua Mungu zaidi.
V) Macho yako yatazame Mbele – Mithali 4:25-27
Kutazama Mbele maana yake uwe na maono. Maono ni PICHA au TASWIRA ya Mbele ya maisha yako. Yeremia aliulizwa unaona nini naye akasema “anaona ufito wa mlozi” anaona kitu kizuri (Yeremia 1:11-12).
VI) Pendezwa na njia za Mungu – Mithali 23:26
Kuanzia sasa anza kupendezwa na njia za Mungu katika maisha yako. Acha kuzifuata njia zako katika kuufurahisha mwili wako wa PICHA zisizofaa.
VII) Tafuta watumishi wa Mungu ili wakufundishe – Isaya 48:17, 30:20-21
Kuna mambo ambayo yanatupa shida katika maisha yetu ni vizuri kuwaona waalimu ili watusaidie jinsi ya kutoka katika mtego huo.
VIII) Omba rehema na neema ya Yesu – Waebrania 4:16
Tunahitaji neema ya Mungu ili kushinda Hali hiyo ya kupenda KUANGALIA PICHA ZA NGONO na pia kufunguliwa kutoka katika vifungo hivyo vya pepo wa tamaa na mahaba.
Mungu atakubariki ukipeleka ujumbe huu kwa wengine

MATATIZO YANAYORUDISHA UIMBAJI WA KWAYA KATOLIKI NYUMA

1.Kuwaimbia binadamu.Yaani tupo kwa ajili ya kuimba ili tusifiwe na watu.
2.Kuimba bila tafakari.Mara nyingi tunaimba tu bila kuzingatia ujumbe Wa ule wimbo
3.Kuimba bila kusali!Yasemekana Kuimba ni kusali Mara mbili.Waimbaji wengi hukariri wimbo na nyimbo nyingi zimetungwa kwa njia ya sala lakini wanakwaya wengi huimba tu wala hali ya sala haimo ndani yao!
4.Walimu wenye hasira na ubinafsi.Mkufunzi Wa kwaya ni nguzo muhimu kwa maendeleo ya uimbaji.Iwapo choirmaster ni mwenye vurugu, mchochezi na mpenda fitina, bila shaka itakuwa vigumu kwa kwaya kupiga hatua kiuimbaji!
5.Sheria Kali zisizoenda na maadili ya kanisa.Kila jamii INA sheria zake na sheria ni nzuri.lakini tukiwa na sheria zinazowakandamiza wengine, tutapoteza kondoo wengi badala ya kuwaleta kwa Mungu!
6.Utoaji Wa albamu au kurekodi nyimbo kwa nia ya kutafuta pesa au kigezo kwa kwaya.Kwaya nyingi zimeanguka pindi tu wanapotoa albamu ya kwanza!Maana tunakosa kufahamu kuwa sisi ni wainjilisiti na tunawasaidia mapadri wetu kuhubiri injili.
7.Kutotii viongozi Wa kanisa.Wanakwaya wanaokosa kufahamu kuwa wapo chini ya viongozi na kanisa husika Mara nyingi hujipata wakiwa kwa makosa bila kunuia!
8.Kutoishi kwa hali ya sakramenti!Kama kuna jambo kubwa ambalo ibilisi hufurahia, ni yule MTU anayeishi katika maisha ya ndoa isiyo halali mbele za Mungu.Yaani Maana yake unaishi na mke au Mme bila ndoa ya kanisa na huna kizuizi chochote kinachokufanya usipate sakramenti hiyo.
9.Kitubio.Wengi tunapokea sakramenti ya ekaristi katika hali ya dhambi na hatushughuliki kabisaa kwenda kitubio.Hii inachochea zaidi kuwepo kwa dhambi za mazoea katika maisha yetu!
10.Kutosali kila siku.Inakuwa rahisi kwetu sisi kujaribiwa tukiwa hatusali.Kuimba kwako kunawasha hasira za shetani kwa hivo usiposali, bila shaka atarudi kulipiza kisasi.

Utaratibu wa Mkristo Mkatoliki Kanisani

Ninapoingia kanisani nachovya maji ya baraka na kusema;
“Unitakase Ee Bwana mimi na uovu wangu wote, ili nipate kustahili kushiriki ibada takatifu’ Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu” Amina!
Ninapiga goti huku nikisema
“Mungu wangu na Bwana wangu”
🙋🏽Nikiinuka nasema
“Nitakusifu na kukuabudu katika Ekaristi takatifu”
🙋🏽Naenda mpaka kwenye bench, napiga magoti au nakaa nikiwa mimeinamisha kichwa (kama mabenchi yameisha nabaki nimejisimamia) huku nikitoa nia yangu ya kusali misa siku hiyo, mfano
“Ee Mungu, ninaungana nawe na jeshi lote la mbinguni, pamoja na Mama Bikira Maria, nikiwa na nia ya kumwombea mama yangu ambaye ni mgonjwa, jirani yangu ambaye mpaka sasa hatuelewani na pia familia yetu ambayo haina amani, Mungu kupitia misa hii rejesha hali ya mama yangu, rejesha uelewano na jirani yangu, na pia rejesha amani ya familia yetu pamoja na familia zote ambazo hazina amani”
🙋🏽Ninaendelea na misa na Kushiriki litrujia kikamilifu
🙋🏽Wakati wa komunyo nikikumbuka kuwa nina dhambi kubwa huwa nakominika kwa sala ya tamaa wala siendi mbele, huwa najikalia tu kwenye bench naangalia wenye moyo safi wanaenda mbele kumpokea Yesu (Kweli huwa najisikia wivu sana, itanibidi katikati ya wiki nifanye kitubio ili nisikae tena)”
🙋🏽Mwisho wakati wa kuondoka nachovya maji ya baraka nikisema
“Unilinde Ee Mwenyezi Mungu, nikapate kuwa mfano katika jamii yangu, na nikushuhudie katika matendo yangu”
(Hapo nachovya maji ya baraka na kufanya ishara ya msalaba) “Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, amina”
Usiku mwema wapendwa. Malaika awalinde

Ibada ya Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Upendo na Ukarimu

Ibada ya Huruma ya Mungu: Kuishi kwa Upendo na Ukarimu

Karibu kwa maelezo ya Ibada ya Huruma ya Mungu. Ibada hii ni sehemu muhimu ya maombi katika Kanisa Katoliki kama ilivyofundishwa na Kanisa. Ibada hii inatufundisha jinsi ya kuishi kwa upendo na ukarimu, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha.

  1. Kuanza Ibada ya Huruma ya Mungu kila siku

Kwa mujibu wa Catechism ya Kanisa Katoliki, Ibada ya Huruma ya Mungu ni muhimu kwa ajili ya maisha ya Kikristo. Kwa hivyo, unapaswa kuianza kila siku kwa kusali chaplet ya Huruma ya Mungu. (CCC 1419). Kusali chaplet hii kunaweza kutufungulia mioyo yetu kwa upendo wa Mungu.

  1. Kusamehe na kuwa tayari kusamehe

Hakuna mtu ambaye hajawahi kufanya makosa. Ni kwa kuwasamehe wengine ndipo tunaweza pia kusamehewa (Matthew 6:14-15). Hiyo ni kwa sababu, Bwana wetu Yesu Kristo alitufundisha kwamba kusamehe ni sehemu muhimu ya upendo na ukarimu.

  1. Kutenda wema na kutoa sadaka

Ibada ya Huruma ya Mungu inatufundisha pia jinsi ya kutenda wema na kutoa sadaka kwa wengine. (CCC 2447). Tunaweza kufanya hivyo kwa kufanya kazi za upendo, kutoa msaada na kuwa tayari kutoa mali zetu ili kusaidia wengine katika shida zao.

  1. Kumuomba Mungu kwa unyenyekevu

Tunapomwomba Mungu kwa unyenyekevu, tunafungua mioyo yetu kwa upendo na huruma yake. (CCC 2559). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kuomba huruma na kumwomba Mungu atusaidie kuishi kwa upendo na ukarimu.

  1. Kuwa na imani

Ibada ya Huruma ya Mungu inatufundisha pia jinsi ya kuwa na imani. Tunahitaji kumwamini Mungu na ahadi zake. Kwa kufanya hivyo, tunakuwa na uhakika kwamba Mungu atatupatia kila kitu tunachohitaji ili kuishi kwa upendo na ukarimu. (CCC 156).

  1. Kuwa tayari kuomba msamaha

Tunapojitokeza mbele ya Mungu kwa unyenyekevu na kuomba msamaha kwa mapungufu yetu, tunamruhusu Mungu kuingia ndani ya maisha yetu na kujaza nafasi zetu za udhaifu na upungufu. (CCC 2631). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kuomba msamaha kila wakati tunapojikuta tumeanguka au kutenda makosa.

  1. Kutafakari juu ya huruma ya Mungu

Kutafakari juu ya Huruma ya Mungu kunaweza kutusaidia kukua katika upendo na ukarimu. Kwa kufanya hivyo, tunaweza kufahamu zaidi jinsi Mungu anatupenda na anatujali. (CCC 2708). Tunaweza kutafakari juu ya Huruma ya Mungu kwa kusoma Injili, kusoma vitabu vya maombezi au hata kusoma Kitabu cha Maisha ya Mtakatifu Faustina Kowalska.

  1. Kujifunza kutoka kwa watakatifu

Watakatifu ni mfano wa kuigwa katika maisha yetu ya Kikristo, na wanaweza kutusaidia kukua katika upendo na ukarimu. (CCC 2683). Kwa hiyo, tunapaswa kujifunza kutoka kwa watakatifu kwa kusoma maisha yao na kufuata mifano yao.

  1. Kuwa na moyo wa shukrani

Kuwa na moyo wa shukrani ni muhimu katika maisha ya Kikristo. Tunapomshukuru Mungu kwa yote anayotufanyia, tunaujaza moyo wetu na upendo na ukarimu. (CCC 2648). Kwa hivyo, tunapaswa kuwa tayari kumshukuru Mungu kwa yote, iwe ni kubwa au ndogo.

  1. Kuishi kwa upendo

Kuishi kwa upendo ni muhimu katika maisha ya Kikristo. Kama ilivyofundishwa na Bwana wetu Yesu Kristo, upendo ni amri kuu ya Kanisa. (John 13:34-35). Kwa hivyo, tunapaswa kuishi kwa upendo kwa kila mtu, iwe ni mtu wa familia yetu, jirani, au mtu yeyote tunayekutana nae.

Ibada ya Huruma ya Mungu ni sehemu muhimu ya maisha yetu ya Kikristo. Inatufundisha jinsi ya kuishi kwa upendo na ukarimu, kama vile Bwana wetu Yesu Kristo alivyotufundisha. Je, umepata nafasi ya kusali Ibada ya Huruma ya Mungu leo? Je, unaishi kwa upendo na ukarimu katika maisha yako ya Kikristo?

Kwa nini tarehe ya Pasaka hubadilika

KALENDA za mwanzo ziliutumia mwezi wa
angani kama kipimo cha muda. Ziliitwa
“Lunar calender” au Kalenda-Mwezi. Tarehe 1
ya Mwezi ilikuwa ni siku ulipoandama yaani
Mwezi-Mdogo (Crescent Moon).
Mwezi unapofika siku ya 15 unakuwa
umefikia ukubwa wa juu na huitwa Mwezi-
Mkubwa (Full Moon). Hivyo kwa kalenda ile
tarehe 15 ilikuwa ni siku ya Mwezi-Mkubwa.
Mwaka 45KK, Julius Caesar alitangaza
kalenda mpya ikaitwa “Julian Calender” iwe
na siku 365. Wakati huo ikijulikana kwamba
jua huzunguka kwa siku 365.25. Hivyo pengo
la kalenda na mzunguko likabaki robo siku.

Robo hiyo ifidiwe kila baada ya miaka minne
mwishoni mwa mwezi Februari ambayo sasa
ulifanywa kuwa wa pili baada ya January.
Inapofanyika hivyo, huo ukaitwa mwaka-
mrefu (Leap year).
Mwaka mrefu ukachaguliwa kuwa ni ule tu
unaogawanywa kwa nne mfano miaka
ifuatayo 1700, 1800, 1900, 2100, 2200, 2300.
Baadaye iligundulika kuwa jua huzunguka
kwa siku 365.24218967 ziitwazo “Tropical
year”. Hizi ni chache kuliko siku 365.25
zilizokadiriwa mwanzoni. Uchache huu
husababisha kuwe na pengo la dakika 11 na
sekunde 14.812512 kwa mwaka.
Pengo hili ni dogo, lakini hupanuka hadi kuwa
siku nzima kila baada ya miaka 128.0355.
Mwaka 1545 lilivuka siku 9.25.
Kuondoa tatizo hili, Papa Gregory XIII
aliamuru iundwe kalenda mpya na akachagua
Oktoba 04, 1582 iwe siku ya mwisho
kutumika “Julian Calender”. Kesho yake,
kalenda mpya ikaanza kutumika.
Ungetegemea hiyo kesho iwe ni Oktoba 05,
1582. Lakini ili uzibe pengo lile lililofikia siku
kumi, ilibidi kalenda mpya kuziruka siku hizo
siku kumi. Hivyo hii mpya iliyoitwa
“Gregorean Calender” ikaanza kama Oktoba
15 badala ya Oktoba 05.
Ndiyo sababu katika historia ya nchi nyingi
Ulaya, hakuna tarehe za Oktoba 05, 1582
hadi Oktoba 14, 1582. Watu walilala Oktoba
04, 1582 kesho yake wakaamka ikiwa ni
Oktoba 15, 1582.
Teresa Alonso huandikwa kwamba alifariki
Oktoba 1582, kwenye usiku wa tarehe NNE
kuamkia tarehe KUMI NA TANO!
Alipotangazwa kuwa Mtakatifu, Kanisa
Katoliki likaifanya Oktoba 15 kuwa siku ya
kumkumbuka, yaani siku ya Mtakatifu Teresa
wa Avila.
Usipofahamu kwamba Mtakatifu Teresa
alifariki siku kalenda zinabadilishwa, utadhani
aliyeandika vile tarehe za kifo chake
amekosea!
Waandishi, William Shakespeare wa
Uingereza na Miguel de Cervantes wa Spain
huandikwa kwamba wote walifariki Aprili 23,
1616. Lakini ukweli ni kwamba hawakufa siku
moja bali walipishana siku kumi kwani
England ilichelewa kwa karibu miaka 200
kuikubali “Gregorean Calender”!
“Gregorean Calender” haikuundwa ili kuishia
kuliziba lile pengo. Bali pia, kuhakikisha
halitokei tena. Tumeshaona kuwa lile pengo
ni dakika 11 na sekunde 14.812512. Hivyo,
linapanuka na kuwa siku tatu ndani ya miaka
400.
Hivyo kuliziba inatakiwa kupunguza siku tatu
kila baada ya miaka 400.

Je, zipunguzweje?

Kipande cha miaka 400 kina miaka mitatu ya
karne inayogawanyika kwa 4 lakini
haigawanyiki kwa 400.
Ikakubalika kwamba unaogawanyika kwa 4,
lakini haugawanyaiki kwa 400, usiendelee
kuwa mrefu. Humo siku moja ichomolewe na
uwe mfupi.
Ndipo miaka 1700, 1800, 1900 haikuwa tena
mirefu. Ndivyo pia miaka 2100, 2200, 2300
nayo haitakuwa mirefu. Kwa sababu ni miaka
ambayo “Gregorean Calender” inachomoa
siku moja ili kutosababisha pengo tena.
Kipande hiki cha miaka 400 kikaleta wastani
mpya wa siku 365.2425 kwa mwaka. Sasa
lile pengo lile la siku moja si rahisi kufikiwa.
Kwenye “Julian Calender” tumeona lilikuwa
miaka 128.0355 lakini sasa limekuwa miaka
3,222.
Sasa tuijadili tarehe ya siku ya Pasaka
tukiwa na ufahamu wa kalenda zile. +++ Je, tarehe ya Pasaka imetajwa ndani ya Biblia?

Kuna kifungu kinasema hivi:
“..Mwezi wa kwanza, siku ya kumi na nne ya
mwezi, wakati wa jioni, ni Pasaka ya BWANA.
Na siku ya kumi na tano ya mwezi huohuo ni
sikukuu ya BWANA, ndiyo siku ya mikate
isiyotiwa chachu. (Walawi 23:5)..”. Hivyo
Pasaka ni tarehe 15 ya mwezi wa Kwanza.
Lakini Biblia pia inautaja mwezi wa kwanza
kwa jina la Nisan (Esta 3:7, Nehemia 2:1).
Yesu alisulubiwa mwaka ambao Ijumaa
iliitangulia sikukuu ya Pasaka kwa siku moja
(Yohana 18: 28, Marko 15:42-43). Hivyo
tarehe ya Yesu kusulubiwa ni Ijumaa, Nisan
14. Siku moja kabla ya Nisan 15. Siku moja
kabla ya Mwezi-Mkubwa.
Baada ya Yesu, Wakristo wengi Pasaka
waliiadhimisha Jumapili, lakini utata
ulijitokeza kuhusu tarehe ya kuiweka hiyo
Jumapili ya Pasaka. Ilifika wakati jimbo moja
la Wakristo linaadhimisha siku tofauti na
jingine na kwa njia wanayoijua wao.
Utata huu uliondolewa kule Nicaea mwaka
325 ambapo Kanisa Katoliki lilipoamua kuwa,
tarehe ya Pasaka iwe moja tu duniani kote,
yaani iwe ni Jumapili inayokuja baada ya
Mwezi-Mkubwa (Full Moon) unaotokea baada
ya siku ya Ikweta, yaani baada ya Machi 21
(Equinox).
Baada ya uamuzi huu, wataalamu walipania
kuunda chati maalum zenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa zitazokasaidia kuitambua tarehe ya
Pasaka kwa mwaka wowote.
Mwezi huizunguka dunia kwa siku
29.5305891203704 (Synodic Month), wakati
dunia hulizunguka jua kwa siku
365.24218967 (Tropical year).
Mizunguko hii miwili ikianza safari siku moja,
itapishana kila mwaka, lakini itakutana tena
mwezi unapokamilisha mizunguko 235. Dunia
nayo inakuwa imekamilisha mizunguko 19,
yaani miaka 19.
Wataalamu wakaitumia hii miaka 19
kutengeneza chati yenye tarehe za Mwezi-
Mkubwa unaotokea March 22 hadi April 18.
Tarehe zile zikaitwa tarehe za Mwezi-
Mkubwa Wa Pasaka au Ecclesiastical Full
Moon (EFM).
Ndani ya ile miaka 19, kila mwaka ukapewa
tarakimu iitwayo Golden Number
inayosimama badala ya mwaka ikiwa na
tarehe zile ziliorekodiwa za Mwezi Mkubwa
wa Pasaka. Chati yenyewe ya Golden
Number na tarehe zake (siku/Mwezi) ni hii
ifuatayo: {1=5/4, 2=25/3, 3=13/4, 4=2/4,
5=22/3, 6=10/4, 7=30/3, 8=18/4, 9=7/4,
10=27/3, 11=15/4, 12=4/4, 13=24/3, 14=12/4,
15=1/4, 16=21/3, 17=9/4, 18=29/3, 19=17/4}
Golden Number ya mwaka inapatikana
kuanza kuugawa mwaka kwa 19.
Tulifundishwa mashuleni kuwa namba
inayosalia baada ya kugawa huitwa “Baki” .
Hii “Baki” ukiijumlisha na 1 unapata Golden
Number (GN).
Mfano unatafuta GN ya 27. Hatua ya kwanza
ni kutafuta “Baki” baada ya kugawa 27 kwa
19. Hizi ni hesabu za “modulo” , yaani
zinahitaji tu namba inayobaki baada ya
kugawa.
Ikiandikwa hivi: (27 mod 19) inatakiwa
namba inayobaki baada ya kuigawa 27 kwa
19. Jibu ni 8. Hivyo tulipaswa tuandike hivi:
(27 mod 19=8). “Baki” 8 tuliyoipata, ndiyo
tunaihitaji ili tuijumlishe na 1 ili tupate GN
ambayo hapa ni 9 kwani (8+1=9).
Tungeweza pia kuandika hivi : 27 mod 19 +
1=9. Hivyo kanuni ya kupata GN kwa mwaka
wowote ni hii:
(MWAKA mod 19 + 1). Yaani, ugawe huo
mwaka kwa 19, kisha namba itakayobaki
ijumlishe na moja.
Ukishaipata GN, itafute kwenye ile chati
ambapo utaiona ikiwa na mwezi na tarehe.
Jumapili inayofuata baada ya tarehe hii ndiyo
tarehe ya Pasaka ya mwaka huo.
Tutumie chati ile na kanuni hii kujua tarehe
ya Pasaka ya mwaka 1474. GN ni (1474 mod
19 + 1=12). Hivyo GN ni 12.
Kwenye chati, 12 inaonyesha ni tarehe 4/4.
Hivyo, mwaka 1474 Mwezi-Mkubwa wa
Pasaka ulikuwa tarehe 4/4/1474. Hiyo ilikuwa
ni Jumatatu. Hivyo Pasaka ilikuwa ni
Jumapili iliyofuata yaani tarehe 10/4/1474.
Lakini, Kanisa Katoliki liliikubali kanuni hii
karne ya sita. Hii ndiyo sababu, tarehe za
Pasaka zinazojulikana ni zile tu zinazoanza
mwaka 533.
Ndivyo Pasaka ilivyotafutwa miaka ile. Sasa
tuone Pasaka ya kizazi chetu. Kizazi cha
“Gregorean Calender” iliyoanza mwaka 1582.
Tumelijadili lile pengo la siku lililofikia ambalo
mwaka 1582 lilishafika siku 10. Ukweli ni
kwamba kabla halijazibwa, Pasaka ilikuwa
inawadia lakini uhalisi ni kwamba inakuwa
tayari imepitwa siku 10. Kinyume kabisa na
maamuzi ya Kanisa kule Nicaea!
Ili kulizuia lisitokee tena, tumeona uchomoaji
wa siku moja toka kwenye miaka inayofunga
karne, isiyogawanyika kwa 400. Uchomoaji
huu umewekwa kwenye kanuni (formula)
iitwayo “Solar Equation”.
Kama mwendo wa kuzunguka jua
umezingatiwa na “Gregorean Calender”, vipi
kuhusu mwendo wa mwezi?
Tumeuona kwamba mizunguko ya mwezi na
dunia hukutana kila baada ya miaka 19.
Kadirio la dunia kuzunguka kwa siku 365.25

linafanya ikizunguka kwa miaka 19 zinakuwa
siku 6,939.75. Mwezi utakuwa nao
umezunguka mara 235, huku kila mzunguko
ukitumia siku 29.5305891203704.
Hivyo, kukutana kule ndani ya kila miaka 19,
huleta pengo dogo la saa 1, dakika 28,
sekunde 38.5.
Mapengo madogo haya tunayoyapuuza
mwanzoni, yameshatugharimu vya kutosha.
Pengo hili kwa mwaka ni dogo lakini kwa
miaka 2500 linakuwa hadi kufika siku nane.
Kwenye hesabu za kutafuta Pasaka
urekebishaji wa hili pengo hutokea kwenye
kanuni iitwayo “Lunar Equation”. Lakini kwa
sababu ya tofauti ya uelekeo wa mzunguko
wa mwezi na dunia, “Lunar Equation”
hujumlisha mara nane kila baada ya miaka
2500.
Hivyo, mahesabu yoyote ya kuitafuta tarehe
ya Pasaka hayakosi kanuni hizi mbili “Solar
Equation” na “Lunar Equation” .
Tumeona kwamba kalenda ilianza mwaka
1582. “Solar Equation” inaondoa siku moja
toka kwenye miaka 1700, 1800, 1900. Hivyo,
ni kujidanganya kusema kwamba miaka yote
inayogawanyika kwa nne ni mirefu, jambo
ambalo hata mimi nilifundishwa shuleni.
Hapa tumeona kwamba “Solar Equation”
imeondoa siku moja kwenye mwaka 1900 na
hivyo haukuwa mwaka mrefu ingawa
unagawanyika kwa nne.
“Lunar Equation” huongeza siku moja kwenye
miaka 1800, 2100, 2400. Mwaka 1800
unaguswa na vyote “Solar Equation” na
“Lunar Equation”. Hivyo hauathiriki.
Kanuni zote za kuitafuta Pasaka huzingatia
zaidi ya niliyoyaeleza, lakini cha muhimu
zaidi ni hizi mbili yaani “Solar Equation” na
“Lunar Equation” ambazo sijawahi kuzisikia
kwa kiswahili.
Ni vigumu kuepuka hesabu za “modulo” au
“mod” unapotafuta tarehe ya Pasaka. Lakini
ukiwauliza wanafunzi wa darasa la nne
kwamba machungwa 2011 yakipangwa
kwenye mafungu 19, ni mangapi yatakosa
fungu?

Wapo watakaopata jibu sahihi kwamba ni
machungwa 16. Kimahesabu swali hilo
linaandikwa hivi: (2011 mod 19) na jibu lake
ni 16, yaani (2011 mod 19=16).
Ifuatayo ni moja ya kanuni zinazotumika
kuipata tarehe za Pasaka ya mwaka wowote
kuanzia 1700 hadi 2099:
(1) : a=MWAKA mod 19;
(2) : b=MWAKA \ 100;
(3) : c=MWAKA mod 100;
(4) : d=b \ 4;
(5) : e=b mod 4;
(6) : f=c \ 4;
(7) : g=c mod 4;
(8) : h=(b + 8)\25;
(9) : i=(b – h + 1)\3;
(10) : j=(19xa + b – d – i + 15) mod 30;
(11) : k=(32 + 2xe + 2xf – j – g) mod 7;
(12) : m=(a + 11xj + 22xk) \ 451;
(13) : n=j + k – 7xm + 114;
(14) : Tarehe=(n mod 31) + 1
(15) : Mwezi =n\31;
Penye neno MWAKA, andika mwaka
unaotafuta kujua tarehe yake ya Pasaka.
Panapotokea alama (\) ni kugawanya
ambako hata kama jibu litaleta desimali, basi
hiyo desimali unatakiwa kuachana nayo ili
jibu libaki namba nzima. Penye alama (x)
hiyo ni ya kuzidisha.
Yafuatayo ni majibu niliyopata kwa hatua
zote baada ya kuuingiza mwaka 2015 ili
kujua siku ya Pasaka ya mwaka huu: (1): 1,
(2): 20, (3): 15, (4): 5, (5): 0, (6): 3, (7): 3,
(8): 1, (9): 6, (10): 13, (11): 1, (12): 0, (13):
128, (14): 5, (15): 4.
Tarehe imepatikana kwenye hatua ya 14
ambako jibu ni “5”. Mwezi umepatikana
kwenye hatua ya 15 ambako jibu ni “4”. Hivyo
Pasaka ya mwaka (2015) huu ni Tarehe 5,
mwezi wa 4.
Hivyo, kwa njia hii, unaweza kujua tarehe za
Pasaka kwa miaka ijayo kama unavyoijua
tarehe ya Krismas. Kama kuna tukio
lilifanyika siku ya Pasaka miaka iliyopita na
hukumbuki tarehe, basi tumia kanuni hii.
Zifuatazo ni siku zinazoitangulia Pasaka kwa
idadi ya siku zilizoandikwa kwenye mabano:
Jumatano Ya Majivu (46), Jumapili ya
Matawi (7), Ijumaa Kuu (2).
Zinazotanguliwa na Pasaka ni hizi zifuatazo:
Kupaa (42), Pentekoste (49), Utatu Mtakatifu
(56), Ekaristi (63).
Mwanzo tuliona kwamba Mwezi-Mkubwa wa

Pasaka au “Ecclesiastical full Moon” ni ule wa
March 22 hadi April 18. Ukitokea March 22
basi kuna uwezekano siku hiyohiyo ikawa
Pasaka na ikawa imevunja rekodi ya kuwahi
mapema.
Ukitokea April 18, kuna uwezekano wa
Pasaka kuwa siku saba zaidi ya hapa yaani
April 25, na hiyo ikawa ni tarehe ya juu mno
ya Pasaka. Hivyo, Pasaka yoyote haiwezi
kuwa chini ya Machi 22, wala haiwezi
kuwazaidi ya April 25.
Pasaka tuliyoiona mwaka 2008 ndiyo ya
mwisho kwa kizazi chetu kuiona ikiwahi
mapema kiasi kile, kwani ilitokea Machi 23 na
itairudia tena tarehe hiyo mwaka 2160!

by JOSEPH MAGATA

Mafundisho makubwa ya Yesu Kristo

Heri

Basi Yesu alipoona makutano, alipanda
mlimani akaketi chini, nao wanafunzi
wake wakamjia. 2Ndipo akaanza kuwafundisha,
akisema:
3 “Wana heri walio masikini wa roho,
maana hao Ufalme wa Mbinguni ni wao.
4Wana heri wale wanaohuzunika,
maana hao watafarijiwa.
5Wana heri walio wapole,
maana hao watairithi nchi.
6Wana heri wenye njaa na kiu ya haki,
maana hao watatoshelezwa.
7Wana heri wenye huruma,
maana hao watapata rehema.
8Wana heri walio na moyo safi,
maana hao watamwona Mungu.
9Wana heri walio wapatanishi,
maana hao wataitwa wana wa Mungu.
10Wana heri wanaoteswa kwa sababu ya haki,
maana hao Ufalme wa Mbinguni ni wao.
11Mna heri ninyi watu watakapowashutumu
na kuwatesa na kunena dhidi yenu mabaya ya
aina zote kwa uongo kwa ajili yangu. 12Furahini
na kushangilia kwa maana thawabu yenu ni
kuu.

Chumvi na Nuru

13‘‘Ninyi ni chumvi ya ulimwengu. Lakini
chumvi ikipoteza ladha yake, yawezaje
kurudishiwa ladha yake tena ? Haifai tena kwa
kitu cho chote, ila kutupwa nje ikanyagwe na
watu.
14‘‘Ninyi ni nuru ya ulimwengu. Mji
uliojengwa kilimani hauwezi kufichika. 15Wala
watu hawawashi taa na kuifunika kwa bakuli.
Badala yake, huiweka kwenye kinara chake,
nayo hutoa mwanga kwa kila mtu aliyemo ndani
ya ile nyumba. 16Vivyo hivyo, nuru yenu iangaze
mbele ya watu, ili wapate kuona matendo yenu
mema wamtukuze Baba yenu aliye mbinguni.

Kutimiza Sheria

17“Msidhani kwamba nimekuja kuondoa
Torati au Manabii, sikuja kuondoa bali kutimiza.
18Kwa maana,amin, nawaambia, mpaka mbingu
na dunia zitakapopita, hakuna hata herufi moja
ndogo wala nukta itakayopotea kwa namna yo
yote kutoka kwenye Torati mpaka kila kitu kiwe
kimetimia. 19Kwa hiyo, ye yote atakayevunja
mojawapo ya amri ndogo kuliko zote ya amri
hizi, naye akawafundisha wengine kufanya
hivyo, ataitwa mdogo kabisa katika Ufalme wa
Mbinguni, lakini ye yote azitendaye na
kuzifundisha hizi amri ataitwa mkuu katika
Ufalme ya Mbinguni. 20Kwa maana nawaambia,
haki yenu isipozidi haki ya waandishi wa sheria
na Mafarisayo, kamwe hamtaingia katika
Ufalme wa Mbinguni.

Mafundisho ya Yesu Kuhusu Hasira

21“Mmesikia walivyoambiwa watu wa
zamani kwamba, ‘Usiue, ye yote atakayeua
atapasiwa hukumu.’ 22Lakini mimi nawaambia
kwamba, ye yote atakayemkasirikia ndugu yake
wa kiume au wa kike, atapasiwa hukumu. Tena,
ye yote atakayemwambia ndugu yake wa kiume
au wa kike, ‘Raca’a, yaani kumdharau na
kumdhihaki, atapasiwa kufanyiwa baraza. Lakini
ye yote atakayesema ‘We mpumbavu ulaaniwe!’
Atapasiwa hukumu ya moto wa jehanam.
23“Kwa hiyo, kama unatoa sadaka yako
madhabahuni, ukakumbuka kuwa ndugu yako
ana kitu dhidi yako, 24iache sadaka yako hapo
hapo, mbele ya madhabahu, uende kwanza
ukapatane na ndugu yako wa kiume au wa kike,
kisha urudi na ukatoe sadaka yako.
25“Patana na mshtaki wako upesi wakati
uwapo njiani pamoja naye kwenda
mahakamani, ili mshtaki wako asije akakutia
mikononi mwa hakimu, naye hakimu akakutia
mikononi mwa walinzi, nawe ukatupwa
gerezani. 26Amin, nakuambia, hutatoka humo
mpaka umelipa hadi senti ya mwisho”

Mafundisho ya Yesu Kuhusu Uzinzi

27“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Usizini’.
28Lakini mimi nawaambia: kwamba ye yote
amtazamaye mwanamke kwa kumtamani,
amekwisha kuzini naye moyoni mwake. 29Jicho
lako la kuume likikufanya utende dhambi, ling’oe
ulitupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza
kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako
mzima utupwe jehanam. 30Kama mkono wako
wa kuume ukikufanya utende dhambi, ukate
uutupe mbali. Ni afadhali kwako kupoteza
kiungo kimoja cha mwili wako kuliko mwili wako
mzima utupwe jehanam.

Mafundisho ya Yesu Kuhusu Talaka

31‘‘Pia ilinenwa kwamba, ‘Mtu ye yote
amwachaye mkewe na ampe hati ya talaka.’
32Lakini mimi nawaambia, ye yote amwachaye
mkewe isipokuwa kwa kosa la uasherati,
amfanya mkewe kuwa mzinzi. Na ye yote
amwoaye yule mwanamke aliyeachwa azini.’’

Mafundisho ya Yesu Kuhusu Kuapa

33“Tena mmesikia walivyoambiwa watu wa
zamani kwamba, ‘Usiape kwa uongo, bali
timizeni, nadhiri zile ulizofanya kwa Bwana’
34Lakini mimi nawaambia,’’Msiape kabisa, ama
kwa mbingu, kwa kuwa ni kiti cha enzi cha
Mungu, 35au kwa nchi, kwa kuwa ndipo mahali
pake pa kuwekea miguu, au kwa Yerusalemu,
kwa kuwa ndio mji wa Mfalme Mkuu. 36Nanyi
msiape kwa vichwa vyenu kwa kuwa hamwezi
kuufanya hata unywele mmoja kuwa mweupe
au mweusi. 37‘Ndiyo,’ yenu iwe ‘Ndiyo’ na
‘Hapana’, yenu iwe ‘Hapana.’ Lo lote zaidi ya hili
latoka kwa yule mwovu.’’

Mafundisho ya Yesu Kuhusu Kulipiza Kisasi

38“Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Jicho kwa
jicho na jino kwa jino.’ 39Lakini mimi nawaambia,
msishindane na mtu mwovu. Lakini kama mtu
akikupiga kwenye shavu la kuume, mgeuzie na
la pili pia, 40Kama mtu akitaka kukushtaki na
kuchukua shati lako, mwachie achukue na koti
pia. 41Kama mtu akikulazimisha kwenda
kilometa moja, nenda naye kilometa mbili.
42Mpe yeye akuombaye, wala usimgeuzie
kisogo yeye atakaye kukukopa.’’

Mafundisho ya Yesu kuhusu Upendo Kwa Adui

43‘‘Mmesikia kwamba ilinenwa, ‘Mpende
jirani yako na umchukie adui yako.’ 44Lakini
mimi ninawaambia : Wapendeni adui zenu na
waombeeni wanaowatesa ninyi, 45ili mpate
kuwa watoto wa Baba yenu aliye mbinguni. Kwa
maana Yeye huwaangazia jua lake watu waovu
na watu wema, naye huwanyeshea mvua
wenye haki na wasio haki. 46Kama mkiwapenda
wale wanaowapenda tu, mtapata thawabu gani?
Je, hata watoza ushuru hawafanyi hivyo?
47Nanyi kama mkiwasalimu ndugu zenu tu, je,
mnafanya nini zaidi ya wengine? Je, hata watu
wasiomjua Mungu, hawafanyi hivyo? 48Kwa hiyo
iweni wakamilifu kama Baba yenu wa mbinguni
alivyo mkamilifu.’’

Mafundisho ya Yesu kuhusu Kuwapa Wahitaji

‘‘Angalieni msitende wema wenu mbele ya
watu ili wawaone. Kwa maana mkifanya
hivyo, hamna thawabu kutoka kwa Baba yenu
aliye mbinguni.
2‘‘Hivyo mnapowapa wahitaji, msipige
panda mbele yenu kama wafanyavyo wanafiki
katika masinagogi na mitaani, ili wasifiwe na
watu. Amin, amin nawaambia wao wamekwisha
kupokea thawabu yao. 3Lakini ninyi mtoapo
sadaka, fanyeni kwa siri, hata mkono wako wa
kushoto usijue mkono wako wa kuume
unachofanya, 4ili sadaka yako iwe ni siri. Ndipo
Baba yako wa mbinguni, Yeye aonaye sirini
atakupa thawabu kwa wazi.

Mafundisho ya Yesu Kuhusu kusali

5“Nanyi msalipo, msiwe kama wanafiki,
maana wao hupenda kusali wakiwa
wamesimama katika masinagogi na kando ya
barabara ili waonekane na watu. Amin, amin
nawaambieni, wao wamekwisha kupata
thawabu yao. 6Lakini wewe unaposali, ingia
chumbani mwako, funga mlango na umwombe
Baba yako aliye sirini. Naye Baba yako aonaye
sirini atakupa thawabu yako. 7“Nanyi mnaposali
msiseme maneno kama wafanyavyo watu
wasiomjua Mungu. Kwa maana wao hudhani
kwamba watasikiwa kwa sababu ya wingi wa
maneno yao. 8Msiwe kama wao, kwa sababu
Baba yenu anajua kile mnachohitaji kabla
hamjamwomba.’’
9‘‘Hivi basi, ndivyo iwapasavyo kuomba :
“Baba yetu uliye mbinguni,
Jina lako litukuzwe.
10Ufalme wako uje.
Mapenzi yako yafanyike hapa duniani
kama huko mbinguni.
11Utupatie leo riziki zetu za kila siku.
12Utusamehe deni zetu,
kama sisi nasi tulivyokwisha
kuwasamehe wadeni wetu.
13 Usitutie majaribuni,
bali utuokoe kutoka kwa yule mwovu,
kwa kuwa Ufalme ni Wako na nguvu
na utukufu hata milele. Amen.”
14Kwa kuwa kama mkiwasamehe watu wengine
wanapowakosea, Baba yenu wa mbinguni
atawasamehe pia na ninyi. 15Lakini
msipowasamehe watu wengine makosa yao,
wala Baba yenu hatawasamehe ninyi makosa
yenu.

Mafundisho ya Yesu Kuhusu Kufunga

16“Mnapofunga, msiwe wenye huzuni kama
wafanyavyo wanafiki. Maana wao hukunja
nyuso zao ili kuwaonyesha wengine kwamba
wamefunga. Amin, amin nawaambia wao
wamekwisha kupata thawabu yao kamilifu.
17Lakini mnapofunga, jipakeni mafuta kichwani
na kunawa nyuso zenu 18ili kufunga kwenu
kusionekane na watu wengine ila Baba yenu
aliye sirini, naye Baba yenu aonaye sirini
atawapa thawabu yenu kwa wazi.”

Akiba Ya Mbinguni

19“Msijiwekee hazina duniani, mahali
ambapo nondo na kutu huharibu, nao wevi
huvunja na kuiba. 20Lakini jiwekeeni hazina
mbinguni, mahali ambapo nondo na kutu
haviharibu, wala wevi hawavunji na kuiba.
21Kwa sababu mahali akiba yako ilipo, hapo
ndipo pia moyo wako utakapokuwa.’’

Jicho Ni Taa Ya Mwili

22‘‘Jicho ni taa ya mwili. Kama jicho lako ni
nyofu, mwili wako wote utakuwa na nuru.
23Lakini kama jicho lako ni ovu, mwili wako wote
utajawa na giza. Kwa hiyo basi, kama nuru
iliyomo ndani yako ikiwa giza, hilo ni giza kuu
namna gani ! ”

Mungu Na Mali

24‘‘Hakuna mtu ye yote awezaye
kuwatumikia mabwana wawili, kwa kuwa ama
atamchukia huyu na kumpenda yule mwingine,
au atashikamana sana na huyu na kumdharau
huyu mwingine. Ninyi hamwezi kumtumikia
Mungu na malia.’’

Msiwe Na Wasiwasi

25‘‘Kwa hiyo nawaambia, msiwe na
wasiwasi kuhusu maisha yenu: mtakula nini au
mtakunywa nini, au kuhusu miili yenu, mtavaa
nini. Je, maisha si zaidi ya chakula na mwili
zaidi ya mavazi? 26Waangalieni ndege wa
angani, wao hawapandi wala hawavuni au
kuweka ghalani, lakini Baba yenu wa mbinguni
huwalisha hao. Je, ninyi si wa thamani zaidi
kuliko hao ndege? 27Ni nani miongoni mwenu
ambaye kwa kujitaabisha kwake aweza
kujiongezea hata saa moja zaidi katika maisha
yake au kuongeza dhiraa mojab kwenye kimo
chake ?
28‘‘Nanyi kwa nini kujitaabisha kwa ajili ya
mavazi? Fikirini maua ya shambani yameavyo.
Hayafanyi kazi wala hayafumi. 29Lakini
nawaambia, hata mfalme Solomoni katika fahari
yake yote hakuvikwa kama mojawapo ya hayo
maua. 30Lakini ikiwa Mungu anayavika hivi
majani ya shambani, ambayo leo yapo na kesho
yanatupwa motoni, je, hatawavika ninyi vizuri
zaidi, enyi wa imani haba? 31Kwa hiyo msiwe na
wasiwasi, mkisema, ‘Tutakula nini?’ Au
‘Tutakunywa nini?’ Au ‘Tutavaa nini?’ 32Kwa
maana watu wasiomjua Mungu ndio
wanaoshindania hayo, lakini Baba yenu wa
mbinguni anafahamu kwamba mnahitaji hayo
yote. 33Lakini utafuteni kwanza Ufalme wa
Mungu na haki yake na haya yote
mtaongezewa. 34Kwa hiyo msiwe na wasi wasi
kuhusu kesho, kwa sababu kesho itajitaabikia
yenyewe. Yatosha kwa siku masumbufu yake.’’

Mafundisho ya Yesu kuhusu Kuwahukumu Wengine

“Usihukumu ili usije ukahukumiwa. 2Kwa
maana kwa jinsi ile unavyowahukumu
wengine, ndivyo utakavyohukumiwa na kwa
kipimo kile utakachotoa ndicho utakachopokea.
3‘‘Kwa nini unatazama kibanzi kidogo
kilichomo kwenye jicho la ndugu yako na wala
huoni boriti iliyoko kwenye jicho lako? 4Au
unawezaje kumwambia ndugu yako, ‘Acha nitoe
kibanzi kwenye jicho lako wakati kuna boriti
kwenye jicho lako mwenyewe ?’ 5Ewe mnafiki,
toa kwanza boriti kwenye jicho lako mwenyewe,
nawe ndipo utakapoona wazi ili kuondoa kibanzi
kilichoko kwenye jicho la ndugu yako.
6‘‘Msiwape mbwa vitu vilivyo vitakatifu, wala
msitupie nguruwe lulu zenu. Kama mkifanya
hivyo, watazikanyaga kanyaga na kisha
watawageukia na kuwararua vipande vipande. ”

Omba, Tafuta, Bisha

7“Ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi
mtapata, bisheni nanyi mtafunguliwa mlango.
8Kwa maana kila aombaye hupewa, naye
atafutaye huona, naye abishaye hufunguliwa
mlango.
9‘‘Au ni nani miongoni mwenu ambaye
mwanawe akimwomba mkate atampa jiwe?
10Au mwanawe akimwomba samaki atampa
nyoka? 11Ikiwa ninyi basi mlio waovu mnajua
jinsi ya kuwapa watoto wenu vitu vizuri, si zaidi
sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa vitu
vizuri wale wamwombao ? 12Kwa hiyo cho chote
ambacho mngetaka mtendewe na watu, ninyi
nanyi watendeeni vivyo hivyo. Kwa kuwa hii
ndiyo Torati na Manabii.’’

Njia Nyembamba Na Njia Pana

13‘‘Ingieni kwa kupitia mlango mwembamba,
kwa maana lango ni pana na njia ni pana
ielekeayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa
kupitia lango hilo. 14Lakini mlango ni
mwembamba na njia ni finyo ielekayo kwenye
uzima, nao ni wachache tu waionao.’’

Mti na Tunda lake

15“Jihadharini na manabii wa uongo,
wanaowajia wakiwa wamevaa mavazi ya
kondoo, lakini ndani wao ni mbwa mwitu
wakali.16Mtawatambua kwa matunda yao. Je,
watu huchuma zabibu kwenye miiba au tini
kwenye michongoma? 17Vivyo hivyo, mti
mwema huzaa matunda mazuri na mti mbaya
huzaa matunda mabaya. 18Mti mwema hauwezi
kuzaa matunda mabaya wala mti mbaya
hauwezi kuzaa matunda mazuri. 19Kila mti
usiozaa matunda mazuri hukatwa na kutupwa
motoni. 20Hivyo, kwa matunda yao,
mtawatambua.’

Mwanafunzi Wa Kweli

21“Si kila mtu aniambiaye, ‘Bwana, Bwana,’
atakayeingia katika Ufalme wa Mbinguni bali ni
yeye afanyaye mapenzi ya Baba yangu aliye
mbinguni. 22Wengi wataniambia siku ile,
‘Bwana, Bwana, hatukutoa unabii kwa jina lako
na kwa jina lako kutoa pepo na kufanya miujiza
mingi? 23Ndipo nitakapowaambia wazi,
`’Sikuwajua kamwe. Ondokeni kwangu, ninyi
watenda maovu!’

Msikiaji Na Mtendaji

24‘‘Kwa hiyo kila mtu ayasikiaye haya
maneno yangu na kuyatenda, ni kama mtu
mwenye busara aliyejenga nyumba yake
kwenye mwamba. 25Mvua ikanyesha, mafuriko
yakaja na upepo ukavuma ukaipiga hiyo
nyumba, lakini haikuanguka kwa sababu msingi
wake ulikuwa kwenye mwamba. 26Naye kila
anayesikia haya maneno yangu wala
asiyatende, ni kama mtu mjinga aliyejenga
nyumba yake kwenye mchanga. 27Mvua
ikanyesha, mafuriko yakaja, nao upepo
ukavuma ukaipiga hiyo nyumba, nayo
ikaanguka kwa kishindo kikubwa.’’
28Yesu alipomaliza kusema maneno haya,
makutano ya watu wakashangazwa sana na
mafundisho yake, 29kwa sababu alifundisha
kama yeye aliye na mamlaka, wala si kama
walimu wao wa sheria.
Shopping Cart
🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About