Mungu alimpenda sana binadamu hata akauvaa Mwili wa Binadamu akashuka duniani na kuishi kama Binadamu ili amkomboe Mwanadamu na hata akaamua kufa kwa ajili ya Binadamu kwa malipizi ya dhambi za Binadamu na kwa maondoleo ya dhambi.
Tag: Tafakari za Ukuu wa Mungu
Kwa nini Mungu hatendi mpaka umwambie au umuombe? Kwa nini tusali?
Mungu anapenda kutenda jambo baada ya mtu kumuomba/kusali ili mtu aelewe Ukuu wa Mungu na ili Mungu atukuzwe.
Kama kila kitu mtu anachotaka kingekua kinafanyika, Binadamu asingemkumbuka Mungu na Mungu asingetukuzwa
Upendo, Huruma, Rehema na Neema za Mungu
Kadiri Mtu anavyoanguka dhambini na kutubu kweli makosa yake ndivyo na upendo, Huruma, Rehema na Neema za MUNGU zinavyoongezeka katika maisha yake.
Mawazo na Mipango ya Mungu kwa mtu
Mungu daima anawaza Mema na Anampangia Mtu Mambo mema.
Kama mtu ataenda katika njia ambayo Ipo katika mipango na mapenzi ya Mungu basi atapokea yale mema Mungu aliyopanga Kwake.
Lakini kama mtu ataishi kwa kufuata mapenzi yake mwenyewe basi atapoteza yale mema Aliyopangiwa.