Ujumbe mzuri kwa mpenzi wako kumuonyesha upendo
yapitayo mdomoni yametokea moyoni ,uyaonayo hadharani
nimeagizwa na manani yakuridhishayo nafsini ni utamu wa
yakini.
yapitayo mdomoni yametokea moyoni ,uyaonayo hadharani
nimeagizwa na manani yakuridhishayo nafsini ni utamu wa
yakini.
Unaonekana kung’ara leo nilijuaje…….ni kwasababu
unaonekana hivyo kila siku. Nakupenda sana Mpenzi wangu vile ulivyo kila siku kwangu wewe ni mpya.
Mvua na jua haviwezi kuwa pamoja, usiku na mchana
hazigongani, lakini mimi na wewe, hata wasemaje,
‘tunafiti’ kuwa pamoja.
Naweza kukuazima mabega yangu upande, masikio yangu usikilizie mikono yangu ushikie, miguu yangu, utembelee, lakini si moyo wangu kwani tayari unao wewe.
macho huona na moyo hurdhia,ila co kila kitu jicho lionalo moyo hurdhia.lakn pind moyo urdhiapo upendo moyon huingia.moyo huwa kpofu japo wng wa hisia.upendo ndan ya moyo haupimwi kwa mizani kwa unayemzimikia. moyo wangu umepata hisia Kwa flan licha bdo cjamjua.
Ewe mwanga angaza mboni ya penzi letu
Ndilo sababu ya nguvu yangu
Tangulia pembeni mwa macho yake
Asubuhi hii hadi usiku ujao
Bongo zenye fikra kali huwa na mawazo, suluhu na sababu;
ubongo wa kisayansi huwa na kanuni, nadharia na takwimu;
wangu una wewe tu!
Sio Maua yote Huonesha Upendo, “Ni Waridi pekee” sio Miti yote Hustawi Jangwani “ni Mtende pekee” sio watu wote wanaokukumbuka muda huu ni mm pekee. Uhali gani?
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Furaha ni kawaida yangu, kununa si busara kwangu, kuishi nawewe vizuri ni sehemu ya Maisha yangu, kukusalimia ni hulka ya Moyo wangu, Uhali gani mpenzi?
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Ukipata tutakula na wala usijali mpenzi wangu.
Ukikosa tutalala na hiyo itabaki siri yanguuuuuuuu.nakupenda mpz
mapenzi ni safari=unifanye nauli ya moyo, mapenzi ni
maradhi=unifanye daktari ni kutibu maradhi yako,mapenzi ni
kiu=niwe maji jangwani,mapenzi ni chakula=nikulishe
maishani mwako na uwe asali moyoni mwangu
Salamu yako ni nusu ya uhai wangu, kuikosa nisawa na kuidhulumu nafsi yangu, kuipata nisawa na ua ridi machoni mwangu, nakila ninapoipata huwa najisikia faraja moyoni mwangu, Nakupenda sana Muhibu wangu.
Siku zote kwangu ni sherehe ni wewe unishereheshaye,ukweli
usio na kejeli mapenzi yako yanatii kiu yangu,moyoni
mwangu nimeridhia… .nakupenda daima mpenzi!
mapenzi ni safari,mapenzi ni ahadi,mapenzi ni
ujasiri,mapenzi ni zawadi,mapenzi mitihani,mapenzi
ramani,mapenzi ajali na ndiyo maana nakupenda wewe bila kujali.
Usiku wa leo uwe ni wenye faraja kwako, utawaliwe na usingizi wa mahaba kwenye kope zako, naomba ujenge taswira yangu katika mawazo yako, Usisahau kuniota sweet wangu. USIKU MWEMA
natamani usaini moyoni mwang,ikiwezekana pia upige muhuri moyoni mwangu wajue nan mmiliki wa huo moyo wenye shibe upendo kwaajili yako mpenzi
Moyo wangu unajua kupenda katu haujui kutenda
mpz, nakupenda tukwepe fitina mpz.
Wanafiki tusiwaombee kifo daima na milele washuhudie penzi
letu linavyozidi kukua,na tunavyopambana na mapito.
Nakupenda sana mwandani wangu ndiyo maana moyo wangu
hupatwa kidonda ninaokuona na mwingine hasa anapokuwa hana
sifa, nahisi kama anakutumia wewe kama mdori wake wa
kumfurahisha. Uwe makini ua la moyo wangu.
mapenzi ni utoto,deka ulie nitakubembeleza,mapenz ni
zawadi,tabasamu,nibusu niambie kiasi gani
unanipenda,naweza kusema asilimia kubwa jina lako
limezunguka ukuta wa moyo wangu,na kamwe jina lako
haliwezi futika.
NAKUPENDA
Recent Comments