SMS, Vichekesho, Mahusiano, Biashara na Ujasiriamali, Afya, Chemsha Bongo, Dini pamoja na Vitabu kwenye PDF

Karibu AckySHINE

🤣😃😂

Chagua Unachotaka Kusoma Hapa

BURUDANI MAKALA DINI VITABU

Unahakikishiwa kusoma kitu kipya kizuri kila saa unapotembelea ukurasa huu.

Mambo ya msingi kufahamu kuhusu uotaji wa meno kwa mtoto

Mtoto wako atakapofikisha miezi sita, ataanza kuota meno. Watoto wengi wanapotaka kuota meno humwaga mate sana na hutaka kutafunatafuna vitu. Wakati mwingine watoto hutapika au kuhara wakiota meno.

Kwa kawaida kuota meno hakufanyi mtoto kupandwa na joto. Kama mtoto wako atapata joto, yaweza kuwa jambo lingine. Hakikisha umemwona daktari wa watoto.

Yafuatayo ni mambo ya msingi kujua kuhusu uotaji wa meno.

·Wakati wa kulala, weka kitambaa safi chini ya kichwa cha mwanao ambapo ute utamwagika. Unaweza kibadilisha kitambaa hichi kitakapo loweka ute.

·Mpatie mtoto kitu cha kutafuna ambacho hakitamdhuru. Usimpatie kitu kidogo sana kwani anaweza kukimeza. Unaweza kumpatia vidunde vya mpira visivyokuwa na majimaji ndani kwani vyaweza kupasuka.

·Usifungilie kidunde cha kutafuna kwa shingo ya mwanao. Kinaweza kushikwa na kummyonga.

·Kuna dawa nyingi dukani za kupiunguza maumivu wakati mwanao anaota meno. Hata hivyo, mwone daktari wa watoto kabla jujampa mwanao dawa yoyote

·Baada ya mwanao kuota meno hakikisha unayatunza vizuri

Huyu bwana leo kapatikana, Jamani nyodo nyingine mbaya

Baada ya kumaliza Degree yake ya sheria Bwana Rwegashora aliamua kurudi nyumbani Bukoba mjini na kufungua ofisi yake kwa ajili ya huduma kwa wateja.
Siku moja akiwa ndani ya ofisi yake alimuona mtanashati na mdada mmoja mrembo anakuja ofisini kwake akajua ni mteja anamletea kesi.

Ndipo akanyanyua mkoni wa wa simu ya TTCL na kuanza kuongea huku anajizunguusha kwenye kiti cha kuzunguuka.
Wakati mdada alipokaribia Rwegashora alimkaribisha kwa ishara maana alijifanya yupo busy na kuongea na simu ya umuhimu.
Wakati anaongea na simu akisikika akisema No, No, No….. Absolutely No. Wajuulishe hao lay person wa New York kua siwezi kushuhulika na kesi ambayo itanilipa chini ya 50 million. Mimi ni profesional lawyer and im crossing the border to sarve international community.

Aka pose kidogo na akanywa maji kisha akaendelea…..
Naweza kuanza kukusanya primary evidence next weak but tell them watume kwanza ten million kwa kuanza…
Hahahahaha you dont know my Account
Mr Roger. Ok waambie watume kwenye Account ileile walionitumia million 100 last month…

Aka pose tena akameza fundo la maji na kurekebisha tai yake kisha akaendelea… Ok usisahau kumueleza muendesha mashtaka mkuu wa marekani kua nitakuja New York mwezi ujao maana nitapita kwanza Amsterdam kuwasilisha utetezi wa yule mteja wangu mholanzi kisha nitaenda Tokyo kulipia ile gari yangu niloagiza.

Wakati anaongea hayo yote yule mdada alikua ametulia na anamuangalia Bwana Rwegashora anavyojizunguusha kwenye
kiti chake huku akiongea kwa tambo kwenye ile simu ya TTCL.
Baada ya kumaliza kuongea na simu Bwana Rwegashora aliweka mkono wa simu yake ya TTCL chini kisha akamgeukia mdada mrembo.

Samahan sana kwa kukupotezea muda wako unajua tena kazi zetu zinaumiza kichwa sana kama unavyoona mwenyewe yaani niko busy sana ninapokea simu sana mpaka nimechoka na simu nyingi ni za wateja wa njee ya nchi.

Anyway nikusaidie nn? Mdada akajibu mimi ni mfanyakazi wa kampuni ya TTCL nimekuja kuunganisha line yako ya simu kwani haipo hewani tangu wiki iliyopita…!!!

Unadhani Bwana Rwegashora alifanyaje…???

Mke alichomfanyia mme wake kabla ya kwenda safari, Chezea mawaifu walokole wewe!

JAMAA alimuaga mke wake mlokole kuwa anaenda semina ya siku tatu, kumbe anakwenda kwa bi mdogo.

Mke akamwambia mumewe; “Tupige magoti tusali”,

Wakapiga magoti…:
MKE: Eee baba msaidie mume wangu afike salama safari yake.
MUME: Emen…

MKE: Mpe nguvu katika yote atakayoyafanya huko.
MUME: Emen…

MKE: Akitaka kufanya uasherati ashindwe.
MUME: Kimya…

MKE: Akifanya uasherati apatwe na janga baya kwa uwezo wako bwana.
MUME: …….!!

MKE: Yaani akifanya uasherati afie hukohuko kwa mateso makali.
MUME: Maombi gani sasa hayo!!?. Haya basi siendi semina ufurahi wewe.

Chezea mawaifu walokole wewe!

Ugumu wa maisha huanzia akilini mwako

Ebu fikiria Dada anayechoma mahindi maeneo ya Manzese Darajani kuanzia saa 12 jioni mpaka SAA 2 usiku, kwa siku moja anauwezo wa kuchoma mahindi .50. Kila hindi moja ananunua shambani kwa shilingi 100/- Na Anauza kwa sh.600/-

Hiyo ina maana mahindi 50 ananunua kwa shilingi 5000/- akichoma na kuuza anapata sh.30,000/-. Akitoa pesa ya mtaji (5000/- ya mahindi na 1500/- ya mkaa) anabakiwa na sh.23,500/- kwa siku.

Hivyo kwa mwezi huyu mchoma mahindi atakuwa ameingiza kiasi cha sh.705,000/-

Mwalimu mwenye Degree anayeanza kazi analipwa 584,000/- akikatwa kodi pamoja na makato mengene ya mifuko ya jamii anabakiwa na sh.425,000/.

Tofauti ya Mwalimu wa degree na Muuza mahindi ni kuwa Mwalimu kaajiriwa, muuza mahindi kajiajiri. Mwalimu anafanya kazi masaa 9 kwa siku, muuza mahindi anafanya kazi masaa matatu kwa siku (saa 12 jioni hadi 2 usiku). Mwalimu anatumia muda wake wa ziada kusahihisha mitihani na homework, mchoma mahindi anatumia muda wake wa ziada kutafuta fursa nyingine za kupata hela.

Uoga wako ndio umaskini wako.
KAMA HUNA FURAHA NA UNACHOKIFANYA BADILI MTAZAMO NA SIKUSHAURI UKAUZE MAHINDI NO HUO NI MF. KAMA SWALA NI KIPATO TU BASI KUNA FURSA NYINGI SANA KIPINDI HIKI NA WAWEZA BILA HATA YA KUWA NA MTAJI CHA MSINGI NI WEWE KUAMUA KUWAONA WATAALAMU WAKUSHAURI NI NINI CHA KUFANYA.

mafanikio yanaanza nawewe

Usiruhusu tabia hii itawale akili yako

Tabia ya kijidharau na kujiona hufai ama huwezi kufanya lolote ukafanikiwa maishani, hakuna mwanadamu aliyeumbwa ili ashindwe,, sote tu washindi zaidi, tunatofautiana njia za kufikia huo ushindi.

Rafiki yawezekana umeshajidharau… na kujitamkia maneno kadha wa kadha ambayo kimsingi yamekukatisha tamaa kabisa ya kufikia lengo fulani maishani… na ukabaki kushuhudia mafanikio ya wengine kila siku maishani.

Embu ondoa dhana ya kushindwa na kujidharau katika kila hatua upitiayo maishani haijalishi umeshindwa mara ngapi, jifunze kuwa na moyo mgumu na wa subila kwa kila hatua upitiayo maishani,, haijalishi upo katika hali gani? Maishani.

Kama ni maskini sana, usijidharau na umaskini wako ukaona wewe ni wa hali hiyo hiyo maisha yako yote,, no.. hapana, haukuumbwa ili uje kuwa maskini. Ila ni juhudi zako mwenyewe ndizo zitakazokutoa katika umaskini ulionao, haijalishi wewe una ulemavu wa aina yeyote ukajidharau na kujiona huwezi fanya lolote mbele ya jamii likakubalika.

Rafiki kuna walemavu kama wewe, wamejitambua na wameamua… hakika wamefikia mafanikio makubwa maishani. Ondoa dharau katika nafsi yako amini unaweza. Kuna walioshindwa kama wewe wakadharauliwa na kutemewa mpaka mate… ila walitambua kusudi la maisha yao na leo hii wamefikia mafanikio makubwa sana maishani, kwa nini?? Wewe ukate tamaa na kujidharau katika hali uliyopo ukajiona hauna maana? Hakika unaweza ukiamua,

Madhara ya Kuvaa viatu virefu

NI wazi kuwa viatu virefu huvutia sana vinapo kuwa vimevaliwa.Tulio wengi hasa mabinti au wanawake tunaokwenda na wakati hupenda kuvaa viatu virefu ilikuongeza muonekano wa umbile lako nikiwa na maana kuwa miguu huonekana yenye kuvutia zaidi unapo kuwa umevaa viatu virefu.

Kutokana na utafiti wa kitaalamu, mwanamke ana uwezo wa kutembea wastani wa hatua 10,000 kwa siku.Visigino virefu hufanya nguvu inayotumika kutembea hatua moja kuwa kubwa kuliko kawaida, huku vikikunyima raha ya kutembea kwa uhuru kiasi kwamba wengine hufikia hatua ya kuvua na kutembea peku.

Leo hii napenda kukujuza madhara ya uvaaji wa wa viatu virefu.Kwa kawaida, miguu ya binadamu hasa visigino, vimeumbwa ili kuuzuia uzito wa mwili juu ya ardhi.Uvaaji wa viatu virefu hufanya uzito wa mwili kubebwa na kisigino, hivyo uzito wa mwili kushindwa kuhimili uzito wote.

Matokeo yake husababisha misuli na mishipa ya miguu, kiuno, mgongo na shingo kufanya kazi kubwa ya kujaribu kusawazisha uzito.Kazi ambayo kwa kawaida hufanywa na visigino.Tatizo hilo hupelekea kiuno,Miguu na mgongo kuwa katika hatari ya matatizo ya kiafya pamoja na kuteguka na kuvunjika miguu.

Visigino virefu hubadili muundo wa mifupa ya miguu, hivyo hupelekea magoti na misuli ya mapaja kufanya kazi ya ziada ili kuupa mwili usawa.Kwa kuwa misuli inafanya kazi kubwa, uwezekano wa kupatwa na maumivu makali ya miguu na kushindwa kutembea katika siku za baadae huwa mkubwa zaidi. Visigino virefu husababisha maumivu ya visigino, damu kuvilia ndani ya miguu, mpangilio wa mifupa ya vidole kuvurugika, mishipa na misuli ya mapaja kuuma, neva za fahamu kufungana na kushindwa kufanya kazi yake.

Tatizo huendelea kwa vifundo vya miguu, magoti, na mifupa ya kwenye mapaja kushindwa kujivuta na kulegea na hivyo kusuguana wakati wa kutembea.

Jambo la kuzingatia kwa wale wanaopenda kuvaa viatu virefu,ni vema kama unapenda kuvaa viatu virefu hakikisha hutembei umbali mrefu kama una usafiri sio mbaya ukivaa viatu virefu,na kwa wale wanao kwenda ofisini jitahidi kuwa na viatu flati ndani ya mkoba wako ili unapokuwa umechoka unavua na kuvaa viatu vyako pia ukiwa ofisini waweza kuvua viatu virefu.

Mpenzi msomaji kama huwezi kutembelea viatu virefu nivema ukipitwa na wakati kuliko kujiabisha barabarani na kuonekana rimbukeni ikiwa wewe ni mjamzito epuka uvaaji wa viatu virefu.Usikose kujumuika nami katika safu hii ya urembo na mitindo.

Ulaji mzuri hupunguza uwezekano wa kupata shinikizo la chini la damu

Ni mhimu kula mlo kamili kila siku. Kula lishe duni kunaweza kupelekea kuzalishwa kwa damu isiyo na afya inayoleta shinikizo la damu.

Kula zaidi vyakula vyenye protini, vyenye vitamini B na C kwa wingi. Kula milo midogo midogo hata mitano kuliko kula miwili au mitatu lakini ya nguvu sana.

Unaweza kutumia kitunguu swaumu hasa kibichi ukitafuna punje 2 kila unapoenda kulala kadharika glasi moja ya juisi ya ubuyu kutwa mara 1.

Acha vilevi vyovyote mara tu unapogundulika na shinikizo la chini la damu. Epuka pia vyakula vyenye wanga sana kama tambi, mikate, viazi, wali nk

Upungufu wa baadhi ya vitamini hasa vitamini za kundi B na madini kunaweza pia kuleta shinikizo la chini la damu. Hivyo ili kudhibiti shinikizo la chini la damu unahitaji kula mlo sahihi kila siku.

Jamaa anayependa kuwafanyia watu uhuni leo kapatikana na huyu mdada

Mdada alienda super-market kununua
kuku, bahati mbaya kwenye frij
kulikuwa na kuku mmoja tu, muuzaji
akamtoa akamuweka kwenye
mzani, akaonekana ana kilo moja na robo.

Mdada akamuuliza
muuzaji,’Huna mkubwa zaidi?’ Muuzaji
akamchukua yule kuku na
kujifanya kamrudisha kwenye friji, halafu
akamtoa tena kwenye friji na
kumrudisha kwenye mzani, safari hii
akagandamiza mzani kwa gumba,
kuku akaonekana ana kilo mbili. Mdada
akasema ‘Duh afadhali huyu
mkubwa kidogo, naomba unifungie
nawachukua wote wawili

Mamaaaaa muuzaji sijui atatoa wap kuku wa pili😂

😅😅😅😅😅Hapo ndipo utagundua kwa nini MUWA co TUNDA 🚶🏽🚶🏽

Mavazi ya Ofisini kwa Wadada

Wengi wetu tunashindwa kutofautisha mavazi ya sehemu husika mfano Ofisini, michezoni, na yale ya usiku na sehemu nyinginezo leo nitagusia vazi la ofisini kwa akina dada.

Unapotaka kuvaa vazi ,lazima uangalie vazi unalolivaa mda gani na mahala unapokwenda,siyo vazi la kutokea usiku au la kimichezo unalivaa ofisini,utakuwa kichekesho mbele za watu hata kwa wafanyakazi wenzio.

Mavazi ya kiofisi yanaeleweka lakini hasa kwa mwanamke basi vaa sketi fupi au ndefu na blauzi ya heshima iliyofunika kitovu chako, au suti ya heshima na koti na hata suruali ambayo haijakubana sana inafaa sana kwa ofisi.

Kama utapendelea kuvaa gauni basi angalia mkao wa hilo gauni ukoje maana mara nyingi gauni huwa halipendezi kuwa vazi la ofisini bali vazi la jioni.

Vyakula 7 vya kuepuka kula ili uwe na afya nzuri

Inasemwa kuwa “wewe ni kile unachokula” kwa kumaanisha kuwa mwonekano wetu na afya ya mwili na akili unajengwa na chakula tunachokula. Madhara ya chakula chetu tunachotumia yako pia katika ngozi. Kuna vyakula vinavyozeesha ngozi kwa haraka na ni budi kuvijua na kuviepuka.

Vyakula hivi japo tunavipenda sana lakini vina athari mbaya kwa miili yetu na muhimu kujenga tabia ya kuviacha katika milo yetu. Kama si rahisi kuacha kabisa basi angalau kupunguza matumizi yake.

Vifuatavyo ni vyakula 7 vinavyozeesha ngozi na unashauriwa kuvitoa katika mlo wako:

1. Nyama Nyekundu
Mojawapo ya vyakula vinavyozeesha ngozi ni nyama hasa nyama nyekundu. Wataalamu wa afya wanaeleza kuwa nyama nyekundu inayotokana na wanyama kama ng’ombe,mbuzi,kondoo,nguruwe n.k ni mbaya kwa afya njema ya binadamu na hivyo kwa ngozi pia. Nyama nyekundu ina kemikali aina ya carnitine ambayo inafanya mishipa ya damu kukakamaa na kusababisha kuzeeka kwa ngozi.

Hivyo nyama nyekundu ni mojawapo ya vyakula vibaya kwa afya ya binadamu na vya kuvizuia.

2. Chumvi

Chumvi hasa yenye madini ya iodine ni mbaya sana kwa afya ya ngozi. Inasababisha chembechembe za nyama katika ngozi kuvimba.

3. Sukari

Sukari japo tunaipenda sana ni adui mkubwa wa afya ya binadamu. Inadhoofisha mfumo wa kinga za mwili. Kiasi kingi cha sukari mwilini kinafanya ngozi kuwa kavu na kufanya mwili utengeneze makunyazi kwa sababu inaharibu kemikali ya collagen na elastin ambazo zinafanya kazi ya matengenezo ya ngozi kuifanya isiharibike na kuwa chakavu.

Sukari nyingi inasababisha mwili kukosa nguvu ya kupambana na bacteria wabaya. Ongezeko la bacteria hawa kunafanya utengenezwaji wa kemikali mbaya ambazo husababisha uchakavu wa ngozi.

Watu wanashauriwa kutumia sukari asilia kama ya matunda na asali kuliko zile zinazopatikana katika vinywaji kama soda na pipi , jojo,biskuti au vitafunwa vingine vyenye sukari ya kuongeza.

4. Vyakula vya Kukaangwa

Vyakula vya kukaangwa kama chipsi,nyama za kukaanga vinasababisha uingizaji wa mafuta mengi mwilini. Mafuta haya yenye vitu vinavyoitwa “Free Radicals” yanasababisha uzibaji wa vijitundu katika ngozi. Ukiachia ngozi mafuta mengi mwilini yanasababisha madhara mengi mengine yakiwemo magonjwa ya moyo na kisukari.

5. Mkate Mweupe,Tambi na Keki

Vyakula hivi vina kemikali ya glucemic kwa kiwango kikubwa ambayo inaleta madhara ya magonjwa ya ngozi (Ugonjwa wa madoa katika ngozi)

6. Pombe

Unywaji wa pombe unasababhisha kupoteza maji mengi mwilini kwa njia ya mkojo na huleta madhara mabaya kwa ngozi kwa kuifanya iwe kavu.

7. Kahawa (Caffeine)

Kemikali ya caffeine iliyomo katika kahawa na vinywaji vingine inasababisha ukosefu wa maji ya kutosha katika ngozi na kuifanya iwe kavu. Lakini pia caffeine inasababisha utengenezwaji wa kemikali ya cortisol ambayo inachangia uzeekaji wa ngozi.

Badilisha Tabia Yako ya Ulaji

Vyakula hivi ni baadhi ya vingi ambayo vimo katika ulaji wetu wa kila siku na una madhara makubwa kwenye ngozi zetu. Wanawake wanaathirika sana na ngozi ukilinganisha na wanaume. Au niseme wanajali sana ngozi zao kuwa zenye afya na kuvutia kuliko wanaume hivyo wanaweza kufaidika sana kwa kupunguza au kutotumia kabisa hivi vyakula vinavyozeesha ngozi.

Fahamu kuwa afya yako ni mtaji mkubwa hivyo ni kitu muhimu kuipa afya ya mwili wako kipaumbele na hivyo zingatia ulaji wako.

Vipodozi Visivyo Salama/Vilivyopigwa Marufuku Na Madhara Yake

SEHEMU YA KWANZA

1.0 UTANGULIZI

Vipodozi visivyo salama ni vipodozi ambavyo vina kemikali zinadhuru au zinazoweza kuudhuru mwili na kuusababishia matatizo. Maana hii inaweza kuongezewa na kujumuisha vipodozi vyote ambavyo usalama wake unatia mashaka na vinaweza kuleta madhara kwa mtumiaji.

Hivyo hujumuisha :

-Vipodozi ambavyo havijasajiliwa na mamlaka ya chakula na dawa Tanzania (TFDA)
-Vipodozi vyenye viambata (kemikali) vya sumu na vilivyopigwa marufuku na mamlaka ya chakula na dawa Tanzania (TFDA)
-Vipodozi ambavyo muda wake wa matumizi umeisha
-Vipodozi ambavyo havioneshi tarehe ya kuharibika (mwisho wa matumizi)
-Vipodozi ambavyo maelezo yake hayajaandikwa kwa Kiswahili au kiingereza

Vinaweza vikawa ni mafuta, losheni, krimu, pafyumu, poda na kadhalika.

1.1 VIAMBATA (KEMIKALI) VYA SUMU VILIVYOPIGWA MARUFUKU

Vingi vikiwa katika lugha ya kiingereza, hizi ndizo kemikali ambazo huongezewa katika vipodozi ili kufanikisha au kusaidia dhumuni lililolengwa kwa kipodozi husika. Viambato vyenye sumu vilivyopigwa marufuku ni:

  • Chloroquinone (Hydroquinone na kemikali zingine)
  • Steroids (Mifano ni Betamethasone, Beclomethasone, Hydrocortisone, Clobetasol, na Dexamethasone)
  • Mercury (Zebaki) na kemikali zinazotokana nayo
  • Chloroform
  • Bithionol
  • Hexachlorophene
  • Mercury (Zebaki) na kemikali zinazotokana nayo
  • Vinyl chloride
  • Zirconium na kemikali zinazotokana nayo
  • Methyelene chloride
  • Halogenated salicylanilides (Dimetabromsalan, Trimetabromsalan na Tetrabromsalan)
  • Chlorofluorocarbons (Kwenye pafyumu na deodorants)

1.2 JINSI YA KUJUA KAMA KIPODOZI KINA KIAMBATO (KEMIKALI) CHA SUMU KILICHOPIGWA MARUFUKU

Angalia kwenye lebo ya kipodozi chako sehemu waliyoandika Ingredients au Contents au neno jingine lolote lenye maana ya Vitu vilivyomo ndani. Hapo angalia kama kuna kiamabato au kemikali yoyote ambayo nimeiandika hapo juu kuanzia namba 1 mpaka 12.

Kama kuna kiambato au kemikali ambayo imepigwa marufuku basi jua kipodozi chako sio salama. Acha kukitumia mara moja na toa taarifa kwa mamlaka ya chakula na dawa Tanzania (TFDA).

Kama hakuna kiambato cha sumu basi kipodozi chako kinaweza kuwa salama. Tatizo linakuja pale watengenezaji wanapofanya uhuni kwa kudanganya au kuficha na kuacha kuandika baadhi ya viambato vilivyomo ndani. Ambalo pia ni kosa kisheria.

Mifano

  • Sabuni ya JARIBU ina kiambato MERCURY. Sabuni hii sio salama, haifai kwa matumizi na imepigwa marufuku.
  • Losheni/krimu ya MEKAKO ina kiambato HYDROQUINONE. Losheni/krimu hizi sio salama, hazifai kwa matumizi na zimepigwa marufuku
  • Krimu za FAIR & LOVELY SUPER CREAM, VISIBLE DIFFERENCE CREAM, SKIN SUCCESS FADE CREAM, DEMOVATE NA DIPROSON CREAM zina viambata Krimu hizi sio salama kutumika kama vipodozi na zimepigwa marufuku

SEHEMU YA PILI

2.0 MADHARA YA VIPODOZI VISIVYO SALAMA

Vipodozi visivyo salama vina madhara mengi sana kwa afya ya mtumiaji. Na kama mtumiaji ni mjamzito basi madhara hayo yanaweza kumpata na mtoto aliyepo tumboni.

Pia vipodozi hivi vina athari nyingi sana kiuchumi kwani vitapelekea mtu kutumia pesa tena kugharamia matibabu ya matatizo atakayopata. Madhara hayo ni pamoja na:

-Ugonjwa wa saratani (kansa) ya ngozi, maini, ubongo, mapafu, mfumo wa damu, utumbo mpana na kibofu cha mkojo
-Uharibifu wa ngozi, macho, ini, mapafu na figo
-Magonjwa ya moyo na kutopumua vizuri
-Kutokwa na chunusi kubwa kubwa
-Ngozi kuungua, maumivu makali, ngozi kuwa nyekundu na kutokwa na vipele
-Ngozi kuwa nyembamba sana na laini na endapo ngozi itapata jeraha au kufanyiwa upasuaji, kidonda kitachelewa kupona au hakitapona
-Mzio (Allergy) na muwasho wa ngozi
-Kichefuchefu, kutapika, kusikia usingizi na kizunguzungu
-Magonjwa ya akili, mishipa ya fahamu (hasa kichwani)
-Uharibifu wa ubongo na mtindio wa ubongo kwa watoto wachanga na waliopo tumboni
-Ngozi kuwa laini na kusababisha kupata magonjwa kama fangasi kwenye ngozi au maambukizi ya vimelea vya maradhi
-Kuchubuka kwa ngozi
-Ngozi kuwa na mabaka meusi na meupe au rangi mbalimbali
-Upofu, uziwi na upotevu wa fahamu wa mara kwa mara
-Kuumwa kichwa, kusikia kizunguzungu na kupoteza fahamu

2.2 USHAURI

Kama tulivyoona hapo juu mengi ya madhara ya vipodozi visivyo salama ni makubwa na huhatarisha kabisa afya za watumiaji na watoto. Hivyo ni vyema kuvijua na kuviepuka kabisa ili usiweze kupata madhara.

Pili msaidie kumuelimisha ndugu, jamaa na rafiki nay eye ajue na asitumie kabisa vipodozi visivyo salama

Pia ukiona mtu au duka ambalo linauza vipodozi visivyo salama acha kununua vipodozi kutoka kwake na toa taarifa kwa mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa

Epuka kabisa vipodozi visivyo salama. Hata kama vinakuletea matokeo mazuri kiasi gani.

SEHEMU YA TATU

3.0 ORODHA YA VIPODOZI VISIVYO SALAMA NA VILIVYOPIGWA MARUFUKU TANZANIA

Vifuatavyo ni vipodozi visivyo salama na vimepigwa marufuku kutumika. Epuka kabisa kutumia vipodozi hivi hata kama vinakuletea matokeo mazuri kiasi gani.

3.1 Krimu, Losheni na Jeli zenye kiambato cha Hydroquinone

  • Mekako Cream
  • Rico Complexion Cream
  • Princess Cream
  • Butone Cream
  • Extra Clair Cream
  • Mic Cream
  • Viva Super Lemon Cream
  • Ultra Skin Tone Cream
  • Fade-Out Cream
  • Palmer’s Skin Success (Pack)
  • Fair & White Active Lightening Cream
  • Fair & White Lightening Cream
  • Fair & White Strong Bleaching Treatment Cream
  • Fair & White Body Clearing Milk
  • Maxi-Tone Fade Cream
  • Nadinola Fade Cream
  • Clear Essence Medicated Fade Cream
  • Peau Claire Body Lotion
  • Reine Clair Rico Super Body Lotion
  • Immediate Claire Maxi –Beauty Lotion
  • Tura Lotion
  • Lkb Medicated Cream
  • Crusader Skin Toning Cream
  • Tura Bright & Even Cream
  • Claire Cream
  • Miki Beauty Cream
  • Peau Claire Crème Eclaircissante
  • Sivoclair Lightening Body Lotion
  • Extra Clair Lightening Body Lotion
  • Precieux Treatment Beauty Lotion
  • Clear Essence Skin Beautifying Milk
  • Tura Skin Toning Cream
  • Madonna Medicated Beauty Cream
  • Mrembo Medicated Beauty Cream
  • Shirley Cream
  • Kiss – Medicated Beauty Cream
  • Uno21 Cream
  • Princess Patra Luxury Complexion Cream
  • Envi Skin Toner
  • Zarina Medicated Skin Lightener
  • Ambi Special Complexion
  • Lolane Cream
  • Glotone Complexion Cream
  • Nindola Cream
  • Tonight Night Beauty Cream
  • Fulani Cream Eclaircissante
  • Clere Lemon Cream
  • Clere Extra Cream
  • Binti Jambo Cream
  • Malaika Medicated Beauty Cream
  • Dera Heart With Hydroquinone Cream
  • Nish Medicated Cream
  • Island Beauty Skin Fade Cream
  • Malibu Medicated Cream
  • Care Plus Fairness Cream
  • Topiclear Cream
  • Carekako Medicated Cream
  • Body Clear Cream
  • A3 Skin Lightening Cream
  • Ambi American Formula
  • Dream Successful
  • Symba Crème Skin Lite ‘N’ Smooth
  • Cleartone Skin Toning Cream
  • Ambi Extra Complexion Cream For Men
  • Cleartone Extra Skin Toning Cream
  • O’nyi Skin Crème
  • A3 Triple Action Cream Pearlight
  • Elegance Skin Lightening
  • Clere Cream
  • Clear Touch Cream
  • Crusader Ultra Brand Cream
  • Ultime Skin Lightening Cream
  • Rico Skin Tone Cream
  • Baraka Skin Lightening Cream
  • Fairlady Skin Lightening Cream
  • Immediate Claire Lightening Body Cream
  • Jaribu Skin Lightening Lotion
  • Amira Skin Lightening Lotion
  • A3 Clear Touch Complexion Lotion
  • A3 Lemon Skin Lightening Lotion
  • Kiss Lotion
  • Princess Lotion
  • Clear Touch Lotion
  • Super Max-Tone Lotion
  • No Mark Cream
  • Body Clear
  • Top Clear
  • Ultra Clear
  • Peau Claire Lightening Body Oil
  • G &G Dynamiclair Lotion
  • G & G Teint Uniforme
  • G & G Cream Lightening Beauty Cream
  • Dawmy – Lightening Body Lotion
  • Maxi White Cream
  • Bioclare Lightening Body Lotion

3.2 Vipodozi vingine vyenye Hydroquinone

  • Fair & White Powder (Exclusive Whitenizer & Serum)
  • New Youth Tinted Vanishing Cream
  • Skin Success Fade Cream Regular
  • Teint Clair Clear Cpmplexion Body Lotion
  • Mareme Cream
  • Si Clair Plus Cream
  • Clair & White Body Cream
  • Body White Lotion
  • Bio Claire Cream
  • Forever Aloe MSM Gel
  • Kroyons Baby Oil
  • 3.3 Sabuni zenye kiambato cha Hydroquinone
  • Body Clear Medicated Antiseptic Soap
  • Blackstar
  • Cherie Claire Body Beauty Lightening & Treating Soap
  • Immediate Claire Body Beauty Soap
  • Lady Claire
  • G.C Extra Clear
  • Top Clear Beauty Complexion Soap
  • Ultra Clear
  • 3.4 Vipodozi vyenye Hydroquinone pamoja na Steroid
  • Clear Essence Skin Beautifying Milk For Sensitive Skin
  • Fair & White Clarifiance Fade Cream
  • Fair & White Exclusive Whitenizer Body Lotion
  • Fair & White Exclusive Whitenizer Cream
  • Fair & White Exclusive Whitenizer Gel
  • Fair & White Maxitone Lightening Lotion Sun Block
  • Fair & White So White Skin Perfect Gel

3.5 Sabuni zenye kiambato cha Mercury (Zebaki) na michanganyo yake

  • Movate Soap
  • Miki Soap
  • Jaribu Soap
  • Binti Jambo Soap
  • Amira Soap
  • Mekako Soap
  • Rico Soap
  • Tura Soap
  • Acura Soap
  • Fair Lady
  • Elegance
  • Block & White Skin Whitener Germicidal Bath Soap
  • Rose Beauty Soap
  • Maxi-Tone Soap (Skin Lightening Soap)
  • Margostara Soap (New Tannin)
  • Rusty – Whitening Soap (New Formula)
  • Emani Natural Fair Pearls Soap

3.6 Krimu zenye kiambato cha Mercury na michanganyiko yake

  • Pimplex Medicated Cream
  • New Shirley Medicated Cream

3.7 Krimu zenye Steroids (Betamethasone, Beclomethasone, Hydrocortisone, Clobetasol,

Dexamethasone nk)

  • Amira Cream
  • Jaribu Cream
  • Fair & Lovely Super Cream
  • Neu Clear Cream Plus (Spots Remover)
  • Age Renewal Cream
  • Visible Difference Cream (Neu Clear Spots Remover)
  • Body Clear Cream
  • Sivo Clair Fade Cream
  • Skin Balance Lemon Cream
  • Peau Claire Cream
  • Skin Success Cream
  • M & C Dynamic Clair Cream
  • Skin Success Fade Cream
  • Fairly White Cream
  • Clear Essence Cream
  • Miss Caroline Cream
  • Lemonvate Cream
  • Movate Cream
  • Soft & Lovely Cream
  • Mediven Cream
  • Body Treatment Cream (Spots Remover)
  • Dark & Lovely Cream
  • Sivo Clair Cream
  • Musk – Clear Cream
  • Fair & Beautiful Cream
  • Beautiful Beginning Cream
  • Diproson Cream
  • Demovate Cream
  • Top Lemon Plus
  • Lemon Cream
  • Beta Lemon Cream
  • Tenovate Cream
  • Unic Clear Super Cream
  • Topifram Cream
  • First Class Lady Cream

3.8 Vipodozi vingine vyenye kiambato cha Steroid

  • Fashion Fair Gel Plus
  • Hot Movate Gel
  • Hyprogel
  • Mova Gel Plus
  • Secret Gel
  • Secret Cream
  • Peau Claire Gel Plus
  • Hot Proson Gel
  • Skin Success Gel Plus
  • Skin Clear Gel Plus
  • Soft & Beautiful Gel
  • Skin Fade Gel Plus
  • Ultra – Gel Plus
  • Zarina Plus Top Gel
  • Action Demovate Gel Plus
  • Prosone Gel
  • Skin Balance Gel Wrinkle Remover
  • TCB Gel Plus
  • Demo – Gel Plus
  • Regge Lemon Gel
  • Ultimate Lady Gel
  • Topifram Gel Plus
  • Clai & Lovely Gel
  • Fair & White Serum Exclusive Whitenizer
  • Maxi White Lightening Body Milk
  • Maxitone Cleansing Milk
  • Avoderm Cream
  • Niomre Cream
  • Niomre Lotion
  • Nyala Lightening Body Cream
  • Si Clair Cream
  • Cute Press White Beauty Lotion
  • White SPA Rose Lotion
  • White SPA UV Lightening Cream

3.9 Vipodozi vya kupunguza unene vilivyopigwa marufuku

  • Bio Valley Sliming Gel

3.10 Vipodozi vya nywele vilivyopigwa marufuku

  • African Gold Super Glo
  • Sofn Free Hair Foodblue Cap Shampoo
  • Marhaba Anti-Dandruff Hair Cream
  • Blue Cap Spray
  • Blue Cap Cream

3.11 Vipodozi vinginevyo vilivyopigwa marufuku

  • Bio Light Cream
  • Salon Dermaplex Amazon Clay 9Normal To Dry Skin)
  • Beauty Secrets Body Cream
  • Swiss Soft N White Lightening Gel
  • Whitening Complex Mask

3.12 Vipodozi Vinavyosababisha muwasho vikitumika karibu na macho

  • Eye Shadow Gel
  • Eye Shadow Gel 02
  • Eye Shadow Gel 07
  • Eye Shadow Gel 08
  • Eye Shadow Gel 09
  • Eye Shadow Gel 10

TAHADHARI : VIPODOZI VISIVYO SALAMA VIPO VINGI ZAIDI YA HIVYO AMBAVYO VIMEORODHESHWA HAPO JUU NA VINGINE VINGI ZAIDI VINAWEZA VIKAFIKA SOKONI.

Mara zote kuwa makini na vipodozi na pata taarifa, elimu na ushauri kutoka Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) na wataalam wa afya, urembo na vipodozi.

Mambo ya msingi kwa mwanamke kuyajua unapojiremba

Kope nazo humpendezesha mwanamke kuna aina ya rangi za kupaka kwenye kope, lakini zinatofautiana. Ni vyema ukawasiliana na wataalamu wa mambo ya urembo kwa ushauri na siyo kukurupuka. Siyo umemuona fulani kapendeza na aina fulani ya rangi ya kwenye kope halafu na wewe ukakimbilia kupaka, utachekesha.

Rangi ya mdomo nayo ni eneo lingine linalompendezesha mwanamke. Ukweli ni kwamba tunatofautiana sana midomo wazungu wanaita ‘Lips’ Kila mwanamke ana tofautiana midomo na mwingine kwa hiyo hata rangi ya midomo nayo inakwenda sambambana aina ya lips na rangi ya ngozi ya mwili aliyo nayo mwanamke, siyo unajisiriba rangi ya mdomo halafu unaonekana kituko. Wasiliana na wataalamu wa urembo kwa ushauri zaidi.

Kucha kwa wanawake ni eneo lingine linolatakiwa kuwekwa katika unadhifu. Kuna baadhi ya wanawake unaweza kukutana nao kucha zao zimelika aidha kwa kung’atwa au kwa kuliwa na fangasi.

Ni vyema wanawake wenye tatizo hilo kumuona mtaalamu wa ngozi kwa msaada wa tiba. Unaweza kukutana na mwanamke kucha zake zimelika na zina sharp edges kiasi kwamba akikugusa utadhani umeguswa na msasa.

Au akishika Glasi ya Kinywaji ukiangalia kucha utadhani mkono ni wa mwanaume maana kwa jinsi kucha zake zilivyo hata hafanani nazo. Kuna kucha za bandia kama mwanamke ana matatizo ya kucha basi akazinunue kusitiri aibu.

Marashi, manukato au unyunyu kama wanavyoita vijana wa mjini ni muhimu kwa wanawake lakini ni vyema nikaweka angalizo. Haipendezi kwa mwanamke anayepulizia manukato yanayonukia sana mpaka yakawakera wengine ni vyema wanawake wakajipulizia marashi yenye staha na yasiyokera.

Ngozi ya mwanamke ni bora ‘sensitive’ sana na inaakiwa ipakwe aina ya mafuta au lotion yenye virutubisho kulingana na aina ya Ngozi. Kuna wanawake wenye Ngozi ya mafuta ‘Oil Skin’ kuna wenye Ngozi mchanganyiko na kuna wale wenye ngozi kavu (Dry Skin).

Ni vyema mwanamke kujua aina ya ngozi yake ili ajie aina ya product ya ngozi anayopaswa kutumia na siyo kwa sababu umemuona mwenzio anapaka aina fulani ya losheni na wewe unakimbilia kununua. Omba ushauri kwa wataalamu wa ngozi watakusaidia. Kuna baadhi ya maduka yanyouza vipodozi wanatoa msaada huo bure kabisa.

Shopping Cart
1
    1
    Your Cart
    🏠 Home 📖 Reading 🖼️ Gallery 💬 AI Chat 📘 About