Dawa gani za kulevya ni hatari zaidi?

Kwa ujumla dawa zote za kulevya zinaweza kuwa ni za hatari. Kati ya dawa zilizohalalishwa kisheria nikotini, ambayo i ipo kwenye sigara, ndiyo hasa ya hatari. Inawezekana kuwa umeshakuwa tegemezi kwa sigara. Hii i ii ina maana ubongo wako utaizoea nikotini na utahitaji nikotini zaidi na zaidi i i ili kuendelea kuwa na hali nzuri. Nikotini pia ni hatari zaidi kwa sababu vijana mara nyingi huanza kutumia sigara kabla ya kuanza kutumia dawa kali zaidi.

Miongoni mwa dawa zisizoruhusiwa kisheria nchini Tanzania, heroini ndiyo labda yenye kusababisha utegemezi. Vilevile inahusishwa na makosa mengi ya jinai. Utumiaji wa heroini ni hatari hasa katika maambukizi ya UKIMWI. Watu wanaposhirikiana katika kutumia sindano za kujidungia heroini wanajiweka katika hatari na uwezekano mkubwa sana wa kuambukizana virusi vya UKIMWI. Hili hutokea pia pale watumiaji wa heroini wanapojiuza mii li yao katika ngono i ili wapate dawa za kulevya au fedha za kununulia dawa hizo.
Uvutaji bangi husaidia kuondoa aibu na vizuizi. Hii i ii inamaanisha kuwa wavuta bangi wanaweza wakasahau kufanya ngono salama na hivyo kuwa katika hatari zaidi ya kupata au kueneza UKIMWI. Matumizi mabaya ya dawa huweza kuwa hatari sana na pengine kusababisha kifo pale zitakapotumiwa kupita kipimo ama zitakapochanganywa na dawa nyngine au pombe.

Melkisedeck Leon Shine

Editor: Melkisedeck Leon Shine, Enjoyed? Drop your Comment Below. OR Chat Live here. Download My Books in PDF Format here. More: Legal Guidelines | About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp

Read and Write Comments
Shopping Cart