SMS ya kumkumbusha mpenzi wako yeye ni nani kwako
Kumbuka kuwa wewe ni wangu
Kitulizo cha moyo wangu
Kwenye shida na raha
Wewe ni sehemu ya maisha yangu milele
Kumbuka kuwa wewe ni wangu
Kitulizo cha moyo wangu
Kwenye shida na raha
Wewe ni sehemu ya maisha yangu milele
Ckia ckupend, cktaki na wala ckhitji tena ww ni kikwzo
ktka maisha yangu ucnizoee! Mwmbie shtan maneno hya kabla
hjalala. g9t
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Hata kama nitajidanganya kwamba sikupendi, moyo wangu
umeganda kwako na hakuna dalili za kukuacha, wewe ni wangu
peke yako dear…
mapenzi ni safari,mapenzi ni ahadi,mapenzi ni
ujasiri,mapenzi ni zawadi,mapenzi mitihani,mapenzi
ramani,mapenzi ajali na ndiyo maana nakupenda wewe bila kujali.
nashtumiwa kwa kumpenda mcchana mmoja aliyeutesa moyo
wangu
mahakama imenihukumu kifo kwa kunyongwa na kamba upendo
lkn kwa msamaha wa raisi mapenzi
nmehukumiwa kuwa mwaminif kwake nakumpenda zaidi ya hapo
daima milele.
nakupenda mpz
Dah! Safari yetu ilikuwa ngumu kweli ila hatimaye tumefika japo ni usiku sana hebu tupige hodi tusije kabwa na vibaka hapa nje. Hodiiiiii, Hodiiiii, Tunaomba tufungulie Mlango,, sisi tunaitwa FURAHA, AMANI na UPENDO. Tumebeba HEKIMA, BUSARA na MAFANIKIO. Tulikuwa wengi HURUMA na UPOLE wanakuja nyuma. CHUKI na WIVU hawana nauli. TABU ni mahututi. SHIDA yuko jela. MATATIZO amepigwa shoti ya umeme. MIKOSI amefariki njiani. LAANA ameliwa na mamba. UVIVU ameungua na maji ya moto hajiwezi. Tutakuwa nawe daima maana tumefika kwa NEEMA . Mungu akulinde na mabaya yote katika dunia hii. ucku mwema.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Mapenzi ni matamu napia yana raha, wewe hauni ishi hamu, siku zote wanipa raha, wewe kwangu ni mtu muhimu, unaeng’aa moyoni mwangu kama nyota ya jaha. “NAKUOMBA USINIACHE MPENZI WANGU”
Tambua kuwa nakujali
Furahia kwamba nitakuwa na wewe
Katika siku zote za maisha yangu
Nitakupenda bila kikomo milele
Kuna miezi 12 katika mwaka…siku 30 katika mwezi…siku 7
katika wiki, masaa 24 katika siku…dakika 60 katika saa……
lakini wewe ni mmoja tu maishani mwangu.
tazama, nimezama
ndani ya bahari
la penzi lako
siwezi
kusonga mbele
kurudi nyuma
sijielewi
haya mapenzi ya fujo hayafai
kama wanipenda
jaribu kunipa raha
Ingawa mwaka umekwisha, mawazo yangu katu sitobadilisha, amini ni wewe pekee unayenipagawisha, hakika kwa penzi lako kiu yangu katu haitakwisha!
nimetuma ndege wangu auzunguke ”moyo” wako kwa ” upendo
” auguse ”uso” wako kwa ”faraja” na mwisho
akunong’oneze sikioni taratibu kuwa nakupenda.
unaweza ukafunga macho kwa usilolitaka kuliona lakini
hauwez kufunga moyo wako kwa Unalo Lipenda. Nakupenda
Mpenzi
Imara hautikisiki,kakamavu halishikiki penzi langu kwako
ni nuru daima halizimiki.upo juu katika mapenzi.
Mvua na jua haviwezi kuwa pamoja, usiku na mchana
hazigongani, lakini mimi na wewe, hata wasemaje,
‘tunafiti’ kuwa pamoja.
sioni zawadi ya kukupatia kwa mapenzi
unayonipatia,
moyoni nimekuridhia wewe pekee penzi langu daima
kukupatia nakupenda
Maji hunitosha nisikiapo kiu, chakula hinitosha nisikiapo njaa, lakini wewe hunifaa kwa kila kitu!
Mapenzi ni kitu kisichotabirika, ndio maana kila mwenye KUPENDA au KUPENDWA hana uhakika na PENZI lake kwa yule AMPENDAE, Muda wote huhisi anasalitiwa. PENZI Ni kama JENGO lililokosa NGUZO muda wowote unahisi litadondoka… Usinielewe vibaya sikukatazi KUPENDA au KUPENDWA, ila tazama wapi UMEPENDA au UMEPENDWA.kilalakher kwa umpendae
Usiku wa leo uwe ni wenye faraja kwako, utawaliwe na usingizi wa mahaba kwenye kope zako, naomba ujenge taswira yangu katika mawazo yako, Usisahau kuniota sweet wangu. USIKU MWEMA
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Ningependa siku moja utamani sana kuwa na mimi, na
uhangaike sana kunitafuta, ili ujue ni kwa kiasi
ninavyotamani kuwa nawe sasa.
Recent Comments