SMS ya kumtumia mpenzi wako kunapokuwa na wanafiki wanaoingilia penzi lenu
Wanafiki tusiwaombee kifo daima na milele washuhudie penzi
letu linavyozidi kukua,na tunavyopambana na mapito.
Wanafiki tusiwaombee kifo daima na milele washuhudie penzi
letu linavyozidi kukua,na tunavyopambana na mapito.
Nakuomba usiondoke, bali ubaki nami
Kwani wewe ndiye kamilisho la maisha
Yangu kwa sasa na siku za usoni
Nakupenda mpenzi W nafasi uliyotawala moyoni mwangu ni
kubwa, hakuna ambaye anaweza kufikia uhodari wako, wewe ni
mtu muhimu sana maishani mwangu.
Penzi langu kwako ni la milele, nitakuhifadhi moyoni
mwangu siku zote za maisha yangu, uwe wangu nami niwe wako
daima, nakupenda dear…
Fikra hutawala mtima wangu, Kwa madhila yalojaa duniani, Kwa muhali wa yanayojiri, Kwa machweo na mawio, Kwa totoro ama nuruni, Nao moyo hukosa ukamilifu, Kwa utashi wa zake hisia, Zinipazo sababu kuu, Ya upendo juu yako, Ya kukufanya daima uwe, Mawazoni mwangu. Mawazoni ama ndotoni, Daima wewe hutawala, Kila asubuhi niamkapo, Nao usiku nilalapo, U chakula changu akilini, Nalo tulizo langu moyoni, Daima huuwaza upekee, Wewe uliojaaliwa, Na hivyo naihisi furaha, Daima wewe uwapo, Mawazoni mwangu.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Kama ungekuwa kidonda kwenye moyo wangu, ningekiacha na
maumivu yake ndani yangu.
Usiku wa leo uwe ni wenye faraja kwako, utawaliwe na usingizi wa mahaba kwenye kope zako,
naomba ujenge taswira yangu katika mawazo yako, Usisahau kuniota sweet wangu. USIKU MWEMA
Katika nyuso za dunia, na kati ya miamba ya jangwani,
Kuna SAUTI! Neno la pendo lako liotapo karibu yangu.
Ni zaidi ya roho iendayo safarini.
pendo la dhati lina sifa
zifuatazo,kuvumilana, kusubiriana, kujaliana, kushauriana, na
La Mwisho Ni Mimi Na Wewe.
Watu husema kwamba, awapo mtu mmoja tu akupendaye, maisha
hayajapoteza maana, kwa hiyo, ukijihisi mpweke hauhitaji
kuishi nikumbuke mimi.
natamani usaini moyoni mwang,ikiwezekana pia upige muhuri moyoni mwangu wajue nan mmiliki wa huo moyo wenye shibe upendo kwaajili yako mpenzi
Mmmh!mpz cjui n kwann nahamu ya kufaid penz lako kiac
hk,?na taman lait ungekuwa krb yang unipme gonjwa hl na
unitibu pia.kwan ww ndiye daktar wa pekee n naye mwamin.
Nmemic kila k2 toka kwako nahc nazd kuchanganyikiwa kwa
ukosef wa penz lako.nakutaman sn wangu laaziz.
Nakupenda kipenz cha moyo wangu.
Si vibaya mimi kukusifia kwani wewe ni wangu, nivingi umejaaliwa, vinavyouvutia moyo wangu, ama hakika uzuri wako umedhibiti matamanio yangu “SINTOMPENDA MWINGINE ZAIDI YAKO”
Nitaenda mbali Zaidi ya maono yako
Safarini nitajenga hekalu la pendo letu
Nitapuliza filimbi kama ishara ya utambulisho wako
Na mwanzo wa sherehe ya ndoa yetu
Licha ya upole ulionao! Pia upendo wako ndio kishawishi cha kunifanya nikukumbuke siku zote. Jiulize! nina namba za watu wangapi ktk cmu yangu,na bado sijatamani kujua hali zao ila wewe! kwa kuwa, nakuthamini nakukujali, ndiyo maana nakutakia, SIKU NJEMA
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Mpenzi unawafahamu maadui wa mapenzi yetu ? Ni wale rafiki zako wanaokuletea maneno ya uongo, ndugu zako wanaotugombanisha na wachawi wanotuotea mabaya, tujihadhari tusiwape ushindi. Mapenzi yetu yadumu daima.
“””””Yule”””””
Anipendezae lazima nimkumbuke””
“”nimpe salamu “”moyo””
wangu “”uridhike””
“”Nimuombee kwa
MWENYEZI “”MUNGU”” mabaya yamuepuke””
“”na kila lililo la kheri kwake lisiondoke””
“”nakutakia””
“ucku mwema”
chekecho la huba ,toka uvunguni mwa moyo wangu
navika moyo wako taji la upendo,na kupulizia marashi ya hubaa ,usimpe mwingine mi ndiye ninayejua kulea.
nakupenda sana mpenzi wangu ,we ndo wa pekee mwenye kujua
furaha ya moyo wangu nikiwa na majonzi huwa upo karibu
nami,nikiwa na furaha huja kushea nami,ahsante wangu
tabibu ,we ndo wangu wa manani.
Wanasema mtu huanguka katika mapenzi mara moja, jambo
ambalo mimi naliona si la kweli kwa maana kila
ninapokutazama najikuta nakupenda tena na tena.
Recent Comments