Vipimo Vya Ugali:
Unga wa mahindi/sembe – 4
Maji – 6 takriban
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Chota unga kidogo katika kibakuli uchanganye na maji kidogo .
Weka maji mengineyo katika sufuria kwenye moto.
Changanya na mchanganyiko mdogo ufanya kama uji.
Kisha kidogo kidogo unaongeza sembe huku unakoroga na kuusonga ugali hadi uive.
Vipimo Vya Mchuzi Wa Samaki Wa Nazi
Samaki nguru – 5 vipande
Pilipili mbichi ilosagwa
Kitunguu maji kilosagwa – 1 kimoja
Nyanya ilosagwa – 2
Haldi/tumeric/bizari ya manjano – ¼ kijiko cha chai
Chumvi – kiasi
Ndimu – 2 kamua
Tui la nazi zito – 2 vikombe
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Baada ya kumuosha samaki, weka katika sufuria.
Tia chumvi, ndimu, pilipili mbichi ilosagwa.
Tia vitunguu na nyanya zilosagwa
Mkaushe kwa hivyo viungo, akianza kukauka tia tui la nazi.
Acha kidogo tu katika moto tui liwive mchuzi ukiwa tayari.
Vipimo Vya Bamia
Bamia – ½ kilo takriban
Nyanya kopo – 1 kijiko cha chai
Methi/uwatu/fenugreek seeds ilosagwa – 1 kijiko cha chai
Dania/corriander ilosagwa – ½ kijiko cha chai
Chumvi – kiasi
Mafuta – 1 kikombe cha kahawa
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Katakata bamia kwa urefu.
Weka mafuta katika karai, kisha tia bizari zote na nyanya kopo, kaanga kidogo.
Tia bamia endelea kukaanga, kisha acha katika moto mdogomdogo ufunike.
Kila baada ya muda funua karai ukaange bamia hadi ziwive zikiwa tayari.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE