Ndiyo, hata akitoa uume nje ya uke kabla ya kumwaga mbegu anaweza akaambukizwa Virusi vya UKIMWI na UKIMWI. Ni hatari kwa mwanamke na pia kwa mwanaume, kwa sababu vijidudu vimo ndani ya majimaji ukeni na uumeni. Hasa kama mmoja kati ya wapenzi ana vidonda au michubuko midogo sehemu za siri, Virusi vya UKIMWI. huingia kwa urahisi.
Kutoa uume nje ya uke kabla ya kumwaga shahawa siyo njia salama ya kujikinga na maambukizi ya Virusi vya UKIMWI.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE
Recent Comments