SMS nzuri kuhusu maana ya mapenzi
mapenzi si pombe lkn yanalewesha, wala si kidonda lakini
yanatonesha,wala si maradhi lakini yanaumiza, wala si
njaa lakini yanakondesha ,mapenzi ni uvumilivu kwa
unaempenda
mapenzi si pombe lkn yanalewesha, wala si kidonda lakini
yanatonesha,wala si maradhi lakini yanaumiza, wala si
njaa lakini yanakondesha ,mapenzi ni uvumilivu kwa
unaempenda
Kuna miezi 12 katika mwaka…siku 30 katika mwezi…siku 7
katika wiki, masaa 24 katika siku…dakika 60 katika saa……
lakini wewe ni mmoja tu maishani mwangu.
tunda langu laangaliwa hawajui nilipoli chuma,
utamu wake maridhawa,hakika utalipenda.si mpi tunda langu mwingine na lila mwenyewe.
Mwanamke ni yule amfanyaye mwanamme auhisi uanaume wake,
wewe ni mwanamke mwenye sifa hizo.
Mvua na jua haviwezi kuwa pamoja, usiku na mchana
hazigongani, lakini mimi na wewe, hata wasemaje,
‘tunafiti’ kuwa pamoja.
Tambua kuwa nakujali
Furahia kwamba nitakuwa na wewe
Katika siku zote za maisha yangu
Nitakupenda bila kikomo milele
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Pendo la kweli ni hisia zilizomo moyoni ambazo sauyi yake haisikiki isipokuwa kwa akupendae kwa dhati. Nakupenda mpenzi wangu.
Fikra hutawala mtima wangu, Kwa madhila yalojaa duniani, Kwa muhali wa yanayojiri, Kwa machweo na mawio, Kwa totoro ama nuruni, Nao moyo hukosa ukamilifu, Kwa utashi wa zake hisia, Zinipazo sababu kuu, Ya upendo juu yako, Ya kukufanya daima uwe, Mawazoni mwangu. Mawazoni ama ndotoni, Daima wewe hutawala, Kila asubuhi niamkapo, Nao usiku nilalapo, U chakula changu akilini, Nalo tulizo langu moyoni, Daima huuwaza upekee, Wewe uliojaaliwa, Na hivyo naihisi furaha, Daima wewe uwapo, Mawazoni mwangu.
Happy birthday mpenzi, nakuombea kwa mwenyezi akupe
maisha marefu na kukuepusha na maradhi,
pongezi kwa wako wazazi
kwa kukuzaa mpenzi,
nakupenda la azizi.
USikimbie nyuki ukakosa asali, utamu wa samaki ni kula na
wali,
usizidishe siki akawa mkali.
Ni
mimi niliye na dhiki nakujulia tu hali.
Je unakubali au unakataa kwa mujibu wa sheria ya mahakama
ya mapenzi kifungu cha mahaba unahukumiwa kuwa na mimi
milele,unaweza kukata rufaa kama hujatendewa haki.sawa?
Tone la mvua huonekana dogo sana, lakini kwa mwenye kiu hulisubiri kwa hamu kubwa. Sms ni kitu kidogo, lakini huonyesha mahali fulani yupo mtu ANAYEKUPENDA, ANAKUKUMBUKA, ANAKUOMBEA,
ANAKUJALI na,
ANAKUTAKIA mafanikio mema
Niliumbwa kwa ajili yako, mbele yako nitakushika mkono, nikuonyesha sayari yangu, pendo langu la undani, na NITAKUHESHIMU milele mpenzi wangu.
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Ni vigumu kumpata mwenye mapenzi ya kweli na zaidi yule
atakayekuwa tayari kukupenda zaidi, hivyo nafasi
inapopatika si busara kuichezea tudumishe penzi letu
laazizi wangu.
Hakika sikutaraji kulikosa lako penzi, wataka kuniacha
kuniacha ningali nakuhitaji, mpenzi tambua nahitaji yako
hifadhi na niko radhi kukupeleka hadi kwa wangu wazazi,
amini kwenda kwa mwingine sihitaji. Nakupenda.
Watu husema kwamba, awapo mtu mmoja tu akupendaye, maisha
hayajapoteza maana, kwa hiyo, ukijihisi mpweke hauhitaji
kuishi nikumbuke mimi.
Maneno huanza na ABC. Namba 123. Muziki na do re mi na
mapenzi huanza na mimi na wewe.
Katika ulimwengu wa mahusiano ya kimapenzi, mawasiliano madhubuti ni nguzo muhimu ya kudumisha uhusiano wenye nguvu na furaha. Uthibitisho wa upendo, hasa kwa njia ya maneno, hucheza jukumu muhimu katika kuimarisha hisia za usalama, kuridhika, na kujiamini kwa pande zote mbili zinazohusika. Nakala hii itaangalia umuhimu wa mawasiliano ya wazi na yenye ufanisi katika kudumisha upendo na kuondoa wasiwasi wowote wa kutokuwa na uhakika katika uhusiano. Tutazingatia nadharia ya Attachment Theory na Kanuni za Maslow’s Hierarchy of Needs ili kufafanua jinsi maneno ya upendo yanavyoweza kukidhi mahitaji ya kisaikolojia ya mpenzi.
Attachment Theory inasisitiza umuhimu wa usalama na uhakika katika mahusiano. Mpenzi anayepokea uthibitisho wa upendo mara kwa mara huhisi usalama na kujiamini katika uhusiano, na hivyo kupunguza wasiwasi wa kuachwa au kukataliwa. Maneno ya upendo, kama vile “nakupenda,” “nakuthamini,” au “nimefurahi kuwa na wewe,” yanaweza kutimiza haja ya usalama na kuimarisha kiambatisho chenye afya. Kwa upande mwingine, kutokuwepo kwa mawasiliano chanya kunaweza kusababisha wasiwasi na kusababisha matatizo katika uhusiano. Hii inahusishwa na kanuni ya Maslow’s Hierarchy of Needs, ambapo haja ya upendo na ushirikiano ni muhimu kwa ustawi wa kisaikolojia.
Ujumbe mfupi kama vile “Kipepeo kipeperushe kunipenda maamuz yako kamwe usijute, nakupenda mpz moyoni mwako unitulize. Nakupenda mpz,” ingawa unaonekana rahisi, unabeba uzito wa hisia kali. Utumizi wa lugha ya mfano, kama “kipepeo kipeperushe,” unaongeza uzuri na kina kwa ujumbe, ukionesha utulivu na upole wa hisia. Kurudiarudia maneno “nakupenda” kunasisitiza ukweli na nguvu ya hisia hizo. Kwa upande wa saikolojia, kurudia huku kunasaidia kuimarisha hisia hizo katika akili ya mpokeaji, na kutengeneza usalama na kuridhika.
Ili kuimarisha mahusiano, ni muhimu kuzidi kutumia lugha ya upendo kwa njia zenye ufanisi. Hii inajumuisha:
Katika uhusiano, mawasiliano ni muhimu sana kwa kudumisha uaminifu na kuridhika. Uthibitisho wa upendo kwa njia ya maneno huimarisha kiambatisho chenye afya na kukidhi mahitaji ya kisaikolojia. Utumizi wa lugha ya upendo, hata kwa njia fupi kama ujumbe wa simu, unaweza kuleta athari kubwa. Tunapendekeza kwamba wanandoa waweke muda wa mawasiliano ya wazi na yaaminifu. Kuelewa kanuni za mawasiliano yenye ufanisi, ikijumuisha kusikiliza kwa makini, kuelezea hisia kwa uwazi, na kuonyesha shukrani, kutaimarisha uhusiano. Utafiti zaidi unahitajika ili kuchunguza athari za aina mbalimbali za lugha ya upendo katika mahusiano mbalimbali, kulingana na tofauti za kitamaduni na kibinafsi. Mtazamo wa kina wa lugha ya upendo katika mazingira tofauti ya kitamaduni utaongeza uelewa wetu wa mahitaji ya kisaikolojia ya watu binafsi katika mahusiano. Hili litasaidia kubuni mikakati bora ya kuimarisha mahusiano yenye kudumu na yenye furaha.
Mungu akupe umri wa mnazi uishi mingi miaka.
Akupe thamani ya mnazi kila kitu chatumika.
Kuanzia kuti lake mpaka kwenye kidaka.
Kitale katikati yake ukila utaridhika.
Matamu na maji yake hukata kiu haraka.
Weupe watui lake lina ladha ukipika.
Kupaka mafuta yake mwili hulainika.
Na kwenye machicha yake kazi nying hufanyika.
Hata na upepo wake uvumapo utacheka.
Sikijui kitu chake kipi kisichotumika.usiku mwema
Unaweza kutuma Ujumbe huu kwa Umpendaye hapa
Usiku Ni “utulivu”
Usiku Ni “mzuri”
Usiku Ni”upole”
Usiku Ni “kimya”
Lakini Usiku
Haujakamilika
Bila..Kukutakia
Wewe..
U
S
I
K
U=m=w=e=m=a!
Recent Comments