Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMS💌💕
AckyShine

ROZARI, MATENDO NA LITANI YA MAMA BIKIRA MARIA

Featured Image

Rozari ya Bikira Maria
Mwongozo wa namna ya Kusali Rozari Takatifu ya Mama Bikira Maria




Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba ukiwa unasema “Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.





Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, “Tusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote, na tuunganishe nia hizo na nia zetu sisi wenyewe, nk).





Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu.





Mojawapo ya maneno yafuatayo huweza kutumika:
“Mungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, …… Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, …… Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, …..”





Au;





“Utuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,…. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,…. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, …..” Au;
“Salamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,….. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,….. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,……”
Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina.





Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi.
Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef.





Kisha endelea na sala zinazofuata kama mpangilio unavyoonyesha hapo juu.





Kila baada ya Tendo moja na makumi ya Salamu Maria…, “Atukuzwe..”, “Ee Yesu wangu…” na “Tuwasifu milele…” kama muda unatosha wimbo ufaao wa Bikira Maria uimbwe (kama muda ni mfupi basi angalau ubeti mmoja mmoja uimbwe kila baada ya makumi hayo). Baada ya Wimbo, Tendo linalofuata litangazwe kwa sauti pamoja na tafakari fupi au ombi linaloambatana na Tendo husika kama inavyoonyeshwa hapa chini.





MATENDO YA ROZARI TAKATIFU





MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)





Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.





Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.





Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara





Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.





Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.





MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)





Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.





Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.





Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.





Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.





Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.





MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)





Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.





Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.





Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.





Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.





Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.





MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)





Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.





Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.





Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.





Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.





Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.





LITANIA YA BIKIRA MARIA





  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utusikie
  • Kristo utusikilize




  • Mungu Baba wa Mbinguni,…… Utuhurumie
  • Mungu Mwana Mkombozi wa dunia ……… Utuhurumie
  • Mungu Roho Mtakatifu …….. Utuhurumie
  • Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja …….. Utuhurumie




  • Maria Mtakatifu ………. utuombee
  • Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
  • Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee




  • Mama wa Kristo ……… utuombee
  • Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
  • Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
  • Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
  • Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
  • Mama usiye na doa ……….. utuombee
  • Mama mpendelevu ………. utuombee
  • Mama mstajabivu ………. utuombee
  • Mama wa Muumba ………. utuombee
  • Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
  • Mama wa Kanisa……….. utuombee




  • Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
  • Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
  • Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
  • Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
  • Bikra mweye huruma ………….. utuombee
  • Bikra mwaminifu………….. utuombee




  • Kioo cha haki ………….. utuombee
  • Kikao cha hekima ………….. utuombee
  • Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
  • Chombo cha neema ………….. utuombee
  • Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
  • Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
  • Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
  • Mnara wa Daudi ………….. utuombee
  • Mnara wa pembe ………….. utuombee
  • Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
  • Sanduku la Agano ………….. utuombee




  • Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
  • Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
  • Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
  • Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
  • Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
  • Msaada wa waKristo ………….. utuombee




  • Malkia wa Malaika ………….. utuombee
  • Malkia wa Mababu ………….. utuombee
  • Malkia wa Manabii ………….. utuombee
  • Malkia wa Mitume ………….. utuombee
  • Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
  • Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
  • Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
  • Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
  • Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
  • Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
  • Malkia wa amani ………….. utuombee









  • Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusamehe ee Bwana.
  • Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusikilize ee Bwana
  • Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utuhurumie.









  • Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,…………..Tujaliwe ahadi za Kristo.




Tuombe





Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.









Karibu Vitatabu vya Kikatoliki









[products orderby="rand" columns="4" category="vitabu-vya-dini" limit="20"]
AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Esther Cheruiyot (Guest) on June 25, 2024

🙏🌟 Mbarikiwe sana

Catherine Mkumbo (Guest) on May 4, 2024

Katika imani, yote yanawezekana

David Sokoine (Guest) on April 30, 2024

Mwamini Bwana; anajua njia

Linda Karimi (Guest) on April 15, 2024

🙏🌟 Mungu akujalie amani

Mary Mrope (Guest) on April 11, 2024

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Ann Wambui (Guest) on February 19, 2024

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Lydia Mahiga (Guest) on January 18, 2024

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Thomas Mwakalindile (Guest) on January 5, 2024

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Kenneth Murithi (Guest) on December 30, 2023

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Peter Mugendi (Guest) on October 31, 2023

Rehema hushinda hukumu

Frank Macha (Guest) on October 28, 2023

Baraka kwako na familia yako.

Brian Karanja (Guest) on October 22, 2023

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Grace Njuguna (Guest) on October 13, 2023

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Tabitha Okumu (Guest) on September 1, 2023

🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha

Paul Ndomba (Guest) on August 26, 2023

Neema na amani iwe nawe.

Peter Mwambui (Guest) on July 11, 2023

🙏🌟❤️ Nakuombea heri

George Mallya (Guest) on May 29, 2023

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Lucy Kimotho (Guest) on May 18, 2023

Mungu ni mwema, wakati wote!

Moses Kipkemboi (Guest) on February 4, 2023

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Lucy Mushi (Guest) on December 9, 2022

🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe

Stephen Mushi (Guest) on October 20, 2022

🙏❤️ Mungu akubariki

Robert Okello (Guest) on September 28, 2022

🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai

Elizabeth Malima (Guest) on September 15, 2022

🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo

Esther Cheruiyot (Guest) on August 17, 2022

Nakuombea 🙏

Ruth Kibona (Guest) on August 15, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Samuel Were (Guest) on July 23, 2022

Mwamini katika mpango wake.

Josephine Nduta (Guest) on July 9, 2022

🙏💖 Nakusihi Mungu

Fredrick Mutiso (Guest) on April 21, 2022

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Joseph Kitine (Guest) on January 6, 2022

🙏✨ Mungu atakuinua

Josephine Nekesa (Guest) on December 28, 2021

Endelea kuwa na imani!

Patrick Akech (Guest) on December 2, 2021

Mungu akubariki!

Agnes Njeri (Guest) on November 23, 2021

🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako

Mary Kidata (Guest) on October 22, 2021

🙏🌟 Mungu alete amani

Ruth Wanjiku (Guest) on October 17, 2021

🙏❤️ Mungu ni mkombozi

Diana Mallya (Guest) on September 20, 2021

Sifa kwa Bwana!

Charles Mrope (Guest) on July 16, 2021

Rehema zake hudumu milele

Samuel Omondi (Guest) on June 9, 2021

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Peter Mbise (Guest) on May 27, 2021

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Stephen Kangethe (Guest) on May 2, 2021

Tumaini ni nanga ya roho

Diana Mallya (Guest) on March 21, 2021

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Anna Malela (Guest) on February 7, 2021

🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka

Violet Mumo (Guest) on December 10, 2020

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Joseph Mallya (Guest) on October 1, 2020

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Dorothy Nkya (Guest) on July 7, 2020

Dumu katika Bwana.

Grace Mligo (Guest) on July 1, 2020

🙏🙏🙏

Rose Mwinuka (Guest) on May 18, 2020

🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote

Grace Majaliwa (Guest) on April 15, 2020

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Ruth Kibona (Guest) on March 12, 2020

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Rose Waithera (Guest) on January 18, 2020

🙏❤️ Mungu ni mwaminifu

Janet Sumaye (Guest) on October 13, 2019

🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu

David Ochieng (Guest) on August 24, 2019

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Elizabeth Mrope (Guest) on August 4, 2019

Nguvu hutoka kwa Bwana

Kenneth Murithi (Guest) on June 19, 2019

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Ruth Kibona (Guest) on June 14, 2019

🙏💖💫 Mungu ni mwema

Grace Majaliwa (Guest) on June 5, 2019

🙏💖 Nakushukuru Mungu

Anna Sumari (Guest) on February 20, 2019

🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha

Francis Njeru (Guest) on January 24, 2019

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Lucy Kimotho (Guest) on December 30, 2018

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

James Malima (Guest) on October 24, 2018

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Ruth Mtangi (Guest) on October 3, 2018

Imani inaweza kusogeza milima

Related Posts

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

LITANIA YA BIKIRA MARIA MAMA WA MATESO

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie B... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo ... Read More

Sala fupi ya Asubuhi

Sala fupi ya Asubuhi

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina... Read More

NOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

NOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Inaweza kusemwa wakati wowote katika mwaka. Kwa ajili ya kujiandaa kwa Sikukuu ya Moyo Mtakatifu ... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

SALA KWA MT. YOSEFU KWA WASIO NA AJIRA WAPATE AJIRA

Ee Mt. Yosefu, tunakuomba kwa ajili ya wale asio na ajira, kwa ajili ya wale wanaotaka kujipatia ... Read More

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sal... Read More

Majitoleo ya Asubuhi

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Ni... Read More

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubw... Read More

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

SALA KWA MTAKATIFU YUDA TADEI

Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yes... Read More

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wa... Read More