
Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba ukiwa unasema “Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.
Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, “Tusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote, na tuunganishe nia hizo na nia zetu sisi wenyewe, nk).
Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu.
Mojawapo ya maneno yafuatayo huweza kutumika:
“Mungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, …… Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, …… Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, …..”
Au;
“Utuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,…. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,…. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, …..” Au;
“Salamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,….. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,….. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,……”
Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina.
Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi.
Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef.
Kisha endelea na sala zinazofuata kama mpangilio unavyoonyesha hapo juu.
Kila baada ya Tendo moja na makumi ya Salamu Maria…, “Atukuzwe..”, “Ee Yesu wangu…” na “Tuwasifu milele…” kama muda unatosha wimbo ufaao wa Bikira Maria uimbwe (kama muda ni mfupi basi angalau ubeti mmoja mmoja uimbwe kila baada ya makumi hayo). Baada ya Wimbo, Tendo linalofuata litangazwe kwa sauti pamoja na tafakari fupi au ombi linaloambatana na Tendo husika kama inavyoonyeshwa hapa chini.
MATENDO YA ROZARI TAKATIFU
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristia. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA YA BIKIRA MARIA
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Bwana utuhurumie
- Kristo utusikie
- Kristo utusikilize
- Mungu Baba wa Mbinguni,…… Utuhurumie
- Mungu Mwana Mkombozi wa dunia ……… Utuhurumie
- Mungu Roho Mtakatifu …….. Utuhurumie
- Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja …….. Utuhurumie
- Maria Mtakatifu ………. utuombee
- Mzazi Mtakatifu wa Mungu …….. utuombee
- Bikira Mtakatifu Mkuu wa Mabikira …….. utuombee
- Mama wa Kristo ……… utuombee
- Mama wa Neema ya Mungu ………….. utuombee
- Mama Mtakatifu sana ……… utuombee
- Mama mwenye usafi wa Moyo ……….. utuombee
- Mama mwenye ubikira ……….. utuombee
- Mama usiye na doa ……….. utuombee
- Mama mpendelevu ………. utuombee
- Mama mstajabivu ………. utuombee
- Mama wa Muumba ………. utuombee
- Mama wa Mkombozi ………….. utuombee
- Mama wa Kanisa……….. utuombee
- Bikira mwenye utaratibu ………….. utuombee
- Bikira mwenye heshima ………….. utuombee
- Bikira mwenye sifa ………….. utuombee
- Bikira mwenye uwezo ………….. utuombee
- Bikra mweye huruma ………….. utuombee
- Bikra mwaminifu………….. utuombee
- Kioo cha haki ………….. utuombee
- Kikao cha hekima ………….. utuombee
- Sababu ya furaha yetu ………….. utuombee
- Chombo cha neema ………….. utuombee
- Chombo cha kuheshimiwa ………….. utuombee
- Chombo bora cha ibada ………….. utuombee
- Waridi lenye fumbo ………….. utuombee
- Mnara wa Daudi ………….. utuombee
- Mnara wa pembe ………….. utuombee
- Nyumba ya dhahabu ………….. utuombee
- Sanduku la Agano ………….. utuombee
- Mlango wa Mbingu ………….. utuombee
- Nyota ya asubuhi ………….. utuombee
- Afya ya wagonjwa ………….. utuombee
- Kimbilio la wakosefu ………….. utuombee
- Mtuliza wenye huzuni ………….. utuombee
- Msaada wa waKristo ………….. utuombee
- Malkia wa Malaika ………….. utuombee
- Malkia wa Mababu ………….. utuombee
- Malkia wa Manabii ………….. utuombee
- Malkia wa Mitume ………….. utuombee
- Malkia wa Mashahidi ………….. utuombee
- Malkia wa Waungama dini ………….. utuombee
- Malkia wa Mabikira ………….. utuombee
- Malkia wa Watakatifu wote ………….. utuombee
- Malkia uliyepalizwa Mbinguni ………….. utuombee
- Malkia wa Rozari takatifu ………….. utuombee
- Malkia wa amani ………….. utuombee
- Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusamehe ee Bwana.
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utusikilize ee Bwana
- Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,…………..Utuhurumie.
- Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,…………..Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
Karibu Vitatabu vya Kikatoliki
[products orderby="rand" columns="4" category="vitabu-vya-dini" limit="20"]
Esther Cheruiyot (Guest) on June 25, 2024
🙏🌟 Mbarikiwe sana
Catherine Mkumbo (Guest) on May 4, 2024
Katika imani, yote yanawezekana
David Sokoine (Guest) on April 30, 2024
Mwamini Bwana; anajua njia
Linda Karimi (Guest) on April 15, 2024
🙏🌟 Mungu akujalie amani
Mary Mrope (Guest) on April 11, 2024
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Ann Wambui (Guest) on February 19, 2024
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Lydia Mahiga (Guest) on January 18, 2024
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Thomas Mwakalindile (Guest) on January 5, 2024
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Kenneth Murithi (Guest) on December 30, 2023
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Peter Mugendi (Guest) on October 31, 2023
Rehema hushinda hukumu
Frank Macha (Guest) on October 28, 2023
Baraka kwako na familia yako.
Brian Karanja (Guest) on October 22, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Grace Njuguna (Guest) on October 13, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tabitha Okumu (Guest) on September 1, 2023
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
Paul Ndomba (Guest) on August 26, 2023
Neema na amani iwe nawe.
Peter Mwambui (Guest) on July 11, 2023
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
George Mallya (Guest) on May 29, 2023
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Lucy Kimotho (Guest) on May 18, 2023
Mungu ni mwema, wakati wote!
Moses Kipkemboi (Guest) on February 4, 2023
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Lucy Mushi (Guest) on December 9, 2022
🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe
Stephen Mushi (Guest) on October 20, 2022
🙏❤️ Mungu akubariki
Robert Okello (Guest) on September 28, 2022
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
Elizabeth Malima (Guest) on September 15, 2022
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
Esther Cheruiyot (Guest) on August 17, 2022
Nakuombea 🙏
Ruth Kibona (Guest) on August 15, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Samuel Were (Guest) on July 23, 2022
Mwamini katika mpango wake.
Josephine Nduta (Guest) on July 9, 2022
🙏💖 Nakusihi Mungu
Fredrick Mutiso (Guest) on April 21, 2022
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Joseph Kitine (Guest) on January 6, 2022
🙏✨ Mungu atakuinua
Josephine Nekesa (Guest) on December 28, 2021
Endelea kuwa na imani!
Patrick Akech (Guest) on December 2, 2021
Mungu akubariki!
Agnes Njeri (Guest) on November 23, 2021
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
Mary Kidata (Guest) on October 22, 2021
🙏🌟 Mungu alete amani
Ruth Wanjiku (Guest) on October 17, 2021
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
Diana Mallya (Guest) on September 20, 2021
Sifa kwa Bwana!
Charles Mrope (Guest) on July 16, 2021
Rehema zake hudumu milele
Samuel Omondi (Guest) on June 9, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Peter Mbise (Guest) on May 27, 2021
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Stephen Kangethe (Guest) on May 2, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
Diana Mallya (Guest) on March 21, 2021
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Anna Malela (Guest) on February 7, 2021
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
Violet Mumo (Guest) on December 10, 2020
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Joseph Mallya (Guest) on October 1, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Dorothy Nkya (Guest) on July 7, 2020
Dumu katika Bwana.
Grace Mligo (Guest) on July 1, 2020
🙏🙏🙏
Rose Mwinuka (Guest) on May 18, 2020
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
Grace Majaliwa (Guest) on April 15, 2020
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Ruth Kibona (Guest) on March 12, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rose Waithera (Guest) on January 18, 2020
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
Janet Sumaye (Guest) on October 13, 2019
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
David Ochieng (Guest) on August 24, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Elizabeth Mrope (Guest) on August 4, 2019
Nguvu hutoka kwa Bwana
Kenneth Murithi (Guest) on June 19, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Ruth Kibona (Guest) on June 14, 2019
🙏💖💫 Mungu ni mwema
Grace Majaliwa (Guest) on June 5, 2019
🙏💖 Nakushukuru Mungu
Anna Sumari (Guest) on February 20, 2019
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha
Francis Njeru (Guest) on January 24, 2019
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Lucy Kimotho (Guest) on December 30, 2018
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
James Malima (Guest) on October 24, 2018
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Ruth Mtangi (Guest) on October 3, 2018
Imani inaweza kusogeza milima