Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.// Waniangalia sana,/ siyo kwa kunipeleleza,/ lakini kwa sababu wapenda kuniona hivi karibu na wewe,/ wafurahiwa nikija kukuabudu./ Wayasikiliza maneno yangu yote/ yenye kutoka mdomoni mwangu,/ na zaidi wapokea maneno yangu yanayotoka moyoni./ Nataka kuzungumza na wewe peke yako,/ na kusahau mambo mengine yote/ na watu wengine walioko kanisani pamoja nami./
Yesu wangu,/ nakushukuru/ kwa sababu umekubali kutupa Sakramenti hii kuu kabisa,/ ukitaka kukaa pamoja na sisi,/ na hata ukakubali kuwa chakula chetu/ chenye nguvu ya ajabu./ Mfalme wangu Yesu,/ Sultani wangu Mkuu,/ naamini kabisa kwamba upo katika Altare/ na kwamba umejificha chini ya umbo la mkate./ Ulipokuwapo bado hapa duniani mbele za watu,/ ulikuwa hujifichi kama sasa;/ lakini hata siku zile/ watu hawakuweza kukuona vile ulivyo./ Hawakuweza kuutambua Umungu wako,/ ikalazimu kukuamini tu sawa kama sisi./ Wakainama kichwa wakisema,/ βBwana wangu na Mungu wanguβ./ Na mimi kadhalika naungama/ U Bwana wangu na Mungu wangu/ na Mkombozi wangu/ na salama yangu yote./ U Yesu wangu tu,/ siwezi kusema zaidi./ Nakuabudu ee Yesu./ Najua sana, mimi ni mdogo kabisa,/ sina maana hata kidogo./ Mimi ni dhaifu na maskini mno./ Lakini Wewe katika hruuma yako kubwa/ waniita nije kwako./ Wewe huuangalii umaskini wangu,/ bali wanivuta katika mapendo yako./
Nasikia maneno yako usemayo:/ βNjooni kwangu ninyi nyote mnaoelemewa na mizigo/ nami nitawasaidiaβ./ Kwa ajili ya maneno hayo/ nakuja kwako bila hofu./ Najua kwamba wanipenda,/ najua wataka kunisaidia na kuniponya,/ najua kuwa wataka kunitakasa./
Nahitaji sana msaada wako, hakika./ Unaniona katika mwendo wangu wa kila siku,/ Jinsi ninavyohangaika na vishawishi mara nyingi;/ jinsi nilivyo na lazima ya kushindana kila siku/ nikitaka kukaa mwema na safi katika utumishi wako./ Naungama mbele yako Wewe Mkombozi wangu,/ kwamba sikukaa imara siku zote vile nilivyopaswa./ Naungama kwamba nimeshindwa mara nyingine/ na kwa hivi naomba toba./ Lakini kwa nini nimeshindwa mara nyingine?/ Kwa nini nikakosa?/ Ni kwa sababu nalikuwa nimekwenda mbali nawe;/ nalianza kujitegemea mwenyewe./ Katika majivuno yangu nikajisifu mwenyewe,/ nikajiona mwema,/ nikasahau udhaifu wangu./ Na kwa ajili hiyo nikajitia katika hatari bure,/ sikujilinda tena,/ nikampa shetani nafasi ya kunishambulia kwa hila zake zote./ Unihurumie ee Yesu wangu./
Sasa nafahamu jinsi nilivyokuwa mjinga kwelikweli./ Ndiyo maana nakuabudu kwa moyo wangu wote./ Najiweka mikononi mwako/ ufanye nami vile unavyotaka./ Wewe utanitunza;/ Wewe utanilinda vema;/ Wewe utaniongoza nijue namna ya kuepa hatari zote,/ na jinsi ya kufukuza kila kishawishi./ Chukua moyo wangu kabisa,/ kwa sababu ni mali yako kamili;/ Wewe ndiwe uliyeniumba,/ ndiwe uliyenipeleka katika Ukristo,/ nawe ndiwe utakayenihukumu siku ya mbele./ Ndivyo ninavyojitolea kwako./ Ndivyo ninavyokuabudu,/ wala sijui njia nyingine ya kukusifu zaidi./
Yesu wangu mpenzi,/ naomba upokee kwa uzuri heshima hiyo yangu./ Angalia: naitolea pamoja na heshima yote/ unayopewa daima na watakatifu wako/ na malaika wako./ Nikipiga magoti hapa mbele yako sasa,/ siko peke yangu,/ nakuabudu pamoja na Mama yako Bikira Maria,/ ambaye sala zake zinakupendeza kabisa./ Sala zangu naweka pamoja na sala zake yeye,/ uzipokee zote pamoja,/ zikupendeze zote sawa./ Ee Mama Maria!/ Nifundishe maneno ya kumsifu Mwanao Yesu vizuri./ Nipeleke kwa Yesu tumwabudu pamoja./ Nifunike na utakatifu wako/ kusudi Yesu asiangalie tena umaskini wangu/ na makosa yangu,/ aniponye katika huruma yake./
Sasa najisikia vizuri, Yesu wangu./ Sasa nina moyo wa kuweza kuendelea vema/ katika njia njema./ Sasa ninatumaini kwamba/ nitakaa mkristo mwema,/ nitakuwa mtumishi wako mwaminifu./ Nasikia amani kubwa sana moyoni mwangu,/ kwa kuwa nimo mikononi mwako./ Baada ya dakika chache/ nitaondoka tena kanisani,/ nitarudi nyumbani kwangu,/ lakini hatutaachana,/ hapana./ Mapendo yetu yatatuunganisha pamoja daima./ Wewe utanikumbuka nikiwa kazini,/ nikilala usingizi,/ nikienda njiani,/ kila mahali nilipo,/ Wewe utaniona,/ utafuatana na mimi./ Kadhalika nitakukumbuka tu./ Nitafanya bidii nisikuache kabisa./ Amina.
James Kimani (Guest) on July 12, 2024
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Henry Sokoine (Guest) on May 15, 2024
ππ Neema za Mungu zisikose
Lucy Mushi (Guest) on March 21, 2024
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Richard Mulwa (Guest) on February 27, 2024
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
David Musyoka (Guest) on December 14, 2023
Rehema zake hudumu milele
Nancy Komba (Guest) on November 13, 2023
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
David Chacha (Guest) on October 2, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Charles Wafula (Guest) on September 14, 2023
πππ
Kevin Maina (Guest) on July 11, 2023
Nakuombea π
Betty Kimaro (Guest) on July 8, 2023
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Nancy Komba (Guest) on May 21, 2023
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
Nancy Kawawa (Guest) on January 30, 2023
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Lydia Mutheu (Guest) on December 1, 2022
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Sharon Kibiru (Guest) on October 18, 2022
ππ Nakusihi Mungu
Lydia Mahiga (Guest) on September 9, 2022
Imani inaweza kusogeza milima
Agnes Sumaye (Guest) on September 2, 2022
πβ¨ Mungu atakuinua
Richard Mulwa (Guest) on September 2, 2022
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Peter Mugendi (Guest) on August 25, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Joyce Mussa (Guest) on August 16, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
George Ndungu (Guest) on August 16, 2022
Endelea kuwa na imani!
John Malisa (Guest) on August 10, 2022
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Linda Karimi (Guest) on July 16, 2022
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Ruth Mtangi (Guest) on January 8, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Betty Cheruiyot (Guest) on September 25, 2021
ππ Mungu alete amani
Lucy Mushi (Guest) on August 30, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Alice Jebet (Guest) on August 14, 2021
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Peter Tibaijuka (Guest) on August 7, 2021
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Richard Mulwa (Guest) on July 31, 2021
Dumu katika Bwana.
Thomas Mwakalindile (Guest) on May 16, 2021
Rehema hushinda hukumu
Benjamin Masanja (Guest) on May 11, 2021
Tumaini ni nanga ya roho
Anna Mahiga (Guest) on March 15, 2021
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Janet Sumaye (Guest) on February 11, 2021
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Alice Wanjiru (Guest) on November 19, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Nancy Akumu (Guest) on September 10, 2020
Baraka kwako na familia yako.
Janet Mwikali (Guest) on May 10, 2020
πβ€οΈ Mungu akubariki
Thomas Mtaki (Guest) on May 5, 2020
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Joseph Kiwanga (Guest) on May 2, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Ruth Kibona (Guest) on March 25, 2020
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Tabitha Okumu (Guest) on March 23, 2020
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Grace Majaliwa (Guest) on March 23, 2020
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
John Kamande (Guest) on March 21, 2020
πππ Mungu akufunike na upendo
Wilson Ombati (Guest) on February 25, 2020
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
Fredrick Mutiso (Guest) on February 14, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Grace Mushi (Guest) on January 19, 2020
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Grace Majaliwa (Guest) on October 9, 2019
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Violet Mumo (Guest) on August 11, 2019
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
Daniel Obura (Guest) on July 2, 2019
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Lucy Mushi (Guest) on December 29, 2018
Mwamini katika mpango wake.
Francis Mrope (Guest) on October 1, 2018
ππ Mbarikiwe sana
Irene Makena (Guest) on July 19, 2018
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rose Kiwanga (Guest) on July 4, 2018
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Irene Akoth (Guest) on June 15, 2018
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Edward Lowassa (Guest) on January 14, 2018
Katika imani, yote yanawezekana
Lydia Mzindakaya (Guest) on December 16, 2017
Amina
Linda Karimi (Guest) on December 7, 2017
ππ Mungu wetu asifiwe
Fredrick Mutiso (Guest) on November 23, 2017
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Thomas Mwakalindile (Guest) on November 20, 2017
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Miriam Mchome (Guest) on November 13, 2017
ππ Nakushukuru Mungu
Azima (Guest) on October 25, 2017
πππ
Miriam Mchome (Guest) on September 24, 2017
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike