Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

Featured Image

Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.// Waniangalia sana,/ siyo kwa kunipeleleza,/ lakini kwa sababu wapenda kuniona hivi karibu na wewe,/ wafurahiwa nikija kukuabudu./ Wayasikiliza maneno yangu yote/ yenye kutoka mdomoni mwangu,/ na zaidi wapokea maneno yangu yanayotoka moyoni./ Nataka kuzungumza na wewe peke yako,/ na kusahau mambo mengine yote/ na watu wengine walioko kanisani pamoja nami./

Yesu wangu,/ nakushukuru/ kwa sababu umekubali kutupa Sakramenti hii kuu kabisa,/ ukitaka kukaa pamoja na sisi,/ na hata ukakubali kuwa chakula chetu/ chenye nguvu ya ajabu./ Mfalme wangu Yesu,/ Sultani wangu Mkuu,/ naamini kabisa kwamba upo katika Altare/ na kwamba umejificha chini ya umbo la mkate./ Ulipokuwapo bado hapa duniani mbele za watu,/ ulikuwa hujifichi kama sasa;/ lakini hata siku zile/ watu hawakuweza kukuona vile ulivyo./ Hawakuweza kuutambua Umungu wako,/ ikalazimu kukuamini tu sawa kama sisi./ Wakainama kichwa wakisema,/ β€œBwana wangu na Mungu wangu”./ Na mimi kadhalika naungama/ U Bwana wangu na Mungu wangu/ na Mkombozi wangu/ na salama yangu yote./ U Yesu wangu tu,/ siwezi kusema zaidi./ Nakuabudu ee Yesu./ Najua sana, mimi ni mdogo kabisa,/ sina maana hata kidogo./ Mimi ni dhaifu na maskini mno./ Lakini Wewe katika hruuma yako kubwa/ waniita nije kwako./ Wewe huuangalii umaskini wangu,/ bali wanivuta katika mapendo yako./

Nasikia maneno yako usemayo:/ β€œNjooni kwangu ninyi nyote mnaoelemewa na mizigo/ nami nitawasaidia”./ Kwa ajili ya maneno hayo/ nakuja kwako bila hofu./ Najua kwamba wanipenda,/ najua wataka kunisaidia na kuniponya,/ najua kuwa wataka kunitakasa./

Nahitaji sana msaada wako, hakika./ Unaniona katika mwendo wangu wa kila siku,/ Jinsi ninavyohangaika na vishawishi mara nyingi;/ jinsi nilivyo na lazima ya kushindana kila siku/ nikitaka kukaa mwema na safi katika utumishi wako./ Naungama mbele yako Wewe Mkombozi wangu,/ kwamba sikukaa imara siku zote vile nilivyopaswa./ Naungama kwamba nimeshindwa mara nyingine/ na kwa hivi naomba toba./ Lakini kwa nini nimeshindwa mara nyingine?/ Kwa nini nikakosa?/ Ni kwa sababu nalikuwa nimekwenda mbali nawe;/ nalianza kujitegemea mwenyewe./ Katika majivuno yangu nikajisifu mwenyewe,/ nikajiona mwema,/ nikasahau udhaifu wangu./ Na kwa ajili hiyo nikajitia katika hatari bure,/ sikujilinda tena,/ nikampa shetani nafasi ya kunishambulia kwa hila zake zote./ Unihurumie ee Yesu wangu./

Sasa nafahamu jinsi nilivyokuwa mjinga kwelikweli./ Ndiyo maana nakuabudu kwa moyo wangu wote./ Najiweka mikononi mwako/ ufanye nami vile unavyotaka./ Wewe utanitunza;/ Wewe utanilinda vema;/ Wewe utaniongoza nijue namna ya kuepa hatari zote,/ na jinsi ya kufukuza kila kishawishi./ Chukua moyo wangu kabisa,/ kwa sababu ni mali yako kamili;/ Wewe ndiwe uliyeniumba,/ ndiwe uliyenipeleka katika Ukristo,/ nawe ndiwe utakayenihukumu siku ya mbele./ Ndivyo ninavyojitolea kwako./ Ndivyo ninavyokuabudu,/ wala sijui njia nyingine ya kukusifu zaidi./

Yesu wangu mpenzi,/ naomba upokee kwa uzuri heshima hiyo yangu./ Angalia: naitolea pamoja na heshima yote/ unayopewa daima na watakatifu wako/ na malaika wako./ Nikipiga magoti hapa mbele yako sasa,/ siko peke yangu,/ nakuabudu pamoja na Mama yako Bikira Maria,/ ambaye sala zake zinakupendeza kabisa./ Sala zangu naweka pamoja na sala zake yeye,/ uzipokee zote pamoja,/ zikupendeze zote sawa./ Ee Mama Maria!/ Nifundishe maneno ya kumsifu Mwanao Yesu vizuri./ Nipeleke kwa Yesu tumwabudu pamoja./ Nifunike na utakatifu wako/ kusudi Yesu asiangalie tena umaskini wangu/ na makosa yangu,/ aniponye katika huruma yake./

Sasa najisikia vizuri, Yesu wangu./ Sasa nina moyo wa kuweza kuendelea vema/ katika njia njema./ Sasa ninatumaini kwamba/ nitakaa mkristo mwema,/ nitakuwa mtumishi wako mwaminifu./ Nasikia amani kubwa sana moyoni mwangu,/ kwa kuwa nimo mikononi mwako./ Baada ya dakika chache/ nitaondoka tena kanisani,/ nitarudi nyumbani kwangu,/ lakini hatutaachana,/ hapana./ Mapendo yetu yatatuunganisha pamoja daima./ Wewe utanikumbuka nikiwa kazini,/ nikilala usingizi,/ nikienda njiani,/ kila mahali nilipo,/ Wewe utaniona,/ utafuatana na mimi./ Kadhalika nitakukumbuka tu./ Nitafanya bidii nisikuache kabisa./ Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

James Kimani (Guest) on July 12, 2024

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Henry Sokoine (Guest) on May 15, 2024

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Lucy Mushi (Guest) on March 21, 2024

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Richard Mulwa (Guest) on February 27, 2024

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

David Musyoka (Guest) on December 14, 2023

Rehema zake hudumu milele

Nancy Komba (Guest) on November 13, 2023

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

David Chacha (Guest) on October 2, 2023

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Charles Wafula (Guest) on September 14, 2023

πŸ™πŸ™πŸ™

Kevin Maina (Guest) on July 11, 2023

Nakuombea πŸ™

Betty Kimaro (Guest) on July 8, 2023

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Nancy Komba (Guest) on May 21, 2023

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Nancy Kawawa (Guest) on January 30, 2023

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Lydia Mutheu (Guest) on December 1, 2022

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Sharon Kibiru (Guest) on October 18, 2022

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Lydia Mahiga (Guest) on September 9, 2022

Imani inaweza kusogeza milima

Agnes Sumaye (Guest) on September 2, 2022

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Richard Mulwa (Guest) on September 2, 2022

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Peter Mugendi (Guest) on August 25, 2022

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Joyce Mussa (Guest) on August 16, 2022

Nguvu hutoka kwa Bwana

George Ndungu (Guest) on August 16, 2022

Endelea kuwa na imani!

John Malisa (Guest) on August 10, 2022

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Linda Karimi (Guest) on July 16, 2022

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Ruth Mtangi (Guest) on January 8, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Betty Cheruiyot (Guest) on September 25, 2021

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Lucy Mushi (Guest) on August 30, 2021

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Alice Jebet (Guest) on August 14, 2021

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Peter Tibaijuka (Guest) on August 7, 2021

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Richard Mulwa (Guest) on July 31, 2021

Dumu katika Bwana.

Thomas Mwakalindile (Guest) on May 16, 2021

Rehema hushinda hukumu

Benjamin Masanja (Guest) on May 11, 2021

Tumaini ni nanga ya roho

Anna Mahiga (Guest) on March 15, 2021

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Janet Sumaye (Guest) on February 11, 2021

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Alice Wanjiru (Guest) on November 19, 2020

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Nancy Akumu (Guest) on September 10, 2020

Baraka kwako na familia yako.

Janet Mwikali (Guest) on May 10, 2020

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Thomas Mtaki (Guest) on May 5, 2020

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Joseph Kiwanga (Guest) on May 2, 2020

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Ruth Kibona (Guest) on March 25, 2020

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Tabitha Okumu (Guest) on March 23, 2020

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Grace Majaliwa (Guest) on March 23, 2020

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

John Kamande (Guest) on March 21, 2020

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Wilson Ombati (Guest) on February 25, 2020

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Fredrick Mutiso (Guest) on February 14, 2020

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Grace Mushi (Guest) on January 19, 2020

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Grace Majaliwa (Guest) on October 9, 2019

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Violet Mumo (Guest) on August 11, 2019

πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

Daniel Obura (Guest) on July 2, 2019

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Lucy Mushi (Guest) on December 29, 2018

Mwamini katika mpango wake.

Francis Mrope (Guest) on October 1, 2018

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Irene Makena (Guest) on July 19, 2018

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Rose Kiwanga (Guest) on July 4, 2018

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Irene Akoth (Guest) on June 15, 2018

πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

Edward Lowassa (Guest) on January 14, 2018

Katika imani, yote yanawezekana

Lydia Mzindakaya (Guest) on December 16, 2017

Amina

Linda Karimi (Guest) on December 7, 2017

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

Fredrick Mutiso (Guest) on November 23, 2017

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Thomas Mwakalindile (Guest) on November 20, 2017

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Miriam Mchome (Guest) on November 13, 2017

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Azima (Guest) on October 25, 2017

πŸ™πŸ™πŸ™

Miriam Mchome (Guest) on September 24, 2017

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Related Posts

Sala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua

Sala ya Kuombea Hali njema ya hewa na mvua

Ee Mungu Mwenyezi wa milele, mpaji wa mema yote, unayetusamehe na kutulinda. Utujalie sisi tunaok... Read More

Sala ya kuomba Kifo chema

Sala ya kuomba Kifo chema

Enyi Yesu na Maria na Yosefu,

nawatolea Moyo, na roho, na uzima wangu.

Enyi Yesu na M... Read More

Majitoleo ya Asubuhi

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Ni... Read More

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

Baba yetu uliye mbinguni
Jina lako litukuzwe
Ufalme wako ufike
Utakalo lifanyikeRead More

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA MUHIMU ZA MKRISTO ZA KILA SIKU ASUBUHI

SALA YA ASUBUHI

Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu,... Read More

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli (maarufu kama novena ya Mt. Andrea)

Husaliwa kuanzia tar 30 Nov hadi usiku ... Read More

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Kumbuka ee Bikira Mwenye Rehema

Read More

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

ROZARI YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Tumia tasbihi ya kawaida yenye chembe ndogo 53.

Kwenye Msalaba Sali:

... Read More
Sala ya Medali ya Mwujiza

Sala ya Medali ya Mwujiza

Ee Bikira Maria uliyekingiwa dhambi ya asili, utuombee sisi wenye kukimbilia kwako, uwaombee na w... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE 1

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KUOMBA KUFAHAMU WITO WAKO

SALA KWA MT. YOSEFU KUOMBA KUFAHAMU WITO WAKO

Ee uliye Mkuu, Mt. Yosefu, uliyatii kabisa maongozi ya Roho Mt. Unijalie neema ya kufahamu aina y... Read More

SALAMU MARIA

SALAMU MARIA

Salamu Maria
Umejaa neema
Bwana yu nawe
Umebarikiwa kuliko wanawake wote
Na Y... Read More