Ishara ya Msalaba ni tendo la mtu kugusa paji la uso, kifua na mabega kwa kutumia mkono wa kulia na kutamka ‘Kwa Jina la Baba, na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina’.
Kugusa paji la uso tuna maana kukubali kwa akili, kugusa kifua maana yake ni kupokea na kuupenda msalaba moyoni na kugusa Mabega maana yake ni kuwa tayari kuubeba Msalaba kwa nguvu zetu zote.
Tunafanya njia ya Msalaba kwa nia ya kumkiri Mungu Mmoja katika Nafsi tatu. Pia Msalaba ni Ishara ya Ukombozi wetu.
Ishara ya Msalaba Juu ya Paji la uso, mdomo na kifua kabla ya injili:
Hii ina maana kwamba Niko tayari kulifahamu Neno la Mungu Kwa Akili yangu,
Nitalitangaza kishujaa kwa midomo yangu, na Nitalipenda na kulishika kwa Moyo wangu Wote.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Huruma ya Mungu: Msamaha na Upendo Usiokoma
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu sakramenti ya Kipaimara?
Siri ya kamba nyekundu
Usipite bila kusoma kisa hiki cha kusisimua
Ni nini imani ya Kanisa Katoliki kuhusu ngono na maadili ya kijinsia?
Huruma ya Mungu: Upendo Usiokuwa na Kifani
Mafundisho na mapokeo Katika Kanisa Katoliki yanapopatikana kwenye Biblia
Ufafanuzi wa Sala ya Baba yetu