Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli

Featured Image

Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli ni sala nzuri sana ya kumheshimu huyu Malaika Mkuu pamoja na makundi yote tisa ya Malaika. Kuendana na jinsi tunavyofunuliwa katika Maandiko Matakatifu, makundi haya tofauti tofauti ya Malaika hujipanga kuanzia karibu sana na Kiti cha Enzi alipo Mwenyezi Mungu, kwenda chini tulipo sisi wanadamu. Makundi hayo kuanzia juu kwenda chini ni Maserafi, Makerubi, Wenye Enzi, Watawala, Wenye Nguvu, Wenye Mamlaka, Wakuu, Malaika Wakuu na Malaika.

Asili ya Rozari hii ni maono aliyopata Mtumishi wa Mungu Antonia d'Astonac, ambaye alitokewa na Malaika Mkuu Mikaeli aliyemfundisha sala za Rozari hii kwa kumwelekeza kuwa anataka aheshimiwe kwa salamu tisa kufuatana na makundi tisa ya Malaika.

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu aliahidi kuwa yeyote anayefanya ibada hii kwa heshima, akaribiapo Meza Takatifu, atasindikizwa na Malaika tisa, mmoja kutoka kila kundi la Malaika. Zaidi ya hayo, kwa kusali rozari hii, aliahidi msaada wa daima, na kwamba Malaika watamsaidia mwenye kuisali duniani na kumtoa toharani akifariki, yeye pamoja na jamaa zake.

ROZARI YA MALAIKA MKUU MIKAELI


Ee Mungu unielekezee msaada, Ee Bwana unisaidie hima!
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele. Amina.

Sali Baba Yetu (mara nne) kwa heshima ya Malaika Wakuu, Mtakatifu Mikaeli, Mtakatifu Gabriel, Mtakatifu Rafaeli na Malaika Mlinzi.

1. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Mikaeli; Baba Yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike, utakalo lifanyike duniani kama mbinguni, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina
2. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Gabrieli; Baba Yetu, …..
3. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Rafaeli; Baba Yetu, …..
4. Kwa heshima ya Malaika Wangu Mlinzi; Baba Yetu, ……

Sali Baba Yetu moja na Salamu Maria tatu baada ya kila salamu katika tisa zifuatazo kwa heshima ya Makundi Tisa ya Malaika

Baba Yetu (mara moja, - tazama hapo juu)

Salamu Maria
Salamu Maria umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu, Amina.

1. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya kundi la Serafin, Bwana awashe mioyoni mwetu moto wa mapendo kamili. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

2. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Kerubin, Bwana atuwezeshe kuacha njia mbaya na kuenenda katika njia ya ukamilifu wa kiKristo. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

3. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Enzi, Bwana atujalie roho ya unyofu na unyenyekevu wa kweli. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

4. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Watawala, Bwana atujalie neema ya kushinda maasi yetu na tamaa mbaya. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

5. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Nguvu, Bwana atukinge na vishawishi na mitego ya shetani. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

6. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Mamlaka, Bwana atukinge na mwovu wala tusianguke vishawishini. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

7. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wakuu, Bwana atujalie kuwa na roho ya utii wa kweli. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

8. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Malaika Wakuu, Bwana atudumishe katika imani na katika kazi zote njema ili tujaliwe utukufu wa Milele. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

9. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Malaika, Bwana atujalie ulinzi wao duniani hapa na baadaye watuongoze kwenye furaha za Mbinguni. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)

SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU

Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kutujaza mapaji saba ya Roho Mtakatifu.

TUOMBE
Ee Mungu Mwenyezi wa milele, kwa wema na huruma yako ya ajabu, umetaka watu wako waokoke, ukamweka Malaika Mkuu Mikaeli kuwa Mkuu wa Kanisa lako, Utukinge na adui zetu, wasitusmbue saa ya kufa kwetu, bali tuongozwe naye kwenye utukufu wako Mkuu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana Wetu Yesu Kristo. Amina.

Utuombee Ee Mtukufu Mtakatifu Mikaeli Mkuu wa Kanisa la Yesu Kristo, tujaliwe ahadi za Kristo. Amina.

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya shetani, Mungu amtiishe, tunaomba sana, nawe Mkuu wa Majeshi ya Mbinguni kwa nguvu ya Mungu uwaangushe motoni shetani na pepo wabaya wengine wote, wanaozunguka duniani, ili kuzipoteza roho za watu.
Amina.

SALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI

Malaika wa Mungu Mlinzi wangu mpenzi,
Ambaye upendo wake unanifanya niwepo hapa,
Uwe nami leo hii,
Kuniangaza na kunilinda,
Kunitawala na kuniongoza.
Amina.

SALA NYINGINE KWA MALAIKA WAKO MLINZI

Ee Malaika wangu Mlinzi, uliyewekwa na Mungu Mwema, naomba unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina

Sali mara kwa mara unapokumbuka, hasa asubuhi uamkapo na usiku kabla ya kulala, Atukuzwe mara saba, kwa heshima ya Malaika wako Mlinzi.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Peter Mugendi (Guest) on June 16, 2024

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Sharon Kibiru (Guest) on June 2, 2024

πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

David Ochieng (Guest) on May 14, 2024

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Grace Mushi (Guest) on May 5, 2024

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Janet Sumari (Guest) on March 22, 2024

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Elizabeth Mrope (Guest) on March 19, 2024

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Charles Mboje (Guest) on February 19, 2024

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Lydia Wanyama (Guest) on December 5, 2023

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Paul Kamau (Guest) on October 9, 2023

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Hellen Nduta (Guest) on July 30, 2023

Katika imani, yote yanawezekana

Jane Muthui (Guest) on July 27, 2023

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Margaret Anyango (Guest) on July 16, 2023

πŸ™πŸ™πŸ™

Joseph Kawawa (Guest) on July 11, 2023

Neema ya Mungu inatosha kwako

Patrick Kidata (Guest) on June 13, 2023

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Elizabeth Mrope (Guest) on January 25, 2023

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Sharon Kibiru (Guest) on January 7, 2023

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Elizabeth Mrema (Guest) on November 22, 2022

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Joseph Mallya (Guest) on November 22, 2022

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Nicholas Wanjohi (Guest) on November 5, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Grace Mushi (Guest) on September 3, 2022

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Samson Tibaijuka (Guest) on July 13, 2022

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Dorothy Mwakalindile (Guest) on July 2, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Rose Kiwanga (Guest) on June 18, 2022

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Peter Tibaijuka (Guest) on April 4, 2022

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

George Tenga (Guest) on March 30, 2022

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Monica Lissu (Guest) on March 28, 2022

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Sarah Karani (Guest) on March 27, 2022

Mungu akubariki!

Peter Otieno (Guest) on March 9, 2022

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Anna Mahiga (Guest) on January 21, 2022

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

John Malisa (Guest) on September 12, 2021

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

Susan Wangari (Guest) on August 9, 2021

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Moses Kipkemboi (Guest) on May 26, 2021

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

John Lissu (Guest) on May 3, 2021

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Margaret Anyango (Guest) on March 8, 2021

Mungu ni mwema, wakati wote!

Janet Mbithe (Guest) on January 21, 2021

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Joseph Njoroge (Guest) on December 17, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Michael Onyango (Guest) on November 20, 2020

Sifa kwa Bwana!

Elizabeth Malima (Guest) on August 22, 2020

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Edith Cherotich (Guest) on July 29, 2020

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Lydia Mahiga (Guest) on June 16, 2020

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Frank Sokoine (Guest) on May 14, 2020

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Patrick Mutua (Guest) on April 12, 2020

Rehema zake hudumu milele

Joyce Aoko (Guest) on February 6, 2020

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Isaac Kiptoo (Guest) on January 18, 2020

Endelea kuwa na imani!

Samuel Were (Guest) on January 2, 2020

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Elizabeth Malima (Guest) on September 2, 2019

Tumaini ni nanga ya roho

Moses Kipkemboi (Guest) on May 15, 2019

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Daniel Obura (Guest) on April 1, 2019

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Sharon Kibiru (Guest) on January 5, 2019

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Vincent Mwangangi (Guest) on November 20, 2018

Nguvu hutoka kwa Bwana

Stephen Kikwete (Guest) on September 17, 2018

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Anna Sumari (Guest) on September 6, 2018

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Patrick Mutua (Guest) on July 15, 2018

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Grace Njuguna (Guest) on July 11, 2018

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Joseph Kiwanga (Guest) on July 5, 2018

Baraka kwako na familia yako.

Samuel Were (Guest) on May 24, 2018

Imani inaweza kusogeza milima

Frank Macha (Guest) on January 11, 2018

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Charles Mrope (Guest) on December 30, 2017

Dumu katika Bwana.

James Malima (Guest) on December 3, 2017

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

Chris Okello (Guest) on October 29, 2017

Mwamini katika mpango wake.

Related Posts

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Mar... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate... Read More

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji ... Read More

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

Kwa njia ya Maji haya ya Baraka,

na kwa njia ya Damu yako azizi,

na kwa maombezi ya M... Read More

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako... Read More

SALA YA IMANI

SALA YA IMANI

Mungu wangu,

nasadiki maneno yote linalosadiki na linalofundisha kanisa katoliki la Roma;Read More

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

Ee Mtakatifu Teresia wa mtoto Yesu, ulistahili kuitwa Msimamizi wa misioni katoliki za dunia yote... Read More

Majitoleo ya Asubuhi

Majitoleo ya Asubuhi

Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Ni... Read More

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA MAOMBI KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakukimbilia, ninakuja kwako katika mikono yako yenye huruma. Ndiwe ... Read More

Litani ya Bikira Maria

Litani ya Bikira Maria

  • Bwana utuhurumie
  • Bwana utuhurumie
  • Kristo utuhurumie
  • Bwana utuhurumie... Read More
AMRI ZA MUNGU

AMRI ZA MUNGU

1. NDIMI BWANA MUNGU WAKO, USIABUDU MIUNGU WENGINE.
2. USILITAJE BURE JINA LA MUNGU WAKO.Read More