Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli ni sala nzuri sana ya kumheshimu huyu Malaika Mkuu pamoja na makundi yote tisa ya Malaika. Kuendana na jinsi tunavyofunuliwa katika Maandiko Matakatifu, makundi haya tofauti tofauti ya Malaika hujipanga kuanzia karibu sana na Kiti cha Enzi alipo Mwenyezi Mungu, kwenda chini tulipo sisi wanadamu. Makundi hayo kuanzia juu kwenda chini ni Maserafi, Makerubi, Wenye Enzi, Watawala, Wenye Nguvu, Wenye Mamlaka, Wakuu, Malaika Wakuu na Malaika.
Asili ya Rozari hii ni maono aliyopata Mtumishi wa Mungu Antonia d'Astonac, ambaye alitokewa na Malaika Mkuu Mikaeli aliyemfundisha sala za Rozari hii kwa kumwelekeza kuwa anataka aheshimiwe kwa salamu tisa kufuatana na makundi tisa ya Malaika.
Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu aliahidi kuwa yeyote anayefanya ibada hii kwa heshima, akaribiapo Meza Takatifu, atasindikizwa na Malaika tisa, mmoja kutoka kila kundi la Malaika. Zaidi ya hayo, kwa kusali rozari hii, aliahidi msaada wa daima, na kwamba Malaika watamsaidia mwenye kuisali duniani na kumtoa toharani akifariki, yeye pamoja na jamaa zake.
ROZARI YA MALAIKA MKUU MIKAELI
Ee Mungu unielekezee msaada, Ee Bwana unisaidie hima!
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele. Amina.
Sali Baba Yetu (mara nne) kwa heshima ya Malaika Wakuu, Mtakatifu Mikaeli, Mtakatifu Gabriel, Mtakatifu Rafaeli na Malaika Mlinzi.
1. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Mikaeli; Baba Yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike, utakalo lifanyike duniani kama mbinguni, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina
2. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Gabrieli; Baba Yetu, β¦..
3. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Rafaeli; Baba Yetu, β¦..
4. Kwa heshima ya Malaika Wangu Mlinzi; Baba Yetu, β¦β¦
Sali Baba Yetu moja na Salamu Maria tatu baada ya kila salamu katika tisa zifuatazo kwa heshima ya Makundi Tisa ya Malaika
Baba Yetu (mara moja, - tazama hapo juu)
Salamu Maria
Salamu Maria umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu, Amina.
1. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya kundi la Serafin, Bwana awashe mioyoni mwetu moto wa mapendo kamili. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
2. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Kerubin, Bwana atuwezeshe kuacha njia mbaya na kuenenda katika njia ya ukamilifu wa kiKristo. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
3. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Enzi, Bwana atujalie roho ya unyofu na unyenyekevu wa kweli. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
4. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Watawala, Bwana atujalie neema ya kushinda maasi yetu na tamaa mbaya. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
5. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Nguvu, Bwana atukinge na vishawishi na mitego ya shetani. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
6. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Mamlaka, Bwana atukinge na mwovu wala tusianguke vishawishini. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
7. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wakuu, Bwana atujalie kuwa na roho ya utii wa kweli. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
8. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Malaika Wakuu, Bwana atudumishe katika imani na katika kazi zote njema ili tujaliwe utukufu wa Milele. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
9. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Malaika, Bwana atujalie ulinzi wao duniani hapa na baadaye watuongoze kwenye furaha za Mbinguni. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU
Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kutujaza mapaji saba ya Roho Mtakatifu.
TUOMBE
Ee Mungu Mwenyezi wa milele, kwa wema na huruma yako ya ajabu, umetaka watu wako waokoke, ukamweka Malaika Mkuu Mikaeli kuwa Mkuu wa Kanisa lako, Utukinge na adui zetu, wasitusmbue saa ya kufa kwetu, bali tuongozwe naye kwenye utukufu wako Mkuu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana Wetu Yesu Kristo. Amina.
Utuombee Ee Mtukufu Mtakatifu Mikaeli Mkuu wa Kanisa la Yesu Kristo, tujaliwe ahadi za Kristo. Amina.
SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU
Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya shetani, Mungu amtiishe, tunaomba sana, nawe Mkuu wa Majeshi ya Mbinguni kwa nguvu ya Mungu uwaangushe motoni shetani na pepo wabaya wengine wote, wanaozunguka duniani, ili kuzipoteza roho za watu.
Amina.
SALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI
Malaika wa Mungu Mlinzi wangu mpenzi,
Ambaye upendo wake unanifanya niwepo hapa,
Uwe nami leo hii,
Kuniangaza na kunilinda,
Kunitawala na kuniongoza.
Amina.
SALA NYINGINE KWA MALAIKA WAKO MLINZI
Ee Malaika wangu Mlinzi, uliyewekwa na Mungu Mwema, naomba unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina
Sali mara kwa mara unapokumbuka, hasa asubuhi uamkapo na usiku kabla ya kulala, Atukuzwe mara saba, kwa heshima ya Malaika wako Mlinzi.
Peter Mugendi (Guest) on June 16, 2024
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Sharon Kibiru (Guest) on June 2, 2024
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
David Ochieng (Guest) on May 14, 2024
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Grace Mushi (Guest) on May 5, 2024
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Janet Sumari (Guest) on March 22, 2024
ππ Mungu akujalie amani
Elizabeth Mrope (Guest) on March 19, 2024
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Charles Mboje (Guest) on February 19, 2024
πβ¨ Mungu atakuinua
Lydia Wanyama (Guest) on December 5, 2023
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Paul Kamau (Guest) on October 9, 2023
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Hellen Nduta (Guest) on July 30, 2023
Katika imani, yote yanawezekana
Jane Muthui (Guest) on July 27, 2023
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Margaret Anyango (Guest) on July 16, 2023
πππ
Joseph Kawawa (Guest) on July 11, 2023
Neema ya Mungu inatosha kwako
Patrick Kidata (Guest) on June 13, 2023
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Elizabeth Mrope (Guest) on January 25, 2023
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Sharon Kibiru (Guest) on January 7, 2023
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Elizabeth Mrema (Guest) on November 22, 2022
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Joseph Mallya (Guest) on November 22, 2022
ππ Mungu alete amani
Nicholas Wanjohi (Guest) on November 5, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Grace Mushi (Guest) on September 3, 2022
ππ Nakusihi Mungu
Samson Tibaijuka (Guest) on July 13, 2022
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Dorothy Mwakalindile (Guest) on July 2, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Rose Kiwanga (Guest) on June 18, 2022
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
Peter Tibaijuka (Guest) on April 4, 2022
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
George Tenga (Guest) on March 30, 2022
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Monica Lissu (Guest) on March 28, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Sarah Karani (Guest) on March 27, 2022
Mungu akubariki!
Peter Otieno (Guest) on March 9, 2022
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Anna Mahiga (Guest) on January 21, 2022
ππβ€οΈ Nakuombea heri
John Malisa (Guest) on September 12, 2021
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Susan Wangari (Guest) on August 9, 2021
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Moses Kipkemboi (Guest) on May 26, 2021
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
John Lissu (Guest) on May 3, 2021
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Margaret Anyango (Guest) on March 8, 2021
Mungu ni mwema, wakati wote!
Janet Mbithe (Guest) on January 21, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Joseph Njoroge (Guest) on December 17, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Michael Onyango (Guest) on November 20, 2020
Sifa kwa Bwana!
Elizabeth Malima (Guest) on August 22, 2020
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Edith Cherotich (Guest) on July 29, 2020
πππ Mungu akufunike na upendo
Lydia Mahiga (Guest) on June 16, 2020
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Frank Sokoine (Guest) on May 14, 2020
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
Patrick Mutua (Guest) on April 12, 2020
Rehema zake hudumu milele
Joyce Aoko (Guest) on February 6, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Isaac Kiptoo (Guest) on January 18, 2020
Endelea kuwa na imani!
Samuel Were (Guest) on January 2, 2020
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Elizabeth Malima (Guest) on September 2, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
Moses Kipkemboi (Guest) on May 15, 2019
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Daniel Obura (Guest) on April 1, 2019
ππ Nakushukuru Mungu
Sharon Kibiru (Guest) on January 5, 2019
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Vincent Mwangangi (Guest) on November 20, 2018
Nguvu hutoka kwa Bwana
Stephen Kikwete (Guest) on September 17, 2018
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Anna Sumari (Guest) on September 6, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Patrick Mutua (Guest) on July 15, 2018
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Grace Njuguna (Guest) on July 11, 2018
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Joseph Kiwanga (Guest) on July 5, 2018
Baraka kwako na familia yako.
Samuel Were (Guest) on May 24, 2018
Imani inaweza kusogeza milima
Frank Macha (Guest) on January 11, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Charles Mrope (Guest) on December 30, 2017
Dumu katika Bwana.
James Malima (Guest) on December 3, 2017
ππ Mungu wetu asifiwe
Chris Okello (Guest) on October 29, 2017
Mwamini katika mpango wake.