Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.
SALA YA KUSHUKURU
Tunakushukuru, ee Mungu, kwa mapaji uliyotujalia leo. Amina.
Baba yetu β¦
Salamu Maria β¦
SALA YA IMANI
Mungu wangu, nasadiki maneno yote. Linayosadiki na linayofundisha Kanisa Katoliki la Roma. Kwani ndiwe uliyetufumbulia hayo. Wala hudanganyiki, wala hudanganyi. Amina.
SALA YA MATUMAINI
Mungu wangu, natumaini kwako, nitapewa kwa njia ya Yesu Kristo. Neema zako hapa duniani, na utukufu mbinguni. Kwani ndiwe uliye agana hayo nasi, nawe mwamini. Amina.
SALA YA MAPENDO
Mungu wangu, nakupenda zaidi ya chochote. Kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza. Nampenda na jirani yangu, kama nafsi yangu, kwa ajili yako. Amina.
KUTUBU DHAMBI
Tuwaze katika moyo wetu makosa ya leo tuliyomkosea Mungu kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo na kwa kutotimiza wajibu. (Husubiri kidogo ).
Nakuungamia Mungu Mwenyezi, nanyi ndugu zangu, kwani nimekosa mno, kwa mawazo, kwa maneno, kwa vitendo, na kwa kutotimiza wajibu.
Nimekosa mimi, nimekosa mimi, nimekosa sana. Ndiyo maana nakuomba Maria mwenye heri, Bikira daima, Malaika na Watakatifu wote, nanyi ndugu zangu, niombeeni kwa Bwana Mungu wetu.
Mungu Mwenyezi atuhurumie, atusamehe dhambi zetu, atufikishe kwenye uzima wa milele. Amina.
SALA YA KUWAOMBEA WATU
Ee Mungu, nawaombea watu wa nchi hii, wapate kusikia maneno yako na kukupenda wewe Bwana Mungu wetu.
SALA KWA MALAIKA MLINZI
Malaika mlinzi wangu, unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina.
MALAIKA WA BWANA
(kipindi kisicho cha Pasaka)
Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria.
Naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu.
Salamu, Maria,β¦..
Ndimi mtumishi wa Bwana.
Nitendewe ulivyonena.
Salamu, Mariaβ¦.
Neno la Mungu akatwaa mwili.
Akakaa kwetu.
Salamu, Mariaβ¦.
Utuombee, Mzazi mtakatifu wa Mungu.
Tujaliwe ahadi za Kristu.
Tuombe:
Tunakuomba, Ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika kwamba Mwanao amejifanya Mtu kwa mateso na msalaba wake tufikishwe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. AMINA.
AU;
MALKIA WA MBINGU (kipindi cha Pasaka)
Malkia wa mbingu, furahi, aleluya.
Kwani uliyestahili kumchukua, Aleluya.
Amefufuka alivyosema, Aleluya.
Utuombee kwa Mungu, Aleluya.
Furahi shangilia, ee Bikira Maria, Alaluya.
Kwani hakika Bwana amefufuka Aleluya.
Tuombe.
Ee Mungu, uliyependa kuifurahisha dunia kwa kufufuka kwake Bwana wetu Yesu Kristu, Mwanao, fanyiza, twakuomba, kwa ajili ya Bikira Maria, tupate nasi furaha za uzima wa milele. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristu Bwana wetu. Amina.
ATUKUZWE (mara tatu)
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu. Kama mwanzo na sasa na siku zote na milele. Amina.
KUJIKABIDHI
Enyi Yesu, Maria na Yosefu nawatolea moyo na roho na uzima wangu!
Enyi Yesu, Maria na Yosefu mnijilie saa ya kufa kwangu!
Enyi Yesu, Maria na Yosefu mnijalie nife mikononi mwenu!
(Rehema ya siku 300).
WIMBO:
Kwa heri Yesu mpenzi mwema,
Naenda usiudhike mno.
Nakushukuru, nakupenda,
Kwa hizo nyimbo za mwisho.
Asubuhi nitarudi.
Yesu kwa heri.
Kwa heri Mama mtakatifu,
Sasa napita pumzika.
Asante kwa moyo na nguvu,
Leo umeniombea.
Asubuhi nitarudi.
Mama kwa heri.
Kwa heri Yosefu mnyenyekevu,
Kazi zatimilizika.
Kama mchana, leo usiku,
Nisimamie salama.
Asubuhi nitarudi.
Yosefu kwa heri.
Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu. Amina.
KUOMBA ULINZI WA USIKU
Mungu wangu naenda kulala naomba malaika 14, waende nami, wawili juu, wawili chini, wawili upande wa kuume, wawili upande wa kushoto, wawili wanifunike, wawili waniamshe, wawili wanipeleke juu mbinguni. Mimi mtoto mdogo, roho yangu ni ndogo, haina nafasi kwa mtu yoyote ila kwa Yesu pekee. Amina.
Dumu katika Bwana.
dua
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Rehema hushinda hukumu
Endelea kuwa na imani!
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Baraka kwako na familia yako.
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πβ€οΈ Mungu akubariki
Mwamini Bwana; anajua njia
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Nguvu hutoka kwa Bwana
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
ππ Nakusihi Mungu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
ππ Neema za Mungu zisikose
Neema na amani iwe nawe.
πβ¨ Mungu atakuinua
ππ Mungu alete amani
Nakuombea π
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Neema ya Mungu inatosha kwako
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πππ
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Mungu ni mwema, wakati wote!
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
Mungu akubariki!
ππ Mungu akujalie amani
Tembea kwa imani, si kwa kuona
ππ Mbarikiwe sana
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Katika imani, yote yanawezekana
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
ππ Nakushukuru Mungu
Imani inaweza kusogeza milima
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Sifa kwa Bwana!
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πππ
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mwamini katika mpango wake.
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Tumaini ni nanga ya roho
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πππ« Mungu ni mwema
Amina
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Rehema zake hudumu milele
πππ Mungu akufunike na upendo
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
ππ Mungu wetu asifiwe
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe