Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye siku zote hutupatia malezi bora kwa ajili ya wokovu wetu. Kanisa halichoki kutuhimiza tutafakari na kuishi utakatifu wa familia ya Nazareti ya Yesu, Maria na Yosefu. Familia hii iliishi upendo uliojengwa kwa fadhila za imani, uaminifu, utii, uvumilivu na upole hata wakawa watakatifu. Tunapoadhimisha mwaka wa Familia, tunaiweka mbele yetu familia ya Nazareti iwe dira, baraka na mfano kwa familia zetu.
Tunakushukuru Baba kwa ajili ya familia zote zinazojitahidi kuishi fadhila hizo za Familia takatifu na tunakuomba uzidi kuwaimarisha wanandoa ili tupate kwao mifano mingi na bora ya kuigwa. Ee Bwana, tunaomba Roho Mtakatifu atuangazie tuweze: kutambua familia kuwa Kanisa la nyumbani na shule ya imani na upendo; kuimarisha familia kwa sala, sakramenti na tunu za kiinjili na kushirikiana kwa heshima katika familia kwa usitawi wa roho na wa mwili kwa wanafamilia wote.
Tunaziombea familia zetu na Jumuiya Ndogondogo za Kikristo ziwe bustani bora na salama za kuchipusha na kulea miito mitakatifu ya Ndoa, Utawa na Upadre. Tunawaombea vijana na watoto wetu Uchaji wa Mungu ili wawe na bidii ya kujitunza kwa kushika amri za Mungu na kuishi fadhila za kiinjili, wawe na roho ya kimisionari yaani walipende Kanisa na kuwa na moyo wa kueneza ufalme wako kwa matendo ya imani. Baba wa huruma, tunakukabidhi familia zenye misukosuko ya mafarakano, ulevi, ubinafsi, uregevu-dini, uvivu, ushirikina, hofu, magonjwa sugu na mengineyo yenye kuleta huzuni; kwa hisani yako uwape neema, mwanga na nguvu za kuanza maisha mapya yenye amani, waweze kufurahia upatanisho na uponyi wa pendo lako la kibaba kati yao.
Tunaomba toba na msamaha kwa ukatili, manyanyaso na hata mauaji katika familia zetu na uwaponye wote waliojeruhiwa kwa maneno, matendo na makwazo ya aina yeyote. Aidha tunakuomba uwe kitulizo na faraja kwa wagonjwa na wazee, pia tegemeo la yatima na wajane. Wenye matatizo ya kiafya au ya kijamii wasikate tamaa bali waunganishe hali zao na msalaba wa Mwanao na kukutumaini wewe Mweza yote. Jamii iwajibike nao kwa kuzijali haki zao na kuwapa misaada wanayohitaji.
Tunakuomba ubariki miradi na kazi zetu ili familia zipate usitawi na maendeleo; na utujalie hekima ya kukushukuru kwa maisha ya haki, amani na ukarimu na mwisho tukaimbe sifa zako pamoja na familia Takatifu ya Yesu, Maria na Yosefuna jeshi lote la mbinguni. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu. Amina.
Baba yetuβ¦ β¦..Salamu Mariaβ¦.β¦Atukuzwe Babaβ¦β¦β¦
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
ππβ€οΈ Nakuombea heri
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
Dumu katika Bwana.
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Nakuombea π
Neema ya Mungu inatosha kwako
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Tumaini ni nanga ya roho
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Endelea kuwa na imani!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mungu akubariki!
Neema na amani iwe nawe.
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
ππ Mungu akujalie amani
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Nguvu hutoka kwa Bwana
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
ππ Mbarikiwe sana
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Amina
Mungu ni mwema, wakati wote!
πππ Mungu akufunike na upendo
Rehema hushinda hukumu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Mwamini katika mpango wake.
πππ« Mungu ni mwema
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πβ¨ Mungu atakuinua
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Katika imani, yote yanawezekana
ππ Nakusihi Mungu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
ππ Mungu wetu asifiwe
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
Mwamini Bwana; anajua njia
πβ€οΈ Mungu akubariki
ππ Mungu alete amani
Rehema zake hudumu milele
πππ
Sifa kwa Bwana!
Imani inaweza kusogeza milima
ππ Neema za Mungu zisikose
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πππ
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
ππ Nakushukuru Mungu
Baraka kwako na familia yako.
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha