Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili yangu,/ nashindwa kuelewa./ Unaficha Ukuu wako usiofahamika/ na kujidhihirisha kwa ajili yangu mimi mnyonge./ Ee Mfalme wa utukufu,/ unaficha uzuri wako,/ lakini jicho la moyo wangu/ linapenya pazia na kuona Majeshi ya Malaika/ wakikuimbia kwa heshima bila kukoma/ na nguvu zote mbinguni zikikusifu bila mwisho zikisema:/ βMtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu..β/
Ni nani awezaye kufahamu Upendo wako/ na huruma yako isiyo na kipimo kwa ajili yetu!/ Ee Mfungwa wa Upendo,/ nafungia moyo wangu masikini/ kwenye Tabarnakulo hii/ ili niweze kukuabudu usiku na mchana bila mwisho./ Najua hakuna kizuizi/ na hata kama naonekana kukaa mbali,/ lakini moyo wangu u pamoja nawe/ katika ibada hii./ Hakuna kinachoweza kuzuia upendo wangu kwako./ Kwangu hakuna kizuizi chochote./
Ee Utatu Mtakatifu,/ Mungu Mmoja usiyegawanyika,/ utukuzwe kwa zawadi yako hii kuu/ na agano hili la huruma!/
Nakuabudu,/ Bwana na Muumba uliyefichika katika Sakramenti Takatifu!/ Ee Bwana,/ nakuabudu kwa kazi zote za mikono yako/ zinazonifunulia Hekima yako kuu,/ Wema wako na Huruma yako kuu./ Uzuri uliousambaza hapa/ Uzuri ulio nao Wewe mwenyewe/ ambaye U Uzuri usioelezeka;/ na ingawaje umejificha na kusitiri uzuri wako,/ jicho langu,/ kwa mwanga wa imani linafika kwako,/ na roho yangu inapata kumtambua Muumba wake/ aliye Uzuri usiopimika,/ ulio juu ya kila uzuri,/ na moyo wangu unazama kabisa katika sala ya kukuabudu./
Bwana wangu na Muumba wangu,/ wema wako wanitia moyo wa kuongea nawe,/ Huruma yako huondoa kiambaza/ kitenganishacho Muumba na kiumbe./ Furaha ya moyo wangu,/ ee Mungu, ni kuongea na Wewe./ Yote ambayo moyo wangu unayatamni nayapata kwako./ Hapa ndipo mwanga wako unaponiangaza akili yangu/ na kuiwezesha kukujua Wewe zaidi na zaidi/ β ndipo mikondo ya neema inapoutiririkia moyo wangu,/ ndipo roho yangu inapochota uzima wa milele./ Ee Bwana na Muumba wangu,/ licha ya mapaji yote haya,/ unajitoa mwenyewe kwangu,/ ili uweze kujiunganisha na kiumbe dhaifu na maskini./
Ee Kristu,/ nafurahi sana nionapo kwamba unapendwa/ na kwamba sifa na utukufu wako vinaongezwa/ hasa ya Huruma yako./ Ee Kristu,/ sitaacha kamwe kuutukuza wema wako na huruma yako,/ hadi dakika ya mwisho ya maisha yangu./ Kwa kila tone la damu yangu/ na kwa kila pigo la moyo wangu/ naitukuza Huruma yako./ Natamani kugeuzwa kabisa/ na kuwa utenzi wa utukufu wako./ Naomba siku ya kufa kwangu/ popote nitakapokuwa nimelala,/ pigo la mwisho la moyo wangu/ liwe utenzi mpendevu/ usifuo Huruma yako isiyo na kipimo./ Amina
(Na Mt. Faustina Kowalska).
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Baraka kwako na familia yako.
πβ€οΈ Mungu akubariki
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Mwamini Bwana; anajua njia
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema hushinda hukumu
Tumaini ni nanga ya roho
Dumu katika Bwana.
Imani inaweza kusogeza milima
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Neema na amani iwe nawe.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
πβ¨ Mungu atakuinua
ππ Nakusihi Mungu
ππ Mungu akujalie amani
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mungu akubariki!
πππ
ππ Nakushukuru Mungu
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Rehema zake hudumu milele
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
πππ« Mungu ni mwema
Amina
ππ Mungu alete amani
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
πππ Mungu akufunike na upendo
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Katika imani, yote yanawezekana
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Nguvu hutoka kwa Bwana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
ππ Asante kwa neema zako Mungu
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
ππβ€οΈ Nakuombea heri
ππ Mbarikiwe sana
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Endelea kuwa na imani!
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Mwamini katika mpango wake.
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Kwa Mungu, yote yanawezekana
ππ Neema za Mungu zisikose
ππ Mungu wetu asifiwe
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
πππ
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Sifa kwa Bwana!
Nakuombea π
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe