Rozari ya Malaika Mkuu Mikaeli ni sala nzuri sana ya kumheshimu huyu Malaika Mkuu pamoja na makundi yote tisa ya Malaika. Kuendana na jinsi tunavyofunuliwa katika Maandiko Matakatifu, makundi haya tofauti tofauti ya Malaika hujipanga kuanzia karibu sana na Kiti cha Enzi alipo Mwenyezi Mungu, kwenda chini tulipo sisi wanadamu. Makundi hayo kuanzia juu kwenda chini ni Maserafi, Makerubi, Wenye Enzi, Watawala, Wenye Nguvu, Wenye Mamlaka, Wakuu, Malaika Wakuu na Malaika.
Asili ya Rozari hii ni maono aliyopata Mtumishi wa Mungu Antonia d’Astonac, ambaye alitokewa na Malaika Mkuu Mikaeli aliyemfundisha sala za Rozari hii kwa kumwelekeza kuwa anataka aheshimiwe kwa salamu tisa kufuatana na makundi tisa ya Malaika.
Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu aliahidi kuwa yeyote anayefanya ibada hii kwa heshima, akaribiapo Meza Takatifu, atasindikizwa na Malaika tisa, mmoja kutoka kila kundi la Malaika. Zaidi ya hayo, kwa kusali rozari hii, aliahidi msaada wa daima, na kwamba Malaika watamsaidia mwenye kuisali duniani na kumtoa toharani akifariki, yeye pamoja na jamaa zake.
ROZARI YA MALAIKA MKUU MIKAELI
Ee Mungu unielekezee msaada, Ee Bwana unisaidie hima!
Atukuzwe Baba na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele. Amina.
Sali Baba Yetu (mara nne) kwa heshima ya Malaika Wakuu, Mtakatifu Mikaeli, Mtakatifu Gabriel, Mtakatifu Rafaeli na Malaika Mlinzi.
1. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Mikaeli; Baba Yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, ufalme wako ufike, utakalo lifanyike duniani kama mbinguni, utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina
2. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Gabrieli; Baba Yetu, β¦..
3. Kwa heshima ya Malaika Mkuu Mtakatifu Rafaeli; Baba Yetu, β¦..
4. Kwa heshima ya Malaika Wangu Mlinzi; Baba Yetu, β¦β¦
Sali Baba Yetu moja na Salamu Maria tatu baada ya kila salamu katika tisa zifuatazo kwa heshima ya Makundi Tisa ya Malaika
Baba Yetu (mara moja, – tazama hapo juu)
Salamu Maria
Salamu Maria umejaa neema, Bwana yu nawe, umebarikiwa kuliko wanawake wote, na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu, Amina.
1. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya kundi la Serafin, Bwana awashe mioyoni mwetu moto wa mapendo kamili. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
2. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Kerubin, Bwana atuwezeshe kuacha njia mbaya na kuenenda katika njia ya ukamilifu wa kiKristo. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
3. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Enzi, Bwana atujalie roho ya unyofu na unyenyekevu wa kweli. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
4. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Watawala, Bwana atujalie neema ya kushinda maasi yetu na tamaa mbaya. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
5. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Nguvu, Bwana atukinge na vishawishi na mitego ya shetani. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
6. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wenye Mamlaka, Bwana atukinge na mwovu wala tusianguke vishawishini. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
7. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Wakuu, Bwana atujalie kuwa na roho ya utii wa kweli. Amina
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
8. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Malaika Wakuu, Bwana atudumishe katika imani na katika kazi zote njema ili tujaliwe utukufu wa Milele. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
9. Kwa maombezi ya Mtakatifu Mikaeli na ya Kundi la Malaika, Bwana atujalie ulinzi wao duniani hapa na baadaye watuongoze kwenye furaha za Mbinguni. Amina.
Baba Yetu (mara moja), Salamu Maria (mara tatu)
SALA MBELE YA KITI CHA ENZI CHA MUNGU
Sali Atukuzwe 7 kwa heshima ya Malaika 7 wateule ujipatie neema ya kuepa dhambi mbaya saba na kutujaza mapaji saba ya Roho Mtakatifu.
TUOMBE
Ee Mungu Mwenyezi wa milele, kwa wema na huruma yako ya ajabu, umetaka watu wako waokoke, ukamweka Malaika Mkuu Mikaeli kuwa Mkuu wa Kanisa lako, Utukinge na adui zetu, wasitusmbue saa ya kufa kwetu, bali tuongozwe naye kwenye utukufu wako Mkuu. Tunaomba hayo kwa njia ya Bwana Wetu Yesu Kristo. Amina.
Utuombee Ee Mtukufu Mtakatifu Mikaeli Mkuu wa Kanisa la Yesu Kristo, tujaliwe ahadi za Kristo. Amina.
SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU
Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya shetani, Mungu amtiishe, tunaomba sana, nawe Mkuu wa Majeshi ya Mbinguni kwa nguvu ya Mungu uwaangushe motoni shetani na pepo wabaya wengine wote, wanaozunguka duniani, ili kuzipoteza roho za watu.
Amina.
SALA KWA MALAIKA WAKO MLINZI
Malaika wa Mungu Mlinzi wangu mpenzi,
Ambaye upendo wake unanifanya niwepo hapa,
Uwe nami leo hii,
Kuniangaza na kunilinda,
Kunitawala na kuniongoza.
Amina.
SALA NYINGINE KWA MALAIKA WAKO MLINZI
Ee Malaika wangu Mlinzi, uliyewekwa na Mungu Mwema, naomba unilinde katika hatari zote za roho na za mwili. Amina
Sali mara kwa mara unapokumbuka, hasa asubuhi uamkapo na usiku kabla ya kulala, Atukuzwe mara saba, kwa heshima ya Malaika wako Mlinzi.
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
ππ Mungu akujalie amani
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
πβ¨ Mungu atakuinua
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Katika imani, yote yanawezekana
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
πππ
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
ππ Mungu alete amani
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
ππ Nakusihi Mungu
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Mungu akubariki!
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
ππβ€οΈ Nakuombea heri
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Mungu ni mwema, wakati wote!
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Sifa kwa Bwana!
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
πππ Mungu akufunike na upendo
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
Rehema zake hudumu milele
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Endelea kuwa na imani!
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Tumaini ni nanga ya roho
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
ππ Nakushukuru Mungu
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Nguvu hutoka kwa Bwana
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Wakati wa Mungu ni kamilifu
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Baraka kwako na familia yako.
Imani inaweza kusogeza milima
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Dumu katika Bwana.
ππ Mungu wetu asifiwe
Mwamini katika mpango wake.
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Neema na amani iwe nawe.
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Rehema hushinda hukumu
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πβ€οΈ Mungu akubariki
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Nakuombea π
Mwamini Bwana; anajua njia
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Amina
πππ« Mungu ni mwema
πππ
ππ Mbarikiwe sana
ππ Neema za Mungu zisikose