Mahitaji
Mchele – 2 Mugs
Viazi – 3
Nyama ya Kusaga – 1 Pound
Mboga mchanganyiko za barafu – 1 Mug
(Frozen vegetable)
Kitunguu saumu(thomu/galic) na tangawizi – 2 vijiko vya supu
Garam masala – 1 kijiko cha supu
Nyanya – 1
Kitungu maji – 1
Mdalasini nzima – 1 vijiti
Karafuu – 3 chembe
Pilipili mbichi – 1
Chumvi – kiasi
Maji – 2 Β½ Mugs
Mafuta – 3 vijiko vya supu
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
Osha mchele na uroweke kiasi kutegemea aina ya mchele.
Katakata viazi kaanga katika mafuta, toa weka kando.
Tia mafuta katika sufuria, kaanga kitunguu maji mpaka kigeuke rangi ya hudhurungi (brown).
Tia nyama ya kusaga, thomu na tangawizi, pilipili, bizari zote na chumvi. Kaanga hadi nyama iwive.
Katakata nyanya uliyokatakata itie katika mchanganyiko wa nyama na endelea kukaanga kidogo tu.
Tia mboga ya barafu (frozen vegetables)
Tia maji, kidonge cha supu.
Yatakapochemka tia mchele.
Punguza moto uwe mdogo funika kwa muda wa Β½ saa hadi wali ukauke na uwive. Utakuwa tayari kuliwa.
Editor: Melkisedeck Leon Shine. About Me | Contact Me | LinkedIn | TikTok | WhatsApp
Read and Write Comments
Recommended Posts
Vitafunio 10 vya Afya kwa Kusaidia Zoezi lako la Mazoezi
Jinsi ya kupika Wali Wa Kichina wa mboga mboga Na Mayai
Jinsi ya kupika vizuri Wali Wa Karoti Na Nyama
Mapishi ya Wali Wa Nazi Wa Adesi, Bamia Na Mchuzi Wa Kamba
Mapishi ya Ugali Kwa Mchuzi Wa Samaki Wa Kuchoma
Mapishi ya Sambusa za nyama
Jinsi ya kuandaa Pilau ya sosi ya soya, nyama na mboga
Nguvu ya Nafaka Zote: Chaguzi za Upishi Zenye Afya