Mahitaji
Mchele wa basmati – 4 cups
Samaki nguru (king fish) – 7 vipande au zaidi
Kitunguu – 5
Nyanya/tungule – 3
Njegere – 1 kikombe
Snuwbar (njugu za pine) – 1 kikombe
Viazi – 2 kata kata mapande makubwa
Tangawizi mbichi – 1 kijiko cha supu
Kitunguu saumu – 1 kijiko cha supu
Pilipili nyekundu – 1 kijiko cha chai
Bizari ya biriani/garama masala – 1 kijiko cha supu
Namna Ya Kupika:
Kaanga samaki mbali kwa viungo upendavyo umkoleze vizuri. Au choma (bake/grill) katika oveni ukipenda.
Weka mafuta katika sufuria, tia vitunguu kaanga hadi vigeuka rangi. Gawa sehemu mbili.
Sehemu moja bakisha katika sufuria kisha tia tangawizi mbichi na kitunguu thomu ukaange.
Tia nyanya kaanga kisha tia bizari zote endelea kukaanga, tia njegere, njugu za snuwbar na ndimu kavu.
Tia viazi ulivyokwishakaanga, na vitunguu vilobakia.
Tia mapande ya samaki, changanya na masala bila ya kumvuruga samaki.
Chemsha wali kisha mwagia juu yake, funika upike ndani ya oveni au mkaa hadi wali uive kama unavyopika kawaida ya biriani.
Epua pakua huku ukichanganya na masala ya samaki.
References:
Google ScholarResearchGate
Semantic Scholar
AckySHINE