Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA ZA IBADA KWA BIKIRA MARIA WA MATESO

Featured Image

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria saba kwa kila teso.

TESO LA KWANZA

Mzee Simeoni aliagua kuwa Moyo wa Mama Maria utachomwa kwa upanga.
Tuombe neema ya kuvumilia mateso.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA PILI

Maria na Yosefu walikimbilia Misri usiku ili kumficha Mtoto Yesu asiuawe na Herodi.
Tuombe neema ili miili yetu iwe kimbilio lake Yesu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA TATU

Mama Maria aliona uchungu sana Mtoto Yesu alipopotea kwa siku tatu.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu mioyoni mwetu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA NNE

Mama Maria aliona uchungu sana alipokutana na Mwanae Yesu katika njia ya Msalaba.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu siku zote.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA TANO

Mama Maria aliona uchungu sana alipomwona Mwanae Yesu akisulibiwa Msalabani.
Tuombe neema ya kufa mikononi mwa Yesu na Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA SITA

Mama Maria aliona uchungu sana alipopakata maiti ya Mwanae Yesu baada ya kushushwa Msalabani.
Tuombe neema ya kutotenda dhambi.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

TESO LA SABA

Mama Maria aliona uchungu sana aliporudi nyumbani baada ya kumzika Mwanae Yesu
Tuombe neema ya kitulizo kwa Mama Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu ……… Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba ……
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.

LITANIA YA MAMA WA MATESO

Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, - Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,

Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie – Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie – Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu ….
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubwa sana ulipotazama mateso na kifo cha Mwana wako mpenzi. Muda ule uliweza kutuliz kidogo kwa sababu ya kumwona angali hai. Lakini je, baada ya kufa na kumzika? Sasa wewe ni mkiwa mkubwa mno! Uh, ukiwa wa pekee, uniombee mimi ninayempoteza mara nyingi kwa dhambi zangu. Unijalie nisimpoteze tena Yesu wangu kwa ubaya wa uvivu wangu, bali nimtumikie kiaminifu duniani hapa ili nimwone na kumfurahia milele mbinguni. Amina.

SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI

Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkingaji na mteteaji wangu. Naweka roho fukara katika moyo wako uliotobolewa na panga nyingi za mateso. Unipokee mimi niwe mtumishi wako wa pekee na mshiriki wa mateso yako. Nijalie nguvu niwe daima karibu na msalaba ule alikosulibiwa Yesu. Nakutolea nafsi yangu na mali yangu yote. Pokea kila tendo langu jema ukalisindikize kwa Mwanao, Mama, nifanye nistahili kuitwa mtumishi wa Maria, Simama karibu yangu katika matendo yangu yote ili yafanwe kwa sifa ya Mungu. Ulivyosimama karibu kabisa ya Mwanao alipokufa msalabani uwe karibu nami saa ya kufa kwangu. Nijalie niweze kutaja jina lako na la Mwana wako nikisema: β€œYesu, Maria na Yosef mnisaidie saa ya kufa kwangu. Yesu, maria na Yosef, naomba nife kwa amani kati yenu!” . Amina.

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na uliyemtazama Mwana wako akifa, unitazame kwa huruma ya kimama ninayekusikitikia. Kwa sababu ya upanga uliochoma moyo wako, kwa mateso ya maisha yako nakuomba uniangalie kwa wema ukasikilize maombi yangu. Nakuomba, ee Mama, uniombee daima kwa Mwana wako, najua hawezi kukuvyima wewe kitu chochote. Basi, ufanye, Moyo wa Mwanao ukubali kunijalia ombi langu hili …………………(taja ombi lako).
Maana nitamkimbilia nani katika mahitaji na misiba yangu isipokuwa kwako, ee Mama wa huruma? Wewe hasa unaweza kutusaidia sisi tulio bado katika bonde la machozi kwa sababu ulishiriki mateso ya Mwanao kutukomboa. Umtolee Yesu tone moja la Damu yake takatifu. Umkumbushe ya kuwa wewe ni matumaini, furaha na maisha yetu ukanipatie jambo ninalokuomba kwa Yesu Kristo, bwana wetu. Amina.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Charles Wafula (Guest) on July 15, 2024

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Nancy Kabura (Guest) on July 11, 2024

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Alice Mwikali (Guest) on May 24, 2024

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Ruth Mtangi (Guest) on May 14, 2024

πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

Esther Cheruiyot (Guest) on February 16, 2024

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Francis Mtangi (Guest) on January 18, 2024

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Anna Kibwana (Guest) on September 28, 2023

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Martin Otieno (Guest) on July 23, 2023

Nguvu hutoka kwa Bwana

Joy Wacera (Guest) on June 22, 2023

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Rose Lowassa (Guest) on May 1, 2023

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Charles Mchome (Guest) on March 13, 2023

Mungu akubariki!

Grace Njuguna (Guest) on November 16, 2022

Mwamini Bwana; anajua njia

Stephen Kangethe (Guest) on October 31, 2022

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Stephen Malecela (Guest) on October 12, 2022

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Mary Njeri (Guest) on August 25, 2022

Endelea kuwa na imani!

Miriam Mchome (Guest) on August 24, 2022

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Robert Okello (Guest) on July 21, 2022

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Ruth Kibona (Guest) on July 13, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Ruth Mtangi (Guest) on July 8, 2022

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Mariam Hassan (Guest) on July 2, 2022

Baraka kwako na familia yako.

Dorothy Mwakalindile (Guest) on June 23, 2022

Nakuombea πŸ™

Patrick Akech (Guest) on June 12, 2022

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Lucy Mahiga (Guest) on June 2, 2022

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Wilson Ombati (Guest) on May 27, 2022

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Tabitha Okumu (Guest) on April 21, 2022

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Samson Mahiga (Guest) on April 11, 2022

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Frank Macha (Guest) on April 11, 2022

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Sarah Mbise (Guest) on March 29, 2022

Amina

Nancy Akumu (Guest) on March 17, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Irene Akoth (Guest) on March 3, 2022

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

David Chacha (Guest) on February 13, 2022

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Thomas Mtaki (Guest) on January 24, 2022

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

David Ochieng (Guest) on December 30, 2021

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Joseph Kiwanga (Guest) on December 18, 2021

Neema ya Mungu inatosha kwako

Catherine Naliaka (Guest) on October 24, 2021

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Tabitha Okumu (Guest) on September 2, 2021

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

George Mallya (Guest) on July 7, 2021

Rehema hushinda hukumu

Rose Amukowa (Guest) on June 6, 2021

Dumu katika Bwana.

Stephen Mushi (Guest) on May 2, 2021

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Stephen Mushi (Guest) on April 8, 2021

Sifa kwa Bwana!

Sarah Karani (Guest) on March 18, 2021

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Josephine Nduta (Guest) on March 12, 2021

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Janet Mwikali (Guest) on December 7, 2020

Imani inaweza kusogeza milima

Anna Sumari (Guest) on November 14, 2020

Neema na amani iwe nawe.

Elizabeth Malima (Guest) on October 18, 2020

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Rose Kiwanga (Guest) on September 29, 2020

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Isaac Kiptoo (Guest) on September 16, 2020

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

James Mduma (Guest) on June 18, 2020

Mwamini katika mpango wake.

Stephen Kangethe (Guest) on February 1, 2020

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Alice Jebet (Guest) on December 31, 2019

πŸ™πŸ™πŸ™

Elizabeth Mtei (Guest) on December 23, 2019

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Monica Adhiambo (Guest) on December 3, 2019

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

James Mduma (Guest) on August 11, 2019

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Elizabeth Mtei (Guest) on August 2, 2019

πŸ™πŸ™πŸ™

Mary Mrope (Guest) on July 25, 2019

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Benjamin Kibicho (Guest) on May 31, 2019

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Alex Nyamweya (Guest) on April 23, 2019

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Vincent Mwangangi (Guest) on January 3, 2019

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Michael Mboya (Guest) on November 26, 2018

Rehema zake hudumu milele

Rose Lowassa (Guest) on November 25, 2018

πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

Related Posts

ATUKUZWE BABA

ATUKUZWE BABA

Atukuzwe Baba
na Mwana
na Roho Mtakatifu
Kama mwanzo
na sasa,
na siku zo... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

SALA KWA MT. YOSEFU KWA AJILI YA KULIOMBEA KANISA LA MAHUJAJI

Ee Mtukufu Mt. Yosefu, ulichaguliwa na Mungu kuwa Baba Mlishi wa Yesu, mchumba safi kabisa wa Mar... Read More

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

Matendo ya Rozari Takatifu: Mchanganuo kwa siku zote za Saba za Juma

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)

Anza Novena hii tarehe 19 Agosti ili kumalizia tarehe 27 Agosti na kush... Read More

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto... Read More