ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA
Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria saba kwa kila teso.
TESO LA KWANZA
Mzee Simeoni aliagua kuwa Moyo wa Mama Maria utachomwa kwa upanga.
Tuombe neema ya kuvumilia mateso.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA PILI
Maria na Yosefu walikimbilia Misri usiku ili kumficha Mtoto Yesu asiuawe na Herodi.
Tuombe neema ili miili yetu iwe kimbilio lake Yesu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TATU
Mama Maria aliona uchungu sana Mtoto Yesu alipopotea kwa siku tatu.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu mioyoni mwetu.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA NNE
Mama Maria aliona uchungu sana alipokutana na Mwanae Yesu katika njia ya Msalaba.
Tuombe neema ya kudumu na Yesu siku zote.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA TANO
Mama Maria aliona uchungu sana alipomwona Mwanae Yesu akisulibiwa Msalabani.
Tuombe neema ya kufa mikononi mwa Yesu na Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SITA
Mama Maria aliona uchungu sana alipopakata maiti ya Mwanae Yesu baada ya kushushwa Msalabani.
Tuombe neema ya kutotenda dhambi.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
TESO LA SABA
Mama Maria aliona uchungu sana aliporudi nyumbani baada ya kumzika Mwanae Yesu
Tuombe neema ya kitulizo kwa Mama Maria.
Mama wa mateso utuombee.
Baba Yetu β¦β¦β¦ Salamu Maria x7. Atukuzwe Baba β¦β¦
Mateso na majonzi ya Mama Maria hayana mfano.
LITANIA YA MAMA WA MATESO
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie β Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana, Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu MMoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu Utuombee (iwe kiitikio)
Mama wa Mkombozi wetu,
Mama mwenye mateso,
Malkia wa mashahidi,
Mama wa wenye uchungu,
Mfariji wa wenye taabu,
Msaada wa wenye shida,
Mlinzi wa wenye upweke,
Nguvu ya dhaifu moyoni,
Makimbilio ya wakosefu,
Afya ya wagonjwa,
Matumaini ya wanaozimia,
Kwa ajili ya ufukara wako ulioona pangoni Bethlehemu, - Utusaidie ee Mama wa mateso (iwe kiitikio)
Kwa ajili ya mateso yako uliyoona katika uaguzi wa Simeoni,
Kwa ajili ya taabu zako ulizopata katika safari ya Misri,
Kwa uchungu wako, Mwanao alipopotea,
Kwa ajili ya huzuni yako Mwanao alipodhulumiwa,
Kwa ajili ya hofu yako Yesu alipokamatwa,
Kwa ajili ya uchungu wako ulipokutana na Yesu katika njia ya Msalaba,
Kwa ajili ya mateso ya Moyo wako aliposulibiwa,
Kwa ajili ya mateso yako makali Yesu alipokufa,
Kwa ajili ya kilio chako juu ya Mwanao mpenzi,
Kwa ajili ya uchungu wako penye kaburi la Mwanao,
Kwa ajili ya upweke wako baada ya maziko ya Mwanao,
Kwa ajili ya uvumilivu wako katika shida zote,
Katika uchungu wetu wote,
Katika ugonjwa na mateso,
Katika huzuni na shida,
Katika umaskini na upweke,
Katika mahangaiko na hatari,
Katika vishawisho vyote,
Katika saa ya kifo chetu,
Katika hukumu ya mwisho,
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utusikilize ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu, unayeondoa dhambi za dunia, Utuhurumie.
Kristo utusikie β Kristo utusikilize
Bwana utuhurumie β Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie.
Baba Yetu β¦.
Utuombee, ee Mama wa Mateso
Tujaliwe kupewa ahadi za Kristo.
TUOMBE: Ee Bwana Yesu Kristo, utusaidie sasa na saa ya kifo chetu msaada wa Bikira Maria Mama yako, ambaye moyo wake mtakatifu ulichomwa na upanga wa mateso ulipoteswa na kufa msalabani. Unayeishi na kutawala milele na milele. Amina.
SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE
Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubwa sana ulipotazama mateso na kifo cha Mwana wako mpenzi. Muda ule uliweza kutuliz kidogo kwa sababu ya kumwona angali hai. Lakini je, baada ya kufa na kumzika? Sasa wewe ni mkiwa mkubwa mno! Uh, ukiwa wa pekee, uniombee mimi ninayempoteza mara nyingi kwa dhambi zangu. Unijalie nisimpoteze tena Yesu wangu kwa ubaya wa uvivu wangu, bali nimtumikie kiaminifu duniani hapa ili nimwone na kumfurahia milele mbinguni. Amina.
SALA YA MAJITOLEO KWA MAMA WA HUZUNI
Mama Mtakatifu, Mama wa Mungu na Malkia wa Mashahidi, leo nakuchagua Wewe uwe mfano wangu, mkingaji na mteteaji wangu. Naweka roho fukara katika moyo wako uliotobolewa na panga nyingi za mateso. Unipokee mimi niwe mtumishi wako wa pekee na mshiriki wa mateso yako. Nijalie nguvu niwe daima karibu na msalaba ule alikosulibiwa Yesu. Nakutolea nafsi yangu na mali yangu yote. Pokea kila tendo langu jema ukalisindikize kwa Mwanao, Mama, nifanye nistahili kuitwa mtumishi wa Maria, Simama karibu yangu katika matendo yangu yote ili yafanwe kwa sifa ya Mungu. Ulivyosimama karibu kabisa ya Mwanao alipokufa msalabani uwe karibu nami saa ya kufa kwangu. Nijalie niweze kutaja jina lako na la Mwana wako nikisema: βYesu, Maria na Yosef mnisaidie saa ya kufa kwangu. Yesu, maria na Yosef, naomba nife kwa amani kati yenu!β . Amina.
SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE
Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na uliyemtazama Mwana wako akifa, unitazame kwa huruma ya kimama ninayekusikitikia. Kwa sababu ya upanga uliochoma moyo wako, kwa mateso ya maisha yako nakuomba uniangalie kwa wema ukasikilize maombi yangu. Nakuomba, ee Mama, uniombee daima kwa Mwana wako, najua hawezi kukuvyima wewe kitu chochote. Basi, ufanye, Moyo wa Mwanao ukubali kunijalia ombi langu hili β¦β¦β¦β¦β¦β¦β¦(taja ombi lako).
Maana nitamkimbilia nani katika mahitaji na misiba yangu isipokuwa kwako, ee Mama wa huruma? Wewe hasa unaweza kutusaidia sisi tulio bado katika bonde la machozi kwa sababu ulishiriki mateso ya Mwanao kutukomboa. Umtolee Yesu tone moja la Damu yake takatifu. Umkumbushe ya kuwa wewe ni matumaini, furaha na maisha yetu ukanipatie jambo ninalokuomba kwa Yesu Kristo, bwana wetu. Amina.
Charles Wafula (Guest) on July 15, 2024
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Nancy Kabura (Guest) on July 11, 2024
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Alice Mwikali (Guest) on May 24, 2024
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Ruth Mtangi (Guest) on May 14, 2024
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
Esther Cheruiyot (Guest) on February 16, 2024
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Francis Mtangi (Guest) on January 18, 2024
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
Anna Kibwana (Guest) on September 28, 2023
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Martin Otieno (Guest) on July 23, 2023
Nguvu hutoka kwa Bwana
Joy Wacera (Guest) on June 22, 2023
ππ Neema za Mungu zisikose
Rose Lowassa (Guest) on May 1, 2023
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Charles Mchome (Guest) on March 13, 2023
Mungu akubariki!
Grace Njuguna (Guest) on November 16, 2022
Mwamini Bwana; anajua njia
Stephen Kangethe (Guest) on October 31, 2022
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Stephen Malecela (Guest) on October 12, 2022
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mary Njeri (Guest) on August 25, 2022
Endelea kuwa na imani!
Miriam Mchome (Guest) on August 24, 2022
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Robert Okello (Guest) on July 21, 2022
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Ruth Kibona (Guest) on July 13, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Ruth Mtangi (Guest) on July 8, 2022
πβ€οΈ Mungu akubariki
Mariam Hassan (Guest) on July 2, 2022
Baraka kwako na familia yako.
Dorothy Mwakalindile (Guest) on June 23, 2022
Nakuombea π
Patrick Akech (Guest) on June 12, 2022
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Lucy Mahiga (Guest) on June 2, 2022
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Wilson Ombati (Guest) on May 27, 2022
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Tabitha Okumu (Guest) on April 21, 2022
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Samson Mahiga (Guest) on April 11, 2022
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Frank Macha (Guest) on April 11, 2022
ππ Mungu alete amani
Sarah Mbise (Guest) on March 29, 2022
Amina
Nancy Akumu (Guest) on March 17, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Irene Akoth (Guest) on March 3, 2022
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
David Chacha (Guest) on February 13, 2022
ππ Nakushukuru Mungu
Thomas Mtaki (Guest) on January 24, 2022
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
David Ochieng (Guest) on December 30, 2021
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Joseph Kiwanga (Guest) on December 18, 2021
Neema ya Mungu inatosha kwako
Catherine Naliaka (Guest) on October 24, 2021
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Tabitha Okumu (Guest) on September 2, 2021
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
George Mallya (Guest) on July 7, 2021
Rehema hushinda hukumu
Rose Amukowa (Guest) on June 6, 2021
Dumu katika Bwana.
Stephen Mushi (Guest) on May 2, 2021
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Stephen Mushi (Guest) on April 8, 2021
Sifa kwa Bwana!
Sarah Karani (Guest) on March 18, 2021
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Josephine Nduta (Guest) on March 12, 2021
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Janet Mwikali (Guest) on December 7, 2020
Imani inaweza kusogeza milima
Anna Sumari (Guest) on November 14, 2020
Neema na amani iwe nawe.
Elizabeth Malima (Guest) on October 18, 2020
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rose Kiwanga (Guest) on September 29, 2020
πβ¨ Mungu atakuinua
Isaac Kiptoo (Guest) on September 16, 2020
ππ Mbarikiwe sana
James Mduma (Guest) on June 18, 2020
Mwamini katika mpango wake.
Stephen Kangethe (Guest) on February 1, 2020
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Alice Jebet (Guest) on December 31, 2019
πππ
Elizabeth Mtei (Guest) on December 23, 2019
πππ« Mungu ni mwema
Monica Adhiambo (Guest) on December 3, 2019
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
James Mduma (Guest) on August 11, 2019
ππ Nakusihi Mungu
Elizabeth Mtei (Guest) on August 2, 2019
πππ
Mary Mrope (Guest) on July 25, 2019
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Benjamin Kibicho (Guest) on May 31, 2019
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Alex Nyamweya (Guest) on April 23, 2019
ππ Mungu akujalie amani
Vincent Mwangangi (Guest) on January 3, 2019
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Michael Mboya (Guest) on November 26, 2018
Rehema zake hudumu milele
Rose Lowassa (Guest) on November 25, 2018
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako