Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuheshimu Damu Takatifu ya Mkombozi wetu.
Yesu alimwahidi Mt. Brigita wa Sweden kwamba wale watakaosali Baba Yetu 7 na Salamu Maria 7 kwa miaka 12 kwa kuheshimu damu yake takatifu na kutafakari juu ya Kutahiriwa kwake, jasho lake la damu, kupigwa kwake mijeledi, kuvikwa taji la miiba, kuchukua kwake Msalaba, kusuliwa kwake na kuchomwa ubavuni; watapata neema 5 zifuatazo: (1) Hawataingia toharani, (2) Yesu atawapa cheo cha mashahidi waliomwaga damu yao kwa ajili ya imani, (3) Yesu atawadumisha jamaa zake watatu katika hali ya neema, (4) Roho za jamaa zake zitakingwa na Jehanam mpaka kizazi cha nne, (5) Mwezi kabla ya kufa, Yesu atawajulisha. Wakifa kabla ya kutimiza miaka ile, watahesabiwa wamemaliza.
Ee Yesu, sasa ninataka kusali Baba yetu mara saba nikiungana na ule upendo ambao kwao uliitakasa sala hii katika Moyo wako. Uichukue kutoka mdomoni mwangu hadi moyoni mwako. Uiboreshe na kuikamilisha hivyo kwamba iupatie heshima na furaha kwa Utatu Mtakatifu kama vile Wewe ulivyoupatia kupitia sala hii wakati ulipokuwa bado hapa duniani. Utukuzwe ee Yesu, itukuzwe Damu Yako Takatifu sana uliyoimwaga kutoka katika Majeraha Yako Matakatifu.
1. Yesu anatahiriwa.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu β¦. Salamu Maria β¦. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Majeraha ya kwanza, maumivu ya kwanza na Damu ya kwanza aliyomwaga Mwanao mpenzi, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu na dhambi za dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi ya kwanza ya mauti, hasa kati ya ndugu zangu.
2. Yesu anatokwa Jasho la Damu bustanini Gethsemane.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu β¦. Salamu Maria β¦. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso na mahangaiko makali sana ya moyoni, ya Bwana wetu Yesu Kristu katika mlima wa mizeituni na kila tone la jasho lake la damu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za kimoyomoyo, na dhambi za namna hiyo zinazotendwa na dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za moyoni na kwa ajili ya kueneza upendo wa kiMungu na wa kindugu.
3. Yesu anapigwa mijeledi.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu β¦. Salamu Maria β¦. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha elfu elfu aliyopata, maumivu makali sana na Damu Takatifu sana aliyomwaga, alipopigwa mijeledi, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za tamaa ya mwili, kwa malipizi ya dhambi za tamaa ya mwili za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za tamaa ya mwili, na kwa kulinda usafi wa moyo, hasa kati ya ndugu zangu.
4. Yesu anavikwa taji la miiba.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu β¦. Salamu Maria β¦. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha, maumivu na Damu Takatifu kutoka katika Kichwa Kitakatifu cha Yesu wakati alipovikwa taji la miiba, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za rohoni, kwa malipizi ya dhambi za rohoni za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za rohoni, na kwa ajili ya kueneza Ufalme wa Kristu hapa duniani.
5. Yesu anachukua Msalaba.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu β¦. Salamu Maria β¦. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso ya njia ya Msalaba, hasa donda lake la begani na Damu Takatifu iliyomwagika, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za ukaidi dhidi ya msalaba, na dhambi za ukaidi dhidi ya msalaba za wanadamu wote, malalamiko yote dhidi ya mipango yako mitakatifu na dhambi zote za ulimi, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za ulimi na kwa ajili ya upendo wa kweli kwa Msalaba.
6. Yesu anasulibiwa.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu β¦. Salamu Maria β¦. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Mwanao Msalabani, kupigwa kwake misumari na kuinuliwa kwake, madonda yake mikononi na miguuni na mifereji mitatu ya Damu yake Takatifu iliyomwagika kutoka katika majeraha haya, mateso yake makali sana ya mwili na roho, kifo chake kitakatifu, ukumbusho usio wa kumwaga wa damu wa kifo hiki katika Misa zote Takatifu ulimwenguni, kwa ajili ya majeraha yote yanayosababishwa na ukaidi wa nadhiri na kanuni katika madaraja matakatifu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu zote na za ulimwenguni mzima, kwa ajili ya wagonjwa na wanaokufa, kwa ajili ya mapadre watakatifu na walei, kwa ajili ya nia za Baba Mtakatifu za kukarabati familia za kikristu, kwa ajili ya kuimarika kwa imani ya kikristu ulimwenguni, kwa ajili ya nchi yetu na muungano kati ya mataifa ndani ya Kristu na Kanisa lake, na kwa ajili ya wokovu wa dunia nzima.
7. Yesu anachomwa kwa mkuki moyoni.
Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu β¦. Salamu Maria β¦. Baba wa Milele, ukubali kupokea, kwa ajili ya mahitaji ya Kanisa Takatifu na kwa ajili ya malipizi ya dhambi za wanadamu wote, Damu na Maji Takatifu vilivyomwagika kutoka jeraha la Moyo Mtakatifu wa Yesu. Utuhurumie. Damu Takatifu ya Yesu, tone lile la mwisho lililomwagika kutoka katika Moyo wake Mtakatifu, unioshe mimi na wengine wote dhambi zetu zote! Ee Maji kutoka katika Moyo Mtakatifu wa Yesu, unioshe na adhabu zote za dhambi zangu na uizime miale ya moto wa toharani kwa ajili yangu na kwa ajili ya roho zote zilizomo toharani. Amina.
Katika mwaka wa Kanisa wa kiliturjia, mwezi Julai ni wa kuiheshimu Damu Takatifu ya Yesu.
Janet Wambura (Guest) on June 20, 2024
πππ Mungu akufunike na upendo
Elizabeth Mrema (Guest) on June 10, 2024
Nakuombea π
Monica Nyalandu (Guest) on April 21, 2024
ππ Mungu wetu asifiwe
Paul Kamau (Guest) on March 18, 2024
ππ Mungu akujalie amani
Rose Amukowa (Guest) on March 7, 2024
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Alice Mrema (Guest) on December 21, 2023
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Joyce Mussa (Guest) on December 9, 2023
Mungu akubariki!
James Mduma (Guest) on November 19, 2023
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Stephen Kikwete (Guest) on June 16, 2023
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Rose Mwinuka (Guest) on April 19, 2023
ππ Mungu alete amani
Wilson Ombati (Guest) on February 23, 2023
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Thomas Mtaki (Guest) on January 3, 2023
ππ Nakusihi Mungu
Francis Mrope (Guest) on December 27, 2022
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Mariam Kawawa (Guest) on December 25, 2022
ππ Mbarikiwe sana
Dorothy Nkya (Guest) on December 20, 2022
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Robert Ndunguru (Guest) on November 26, 2022
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Stephen Kikwete (Guest) on November 2, 2022
πππ
Joseph Kitine (Guest) on October 29, 2022
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Faith Kariuki (Guest) on October 1, 2022
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Robert Ndunguru (Guest) on August 13, 2022
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
David Nyerere (Guest) on July 25, 2022
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
George Tenga (Guest) on July 5, 2022
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
Betty Cheruiyot (Guest) on April 28, 2022
Dumu katika Bwana.
Raphael Okoth (Guest) on April 21, 2022
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Benjamin Kibicho (Guest) on February 10, 2022
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Stephen Kikwete (Guest) on January 14, 2022
Mwamini katika mpango wake.
Peter Mbise (Guest) on January 8, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Lucy Kimotho (Guest) on October 15, 2021
Amina
Nancy Kawawa (Guest) on September 15, 2021
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
John Malisa (Guest) on August 25, 2021
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Susan Wangari (Guest) on July 1, 2021
Sifa kwa Bwana!
Stephen Amollo (Guest) on April 29, 2021
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
Linda Karimi (Guest) on April 14, 2021
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Wilson Ombati (Guest) on March 8, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Joyce Aoko (Guest) on February 19, 2021
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Nancy Komba (Guest) on January 18, 2021
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
Lucy Wangui (Guest) on August 18, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Chris Okello (Guest) on July 26, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Anna Malela (Guest) on July 3, 2020
Neema na amani iwe nawe.
Peter Mbise (Guest) on June 4, 2020
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Stephen Amollo (Guest) on April 7, 2020
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Grace Minja (Guest) on March 23, 2020
πβ€οΈ Mungu akubariki
David Chacha (Guest) on November 26, 2019
Endelea kuwa na imani!
Tabitha Okumu (Guest) on August 9, 2019
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Lydia Wanyama (Guest) on July 20, 2019
πππ« Mungu ni mwema
Andrew Odhiambo (Guest) on July 9, 2019
Tumaini ni nanga ya roho
Edward Lowassa (Guest) on April 28, 2019
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
Patrick Mutua (Guest) on April 6, 2019
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Mariam Hassan (Guest) on February 11, 2019
Mungu ni mwema, wakati wote!
Andrew Mchome (Guest) on December 25, 2018
ππ Neema za Mungu zisikose
Patrick Akech (Guest) on December 20, 2018
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
Grace Wairimu (Guest) on November 28, 2018
ππ Nakushukuru Mungu
Carol Nyakio (Guest) on November 15, 2018
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Mary Njeri (Guest) on October 25, 2018
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Anna Malela (Guest) on October 23, 2018
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Victor Kamau (Guest) on October 9, 2018
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Rose Waithera (Guest) on September 30, 2018
Rehema zake hudumu milele
Catherine Mkumbo (Guest) on September 24, 2018
πβ¨ Mungu atakuinua
Patrick Kidata (Guest) on August 16, 2018
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Peter Mugendi (Guest) on August 14, 2018
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika