Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

Sala za kuheshimu Damu Takatifu ya Yesu

Featured Image

Tusali kila siku sala hizi, angalau kwa mwezi wa saba (Julai) kila mwaka, mwezi wa kuheshimu Damu Takatifu ya Mkombozi wetu.

Yesu alimwahidi Mt. Brigita wa Sweden kwamba wale watakaosali Baba Yetu 7 na Salamu Maria 7 kwa miaka 12 kwa kuheshimu damu yake takatifu na kutafakari juu ya Kutahiriwa kwake, jasho lake la damu, kupigwa kwake mijeledi, kuvikwa taji la miiba, kuchukua kwake Msalaba, kusuliwa kwake na kuchomwa ubavuni; watapata neema 5 zifuatazo: (1) Hawataingia toharani, (2) Yesu atawapa cheo cha mashahidi waliomwaga damu yao kwa ajili ya imani, (3) Yesu atawadumisha jamaa zake watatu katika hali ya neema, (4) Roho za jamaa zake zitakingwa na Jehanam mpaka kizazi cha nne, (5) Mwezi kabla ya kufa, Yesu atawajulisha. Wakifa kabla ya kutimiza miaka ile, watahesabiwa wamemaliza.

Ee Yesu, sasa ninataka kusali Baba yetu mara saba nikiungana na ule upendo ambao kwao uliitakasa sala hii katika Moyo wako. Uichukue kutoka mdomoni mwangu hadi moyoni mwako. Uiboreshe na kuikamilisha hivyo kwamba iupatie heshima na furaha kwa Utatu Mtakatifu kama vile Wewe ulivyoupatia kupitia sala hii wakati ulipokuwa bado hapa duniani. Utukuzwe ee Yesu, itukuzwe Damu Yako Takatifu sana uliyoimwaga kutoka katika Majeraha Yako Matakatifu.

1. Yesu anatahiriwa.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Majeraha ya kwanza, maumivu ya kwanza na Damu ya kwanza aliyomwaga Mwanao mpenzi, Bwana wetu Yesu Kristu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu na dhambi za dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi ya kwanza ya mauti, hasa kati ya ndugu zangu.

2. Yesu anatokwa Jasho la Damu bustanini Gethsemane.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso na mahangaiko makali sana ya moyoni, ya Bwana wetu Yesu Kristu katika mlima wa mizeituni na kila tone la jasho lake la damu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za kimoyomoyo, na dhambi za namna hiyo zinazotendwa na dunia nzima, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za moyoni na kwa ajili ya kueneza upendo wa kiMungu na wa kindugu.

3. Yesu anapigwa mijeledi.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha elfu elfu aliyopata, maumivu makali sana na Damu Takatifu sana aliyomwaga, alipopigwa mijeledi, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za tamaa ya mwili, kwa malipizi ya dhambi za tamaa ya mwili za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za tamaa ya mwili, na kwa kulinda usafi wa moyo, hasa kati ya ndugu zangu.

4. Yesu anavikwa taji la miiba.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea majeraha, maumivu na Damu Takatifu kutoka katika Kichwa Kitakatifu cha Yesu wakati alipovikwa taji la miiba, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za rohoni, kwa malipizi ya dhambi za rohoni za wanadamu wote, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za rohoni, na kwa ajili ya kueneza Ufalme wa Kristu hapa duniani.

5. Yesu anachukua Msalaba.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea mateso ya njia ya Msalaba, hasa donda lake la begani na Damu Takatifu iliyomwagika, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu za ukaidi dhidi ya msalaba, na dhambi za ukaidi dhidi ya msalaba za wanadamu wote, malalamiko yote dhidi ya mipango yako mitakatifu na dhambi zote za ulimi, kwa ajili ya ulinzi dhidi ya dhambi za ulimi na kwa ajili ya upendo wa kweli kwa Msalaba.

6. Yesu anasulibiwa.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, kupitia mikono safi ya Maria na Moyo Mtakatifu wa Yesu, ninakutolea Mwanao Msalabani, kupigwa kwake misumari na kuinuliwa kwake, madonda yake mikononi na miguuni na mifereji mitatu ya Damu yake Takatifu iliyomwagika kutoka katika majeraha haya, mateso yake makali sana ya mwili na roho, kifo chake kitakatifu, ukumbusho usio wa kumwaga wa damu wa kifo hiki katika Misa zote Takatifu ulimwenguni, kwa ajili ya majeraha yote yanayosababishwa na ukaidi wa nadhiri na kanuni katika madaraja matakatifu, kwa ajili ya malipizi ya dhambi zangu zote na za ulimwenguni mzima, kwa ajili ya wagonjwa na wanaokufa, kwa ajili ya mapadre watakatifu na walei, kwa ajili ya nia za Baba Mtakatifu za kukarabati familia za kikristu, kwa ajili ya kuimarika kwa imani ya kikristu ulimwenguni, kwa ajili ya nchi yetu na muungano kati ya mataifa ndani ya Kristu na Kanisa lake, na kwa ajili ya wokovu wa dunia nzima.

7. Yesu anachomwa kwa mkuki moyoni.

Tafakari fupi (kimya kidogo). Baba Yetu …. Salamu Maria …. Baba wa Milele, ukubali kupokea, kwa ajili ya mahitaji ya Kanisa Takatifu na kwa ajili ya malipizi ya dhambi za wanadamu wote, Damu na Maji Takatifu vilivyomwagika kutoka jeraha la Moyo Mtakatifu wa Yesu. Utuhurumie. Damu Takatifu ya Yesu, tone lile la mwisho lililomwagika kutoka katika Moyo wake Mtakatifu, unioshe mimi na wengine wote dhambi zetu zote! Ee Maji kutoka katika Moyo Mtakatifu wa Yesu, unioshe na adhabu zote za dhambi zangu na uizime miale ya moto wa toharani kwa ajili yangu na kwa ajili ya roho zote zilizomo toharani. Amina.

Katika mwaka wa Kanisa wa kiliturjia, mwezi Julai ni wa kuiheshimu Damu Takatifu ya Yesu.

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Janet Wambura (Guest) on June 20, 2024

πŸ™πŸ’–πŸ™ Mungu akufunike na upendo

Elizabeth Mrema (Guest) on June 10, 2024

Nakuombea πŸ™

Monica Nyalandu (Guest) on April 21, 2024

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

Paul Kamau (Guest) on March 18, 2024

πŸ™πŸŒŸ Mungu akujalie amani

Rose Amukowa (Guest) on March 7, 2024

Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako

Alice Mrema (Guest) on December 21, 2023

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Joyce Mussa (Guest) on December 9, 2023

Mungu akubariki!

James Mduma (Guest) on November 19, 2023

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Stephen Kikwete (Guest) on June 16, 2023

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Rose Mwinuka (Guest) on April 19, 2023

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Wilson Ombati (Guest) on February 23, 2023

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Thomas Mtaki (Guest) on January 3, 2023

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Francis Mrope (Guest) on December 27, 2022

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Mariam Kawawa (Guest) on December 25, 2022

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Dorothy Nkya (Guest) on December 20, 2022

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Robert Ndunguru (Guest) on November 26, 2022

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Stephen Kikwete (Guest) on November 2, 2022

πŸ™πŸ™πŸ™

Joseph Kitine (Guest) on October 29, 2022

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Faith Kariuki (Guest) on October 1, 2022

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Robert Ndunguru (Guest) on August 13, 2022

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

David Nyerere (Guest) on July 25, 2022

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

George Tenga (Guest) on July 5, 2022

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Betty Cheruiyot (Guest) on April 28, 2022

Dumu katika Bwana.

Raphael Okoth (Guest) on April 21, 2022

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Benjamin Kibicho (Guest) on February 10, 2022

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Stephen Kikwete (Guest) on January 14, 2022

Mwamini katika mpango wake.

Peter Mbise (Guest) on January 8, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Lucy Kimotho (Guest) on October 15, 2021

Amina

Nancy Kawawa (Guest) on September 15, 2021

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

John Malisa (Guest) on August 25, 2021

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Susan Wangari (Guest) on July 1, 2021

Sifa kwa Bwana!

Stephen Amollo (Guest) on April 29, 2021

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Linda Karimi (Guest) on April 14, 2021

Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha

Wilson Ombati (Guest) on March 8, 2021

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

Joyce Aoko (Guest) on February 19, 2021

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Nancy Komba (Guest) on January 18, 2021

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Lucy Wangui (Guest) on August 18, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Chris Okello (Guest) on July 26, 2020

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Anna Malela (Guest) on July 3, 2020

Neema na amani iwe nawe.

Peter Mbise (Guest) on June 4, 2020

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Stephen Amollo (Guest) on April 7, 2020

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Grace Minja (Guest) on March 23, 2020

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

David Chacha (Guest) on November 26, 2019

Endelea kuwa na imani!

Tabitha Okumu (Guest) on August 9, 2019

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Lydia Wanyama (Guest) on July 20, 2019

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Andrew Odhiambo (Guest) on July 9, 2019

Tumaini ni nanga ya roho

Edward Lowassa (Guest) on April 28, 2019

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Patrick Mutua (Guest) on April 6, 2019

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Mariam Hassan (Guest) on February 11, 2019

Mungu ni mwema, wakati wote!

Andrew Mchome (Guest) on December 25, 2018

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Patrick Akech (Guest) on December 20, 2018

πŸ™βœ¨ Neema ya Mungu iwe nawe

Grace Wairimu (Guest) on November 28, 2018

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Carol Nyakio (Guest) on November 15, 2018

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Mary Njeri (Guest) on October 25, 2018

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Anna Malela (Guest) on October 23, 2018

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Victor Kamau (Guest) on October 9, 2018

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Rose Waithera (Guest) on September 30, 2018

Rehema zake hudumu milele

Catherine Mkumbo (Guest) on September 24, 2018

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Patrick Kidata (Guest) on August 16, 2018

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Peter Mugendi (Guest) on August 14, 2018

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Related Posts

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubw... Read More

Sala ya Saa Tisa

Sala ya Saa Tisa

✝⌚✝

Sala ya saa tisaπŸ™πŸΎ

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.... Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

SALA YA NOVENA YA SIKU TISA KWA MT. YOSEFU, YA ZAMANI, MIAKA 1900 ILIYOPITA

Ee Mt. Yosefu, ambaye ulinzi wako ni mkubwa, wenye nguvu na wa haraka mbele ya Kiti cha Enzi cha ... Read More

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

SALA YA NOVENA KWA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Ee Moyo Mtakatifu sana wa Yesu, chemchemi ya kila baraka, ninakuabudu, ninakupenda, na kwa majuto... Read More

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

Ee Mt. Yosefu, Baba Mlishi wa Mwokozi wangu, na mchumba safi wa Mama wa Mungu, leo ninakuchagua w... Read More

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

SALA YA KUMWABUDU BWANA YESU KATIKA SAKRAMENTI TAKATIFU

Ee Yesu Kristu,/ Bwana wangu na Mungu wangu/ ambaye ninasadiki kuwa upo hapa/ katika Sakramenti T... Read More

SALA YA KUTUBU

SALA YA KUTUBU

Mungu wangu ninatubu sana, niliyokosa kwako, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukiz... Read More

SALA KWA MT. YOSEFU KUOMBA KUFAHAMU WITO WAKO

SALA KWA MT. YOSEFU KUOMBA KUFAHAMU WITO WAKO

Ee uliye Mkuu, Mt. Yosefu, uliyatii kabisa maongozi ya Roho Mt. Unijalie neema ya kufahamu aina y... Read More

NOVENA YA ROHO MTAKATIFU KWA SIKU ZOTE TISA

NOVENA YA ROHO MTAKATIFU KWA SIKU ZOTE TISA

Ufuatao ni mtiririko wa Novena ya Roho Mtakatifu kwa siku zote tisa.

Kusali nov... Read More

NOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

NOVENA KWA AJILI YA KUJIANDAA KWA SIKUKUU YA MOYO MTAKATIFU WA YESU

Inaweza kusemwa wakati wowote katika mwaka. Kwa ajili ya kujiandaa kwa Sikukuu ya Moyo Mtakatifu ... Read More

Sala kwa wenye kuzimia

Sala kwa wenye kuzimia

Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu... Read More