Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako, ukachagua Mapadri wawe Wachungaji na Viongozi wa roho za watu. Nakuomba sana; ubariki nia na bidii inayowapasa Mapadri wote katika kazi zao. Uwaongezee Utakatifu.
Uwatie moyo mzuri wenye mapendo makubwa kwako na roho za watu. Hivyo wakiisha kupata wenyewe Utakatifu, waweze kuwaongoza vizuri watu walio chini ya ulinzi wao, katika njia ya Utakatifu na furaha ya milele. Uwajalie neema zote za hali ya Upadri. Uwajalie ili waonyeshe kila siku ya maisha yao mfano wa kila fadhila ya mapendo na ya uaminifu katika Kanisa, kwa Baba Mtakatifu na kwa Maaskofu.
Yesu mpendelevu, uangalie kwa mapendo kazi na mateso ya Mapadri wako; ubariki na ustawishe mafundisho yao; wanapowafundisha watoto, wanapowahubiria watu, wanapowatuliza wakosefu watubu na wanapowasaidia wagonjwa na wale wanaokaribia mauti, Ee Yesu uwe pamoja nao. Uwakinge na hatari zote za roho na za mwili.
Mwokozi Yesu, ulijalie Kanisa liwe na Mapadri wengi walio Watakatifu. Uwajalie watoto na vijana wengi wasikie wito wa Upadri, uwatie furaha na Utakatifu na roho za Mapadri waliokufa uzijalie punziko la amani.
Kwa mimi mwenyewe Ee Yesu mpendelevu, naomba unijalie roho ya imani na utii mnyenyekevu ili niwaheshimu Mapadri kama Mawakili wa Mungu. Niwatii katika njia zote za wokovu wa roho yangu. Amina.
Faith Kariuki (Guest) on August 20, 2017
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Nancy Kabura (Guest) on August 16, 2017
πππ
Elizabeth Mtei (Guest) on July 17, 2017
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
Sarah Achieng (Guest) on June 22, 2017
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Peter Mwambui (Guest) on June 12, 2017
πβ€οΈ Mungu akubariki
Grace Majaliwa (Guest) on May 23, 2017
Neema ya Mungu inatosha kwako
Lucy Mushi (Guest) on March 29, 2017
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Anna Sumari (Guest) on December 31, 2016
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Peter Mwambui (Guest) on November 5, 2016
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
James Malima (Guest) on October 31, 2016
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Irene Akoth (Guest) on August 5, 2016
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
James Malima (Guest) on July 24, 2016
Baraka kwako na familia yako.
Joyce Nkya (Guest) on July 5, 2016
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Grace Mushi (Guest) on May 17, 2016
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Grace Njuguna (Guest) on May 9, 2016
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Christopher Oloo (Guest) on February 17, 2016
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mary Kendi (Guest) on January 6, 2016
Tumaini ni nanga ya roho
John Lissu (Guest) on January 6, 2016
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Agnes Lowassa (Guest) on November 14, 2015
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Sharon Kibiru (Guest) on September 4, 2015
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Anna Mahiga (Guest) on July 11, 2015
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Irene Makena (Guest) on June 28, 2015
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
Joseph Njoroge (Guest) on June 7, 2015
Rehema hushinda hukumu