Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU I

Featured Image

Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate wa kidunia/ ukafanya mwujiza na kuugeuza/ kuwa Mwili wako azizi./ Kwa mapendo ukawapa Mitume Mwili huo/ uwe kumbukumbu la mateso yako mastahivu./ Uliwaosha miguu kwa Mikono yako Mitakatifu./

Uheshimiwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Kwa kuhofu mateso na kifo,/ Mwili wako usio na kosa ulitoka jasho la damu/ badala ya maji./ Juu ya hayo uliutimiza wokovu wetu/ uliokuwa umetaka kuufanya./ Hivyo ulionyesha waziwazi mapendo yako/ uliyo nayo kwa wanadamu./

Utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipelekwa kwa Kayafa,/ Wewe uliye Hakimu wa wote./ Ukaruhusu kwa unyenyekevu kutolewa kwa Pilato/ uhukumiwe naye./

Utukufu uwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kuwa ulivumilia kuchekwa tena/ uliposimama huko,/ umevaa joho jekundu,/ umetiwa taji ya miiba mikali sana Kichwani,/ ukavumilia kwa saburi kubwa/ kutemewa mate katika Uso wako mzuri,/ kufumbwa Macho,/ na kupigwa mno na wajeuri/ ngumi na makofi Mashavuni na Shingoni./

Sifa iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ Kwa uvumilivu mkubwa ulikubali kufungwa nguzoni,/ kupigwa mijeledi kijeuri,/ kujaa damu na hivyo kusukumwa barazani kwa Pilato./ Ulionekana kama mwanakondoo asiye na kosa./

Heshima iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo./ Umehukumiwa Mwili wako mzima/ Mtukufu wenye kutoka damu/ ufe msalabani./ Ulichukua msalaba kwa Mabega yako Matakatifu/ na kuumwa sana./ Kwa ghadhabu walikusukuma mbele/ mpaka mahali pa mateso,/ wakakunyang’anya nguo zako./ Hivyo ulikubali kupigiliwa msalabani./

Heshima ya milele upate Wewe,/ Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipokuwa katika taabu kubwa hii,/ ulimkazia Mama yako mstahivu/ Macho yako ya hisani na mapendo/ na unyenyekevu,/ ndiye Mama yako asiyekosa hata mara moja/ wala kukubali dhambi yeyote./ Ulimweka katika ulinzi mwaminifu/ wa Mfuasi wako ili kumtuliza./

Milele utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipokuwa mwenyewe taabani,/ uliwapa wakosefu wote/ matumaini ya kuondolewa dhambi/ kwa kumwahidia mnyang’anyi aliyekuendea/ utukufu wa paradisi kwa huruma yako./

Sifa ya milele iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kila saa ulipovumilia uchungu/ na taabu kubwa mno msalabani kwa ajili yetu sisi wakosefu,/ maumivu makali sana/ yaliyotoka katika majeraha yako,/ yakapenya bila huruma Roho yako Takatifu./ Yakaingia kikatili katika Moyo wako Mtakatifu/ hata ukakatika,/ ukapumua Roho yako,/ ukainama Kichwa,/ ukaweka Roho yako mikononi mwa Mungu, Baba yako./ Na baada ya kufa uliacha nyuma Mwili baridi./

Utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa Damu yako azizi na kwa kifo chako kitakatifu/ ulizifidia roho za watu,/ ukazitoa ugenini/ na kuzipeleka kwa hisani yako katika uzima wa milele./

Milele uheshimiwe, Wewe Bwana wangu Yesu Kristo./ Siku ya tatu ulifufuka katika wafu,/ ukajionyesha kwa wafuasi wako,/ ukapaa mbinguni/ mbele ya macho yao siku ya arobaini./

Shangilio na sifa ya milele upate Wewe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kuwa umewapelekea wafuasi wako mioyoni mwao/ Roho Mtakatifu,/ ukawasha rohoni mwao mapendo makuu ya Mungu./

Pia, utukuzwe, usifiwe na kushangiliwa milele, Bwana wangu Yesu Kristo./ Umekaa katika ufalme wako wa mbinguni/ juu ya kiti cha enzi cha Umungu wako,/ ukaishi pamoja na Viungo vyako vyote Vitakatifu./ Na hivyo utakuja tena/ kuzihukumu roho za wazima na wafu wote./ Unaishi na kutawala/ pamoja na Baba na Roho Mtakatifu,/ milele. Amina.

(Na Mt. Birgita wa Sweden)

AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Betty Akinyi (Guest) on June 22, 2024

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Victor Mwalimu (Guest) on May 29, 2024

Rehema hushinda hukumu

Stephen Malecela (Guest) on February 18, 2024

Endelea kuwa na imani!

John Malisa (Guest) on February 17, 2024

πŸ™πŸ™πŸ™

Stephen Malecela (Guest) on February 1, 2024

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Mary Mrope (Guest) on November 26, 2023

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

George Mallya (Guest) on September 26, 2023

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Mary Mrope (Guest) on August 31, 2023

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Rose Amukowa (Guest) on August 28, 2023

Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe

Chris Okello (Guest) on August 25, 2023

πŸ™βœ¨ Mungu asikie maombi yetu

Charles Mboje (Guest) on June 19, 2023

Wakati wa Mungu ni kamilifu

David Nyerere (Guest) on May 27, 2023

Tumaini ni nanga ya roho

Vincent Mwangangi (Guest) on May 5, 2023

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Anna Malela (Guest) on April 15, 2023

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Rose Lowassa (Guest) on March 21, 2023

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Agnes Sumaye (Guest) on February 27, 2023

πŸ™β€οΈπŸ’– Baraka za Mungu ziwe nawe

Miriam Mchome (Guest) on January 19, 2023

πŸ™πŸ™πŸ™

Kenneth Murithi (Guest) on December 30, 2022

Dumu katika Bwana.

John Lissu (Guest) on November 21, 2022

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Charles Wafula (Guest) on November 15, 2022

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Alice Wanjiru (Guest) on September 27, 2022

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Alice Mwikali (Guest) on September 2, 2022

Sifa kwa Bwana!

Lucy Kimotho (Guest) on August 31, 2022

Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia

Samuel Were (Guest) on July 19, 2022

Nguvu hutoka kwa Bwana

Diana Mallya (Guest) on March 4, 2022

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Nancy Komba (Guest) on March 3, 2022

Neema ya Mungu inatosha kwako

Rose Amukowa (Guest) on January 31, 2022

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

Samuel Omondi (Guest) on September 9, 2021

Hauko peke yako; Mungu yuko nawe

Martin Otieno (Guest) on September 5, 2021

Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika

Joyce Mussa (Guest) on August 16, 2021

Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao

Monica Adhiambo (Guest) on August 11, 2021

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Nicholas Wanjohi (Guest) on June 2, 2021

Nakuombea πŸ™

Lucy Wangui (Guest) on April 22, 2021

Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine

Betty Akinyi (Guest) on April 12, 2021

Ahadi za Mungu ni za kweli daima

Frank Sokoine (Guest) on March 16, 2021

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Alex Nyamweya (Guest) on March 15, 2021

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Lydia Mahiga (Guest) on March 3, 2021

Upendo wa Mungu haukosei kamwe.

James Kawawa (Guest) on December 29, 2020

Amina

Lucy Wangui (Guest) on December 27, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Bernard Oduor (Guest) on December 20, 2020

Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako

Catherine Naliaka (Guest) on November 18, 2020

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Hellen Nduta (Guest) on November 4, 2020

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Sharon Kibiru (Guest) on November 1, 2020

Mwamini Bwana; anajua njia

Mercy Atieno (Guest) on October 11, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Mary Kidata (Guest) on August 21, 2020

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Susan Wangari (Guest) on June 9, 2020

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Linda Karimi (Guest) on May 16, 2020

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Joseph Njoroge (Guest) on May 6, 2020

πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

Sharon Kibiru (Guest) on May 1, 2020

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Diana Mumbua (Guest) on April 9, 2020

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Jane Malecela (Guest) on February 20, 2020

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Violet Mumo (Guest) on December 26, 2019

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

Monica Nyalandu (Guest) on December 1, 2019

Imani inaweza kusogeza milima

John Kamande (Guest) on November 24, 2019

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Mercy Atieno (Guest) on November 7, 2019

Mwamini katika mpango wake.

Anna Malela (Guest) on September 29, 2019

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Samuel Were (Guest) on September 16, 2019

Baraka kwako na familia yako.

Elizabeth Mrope (Guest) on August 24, 2019

Neema na amani iwe nawe.

Carol Nyakio (Guest) on July 4, 2019

Mungu akubariki!

Nicholas Wanjohi (Guest) on March 26, 2019

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Related Posts

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

SALA WAKATI WA KUJIBARIKI NA MAJI YA BARAKA

Kwa njia ya Maji haya ya Baraka,

na kwa njia ya Damu yako azizi,

na kwa maombezi ya M... Read More

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Sala ya Asubuhi ya kila siku

Kwa jina la Baba….. Ee Baba yetu Mungu mkuu,umenilinda usiku huu. Nakushukuru kwa moyo, ee Baba,M... Read More
Novena ya Noeli

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli (maarufu kama novena ya Mt. Andrea)

Husaliwa kuanzia tar 30 Nov hadi usiku ... Read More

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

SALA KWA BIKIRA MARIA KATIKA UKIWA WAKE

Nakusikitikia sana Mama Mtakatifu Maria kwa sababu ya ukiwa wako mkuu. Uchungu wako ulikuwa mkubw... Read More

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

SALA KWA MTAKATIFU MIKAELI MALAIKA MKUU

Mtakatifu Mikaeli Malaika Mkuu, utulinde katika vita, uwe kinga yetu katika maovu na maoteo ya sh... Read More

SALA YA IMANI

SALA YA IMANI

Mungu wangu,

nasadiki maneno yote linalosadiki na linalofundisha kanisa katoliki la Roma;Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na ... Read More

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

ROZARI YA MATESO SABA YA BIKIRA MARIA

Tumia Rozari ya Mateso Saba ya Bikira Maria iliyo na mafungu 7 yaani mateso 7 yenye Salamu Maria... Read More

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

SALA YA KUMWOMBA MTAKATIFU TERESIA WA MTOTO YESU

Ee Mtakatifu Teresia wa mtoto Yesu, ulistahili kuitwa Msimamizi wa misioni katoliki za dunia yote... Read More

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

SALA YA KUANGUKA MIGUUNI PA BWANA YESU KATIKA EKARISTI

Ee Yesu Mfungwa wa Upendo wa Mungu,/ ninapofikiri Upendo wako na jinsi ulivyojitolea kwa ajili ya... Read More

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

SALA YA KUWAOMBEA MAPADRE

Ee Bwana Yesu Kristo. Mkombozi wetu, kwa mapendo na tamaa yako ya kutaka kulinda vema Kanisa lako... Read More