Utukuzwe ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Uliagua kifo chako./ Katika karamu ya mwisho ulitumia mkate wa kidunia/ ukafanya mwujiza na kuugeuza/ kuwa Mwili wako azizi./ Kwa mapendo ukawapa Mitume Mwili huo/ uwe kumbukumbu la mateso yako mastahivu./ Uliwaosha miguu kwa Mikono yako Mitakatifu./
Uheshimiwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Kwa kuhofu mateso na kifo,/ Mwili wako usio na kosa ulitoka jasho la damu/ badala ya maji./ Juu ya hayo uliutimiza wokovu wetu/ uliokuwa umetaka kuufanya./ Hivyo ulionyesha waziwazi mapendo yako/ uliyo nayo kwa wanadamu./
Utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipelekwa kwa Kayafa,/ Wewe uliye Hakimu wa wote./ Ukaruhusu kwa unyenyekevu kutolewa kwa Pilato/ uhukumiwe naye./
Utukufu uwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kuwa ulivumilia kuchekwa tena/ uliposimama huko,/ umevaa joho jekundu,/ umetiwa taji ya miiba mikali sana Kichwani,/ ukavumilia kwa saburi kubwa/ kutemewa mate katika Uso wako mzuri,/ kufumbwa Macho,/ na kupigwa mno na wajeuri/ ngumi na makofi Mashavuni na Shingoni./
Sifa iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ Kwa uvumilivu mkubwa ulikubali kufungwa nguzoni,/ kupigwa mijeledi kijeuri,/ kujaa damu na hivyo kusukumwa barazani kwa Pilato./ Ulionekana kama mwanakondoo asiye na kosa./
Heshima iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo./ Umehukumiwa Mwili wako mzima/ Mtukufu wenye kutoka damu/ ufe msalabani./ Ulichukua msalaba kwa Mabega yako Matakatifu/ na kuumwa sana./ Kwa ghadhabu walikusukuma mbele/ mpaka mahali pa mateso,/ wakakunyangβanya nguo zako./ Hivyo ulikubali kupigiliwa msalabani./
Heshima ya milele upate Wewe,/ Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipokuwa katika taabu kubwa hii,/ ulimkazia Mama yako mstahivu/ Macho yako ya hisani na mapendo/ na unyenyekevu,/ ndiye Mama yako asiyekosa hata mara moja/ wala kukubali dhambi yeyote./ Ulimweka katika ulinzi mwaminifu/ wa Mfuasi wako ili kumtuliza./
Milele utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo./ Ulipokuwa mwenyewe taabani,/ uliwapa wakosefu wote/ matumaini ya kuondolewa dhambi/ kwa kumwahidia mnyangβanyi aliyekuendea/ utukufu wa paradisi kwa huruma yako./
Sifa ya milele iwe nawe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kila saa ulipovumilia uchungu/ na taabu kubwa mno msalabani kwa ajili yetu sisi wakosefu,/ maumivu makali sana/ yaliyotoka katika majeraha yako,/ yakapenya bila huruma Roho yako Takatifu./ Yakaingia kikatili katika Moyo wako Mtakatifu/ hata ukakatika,/ ukapumua Roho yako,/ ukainama Kichwa,/ ukaweka Roho yako mikononi mwa Mungu, Baba yako./ Na baada ya kufa uliacha nyuma Mwili baridi./
Utukuzwe, ee Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa Damu yako azizi na kwa kifo chako kitakatifu/ ulizifidia roho za watu,/ ukazitoa ugenini/ na kuzipeleka kwa hisani yako katika uzima wa milele./
Milele uheshimiwe, Wewe Bwana wangu Yesu Kristo./ Siku ya tatu ulifufuka katika wafu,/ ukajionyesha kwa wafuasi wako,/ ukapaa mbinguni/ mbele ya macho yao siku ya arobaini./
Shangilio na sifa ya milele upate Wewe, Bwana wangu Yesu Kristo,/ kwa kuwa umewapelekea wafuasi wako mioyoni mwao/ Roho Mtakatifu,/ ukawasha rohoni mwao mapendo makuu ya Mungu./
Pia, utukuzwe, usifiwe na kushangiliwa milele, Bwana wangu Yesu Kristo./ Umekaa katika ufalme wako wa mbinguni/ juu ya kiti cha enzi cha Umungu wako,/ ukaishi pamoja na Viungo vyako vyote Vitakatifu./ Na hivyo utakuja tena/ kuzihukumu roho za wazima na wafu wote./ Unaishi na kutawala/ pamoja na Baba na Roho Mtakatifu,/ milele. Amina.
(Na Mt. Birgita wa Sweden)
Betty Akinyi (Guest) on June 22, 2024
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Victor Mwalimu (Guest) on May 29, 2024
Rehema hushinda hukumu
Stephen Malecela (Guest) on February 18, 2024
Endelea kuwa na imani!
John Malisa (Guest) on February 17, 2024
πππ
Stephen Malecela (Guest) on February 1, 2024
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Mary Mrope (Guest) on November 26, 2023
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
George Mallya (Guest) on September 26, 2023
πβ¨ Mungu atupe nguvu
Mary Mrope (Guest) on August 31, 2023
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Rose Amukowa (Guest) on August 28, 2023
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Chris Okello (Guest) on August 25, 2023
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Charles Mboje (Guest) on June 19, 2023
Wakati wa Mungu ni kamilifu
David Nyerere (Guest) on May 27, 2023
Tumaini ni nanga ya roho
Vincent Mwangangi (Guest) on May 5, 2023
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
Anna Malela (Guest) on April 15, 2023
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
Rose Lowassa (Guest) on March 21, 2023
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Agnes Sumaye (Guest) on February 27, 2023
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
Miriam Mchome (Guest) on January 19, 2023
πππ
Kenneth Murithi (Guest) on December 30, 2022
Dumu katika Bwana.
John Lissu (Guest) on November 21, 2022
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Charles Wafula (Guest) on November 15, 2022
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu
Alice Wanjiru (Guest) on September 27, 2022
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Alice Mwikali (Guest) on September 2, 2022
Sifa kwa Bwana!
Lucy Kimotho (Guest) on August 31, 2022
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Samuel Were (Guest) on July 19, 2022
Nguvu hutoka kwa Bwana
Diana Mallya (Guest) on March 4, 2022
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Nancy Komba (Guest) on March 3, 2022
Neema ya Mungu inatosha kwako
Rose Amukowa (Guest) on January 31, 2022
πβ¨ Mungu atakuinua
Samuel Omondi (Guest) on September 9, 2021
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Martin Otieno (Guest) on September 5, 2021
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Joyce Mussa (Guest) on August 16, 2021
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Monica Adhiambo (Guest) on August 11, 2021
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Nicholas Wanjohi (Guest) on June 2, 2021
Nakuombea π
Lucy Wangui (Guest) on April 22, 2021
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Betty Akinyi (Guest) on April 12, 2021
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Frank Sokoine (Guest) on March 16, 2021
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Alex Nyamweya (Guest) on March 15, 2021
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Lydia Mahiga (Guest) on March 3, 2021
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
James Kawawa (Guest) on December 29, 2020
Amina
Lucy Wangui (Guest) on December 27, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Bernard Oduor (Guest) on December 20, 2020
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Catherine Naliaka (Guest) on November 18, 2020
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Hellen Nduta (Guest) on November 4, 2020
ππ Mungu alete amani
Sharon Kibiru (Guest) on November 1, 2020
Mwamini Bwana; anajua njia
Mercy Atieno (Guest) on October 11, 2020
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mary Kidata (Guest) on August 21, 2020
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Susan Wangari (Guest) on June 9, 2020
ππ Nakushukuru Mungu
Linda Karimi (Guest) on May 16, 2020
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
Joseph Njoroge (Guest) on May 6, 2020
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
Sharon Kibiru (Guest) on May 1, 2020
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Diana Mumbua (Guest) on April 9, 2020
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Jane Malecela (Guest) on February 20, 2020
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Violet Mumo (Guest) on December 26, 2019
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Monica Nyalandu (Guest) on December 1, 2019
Imani inaweza kusogeza milima
John Kamande (Guest) on November 24, 2019
πππ« Mungu ni mwema
Mercy Atieno (Guest) on November 7, 2019
Mwamini katika mpango wake.
Anna Malela (Guest) on September 29, 2019
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Samuel Were (Guest) on September 16, 2019
Baraka kwako na familia yako.
Elizabeth Mrope (Guest) on August 24, 2019
Neema na amani iwe nawe.
Carol Nyakio (Guest) on July 4, 2019
Mungu akubariki!
Nicholas Wanjohi (Guest) on March 26, 2019
ππ Neema za Mungu zisikose