Sidebar with Floating Button
AckySHINE SMSπŸ’ŒπŸ’•
☰
AckyShine

LITANIA YA KUWAOMBEA MAPADRE WOTE II

Featured Image

Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji mwema
Kwa ajili ya makardinali na maaskofu wakuu; Uwape moyo wa kichungaji ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wa majimbo; Uwajaze na Roho wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre watawa; Wakamilishe katika wito wao ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre walioko hatarini; Uwaokoe ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wenye udhaifu; Uwatie nguvu ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wenye hofu; Uwape amani ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre waliokata tamaa; Uwavuvie upya ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wakaao upweke; Uwasindikize ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wamisionari; Uwalinde ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wanaohubiri; Uwaangazie ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre na watawa waliokufa; Uwafikishe kwenye utukufu wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie hekima na ufahamu wako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; Uwajalie elimu na shauri lako
Kwa ajili ya mapadre wako; wajalie wakuheshimu na wakuogope
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie subira na upendo
Kwa ajili ya mapadre wote; wajalie utii na upole
Kwa ajili ya mapadre wote; uwajalie hamu kuu ya kuokoa roho za watu
Kwa ajili ya mapadre wote; wape fadhila za imani, matumaini na mapendo
Kwa ajili ya mapadre wote; Wajalie upendo mkuu kwa Ekaristi
Tunakuomba uwajalie mapadre wote; Waheshimu uhai na hadhi ya mtu ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote nguvu na bidii katika kazi zao ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote amani katika mahangaiko yao ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote upendo mkuu kwa Utatu Mtakatifu ee Bwana
Tunakuomba uwajalie mapadre wote upendo mkuu kwa Bikira Maria ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe mwanga wa Kristo ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wawe chumvi kwa ulimwengu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wajizoeze kujitoa sadaka na kujinyima ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, wawe watakatifu kimwili, kiakili na kiroho ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe watu wa sala ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe kioo cha imani kwako ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wajali sana wongofu wetu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawe waaminifu kwa wito wao wa kikuhani ee Bwana
Uwajalie mapadre wote, ili mikono yao ibariki na kuponya ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wawake moto wa mapendo yako ee Bwana
Uwajalie mapadre wote hatua zao zote ziwe kwa ajili ya utukufu wa Mungu ee Bwana
Uwajalie mapadre wote wajazwe na Roho Mtakatifu na uwajalie karama zake kwa wingi ee Bwana.





Tuombe.
Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, usikie sala tunazokutolea kwa ajili ya mapadre wetu. Uwajalie wafahamu waziwazi kazi uliyowaitia kuifanya, uwape neema zote wanazohitaji ili waitikie wito wako kwa ushujaa, kwa upendo, na majitoleo yenye udumifu katika mapenzi yako matakatifu. Amina.


AckySHINE Solutions

Comments

Please Join AckySHINE to Participate in Discussion.

Elizabeth Mtei (Guest) on June 6, 2024

πŸ™βœ¨πŸ’– Mungu atajibu maombi yako

Lydia Mahiga (Guest) on April 20, 2024

πŸ™βœ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike

Janet Mwikali (Guest) on March 28, 2024

πŸ™πŸŒŸ Mbarikiwe sana

Joseph Kitine (Guest) on February 20, 2024

Tembea kwa imani, si kwa kuona

Miriam Mchome (Guest) on October 26, 2023

Mwamini Bwana; anajua njia

Lydia Mahiga (Guest) on October 8, 2023

πŸ™πŸ’– Nakushukuru Mungu

Edward Lowassa (Guest) on July 19, 2023

πŸ™πŸ’– Asante kwa neema zako Mungu

Grace Njuguna (Guest) on June 22, 2023

Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe

Nicholas Wanjohi (Guest) on May 16, 2023

πŸ™β€οΈ Mungu ni mkombozi

Andrew Odhiambo (Guest) on May 13, 2023

πŸ™πŸŒŸ Namuomba Mungu akupiganie

Ruth Wanjiku (Guest) on March 15, 2023

Baraka kwako na familia yako.

Paul Kamau (Guest) on November 11, 2022

πŸ™β€οΈ Mungu ni mlinzi wetu

Josephine Nduta (Guest) on October 30, 2022

πŸ™βœ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku

Patrick Kidata (Guest) on September 28, 2022

πŸ™πŸŒŸ Neema za Mungu zisikose

Edith Cherotich (Guest) on August 4, 2022

Kwa Mungu, yote yanawezekana

Jane Muthui (Guest) on February 28, 2022

πŸ™βœ¨ Mungu atupe nguvu

Andrew Odhiambo (Guest) on January 24, 2022

Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi

Sarah Mbise (Guest) on November 21, 2021

Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote

Ruth Kibona (Guest) on October 7, 2021

πŸ™πŸ’– Mungu wetu asifiwe

Tabitha Okumu (Guest) on August 17, 2021

πŸ™πŸ’– Nakusihi Mungu

Brian Karanja (Guest) on August 16, 2021

Tumaini ni nanga ya roho

Kevin Maina (Guest) on June 20, 2021

Neema na amani iwe nawe.

Lucy Mushi (Guest) on May 5, 2021

Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake

Irene Akoth (Guest) on March 31, 2021

Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida

Agnes Lowassa (Guest) on March 29, 2021

πŸ™β€οΈβœ¨ Mungu akujalie furaha

Joyce Mussa (Guest) on March 25, 2021

πŸ™πŸ’–βœ¨ Neema yako ni ya kutosha

Rose Waithera (Guest) on March 1, 2021

πŸ™πŸŒŸβ€οΈ Nakuombea heri

Anthony Kariuki (Guest) on February 25, 2021

Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia

Patrick Kidata (Guest) on February 19, 2021

πŸ™β€οΈ Mungu ni mwaminifu

Edward Lowassa (Guest) on January 4, 2021

Neema ya Mungu inatosha kwako

Michael Onyango (Guest) on September 5, 2020

Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi

Anthony Kariuki (Guest) on August 12, 2020

Nakuombea πŸ™

Victor Kamau (Guest) on June 8, 2020

Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini

Edward Chepkoech (Guest) on April 14, 2020

πŸ™β€οΈβœ¨ Asante Mungu kwa kila kitu

Anna Sumari (Guest) on January 6, 2020

Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia

Alex Nyamweya (Guest) on December 4, 2019

Wakati wa Mungu ni kamilifu

Linda Karimi (Guest) on November 21, 2019

Bwana yuko karibu na wote wanaomwita

Anna Kibwana (Guest) on September 27, 2019

Mungu ni mwema, wakati wote!

Nicholas Wanjohi (Guest) on August 18, 2019

Endelea kuwa na imani!

Victor Sokoine (Guest) on July 18, 2019

Sifa kwa Bwana!

Victor Mwalimu (Guest) on May 11, 2019

πŸ™βœ¨ Mungu atakuinua

David Kawawa (Guest) on January 10, 2019

Amina

James Mduma (Guest) on November 27, 2018

Rehema hushinda hukumu

Betty Cheruiyot (Guest) on November 13, 2018

Nguvu hutoka kwa Bwana

Benjamin Kibicho (Guest) on October 21, 2018

πŸ™πŸ™πŸ™

Moses Kipkemboi (Guest) on October 1, 2018

Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi

Wilson Ombati (Guest) on August 12, 2018

Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu

Samson Tibaijuka (Guest) on July 4, 2018

Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu

Alice Mrema (Guest) on May 20, 2018

πŸ™πŸŒŸ Mungu alete amani

Josephine Nduta (Guest) on May 7, 2018

πŸ™β€οΈπŸŒŸ Asante Mungu kwa uhai

Charles Mrope (Guest) on May 5, 2018

Mungu akubariki!

Stephen Kangethe (Guest) on March 13, 2018

πŸ™β€οΈ Mungu akubariki

Samson Tibaijuka (Guest) on March 12, 2018

Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima

Stephen Kikwete (Guest) on January 21, 2018

πŸ™β€οΈπŸ’– Bwana akujalie baraka

Lydia Mahiga (Guest) on January 14, 2018

Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni

Fredrick Mutiso (Guest) on January 12, 2018

Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha

Ann Awino (Guest) on January 9, 2018

πŸ™β€οΈπŸ’– Tumshukuru Mungu kwa yote

Agnes Njeri (Guest) on November 23, 2017

Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia

Joseph Kawawa (Guest) on October 11, 2017

Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu

Janet Sumari (Guest) on September 30, 2017

πŸ™πŸ’–πŸ’« Mungu ni mwema

Related Posts

SALA YA IMANI

SALA YA IMANI

Mungu wangu,

nasadiki maneno yote linalosadiki na linalofundisha kanisa katoliki la Roma;Read More

SALA YA KUTUBU

SALA YA KUTUBU

Mungu wangu ninatubu sana, niliyokosa kwako, kwani ndiwe mwema, ndiwe mwenye kupendeza, wachukiz... Read More

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

KUJIWEKA CHINI YA ULINZI WA MT. YOSEFU

Ee Mt. Yosefu, Baba Mlishi wa Mwokozi wangu, na mchumba safi wa Mama wa Mungu, leo ninakuchagua w... Read More

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

SALA YA KUOMBEA FAMILIA

Ewe Mungu Mwenyezi, sisi kama familia tunakushukuru kwa zawadi ya Mama Kanisa Katoliki ambaye sik... Read More

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

SALA YA KUUABUDU MOYO MTAKATIFU WA YESU KATIKA EKARISTI TAKATIFU

Kwa nguvu zangu zote za moyo wangu/ ninakuabudu ee Moyo Mtakatifu/ na Mwabudiwa sana,/ Moyo Mtaka... Read More

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

SALA YA BWANA: SALA YA BABA YETU

Baba yetu uliye mbinguni
Jina lako litukuzwe
Ufalme wako ufike
Utakalo lifanyikeRead More

Sala ya Saa Tisa

Sala ya Saa Tisa

✝⌚✝

Sala ya saa tisaπŸ™πŸΎ

Kwa jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu.... Read More

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

SALA MBELE YA SAKRAMENTI KUU II

Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.... Read More

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Majitoleo ya asubuhi kwa Bikira Maria

Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sal... Read More

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

SALA KWA MAMA WA UCHUNGU KUOMBA NEEMA YA PEKEE

Ee Mama mbarikiwa na Bikira mwenye uchungu, Malkia wa Mashahidi, uliyesimama chini ya msalaba na ... Read More

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli

Novena ya Noeli (maarufu kama novena ya Mt. Andrea)

Husaliwa kuanzia tar 30 Nov hadi usiku ... Read More

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Sala kwa Mtakatifu Yosefu

Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wa... Read More