SALA YA ASUBUHI
Tuusifu Utatu Mtakatifu wa Mungu Mwenyezi, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, milele na milele, Amina.
Ee Utatu Mtakatifu wa Mwenyezi Mungu, Baba, Mwana na Roho Mtakatifu, nasadiki kuwa upo hapa na mahali pote. Ee Mungu wangu, umeniumba, umenikomboa, umenifanya mkristo, umenizidishia neema zako hapa duniani, umenitayarishia makao yangu mbinguni, umenijalia na siku hii nikutumikie. Ee Mungu wangu! Nakuabudu, nakushukuru, nakuomba toba, nakupenda! Ee Mungu wangu, nakutolea roho yangu, na mawazo, na maneno, na kazi, na furaha, na mateso yangu: uyapokee unipe neema yako nisikutende leo dhambi!
Majitoleo ya Asubuhi
Ee Baba yetu Mungu Mkuu, Umenilinda usiku huu, Ninakushukuru kwa moyo, Ee Baba, Mwana na Roho, Nilinde tena siku hii, Niache dhambi nikutii, Naomba sana Baba wee, Baraka yako nipokee, Bikira safi ee Maria, Nisipotee unisimamie, Mlinzi Mkuu Malaika wee, Kwa Mungu wetu niombee, Nitake nitende mema tu, Na mwisho nije kwake juu, Amina.
Kuweka nia njema
Kumheshimu Mungu wangu, Namtolea roho yangu, Nifanye kazi nipumzike, Amri zake tu nishike, Wazo neno tendo lote, Namtolea Mungu pote, Roho, mwili chote changu, pendo na uzima wangu, Mungu wangu nitampenda, Wala dhambi sitatenda, Jina lako nasifia, Utakalo hutimia, Kwa utii navumilia, Teso na matata pia, Nipe Bwana neema zako, Niongezee sifa yako, Amina.
Majitoleo
Ee Yesu, kupitia mikono safi ya Bikira Maria, na kwa maungano na sadaka yako kuu, ninakutolea sala, matendo, kazi, masumbuko, na furaha zangu zote za siku hii ya leo, kwa ajili ya nia za Moyo wako Mtakatifu, Ee Yesu ufalme wako utufikie!
Baba Yetu….
Salamu Maria, …..
Nasadiki …….
Amri za Mungu ……
Amri za Kanisa ……
Sala ya Malaika wa Bwana
Malaika wa Bwana alimpasha habari Maria, naye akapata mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu. Salamu Maria,….
Ndimi Mtumishi wa Bwana, nitendewe ulivyonena. Salamu Maria, ……
Neno wa Bwana akatwaa Mwili, akakaa kwetu. Salamu Maria, …..
Utuombee, ee Mzazi Mtakatifu wa Mungu, tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe:
Tunakuomba ee Bwana, utie neema yako mioyoni mwetu, ili sisi tuliojua kwa maelezo ya Malaika, kwamba, Kristo Mwanao amejifanya mtu: kwa mateso na Msalaba wake, utufikishe kwenye utukufu wa ufufuko. Tunaomba hayo kwa njia ya Kristo Bwana wetu, Amina.
Sala kwa Malaika Mlinzi
Ee Malaika wangu, uliyewekwa na Mungu mwema unilinde, naomba uniongoze leo, unitunze, unisimamie, unishauri. Amina.
Sala kwa wenye kuzimia
Ee Yesu mwenye huruma, mpenda roho za watu, nakuomba kwa ajili ya kuzimia kwa Moyo wako Mtakatifu, na kwa ajili ya Mama Yako asiye na doa, uwatakase kwa damu yako, watu wote wenye dhambi wanaokufa sasa, na watakaokufa leo.
Moyo wa Yesu uliozomia, uwahurumie watu wanaokufa X3.
Sala kwa Mtakatifu Yosef
Ee Yosef mwenye heri, tunakimbilia kwako, katika masumbuko yetu, na kishaomba shime ya Mchumba wako Mtakatifu, tunaomba pia kwa matumaini usimamizi wako. Kwa ajili ya mapendo uliyompenda nayo Bikira Mtakatifu, Mzazi wa Mungu, na kwa ajili ya tunza ya Baba, uliyomtunza nayo Mtoto Yesu, tunakuomba sana, utuangalie kwa wema, sisi tuliokuwa fungu lake Yesu Kristo, tuliokombolewa kwa damu yake, utusimamie katika masumbuko yetu, kwa enzi na shime yako.
Ee Mlinzi amini wa Jamaa Takatifu, uwakinge watoto wateule wa Yesu Kristo, ee Baba uliyetupenda mno, utuepusha na kilema chochote cha madanganyo na upotevu. Ee kinga yetu mwezaji,utusimamie huko juu mbinguni ulipo, tunaposhindana na wenye nguvu wakaao gizani. Kama vile siku za kale ukamwokoa Mtoto Yesu katika hatari ya kuuawa, na leo hivi, ulikinge Kanisa Takatifu la Mungu katika mitego ya adui, na katika shida yote, mtunze daima kila mmoja wetu, tupate mfano wako, tusaidie kwa msaada wako, kukaa na utakatifu maisha, kufa kifo chema, na kupokelewa mbinguni makao ya raha milele. Amina
Sala kwa Mtakatifu Yuda Thadei
(Sala hii inaweza kusaliwa kila siku au kama Novena ya siku tisa mfululizo kuomba kitu kilekile)
Mtakatifu Yuda Tadei,/ Mtume Mtakatifu,/ Mtumishi mwaminifu na rafiki wa Yesu./ Jina la yule msaliti aliyemwuza Yesu/ limewafanya wengi wakusahau./ Walakini Kanisa zima linakuheshimu/ na kukuomba kama Msaidizi katika mashaka makubwa,/ na katika mambo yasiyo na matumaini tena./
Uniombee mimi mnyonge./ Ninaomba utumie uwezo ule uliojaliwa/ wa kuleta upesi msaada kwa watu walioukosa./ Unisaidie sasa katika mahitaji yangu,/ ili nipate kitulizo na msaada wa mbinguni/ katika lazima zangu,/ masumbuko na mateso,/ hasa/ (taja shida yako)./ Pia ili niweze kumsifu Mungu nawe na wateule wote milele./
Mtakatifu Yuda Tadei,/ utuombee,/ na uwaombee watu wote wanaokuheshimu na kukuomba msaada./
Baba yetu……. Salamu Maria ……… Atukuzwe ……….
Sala ya Medali ya Mwujiza
Ee Bikira Maria uliyekingiwa dhambi ya asili, utuombee sisi wenye kukimbilia kwako, uwaombee na wale wasioukimbilia kwako, hasa maadui wa Kanisa Takatifu, na wale waliokabidhiwa kwako. Amina.
Majitoleo kwa Bikira Maria
(Sala iliyotungwa na Mtk. Aloisi)
Bibi yangu mtukufu Maria, nakuwekea amana ya roho yangu na mwili wangu, nikikuomba uipokee amana yangu, kuitunzia ulinzi mwema ulinzi bora, ninakuaminia na kila neno langu, matumaini na kitulizo na kisongo chote, na masumbuko na uzima na ukomo wa uzima wangu: nitakayo ndiyo unifanyizie kwa maombezi na stahili zako, ili mambo yangu yote yapate kuongoka, yakiwa na kufuata mapenzi yako, pamoja na mapenzi ya Mwanao. Amina.
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
🙏❤️ Mungu akubariki
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
🙏🌟 Mbarikiwe sana
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Mungu akubariki!
Baraka kwako na familia yako.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
🙏💖 Nakusihi Mungu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie
Mwamini katika mpango wake.
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
🙏🌟 Mungu akujalie amani
🙏✨ Mungu atupe nguvu
Nguvu hutoka kwa Bwana
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Endelea kuwa na imani!
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
🙏🌟 Mungu alete amani
Nakuombea 🙏
Sifa kwa Bwana!
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Rehema zake hudumu milele
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Rehema hushinda hukumu
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
🙏💖 Nakushukuru Mungu
Amina
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tumaini ni nanga ya roho
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
Dumu katika Bwana.
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
🙏🙏🙏
🙏💖💫 Mungu ni mwema
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
Tembea kwa imani, si kwa kuona
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Neema ya Mungu inatosha kwako
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
🙏🙏🙏
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
Mwamini Bwana; anajua njia
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Neema na amani iwe nawe.
Katika imani, yote yanawezekana
🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
🙏✨ Mungu atakuinua
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Imani inaweza kusogeza milima