Yesu, Mungu wangu mpenzi,/ upo hapa katika Altare mbele yangu;/ na mimi napiga magoti mbele yako.// Waniangalia sana,/ siyo kwa kunipeleleza,/ lakini kwa sababu wapenda kuniona hivi karibu na wewe,/ wafurahiwa nikija kukuabudu./ Wayasikiliza maneno yangu yote/ yenye kutoka mdomoni mwangu,/ na zaidi wapokea maneno yangu yanayotoka moyoni./ Nataka kuzungumza na wewe peke yako,/ na kusahau mambo mengine yote/ na watu wengine walioko kanisani pamoja nami./
Yesu wangu,/ nakushukuru/ kwa sababu umekubali kutupa Sakramenti hii kuu kabisa,/ ukitaka kukaa pamoja na sisi,/ na hata ukakubali kuwa chakula chetu/ chenye nguvu ya ajabu./ Mfalme wangu Yesu,/ Sultani wangu Mkuu,/ naamini kabisa kwamba upo katika Altare/ na kwamba umejificha chini ya umbo la mkate./ Ulipokuwapo bado hapa duniani mbele za watu,/ ulikuwa hujifichi kama sasa;/ lakini hata siku zile/ watu hawakuweza kukuona vile ulivyo./ Hawakuweza kuutambua Umungu wako,/ ikalazimu kukuamini tu sawa kama sisi./ Wakainama kichwa wakisema,/ โBwana wangu na Mungu wanguโ./ Na mimi kadhalika naungama/ U Bwana wangu na Mungu wangu/ na Mkombozi wangu/ na salama yangu yote./ U Yesu wangu tu,/ siwezi kusema zaidi./ Nakuabudu ee Yesu./ Najua sana, mimi ni mdogo kabisa,/ sina maana hata kidogo./ Mimi ni dhaifu na maskini mno./ Lakini Wewe katika hruuma yako kubwa/ waniita nije kwako./ Wewe huuangalii umaskini wangu,/ bali wanivuta katika mapendo yako./
Nasikia maneno yako usemayo:/ โNjooni kwangu ninyi nyote mnaoelemewa na mizigo/ nami nitawasaidiaโ./ Kwa ajili ya maneno hayo/ nakuja kwako bila hofu./ Najua kwamba wanipenda,/ najua wataka kunisaidia na kuniponya,/ najua kuwa wataka kunitakasa./
Nahitaji sana msaada wako, hakika./ Unaniona katika mwendo wangu wa kila siku,/ Jinsi ninavyohangaika na vishawishi mara nyingi;/ jinsi nilivyo na lazima ya kushindana kila siku/ nikitaka kukaa mwema na safi katika utumishi wako./ Naungama mbele yako Wewe Mkombozi wangu,/ kwamba sikukaa imara siku zote vile nilivyopaswa./ Naungama kwamba nimeshindwa mara nyingine/ na kwa hivi naomba toba./ Lakini kwa nini nimeshindwa mara nyingine?/ Kwa nini nikakosa?/ Ni kwa sababu nalikuwa nimekwenda mbali nawe;/ nalianza kujitegemea mwenyewe./ Katika majivuno yangu nikajisifu mwenyewe,/ nikajiona mwema,/ nikasahau udhaifu wangu./ Na kwa ajili hiyo nikajitia katika hatari bure,/ sikujilinda tena,/ nikampa shetani nafasi ya kunishambulia kwa hila zake zote./ Unihurumie ee Yesu wangu./
Sasa nafahamu jinsi nilivyokuwa mjinga kwelikweli./ Ndiyo maana nakuabudu kwa moyo wangu wote./ Najiweka mikononi mwako/ ufanye nami vile unavyotaka./ Wewe utanitunza;/ Wewe utanilinda vema;/ Wewe utaniongoza nijue namna ya kuepa hatari zote,/ na jinsi ya kufukuza kila kishawishi./ Chukua moyo wangu kabisa,/ kwa sababu ni mali yako kamili;/ Wewe ndiwe uliyeniumba,/ ndiwe uliyenipeleka katika Ukristo,/ nawe ndiwe utakayenihukumu siku ya mbele./ Ndivyo ninavyojitolea kwako./ Ndivyo ninavyokuabudu,/ wala sijui njia nyingine ya kukusifu zaidi./
Yesu wangu mpenzi,/ naomba upokee kwa uzuri heshima hiyo yangu./ Angalia: naitolea pamoja na heshima yote/ unayopewa daima na watakatifu wako/ na malaika wako./ Nikipiga magoti hapa mbele yako sasa,/ siko peke yangu,/ nakuabudu pamoja na Mama yako Bikira Maria,/ ambaye sala zake zinakupendeza kabisa./ Sala zangu naweka pamoja na sala zake yeye,/ uzipokee zote pamoja,/ zikupendeze zote sawa./ Ee Mama Maria!/ Nifundishe maneno ya kumsifu Mwanao Yesu vizuri./ Nipeleke kwa Yesu tumwabudu pamoja./ Nifunike na utakatifu wako/ kusudi Yesu asiangalie tena umaskini wangu/ na makosa yangu,/ aniponye katika huruma yake./
Sasa najisikia vizuri, Yesu wangu./ Sasa nina moyo wa kuweza kuendelea vema/ katika njia njema./ Sasa ninatumaini kwamba/ nitakaa mkristo mwema,/ nitakuwa mtumishi wako mwaminifu./ Nasikia amani kubwa sana moyoni mwangu,/ kwa kuwa nimo mikononi mwako./ Baada ya dakika chache/ nitaondoka tena kanisani,/ nitarudi nyumbani kwangu,/ lakini hatutaachana,/ hapana./ Mapendo yetu yatatuunganisha pamoja daima./ Wewe utanikumbuka nikiwa kazini,/ nikilala usingizi,/ nikienda njiani,/ kila mahali nilipo,/ Wewe utaniona,/ utafuatana na mimi./ Kadhalika nitakukumbuka tu./ Nitafanya bidii nisikuache kabisa./ Amina.
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
๐๐ Neema za Mungu zisikose
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Rehema zake hudumu milele
๐โค๏ธ Mungu ni mlinzi wetu
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
๐๐๐
Nakuombea ๐
๐โจ Mungu atupe nguvu
๐โค๏ธ Mungu ni mkombozi
๐๐โค๏ธ Nakuombea heri
๐โค๏ธโจ Mungu akujalie furaha
๐๐ Nakusihi Mungu
Imani inaweza kusogeza milima
๐โจ Mungu atakuinua
๐โค๏ธ๐ Bwana akujalie baraka
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Nguvu hutoka kwa Bwana
Endelea kuwa na imani!
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
๐โจ Mungu asikie maombi yetu
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
๐๐ Mungu alete amani
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
๐๐ Asante kwa neema zako Mungu
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Dumu katika Bwana.
Rehema hushinda hukumu
Tumaini ni nanga ya roho
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Baraka kwako na familia yako.
๐โค๏ธ Mungu akubariki
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
๐โค๏ธ๐ Asante Mungu kwa uhai
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
๐๐๐ Mungu akufunike na upendo
๐โจโค๏ธ Tumwombe Mungu kila siku
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Tembea kwa imani, si kwa kuona
๐โจ๐ Mungu atajibu maombi yako
๐๐ Namuomba Mungu akupiganie
Mwamini katika mpango wake.
๐๐ Mbarikiwe sana
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
๐๐โจ Neema yako ni ya kutosha
๐โค๏ธ Mungu ni mwaminifu
Katika imani, yote yanawezekana
Amina
๐๐ Mungu wetu asifiwe
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
๐๐ Nakushukuru Mungu
๐๐๐
๐โจโค๏ธ Neema za Mungu zikufunike
๐โค๏ธ๐ Baraka za Mungu ziwe nawe
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
๐๐ Mungu akujalie amani
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Neema ya Mungu inatosha kwako
Mungu akubariki!
Sifa kwa Bwana!
๐โค๏ธ๐ Tumshukuru Mungu kwa yote
Mwamini Bwana; anajua njia
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
๐๐๐ซ Mungu ni mwema
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
๐โจ Neema ya Mungu iwe nawe
Neema na amani iwe nawe.
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
๐โค๏ธโจ Asante Mungu kwa kila kitu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Kwa Mungu, yote yanawezekana