Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie Bwana utuhurumie
Kristo utusikie Kristo utusikilize
Baba wa mbinguni Mungu Utuhurumie
Mwana, Mkombozi wa dunia Mungu Utuhurumie
Roho Mtakatifu Mungu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu mmoja Utuhurumie
Moyo wa Yesu Mwana wa Baba wa Milele Utuhurumie
Moyo wa Yesu uliotungwa na Roho Mtakatifu mwilini mwa Mama Bikira Maria Utuhurumie
Moyo wa Yesu ulioungana na Neno wa Mungu Utuhurumie
Moyo wa Yesu ulio na utukufu pasipo mfano Utuhurumie
Moyo wa Yesu, hekalu takatifu la Mungu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, hema la Yule aliye juu Utuhurumie
Moyo wa Yesu tanuru lenye kuwaka mapendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, nyumba ya Mungu na mlango wa Mbingu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, tanuru yenye kuwaka mapendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chombo cha haki na upendo Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaojaa upendo na wema Utuhurumie
Moyo wa Yesu, kilindi cha fadhila zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaostahili sifa zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unaotawala mioyo yote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, zinamokaa hazina za hekima na elimu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliopendelewa na Mungu Baba Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliotuenezea maziada yake Utuhurumie
Moyo wa Yesu, mtamaniwa wa vilima vya milele Utuhurumie
Moyo wa Yesu, wenye uvumilivu na huruma nyingi Utuhurumie
Moyo wa Yesu, tajiri kwa wote wenye kukuomba Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chemchemi ya uzima na utakatifu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, malipo kwa dhambi zetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, ulioshibishwa matusi Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliovunjika kwa sababu ya ubaya wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliotii mpaka kufa Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uliochomwa kwa mkuki Utuhurumie
Moyo wa Yesu, chemchemi ya faraja zote Utuhurumie
Moyo wa Yesu, uzima na ufufuo wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, amani na upatanisho wetu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, sadaka ya wakosefu Utuhurumie
Moyo wa Yesu, unamokaa wokovu wao wenye kukutumaini Utuhurumie
Moyo wa Yesu, matumaini yao wenye kuzimia kwako Utuhurumie
Moyo wa Yesu, sababu ya furaha ya watakatifu wote Utuhurumie
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusamehe Bwana
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utusikilize Bwana
Mwanakondoo wa Mungu, uondoaye dhambi za dunia Utuhurumie
Kiongozi: Yesu mwenye Moyo mpole na mnyenyekevu,
Wote: Ufanye mioyo yetu ifanane na Moyo wako
TUOMBE: (W) Ee Mungu Mwenyezi milele, uuangalie Moyo wa mwanao mpendelevu, pia na heshima na malipo aliyokutolea kwa ajili ya wenye dhambi, uridhike, uwaondolee wenye kuomba toba kwako kwa njia ya huyo Mwanao Yesu Kristo anayeishi na kutawala nawe pamoja na Roho Mtakatifu, Mungu milele. Amina.
πβ€οΈ Mungu ni mkombozi
ππ Mbarikiwe sana
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
πβ€οΈ Mungu ni mwaminifu
πβ¨ Mungu atupe nguvu
ππ Nakusihi Mungu
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
πβ€οΈ Mungu ni mlinzi wetu
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Dumu katika Bwana.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
πβ€οΈπ Baraka za Mungu ziwe nawe
Mwamini katika mpango wake.
πβ€οΈπ Asante Mungu kwa uhai
Imani inaweza kusogeza milima
Sifa kwa Bwana!
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
ππ Mungu alete amani
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
πβ€οΈπ Tumshukuru Mungu kwa yote
Nakuombea π
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
πππ
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Neema ya Mungu inatosha kwako
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
ππ Neema za Mungu zisikose
πβ€οΈ Mungu akubariki
ππ Mungu akujalie amani
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Rehema zake hudumu milele
πβ¨π Mungu atajibu maombi yako
πβ¨ Neema ya Mungu iwe nawe
ππ Asante kwa neema zako Mungu
Baraka kwako na familia yako.
ππβ¨ Neema yako ni ya kutosha
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Neema na amani iwe nawe.
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
πππ« Mungu ni mwema
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
ππβ€οΈ Nakuombea heri
Tumaini ni nanga ya roho
Amina
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Mungu akubariki!
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
πβ¨β€οΈ Tumwombe Mungu kila siku
Katika imani, yote yanawezekana
Kwa Mungu, yote yanawezekana
πβ€οΈπ Bwana akujalie baraka
πβ¨β€οΈ Neema za Mungu zikufunike
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
πβ¨ Mungu asikie maombi yetu
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Rehema hushinda hukumu
ππ Mungu wetu asifiwe
πβ¨ Mungu atakuinua
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
πππ Mungu akufunike na upendo
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
ππ Nakushukuru Mungu
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
Mwamini Bwana; anajua njia
ππ Namuomba Mungu akupiganie
Endelea kuwa na imani!
πππ
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
πβ€οΈβ¨ Mungu akujalie furaha
πβ€οΈβ¨ Asante Mungu kwa kila kitu