Kwa ajili ya Baba Mtakatifu wetu ..(N); Bwana, umpe moyo wako wa uchungaji mwema
Kwa ajili ya warithi wa Mitume; Bwana, uwape wawe na uangalifu uliojaa upendo kwa mapadre wao
Kwa ajili ya Maaskofu wako waliochaguliwa na Roho Mtakatifu; Bwana, uwabakishe karibu na kondoo wako
Kwa ajili ya wachungaji wako; Bwana, uwafundishe kutumikia kuliko kutafuta kutumikiwa
Kwa ajili ya waungamishi na washauri wa kiroho; Bwana, uwafanye kuwa vyombo visikivu kwa Roho wako Mtakatifu
Kwa ajili ya mapadre wanaotangaza neno lako; Bwana, uwawezeshe kushirikisha Roho wako na Uzima wako
Kwa ajili ya mapadre wanaosaidia utume wa walei; Bwana, uwatie moyo wa kuwa mifano bora
Kwa ajili ya mapadre wanaofanya kazi na vijana; Bwana, uwajalie wawakabidhi vijana kwako
Kwa ajili ya mapadre wanaofanya kazi kati ya watu fukara; Bwana, uwajalie wakuone na wakutumikie kupitia hao
Kwa ajili ya mapadre wanaoangalia wagonjwa; Bwana, uwajalie wawafundishe thamani ya mateso
Kwa ajili ya mapadre fukara; – Uwasaidie ee Bwana
Kwa ajili ya mapade wagonjwa; – Uwaponye ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wazee; – Uwapatie tumaini la raha ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wenye huzuni na walioumizwa; -Uwafariji ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wanaohangaishwa na wale wanaosumbuliwa; – Uwape amani yako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wanaodharauliwa na wanaonyanyaswa; – Uwatetee ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre waliokata tamaa; – Uwatie moyo ee Bwana
Kwa ajili ya wale wanaosomea upadre; – Uwape udumifu ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; – Uwape uaminifu kwako na kwa Kanisa lako ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; – Uwajalie utii na upendo kwa Baba Mtakatifu na kwa maaskofu wao ee Bwana
Kwa ajili ya mapadre wote; – Uwajalie waishi katika umoja na maaskofu wao ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote; – Wawe wamoja kama Wewe na Baba mlivyo wamoja ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote; – Waishi na kuendeleza haki yako ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote; – Washirikiane katika umoja wa ukuhani wako ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote, wakiwa wamejawa na uwepo wako; – Waishi maisha yao ya useja kwa furaha ee Bwana
Tunawaombea mapadre wote; – Wajalie ukamilifu wa Roho wako na uwageuze wafanane nawe ee Bwana
Kwa namna ya pekee, ninawaombea mapadre wale ambao kwa njia yao nimepokea neema zako. Ninamwombea padre aliyenibatiza na wale walioniondolea dhambi zangu, wakinipatanisha na Wewe na Kanisa lako.
Ninawaombea mapadre ambao nimeshiriki Misa walizoadhimisha, na walionipa Mwili wako kama chakula. Ninawaombea mapadre walionishirikisha Neno lako, na wale walionisaidia na kuniongoza kwako. Amina.
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
🙏❤️🌟 Asante Mungu kwa uhai
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Baraka kwako na familia yako.
Dumu katika Bwana.
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
🙏💖 Nakusihi Mungu
🙏🌟 Mungu alete amani
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
🙏🙏🙏
Neema na amani iwe nawe.
Rehema hushinda hukumu
🙏✨ Mungu atupe nguvu
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Nakuombea 🙏
🙏❤️💖 Tumshukuru Mungu kwa yote
🙏❤️💖 Bwana akujalie baraka
🙏💖 Mungu wetu asifiwe
Rehema zake hudumu milele
🙏🌟 Namuomba Mungu akupiganie
Tembea kwa imani, si kwa kuona
🙏✨❤️ Neema za Mungu zikufunike
Nguvu hutoka kwa Bwana
Endelea kuwa na imani!
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Katika imani, yote yanawezekana
Mungu ni mwema, wakati wote!
Amina
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Neema ya Mungu inatosha kwako
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
🙏🌟 Mbarikiwe sana
🙏🌟 Neema za Mungu zisikose
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake
🙏❤️ Mungu akubariki
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Mwamini Bwana; anajua njia
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Tumaini ni nanga ya roho
🙏✨❤️ Tumwombe Mungu kila siku
🙏🙏🙏
Imani inaweza kusogeza milima
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
🙏💖✨ Neema yako ni ya kutosha
🙏🌟❤️ Nakuombea heri
🙏💖💫 Mungu ni mwema
🙏✨💖 Mungu atajibu maombi yako
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
🙏✨ Mungu asikie maombi yetu
🙏❤️ Mungu ni mwaminifu
🙏❤️ Mungu ni mlinzi wetu
🙏❤️ Mungu ni mkombozi
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
🙏✨ Neema ya Mungu iwe nawe
Mungu akubariki!
Mwamini katika mpango wake.
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
🙏❤️💖 Baraka za Mungu ziwe nawe
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
🙏💖🙏 Mungu akufunike na upendo
🙏✨ Mungu atakuinua
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
🙏🌟 Mungu akujalie amani
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
🙏❤️✨ Asante Mungu kwa kila kitu
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Sifa kwa Bwana!
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
🙏❤️✨ Mungu akujalie furaha
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
🙏💖 Asante kwa neema zako Mungu
🙏💖 Nakushukuru Mungu
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao