Mtu ni kiumbe pekee chenye mwili na roho kilichoumbwa kwa sura na mfano wa Mungu. Mungu alipotaka kumuumba mtu alisema “Tumfanye mtu kwa mfano wetu na sura yetu” (Mwa. 1:26-27)
Kuumbwa kwa sura na mfano wa Mungu maana yake tuna roho zenye akili na utashi yaani uwezo wa kutofaitisha mema na mabaya na zitakazoishi milele.
Watu wa kwanza walikua ni Adamu na Eva(Hawa), ambapo Adamu aliumbwa kwa udongo na kupuliziwa roho yenye uhai, na Eva aliumbwa kwa mfupa wa ubavu wa Adamu, akamtia roho (Mwa 2:7 na Mwa 2:21-24)
Baada ya kuumba watu Mungu aliwafundisha Dini, ambapo Dini ni mabo yatupasayo kutenda kwa Mungu Bwana wetu na Baba yetu
Mungu ametuumba ili tumjue, tumpende, tumtumikie tulipo wazima hapa duniani hata mwisho tukishakufa tuende kwake Mbinguni katika makao ya raha milele (Mwa. 2:7; Mt 19:17; Yoh 14:1-3 na Yoh 17:24).
Mungu ametuumba ili tumjue, tumpende, tumtumikie tulipo wazima hapa duniani hata mwisho tukishakufa tuende kwake Mbinguni katika makao ya raha milele (Mwa. 2:7; Mt 19:17; Yoh 14:1-3 na Yoh 17:24).
Mungu aliwapa watu wa kwanza neema ya utakaso na neema nyingine nyingi na kukaa paradisi wenye heri bila kufa (Mwa 2:16-17), Lakini Adamu na Eva walitenda dhambi ya kutotii, wakataka kuwa kama Mungu lakini bila Mungu na pasipo kufuata maagizo ya Mungu.(Mwa 3:1-16)
Dhambi ya asili na kosa la Adamu na Eva
Adamu na Eva walitenda dhambi ya asili ambayo ni hali ya kukosa utakatifu na hali ya asili ya urafiki na Mungu ambayo kila binadamu anazaliwa nayo.
Baada ya kutenda dhambi yao ya kiburi na uasi walipewa adhabu zifuatazo;
- Walipoteza neema ya utakaso
- Walifukuzwa paradisini
- Walipungukiwa na akili na kushikwa na tamaa ya kutenda dhambi
- Walipata mahangaiko na tabu nyingi
- Kupaswa kufa (Mwa 3:16-20; 5:5)
Baada ya kosa la Adamu Mungu aliahidi kuwaletea Mkombozi. (Mwa 3;15)
Mwamini katika mpango wake.
Nakuombea 🙏
Imani ni kuwa na uhakika wa kile tunachotarajia na kujua kwa hakika kile ambacho hatuoni
Nguvu hutoka kwa Bwana
Mungu akubariki!
Endelea kuamini, hata ikiwa ni vigumu kuona njia
Wakati wa Mungu ni kamilifu
Wacha imani yako iwe kubwa kuliko hofu yako
Ahadi za Mungu ni za kweli daima
Neema na amani iwe nawe.
Mungu ni mwema, wakati wote!
Mungu ni mwaminifu; hatakuacha kamwe wala hatakupungukia
Tumaini ni nanga ya roho
Upendo wa Mungu na rehema zake havikosei kamwe
Rehema zake hudumu milele
Hadithi yako haijaisha; Mungu bado anaandika
Endelea kuwa na imani!
Mungu ana mpango kwa ajili yako, muamini
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Imani inakua imara zaidi wakati wa majaribu
Katika uwepo wake, kuna ukamilifu wa furaha
Rehema hushinda hukumu
Mungu ana kusudi hata katika maumivu yako
Baraka kwako na familia yako.
Dumu katika Bwana.
Rehema za Mungu ni kubwa kuliko kosa lolote
Wacha nuru yako iangaze mbele ya wengine
Tembea kwa imani, si kwa kuona
Hauko peke yako; Mungu yuko nawe
Upendo wa Mungu haukosei kamwe.
Bwana atapigana kwa ajili yako; wewe unahitaji tu kutulia
Sifa kwa Bwana!
Imani inaweza kusogeza milima
Katika giza, nuru yake inaangaza zaidi
Mungu ni kimbilio letu na nguvu zetu, siku zote tayari kusaidia wakati wa shida
Kupitia Kristo, tunapokea rehema za Mungu kwa wingi
Katika rehema zake, Mungu husamehe na kurejesha
Rehema za Mungu ni mpya kila asubuhi
Tumeokolewa kwa rehema zake, si kwa matendo yetu
Neema ya Mungu inatosha kwako
Kuna tumaini kwa ajili ya siku zijazo, maana Mungu anajua mipango aliyokupangia
Katika imani, yote yanawezekana
Hata chembe ya haradali ya imani inaweza kusogeza milima
Mwamini Bwana; anajua njia
Anaponya mioyo iliyovunjika na kufunga majeraha yao
Bwana yuko karibu na wote wanaomwita
Katika udhaifu wetu, rehema za Mungu zinatupa nguvu
Mwamini Bwana kwa moyo wako wote, na usitegemee ufahamu wako mwenyewe
Kwa Mungu, yote yanawezekana
Rehema zake ni ukumbusho wa daima wa upendo wake